text
stringlengths
5
25.1k
label
int64
0
5
Chanzo cha picha, Getty Images Pazia limeshushwa katika kampeni za Ligi Kuu ya 2023-24, huku Manchester City ikiweka historia kwa kunyakua taji la nne mfululizo. Miezi 12 iliyopita Riyad Mahrez alikuwa sehemu ya kusherehekea kombe la The Blues lakini baada ya winga huyo wa Algeria kuhamia Saudi Arabia mabingwa hao hawana tena Mwafrika yeyote katika kikosi chao cha kwanza Hapa BBC Sport Africa inachagua wachezaji wachache kutoka barani kote ambao wamevutia macho, kwa bora au ubaya, katika kipindi cha miezi tisa iliyopita. Baadhi wanaweza kuvutia soko la uhamisho, wakati wengine watakuwa na wasimamizi wapya wa kufanya kazi chini yao msimu mpya utakapoanza Agosti. Katika msimu wa kusikitisha kwa The Bees , mabao 12 ya Wissa yalikuwa muhimu sana katika kuepusha kushushwa daraja. Kufikia kiwango chake bora zaidi England, aliongoza safu ya Brentford kwa ustadi kwa muda mrefu bila Ivan Toney aliyesimamishwa na kumjeruhi Bryan Mbeumo. Fowadi huyo alifanikiwa yote licha ya kukosa mwezi mmoja wa msimu katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon), ambapo aliisaidia DR Congo kutinga nusu fainali kabla ya kushindwa na mabingwa na wenyeji Ivory Coast. Si mchezaji wa sehemu ndogo tena, itapendeza kuona ni kiasi gani mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anaweza kuendeleza msimu ujao - hasa Toney akitarajiwa kuondoka. Mshambulizi huyo wa Senegal alikuwa na msimu wa kwanza akiwa na Chelsea, ambao bado wana kazi kubwa licha ya kutumia $1.23bn (£1bn) katika uhamisho tangu kununuliwa na Todd Boehly. Jackson alifunga mara mbili pekee katika mechi zake saba za kwanza za ligi - huku akiendelea kufungiwa - kabla ya kufunga hmabao matatu katika ushindi wa fujo dhidi ya wachezaji tisa Tottenham. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 alijitahidi kufanya vyema kati ya Novemba na Machi lakini kiwango chake mwishoni mwa msimu, alifunga mabao manne huku Chelsea ikishinda mechi zao tano za mwisho, na kuashiria mustakabali mzuri kwa Mwafrika huyo wa Magharibi. Hata hivyo, iwapo Mauricio Pochettino atasalia dimbani au The Blues kuamua kusajili washambuliaji zaidi kunaweza kuathiri muda wake wa kucheza Stamford Bridge. Chanzo cha picha, Getty Images Mghana huyo ameharibu sifa yake ya kuwa tishio baada ya uhamisho wa pesa nyingi kutoka Ajax. Baada ya kipindi cha utulivu Kudus alifikisha kilele cha ubora wa juu mnamo Desemba mtindo wake wa kipekee wa kusherehekea kufunga bao umemfanya kuwa kwenye ukumbi wa matangazo ya uwanja na kuwa jambo la kawaida kwa mashabiki Black Stars ilivumilia kuondolewa tena mapema Afcon lakini Kudus alimaliza akiwa na mabao 14 na pasi za mabao sita katika mashindano yote kwa The Hammers huku klabu hiyo ikikosa kucheza soka la Ulaya msimu ujao. Julen Lopetegui anatazamiwa kuchukua nafasi ya David Moyes katika klabu hiyo ya London mashariki, na bila shaka Mhispania huyo atakuwa na nia ya kusalia na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 iwapo klabu kubwa zitamwita mara tu dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. Matokeo ya Bournemouth chini ya bosi mpya Andoni Iraola yalishangaza wengi, na umbo la fowadi wa Ghana Semenyo lilieleza mabadiliko hayo kikamilifu. Haraka na bila kuchoka, aliwapa mabeki wakati mgumu na kuwa nyota kwa kuanza katika kila mechi Ongeza mabao manane na inakuwa wazi Bournemouth ilifanya biashara yenye tija ilipotumia £10m ($12.7m) kumleta kutoka Bristol City Januari 2023. Uimara wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 pia ulithibitishwa na ukweli kwamba hakukosa mechi, alishiriki katika mechi 33 za Ligi Kuu ya England na 10 za kimataifa kwa Black Stars. Chanzo cha picha, Getty Images Baada ya muda wa mkopo nchini Ubelgiji msimu uliopita, Simon Adingra alifunga bao lake la kwanza kwa Brighton na kumalizia na mabao sita ya ligi. Lakini utukufu wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 ulikuja na Ivory Coast kwenye Afcon, ambapo alifunga bao la kusawazisha dakika za lala salama kwenye robo fainali dhidi ya Mali na kisha kuweka mabao yote mawili kwenye fainali huku The Elephants wakinyakua taji lao la tatu la bara. Mwanzoni mwa Aprili, Everton walikuwa wameshikilia rekodi ya klabu katika mechi 13 za Ligi Kuu ya England bila kushindwa na kuchupa kushuka daraja. Sogeza mbele shujaa ambaye haonekani kama Idrissa Gana Gueye, ambaye alifunga mara tatu katika mechi sita za mwisho, akigeuza saa na kuonyesha mchezo mzuri uliompa kiungo huyo mkongwe wa Senegal kandarasi mpya. Wakati huo huo, hii ilikuwa kampeni ya Rayan Ait-Nouri alikomaa na kujigeuza kuwa chaguo la kwanza kwa Wolves na Algeria. Tishio kubwa mbeleni, beki huyo wa kushoto mwenye umri wa miaka 22 amehusishwa na uhamisho wa kwenda timu tatu zilizopigania taji msimu huu Kwa mwanamume ambaye alikuwa Mwafrika aliyefunga mabao mengi zaidi msimu huu akiwa na mabao 18 ya Ligi Kuu, inaweza kuonekana ajabu kuona jina la Salah likiwa miongoni mwa waliopoteza. Kufumania nyavu mara moja tu katika mechi saba za mwisho za ligi kulimfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kumaliza na idadi ndogo zaidi ya mabao yake tangu ajiunge na Liverpool mwaka 2017. Msimu wa Salah ulikatizwa na jeraha la msuli wa paja akiwa Misri kwenye Kombe la Mataifa, na pia alikosa ushindi wa fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Chelsea. Kisha ikafuata kufuzu kwa Liverpool kwa Ligi ya Europa katika robo-fainali na makabiliano ya hadharani na kocha anayeondoka Jurgen Klopp huku changamoto ya kuwania taji la Reds ikififia. Kandanda ya Ligi ya Mabingwa ina uhakika wakati Arne Slot akielekea Anfield bado, huku wachumba nchini Saudi Arabia wakijitokeza, je Salah atatafuta mwanzo mpya? Tottenham walianza msimu huu chini ya bosi mpya Ange Postecoglu wakiwa katika kiwango kizuri na walikuwa kileleni mwa jedwali mwishoni mwa Oktoba. Kisha ukafuata msururu wa mechi tano bila ushindi kabla ya Bissouma kusalia nje mechi tatu za mwisho za 2023 kwa kufungiwa baada ya kupata kadi nyekundu ya pili msimu huu. Ugonjwa wa malaria uliathiri kiwango cha kiungo huyo kwenye Afcon na Spurs wakakosa kucheza Ligi ya Mabingwa baada ya kushindwa mara nne mfululizo mnamo Aprili na Mei. Bissouma hakuwepo katika mechi mbili za mwisho za msimu huu kutokana na jeraha la goti, ambalo linaweza pia kumfanya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kutoshiriki mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia 2026 nchini Mali mwezi ujao. Chanzo cha picha, Getty Images Kama mmoja wa watu muhimu katika kampeini ya kihistoria ya Morocco hadi nusu fainali ya Kombe la Dunia la 2022, Amrabat alitarajiwa kuongeza safu ya kiungo ya United baada ya kujiunga kwa mkopo kutoka Fiorentina. Lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alianza mechi 10 pekee za ligi huku Mashetani Wekundu wakiandika mwisho wao mbaya zaidi (wa 8) tangu ligi kuu ya Uingereza ilipobadilishwa jina mwaka 1992. Kikosi cha Erik ten Hag pia kiliangukia nje ya Uropa mapema na Amrabat akatolewa kwa kadi nyekundu huku timu ya Morocco iliyokuwa ikishabikiwa sana na Afrika Kusini katika hatua ya 16 bora kwenye Afcon. Matumaini ya mwisho ya United katika soka la bara msimu ujao ni kuwashinda wapinzani wao City katika fainali ya Kombe la FA - lakini iwapo watalipa euro milioni 20 ($21.7m, £17.1m) kufanya mkataba wa Amrabat kudumu ni suala jingine. Kwa mkopo kutoka kwa Manchester City, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alishindwa kupata matokeo ambayo wengi walitarajia angeweza - ingawa ni sawa kusema kwamba kampeni yake ilikwama katikati ya Afcon na jeraha la msuli wa paja liliongezeka muda mfupi baada ya kurudi. Kabore alianza mechi 21, mara nyingi akiwa beki wa pembeni wa kulia, na kutoa pasi mbili za mabao huku Hatters wakishushwa daraja. Sasa atarejea kwenye timu ya washindi wa taji, lakini mustakabali wa muda mrefu wa raia huyo wa Burkina Faso huko Etihad upo mashakani. Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United ililipa karibu $60m (£47.2m) kumsajili Andre Onana kutoka Inter Milan Julai mwaka jana na ni salama kusema uamuzi bado haujatolewa. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alifanya vyemakukosa kufungwa mabao mara tisa nyuma ya safu ya ulinzi inayobadilika kila mara - nambari moja tu nyuma ya mpinzani wa Manchester City Ederson - lakini pia kulikuwa na msururu wa makosa ya hali ya juu. Wakati huohuo, kuwasili tu siku ya mechi ya kwanza ya Cameroon Afcon ilikuwa taswira mbaya na alianza mchezo mmoja tu kati ya nne za taifa lake katika mashindano hayo. Ibrahim Sangare wa Ivory Coast alikuwa na Afcon bora zaidi, aliyoshiriki katika mechi sita kati ya saba, lakini athari yake huko Nottingham Forest kufuatia kuripotiwa kununuliwa kwa $38m (£30m) kutoka PSV Eindhoven ilikuwa chini ya ilivyotarajiwa kwa usajili uliovunja rekodi ya klabu. Kiungo huyo wa kati alicheza mechi 13 katika timu ambayo ilikuwa na matatizo, bila kuchangia mabao na bila kutoa pasi za mabao. Sheffield United ilisajili wachezaji watatu wa Kiafrika kabla ya msimu huu lakini, kama klabu yenyewe, wote walitatizika vibaya. Beki wa pembeni wa Algeria, Yasser Larouci aliingia kwa mkopo kutoka Troyes na alifanikiwa kuanza ligi mara sita tu, kumaanisha lazima iwe na shaka kwamba Blades sasa wataanzisha kipengele cha kufanya uhamisho wake kuwa wa kudumu kufuatia kushushwa daraja. Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanaweza kubadilisha meneja wao, wakati Manchester City wanafikiria kumruhusu mchezaji nyota kuondoka ... Mauricio Pochettino yuko kwenye rada ya Manchester United na Bayern Munich baada ya kuondoka Chelsea kwa "makubaliano ya pande zote".(Standard), Meneja wa Stuttgart Sebastian Hoeness na Kieran McKenna wa Ipswich Town wametajwa na Chelsea kama wanaoweza kuchukua nafasi ya Pochettino(Teamtalk) Mkufunzi wa Girona Michel na Enzo Maresca wa Leicester City pia huenda wakawa miongoni mwa majina yanayozingatiwa na Chelsea .(Daily Telegraph ) Thomas Tuchel amefanya mazungumzo na Chelsea kuhusu kurejea katika klabu hiyo kwa kipindi cha pili. (Florian Plettenberg) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester City wako tayari kutoa ofa kwa mlinda lango wa Brazil Ederson, 30, ambaye anavutiwa na Saudi Arabia. (Fabrizio Romano) Manchester United inachunguza uwezekano wa kumsajili mlinzi wa Crystal Palace na England Marc Guehi, 23, ikiwa watashindwa kufikia makubaliano na Everton kumnunua beki wa kati wa England Jarrad Branthwaite, 21(Mail) Manchester United wako katika nafasi ya kutumia fedha nyingi katika dirisha la usajili la majira ya joto huku hasara kubwa katika miaka ya hivi karibuni sasa ikiwaacha nje ya kanuni za faida na uendelevu (PSR). (Football Insider) Arsenal , Manchester United na Liverpool wamefanya mawasiliano na Benfica kuhusu uwezekano wa kumnunua beki wa kati wa Ureno Antonio Silva, 20.(Caught Offside) Meneja mpya wa Liverpool Arne Slot amemweka kiungo wa kati wa Benfica na Uturuki Orkun Kokcu, 23, juu ya orodha yake ya wachezaji anaotaka kuwasajili (Givemesport) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wataanzisha kipengele cha chaguo lao la kumnunua mlinda lango wa Uhispania David Raya, 28, na kufanya uhamisho wake wa mkopo kutoka Brentford kuwa wa kudumu msimu huu kwa pauni milioni 27. (Football Insider) Tottenham wameiuliza Chelsea kuhusu kupatikana kwa Trevoh Chalobah, 24, wakati wakijiandaa kuanzisha 'uvamizi' mara dufu kuipata sahihi ya beki wa Uingereza Conor Gallagher, 24. (HITC). Manchester United na Bayern Munich zilituma maskauti kumtazama kiungo wa Mali mwenye umri wa miaka 18, Malick Junior Yalcouye akiichezea IFK Gothenburg katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Mjallby siku ya Jumanne. (Expressen - kwa Kiswidi) Aston Villa wamewasilisha ombi la £12.8m kwa Sevilla kumnunua beki wa Argentina Marcos Acuna, 32. (Fichajes - kwa Kihispania) Villa pia wanavutiwa na mlinzi wa Italia Raoul Bellanova, 24, baada ya kuonyesha kiwango kizuri msimu wake wa kwanza akiwa na Torino , lakini West Ham na Manchester United pia wana hamu ya kumnunua (Tuttosport - kwa Kiitaliano) West Ham wanafikiria kumnunua Serhou Guirassy, ​​28, baada ya mshambuliaji huyo wa Guinea kuifungia Stuttgart mabao 28 ya Bundesliga msimu huu. (Standard) Tottenham itapambana na Aston Villa kwa ajili ya kumnunua beki wa Italia Andrea Cambiaso, 24, ambaye Juventus inasema thamani yake ni pauni milioni 34 (Calciomercato - kwa Kiitaliano) Fulham na West Ham wamefanya mazungumzo na Corinthians kuhusu uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Brazil Wesley mwenye umri wa miaka 19(Caught Offside) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Burnley Vincent Kompany, 38, ni miongoni mwa watu wanaopigiwa upatu kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel huko Bayern Munich . (Fabrizio Romano) Aston Villa wanakaribia kufikia makubaliano ya kumnunua tena mchezaji wa Luton Town na kiungo wa kati wa zamani wa Uingereza Ross Barkley kwa mkataba wa kudumu, miaka minne baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kujiunga kwa mkopo kutoka Chelsea(Guardian) Arsenal wanataka kusajili mshambuliaji kabla ya ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya, huku nyota wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 24, na mshambuliaji wa Ajax na Uholanzi, Brian Brobbey, wakiongoza orodha hiyo.(Independent) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea na Manchester United zote zimewasiliana na mkufunzi wa Ipswich Town Kieran McKenna, huku raia huyo wa Ireland Kaskazini akiwa katika harakati za kuchukua nafasi ya Mauricio Pochettino au Erik ten Hag. (Manchester Evening News) Wolves itadai kiasi cha kuvunja rekodi ya klabu cha pauni milioni 60 kwa winga wa Ureno mwenye umri wa miaka 24 Pedro Neto, ambaye analengwa na Manchester City na Newcastle msimu wa joto(Telegraph ) Aston Villa wako tayari kusikiliza ofa kwa mlinzi wa Brazil Diego Carlos, 31, huku wakitarajia kufuata sheria za faida na uendelevu(Telegraph) Mkufunzi wa Villa Unai Emery anataka kumsajili beki wa Barcelona na Uruguay Ronald Araujo, 25. (Sport kwa Kihispania) Stoke wameonyesha nia ya kutaka kumsajili beki wa Uingereza Conor Coady, 31, kutoka Leicester(Teamtalk), Leicester wanajiandaa kushindana na vilabu vya Ufaransa Lyon na Brest kumnunua fowadi wa Burkina Faso Mohamed Konate, 26, ambaye mkataba wake na klabu ya Urusi Akhmat Grozny unamalizika msimu huu. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Tottenham Ange Postecoglou ameiomba klabu hiyo takriban wachezaji watatu wapya msimu huu wa joto. (ESPN) Manchester United wanavutiwa na mlinzi wa Everton Muingereza Jarrad Branthwaite, 21, na The Toffees wanaweza kumnunua beki wa kati wa Galatasaray na Colombia Davinson Sanchez, 27, kuziba nafasi yake.(Caught Offside) Tottenham wako tayari kumuuza mlinzi wa Brazil Emerson Royal, 25, huku Juventus , AC Milan na Bayern Munich zikiwa na hamu ya kumnunua (Givemesport) Newcastle wanaweza kumnunua Lloyd Kelly, 25, huku beki huyo wa Uingereza akitarajiwa kuondoka Bournemouth kama mchezaji huru. (Fabrizio Romano) Chelsea itadai ada ya pauni milioni 25 kwa mlinzi wa Uingereza Trevoh Chalobah, 24, ambaye anatarajiwa kuvutia vilabu kadhaa (Telegraph) Rais wa Corinthians Augusto Melo atasafiri hadi Uingereza wiki ijayo kuzungumza na vilabu kuhusu uwezekano wa kuuzwa kwa mshambuliaji wa Brazil Wesley mwenye umri wa miaka 19. (Globo Esporte - kwa Kireno), ya nje Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanataka takriban asilimia 75 ya pauni milioni 75 walizolipa Borussia Dortmund kwa winga wa Uingereza Jadon Sancho, 24, ambaye atahitaji kupunguzwa mshahara wake wa pauni 275,000 kwa wiki ikiwa klabu hiyo ya Bundesliga itakamilisha dili la kumsaini tena(Sun) RB Leipzig wamempa mshambuliaji wa Slovenia Benjamin Sesko mwenye umri wa miaka 20 - ambaye anahusishwa na kuhamia Arsenal - nyongeza ya muda wa kandarasi ya mwaka mmoja. (Fabrizio Romano) Sheffield United ingelazimika kulipa kiasi cha tarakimu sita kwa kiungo wa kati wa Brazil Vinicius Souza kwa klabu ya zamani ya Lommel iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 angeanza katika mechi dhidi ya Tottenham Jumapili (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Bayern Munich na Ajax wanaendelea kupigania sahihi ya Erik ten Hag, 54, kwa imani kwamba atafutwa kazi kama meneja wa Manchester United mwishoni mwa msimu huu(Mirror) Kipa wa Uhispania David Raya, 28, anasema hajafanya mazungumzo yoyote na Arsenal kuhusu iwapo watafanya uhamisho wake wa mkopo kutoka Brentford kuwa wa kudumu. (Express) Meneja wa Tottenham Ange Postecoglou ataweka kipaumbele kumsaini mshambuliaji mpya na kiungo wa safu ya ulinzi huku akipanga kuwaachilia wachezaji wengi msimu wa joto (Mirror) Ipswich wanasema wanafanya kila linalowezekana kusalia na meneja Kieran McKenna huku kukiwa na nia ya kumchukua kocha huyo kutoka kwa Brighton , Chelsea na Manchester United .(Teamtalk) Chanzo cha picha, Getty Images Mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino anasema atafurahi kusalia na 80-85% ya kikosi chake msimu ujao(football.london) Mwenyekiti mwenza wa Arsenal Josh Kroenke amewaambia mashabiki "klabu haitasimama tuli" inapotafuta wachezaji ili kusaidia kupata taji la Uingereza na Ulaya(Goal) West Ham wanakaribia kumsajili mlinzi mwenye umri wa miaka 18 Mwingereza Luis Brown kutoka Arsenal(Caught Offside) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Aston Villa wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Chelsea na England Conor Gallagher, 24, na huenda wakamtumia fowadi wa Colombia Jhon Duran, 20, kama sehemu ya mkataba huo. (Telegraph – Subscription required) Mshambulizi wa Brentford na England Ivan Toney, 28, anasakwa na Tottenham kama mmoja wa washambuliaji wawili wanaotarajiwa kusajiliwa msimu huu. (Football Insider) Bosi wa Ipswich Kieran McKenna ndiye mgombea anayeongoza kuchukua nafasi ya Mauricio Pochettino katika klabu ya Chelsea, ambaye hatma yake kama meneja haijaamuliwa. (Guardian) Kocha wa Brighton anayeondoka Roberto de Zerbi ndiye anayelengwa na Bayern Munich kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel kama meneja. (Bild) Chanzo cha picha, PA Media Bayern na Muitaliano De Zerbi tayari wameamua kuwa hawatafanya kazi pamoja, kwa mujibu wa mkurugenzi wa klabu hiyo Max Eberl. (Fabrizio Romano) Newcastle, Everton na Crystal Palace wana nia ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Uingereza Kasey McAteer, 22, ambaye anatazamiwa kuingia mwaka wa mwisho wa kandarasi yake na Leicester City. (Football Insider) Everton wanajiandaa kukabiliana na ofa za ufunguzi kwa mlinzi wa kati Jarrad Branthwaite, 21, huku Manchester United, Manchester City na Tottenham zote zikiwa na nia ya kumnunua mchezaji huyo wa England. (Mail) Manchester United wanataka kumuuza mshambuliaji Muingereza Mason Greenwood, 22, ambaye amekuwa akihusishwa na Napoli, Juventus na Atletico Madrid baada ya kucheza kwa mkopo Getafe. (Sports) Chanzo cha picha, Getty Images Klabu ya Napoli ya Italia imefanya mawasiliano na Manchester United juu ya kutaka kumnunua Greenwood. (Subscription Required) Borussia Dortmund pia wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania saini ya Greenwood. (Mirror) Kocha anayetarajiwa Liverpool Arne Slot ametanguliza saini ya beki wa Ureno Antonio Silva, 20, kutoka Benfica. (Give me Sport) RB Leipzig wameweka kipengele chao cha kuachiliwa kwa mshambuliaji wa Slovenia Benjamin Sesko, 20, ambaye anahusishwa na Arsenal, kwa £55.6m. (Sky Sports Germany) Kocha wa Barcelona Xavi anasema bado anaungwa mkono na klabu hiyo licha ya ripoti kueleza kuwa huenda akafutwa kazi. (Saa – Subscription Required)
2
Chanzo cha picha, Getty Images Tyson Fury alishindwa kwa pointi nchini Saudi Arabia huku Oleksandr Usyk akiwa bingwa wa kwanza wa ndondi za uzani mzito zaidi kushikilia mikanda minne duniani. Katika usiku uliosheheni ujuzi wa kila aina kutoka kwa mabondia hao Tyson Fury alianza vyema mechi hiyo lakini akaokolewa na kengele katika raunndi ya tisa kutokanna na kichapo cha Usyk. Akiwa katika hali ya kusubiri kadi za matokeo kusomwa, Fury alionekana kushawishika kupata ushindi kabla ya kadi hizo kumpatia ushindi Usyk .. Kadi za matokeo zilisomeka 115-112 na 114-113 kwa raia wa Ukraine, huku jaji wa tatu akifunga 114-113 kwa Fury. Ilimaanisha Fury, 35, alipoteza kwa mara ya kwanza katika taaluma ya miaka 16. Atapata fursa ya kulipiza kisasi kwa mechi ya marudiano iliyopangwa kufanyika baadaye mwaka huu. "Ninaamini alishinda raundi chache, lakini nilishinda nyingi," Fury alinukuliwa akisema kwenye jukwaa hilo. "Ilikuwa moja ya maamuzi mabaya zaidi katika historia ya ndondi. Nitarejea." Usyk anachukua mkanda wa WBC kutoka kwa Fury, ili kuongeza kwenye mkusanyiko wake wa WBA, WBO na IBF. Bondia huyo mwenye umri wa miaka 37 bado hajashindwa na anakuwa bondia wa kwanza katika takriban miaka 25 kusimama kidete kama bingwa pekee wa dunia wa uzito wa juu. "Asante sana kwa timu yangu. Ni fursa kubwa kwa familia yangu, kwangu, kwa nchi yangu. Ni wakati mzuri, ni siku nzuri," Usyk alisema. "Ndiyo, bila shaka. Niko tayari kwa mechi ya marudiano." Chanzo cha picha, Getty Images Tyson Fury hakuwahi kupoteza pambano la kulipwa kwa miaka 16 Usyk - bingwa wa zamani wa dunia wa uzani wa cruiserweight - alishinda katika pambano ambalo linamuweka katika historia ya ndondi kuwa mmoja wa nguli wa mchezo huo duniani. Baada ya kukosekana kwa mbwembwe na kelele uwanjani kwa mapigano ya yaliofanyika mapema, takriban mashabiki 20,000 waliojumuisha sura maarufu kama Cristiano Ronaldo walijipata wakishangilia ghafla. Usyk - anayefanana na shujaa – aliingia katika jukwaa hilo akiwa amevalia mavazi ya kitamaduni ya Ukraine ya kijani kibichi, macho yake yakilimwilika jukwaa hilo. Kinyume na ukali wa Usyk, Fury ambaye ni mcheshi aliimba na kucheza ngoma ya Bonnie Tyler Holding Out For A Hero. Mechi ikianza Fury alielekea katika kona ya mpinzani wake na kuanza kummiminia makonde mazito hatua iliowafurusha mashabiki 2,500 wa Uingereza waliosafiri. Huku mabingwa hao wawili wakikabiliana katikati ya jukwaa , mechi ilibadilika na Usyk akaanza kumshambulia mpinzani wake na kumrudisha nyuma kwa ngumi nzito. Hatahivyo Fury aliyekuwa akitabasamu wakati wote huo alionesha ushupavu wake na kumaliza raundi ya kwanza licha ya Usyk kumpata ngumu ya kushoto na kumrudisha nyuma kwa kasi. mwenye tabasamu na shupavu alipitia raundi ya kwanza. Hata wakati Usyk alipotua ndoano thabiti ya kushoto na kumuunga mkono kwenye kona, Mfalme wa Gypsy alicheka kwa ghadhabu. Fury alijibu kwa njia mbili za juu zenye sura chungu kwa Usyk katikati ya dakika ya pili. Urefu na faida ya kufikia ya Fury ilikuwa inaleta fumbo nyingi sana kwa Usyk kutatua, au ndivyo ilionekana. Usyk alirudi kwenye shindano katika nusu ya pili ya pambano Bondia huyo amekuwa akianza mapigano yake kwa kasi ya chini hatua ambayo imesababisha kujeruhiwa mara nyingi. Lakini alirudi kwa kishindo katika raundi ya tisa . Huku Lennox Lewis, bingwa wa mwisho ambaye alishikilia mikanda mitatu katika uzani mzito zaidi duniani, na mabingwa wenzake wa zamani Larry Holmes na Evander Holyfield wakitazama pigano hilo, Usyk hatimaye alionyesha umahiri wake. Baada ya msururu wa makonde ya kushoto kulia dhidi ya, Fury aliyekuwa akirudi nyuma na kuduwaa, refa aliingilia kati na kumzuia Usyk kuendeleza mashambulizi yake – ikiashiria knock out. Akionekana kutetereka na kutegemea kamba za ulingo , refa alihesabu hadi 10 kabla ya kengele . Hii haikuwa mechi ya kuchosha, ya kimbinu, kama ilivyotabiriwa na baadhi ya wachambuzi bali pigano lililosheheni makabiliano kutoka kwa mabondia wote wawili . Ngumi nyengine ya kushoto kutoka kwa Usyk ilimpata Fury katika raundi ya 11. Wawili hao walisalimiana kabla ya kuanza kwa raundi ya 12 huku mashabiki wakihisi kwamba mechi bado haijakamilika. Lakini ilikuwa Usyk ambaye alionekana kumaliza raundi ya mwisho akiwa mchangamfu hali iliomfanya kushinda mechi hiyo . Chanzo cha picha, Getty Images Pigano lisilo na mvuto la Oktoba dhidi ya Francis Ngannou liliwaacha wengi wakijiuliza ikiwa siku bora za Fury zilikuwa zimepita. Lakini alikuwa mshindani mzuri na anayefaa na maoni yoyote dhidi yake yake kwamba alikuwa amepitwa na wakati yalizikwa katika kaburi la sahau alipodhibiti sehemu za mapema za mechi hiyo. Fursa yake ya kuwa bingwa anayeshikilia mataji manne duniani huenda isije tena hivi karibuni. Mechi ya marudiano inatarajiwa mwezi Oktoba lakini hakuna uwezekano kuwa itashirikisha mikanda yote minne - IBF inapanga kumvua Usyk taji hilo kwani hayuko tayari kukabiliana na mpinzani wao wa lazima. "Tutarudi, napumzika. Ninaamini nilishinda pambano lakini sitakaa hapa kulia na kutoa visingizio. Tutapigana tena," Fury aliongeza. Taji la dunia la uzito wa juu linazingatiwa na wapenzi wa ndondi kama tuzo kuu zaidi, inayotamaniwa zaidi katika mchezo, na mpiganaji huyo mzaliwa wa Crimea aliacha ulingo akiwa amejifunga mikanda yote minne kwenye fremu yake ya futi 6 na inchi 3.
2
Chanzo cha picha, Getty Images Newcastle United wanataka kumsajili mlindalango wa Arsenal na England Aaron Ramsdale na wako tayari kulipa pauni milioni 15 kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Telegraph) Crystal Palace na Fulham zote zimetuma mawakala wao kumtazama kiungo wa kati wa Fiorentina na Morocco Sofyan Amrabat, 27, ambaye yuko kwa mkopo Manchester United. (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United huenda ikalazimika kumpa kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 29, nyongeza ya mshahara kutoka kwa mkataba wake wa sasa wa pauni 230,000 kwa wiki ikiwa wanataka kumbakiza nahodha wao. (Star) United itakataa ofa zozote zitakazowasili kwa Fernandes msimu huu kwa kuwa wanaona kiungo huyo hawezi kuguswa.(Caught Offside) United wamepewa fursa ya kumteua Massimiliano Allegri anayelengwa kwa muda mrefu kama meneja baada ya Muitaliano huyo, 56, kutimuliwa na Juventus. (Express) Chanzo cha picha, Getty Images Mgombea mkuu wa Bayern Munich kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel kama meneja msimu huu ni mkufunzi wa Brighton Muitaliano Roberto de Zerbi, 44. (Bild, in German). Bayern wameiambia kambi ya De Zerbi kuwa watakuwa tayari kulipa ada yake ya pauni milioni 12 katika klabu ya Brighton. Muitaliano huyo ameamua kutokwenda kuinoa AC Milan , lakini anavutiwa na wababe hao wa Ujerumani. (HITC) Chanzo cha picha, Goal Chelsea wanahisi wameshinda mbio za kumsajili winga wa Brazil Estevao Willian mwenye umri wa miaka 17 baada ya kuafikiana kuhusu mkataba wenye thamani ya hadi £60m na ​​Palmeiras. (HITC) Wolves wako tayari kumsajili fowadi wa Southampton na Scotland Che Adams, 27, kwa uhamisho wa bila malipo licha ya Everton na Leeds United pia kumtaka. (Teamtalk)) Manchester United wanataka dili la bei iliyopunguzwa kwa Jarrad Branthwaite baada ya kuamua hawatakidhi bei ya Everton ya pauni milioni 80 kwa mlinzi huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 21. Wako tayari kulipa hadi £55m. (Givemesport) Chanzo cha picha, Getty Images mazungumzo yake ya kandarasi ya mlindalango wa Uingereza Alex McCarthy, 34, yamesitishwa na Southampton huku kukiwa na taarifa za kutaka kutoka kwa Celtic msimu huu wa joto. (Soka Scotland) Celtic wanatumai kuwa Champions League soka itatosha kumjaribu mlinzi wa Queens Park Rangers Muingereza Jake Clarke-Salter kusajili kwa ajili yao, 26, huku Crystal Palace, Burnley na Bournemouth wakitarajiwa kutoa mishahara zaidi. (Football Insider) Meneja wa Uingereza Michael Carrick, 42, anatarajiwa kusaini mkataba mpya katika klabu ya Middlesbrough na kuweka mustakabali wake katika klabu hiyo baada ya kutakiwa na Premier League. (Telegraph) Chanzo cha picha, Getty Images Bosi wa Lens Franck Haise anasema angependelea kumsajili mlinzi anayeondoka wa Manchester United Raphael Varane, lakini klabu hiyo ya Ligue 1 inaweza kushindwa kumnunua Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye alianza soka lake katika klabu hiyo. (L'Equipe, in French) Real Madrid wamefikia makubaliano kimsingi na Luka Modric kuongeza mkataba wa kiungo huyo wa kati wa Croatia mwenye umri wa miaka 38 kwa mwaka mmoja zaidi kwa kupunguzwa mshahara. (Onda Madrid, via Mundo Deportivo, in Spanish) AC Milan wamefanya mawasiliano mapya na kocha wa Lille Paulo Fonseca. Mreno huyo, 51, anataka kuchukua nafasi ya Stefano Pioli huko San Siro. (Fabrizio Romano) Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi
2
Chanzo cha picha, PA Media Tumemwona kama mchezaji na tunamfahamu kama meneja, lakini Mikel Arteta ni nani hasa? Katika wiki ya mwisho ya msimu wa kusisimua wa Ligi Kuu ya Uingereza, meneja wa Arsenal alimualika mwandishi wa BBC Sport Guillem Balague nyumbani kwake kwa mahojiano ya kipekee ya saa moja. Arteta anazungumza juu ya utoto wake, kazi yake, maisha yake ya familia na Umeneja wake kazi anayoifanya sasa. Arteta alikulia katika kitongoji kizuri cha Antiguo huko San Sebastian. "Ninapenda maji, napenda jua na napenda ufuo, na jumuisha mpira wa miguu juu ya hayo..." anasema. "Hapo ndipo nilitumia saa nyingi za mchana, nikicheza ufukweni nilipokuwa mtoto. Kwangu mimi, ilikuwa mchanganyiko mzuri." Akiwa na umri wa miaka 14, Arteta alikutana na kipa wa baadaye wa Uhispania na Liverpool Pepe Reina katika siku yake ya kwanza katika Chuo cha mafunzo ya soka cha Barcelona, ​​La Masia. Alikuwa rafiki na kulala chumba kimoja na magwiji wa Barca, Victor Valdez na Andres Iniesta wakiwa vijana. "Yeye (Reina) amekuwa mmoja wa marafiki zangu wa karibu," asema. "Tulishiriki vitanda vyetu kwa miaka mitatu. Mojawapo ya kumbukumbu nzuri zaidi ambayo ninayo maishani mwangu ni wakati tuliotumia pamoja. "Tulikuwa tukishindana kwa sababu ilitubidi - kwa sababu sote tulitaka kufika kwenye kikosi cha kwanza - lakini ilikuwa hisia halisi ya familia." Chanzo cha picha, Getty Images Akiwa na miaka 17, Arteta alihamia kwa mkataba wa mkopo katika Paris St-Germain, ambapo alikutana na Mauricio Pochettino, ambaye alikua kaka mkubwa na rafiki mzuri. "Mauricio alikuwa kama ngao kwangu - alikuwa akinilinda dhidi ya kila kitu. Alinipa imani na kujiamini sana," Arteta anasema. "Alikuwa akicheza nyuma yangu na ilikuwa kama kuwa na mtu anayekusukuma mgongoni mwako na kukufundisha na kukusaidia kila wakati. Sikuweza kupata mtu yeyote bora zaidi." [yake] Kuhusu kuhamia PSG, Arteta anasema: "Ulikuwa uamuzi mgumu. Ndoto yangu ilikuwa kuichezea Barcelona lakini wakati huo ilibidi nifuate uhalisia wa mambo." Chanzo cha picha, Getty Images Mnamo 2002 Arteta alisaini mkataba wa kujiunga na Rangers, alipoondoka Barcelona. "Sijawahi kuona hali kama hii - kuangalia jinsi watu hawa wanavyopenda," soka, anasema Arteta kuhusu ziara yake ya kwanza katika Rangers, ambapo walikuwa wakicheza na PSG katika Ligi ya Mabingwa. "Uamuzi bora zaidi tuliofanya. Ilikuwa ngumu sana - soka tofauti kabisa. Lazima uishi au ufe." Wakati akiwa katika Rangers, Arteta alikutana na mwanamke ambaye alikuwa mke wake baadaye, Bi Lorena, mkufunzi wa masuala ya maisha, kwenye safari ya kwenda San Sebastian. Sasa wana watoto watatu pamoja. “Amebadilisha maisha yangu. Amebadilisha mtazamo wangu kuhusu maisha,” anasema. "Tumepitia hali nyingi, nyingi tofauti, zingine za kuvutia, zingine ngumu sana. "Nina hisia na yeye kwamba hatuwahi kuchoka. Ninaweza kukaa hapo saa tano, saa 10, kwenda popote duniani na kufurahia na kufurahi na kucheka. “Katika taaluma yetu huwa tunazungumza kuhusu mhusika mkuu ambaye ni mchezaji au kocha au meneja. "Lakini vipi kuhusu mtu ambaye yuko karibu na huyo? Na bila huyo hakuna misingi ya kutosha na hakuna nguvu za kutosha za kuwa thabiti." Chanzo cha picha, BBC SPORT Baada ya kuishi Uskochi, Arteta mwenye umri wa miaka 24 alihamia Real Sociedad ya Uhispania kwa matumaini ya kuweka familia yake pamoja baada ya wazazi wake kusema walikuwa wakitalikiana. “Nilijihisi kuwa na huisia za huzunni na hatia. Sikujua kama hiyo ilikuwa ni kwa sababu yangu na kujaribu kutekeleza ndoto yangu. Ninahisi kuwajibika sana kwa hilo,” anasema. "Sikuwahi kuhisi kuwa ulikuwa wito sahihi [kurejea Uhispania], lakini nilikuwa na jukumu na nilitaka kuwaunganisha tena wazazi wangu na familia yangu. “Ilikuwa balaa. Haijawahi kufanya kazi kwa maana hiyo. Sijawahi kuhisi kuunganishwa kwa wakati wowote." Arteta alijiunga na Everton mwaka wa 2005 kwa pauni milioni 2 baada ya kufanikiwa kwa kupata mkataba wa mkopo kutoka Sociedad. “Moja kwa moja, unaungana na timu; unaungana na wachezaji; unaungana na wafanyakazi; unaungana na wafuasi. Na hisia hiyo inahitajika,” anasema. "Unajiamini, unajisikia msisimko kila asubuhi kushuka kitandani na kwenda kwenye mazoezi. Nilipenda kila dakika." Chanzo cha picha, Getty Images Muda mfupi baada ya maisha yake ya uchezaji kuisha, Arteta mwenye umri wa miaka 34 alijiunga na Manchester City kama meneja msaidizi wa Pep Guardiola. "Tulikuwa na uelewano mzuri wa ajabu," anasema. "Kwa kutazamana kwa macho tu tulielewana wazi juu ya kile tulichopaswa kukifanya au kile tulichokuwa tunafikiria wakati huo. "Lilikuwa ni jambo la kuvutia kuwa sehemu ya kitu kipya." Arteta aliichezea Arsenal kati ya 2011 na 2016. Alipojiunga mara ya kwanza, alikuwa akiongea kwenye chumba tulivu cha kubadilisha. Anasema: "Nilianza kuzungumza na nikaanza kuwaunganisha watu wote - 'Njoo, tufanye hivi, nyie'. Nilisisimka sana. “Nitafanya kila kitu. Nitavunja kila ukuta hapa. Tunapaswa kufanya hili kutokea.", anakumbuka. Anasema kuhusu kustaafu: "Ilikuwa inafikia hatua ambayo nilikuwa nahisi kupendezwa zaidi na upande wa kufundisha kuliko upande wa kucheza." Mnamo Desemba 2019 Arteta alikua meneja wa Arsenal. "Suala lilikuwa la kina zaidi. Suala lilikuwa kwenye mizizi yetu. Yote yalikuwa ni fujo,” anasema. "Tunahitaji watu wetu. Tunahitaji kuwashawishi kwamba umejitolea na uko tayari kuipeleka klabu hii sehemu tofauti kabisa.” Arteta alipanda mzeituni mbele ya ofisi yake, kuashiria umri na mizizi ya klabu. Anasema hivi: “Niliupanda mti huo na kusema, ‘Hii ni zawadi yangu. Sasa unapaswa kuuangalia. Ni kitu kilicho hai. Huwezi kuuacha ife.' "Mti huo ni kiasi sawa cha miaka katika klabu yetu ya soka - zaidi ya miaka 130. "Utakuwa huko kila siku. Lazima muuangalie na nyote muwajibika." Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi
2
Chanzo cha picha, Reuters Cristiano Ronaldo ameongoza orodha ya Forbes ya wanariadha wanaolipwa fedha nyingi zaidi duniani kwa mara ya nne katika maisha yake ya soka, huku Jon Rahm mcheza gofu akipanda hadi nafasi ya pili. Ronaldo pia aliongoza orodha hiyo mwaka jana baada ya kuhamia klabu ya soka ya Saudi Arabia ya Al Nassr. Jarida la biashara la Forbes linasema, mshambuliaji huyo wa Ureno mwenye umri wa miaka 39 alipata kiasi cha $260m (£205m) - kutoka $136m (£108.7m) - katika kipindi cha miezi 12 iliyopita. Mpinzani mkubwa wa Ronaldo Lionel Messi ameporomoka hadi nafasi ya tatu nyuma ya Rahm. Mchezaji gofu wa Uhispania amepanda hadi nafasi pili nyuma kabla ya kufanyika kwa safari yake ya kwenda kucheza Gofu ya LIV inayofadhiliwa na Saudia na anaripotiwa kupata $218m (£172m). Mcheza gofu huyo wa Uhispania ni mmoja wa wanariadha 22 walio na umri wa chini ya miaka 30 kwenye orodha hiyo, jambo ambalo linaweza kuashiria mabadiliko. Wachezaji waliodumu katika hiyo orodha kama vile Serena Williams, Roger Federer na Tom Brady tayari wamestaafu , wakati Ronaldo, LeBron James, Tiger Woods na wanariadha wengine watatu wenye umri wa miaka 39 au zaidi, pia nao wakitarajiwa kuchukua hatua hiyo hivi karibuni. Wanasoka Neymar na Karim Benzema pia wameingia kwenye 10 bora baada ya kuhamia katika ligi ya soka ya Saudi Pro League. Giannis Antetokounmpo (katika nafasi ya tano) anaungana na nyota wenzake wa mpira wa vikapu LeBron James (wa nne) na Stephen Curry (wa tisa) kwenye orodha hiyo , huku beki wa pembeni wa kandanda wa Marekani Lamar Jackson akiwa katika nafasi ya 10. Kulingana na Forbes, wanariadha 10 wanaolipwa zaidi duniani kwa pamoja walipata kiasi cha $1.38 bn (£1.06bn) kabla ya ushuru na ada za mawakala katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, ambayo ni jumla ya juu zaidi kuwahi kutokea. Katika nafasi ya 14 bora , Canelo Alvarez bondia ambaye alikulia katika maisha ya umaskini wa mashambani na alianza kupigana akilipwa dola 40, anakadiriwa na Jarida la Forbes kuna na thamani ya angalau $275 milioni. Katika nafasi ya 16 ni bondia wa uzani mzito duniani Anthony Joshua kutoka Uingereza anayedaiwa kuwa na thamani ya $83m. Joshua alishinda mapambano yake ya kwanza 22 ya kulipwa na alikuwa bingwa wa dunia kutoka 2016 hadi 2019, hadi alipopoteza kwa Andy Ruiz Jr. Mshambuliaji wa Manchester City Erling Halaand ambaye ameorodheshwa katika nafasi ya 27 ana thamani ya $61m. Akiwa miongoni mwa nyota wanaochipuka kwa kasi katika soka, Haaland aliamuru ada ya uhamisho ya dola milioni 63 katika uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund kwenda Manchester City mnamo 2022. Mchezaji soka kutoka Afrika anayelipwa fedha nyingi zaidi ni Mohammed Salah kutoka Misri mwenye thamani ya $53m. Salah anashikilia nafasi ya 38. Nyuma yake ni Sadio Mane mshambuliaji wa Senegal mwenye thamani ya $52m katika nafasi ya 40. Mané ndiye nahodha na mfungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya soka ya Senegal. Alimfuata Cristiano Ronaldo hadi klabu ya Saudi Pro League ya Al Nassr baada ya kukaa msimu wa 2022-23 na klabu ya Ujerumani Bayern Munich. 1. Cristiano Ronaldo, football: $260m (£205m) 2. Jon Rahm, Gofu: $218m (£172m) 3. Lionel Messi, Soka: $135m (£107m) 4. LeBron James, Mpira wa vikapu: $128.2m (£101m) 5. Giannis Antetokounmpo, Mpira wa vikapu: $111m (£88m) 6. Kylian Mbappe, Soka $110m (£87m) 7. Neymar, Soka: $108m (£85m) 8. Karim Benzema, Soka: $106m (£84m) 9. Stephen Curry, Mpira wa vikapu $102m (£80m) 10. Lamar Jackson, Soka ya Marekani: $100.5m (£79m) Imetafsiriwa na Seif Abdalla
2
Chanzo cha picha, Getty Images Napoli wanavutiwa na mshambuliaji wa England Mason Greenwood, ambaye yuko Getafe kwa mkopo kutoka Manchester United, lakini huenda wakakabiliwa na ushindani kutoka kwa Juventus ikiwa wanataka kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano) Atletico Madrid pia wanataka kumsajili Greenwood. (Star) Kocha wa Bayern Munich Thomas Tuchel anataka klabu hiyo kumhakikishia kwamba itamleta kiungo mkabaji na mchezaji nyota katika majira ya joto kabla hajajitolea kubadili mawazo yake na kusalia na kikosi hicho cha Bundesliga hadi mwisho wa msimu huu, lengo likiwa Bruno Fernandes,29, wa Manchester United. (Independent) Chanzo cha picha, Getty Images Hamu ya Real Madrid kumnunua beki wa Canada Alphonso Davies, 23, ambaye kandarasi yake na Bayern Munich inakamilika msimu wa joto wa 2025 imefifia. (COPE - kwa Kihispania). Napoli wanamtafuta mshambuliaji wa Atletico Madrid, Samu Omorodion, 20, ambaye amekuwa Alaves kwa mkopo msimu huu, kama mbadala wa mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 25. (Sky Sports Italy). Mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino anaungwa mkono na watu mashuhuri katika klabu hiyo kabla ya tathmini ya mwisho wa msimu utakaoamua mustakabali wake Stamford Bridge. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Kiungo wa kati wa Chelsea na England Conor Gallagher hana nia ya kuhamia Newcastle United, ambao kwa muda mrefu wanavutiwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, msimu huu wa joto. (Football Insider) Real Madrid wanatazamiwa kuwapa Espanyol euro 1.5m ili kumbakisha mshambuliaji wa Uhispania Joselu, 34, kwa mkopo kabla ya kuamua iwapo watammpa mkataba wa kudumu msimu huu wa joto. (Sport - kwa Kihispania) Kiungo wa kati wa Aston Villa Mbrazil Philippe Coutinho, 31, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo katika klabu ya Al-Duhail SC ya Qatar, anaweza kujiunga na timu yake ya zamani ya Vasco da Gama kwa mkataba wa mkopo na kulazimika kuinunua kwa £5m. (TNT Sports Brazil, via Mail) Chanzo cha picha, Getty Images Juventus wanatafakari iwapo watamfukuza meneja Massimiliano Allegri, licha ya kunyanyua taji lao kuu la kwanza katika kipindi cha miaka mitatu kwa ushindi katika fainali ya Coppa Italia siku ya Jumatano. (Sky Italia - kwa Kiitaliano) Juve wamempa Thiago Motta wa Bologna mkataba wa miaka mitatu kuchukua nafasi ya Allegri kama kocha wao mpya. (Fabrizio Romano) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanataka kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Ollie Watkins kutoka Aston Villa kwani mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 analingana na wasifu wa mchezaji ambaye wanataka kumsajili. (Talksport) Arsenal wanafikiria kuwasilisha dau la pauni milioni 60 kumnunua mshambuliaji wa RB Leipzig wa Slovenia Benjamin Sesko, 20. (Telegraph - usajili unahitajika) Mshambulizi wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohamed Salah,31 na kipa wa Brazil Alisson Becker, 31, ni miongoni mwa wachezaji wanaosakwa na klabu za Saudi Pro League msimu huu. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Nafasi ya Erik ten Hag kubaki kocha wa Manchester United inalegalega, huku mustakabali wa Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 54 ikitarajiwa kuamuliwa baada ya fainali ya Kombe la FA mnamo Mei 25. (Guardian) Thomas Tuchel, ambaye yuko kwenye orodha fupi ya Manchester United ya wachezaji wanaotarajiwa kuchukua nafasi ya Ten Hag, yuko kwenye mazungumzo ya kusalia Bayern Munich, baada ya kupangwa kuondoka mwishoni mwa msimu huu. (Times - usajili unahitajika) Chelsea wameandaa ofa mpya kwa winga wa Palmeiras Willian Estevao baada ya kuafikiana na mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 17 wiki iliyopita. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Licha ya kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Aston Villa italazimika kuuza angalau mchezaji mmoja kwa ada kubwa msimu huu wa joto ili kuzingatia Kanuni za Faida na Uendelevu za Ligi Kuu. (Sun) Kocha wa zamani wa Chelsea, Manchester United na Tottenham Jose Mourinho ananyatiwa na klabu ya Al-Qadsiah ya Saudi Arabia. (Mail) Chelsea watapata nyongeza ya pauni milioni 5 chini ya masharti ya uhamisho wa Eden Hazard kwenda Real Madrid 2019 baada ya timu hiyo ya Uhispania kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa - licha ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 33 kustaafu miezi saba iliyopita. (Telegraph - usajili unahitajika) Imetafsiriwa na Ambia Hiris
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester City ilipata shujaa mpya kutoka kwa nyota wao wakubwa katika harakati zao za kunyakua taji la nne mfululizo la ligi ya Premier. Pep Guardiola alichukua hatua ya tahadhari alipomtoa kipa Ederson, huku City wakiwa kifua mbele kwa bao 1-0, baada ya mlinda lango namba moja kupata pigo baya kichwani baada ya kugongana na beki wa Tottenham, Cristian Romero. Ederson, ambaye alikuwa na tatizo la jicho lake, hakuonekana kufurahishwa na uamuzi huo - uliotokana na ushauri wa daktari wa klabu - lakini meneja wake alikuwa na haki kabisa, sio tu kumlinda kipa huyo wa Brazil lakini pia alikuwa na imani na mbadala wake Stefan Ortega. Na katika kipindi cha dakika 21 cha mchezo wa hali ya juu, Ortega - ambaye amefanya vyema kila anapotoka benchi kuchukua mahala pake Ederson msimu huu – huenda amekaribia kuipatia City taji lake la sita katika misimu saba. Wakati filimbi ya mwisho ilipolia na klabu ikasalia na ushindi mmoja kabla ya kutawazwa mabingwa kwa mara ya nne mfululizo, Guardiola alielekea moja kwa moja kwa Ortega na kumsalimia Mjerumani huyo kwa busu shavuni kwa mchango wake muhimu. Guardiola hakujizuia kwani alisema: "Ortega ni kipa wa kiwango cha kimataifa. Kipa wa kipekee. Ederson hakupata mtikisiko, alikuwa na tatizo kwenye jicho lake. Hakuona vizuri hivyo daktari alisema. Ninapaswa kumbadilisha." Spurs waliwafanyia dhihaka wakosoaji ambao walipendekeza wanaweza kutocheza vizuri kimakusudi kwa sababu matokeo yoyote chanya yanaweza kuwapa wapinzani wao Arsenal taji lao la kwanza la Ligi ya Premia ndani ya miaka 20. Athari ya Ortega ilikuwa ya papo hapo, akimnyima goli mchezaji wa akiba wa Spurs, Dejan Kulusevski , halafu akaokoa shambulio jingine la mchezaji huyo huyo muda mfupi baadaye. Hatari kubwa zaidi ilikuwa katika dakika za lala salama, huku City wakiwa mbele kwa bao moja, wakati Son Heung-min alipouchukua mpira na kusalia na Ortega pekee. Ilikuwa ni aina ya fursa ambayo Mkorea Kusini huyo angetumia kwa ustadi mara nyingi katika maisha yake ya Spurs. Chanzo cha picha, Getty Images Hatahivyo Ortega alibaki imara, alisimama kwa miguu yake, akimngoja Son achukue hatua yake kabla ya kunyoosha mguu wake wa kulia na kufanya uokoaji ambao unaweza kuhitimisha ushindi mwingine wa Ligi Kuu. Guardiola, ambaye ni wazi alikuwa na wasiwasi, alionyesha furaha, uchungu na utulivu mkubwa, huku nahodha wa Manchester City, Kyle Walker akimfananisha Ortega, na kipa mwenzake, Bayern Munich Manuel Neuer.. Ilikuwa ni nafasi ya mwisho kwa Spurs huku Erling Haaland akiongeza bao lake la pili usiku kwa mkwaju wa penalti katika muda wa ziada kwa bao lake la 38 msimu huu. Iwapo City wataifunga West Ham United kwenye Uwanja wa Etihad siku ya Jumapili, taratibu zitakuwa zimekamilika. Haaland anaweza kugonga vichwa vya habari huku mafanikio yake ya kufunga mabao yakiendelea, licha ya msimu huu kutokuwa mzuri kama wake wa kwanza, ila Ortega alikuwa jna mchezo mzuri na wa hali ya juu. Ushiriki wa mlinda lango huyo ulikuwa mfupi lakini wa kuvutia na pengine wenye maamuzi mazuri. Tangu City washindwe na Aston Villa mwezi Disemba, hawajafungwa katika mechi 22 za Ligi Kuu ya Uingereza, wameshinda 18 na kupata sare nne katika aina ya matokeo ambayo yanatishia kuvunja mioyo ya Arsenal kama vile walivyoivunja Liverpool katika siku ya mwisho ya mechi miaka iliyopita. Imetafsiriwa na Seif Abdalla
2
Chanzo cha picha, Reuters Bayern Munich wana mpango wa kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United Bruno Fernandes msimu huu wa joto na wanaamini kuwa wanaweza kumpata mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 29 kwa sababu ya hali ya kufadhaika Old Trafford. (Independent) Wachezaji kadhaa wakuu wa Bayern Munich akiwemo mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 30, wanataka meneja Thomas Tuchel kubadili uamuzi wake wa kuondoka katika klabu hiyo ya Bundesliga mwishoni mwa msimu huu. (Abendzeitung - kwa Kijerumani) Manchester United wako tayari kutoa pauni milioni 55 kumnunua beki wa Everton na England chini ya umri wa miaka 21 Jarrad Branthwaite, 21. (Daily Mail). Mlinzi wa Uholanzi Jeremie Frimpong, 23, anaelekea kuondoka Beyer Leverkusen msimu huu wa joto huku Real Madrid, Manchester City, Arsenal na Manchester United zikiwa na nia ya kunufaika na kipengele cha pauni milioni 35 katika mkataba wake. (Bild - kwa Kijerumani - usajili unahitajika) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal na Manchester City wamewasiliana na kiungo wa kati wa Newcastle United na Brazil Bruno Guimaraes, 26, kuhusu uwezekano wa uhamisho msimu wa joto. (Caughtoffside) Mkufunzi wa Brentford Thomas Frank ni miongoni mwa makocha wanaotarajiwa kujiunga na Manchester United endapo wataamua kumfuta kazi meneja Erik ten Hag. (Telegraph - usajili unahitajika) Napoli wamempa mkufunzi wa zamani wa Chelsea na Tottenham Antonio Conte pauni milioni 5.6 kwa mwaka kuwa kocha wao ajaye lakini nia ya AC Milan ya kumnunua Muitaliano huyo mwenye umri wa miaka 54 imefifia. (Sport Italia kupitia Football Italia) Chanzo cha picha, Getty Images AC Milan wanamsaka beki mpya na beki wa Tottenham mwenye umri wa miaka 25 wa Brazil Emerson Royal yuko juu kwenye orodha yao ya wachezaji walioteuliwa. (Fabrizio Romano) Manchester United wanamenyana na Newcastle United katika mbio za kumnunua beki wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo, 26. (Talksport) Liverpool wamepewa nafasi ya kumsajili kiungo wa kati wa Nice na Ufaransa Khephren Thuram, 23, kwa pauni milioni 13 msimu huu. (Mirror) Mkufunzi wa Feyenoord Arne Slot anapanga kumfanya meneja wake msaidizi Sipke Hulshoff uteuzi wa kwanza wa wahudumu wake wa klabu ya Liverpool atakaporithi mikoba ya Jurgen Klopp. (ESPN) Chanzo cha picha, Getty Images Wolves wanatarajiwa kumpa meneja Gary O'Neil kandarasi mpya ya miaka mitatu. (i Sport - usajili unahitajika) Juventus wanataka kuachana na meneja Massimiliano Allegri mwishoni mwa msimu huu. (Rudy Galetti) Aston Villa wanataka kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Gabri Veiga baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 wa Al-Ahli kuashiria kuwa ana hamu ya kurejea Ulaya msimu wa joto. (Givemesport) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Klabu za Ligi Kuu ya Saudia (Saudi Pro) zina nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Casemiro, 32, na kiungo wa kati wa Ureno mwenye umri wa miaka 29 Bruno Fernandes. (Telegraph - usajili unahitajika) Arsenal wanakaribia kumpoteza mlinzi Reuell Walters, 19, baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza wa wachezaji wa chini ya miaka 20 kukataa ofa ya kandarasi mpya ili kutafuta nafasi kwingineko. (Athletic- Usajili unahitajika) Real Madrid bado wana nia ya kumsajili mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Trent Alexander-Arnold, 25, kutoka Liverpool. (Fabrizio Romano kupitia Football365) Ripoti za mzozo kuibuka kwa mkubwa kati ya mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 25, na rais wa Paris St-Germain Nasser Al-Khelaifi kabla ya mechi ya Ligue 1 dhidi ya Toulouse zimetupiliwa mbali na vyanzo vya mabingwa hao wa Ufaransa. (Marca kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso anatumai kusimamia klabu zake zote tatu za zamani za Liverpool, Real Madrid na Bayern Munich lakini hana uhakika ni kwa utaratibu gani. (Abendzeitung - kwa Kijerumani) Nia ya Bayern Munich kumnunua mkufunzi wa Crystal Palace Oliver Glasner ilififia baada ya klabu hiyo ya Bundesliga kuambiwa itawagharimu pauni milioni 86 ili kumzawadia kutoka Selhurst Park. (Bild - kwa Kijerumani - usajili unahitajika) Napoli wameanzisha tena mazungumzo na Antonio Conte kuhusu kuwa meneja wao baada ya Muitaliano huyo kupunguza mahitaji yake ya mshahara, huku AC Milan pia ikitaka kuzungumza na kocha huyo wa zamani wa Chelsea na Tottenham. (Il Mattino - kwa Kiitaliano - usajili unahitajika) Chanzo cha picha, PA Media Mlinzi wa zamani wa Sevilla na timu ya taifa ya Uhispania Sergio Ramos, 38, amepiga hatua katika mazungumzo yake klabu ya San Diego FC kuhusu kuhamia Ligi Kuu ya Soka (MLS). (Athletic - Usajili unahitajika) Beki wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza, klabu za ligi kuu ya England Arsenal na Chelsea Ashley Cole, 43, ananyatiwa na klabu kadhaa vya Championship ili kuchukua nafasi ya kocha. (Mirror) Chelsea wanatazamia kusajili mshambuliaji na mabeki wawili msimu huu wa joto huku wakurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Paul Winstanley na Laurence Stewart wakitarajiwa kukabidhiwa tena majukumu yao ya uhamisho. (Telegraph - usajili unahitajika) Chanzo cha picha, Getty Images Winga wa zamani wa Manchester United Nani, 37, anasaka klabu mpya baada ya mkataba wa Mreno huyo katika klabu ya Adana Demirspor ya Uturuki kuvunjwa. (Mirror) Wachezaji kadhaa wa Manchester United hawajashawishika na uwezo wa Rasmus Hojlund wa kufunga mabao hivyo wamekuwa wakisita kumwekea pasi mshambuliaji huyo wa Denmark mwenye umri wa miaka 21 wakati wa mechi. (Manchester Evening News)
2
Chanzo cha picha, Getty Images Wakati Manchester United wakisaka bao la kusawazisha dhidi ya Arsenal siku ya Jumapili, anga ya buluu juu ya Old Trafford ilitoa nafasi ya ngurumo na mvua kubwa. Hali hiyo inaweza kuwa kielelezo kwa msimu wa Man United, ambapo matumaini ya kumenyana na The Gunners pamoja na Manchester City kileleni mwa jedali yamegeuka na kuwa kampeni nyingine ya kukatisha tamaa. Katika miaka ya nyuma, mechi kati ya Manchester United na Arsenal zilikuwa kati ya pande mbili zinazomenyana kileleni mwa jedwali, lakini safari hii jukumu la kikosi cha Erik ten Hag lilikuwa kuwa mharibifu katika mbio za kuwania taji la wapinzani wao, kazi ambayo walishindwa kutimiza. "Hii ni moja ya timu mbaya zaidi za Manchester United kuwahi kutokea," kiungo wa zamani wa Mashetani Wekundu Robbie Savage alisema kwa ukali, huku akitazama timu yake ya zamani ikijaribu bila mafanikio kupata bao la kusawazisha dhidi ya The Gunners. Mwishowe, bao la kipindi cha kwanza la Leandro Trossard lilithibitika kuwa muhimu Arsenal ilipoondoka Old Trafford na pointi tatu ambazo ziliwapandisha kileleni mwa jedwali na kuhakikisha wanapambana na Manchester City kuwania taji la Ligi Kuu hadi siku ya mwisho. "Walionikatisha tamaa haswa nusu saa iliyopita, ilikuwa Manchester United," nahodha wa zamani wa klabu hiyo, Roy Keane, alisema kwenye Sky Sports. "Dhidi ya timu hiyo leo, Arsenal hawakuamini jinsi United ilivyokuwa katika hali mbaya." Chanzo cha picha, Getty Images Katika maelezo yake ya mpango wa kabla ya mechi, Ten Hag alikuwa ameitaka timu yake kuonesha umahiri wao na kurekebisha kichapo cha 4-0 walichokipata dhidi ya Crystal Palace wiki iliyopita. Lakini, kwa Keane, unahiri huo haukuonekana popote. "Ukitazama nusu saa iliyopita - kufanya maamuzi, hakuna mtu anayemlaumu yeyote, watu wanafanya makosa na kuanguka, na kila mtu anaondoka tu, hakuna mtu anayemlaumu mwengine," aliongeza. "Hii ndio ndio timu mbaya zaidi ya United - mbaya sana." Hatahivyo ushindi mwembamba wa Arsenal dhidi ya Man United hauonekani kuwa matokeo mabaya kwa United ilioanza mechi hiyo ikiwa katika nafasi ya 8 na pointi 29 nyuma ya The Gunners. Lakini kilikuwa ni kipigo chao cha 14 msimu huu katika Ligi ya Premia - zaidi ya timu nyingine yoyote ile katika nusu ya juu ya jedwali - ambacho kinawaacha katika hatari ya kutokuwepo tena katika soka ya barani Ulaya msimu ujao. Pia wamepoteza mechi tisa nyumbani Old Trafford muhula huu - nyingi zaidi wakiwa nyumbani kwa msimu mmoja - na wameruhusu mabao 82 katika mashindano yote, ambayo ni mengi kwao tangu 1970-71. "Unapopoteza michezo kwa jinsi Manchester United walivyo kwa sasa kutakuwa na maswali kutoka kwa meneja," mfungaji bora wa klabu hiyo Wayne Rooney alisema kwenye Sky Sports. "Lakini nadhani wachezaji wanatakiwa kujiangalia. Kwa baadhi ya wachezaji inaonekana wanajaribu tu kufikia mwisho wa msimu. "Iwapo wanamchezea Erik ten Hag sidhani kama wanafanya hivyo kwa kweli" Chanzo cha picha, Getty Images Mustakabali wa Ten Hag Old Trafford bado haujulikani. Ana mwaka mmoja kwenye mkataba wake lakini kumekuwa na uvumi unaokua ukiongezeka kwamba mmiliki mwenza Sir Jim Ratcliffe, ambaye alitazama mechi siku ya Jumapili, anaweza kufanya mabadiliko. Kocha huyo wa zamani wa Ajax inaeleweka anaashiria kiasi cha majeraha ambayo timu yake imelazimika kukabiliana nayo msimu huu. "Kila meneja anaweza kufanya vyema kila wakati," alisema baada ya mechi ya Jumapili. "Nimekuwa hapa kwa miaka miwili na mara moja tu nilikuwa na kundi kamili la wachezaji. "'Ni kama kuogelea huku ukiwa umeweka mikono yako mgongoni na inabidi kuweka kichwa chako juu ya usawa wa maji." Licha ya masuala ambayo United imekuwa nayo msimu huu, wanatarajiwa kucheza katika fainali ya kombe la FA. Lakini wapinzani wao katika mchezo huo ni Manchester City na Ten Hag anajua kikosi chake kitahitaji kuonyesha umahiri wa hali ya juu zaidi ikiwa wanataka kumaliza msimu wa kusikitisha wakiwa juu. Imetafsiriwa na Seif Abdalla
2
Chanzo cha picha, Getty Images "Katika soka kila wakati kuna uwezekano." Hayo yalikuwa maneno ya mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta baada ya ushindi wao wa bao 1-0 dhidi ya Manchester United kuwarudisha kileleni mwa jedwali la Ligi ya Premia na kuweka kimyang’anyiro cha kuwania taji hilo kuelekea wiki ya mwisho ya msimu. The Gunners sasa wako pointi moja mbele ya Manchester City wanaoshika nafasi ya pili, ingawa vijana wa Pep Guardiola wana mchezo mmoja mkononi dhidi ya Tottenham siku ya Jumanne. Kwa vyovyote vile matokeo ya mchezo huo kwenye Uwanja wa Tottenham Hotspur, ushindi wa Arsenal katika uwanja wa Old Trafford unahakikisha vita vya kuwania taji hilo vitafikia hadi siku ya mwisho. "Leo tulitaka kufungua lango hilo," Arteta aliambia Sky Sports. "Mbele ya watu wetu tuishi moja ya siku nzuri zaidi ambazo tumeishi pamoja. "Tutakuwa tumekaa tukitazama mechi hiyo [kati ya Tottenham na Manchester City] na ni kweli tunahitaji matokeo ili kafikia lengo letu. Ikiwa timu zitakuwa sawa baada ya mechi 38, taji litaamuliwa kwa tofauti ya mabao na ikiwa bado ni sawa, litaamuliwa kupitia kupitia mabao yaliofungwa. Chanzo cha picha, BBC Sport Kulingana na Opta, nafasi ya Arsenal kushinda Ligi ya Premia sasa iko 41.3%, huku Manchester City ikisalia na 58.7%. The Gunners walikuwa na nafasi ya chini ya 23.6% tu kabla ya mechi ya Jumapili - na baada ya City kushinda 4-0 dhidi ya Fulham - Walidhihirisha umuhimu wa ushindi wao dhidi ya United. Arsenal watawakaribisha Everton siku ya mwisho ya msimu na City watakuwa nyumbani kumenyana na West Ham (wote Jumapili, 19 Mei saa kumi na mbili saa za Afrika Mashariki). Hata hivyo, onyo ni kwamba - hakuna timu katika historia ya Ligi Kuu ambayo imewahi kuanza siku ya mwisho katika nafasi ya pili na kushinda taji. Hilo linawaacha Arsenal katika hali ya kushangaza ya kushangilia wapinzani wao wakubwa Spurs watakapomenyana na mabingwa hao watetezi Jumanne. Kama mshambulizi wa The Gunners, Kai Havertz alivyosema: "Nitakuwa shabiki mkubwa zaidi wa Tottenham ! Hebu tuwe na tumaini." Kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Roy Keane anasema "haoni Manchester City ikizuiwa sasa" licha ya Arsenal kuwasukuma. "Nilihoji Manchester City wiki nne au tano zilizopita, nikifikiri kwamba sina uhakika kabisa wanaweza kusinda taji," alisema kwenye Sky Sports. "Lakini katika wiki chache zilizopita sijui kwa nini niliwatilia shaka. "Hata jana ugenini kwa Fulham, ulikuwa mchezo rahisi na walishinda kwa mabao manne." Mchambuzi mwenzake na mchezaji wa zamani wa Arsenal Paul Merson anaamini mengi yataambatana na matokeo ya Aston Villa dhidi ya Liverpool siku ya Jumatatu, huku Villa wakichuana na Tottenham kuwania nafasi ya nne. Ikiwa Villa itashindwa kuilaza Liverpool, Spurs bado watakuwa na nafasi ya kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa - lakini tu iwapo wataifunga City. "Ikiwa Liverpool wanaweza kuifunga Villa basi hiyo itaifanya Tottenham kuwa na njaa siku ya Jumanne," alisema. "Kila shabiki wa Tottenham atakuwa akiishangilia Liverpool." Lakini ikiwa Villa itafanikiwa kushinda? "Wao [Tottenham] hawataki Arsenal kushinda ligi. Itafikia hatua ambayo mashabiki wa Tottenham watashangilia ikiwa Manchester City watafunga." Sare tatu mfululizo mnamo Aprili 2023 ziliigharimu Arsenal wakati Manchester City iliposhinda taji la msimu uliopita, huku uwezekano wa The Gunners kuwa mabingwa ukididimia. Iwapo kutakuwa na sare, ligi inaamuliwa kwa tofauti ya mabao, kisha mabao yaliofungwa, kisha pointi nyingi katika mechi za ana kwa ana, kisha mabao mengi ya ugenini katika rekodi ya ana kwa ana. Chochote kile, usishangae ikiwa kutakuwa na misukosuko na mabadiliko kati ya sasa na siku ya mwisho ya msimu tarehe 19 Mei. Imetafsiriwa na Seif Abdalla
2
Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wanavutiwa na winga wa Newcastle mwenye umri wa miaka 23 Anthony Gordon, ambaye alianza kucheza soka katika klabu ya Everton. (Star) Mkataba wowote kwa Gordon unaweza kukatiza matumaini ya Arsenal ya kumsajili mshambuliaji wa Newcastle mwenye umri wa miaka 24 raia wa Uswidi Alexander Isak msimu huu wa joto. (Express) Mshambuliaji wa Colombia Luis Diaz, 27, amepuuza tetesi zinazomhusisha na uhamisho wa kwenda Paris St-Germain, akisema "mambo mazuri yanakuja" Liverpool. (Mirror) Sheffield United iko tayari kutoa ofa ya pauni milioni nane kwa mlinda mlango wa Sunderland Muingereza Anthony Patterson, 23. (Sun) Chanzo cha picha, Action Images/Reuters Manchester City wanavutiwa na mlinda mlango wa chuo cha mafunzo ya soka ya Everton mwenye umri wa miaka 16 Douglas Lukjanciks na wanaweza kulipa hadi pauni milioni 10 kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza wa chini ya miaka -17. (Sun) Newcastle wanapigiwa upatu kumsajili mlinzi Tosin Adarabioyo mwenye umri wa miaka 26 kwa uhamisho wa bure mkataba wake wa Fulham utakapokamilika msimu huu wa joto. (Mail) Crystal Palace haitamruhusu meneja wa Austria Oliver Glasner, 49, kuondoka msimu wa joto, licha ya tetesi zinazomhusisha na nafasi ya ukocha mkuu katika klabu ya Bayern Munich. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Mustakabali wa Luka Modric utawekwa wazi "wiki ijayo", asema wakala wake, huku kandarasi ya kiungo huyo wa kati wa Croatia mwenye umri wa miaka 38 katika klabu ya Real Madrid ikikamilika msimu huu wa joto. (Goal) Eintracht Frankfurt haitaanzisha mchakato wa pauni milioni 13 wa kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Uholanzi aliyeko kwa mkopo Donny van de Beek, 27. (Fabrizio Romano) Everton, Brighton, Inter Milan na Wolfsburg wanapania kumnunua beki wa wa AZ Alkmaar wa Japan Yukinari Sugawara, 23. (Florian Plettenberg) Chanzo cha picha, Getty Images Mkufunzi wa Everton Sean Dyche ana matumaini ya kuchunguza mpango wa kubadilisha mkopo wa winga wa Uingereza Jack Harrison kutoka Leeds kuwa uhamisho wa kudumu (Liverpool Echo) West Ham wanapanga kumnunua mshambuliaji wa Sevilla raia wa Morocco, 26, Youssef En-Nesyri msimu wa joto. (Football Insider) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Mabingwa wa Saudi Pro League Al-Hilal wana uhakika wa kumsajili mshambuliaji wa Tottenham na Brazil Richarlison msimu huu, huku Spurs wakiwa tayari kutoa ofa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Mail) Tottenham wanaweza kumbadilisha Richarlison kwa Eberechi Eze wa Crystal Palace, 25, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka Manchester City kwa winga huyo wa England. (Football Insider) Napoli wanamlenga mlinzi wa Tottenham na Romania, Radu Dragusin, ambaye alihamia England mnamo mwezi Januari, lakini Spurs wanataka pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Barcelona na Atletico Madrid wanamlenga mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, huku Manchester United wakiweka dau la pauni milioni 51.7 kwa fowadi huyo. (Marca - in Spanish) Manchester United itafufua uhamisho wa kiungo wa Barcelona Frenkie de Jong, 26, baada ya kushindwa kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi mwaka 2022. (Mundo Deportivo - in Spanish). Meneja Msaidizi Steve McClaren anaweza kubaki Manchester United msimu ujao - hata kama bosi Erik ten Hag na wafanyikazi wengine nyuma ya pazia watafutwa kazi. (Mirror) Chanzo cha picha, Reuters Arsenal imeweka wachezaji saba wa kikosi cha kwanza kuuzwa, wakiwemo wachezaji watatu wa kimataifa wa Uingereza - kipa Aaron Ramsdale, 25, fowadi Eddie Nketiah, 24, na kiungo Emile Smith Rowe, 23. (Mirror). Matumaini ya Arsenal kumsajili kiungo wa kati Mhispania Martin Zubimendi yamefifia baada ya mkufunzi wa Real Sociedad Imanol Alguacil kusema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 hatauzwa msimu huu wa joto. (Metro) Kiungo wa kati wa Ujerumani Pascal Gross, 32, anaweza kuondoka Brighton na kujiunga na Eintracht Frankfurt msimu huu wa joto. (Florian Plettenberg) Chanzo cha picha, PA Media Everton wana nia ya kumsajili fowadi wa Leicester City na Nigeria Kelechi Iheanacho, 27. (Football Insider) Bayern Munich wameonyesha nia ya kumteua mkufunzi wa Crystal Palace Oliver Glasner kama mbadala wa Thomas Tuchel, lakini raia huyo wa Austria, 49, anataka kusalia Selhurst Park. (Sky Sports) Real Madrid itasubiri hadi baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Borussia Dortmund tarehe 1 Juni ili kutangaza kumsajili mshambuliaji wa PSG na Ufaransa Kylian Mbappe, 25 (Athletic - subscription)
2
Chanzo cha picha, Gettu Images Mustakabali wa kiungo wa kati wa Uingereza Jordan Henderson mwenye umri wa miaka 33 katika klabu ya Ajax umetiwa shaka baada ya timu hiyo ya Uholanzi kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo. (Athletic - subscription required) Ripoti zinazomuhusisha kiungo wa kati wa Newcastle Bruno Guimaraes na kuhamia Paris Saint-Germain msimu huu sio sahihi na Timu hiyo ya Ufaransa haina nia ya kumsajili Mbrazil huyo. (Mirror) Meneja Mholanzi Arne Slot anatazamiwa kuhamia katika nyumba ya sasa ya Jurgen Klopp iliyoko Formby atakapomrithi Mjerumani huyo ukufunzi wa Liverpool . (Mirror) Chanzo cha picha, Getty Images Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 25, atakuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi Real Madrid ikiwa atasaini klabu hiyo baada ya kuondoka Paris Saint-Germain . (RMCsport) Kuondoka kwa Mbappe kutaokoa PSG €220m (£189m) licha ya mshambuliaji huyo kuondoka kwa uhamisho huru. (Sky Sports) Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wanaweza kumsajili mshambuliaji wa Algeria mwenye umri wa miaka 24 Mohamed Amoura kutoka Union Saint-Giloise . (TEAMtalk) Mazungumzo kuhusu mkataba mpya kati ya Barcelona na kiungo wao wa kati Mhispania Marc Casado mwenye umri wa miaka 20 yamekuwa yakiendelea tangu Aprili. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Bayern Munich wameanza mazungumzo na aliyekuwa kocha wao mkuu Hansi Flick kuhusu kurejea kwenye uongozi na kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel. (Sky Germany) Barca wanakabiliwa na upinzani kutoka kwa Arsenal na Juventus kwa mkataba na Real Sociedad kumnunua kiungo wa kati wa Uhispania Martin Zubimendi, 25. (Mundo Deportivo - in Spanish) Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea watafanya tathmini ya mwisho wa msimu kufuatia mchezo wao wa mwisho wa ligi msimu huu dhidi ya Bournemouth, ambapo wataamua mustakabali wa meneja Mauricio Pochettino. (Telegraph) Arsenal inamtazama mlinda lango wa zamani na mchezaji wa kimataifa wa Poland Wojciech Szczesny, 34, pamoja na mlinda lango wa Brighton Muingereza Jason Steele na kipa wa Ajax Mjerumani Diant Ramaj wakitafuta atakayeziba nafasi ya Mwingereza Aaron Ramsdale, 25, ambaye anatarajiwa kuondoka The Gunners. (Standard) Arsenal pia wanafikiria kumnunua kipa wa Everton na England Jordan Pickford, 30 katika dirisha la usajili la majira ya joto. (Teamtalk). The Gunners wanalenga kusajili beki, kiungo na mshambuliaji huku wakipania kuimarisha kikosi cha meneja Mikel Arteta. (Standard) Chanzo cha picha, Getty Images Graham Potter amekataa nafasi ya kuwa kocha mkuu wa Ajax , baada ya kuibuka mshindani mkuu wa kuchukua nafasi ya kuongoza miamba hao wa Uholanzi. (Usajili unahitajika) Mshambulizi wa Manchester United Nikita Parris alikataa uhamisho wa kuhamia North Carolina Courage nchini Marekani mwezi Aprili huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 30 akitaka kucheza fainali ya Kombe la FA kwa upande Wanawake Jumamosi dhidi ya Tottenham. (Usajili unahitajika) Bayern Munich wamekuwa wakijadili uwezekano wa kumteua kocha wa zamani wa Ujerumani Hansi Flick kama meneja wao mpya, huku kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 akiwa tayari kurejea katika wadhifa wake wa zamani kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel anayeondoka. (Sky Sports Ujerumani) Beki wa Manchester City na Brazil Yan Couto, 21, ambaye yuko kwa mkopo Girona, anazivutia Bayern Leverkusen , Juventus na vilabu kadhaa vya Ligi Kuu ya England kwa uhamisho wa majira ya joto. (Sports) Eintracht Frankfurt wanataka euro 50-60m kwa mlinzi wa Ecuador mwenye umri wa miaka 22 Willian Pacho, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool. (Sky Sports Ujerumani) Kampuni ya Marekani ya MSP Sports Capital, ambayo ilionyesha nia ya kuinunua Tottenham mwaka jana, inasemekana kuwa inasubiriwa kwa hamu na Toffees ikiwa dili la 777 Group litasambaratika. (Football London) Newcastle United wamefanya mazungumzo ya juu na Dougie Freedman wa Crystal Palace na Johannes Sports, ambaye ni mkurugenzi wa michezo wa kimataifa katika 777 Group kuhusu nafasi ya ukurugenzi wa michezo. (Sky Sports) Manchester City wamekubali mkataba wa kumsaini kiungo wa kati wa Marekani Cavan Sullivan, 14, ambaye amejiunga na klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya Philadelphia Union, baada ya kufikisha umri wa miaka 18. (ESPN). Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Aston Villa wana imani kuwa wanaweza kuzishinda Arsenal na Manchester United katika kumsajili winga Mfaransa Michael Olise, 22, kutoka Crystal Palace. (Football Transfers) Tottenham wako tayari kumpa meneja Ange Postecoglou fedha za kusajili mshambuliaji, beki wa kati na kiungo wa kati msimu huu wa joto. (Times - usajili unahitajika) Takriban vilabu viwili vya Ligi Kuu ya Englang vimetaka maelezo kuhusu uwezekano wa kumsajili Mason Greenwood, 22, lakini mshambuliaji huyo wa Manchester United Muingereza bado ana uwezekano mkubwa wa kuhamia ng'ambo iwapo atauzwa msimu huu wa joto . (Telegraph) Kiungo wa kati wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva, 29, anataka mustakabali wake uwekwe wazi ifikapo mwisho wa Euro 2024 msimu huu wa joto. (Mirror) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United haitamteua atakayeziba nafasi ya meneja Erik ten Hag kwa kuzingatia rekodi yao ya kutwaa mataji pekee, jambo ambalo linaongeza nafasi ya kocha wa sasa wa England Gareth Southgate kuteuliwa kuwa mrithi wake. (Telegraph) Wakati huo huo, kumekuwa na mawasiliano ya awali kati ya United na washauri wa kocha wa Bayern Munich Thomas Tuchel ili kupima nia ya Mjerumani huyo kuhamia Old Trafford. (talkSPORT) Chelsea wamefikia makubaliano ya mdomo kuhusu masuala ya kibinafsi na winga wa Palmeiras mwenye umri wa miaka 17 kutoka Brazil Willian Estevao. (Fabrizio Romano) Kiungo mshambulizi wa zamani wa Borussia Dortmund, Marco Reus, mwenye umri wa miaka 34 ambaye mkataba wake unamalizika majira ya joto, yuko kwenye mazungumzo ya awali kuhusu mkataba na klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya St Louis City (Usajili unahitajika) Chanzo cha picha, Getty Images Galatasaray iko tayari kumsajili winga wa Chelsea Hakim Ziyech kwa mkataba wa kudumu baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Morocco mwenye umri wa miaka 31 kufurahishwa na klabu hiyo ya Uturuki kwa mkopo msimu huu. (Standard) Mshambulizi wa Denmark Martin Braithwaite anaweza kuondoka Espanyol kama mchezaji huru mwezi Julai iwapo klabu hiyo itapanda daraja. Wasipofanya hivyo, kijana huyo mwenye umri wa miaka 32 anaweza kuondoka kwa euro 600,000. (Fabrizio Romano) West Ham wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa timu ya Serie A, Napoli katika harakati zao za kumsaka beki wa kati wa Anderlecht mwenye umri wa miaka 20 na Ubelgiji Zeno Debast. (AreaNapoli kupitia Sport Shahidi) Kocha wa zamani wa Hamburg, Tim Walter, anagombea kuchukua nafasi ya Liam Rosenior katika klabu ya Hull City inayoshiriki Championship . (Sky Sports) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United hawana nia ya kumfukuza meneja Erik ten Hag kabla ya fainali ya Kombe la FA mnamo Mei 25. (Telegraph - usajili unahitajika) Hata hivyo, Mholanzi Ten Hag atafutwa kazi mwishoni mwa msimu huu. (Football Insider) Kocha wa Bayern Munich Thomas Tuchel ana nia ya kuwa meneja wa Manchester United iwapo klabu hiyo itaamua kumfukuza Ten Hag. (Telegraph - usajili unahitajika) Tuchel ndiye mgombea anayeongoza kuchukua mikoba Old Trafford, lakini kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim na meneja wa zamani wa Chelsea Graham Potter pia wako kwenye kinyang'anyiro. (habari) Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa zamani wa Manchester United Jose Mourinho angependa kurejea kwa kipindi cha pili lakini klabu hiyo haitaki kumteua tena Mreno huyo mwenye umri wa miaka 61, ambaye alitimuliwa na Roma mwezi Januari. (Manchester Evening News) Crystal Palace wako tayari kumuuza mlinzi wa Uingereza Marc Guehi, 23, badala ya kumtoa winga wa Ufaransa Michael Olise, 22, au winga wa Uingereza Eberechi Eze, 25, msimu huu. (Givemesport) West Ham wameanza mazungumzo ya kumsajili winga wa Corinthians, 19, raia wa Brazil, Wesley Gassova, ambaye pia analengwa na Liverpool . (Standard) Chelsea inatafuta mnunuzi wa mshambuliaji wa Albania Armando Broja kufuatia kipindi cha mkopo cha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 na Fulham . (Fabrizio Romano) Chelsea wako kwenye mazungumzo ya kumsajili winga Estevao Willian mwenye umri wa miaka 17 kutoka Palmeiras . (Usajili unahitajika) The Blues pia wamemtambua mlinda lango wa Everton Muingereza Jordan Pickford, 30, kama wanayemlenga majira ya joto. (Football Insider) Chanzo cha picha, EPA Newcastle wamefikia makubaliano ya kumsajili beki wa Bournemouth Muingereza Lloyd Kelly, 25. (Foot Mercado - in French) Beki wa kushoto The Magpies na Uingereza Lewis Hall, 19, ameibuka kama nyota anayelengwa na Borussia Dortmund msimu wa joto . (Givemesport) Rais wa Barcelona Joan Laporta amewasiliana na Getafe kuhusiana na hali ya mshambuliaji wa Manchester United Mwingereza anayecheza kwa mkopo Mason Greenwood, 22. (Radio Marca, via Mundo Deportivo - kwa Kihispania). Manchester United inamfuatilia beki wa pembeni wa Uholanzi Denzel Dumfries baada ya mazungumzo ya kandarasi kati ya mchezaji huyo wa miaka 28 na Inter Milan kukwama. (Mchezo) Tottenham itasikiliza ofa kwa mlinzi wa Wales Ben Davies, 31, msimu huu wa joto. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Newcastle na Inter Milan wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Barcelona na Ufaransa Jules Kounde , 25 , ambaye pia amewavutia Chelsea , Manchester United na Paris St-Germain . (Mundo Deportivo - kwa Kihispania) Mshambulizi wa Roma na England Tammy Abraham yuko tayari kurejea kwenye Ligi ya Premia, huku West Ham ikiwa moja ya timu zinazomfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (HITC) Barcelona wanafikiria kumrejesha meneja wa Paris St-Germain Luis Enrique kwenye klabu ili kurithi mikoba ya Xavi mwaka wa 2025. (Sport - in Spanish) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Reuters Mshindi mara mbili wa mbio za marathon katika mashindano ya Olimpiki Eliud Kipchoge anasema alihofia maisha ya familia yake wakati wa kampeni ya unyanyasaji mtandaoni dhidi yake ambayo ilimhusisha kimakosa na kifo cha mwanariadha mwenzake wa Kenya wa mbio za marathon Kelvin Kiptum. Kiptum, mshikilizi wa rekodi ya dunia ambaye alionekana kumaliza ushindi wa Kipchoge zaidi ya maili 26.2, alifariki katika ajali ya barabarani mnamo Februari akiwa na umri wa miaka 24. Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii walianza kukisia kwamba Kipchoge alikuwa sehemu ya njama ya kumuua Kiptum, ambaye alikuwa amepunguza kiwango bora cha dunia hadi saa mbili, sekunde 35 Oktoba iliyopita huko Chicago. "Nilishtuka kwamba watu [kwenye] mitandao ya kijamii wanasema 'Eliud anahusika katika kifo cha kijana huyu'," mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 39 aliiambia BBC Michezo Afrika. "Hiyo ilikuwa taarifa mbaya zaidi kunihusu maishani mwangu. "Niliambiwa mambo mengi mabaya; kwamba watachoma kambi ya (mazoezi), watachoma mali yangu mjini, watachoma nyumba yang, watachoma familia yangu. "Haikufanyika lakini hivyo ndivyo ulimwengu ulivyo." Maoni ya awali ya Kipchoge alipoona uvumi wa uwongo ukisambaa mitandaoni jambo ala kwanza alilofanya ni kuangalia ikiwa familia yake ilikuwa salama. "Sina uwezo wa kwenda kwa polisi na kuwaambia maisha yangu yako hatarini. Kwa hiyo wasiwasi wangu ulikuwa ni kuiambia familia yangu kuwa makini zaidi na waangalifu," alisema. "Nilianza kuwapigia simu watu wengi. "Niliogopa sana watoto wangu kwenda shule na kurudi. "Wakati mwingine wanaendesha baiskeli, lakini tulilazimika kuwazuia kwa sababu huwezi kujua nini kitatokea. Tulianza kuwaacha na kuwachukua jioni. "Msichana wangu alikuwa katika shule ya bweni - hiyo ilikuwa ahueni kwamba hakuwa na ufikiaji wa mitandao ya kijamii, lakini ni ngumu kwa wavulana wangu kusikia 'Baba yako ameua mtu'." Chanzo cha picha, Getty Images Kipchoge alitekwa na hisia wakati wa mahojiano nyumbani kwake mjini Eldoret alipokuwa akielezea jinsi unyanyasaji mtandaoni ulivyomuathiri mama yake mzazi. "Wakati wangu mbaya zaidi ulikuwa (wakati) nilipojaribu kumpigia simu mama yangu," alisema. "Aliniambia 'Jihadhari' na 'Mengi yamekuwa yakiendelea'. "Kwetu nyumbani ni vijijini. Na kwa umri wa mama yangu, niligundua kuwa mitandao ya kijamii umefika kila mahali. "Lakini alinipa ujasiri. Ulikuwa mwezi mgumu sana." Hata hivyo, Kipchoge, ambaye alikua mtu wa tatu kushinda mbio za Olimpiki mfululizo alipotetea taji lake mjini Tokyo mwaka wa 2021, aliamua kutochukua tahadhari kuhusu usalama wake. “Sikuona haja ya kubadili sehemu za kufanyia mazoezi kwa sababu maisha yangu yako wazi,” alieleza. "Mchezo wetu hatufanyi mazoezi katika ukumbi wa kufanyia mazoezi, ni kwenda nje kukimbia. Ninatembea mitaani kwa uhuru." Kipchoge anadai "alipoteza takriban 90%" ya marafiki zake huku kukiwa na kiungo kisicho sahihi cha ajali ya Kiptum na unyanyasaji mtandaoni. "Ilikuwa uchungu sana kwangu kujifunza hata kutoka kwa watu wangu, wale tunaofanya mafunzo pamoja, wale ambao nina mawasiliano nao, na maneno mabaya yanatoka kwao," aliongeza. "Nilisikitika sana kuona hivyo." Chanzo cha picha, Getty Images Timu ya Kipchoge iliamua kumtenganisha na mitandao ya kijamii kufuatia dhuluma hiyo, lakini alisema hakuwahi kufikiria kufuta akaunti zake. “Nikifuta akaunti zangu basi inaonyesha kuna kitu naficha,” alisema. "Nitasalia na akaunti zangu. Sikufanya lolote." Hata hivyo, anaamini matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yaliathiri utendaji wake katika mashindano. Kipchoge aliibuka wa 10 katika mbio za Tokyo Marathon tarehe 3 Machi, matokeo ya chini zaidi tangu aanze mchezo wa riadha mwaka wa 2013, akivuka mstari kwa dakika mbili na nusu nyuma ya mshindi Benson Kipruto. "Nilipokuwa Tokyo sikulala kwa siku tatu," alifichua. "Ilikuwa matokeo yangu mabaya zaidi kuwahi kutokea." Licha ya kushindwa huko aliteuliwa katika timu ya Kenya ya mbio za marathon kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024 wiki iliyopita, na sasa anaangazia kuandikisha historia zaidi katika Michezo hiyo huku akilenga kushinda medali ya tatu mfululizo ya dhahabu. "Inamaanisha kujizoazoa kuamka na kwenda moja kwa moja tena, kwa lengo lako," aliongeza Kipchoge, ambaye mwaka wa 2019 alikuwa mtu wa kwanza kukimbia mbio za marathon chini ya saa mbili, ingawa katika hali zilizodhibitiwa mjini Vienna. "Nataka kuingia katika vitabu vya historia, kuwa binadamu wa kwanza kushinda-mataji mtawalio." Chanzo cha picha, Getty Images Baada ya kukabiliwa na vitisho na unyanyasaji mitandaoni, Kipchoge anaamini kuwa kampuni za mitandao ya kijamii "hazijachukua hatua" kuzuia unyanyasaji kwenye majukwaa yao. “Hawa watu wasio na uso wanachapisha mambo mabaya na ni hatari sana,” alisema. “Ukiripoti baadhi ya akaunti zinachukua muda kuzifungia akaunti hizo. "Wanapaswa kuchukua hatua haraka, kupata ukweli, kufuta akaunti. Watu [wanapaswa] kujua kwamba ikiwa unasema kitu ambacho si kizuri basi akaunti yako itafungiwa." Hata hivyo, Kipchoge amekaribisha tangazo kutoka kwa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC), kwamba inapanga "kuchukua hatua kikamilifu" ili kuwalinda wanariadha dhidi ya unyanyasaji mtandaoni wakati wa Paris 2024. IOC inakusudia kutumia akili bandia kusaidia kutambua machapisho yenye matusi na kuyaripoti kwa makampuni ya mitandao ya kijamii. "Nadhani ni mwelekeo sahihi," alisema. "Sasa wanapiga muhuri mamlaka yao na kazi yao kama shirika linaloshughulikia wanariadha ili kuwalinda dhidi ya unyanyasaji." Lakini, kwa Kipchoge, tayari wamechelewa sana kuepusha majeraha ya kihisia ambayo amekumbana nayo. "Nilijifunza kwamba urafiki hauwezi kudumu milele," alisema. "Nadhani ni bahati mbaya kwamba ilitokea wakati ninasherehekea zaidi ya miaka 20 katika mchezo wa riadha. "Kilichotokea kimenifanya nisimuamini mtu yeyote. Hata kivuli changu mwenyewe, sitakiamini." Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Mshambulizi wa Liverpool na Uruguay Darwin Nunez ameibuka kama lengo kuu la kushtukiza kwa Barcelona, ​​huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 akionekana kama mbadala wa mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski, 35.(Sun) Nunez amechochea uvumi wa kuondoka Liverpool majira ya joto kwa kufuta picha zote za wakati wake Anfield kwenye ukurasa wake wa Instagram. (90min) Mshambuliaji wa England Jadon Sancho, 24, hataki kurejea Manchester United mwishoni mwa muda wake wa mkopo katika klabu ya Borussia Dortmund.(Talksport) Chelsea imezidisha juhudi zao za kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Shakhtar Donetsk wa Ukraine mwenye thamani ya pauni milioni 65 Georgiy Sudakov, 21, ambaye pia anafuatiliwa na Arsenal, Manchester City na Liverpool.Mail) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea pia wanataka kumsajili mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 25, ambaye ana kipengele cha kuachiliwa kwa zaidi ya £100m.(Sky Italia) Kipa wa Atletico Madrid na Slovenia Jan Oblak, 31, ni mchezaji mwingine ambaye yuko kwenye rada ya Chelsea msimu huu wa joto, huku klabu yake ya Uhispania ikitaka kuchangisha fedha kwa ajili ya kujenga upya kikosi.(Fichajes) West Ham United na Tottenham Hotspur ndio walio mstari wa mbele kumsajili mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 28, msimu huu wa joto, huku timu zote zikipanga kutoa takriban £50m.(Football Transfers) Mshambulizi wa Uswidi Viktor Gyokeres, 25, amekataa kutoa hakikisho la kusalia katika klabu ya Sporting Lisbon huku Arsenal kumtaka (Standard) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United inajaribu kutafuta mnunuzi wa kiungo wa kati wa Brazil Casemiro mwenye umri wa miaka 32 msimu huu wa joto ili kujaribu kupunguza mzigo wao mishahara.(TEAMtalk) Arne Slot, ambaye anatarajiwa kuchukua nafasi ya meneja anayeondoka Jurgen Klopp huko Liverpool, anaweza kurejea Feyenoord ili kuwasajili kiungo wa kati wa Uholanzi Mats Wieffer, 24, na mlinzi wa Uholanzi Lutsharel Geertruida, 23.(Football Insider) Sevilla ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia meneja wa Leicester City Enzo Maresca baada ya kocha huyo mwenye umri wa miaka 44 kuiongoza timu hiyo kurejea Premier League.(Mail) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wako tayari kusikiliza ofa za kumuuza mshambuliaji wa Brazil Gabriel Jesus, 27, msimu huu wa joto. (Football Insider) Kiungo wa kati wa Ghana Thomas Partey, 30, na Jesus wanasemekana kuwa kwenye rada za vilabu kadhaa nchini Saudi Arabia huku kandarasi za kiasi kikubwa cha fedha zikiandaliwa kwa wachezaji hao wawili wa Arsenal . (Express) Mustakabali wa mshambuliaji wa Newcastle Callum Wilson bado haujulikani huku Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 32 akihusishwa na uwezekano wa kuondoka St James' Park. (Mirror) Kocha anayeondoka wa Bayern Munich Thomas Tuchel ndiye anayeongoza kuwania nafasi ya meneja ajaye wa Manchester United huku klabu hiyo ya Ligi ya Premia iikilenga kuiziba nafasi ya Erik ten Hag. (Football Insider) Chanzo cha picha, PA Media Borussia Dortmund wanataka kusalia na winga wa England Jadon Sancho, 24, kwa mkopo msimu ujao, lakini uhamisho wa kudumu kutoka Manchester United kwa sasa hauwezekani na gharama yake ni ya juu kwa klabu hiyo ya Ujerumani. (Sky Sport Ujerumani) Manchester United wanatumai kupata pauni milioni 100 kwa kumuuza mshambuliaji Sancho na Muingereza Mason Greenwood, 22, msimu huu wa joto(Give Me Sport) Mshambulizi wa Stuttgart kutoka Guinea Serhou Guirassy, ​​28, ameonekana kulengwa na Arsenal huku Mikel Arteta akijaribu kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. (Fichajes - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Rex Features Matumaini ya kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips kuungana tena na Leeds United msimu huu wa joto yanategemea timu hiyo ya Elland Road kupata nafasi ya kurejea Ligi Kuu ya Uingereza. (Football Insider) Aston Villa wanakaribia kumsajili beki wa Atletico Madrid Mario Hermoso, 28. (AS - kwa Kihispania ) AC Milan wako tayari kufikiria kumsajili mshambuliaji wa Canada Jonathan David, 24, kutoka Lille katika dirisha la usajili la kipindi cha majira ya joto (Calciomercato - kwa Kiitaliano) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Wahasibu wa vilabu vya Premier League hufurahi kuwauza wachezaji – na kuzalisha faida nzuri - na kusaidia kufuata sheria kali za kifedha. Everton, Nottingham Forest na Leicester zote zimekumbwa na ukiukaji wa kanuni za fedha huku vilabu kama Chelsea, Tottenham, Aston Villa, Newcastle na Wolves zikiwa zimepata hasara kubwa katika akaunti zao za hivi karibuni. Baada ya mhitimu wa akademi ya Manchester City, Cole Palmer kuondoka kwenda Chelsea kwa dili la kushangaza la pauni milioni 42.5 msimu uliopita wa joto. Je, tunaweza kuona msururu wa uhamisho kama huu msimu huu wa joto? Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Conor Gallagher ana umri wa miaka 24, kiungo wa kati wa Chelsea. Mkataba wake wa mwaka mmoja unamaliza mwishoni mwa msimu. Sokoni anakadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 68. Anahusishwa na Tottenham. Kabla ya Cole Palmer kuchukua nafasi ya katikati, inaweza kusema alikuwa ni mchezaji bora wa Chelsea kwa msimu. Gallagher amechukua nafasi ya nahodha na amekuwa akisifiwa mara kwa mara na meneja Mauricio Pochettino katika msimu huu. Uchezaji wa Gallagher umewavutia viongozi waandamizi wa klabu hiyo, hasa ikizingatiwa uwekezaji ambao umefanywa katika nafasi anayocheza kwa kumsajili Enzo Fernandez kwa pauni milioni 106 na dili lenye thamani ya pauni milioni 115 kwa Moises Caicedo. Mazungumzo kati ya klabu hiyo na wakala wa Gallagher yamekuwa yakiendelea na Gallagher ana furaha klabuni hapo, lakini inafahamika ikiwa ofa ya bei inayostahili itatolewa, Chelsea watakuwa tayari kumuuza. Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Marcus Rashford, 26, mshambuliaji wa Manchester United. Alisaini mkataba wa miaka mitano hadi 2028 msimu uliopita. Thamani yake sokoni ikakadiriwa kuwa pauni milioni 85. Anahusishwa kuhamia Paris St-Germain. Manchester United wako tayari wako wazi kuuza takribani mchezaji yoyote katika msimu huu wa joto, akiwemo Marcus Rashford . Kampeni ya mwaka jana ya mabao 30 ndiyo iliyomletea mafanikio zaidi, ikifuatiwa na mabao manane pekee msimu huu. Ana kasi na nguvu ya kumaliza ambayo hutishia mabeki wa timu pinzani. Lakini mara nyingi kiwango chake cha uchezaji hushuka. Kama mmoja wa wachezaji wanaopata pesa nyingi zaidi United, kiuhalisia soko la Rashford ni dogo. Inaonekana kuna uwezekano mkubwa atabaki Old Trafford. Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Evan Ferguson, 19, mchezaji wa mbele wa Brighton. Alitia saini mkataba mpya mwaka jana ambao utakamilika 2029. Thamani yake sokoni inakadiriwa kuwa ni pauni milioni 68. Anahusishwa na Arsenal na Chelsea. Evan Ferguson alivutia vilabu vingi vilivyoongoza msimu uliopita, alipoteuliwa kuwania tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi wa PFA. Ulikuwa msimu wa mafanikio kwa mchezaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Ireland huku Brighton ikifuzu kucheza kombea la Ulaya kwa mara ya kwanza. Amefunga mabao sita pekee msimu huu, matatu kati ya hayo aliifunga Newcastle 2 Septemba na safari yake imesita kwa jeraha la kifundo cha mguu. Hata hivyo, bado anavutia na klabu zote zinazoongoza zinatafuta washambuliaji. Swali kubwa ni, Brighton itakuwa tayari kumuuza ikiwa ada itakuwa nzuri? Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Kiernan Dewsbury-Hall, 25, kiungo wa kati wa Leicester. Ana mkataba hadi 2027. Thamani yake inakadiriwa kuwa pauni milioni 35 sokoni. Anahusishwa kuhamia Brentford, Brighton na Fulham. Brighton walihusishwa pakubwa kutaka kumnunua Kiernan Dewsbury-Hall mwezi Januari lakini Leicester walishikilia msimamo na kukataa kumuuza walipokuwa wakitafuta kurejea Ligi Kuu. Uhamisho wa Alex Scott wa pauni milioni 25 kwenda Bournemouth kutoka Bristol City mwaka 2023 na uhamisho wa Adam Wharton wa pauni milioni 22 kutoka Blackburn hadi Crystal Palace mwezi Januari huenda ukawa ndio viwango vya chini zaidi - lakini kwa kuwa Dewsbury-Hall ana uzoefu wa Ligi Kuu ya Uingereza, Leicester huenda ikahitaji pesa zaidi. Amefunga mabao 12 katika mechi 44 na kuisaidia Foxes kushinda taji la Ubingwa na kurudi mara moja kwenye ligi kuu. Klabu hiyo ilirekodi hasara ya pauni milioni 89 mwaka 2022-23 na tayari imeshtakiwa kwa ukiukaji wa kanuni za faida na uendelevu. Watahitaji kuwauza wachezaji kabla ya tarehe 30 Juni ili kujaribu kuzuia kutozwa faini mara ya pili 2023-2024 na Dewsbury-Hall ndiyo atatoa faida nyingi zaidi. Kuhusu mchezaji bora wa mwaka katika tuzo za Leicester za mwisho wa msimu siku ya Jumanne, Dewsbury-Hall alisema: "Nimekuwa katika klabu hii tangu nikiwa na umri wa miaka minane. Sina nia ya kuondoka." Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Jarrad Branthwaite, 21, mlinzi wa Everton. Alisaini mkataba mpya mwezi Oktoba hadi 2027. Thamani yake sokoni inakadiriwa kuwa pauni milioni 43. Anahusishwa kuhamia Manchester United. Jarrad Branthwaite alikuwa akiichezea Carlisle United katika Ligi ya Pili akiwa na umri wa miaka 17, kabla ya Everton kulipa pauni milioni 1 na kuanza kumkuza katika kikosi chao cha chini ya miaka 23. Amekuwa muhimu katika katika msimu mwingine wenye misukosuko kwa Everton kwa kuonyesha utulivu kwenye safu ya ulinzi na kumfanya kuitwa katika kikosi cha England mara kwa mara. Beki huyo wa kati mwenye kasi na mahiri ameunda ushirikiano mzuri na nahodha James Tarkowski katika kikosi ambacho kimecheza mechi 12 bila kufungwa msimu huu. Kwa uchezaji wake wa kuvutia kufikia sasa, Branthwaite atalenga kuwa katika kikosi cha wachezaji 26 cha Gareth Southgate na atakuwa katika nafasi ya kuwania mchezaji bora wa Everton. Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Jacob Ramsey, 22, kiungo wa kati wa Aston Villa. Ana mkataba hadi 2027. Thamani yake sokoni inakadiriwa kuwa pauni milioni 34. Anahusishwa kuhamia Newcastle, Bayern Munich au Tottenham. Jacob Ramsey alishinda tuzo ya akademi ya Ligi ya Kuu ya Uingereza, msimu uliopita baada ya kufunga mabao sita katika michezo 38, na kuisaidia Villa kurejea katika ligi ya Ulaya. Lakini alivunjika uti wa mgongo, jeraha ambalo limemzuia kurudi Ligi Kuu. Villa wamesisitiza hauzwi huku meneja Unai Emery akiweka wazi msimamo wake mwezi Januari. Emery alisema: "Katika sehemu ya pili ya msimu atakuwa muhimu sana kwetu. Uwezo wake ni wa juu sana, na kiwango cha juu zaidi kuliko matarajio yangu." Hata hivyo, kumuuza mchezaji huyo kungesaidia klabu katika juhudi zao za kufuata faida baada ya kupoteza pauni milioni 119.6 mwaka unaoishia Mei 31, 2023. Imetafsiriwa na Rashid Abdallah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Manchester United Erik ten Hag ndiye anayetarajiwa kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel anayeondoka Bayern Munich. (Falk Christian) Mshambuliaji wa Liverpool na Uruguay Darwin Nunez, 24, analengwa na Barcelona msimu huu kama mbadala wa mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski, 35. (Sun). Man United wanasubiri ofa kwa winga wa Brazil Antony, 24, huku wakitafuta nafasi katika kikosi chao kumnunua kiungo wa kati wa kimataifa wa Ufaransa na Crystal Palace aliyezaliwa Uingereza Michael Olise, 22. (Rudy Galetti). Arsenal wana makubaliano ya mazungumzo na Brentford kukamilisha usajili wa kudumu wa mlinda lango wa Uhispania David Raya, 28, msimu huu kwa pauni milioni 27. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wana matumaini kuwa meneja msaidizi Pep Lijnders, ambaye anatazamiwa kuondoka msimu huu pamoja na meneja Jurgen Klopp, watarejea Anfield siku zijazo. (Mirror) Manchester United inanuia kumtumia mlinzi wa Uingereza Harry Maguire, 31, kama chambo cha kuwashawishi Everton kumuuza mlinzi wa Uingereza Jarrad Branthwaite, 21, msimu huu. (Star) Mkufunzi wa Palmeiras Abel Ferreira anataka rais wa klabu Leila Pereira kuzuia kuuzwa kwa winga wa Brazil Estevao Willian mwenye umri wa miaka 17 kwa Chelsea, ambao wameweka mezani ofa ya euro 55m (£47m). (Goal) Kocha wa zamani wa Chelsea Graham Potter yuko katika kinyang'anyiro cha kuwa meneja wa Ajax baada ya mabingwa hao mara nne wa Uropa kukata tamaa ya kurejea tena kwa Ten Hag wa Manchester United. (De Telegraaf) Chanzo cha picha, Getty Images Getafe wameanza mazungumzo na Manchester United kuhusu uwezekano wa kusaini mkataba mwingine wa mkopo kwa mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22. (Subscription Required) Mshambulizi wa Juventus na Serbia Dusan Vlahovic, 24, anavutiwa na Arsenal huku Mikel Arteta akijaribu kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. (Tuttosport – In Itali) Beki wa Uingereza Jarell Quansah, 21, yuko mbioni kupata kandarasi mpya ya muda mrefu baada ya kuonyesha kiwango kizuri msimu wake akiwa Liverpool. (Mirror) Inter Milan wako tayari kumenyana na Manchester United na Arsenal katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Bologna Mholanzi Joshua Zirkzee, 22. ( 90 min)
2
Chanzo cha picha, Getty Images Kocha wa zamani wa Bayern Munich wa Chelsea Thomas Tuchel ni miongoni mwa orodha ya Manchester United ya watu wanaoweza kuchukua nafasi ya Erik ten Hag iwapo Mholanzi huyo ataondoka msimu wa joto. (Times) Lakini Tuchel amefungua milango ya kusalia Bayern Munich baada ya msimu huu licha ya kutangazwa Februari kwamba ataondoka. (Florian Plettenburg) Meneja wa Arsenal Mikel Arteta amemfanya mshambuliaji wa Newcastle na Sweden Alexander Isak, 24, kuwa shabaha yake kuu msimu huu wa joto. (Independent) Arsenal wameanza mazungumzo ya kandarasi na mlinzi wa kati wa Brazil Gabriel, 26, katika jitihada za kupigana na klabu kubwa za Ulaya. (Football Insider) Makamu wa rais wa Inter Milan Javier Zanetti amependekeza kuwa mabingwa hao wa Serie A huenda wakashindana na Manchester United na Arsenal katika kuinasa saini ya mshambuliaji wa Bologna Mholanzi Joshua Zirkzee mwenye umri wa miaka 22. (Mirror) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United imefanya mawasiliano na wakala wa kiungo wa kati wa kimataifa wa Ufaransa Adrien Rabiot, 29, ambaye mkataba wake na Juventus unakamilika msimu huu wa joto. (Team Talk) Mlinzi wa kati wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo, 26, anaelekea kujiunga na Newcastle mkataba wake utakapokamilika msimu wa joto. (Mail) Everton wanatumani ya kumshawishi Jarrad Branthwaite, 21, kusalia Goodison Park kwa mwaka mmoja zaidi lakini Manchester United wana imani kwamba dau la £60-70m kwa beki huyo wa kati wa Uingereza litakubaliwa. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Tottenham itasikiliza ofa kwa mshambuliaji wa Brazil Richarlison, 26 msimu huu wa joto. (Telegraph) Real Madrid imefanya uchunguzi kwa River Plate kuhusu kiungo wa kati wa Argentina mwenye umri wa chini ya miaka 20, Franco Mastantuono, 16. (Fabrizio Romano) Barcelona wamemfanya kiungo wa kati wa Arsenal na Ghana Thomas Partey, 30, kuwa mlengwa wao mkuu katika usajili msimu huu. (Caught offside) Manchester City wanafikiria kumnunua mlinda mlango wa Lazio Christos Mandas, huku Manchester United pia ikimtaka mlinda mlango huyo wa Ugiriki mwenye umri wa miaka 22. (Corriere dello Sport) Chanzo cha picha, Getty Images Inter Miami wako kwenye mazungumzo ya kumleta kiungo wa kati wa zamani wa Real Madrid na Argentina Angel Di Maria, 36, kwenye orodha ya Ligi Kuu ya Soka. (ESPN Argentina)
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wako mbioni kumsajili kiungo wa kati wa Crystal Palace na Ufaransa chini ya umri wa miaka 21 Michael Olise, 22. (ESPN) Juventus wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili mashambuliaji wa Manchester United na Uingereza Mason Greenwood, 22, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya Getafe ya Uhispania. (i Sport) Kocha wa Barcelona Xavi ameiambia klabu hiyo kwamba anamtaka kiungo wa kati wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva, 29, lakini Bayern Munich pia wanamtaka. (Sport - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea wanafikiria kumnunua mlinda lango wa Poland Wojciech Szczesny, 34 - mlinda mlango wa zamani wa Arsenal ambaye sasa anachezea Juventus. (Tutto Juve - kwa Kiitaliano) Chelsea wameungana na Newcastle kuulizia hali ya mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uingereza Tosin Adarabioyo, 26, ambaye ataondoka Fulham kama mchezaji huru msimu huu wa joto. (Fabrizio Romano) Manchester City walikuwa miongoni mwa timu zilizomchunguza beki wa Borussia Dortmund Mholanzi Ian Maatsen, 22. (TBR Football) Chanzo cha picha, Getty Images Mshambuliaji wa Brazil Gabriel Jesus, 27, yuko tayari kupigania nafasi yake katika klabu ya Arsenal huku kukiwa na tetesi zinazoashiria mchezji huyo anaweza kuondoka majira ya kiangazi. (Sun) Meneja wa Brighton Roberto de Zerbi asalia kwenye orodha ya kocha wa Bayern Munich baada ya Ralf Rangnick kukataa ofa ya klabu hiyo ya Ujerumani. (Bild - kwa Kijerumani) Leicester City wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Coventry City Muingereza Callum O'Hare, 26. (Football Insider) Beki wa kati wa Aston Villa na Brazil Diego Carlos, 31, ni mmoja wa walengwa wakuu wa AC Milan. (Team Talk) Chanzo cha picha, Getty Images Brighton, Fulham, West Ham na Benfica wanamfuatilia winga wa Vitoria de Guimaraes na Ureno Jota Silva, ambaye ana kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 17. (Rudy Galetti) Villa wanataka kumsajili shambuliaji wa Leicester na Nigeria Kelechi Iheanacho, 27, kama mshambuliaji msaidizi wa mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Ollie Watkins, 28. (Football Insider) Inter Miami wameanza mazungumzo na winga wa Benfica mwenye umri wa miaka 36 na Argentina Angel di Maria. (ESPN Ajentina - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wako tayari kupokea ofa ya kumuuza mshambuliaji wao wa Brazil Gabriel Jesus, 27, wakati wa majira ya joto ya msimu huu. (Athletic- Usajili unahitajika) The Gunners wana matumaini kuwa kiungo wa kati wa Italia Jorginho, 32, atapuuza nia ya Juventus, Lazio na Napoli kutaka kumsajili na kusaini mkataba wa nyongeza. (Standard) Brighton watajaribu kumnunua Kieran McKenna kutoka Ipswich Town ikiwa meneja Roberto de Zerbi ataondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Tottenham wanawasaka kiungo wa kati wa Chelsea na England Conor Gallagher, 24, pamoja na mshambuliaji wa Feyenoord mwenye umri wa miaka 23 na Mexico Santiago Gimenez msimu huu wa joto, huku pia wakimfuatilia mlinzi wa Bournemouth Muingereza Lloyd Kelly, 25. (Telegraph - usajili unahitajika). Everton huenda wakalazimika kumuuza mlinda lango wa England Jordan Pickford, 30, iwapo pendekezo lao kununuliwa na wamiliki wapya 777 Partners litaporomoka. (Talksport) Arsenal, Bayern Munich na Newcastle ni miongoni mwa klabu zilizopewa nafasi kubwa ya kumsajili kiungo wa kati wa Everton na Ubelgiji Amadou Onana, 22. (Football Transfers) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanapanga kubaki na kocha wao Erik ten Hag msimu ujao kwa sababu ya kukosekana kwa mbadala wake, pamoja na gharama ya kumuondoaMholanzi huyo. (Athletic - Usajili unahitajika) Kiungo wa kati wa Manchester United na Ureno Bruno Fernandes, 29, anasema mustakabali wake Old Trafford utategemea ikiwa klabu hiyo itamtaka abaki. (Telegraph - usajili unahitajika) Newcastle United haitashinikizwa kumuuza kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes, 26, chini ya kifungu chake cha pauni milioni 100 au kuachana na mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, 24. (i Sport) Chanzo cha picha, Getty Images Newcastle wanakaribia kumsajili beki wa Fulham mwenye umri wa miaka 26 Tosin Adarabioyo kwa uhamisho wa bure. (Sun) Adarabioyo, ambaye pia anawaniwa na AC Milan, Manchester United na Liverpool, ameifahamisha Fulham kwamba hatasaini mkataba mpya wakati mkataba wake wa sasa utakapokamilika msimu huu wa joto. (Mail) Borussia Dortmund wanafikiria kumrejesha kocha wa zamani Jurgen Klopp kama mkuu wa soka mwaka 2025 baada ya meneja huyo wa Liverpool kuondoka Anfield mwishoni mwa msimu huu. (Independent) West Ham wanamtarajia kiungo wa kati wa Ghana Mohammed Kudus, 23, kiungo wa kati wa Brazil Lucas Paqueta, 26, na kiungo wa kati wa Mexico Edson Alvarez, 26, kushinikiza kuondoka katika klabu hiyo msimu huu. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Fluminense wamewasilisha pendekezo rasmi la kutaka kumsajili beki wa Brazil Thiago Silva baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 kutangaza kuwa ataondoka Chelsea mwishoni mwa msimu huu. (Fabrizio Romano) Meneja msaidizi wa Feyenoord Sipke Hulshoff, mkuu wa utendaji Ruben Peeters na mchambuzi Etienne Reijnen wamekubali kumfuata kocha Arne Slot kwenda Liverpool. (Football Insider) Everton inawafuatilia beki wa Hull City Muingereza Jacob Greaves, 23, na mshambuliaji wa Blackburn Rovers' Jamhuri ya Ireland Sammie Szmodics, 28. (Football Transfers) Beki wa Barcelona na Uruguay Ronald Araujo, 25, anatathmini iwapo atasaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Uhispania huku Manchester United na Bayern Munich zikiwa na nia ya kumsajili. (Sport - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United haitarajii klabu yoyote kufikia thamani ya £70m ya mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 26, msimu huu wa joto. (ESPN) Paris St-Germain wamepiga breki nia yao ya kutaka kumnunua Rashford na watafuatilia malengo mengine ya uhamisho kabla ya dirisha la kiangazi. (i Sport) Wakati huo huo, kocha wa United Erik ten Hag, 54, hajui kama atakuwa kocha wa Old Trafford msimu ujao. (HITC) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wamempa kiungo wa Italia Jorginho mkataba mpya na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 anatarajiwa kuusaini. (Athletic- Usajili unahitajika) West Ham itakabiliwa na ushindani kutoka kwa AC Milan kumnunua kocha wa Lille Paulo Fonseca huku mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 51 akionekana kuchukua nafasi David Moyes wa Hammers. (i Sports) Moyes, 61, anawaniwa na Spartak Moscow huku kukiwa na suitafahamu juu ya mustakabali wake katika klabu ya West Ham. (Mail) Chanzo cha picha, Getty Images Mshambulizi wa Chelsea na England Raheem Sterling, 29, hajawasiliana na Ligi ya Saudi Pro kuhusu uhamisho wa majira ya kiangazi, hata hivyo, The Blues watakuwa tayari kumuuza mshambuliaji wa Ubelgiji kwa mkopo Romelu Lukaku, 30, kwao. (Caughtoffside) Kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 29, amedokeza kuwa atafikiria mustakabali wake Manchester United baada ya Euro 2024, lakini kwa sasa anaangazia fainali ya Kombe la FA na dimba nchini Ujerumani msimu huu wa joto. (Danz Ureno - kwa Kireno) Vilabu kadhaa nchini Saudi Arabia vinavutiwa na mshambuliaji wa Barcelona mwenye umri wa miaka 21 Ansu Fati, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Brighton, na mlinzi wa zamani wa Ufaransa Clement Lenglet, 28, ambaye yuko Aston Villa kwa mkopo . (Sport - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United bado wanapanga kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Mason Greenwood, 22, msimu huu wa joto, na uamuzi wa mwisho kufanywa mwishoni mwa msimu. (Fabrizio Romano) Chelsea wamekanusha kuwa walilipia ndege ya Ruben Amorim kuelekea London wiki iliyopita, au kwamba walikuwa na mikutano yoyote na bosi huyo wa Sporting Lisbon mwenye umri wa miaka 39. (Matt Law, Telegraph, kupitia X) Borussia Dortmund wanataka kumbakisha Ian Maatsen katika klabu hiyo zaidi ya msimu huu kufuatia winga huyo wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 22 kufanikiwa kwa mkopo kutoka Chelsea. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Leicester wamefanya mazungumzo na mshambuliaji wa Uingereza Jamie Vardy mwenye umri wa miaka 37 kuhusu kuongeza muda wake wa kusalia katika klabu hiyo. (Mail) Crystal Palace huenda wakamuuza kiungo wa kati wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Ireland ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 Killian Phillips, 22, katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (Team Talk) Kiungo wa kati wa Uingereza Callum O'Hare, 25, ambaye anawaniwa na Aston Villa na West Ham, ameiambia Coventry City kuwa ataondoka katika klabu hiyo kwa uhamisho wa bure msimu huu wamajira ya joto. (Football Insider) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wanatarajia Mohamed Salah atasalia katika klabu hiyo na wanataka mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Misri mwenye umri wa miaka 31 kuwa sehemu ya kikosi chao msimu ujao. (The Athletic-Usajili unahitajika) Mkurugenzi wa michezo wa Liverpool ajaye, Richard Hughes ataongoza mazungumzo kuhusu mkataba mpya wa Salah, ambaye mkataba wake wa sasa utaendelea hadi 2025. (Times - usajili unahitajika). Marcus Rashford atakabiliwa na mtihani wa kuamua klabu atakayohamia iwapo ataamua kuondoka Manchester United, huku Paris St-Germain wakisitisha nia yao ya kumnunua mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 26. (i) Chanzo cha picha, Getty Images Beki wa Crystal Palace mwenye thamani ya pauni milioni 55 kutoka Uingereza Marc Guehi, 23, ananyatiwa na Liverpool huku klabu hiyo ikimtafuta mbadala wa mlinzi wa Cameroon Joel Matip, 32, ambaye anatazamiwa kuondoka mkataba wake utakapokamilika msimu wa joto. (Football Insider) Ajax wana nia ya kumteua tena Erik ten Hag kama kocha wao iwapo ataondoka Manchester United msimu huu wa joto. (Mail) Nia ya West Ham kumnunua mkufunzi wa zamani wa Uhispania Julen Lopetegui imesitishwa baada ya kujua kwamba AC Milan ina mashaka kuhusu kumteua kama mbadala wa Stefano Pioli. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images The Hammers pia wanataka kuwasajili winga wa Coventry Callum O'Hare mwenye umri wa miaka 25 na mlinzi wa Hull Muingereza Jacob Graves msimu huu wa joto. (Guardian) Leicester wataweza kuwasajili wachezaji wakati dirisha la usajili la majira ya kiangazi litakapofunguliwa licha ya kuwekewa vikwazo na Ligi ya Soka ya Uingereza. (Mail) Hata hivyo, Foxes watalazimika kuwauza wachezaji kabla ya Juni 30 ili kuepuka malipo ya sheria ya faida na uendelevu (PSR) msimu ujao huku kiungo wa kati wa Uingereza Kiernan Dewsbury-Hall, 25, akiwaniwa na Brentford, Brighton na Fulham. (Mail) Manchester United bado wanapanga kumteua Dan Ashworth kama mkurugenzi wa michezo msimu huu huku wakitarajia kwamba makubaliano ya kulipwa fidia na Newcastle yatakubaliwa hivi karibuni. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Mshambulizi wa zamani wa Uingereza Jermain Defoe, 41, huenda akapata nafasi yake ya kwanza ya umeneja baada ya kufanya mazungumzo na klabu ya zamani ya Sunderland. (Sun) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen ataondoka Napoli msimu huu wa joto, huku Chelsea na PSG zikitarajiwa kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Gazetta - kwa Kiitaliano) Crystal Palace wanahofia kwamba beki wa England mwenye thamani ya pauni milioni 55 Marc Guehi huenda akaondoka msimu huu, huku Manchester United na Arsenal wakimwania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23. (Times - usajili unahitajika) Borussia Dortmund itajaribu kubadilisha mkataba wa mkopo wa winga wa Uingereza Jadon Sancho, 24, kutoka Manchester United kuwa mkataba wa kudumu msimu huu. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wanajiandaa kupokea dau la hadi pauni milioni 150 kutoka kwa vilabu vya Saudi Arabia kumnunua mshambuliaji wa Misri mwenye umri wa miaka 31 Mohamed Salah. (Football Insider) Beki wa Uholanzi Lutsharel Geertruida, 23, anaweza kuondoka Feyenoord pamoja na kocha Arne Slot kujiunga na Liverpool baada ya mlinzi huyo kuonekana uwanjani wakati wa mechi ya Jumamosi yao Reds dhidi ya West Ham Jumamosi. (Express) Mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski anataka kusalia Barcelona msimu huu wa joto, licha ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 kunyatiwa na klabu za Saudi Arabia. (Sport - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Reuters Arsenal, Liverpool na Manchester United wanavutiwa na kiungo wa kati wa Brighton raia wa Cameroon Carlos Baleba, 20. (Caught Offside) Leeds wanataka kumsajili beki wa Liverpool Muingereza Nat Phillips, 27, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Cardiff. (Mirror, kupitia Yorkshire Post) Beki wa kati wa Brazil Thiago Silva anataka kuondoka Chelsea mwishoni mwa msimu huu huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 akihusishwa na Fluminense. (TEAMtalk) Everton huenda ikalazimika kumuuza beki wa Uingereza Jarrad Branthwaite mwenye umri wa miaka 21 ili kutii sheria za Usawa wa Fedha michezoni, na hivyo kufungua mlango wa kuhamia Manchester United. (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wameanza mazungumzo juu ya mkataba mpya na beki wa Brazil mwenye umri wa miaka 26 Gabriel. (Fichajes - kwa Kihispania) Arsenal na Borussia Dortmund wanavutiwa na kiungo wa kati wa Barcelona Mhispania Brian Farinas mwenye umri wa miaka 18. (Caught Offside) Blackburn wanataka hadi pauni milioni 20 kumnunua mshambuliaji wa Jamhuri ya Ireland Sammie Szmodics, huku Brentford, Luton na Sheffield United wakimwania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Sun) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Bayern Munich wanapanga uhamisho mwingine wa kumnunua mlinzi wa Manchester City Muingereza Kyle Walker, baada ya kushindwa kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 msimu uliopita wa joto. (Star) Mmiliki mwenza wa Manchester United Sir Jim Ratcliffe amekutana na wakala bora Jorge Mendes, ambaye wateja wake ni pamoja na mmoja wa walengwa wa klabu hiyo katika kiungo wa kati wa Benfica na Ureno Joao Neves, 19. (Mirror) Crystal Palace wako tayari kujiunga na mbio za kumsajili beki wa kati wa Wolfsburg Mfaransa Maxence Lacroix mwenye umri wa miaka 24 msimu huu wa joto. (Telegraph ) Chanzo cha picha, Getty Images Arne Slot atateuliwa kuwa kocha mkuu wa Liverpool badala ya kuwa meneja katika mabadiliko ya muundo wa klabu. (Times) Matumaini ya West Ham ya kumteua kocha wa zamani wa Wolves Julen Lopetegui kuchukua nafasi ya David Moyes kama meneja msimu huu yanaonekana kukamilika huku AC Milan wakikaribia kuafikiana. (Guardian) Barcelona wanakaribia kumsajili kiungo wa kati wa Argentina Guido Rodriguez, 30, kutoka klabu nyingine ya La Liga ya Real Betis.(Sport - in Spanish). Chanzo cha picha, Getty Images Barcelona wanapanga kulinda mustakabali wa mlinzi wa kati Pau Cubarsi mwenye umri wa miaka 17 baada ya kupendekeza mkataba mpya kwa Mhispania huyo ambao unajumuisha kipengele cha kutolewa cha €500m (£423.2m). (AS) Kiungo wa zamani wa Manchester United na Uhispania Juan Mata, 35, anaamini kuwa klabu yake ya zamani inapaswa kujenga timu yoyote ya baadaye karibu na Bruno Fernandes wa Ureno, 29. (ESPN) Kipa wa Ujerumani Loris Karius, 30, ataondoka Newcastle United kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu. (Fabrizio Romano) Juventus wanashughulikia mikataba ya kuongeza kandarasi za mshambuliaji wa Italia Federico Chiesa, 26, na mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 24. (Rudy Galetti). Juventus wanashughulikia mikataba ya kuongeza kandarasi za mshambuliaji wa Italia Federico Chiesa, 26, na mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 24. (Rudy Galetti).
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wako tayari kumwachia mlinzi wa zamani wa Ufaransa Raphael Varane, 31, kuondoka bure mkataba wake utakapokamilika msimu huu wa joto. (Mirror) Barcelona wanatazamia kuimarisha safu yao ya mashambulizi huku mshambuliaji wa Liverpool na Colombia Luis Diaz, 27, akiwa mmoja wa walengwa wao wakati The Reds "wakiishiwa na subira" na uchezaji wake. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania) Beki wa Cameroon Joel Matip, 32, ni mchezaji mwingine ambaye anaweza kuondoka Liverpool msimu huu wa joto huku Roma na Lazio zikimwania. (Corriere - kwa Kiitaliano) Chanzo cha picha, Action Images/Reuter Manchester United inatarajia wachezaji kadhaa kuondoka majira ya joto ili kukidhi mahitaji ya usawa wa kifedha michezoni, huku mustakabali wa mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 26, ukizingatiwa. (Express) AC Milan wanavutiwa na beki wa Aston Villa Mbrazil Diego Carlos, 31, baada ya kufanya vyema aliporejea kutoka kwa jeraha la Achilles. (Sport - via TeamTalk) Beki wa Fulham Tosin Adarabioyo, 26, ameiambia klabu hiyo kuwa anakusudia kuondoka kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto, huku Liverpool, Tottenham na Newcastle zikivutiwa na Muingereza huyo. (Express) Chanzo cha picha, Getty Images Winga wa Brighton na Japan Kaoru Mitoma, 26, ananyatiwa na klabu za Arsenal, Manchester City na Manchester United. (Fichajes - via 90 min) Paris St-Germain wanakabiliwa na kizingiti katika jaribio lao la kumsajili kinda wa Barcelona na Uhispania Lamine Yamal, 16, huku wakala wa kinda huyo akiiambia klabu hiyo hauzwi. (AS - kwa Kihispania) Klabu za Arsenal na Tottenham Hotspur zinatazamia kumsajili kiungo wa West Ham aliyewahi kuchezea timu ya Uingereza ya wachezaji wa chini ya miaka 16 Daniel Rigge, 18. (ESPN) Bayern Munich wamethibitisha kuwa wanafanya mazungumzo na kocha wa zamani wa Manchester United Ralf Rangnick kuchukua nafasi ya Thomas Tuchel kama mkufunzi. (Goal) Chanzo cha picha, Getty Images Kocha wa zamani wa Chelsea na Tottenham Antonio Conte amefikia makubaliano ya mkataba wa miaka mitatu kuchukua nafasi ya meneja wa Napoli. (Rai kwa Kiitaliano) Real Madrid hawana mpango wa kumnunua mlinzi wa Bayern Munich Alphonso Davies, 23, msimu huu wa joto lakini wana nia ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Canada bila malipo kandarasi yake itakapokamilika 2025. (Relevo - kwa Kihispania). Arsenal wameanza mazungumzo ya kumpa mkataba mpya beki wa Brazil Gabriel Magalhaes, 26, baada ya kuwa na msimu wa mchezo mzuri. (Mirror) Chanzo cha picha, Getty Images Beki wa Barcelona Pau Cubarsi, 17, amepewa mkataba wa miaka mitano ambao anatarajiwa kutia saini atakapofikisha umri wa miaka 18 mwezi Januari, licha ya kutakiwa na Manchester City. (AS - kwa Kihispania) Bologna bado wana matumaini ya kuongeza mkataba wa kocha Thiago Motta baada ya Juni 2024 licha ya Juventus na Manchester United kumtaka Mbrazil huyo mwenye umri wa miaka 41. (Gazzetta dello Sport, kupitia Football Italia) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Winga wa Crystal Palace Mfaransa Michael Olise, 22, atakuwa tayari kuhamia Manchester United msimu ujao.(90min) Manchester United wana imani dau la kati ya £60-70m litatosha kumsajili beki wa Uingereza Jarrad Branthwaite, 21, kabla ya Juni 30, na hivyo kuiruhusu Everton kujumuisha ada hiyo katika akaunti zao za 2023-24 na kuepuka kukatwa pointi zaidi. (Football Insider) Arsenal na Manchester City wamefahamishwa kuwa Newcastle United wako tayari kusikiliza ofa zinazozidi thamani ya £80m kwa kiungo wa kati wa Brazil Bruno Guimaraes, 26, msimu huu ujao. (90min) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanaweza kuanza kusaka usajili wa beki wa kushoto wa Uhispania Miguel Gutierrez, 22, kutoka Girona lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Arsenal na West Ham . (GiveMeSport) Kifungu cha kutolewa cha Guimaraes cha pauni milioni 100 kitaanza kutumika kwa mwezi mmoja pekee, kuanzia mwishoni mwa Mei hadi mwishoni mwa Juni.(Fabrizio Romano, via Caught Offside) Arsenal wanafuatilia wachezaji wengi wanaolengwa katika safu ya kati huku kukiwa na wasiwasi kwamba mkataba wa kiungo wa kati wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi, 25, unaweza kuwa mgumu kufikiwa.(Standard) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United itamlenga beki mpya wa kati, kiungo wa kati na mshambuliaji katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi, huku mshambuliaji wa Ufaransa Anthony Martial, 28, akiwa miongoni mwa wachezaji ambao hawapo tena katika mipango ya klabu hiyo. (Football Insider) Zubimendi anasema ripoti zinazomhusisha na baadhi ya vilabu vikubwa barani Ulaya "ni uvumi tu" na ana furaha Real Sociedad. (Marca - in Spanish)) Meneja wa Wolves Gary O'Neil huenda akasaini mkataba mpya huko Molineux licha ya ripoti zinazomhusisha na kazi ya Liverpool .(GiveMeSport) Ajax wana nia ya kumteua meneja wa zamani wa Chelsea na Brighton Graham Potter, ambaye pia yuko kwenye orodha ya Manchester United ya watu wanaoweza kuchukua nafasi ya Erik ten Hag. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Potter amekataa ofa ya kwanza kutoka kwa Ajax kwa sababu mshahara uliopendekezwa haukukidhi matarajio yake. (Het Parool - in Dutch) Manchester United, Paris St-Germain na Bayern Munich zote zinavutiwa na mlinda mlango wa Real Madrid raia wa Ukrain Andriy Lunin, 25. (Fichajes - in Spanish) Meneja wa zamani wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer na mkufunzi wa zamani wa Leeds United Jesse Marsch wamewasiliana na Canada kuhusu kuiongoza timu ya taifa katika Kombe la Dunia la 2026. (Standard) Napoli wamejiunga na kinyang'anyiro cha kumsajili fowadi wa Canada Jonathan David, 24, kutoka Lille . (Calciomercato - in Italian) Klabu ya Bundesliga Stuttgart iko tayari kufanya uhamisho wa fowadi wa Ujerumani Deniz Undav, 27, kuwa wa kudumu baada ya kumsajili kwa mkopo kutoka Brighton msimu uliopita wa joto. (Caught Offside)
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanavutiwa na mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney na wanaamini kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ataleta uzoefu na uongozi kwenye kikosi chao (90min) Hata hivyo, Tottenham wanaweza kumnunua Toney iwapo kutakuwa na ushindani wa kutosha kuipata sahihi yake na kutoa pauni milioni 45. (GivemeSport) Manchester United inalenga kuwaachilia wachezaji 12 msimu huu wa joto, akiwemo fowadi wa Uingereza Marcus Rashford, 26, na kiungo wa kati wa Brazil Casemiro, 32. (Mirror). Mustakabali wa Mauricio Pochettino kama meneja wa Chelsea upo katika mizani na unaweza kutegemea iwapo anaweza kufuzu kwa shindano la Uropa kwa msimu ujao(Times) Chanzo cha picha, Getty Images Mshambulizi wa Napoli Victor Osimhen, 25, anakaribia kujiunga na Paris Saint-Germain , lakini mshambuliaji huyo wa Nigeria pia ameivutia Chelsea . (Il Mattino - kwa Kiitaliano) Newcastle United wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa kati wa Sporting Lisbon mwenye umri wa miaka 20 Ousmane Diomande, ambaye ana kipengele cha kutolewa cha euro 80m (£68.7m). (A Bola - kwa Kireno) Tottenham wako katika nafasi nzuri ya kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, kutoka Chelsea msimu huu - licha ya kumezewa mate na Newcastle. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wanahusishwa na kutaka kumnunua beki wa kushoto wa Real Madrid Ferland Mendy, 28, huku Liverpool, Manchester United na Newcastle pia wakimtaka Mfaransa huyo. (L'Equipe - kwa Kifaransa) Meneja wa Aston Villa Unai Emery anashinikiza klabu hiyo kumsajili winga wa Athletic Bilbao mwenye umri wa miaka 21 Nico Williams.(GiveMeSport) Villa wanamfuatilia kwa karibu winga wa Leeds United Mholanzi Crysencio Summerville, 22. (Football Insider) Tottenham inaweza kuipa Genoa fursa ya kumsajili kwa mkopo beki wao Mwingereza Djed Spence, 23, kwa mkataba wa kudumu ili kubadilishana na mshambuliaji wa Iceland Albert Gudmundsson, 26. (Calcio Mercato - kwa Kiitaliano). Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wako tayari kukubali ofa za pauni milioni 20-25 kwa kiungo wa kati wa Ghana Thomas Partey, 30, na bado wanavutiwa na kiungo wa kati wa Aston Villa wa Brazil Douglas Luiz, 25, kama mbadala wake. (Football Insider) Feyenoord wamemtambua mkufunzi wa FC Twente Joseph Oosting kama mmoja wa walengwa wao wakuu wa ukocha, iwapo watampoteza Arne Slot kwa Liverpool (Mirror) West Ham wamekuwa kwenye mazungumzo na meneja wa zamani wa Uhispania Julen Lopetegui "kwa miezi", na mkataba wa bosi wa sasa David Moyes unamalizika Juni. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania) Newcastle wanatazamiwa kumsaini beki wa Uingereza wa kikosi cha Chini ya miaka 21 Lewis Hall, 19, kwa mkataba wa kudumu msimu wa joto. (Football Insider) Erik ten Hag atakabiliwa na kupunguzwa kwa mshaharawake kwa 25% kama meneja wa Manchester United ikiwa ataendelea kuwa meneja huku klabu hiyo ikitarajiwa kukosa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa. (ESPN) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal na Manchester City wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Newcastle United na Brazil Bruno Guimaraes, 26. (Telegraph) Kiungo wa kati wa Ureno Bernardo Silva ameamua kuondoka Manchester City na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30, ambaye ana kipengee cha kumuachilia cha pauni milioni 50 ana nia ya kuhamia Barcelona. (Sport - kwa Kihispania) Chelsea imetaka habari kuhusu mlinzi wa kati wa RB Leipzig na Ufaransa Castello Lukeba, 21, ambaye ana kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 60 katika mkataba wake na klabu hiyo ya Bundesliga. (FootMercato - kwa Kifaransa) Meneja wa Manchester United Erik ten Hag anataka klabu hiyo kumleta mshambuliaji mwingine katika majira ya joto ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. (Goal) Chanzo cha picha, Reuters Beki wa Chelsea Thiago Silva, 39, amefikia makubaliano ya mdomo na Fluminense , huku Mbrazil huyo akimaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu(Goal) Mshambulizi wa zamani wa Arsenal na Manchester United Robin van Persie anakaribia kuchukua wadhifa wake wa kwanza wa ukocha, baada ya kufanya mazungumzo na klabu inayoshiriki ligi kuu ya Uholanzi Heerenveen. (Algemeen Dagblad - kwa Kiholanzi) Real Madrid wanapanga kumuongezea mkataba mlinzi wa Uhispania Lucas Vazquez, 32, ambaye mkataba wake wa sasa unakamilika mwezi Juni. (AS - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Paris St-Germain wamsaka kinda wa Barcelona mwenye umri wa miaka 16 Lamine Yamal. (Le Parisien - kwa Kifaransa) Manchester United wanavutiwa na mlinzi wa Inter Milan na Italia Alessandro Bastoni, 25, na wako tayari kutoa takriban £52m. (Fichajes - kwa Kihispania) Klabu ya Uholanzi Feyenoord inavutiwa na winga wa Tottenham mwenye umri wa miaka 23 Bryan Gil, ambaye anatarajiwa kuondoka Spurs msimu wa joto. (Standard) Mshambulizi wa Ufaransa Olivier Giroud, 37, atatia saini mkataba na klabu ya Ligi Kuu ya Soka (MLS) Los Angeles FC na atajiunga nao kwa uhamisho wa bure msimu wa joto wakati mkataba wake wa AC Milan utakapokamilika. (RMC Sport - kwa Kifaransa) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Brighton Roberto de Zerbi ndiye mgombea anayeongoza kuchukua nafasi ya Ten Hag ikiwa ataondoka Old Trafford, na Seagulls wanamfikiria kocha mkuu wa Burnley Vincent Kompany kama mbadala wake. (Teamtalk) West Ham watafanya mazungumzo na kocha mkuu wa Sporting Lisbon Ruben Amorim, 39, huku wakiamua iwapo wataongeza mkataba wa David Moyes msimu huu wa joto. Haijabainika ni wapi Wana Nyundo wangeshika nafasi katika chaguzi za Amorim. (The Athletic) Kocha wa zamani wa Wolves Julen Lopetegui ni mshindani mkubwa kuchukua nafasi ya Moyes kwenye Uwanja wa London Stadium. (Telegraph) Amorim anasalia kuwa chaguo la kwanza la Liverpool kuchukua nafasi ya Jurgen Klopp lakini meneja wa Brentford Thomas Frank anazingatiwa ikiwa Mreno huyo ataenda kwingine. (Team Talk) Uwezo wa Erik ten Hag utatathminiwa na mkurugenzi mpya wa kiufundi wa Manchester United Jason Wilcox kabla ya klabu hiyo kufanya uamuzi kuhusu mustakabali wa Mholanzi huyo. (Telegraph) Chanzo cha picha, Getty Images Klabu ya Saudi Arabia Al-Nassr bado ina nia ya kumsajili Kevin de Bruyne wa Manchester City msimu wa joto na inatarajiwa kuwasiliana na kiungo huyo wa kati wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 32 hivi karibuni. (Rudy Galetti) Barcelona wamejiunga na Arsenal kutaka kumnunua mshambuliaji wa Newcastle United na Uswidi Alexander Isak, 24, mwenye thamani ya pauni milioni 90, huku klabu hiyo ya Uhispania ikitarajia kufanya makubaliano huku Magpies wakitafuta kufuata sheria za usawa wa kifedha. (Sun) Arsenal na Manchester United wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili winga wa Crystal Palace na Ufaransa Michael Olise, 22, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Chelsea, Manchester City na Juventus . (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wanatarajia kuongeza wachezaji watatu au wanne msimu huu wa joto huku wakikamilisha kufanyia marekebisho kikosi chao,naye mshambuliaji wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres, 25, akiwa lengo lao kuu. (Footbal Transfer) Liverpool walimtazama Gyokeres katika ushindi wa 3-0 wa Sporting dhidi ya Vitoria wikendi huku wakilenga mshambuliaji mpya na beki wa kati msimu huu wa joto. (HITC) Manchester United imemfanya beki wa Everton na England mwenye umri wa miaka 21 Jarrad Branthwaite, kuwa lengo lao kuu msimu huu na wanataka kukubaliana mkataba wa mapema. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Real Betis wanalenga kumsajili mlinda lango wa zamani wa Manchester United na Uhispania David de Gea, 33, ambaye amekuwa mchezaji huru tangu kuondoka Old Trafford mwishoni mwa msimu uliopita. (Estadio Deportivo - kwa Kihispania) Beki wa Brazil Thiago Silva, 39, ataondoka Chelsea mkataba wake utakapokamilika msimu wa joto. (Fabrizio Romano) Crystal Palace wanavutiwa na kiungo wa kati wa Leicester City na Nigeria Wilfred Ndidi, 27, kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto. (sport) Bayern Munich wanafuatilia hali ya mchezaji wa Barcelona Frenkie de Jong, ingawa mshahara wa kiungo huyo wa kati wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 26 unaweza kukatiza uhamisho wake. (Sky Sports Ujerumani) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Barcelona wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Liverpool mwenye umri wa miaka 27 raia wa Colombia Luis Diaz msimu huu wa joto. (Sport - kwa Kihispania) Wolves inawazingatia kipa wa Arsenal Muingereza Aaron Ramsdale, 25, mlinda lango wa Liverpool na Jamhuri ya Ireland, Caoimhin Kelleher, 23, na kipa wa Sunderland Anthony Patterson kamawanaoweza kuziba nafasi ya kipa wa Ureno Jose Sa, 31, anayeondoka kutoka klabu hiyo msimu huu wa joto. (Sun) Manchester City wako tayari kusikiliza ofa kwa kiungo wa kati wa Uingereza Jack Grealish mwenye umri wa miaka 28 msimu huu wa joto. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Barcelona itasikiliza ofa kwa mlinzi wa Uruguay Ronald Araujo, 25, msimu huu, huku Manchester United ikionyesha nia. (Sport - kwa Kihispania, kupitia Goal) Crystal Palace wanaweza kujiunga na harakati za kumsaka kiungo wa kati wa Club Bruges wa Nigeria Raphael Onyedika, 23. (Sun) Arsenal, Liverpool na Manchester United ni miongoni mwa vilabu vinavyotaka kumsajili beki wa Real Madrid na Ufaransa Ferland Mendy, 28. (L'Equipe - kwa Kifaransa) Borussia Dortmund italazimika kulipakiasi cha kuvunja rekodi ya klabu cha £35m iwapo wanataka kubadilisha mkopo wao kwa mlinzi wa Chelsea Mholanzi Ian Maatsen, 22, kuwa mkataba wa kudumu. (Mirror) Chanzo cha picha, Reuters Manchester City wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Arsenal na Liverpool kumsajili beki wa kushoto wa Wolves wa Algeria Rayan Ait-Nouri. (Mirror) Vilabu vingi vya Premier League vinafikiria kumnunua mshambuliaji wa Atletico Madrid Mhispania Samu Omorodion, 19, ambaye yuko kwa mkopo Alaves. (AS - kwa Kihispania) Arsenal italazimika kulipa euro 60m (£51m) ikiwa wanataka kumsajili mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic mwenye umri wa miaka 24 kutoka Juventus msimu huu wa joto. (Tuttosport - kwa Kiitaliano) Newcastle wanapanga kumnunua mlinzi wa Juventus mwenye umri wa miaka 19 wa Juventus Dean Huijsen ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Roma kwa pauni milioni 25. (Mirror) Manchester United na Newcastle huenda zikamnunua kiungo wa kati wa Ufaransa Adrien Rabiot, 29, ikiwa hatasaini mkataba mpya na Juventus msimu huu wa joto. (Calciomercato - kwa Kiitaliano) Leeds huenda ikakubali ofa ya karibu pauni milioni 30 kwa winga wa Italia Wilfried Gnonto, 20, ambaye anavutia vilabu kadha vya Premier League. (Football Insider) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Real Madrid wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa Manchester City na Ureno Bernardo Silva mwenye umri wa miaka 29 msimu huu. (Star) Barcelona wanatarajiwa kumenyana na Real, huku rais wa klabu hiyo Joan Laporta akipatia kipaumbele usajili wa Silva. (Sport - kwa Kihispania) West Ham walikuwa na mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Cole Palmer, 21, kutoka Manchester City kabla ya Chelsea kumnunua msimu uliopita. (Sun) Atletico Madrid inapania kumpa mkataba mpya mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 33, huku mkataba wake wa sasa ukikamilika 2026. (Rudy Galetti). Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal, Juventus na Atletico Madrid wanawania kumsajili mshambuliaji wa Mexico Santiago Gimenez, 23, ambaye yuko tayari kuondoka Feyenoord ya Uholanzi. (Rekodi - kwa Kihispania) Barcelona wanatamani kumrejesha mchezaji wa zamani wa chuo chao Dani Olmo, 25, kutoka RB Leipzig. Mshambuliaji huyo wa Uhispania ana kipengele cha kutolewa cha euro milioni 60 katika mkataba wake. (Mundo Deportivo) Borussia Dortmund wako kwenye "mazungumzo" ya kuongeza mkataba wa beki wa kati wa Ujerumani Mats Hummels, ambaye atatimiza umri wa miaka 36 mwezi Desemba. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Klabu ya Uturuki ya Super Lig, Galatasaray inapanga kumnunua kiungo wa Liverpool Mholanzi Ryan Gravenberch, 21, msimu wa joto. (Fotomaki) Manchester United na Arsenal wako tayari kuchuana na AC Milan kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee mwenye umri wa miaka 22 kutoka Bologna. (Gazetta - kwa Kiitaliano) Beki wa Real Madrid Nacho Fernandez ameamua kuondoka katika klabu hiyo msimu huu wa joto huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 akitarajia kuhamia Ligi Kuu ya Soka. (Marca kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United, Juventus na Inter Milan pia ni ni baadhi ya klabu ambazo zinamvutia nahodha huyo wa Real Madrid . (Fichajes - kwa Kihispania) Kiungo wa kati wa Ureno Fabio Carvalho anatazamiwa kusalia na kupigania nafasi yake Liverpool msimu ujao chini ya kocha mpya wa klabu hiyo, licha ya kutakiwa na Hull City ambako mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 anacheza kwa mkopo. (Football Insider) PSG wako tayari kuachana na nia yao ya kutaka kumsajili kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 26, kutokana na masuala ya usawa wa kifedha michezoni . (Sport - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane anafuatilia kwa karibu hali ya meneja wa Manchester United Erik ten Hag na angependelea kuinoa Old Trafford badala ya Bayern Munich. (L'Equipe, via Get French Football News) Bayern Munich haijawasiliana na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa Zidane kuhusu kumrithi Thomas Tuchel, ambaye anaondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu. (ESPN) Aliyekuwa mkufunzi wa muda wa Manchester United Ralf Rangnick, ambaye ni meneja wa Austria, amejadiliwa na uongozi wa Bayern , huku kocha wa Brighton Roberto de Zerbi pia akiwa kwenye orodha yao ya watu wanaoweza kuwania nafasi hiyo. (Sky Sport Germany) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United inaweza kuwa katika mstari wa kupokea pauni milioni 3.4 za ziada kwa ajili ya mkopo wa winga wa Uingereza Jadon Sancho kwenda Borussia Dortmund ikiwa timu hiyo ya Ujerumani itatinga fainali ya Ligi ya Mabingwa.(Times - subscription required) Kiungo wa kati wa Newcastle United na Brazil Bruno Guimaraes, 26, amedokeza kuwa ana nia ya kusalia katika klabu hiyo msimu ujao baada ya kununua nyumba mpya Kaskazini Mashariki.(Telegraph - subscription required) Beki wa kushoto wa Uholanzi Ian Maatsen, 22, ameiambia Chelsea kwamba anataka kuondoka huko na ana nia ya kusalia Dortmund, ambako yupo kwa mkopo. (Sky Sport Germany) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanakabiliwa na ushindani kutoka Atletico Madrid kuwania saini ya beki wa kati wa Nice na Ufaransa Jean-Clair Todibo, 24. (Mirror). Bayern Munich wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 26 , ambaye anaweza kugharimu kati ya Euro 60-70m.(Relevo - in Spanish) Fulham wako tayar kwa ajili ya ofa ya mshambuliaji wa Brazil Carlos Vinicius, 29, ambaye ana mkataba wa mkopo katika klabu ya Galatasaray ya Uturuki ya Super Lig hadi mwisho wa msimu. (Standard) Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Mshambuliaji wa Bayern Munich, Jamal Musiala anaibuka kama shabaha kuu ya Manchester City msimu wa joto, huku Chelsea pia wakifuatilia hali ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani. (Guardian) Hata hivyo, Bayern hawana nia ya kumuuza Musiala na wanatayarisha ofa ya mkataba mpya kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (Fabrizio Romano) Arsenal wanatazamia kumsajili mshambuliaji na winga katika msimu wa joto, huku mshambuliaji wa Newcastle Uswidi Alexander Isak, 24, na winga wa Ufaransa Michael Olise, 22, ambaye yuko Crystal Palace, wakiwa miongoni mwa malengo yao. (Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal inamfuatilia mshambuliaji wa RB Leipzig na Slovenia Benjamin Sesko mwenye umri wa miaka 20 huku wakiongeza juhudi za kusajili mshambuliaji msimu huu. (Standard) Chelsea na Manchester United pia wanamfuatilia Sesko, ambaye ana kipengele cha kutolewa cha euro milioni 50. (Ben Jacobs) Meneja msaidizi wa Liverpool Pep Lijnders ananyatiwa na Besiktas kwa ajili ya nafasi ya kocha mkuu wa timu hiyo ya Uturuki iliyo wazi. (Athletic- Usajili unahitajika) Liverpool na Paris St-Germain wanafikiria kumnunua mlinzi wa Chelsea na Uingereza Levi Colwill, 21. (GiveMeSport) Chanzo cha picha, Getty Images Tottenham wanavutiwa na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Serge Gnabry, huku Bayern Munich wakiwa tayari kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, 28. (Football Insider) Spurs pia wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumnunua kiungo wa Nottingham Forest Morgan Gibbs-White, 24, na wako tayari kumnunua Muingereza huyo msimu wa joto. (Football Insider) Mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku anatarajiwa kurejea Chelsea mwishoni mwa msimu wake wa mkopo wa muda mrefu nchini Italia huko Roma, ambayo haiweza kumudu euro milioni 43 kumsajili mchezaji huyo wa miaka 30 kwa mkataba wa kudumu. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea na Newcastle United wanavutiwa na mlinda lango wa Arsenal na Uingereza Aaron Ramsdale, 25. (CaughtOffside) Mkufunzi wa Ujerumani Julian Nagelsmann haongei tu na Bayern Munich kuhusu kuwa meneja wao na atafanya uamuzi ndani ya wiki ijayo au zaidi, kulingana na wakala wake. (Podikasti ya Spielmacher, kupitia Metro) Kocha wa zamani wa Liverpool na Everton Rafael Benitez anatazamiwa kuinoa Sao Paulo mwezi mmoja baada ya kutimuliwa na Celta Vigo. (Sun) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Manchester City na Real Madrid zilicheza mechi yao ya robo fainali ambapo City waliondolewa katika michuano hiyo na Real Madrid. Mechi hiyo hatahivyo ilikuwa kubwa kuwapima wachezaji wawili wa England wanaopigania jezi moja ya England, Phil Foden wa Manchester City na Jude Belligham wa Real Madrid. Phil Foden ameng’aa katika Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu kwa kiwango chake akiwa na City, huku kiwango cha Jude Bellingham akiwa na Real Madrid kikivutia kote Ulaya. Wachezaji wote wawili watakuwa muhimu kwa England kwenye Euro 2024, lakini kocha Gareth Southgate ana mtanziko - ni nani atacheza nafasi ya namba 10? Wote wawili walicheza namba kumi katika vilabu vyao katika mechi ya kwanza iliyovutia mno, ambayo ilimalizika kwa mabao 3-3 mjini Madrid wiki iliyopita. Foden alichezaji vizuri sana, akitwaa tuzo ya mchezaji bora wa mechi baada ya kufunga katika kipindi cha pili, akicheza katika nafasi ambayo amecheza mara tisa akiwa na City msimu huu. Bellingham amecheza mechi 24 kwenye nafasi hiyo akiwa na Real na ana uwezekano wa kucheza tena nafasi hiyo katika mechi ya marudiano Jumatano. Lakini wachezaji hao wanalingana vipi kitakwimu? Chanzo cha picha, getty images Tovuti ya takwimu za kandanda WhoScored Foden ana mabao saba na pasi za mwisho tatu katika mechi 10, na kuchangia mabao zaidi (12) kutoka upande wa kulia, ambapo amecheza mara 18 katika mashindano yote kwa klabu na nchi. Bellingham amechangia mabao 24 (mabao 16, pasi za mwisho nane) kama kiungo mshambuliaji, lakini amecheza mara nyingi zaidi katika nafasi hiyo kuliko Foden msimu huu. Nyota huyo wa Real Madrid kwa ujumla anaonekana kufanya vyema zaidi katikati - pia ana mabao mawili na pasi ya mwisho moja katika mechi 12 katika nafasi ya kiungo wa kati. Kwa England, Bellingham amekuwa ndio namba 10 msimu huu. Ameanza mechi nne kama kiungo mshambuliaji, mchezo mmoja upande wa kushoto na alipumzishwa katika mechi ya kirafiki ya Oktoba dhidi ya Australia. Bellingham aliumia mwezi Novemba, Foden alianza dhidi ya Macedonia Kaskazini akiwa na jezi namba 10 - mara yake ya kwanza kuvaa hivyo chini ya Southgate msimu huu. Msimamo bora wa Foden ni upi unabaki kuwa mjadala, ingawa alisema mwaka huu "100%" anapendelea kucheza nambari 10. Beki wa zamani wa Manchester City, Micah Richards aliiambia BBC "Wakati mwingine ninapomtazama Phil Foden akicheza mbali na katikati, nahisi kama anatengwa. "Lakini yeye huchagua nafasi za kati kati kama safu ya kiungo na safu ya ulinzi. Hata akiwa mlinzi hushuka sana, anaweza kufika katikati ya uwanja na kupiga pasi. Kwa hivyo napenda awe katikati." Alipoulizwa kuhusu kumtumia mara nyingi zaidi, kocha wa England Southgate alisema: "Hhachezi mara nyingi kwa klabu yake. Inawezekana kuna sababu. Inategemea kiwango cha mchezo. Chanzo cha picha, getty images "Katikati ya uwanja, kila mtu anataka kuzungumza juu ya "na mpira" lakini kuna maelezo mengi bila mpira. "Itabidi uzungumze na Pep [Guardiola], ambaye ni kocha bora zaidi duniani, anayemchezesha kutoka pembeni." Ingawa Bellingham kuna nyakati amekuwa akicheza nafasi ya kiungo mlinzi kwa sababu ya uwezo wake wa kujilinda, Southgate anamuona wazi kama nambari 10, ambapo amefanikiwa kwa Real Madrid. Kabla ya mkondo wa kwanza wa mchujo wao wa robo fainali, bosi wa City Guardiola alisema Bellingham amekuwa na "athari kubwa" tangu kuhamia Uhispania. "Real Madrid nit imu tofauti na msimu uliopita. Athari yake ni kubwa, na inabidi tujaribu kugundua anachofanya ili kuidhibiti." Je, unadhani nani anafaa kuwa namba 10 wa England?
2
Chanzo cha picha, Getty Images Barcelona na Manchester City wamefanya mazungumzo na wawakilishi wa kiungo wa kati wa RB Leipzig na Uhispania Dani Olmo, 25, wiki iliyopita. (Mundo Deportivo – kwa Kihispania) Chelsea na Barcelona ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ulaya zinazofikiria kumnunua mshambuliaji wa Roma mwenye umri wa miaka 30 kutoka Argentina Paulo Dybala. (Rudy Galetti) Beki wa zamani wa Mexico Rafa Marquez ni mmoja wa wanaowania kurithi mikoba ya Xavi wakati Mhispania huyo atakapojiuzulu kama kocha wa Barcelona mwishoni mwa msimu huu. (ESPN) Chanzo cha picha, Getty Images Bayern Munich na Tottenham wameungana na Manchester United katika kufikiria kumnunua beki wa Everton mwenye umri wa miaka 21 Muingereza Jarrad Branthwaite. (TeamTalks) Klabu za Saudi Pro League zinavutiwa na kiungo wa kati wa Senegal Idrissa Gana Gueye, 34, ambaye huenda asipewe ofa mpya na Everton mkataba wake utakapokamilika mwishoni mwa msimu huu. (Football Insider) Newcastle na Liverpool zimeingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Sporting Lisbon mwenye umri wa miaka 20 kutoka Ivory Coast Ousmane Diomande, ambaye pia anasakwa na Chelsea. (Football Transfers) Chanzo cha picha, Reuters Newcastle imetuma maskauti kuwatazama kiungo wa Boca Juniors Muargentina Kevin Zenon, 23, na mlinzi wa Argentina Nicolas Valentini, 23. (HITC) Kazi ya Sean Dyche kama meneja wa Everton haiko hatarini licha ya matokeo mabaya ya klabu hiyo. (News – Subscription Required) Nottingham Forest wanataka zaidi ya pauni milioni 20 kumnunua beki wa kati wa Brazil Murillo, 21, huku Liverpool, Chelsea, Manchester United na Paris St-Germain pia zikimnyatia . (Football Insider) Manchester United wanaweza kumuuza Mason Greenwood kama sehemu ya mpango wa kumsajili beki wa Brazil Gleison Bremer, 27, kutoka Juventus. (Gazzetta dello Sport – In Italy , Subscription Required) Imetafsiriwa na Abdalla Seif Dzungu
2
Chanzo cha picha, AL HILAL SPORTS CLUB Takriban mwaka mmoja baada ya kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan, klabu yenye mafanikio makubwa zaidi ya soka nchini humo, Al Hilal, inasema inaendelea kucheza ili kutoa " bughudha" kwa watu nchini Sudan. Mzozo huo umesababisha vifo vya zaidi ya watu 14,000 na kuwalazimu milioni nane kuyakimbia makazi yao na Umoja wa Mataifa umeonya kuwa huenda ukasababisha mzozo mkubwa zaidi wa chakula duniani. Michuano ya taifa ilikatizwa lakini mabingwa hao wa Sudan walipata mwanya wa kuendelea na shughuli zao uwanjani kwa kufikia makubaliano na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kucheza na timu zake kuanzia Agosti. "Tunacheza wakati huu wa mzozo ili kundoka fikra za watu wetu kutoka kwenye vita," Dk Hassan Ali, katibu mkuu wa Al Hilal, aliiambia BBC Sport Africa. “Wengi wa mashabiki wa soka nchini Sudan wakati mwingine hawana lolote hata katika nyakati za kawaida, walichonacho ni ushindi wa Al Hilal ambao unawafanya wawe na furaha na familia zao. "Ni jukumu la kimaadili. Sio kucheza ili kushinda alama au vikombe. Hapana, tunacheza kwa ajili ya wafuasi wetu ili kuweka ari yao." Klabu hii ya takribani karne moja, inayoshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika, ilituma maombi kwa mashirikisho mengine kadhaa barani kote na kupokea majibu chanya kutoka Uganda na Libya kabla ya kufanya makubaliano na Tanzania. "Tulipendelea Tanzania kwa sababu mpira wa miguu huko ni wa maendeleo na wenye ushindani, na tungependa kujiandaa vyema kwa mashindano yajayo katika ngazi ya Afrika," aliongeza Dk Ali. Kuifahamu Tanzania pia kulichangia, kwani Tanzania ndiyo iliyokuwa tegemeo la klabu hiyo wakati wa kampeni za Ligi ya Mabingwa msimu huu ambazo zilimalizika kwa kuondolewa katika hatua ya makundi. Msemaji wa TFF , nchini Tanzania, Clifford Mario Ndimbo aliambia BBC kwamba vilabu vyote kwenye ligi vinaunga mkono kujumuishwa kwa Al Hilal, lakini mechi zao zitahesabiwa kuwa za kirafiki. Kucheza nchini Tanzania kunaweza pia kuisaidia Al Hilal kuepuka kuhama kwa wachezaji wengi kabla ya ushiriki wao katika mashindano ya bara msimu ujao. Klabu hiyo yenye maskani yake Omdurman kwa sasa ina takribani wachezaji kumi wa kigeni katika kikosi chake. "Nadhani itawasaidia Al Hilal kuwabakisha wachezaji wao na Florent Ibenge, kocha ambaye anajulikana katika bara zima na ana jukumu kubwa katika kile wanachojaribu kufanya," mchambuzi wa soka wa Sudan Abdul Musa alisema. katika BBC Sport Africa. "Wanahitaji aina fulani ya ushindani ambao wanaweza kuwa tayari kushindana katika ngazi ya bara. Ikiwa hutacheza ligi, ni vigumu." Chanzo cha picha, AL HILAL SPORTS CLUB Uamuzi wa Al Hilal kuhamia ng'ambo ni hali ambayo Wasudani wengi wamekabiliana nao, na kulazimika kuyahama makazi yao tangu kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwezi Aprili mwaka jana. "Vita daima huwa na athari mbaya," Dk Ali alisema. "Tuko uhamishoni na wachezaji wanacheza katika hali ngumu sana, hali ya vita mbali na familia zao. "Katika ngazi ya uongozi, hatuwezi kuonana ana kwa ana. Wajumbe wa bodi wametawanyika sehemu mbalimbali za dunia. Lini soka ya kulipwa itarejea Sudan bado haijafahamika, huku makundi ya kijeshi yakiendelea kupigania udhibiti wa nchi. Lakini hata kama vita vitakwisha sasa, Al Hilal haitaweza kutumia uwanja wake wa kisasa uliokarabatiwa mwaka wa 2018. Klabu hiyo inasema itagharimu takribani pauni milioni 3.2 (dola milioni 4) kukarabati uharibifu wa uwanja wake wa Omdurman, uliopewa jina la utani la "Blue Jewel", ambao uliporwa. "Kabla ya vita, tuliagiza vifaa vipya vya taa vya kisasa. Vifaa hivi vyote vilivyoagizwa kutoka Uhispania viliibwa," alilalamika Dkt Ali. "Nyasi zinahitaji kukarabatiwa. Ofisi zetu, vitu hivyo vyote, viliharibiwa vibaya." Chanzo cha picha, Getty Images Al Merreikh, klabu kongwe zaidi ya Sudan, pia inatafuta makao mapya. Klabu hiyo imepokea majibu chanya kutoka kwa Tanzania, Libya, Uganda, Kenya na Ghana, lakini BBC Sport Africa inaelewa kuwa watatua Tanzania kama wapinzani wao Al Hilal. Wakati vilabu viwili vikubwa nchini humo vikiwa na mbinu za kujinasua kutoka katika mzozo huo na kuendelea kucheza, klabu nyingi za soka za Sudan zimelazimika kuachana na wachezaji wao tangu michuano hiyo ilipomalizika. "Takriban vilabu vingine 15 vimekoma kabisa kufanya kazi," Musa alisema. "Hawana uwezo wa kuendelea kulipa mishahara yao. Bila mapato hali ni ngumu sana, hivyo wachezaji wengi sasa wako huru." Matokeo yake, wachezaji wengi wanatafuta nafasi kwingine. Chanzo cha picha, DANY ABI KHALIL / BBC Ingawa mishahara Afrika Kaskazini ni ya chini kuliko ile ya wachezaji wa Sudan walio nyumbani, mshambuliaji huyo ana nia ya kuendelea kufanya kazi licha ya dhiki ya kisaikolojia anayohisi akijaribu kuangazia kazi yake huku usalama wa familia yake ukiwa hauna uhakika katika nchi yake. "Mchezaji yeyote ambaye yuko Libya ataenda kwenye mazoezi au mechi na kumalizia siku yake kutazama habari kutoka Sudan," Mano aliiambia BBC Sport Africa. “Wachezaji wanahitaji faraja ya kisaikolojia ili wawe wabunifu, kuna msaada lakini lazima tuwepo ili familia zetu zile. "Hatupati mapato sawa na yale ya Sudan, lakini ndiyo suluhu pekee. Tuna fursa ya kujiuza na kurudi kwenye soka kama tulivyokuwa Sudan." Kwa sasa, Wasudani wanajaribu kujinusuru na vita. Wakati bunduki zitakimya, Musa anaamini kwamba urejesho wa soka ya kitaifa utachukua muda. "Vita viliturudisha nyuma kwa muda mrefu," alisema. “Wachezaji wengi wameondoka, hivyo timu zitalazimika kusajili tena ili kuweza kushindana. "Kazi nyingi itahitajika, lakini jambo kuu ni kukomesha vita."
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wanapanga kumuuza winga wa Brazil Antony, 24, msimu wa joto kwa kiwango "kinachokubalika", huku winga wa Crystal Palace Mwingereza Michael Olise, 22 akiwindwa na United. (Rudy Galetti via X) Inter Milan wanavutiwa na mlinzi wa Manchester United na England Aaron Wan-Bissaka, 26, ikiwa beki wa kulia wa Uholanzi Denzel Dumfries, 27, ataondoka Serie A msimu huu. (Gazzetta dello Sport - in Italian) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal wana nia ya kuleta mshambuliaji ili kutoa ushindani kwa fowadi wa Brazil Gabriel Jesus, 27, na kiungo wa kati wa Ujerumani Kai Havertz, 24, huku fowadi wa Bologna Mholanzi Joshua Zirkzee, 22, akiwa miongoni mwa walengwa wao wakuu. (TeamTalk) Kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim atapewa muda wa kutekeleza mtindo wake wa uchezaji Liverpool iwapo atakuwa meneja wao mpya. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United imeibuka kuwa anayeweza kuwa mnunuzi wa mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 28. (Mirror) Tottenham wanaripotiwa kuwa tayari kuongeza juhudi zao za kumsajili kiungo wa kati wa Atalanta Mbrazil Ederson mwenye umri wa miaka 22. (TeamTalk) Chanzo cha picha, Getty Images Beki wa Uingereza Lewis Hall, 19, ambaye yuko kwa mkopo Newcastle United kutoka Chelsea, anatarajiwa kuondoka The Blues msimu huu wa joto kwa uhamisho wa kudumu kwenda St James' Park. (Mirror) Kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, anakubali kwamba atalazimika kuondoka Chelsea msimu huu wa joto ikiwa hatapewa kandarasi mpya kabla ya mwisho wa msimu huu. (HITC)
2
Manchester City wanaweza kutumia vyema nia ya Lucas Paqueta ya kuondoka West Ham msimu ujao - lakini iwapo tu uchunguzi wa Shirikisho la Soka kuhusu madai ya ukiukaji wa kamari uliofanywa na kiungo huyo wa kati wa Brazil, 26, utatupiliwa mbali. (Guardian) Kipengele cha Paqueta cha pauni milioni 85 cha kumtoa West Ham kitaanza kutekelezwa mwezi Juni na Manchester City hawatarajii suala la kibinafsi kuwa suala. ((Athletic - subscription required) Chanzo cha picha, Getty Images City wako tayari kutumia £120m kumsajili mshambuliaji wa Ujerumani Jamal Musiala, 21 kutoka Bayern Munich . (TeamTalk) Liverpool wanatayarisha uhamisho wa msimu wa majira ya joto kwa ajili ya mshambuliaji wa Sporting Lisbon Muingereza Marcus Edwards, 25, na mlinzi wa Ureno Goncalo Inacio, 22. (Football Insider) Mshambulizi wa Paraguay Miguel Almiron, 30, na mshambuliaji wa Uingereza Callum Wilson, 32, ni miongoni mwa wachezaji ambao wanaweza kuondoka Newcastle United huku klabu hiyo ikijiandaa kwa ujenzi wa majira ya joto. (Telegraph - subscription required) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United na Tottenham wamewasiliana na beki wa kati wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo katika kujaribu kufikia makubaliano ya awali ya kandarasi na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (TeamTalk) Aaron Wan-Bissaka wa United analengwa kwa pauni milioni 13 na Inter Milan huku beki huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 26 akimalizika kandarasi yake msimu wa joto wa 2025. (Gazetta dello Sport - in Italian). Tottenham wanatumai kufkamilisha mkataba wa haraka kwa ajili ya kumnunua kiungo wa kati wa Chelsea na Muingereza Conor Gallagher, 24, dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Brentford Thomas Frank amepuuzilia mbali ripoti kwamba mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 28, anaweza kuondoka kwa pauni milioni 30 msimu wa joto. (Evening Standard) Arsenal na Liverpool wameungana na Bayern Munich katika mbio za kumsajili beki wa kushoto wa Uhispania Alejandro Grimaldo, 28, kutoka Bayer Leverkusen . (Express) Beki wa Barcelona Pau Cubarsi anataka kusaini kandarasi mpya huko Nou Camp licha ya vilabu vikubwa kote barani Ulaya kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 kufuatia kiwango chake kizuri dhidi ya Paris St-Germain. (Mundo Deportivo - in Spanish) Chanzo cha picha, Getty Images Huku mchezaji nyota Kylian Mbappe akikaribia kuondoka Paris St-Germain kwenda Real Madrid, klabu hiyo ya Ufaransa inamfuatilia mshambuliaji wa Inter Milan Mfaransa Marcus Thuram, 26. (Tuttosport, via Bild - in German) Kiungo wa kati wa Luton Town Muingereza Ross Barkley anasema hatazingatia mustakabali wake hadi mwisho wa msimu huu, huku kukiwa na nia ya Manchester United . (Express) Vilabu vya Ligi ya Premia vinaweza kufaidika na hitaji la Nottingham Forest la kuuza wachezaji muhimu kwa kumnunua mshambuliaji wa New Zealand Chris Wood, 32. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Meneja wa Barcelona Xavi bado anaweza kushawishiwa kusalia katika klabu hiyo baada ya kutangaza kuwa ataondoka mwishoni mwa msimu huu - lakini iwapo tu atapokea hakikisho kwamba ataungwa mkono katika soko la uhamisho. (Mundo Deportivo - in Spanish) Mmiliki wa AC Milan, Gerry Cardinale ameamua dhidi ya kumwajiri mkurugenzi wa zamani wa Liverpool na Tottenham Damien Comolli kama mtendaji mkuu mpya wa klabu hiyo. (Sky Italia - in Italian) Fulham, Sheffield United, Southampton na Queens Park Rangers zote zinapanga kumnunua mshambuliaji wa Rangers raia wa Jamaika Kemar Roofe, 31. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Wolves na Leeds United wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Southampton na Scotland Che Adams, 27, ambaye atapatikana bila malipo mwishoni mwa msimu huu. (TeamTalk) Meneja wa Manchester United Erik ten Hag amekiri kwamba beki wa Uingereza Harry Maguire, 31, anataka kucheza mara kwa mara, akihusishwa na West Ham . (Metro) Aliyekuwa meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer yuko kwenye mfumo wa kuteuliwa kuwa meneja ajaye wa Jamhuri ya Ireland. (Irish Times) Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester City wanaongoza kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Bayern Munich Mjerumani Jamal Musiala, 21 - lakini Liverpool , Barcelona na Paris St-Germain wote pia wanamtaka nyota huyo . (Independent) Brentford wanatarajia mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney kuondoka katika klabu hiyo msimu wa joto, lakini The Bees watadai pauni milioni 50, huku Manchester United wakiwa miongoni mwa vilabu kadhaa vya Premier League vinavyomfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28.(HITC) Sir Jim Ratcliffe amefanya mazungumzo ya ana kwa ana na mmiliki mwenza wa Newcastle United Amanda Staveley katika kujaribu kufikia makubaliano juu ya uhamisho wa mkurugenzi wa michezo Dan Ashworth kwenda Manchester United(Times) Hali nzuri ya mchezo wa fowadi wa Arsenal Kai Havertz, 24,imewafanya The Gunners kufikiria upya mipango yao ya uhamisho wa majira ya joto, huku kukiwa na uwezekano wa kilabu hiyo kuacha mipango ya kumnunua Toney.(Mirror) Mfaransa Raphael Varane, 30, hatapewa mkataba mpya kwa pesa sawa na Manchester United na anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo mkataba wake wa sasa utakapokamilika mwezi Juni.(Chris Wheeler, Mail) Kiungo wa kati wa Arsenal Mwingereza Charlie Patino, 20, yuko tayari kwa uhamisho wa majira ya joto nje ya nchi.(Evening Standard) Liverpool wamekubaliana na kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim. (Football Insider) Meneja wa Tottenham Ange Postecoglou ameweka beki mpya wa kati kuwa mojawapo ya vipaumbele vyake vya uhamisho na mchezaji wa kimataifa wa Ecuador wa Bayer Leverkusen Piero Hincapie, 22, yuko kwenye orodha yake fupi. (Bild, kupitia TeamTalk) Spurs pia wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Union Saint-Gilloise na Algeria Mohamed Amoura msimu huu wa joto lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa West Ham na Wolves kwa mchezaji huyo wa miaka 23. (NipeSport) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea wanaweza kutarajia kusajili wachezaji 11 msimu huu wa joto wanapojaribu kupunguza kikosi chao kikubwa, huku kiungo wa kati wa Uingereza Conor Gallagher, 24, akiwa miongoni mwa wale wanaotarajiwa kuondoka(Sun) Barcelona wanajiandaa kumpa kiungo wa kati wa Uhispania Pedri, 21, ambaye amekataa ofa ya Paris St-Germain , nyongeza ya kandarasi. (Fabrizio Romano) Mshambulizi wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres analengwa zaidi na Arsenal lakini kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ina kipengele cha kutolewa cha euro 100m (£85.4m).(Football Transfers) Manchester United na Newcastle wameripotiwa "kuanzisha mazungumzo" na kiungo wa kati wa Juventus na Ufaransa Adrien Rabiot, 29, ambaye anaweza kupatikana kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto. (Calciomercato kupitia TeamTalk) Mabosi wa Newcastle wameweka pauni milioni 37 kwa klabu ikiwa ni toleo jipya la hisa, ingawa haijabainika iwapo fedha hizo zitachangia katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (Football Insider) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal na Chelsea wanamfuatilia kwa karibu mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 28, ambaye atagharimu hadi £40m msimu huu wa joto. (Florian Plettenberg) Wakala wa mshambuliaji wa Uswidi Viktor Gyokeres anasema itakuwa vigumu kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kusalia Sporting Lisbon ikiwa meneja Ruben Amorim, ambaye anahusishwa na Liverpool, ataondoka katika klabu hiyo. (A Bola - kwa Kireno) Meneja wa Lille, Paulo Fonseca anaongoza orodha ya wanaozingatiwa na West Ham kuchukua nafasi ya umeneja ikiwa The Hammers wataachana na David Moyes katika majira ya joto. (I) Chelsea inamlenga mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 25, msimu huu wa joto lakini klabu hiyo itahitaji kwanza kuuza wachezaji ili kupata fedha.(Football Transfers) Chanzo cha picha, Getty Images Mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino na makocha wake hawajafurahishwa na mchezo wa fowadi wa Ukraine Mykhaylo Mudryk mwenye umri wa miaka 23 msimu huu na The Blues watakuwa sokoni kutafuta winga mpya msimu huu. (Football Insider) Bayer Leverkusen wameungana na Liverpool na Tottenham katika harakati za kumsajili winga wa Leeds United Mholanzi Crysencio Summerville, 22. (Bild via Teamtalk) Aston Villa wanazidi kuwa na matumaini kuwa kiungo wa kati wa Brazil Douglas Luiz, 25, atasaini mkataba mpya wa muda mrefu. (Talksport) Shakhtar Donetsk wanajiandaa kumuuza kiungo wa kati wa Ukraine Georgiy Sudakov, huku Liverpool, Aston Villa, Arsenal na Manchester City wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (HITC) Beki wa Inter Milan Denzel Dumfries anaweza kuwa analengwa na Aston Villa na klabu hiyo ya Italia itazingatia ofa ya zaidi ya euro 30m kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi, 27, ambaye mkataba wake na klabu hiyo ya Serie A unamalizika 2025. (Calciomercato - kwa Kiitaliano) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United itawaacha wachezaji 12 wa kikosi chao cha kwanza kuondoka Old Trafford katika hatua ambayo itakuwa kubwa katika kuunda timu mpya ya klabu hiyo msimu huu wa joto. (FourFourTwo) Kipa wa Ujerumani Alexander Nubel, 27, anatazamiwa kusaini mkataba mpya wa miaka mitano na Bayern Munich ambao utahusisha kuendeleza mkataba wake wa mkopo na Stuttgart kwa msimu mwingine. (Bild) Washirika wa 777, mwekezaji anayejaribu kuchukua udhibiti wa Everton, ameahirisha tarehe iliyolengwa ya kukamilisha mpango huo huku ikijaribu kukusanya mamia ya mamilioni ya pauni kuufadhili.(Sky News) Makubaliano yameafikiwa kwa mkufunzi wa Lyon Sonia Bompastor kuwa meneja ajaye wa klabu ya Chelsea ya Ligi Kuu ya Wanawake msimu huu akirithi mikoba ya Emma Hayes. (Telegraph - usajili unahitajika) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Ni jambo ambalo wachambuzi wa masuala ya michezo wameanza kulifikiria, kwa sababu timu ya Arsenal imeshinda kwa mara ya nane mfululizo, na siku ya Jumamosi walichukua nafasi ya kwanza katika ligi ya Uingereza. Kila mwaka, inapofika mwisho wa ligi, utabiri hufanywa na kompyuta ambayo hutumiwa kutabiri michezo. Liverpool waliokuwa wanaongoza, walitoka sare na Manchester United siku chache zilizopita, na hivyo kushika nafasi ya pili, huku Manchester City, wanaotetea ubingwa, wakiwa katika nafasi ya tatu. Inazidi kuwa vigumu kutabiri nani atashinda ligi ikiwa imesalia mechi saba. Kwa hiyo kompyuta inayotabiri timu itakayotwaa kombe inaashiria timu ambayo inadhani itatwaa kombe hilo, na swali ni jinsi inavyokadiria mshindi. Kompyuta hii bora mara 100,000 huunda upya mechi za timu zote, kwa kutumia vigezo vya data kutabiri vyema matokeo ya msimu uliosalia. Chanzo cha picha, ARSENAL.COM Huhesabu uwezekano wa timu kumaliza katika nafasi zao ama chini au juu. Pia huhesabu watakaoshinda, watakaoshindwa na watakaotoka sare, kwa kuzingatia matokeo ya zamani. Kwa hivyo ilipotokea, kompyuta ilitabiri kuwa timu tatu za juu kwenye ligi zitakuwa mbele kwa alama mbili, na ligi itachukuliwa kwa tofauti ya mabao. Kulingana na kompyuta, Arsenal itashinda Ligi ya Primia baada ya miaka 20. Pia ilitabiri kuwa timu ya Liverpool itakuwa sawa kwa pointi na Arsenal, lakini tofauti ya mabao itakuwa 10. Vile vile, ilitabiri kuwa Manchester City inatarajiwa kuwa nyuma kwa pointi mbili. Utabiri alioutoa kwa timu hizo ni kwamba Manchester City ina nafasi ya 17.3 kutwaa taji hilo kwa mara ya nne mfululizo, huku Liverpool ikiwa na nafasi 30.3 kutwaa kombe hilo, na Arsenal ina nafasi ya 52.3. “Matokeo siku zote yanategemea timu ina nini, lakini kwa kuwa kompyuta hii imetumika kwa muda mrefu, ni nzuri kwa utabiri wa muda mfupi,” alisema Mohamed Ahmed Deysane, ambaye anatoa maoni yake kuhusu mchezo huo. "Watu wanavutiwa sana na utabiri wa hii kompyuta, kwa sababu inazingatia – mambo kama wachambuzi - wachezaji waliojeruhiwa, wanaoanza mchezo uwanjani, nafasi na uwanja wa kucheza," Deysane aliongeza. Timu tatu zitakazosalia kwenye Ligi ya Primia, alisema kulingana na kompyuta hii, zitakuwa Luton, Burnley na Sheffield United. Imefasiriwa na Asha Juma
2
Chanzo cha picha, Getty Images Manchester City na Real Madrid zilifunga mabao sita katika mchezo wa kusisimua na kuhitimisha robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya mkondo wa kwanza kwa sare ya 3-3 katika uwanja wa Bernabeu. Kikosi cha Pep Guardiola kiliongoza katika dakika ya pili wakati Bernardo Silva alipopiga mkwaju wa wa adhabu ndogo kutoka umbali wa yadi 25 lililompita mlinda lango Andriy Lunin. Mshambulizi mawili ambayo hayakuzaa matunda yaliwafanya mabingwa mara 14 wa ligi ya mabingwa Ulaya Real Madrid kuutawala mchezo. Mkwaju wa mbali wa kwanza wa Eduardo Camavinga ulimgonga Ruben Dias na kutinga. komiani katika kona ya mbali ya goli la Stefan Ortega, kabla ya Rodrygo kuichsmbua ngome ya walinzi wa City na kutikisa nyavu kupitia kisigino cha Manuel Akanji. City walikuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira ugenini katika dimba la Bernabeu lakini walishindwa kuingia katika eneo la hatari la wapinzani - hadi Phil Foden alipoachia mkwaju mkali na kuiandikia City goli la kusawazisha. Kiungo huyo wa kati raia wa England alikuwa pembeni mwa uwanja lakini alipata nafasi nje ya eneo la hatari na kugeuka na kuwa moto katika kona ya juu na hivyo kuirejesha City mchezoni Muda mfupi baadaye beki wa kushoto Josko Gvardiol aliachia shuti kali la mguu wa kulia na kufunga bao lake la kwanza tangu alipojiunga na City kutoka RB Leipzig msimu katikati mwa mwaka jana. Hata hivyo, Madrid ilisawazisha kwa mkwaju mkali wa guu la kulia kutoka kwa Federico Valverde. Chanzo cha picha, Getty Images Katika mechi nyingine Muingereza Harry Kane alirejea kaskazini mwa London akiwa na goli wakati matumaini ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Ulaya yakiachwa mashskani baada ya kutoka sare ya 2-2 na Bayern Munich katika mechi ya robo fainali ya kwanza katika uwanja wa Emirates. Kane, ambaye ni mfungaji bora wa mabao wa Tottenham, alipata mapokezi ya hasira kutoka kwa mashabiki wa Arsenal, ambao walishuhudia Gunners wakianza vizuri wakati Bukayo Saka alipowatanguliza baada ya dakika 12 tu za mchezo Bayern walijizatiti na kuijiepusha na mbaya kimchezo inayowakabili katika ligi ya nyumbani kwao Bundesliga na kuugeuza mchezo huo kabla ya mapumziko wakati mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Serge Gnabry aliposawazisha dakika sita baadaye. Chanzo cha picha, Getty Images Wasaa wa Kane ulifika wakati William Saliba alipomwangusha Leroy Sane wakati wakikimbizana baada ya dakika 32za mchezo. Nahodha huyo wa England alisonga mbele kwa mkwaju wa penalti na kuwanyamazisha mashabiki waliokuwa wakimzomea kwa bao lake la 15 katika mechi 20 dhidi ya Arsenal. Kikosi cha Mikel Arteta hakikuwa katika ubora wake wa kawaida, lakini mchezaji aliyetokea benchinla wachezaji wa akiba, Leandro Trossard alinufaika na kazi bora ya Gabriel Jesus na akasawazisha Arsenal walihisi kuwa walistahili kupata penalti katika sekunde za mwishoni mwa mchezo, lakini mwamuzi aliamuru mchezo uendelee wakati Saka alipogaagaa chini wakati alipokabiliana mlinda lango wa Beyern, Manuel Neuer. The Gunners walikuwa na bahati pia ya kutopigiwa penalti mapema katika kipindi hicho, wakati Gabriel alipochukua mpira kwa mikono baada ya mwamuzi kuashiria kupigwa kwa goli kiki. Wachezaji kadhaa wa Bayern walilalamika wakati huo lakini mwamuzi alisimamia uamuzi wake. Mechi za mkondo wa pili baina ya timu zilizocheza jana Jumanne zitapigwa juma lijalo Jumatano, Aprili 17. Imetafsiriwa na Dinah Gahamanyi na kuhaririwa na Floriane Kaijage
2
Chanzo cha picha, EPA Tottenham inamfuatilia mshambuliaji wa Athletic Bilbao mwenye umri wa miaka 21 Nico Williams, ambaye ana kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 42.8 katika mkataba wake. (Telegraph - usajili unahitajika) Williams anaweza kusalia kwa msimu mwingine Athletic Bilbao kabla ya Barcelona kujaribu kumsajili msimu wa joto wa 2025(Sport -Kwa Kihispania) Mazungumzo ya Newcastle United na kiungo wa kati wa Brazil Joelinton yanaendelea vyema na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 anakaribia kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Tyneside. (Telegraph) Beki Mfaransa Raphael Varane, 30, na kiungo wa kati wa Brazil Casemiro, 32, wanatarajiwa kuongoza orodha ya wachezaji ambao Manchester United itawauza msimu wa joto.(Talksport) Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wako tayari kumruhusu Mohamed Salah kuhamia Saudi Pro League msimu huu ikiwa fowadi huyo wa Misri mwenye umri wa miaka 31 ataweka wazi kuwa anataka kuondoka. (HITC) Manchester City wanavutiwa na winga wa Wolves Pedro Neto lakini huenda wakakabiliana na ushindani kutoka kwa vilabu vya Saudi Arabia kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 24(Teamtalk) Crystal Palace na Fulham wanalenga kumnunua mlinzi wa Union Berlin Mholanzi Danilho Doekhi, 25. (Football Insider) Mshambulizi wa Real Madrid Rodrygo, 23, anasema alikataa kuhamia Liverpool mwaka wa 2017, ingawa Reds walikuwa na ofa ya euro milioni 3 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil iliyokubaliwa na Santos. (90 Min) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal itashindana na Manchester United kumsajili kiungo wa kati wa Wolves na Brazil Joao Gomes, 23, msimu huu wa joto. ( O Dia - kwa Kireno) Mlinzi wa pembeni wa kulia wa Bayer Leverkusen wa kimataifa wa Uholanzi Jeremie Frimpong, 23, anavutiwa na Liverpool katika hatua ambayo inaweza kumfanya Trent Alexander-Arnold kuhamia katikati ya uwanja. (Football Insider) Manchester United bado hawajakubali mkataba wa fidia na Newcastle kwa ajili ya Dan Ashworth na huenda ikalazimika kusubiri miezi kadhaa kabla ya kumteua kama mkurugenzi wao wa michezo.(Guardian) Paris St-Germain na Barcelona wanavutiwa na mshambuliaji wa Liverpool Luis Diaz, ambaye wakala wake alimtembelea mchezaji huyo wa kimataifa wa Colombia, 27 hivi majuzi. (Telegraph - usajili unahitajika) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, GETTY IMAGES Huenda Arsenal walifurahia kutimka Harry Kane alipoondoka Tottenham na kwenda Bayern Munich majira ya joto. Lakini anarejea Kaskazini mwa London akijaribu kuwaondoa vijana hao wa Mikel Arteta katika Ligi ya Mabingwa Ulaya. The Gunners wanawakaribisha Bayern katika mechi ya Jumanne ya robo fainali ya kwanza. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 amefunga mabao mengi zaidi katika Ligi ya Uingereza dhidi ya Arsenal kuliko mchezaji mwingine yeyote - amefunga mara 14. Kane amevunja rekodi nchini Ujerumani kwa kufunga mabao 38 katika mechi 37 za kwanza. Anakaribia kupata Kiatu cha Dhahabu cha Ulaya, kama mfungaji bora anavyozawadiwa katika ligi zote za Ulaya na kiatu ambacho hajawahi kukipata hapo awali. Kwa sasa ana mabao 32. Nahodha huyo wa Uingereza ni mchezaji wa nne kufikisha magoli hayo katika ligi ya Bundesliga, nyuma ya wachezaji magwiji wa Bayern, Gerd Muller na Robert Lewandowski, ambao walifikia magoli hayo mara tatu kila mmoja, na Dieter Muller wa Cologne. Rekodi ya mabao mengi 41 katika ligi ya Bundesliga iliwekwa na Lewandowski akichezea Bayern mwaka 2020-21, rekodi ambayo Kane atahitaji mabao 10 katika mechi zake sita za mwisho ili kuivunja. "Atashinda Kiatu cha Dhahabu mwaka huu na hilo litaongeza mtazamo kwamba, ni mshambuliaji mzuri," alisema mwandishi wa habari wa soka barani Ulaya Guillem Balague kwenye BBC Radio 5. "Amezoea haraka sana na anajaribu kujifunza Kijerumani na anafanya vizuri uwanjani. Huku watoto wake wanne na mke wake wakiwa pamoja nae." Chanzo cha picha, Getty Images Zaidi ya hayo, hakuna aliyefunga mabao mengi katika Ligi ya Mabingwa msimu huu kuliko mabao sita ya Kane. Mashindano hayo yanaweza kuwa nafasi nzuri zaidi kwa Kane kushinda taji lake kuu la kwanza la mashindano hayo. Ikumbukwe hakushinda taji lolote katika muongo mmoja akiwa katika kikosi cha kwanza cha Tottenham. Alihamia Bayarn ambayo ilikuwa imeshinda mfululizo mataji 11 ya Bundesliga lakini sasa wako pointi 16 nyuma ya vinara Bayer Leverkusen, zikiwa zimesalia mechi sita. Iwapo Leverkusen wataifunga Werder Bremen siku ya Jumapili - itakuwa mara ya kwanza tangu Aprili 2013 kwa Bayern kutokuwa mabingwa wa Ujerumani. Na ushindi wa Leverkusen utathibitishwa zaidi siku ya Jumamosi ikiwa vijana wa Thomas Tuchel watafungwa na wakiwa nyumbani. "Kama Kane angekuwa na mataji mengi angeonekana kama mchezaji wa tofauti zaidi kwa kila mtu," anasema Balague. "Bila shaka sasa, yuko kwenye klabu kubwa, akijaribu kushinda mambo mengi katika klabu hiyo na anafanya vyema." Mwandishi wa kandanda barani Ulaya Mina Rzouki anasema: "Bayern wamekuwa na wakati mgumu msimu huu lakini amekuja na kuipeleka mbele. Itakuwa ajabu sana ikiwa hatashinda chochote."
2
Chanzo cha picha, Getty Images Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola anaamini kuwa Real Madrid watadhamiria kulipiza kisasi baada ya kuwalaza wababe hao wa Uhispania katika harakati za kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita. City iliifunga Real 5-1 kwa jumla ya mabao 5-1 katika nusu fainali. Hata hivyo, Guardiola hana shaka kwamba washindi hao mara 14 watafanya mtihani kuwa mgumu katika mechi ya Jumanne ya robo fainali ya kwanza mjini Madrid (20:00 BST). "Ni vigumu sana kwa jambo hilo hilo kutokea tena," Guardiola alisema. "Kuifunga Real Madrid mara mbili mfululizo haiwezekani. Wamejifunza na watataka kulipiza kisasi. Wana kiburi." Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti anataka kikosi chake kionyeshe nguvu zaidi kiakili kuliko ilivyokuwa wakati timu hizo mbili zilipokutana msimu uliopita. Baada ya sare ya 1-1 huko Madrid, Manchester City iliizaba Real katika mechi ya pili kwa mabao 4-0. "Tulicheza bila ujasiri, bila utu," Ancelotti alisema. “Ujasiri na utu ni jambo la msingi katika mchezo wa aina hii, ni kitu tulichokosa katika mechi ya mkondo wa pili. "Jambo muhimu ni kuwa katika ubora wetu, nyanja ya kiakili ni muhimu sana." Chanzo cha picha, Getty Images Beki wa zamani wa Chelsea Antonio Rudiger alimfanya Erling Haaland kuwa kimya katika mechi ya mkondo wa kwanza msimu uliopita lakini hakuanza mchezo huko Manchester. "[Mchuano wa kwanza] ulikuwa mchezo mzuri na tulimzuia Haaland kupata pasi," Rudiger alisema. "Kocha hakuomba msamaha [kwa kuniacha] na haitaji, nakubali, ingawa ilikuwa ngumu kukubali. "Sasa kwa mchezo huu mpango ni kujaribu na kudhibiti wachezaji hatari kama Phil Foden, [Kevin] de Bruyne na, bila shaka, Haaland." Real Madrid hawakuwa na Jude Bellingham mwaka jana na kiungo huyo wa kati wa Uingereza amekuwa muhimu kwao msimu huu, akifunga mabao 20 katika michuano yote. Ancelotti aliongeza: "Ana msimu mzuri sana kwenye sanduku la penalti. "Ana nguvu sana na anatusaidia sana katika safu ya ulinzi na mbele, kutengeneza nafasi na kutoa usaidizi wa magoli "Ana utu uzima. Ana umri wa miaka 20 tu lakini ni mtaalamu sana, makini sana na mnyenyekevu." Guardiola hana uhakika kama atamuanzisha Ederson langoni dhidi ya Real Madrid katika mechi ya Jumanne ya robo fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil hajacheza tangu alipojeruhiwa katika sare ya 1-1 na Liverpool mnamo Machi 10. Badala yake, Stefan Ortega amekuwa golini kwa mechi nne zilizopita, akitoa pasi mbili safi. "Lazima nifikirie juu yake. Yeye [Ederson] anajisikia vizuri," Guardiola alisema. "Sasa ni lazima niamue kama atacheza , lazima niamue, lakini tumefurahishwa sana na [utendaji] kutoka kwa Stefan Ortega. Ni kipa wa kipekee." Mabeki Nathan Ake na Kyle Walker hawakusafiri kwenda Madrid kwa mchezo huo huku Josko Gvardiol akiwa mashakani baada ya kwenda mapumziko katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Crystal Palace wikendi.
2
Chanzo cha picha, Reuters Mohamed Salah anatarajiwa kuwaniwa na vilabu vya Saudi Pro League tena msimu huu wa joto huku Al-Ittihad wakijiandaa kutoa pauni milioni 70 kwa mshambuliaji huyo wa miaka 31 wa Liverpool na Misri. ( Talksport) Chelsea wanajaribu kuwapiku wapinzani wao na kutoa ofa ya pauni milioni 43 kwa mshambuliaji wa Athletic Bilbao Nico Williams, 21, kabla ya dirisha la uhamisho kufunguliwa.(Football Insider) Manchester City wamekubaliana na kiungo wa West Ham Lucas Paqueta kabla ya uhamisho wa majira ya joto. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil, 26, alihusishwa pakubwa na kuhamia Etihad Stadium mwaka jana. ( Foot Mercato - kwa Kifaransa) Liverpool wamempa meneja wa Sporting Lisbon Ruben Amorim mkataba wa miaka mitatu kuchukua nafasi ya Jurgen Klopp huko Anfield. (Pedro Sepulveda, kupitia GiveMeSport) West Ham wameungana na Liverpool , Tottenham na AC Milan katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa kati wa Fulham Tosin Adarabioyo, 26, ambaye kandarasi yake inamalizika msimu wa joto.(Guardian) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea inapaswa kuwavutia kiungo wa kati wa Ureno Bruno Fernandes, 29, na mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 26, kuondoka Manchester United msimu huu wa joto, kulingana na mlinzi wa zamani wa Blues William Gallas (Mirror) Chelsea hawana nia ya kumsajili mlinda lango wa Athletico Paranaense Bento, 24, lakini Inter Milan wanatazamiwa kukabiliwa na ushindani kutoka kwingineko kwenye Ligi ya Premia kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil. (Gazetto dello Sport - kwa Kiitaliano) Borussia Dortmund wana nia ya kumsajili winga wa PSV Eindhoven Johan Bakayoko, 20 . Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji pia anaripotiwa kulengwa na Burnley na Brentford . (Voetbal International - kwa Kiholanzi) Beki wa Everton na England Jarrad Branthwaite anasema anazuia kelele kuhusu mustakabali wake huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 akivutia Manchester United na Real Madrid .(90min) Chanzo cha picha, Getty Images The Toffees pia wanaweza kutarajia ofa kwa kiungo wa Ubelgiji Amadou Onana hukuAfisa mkuu mtendaji wa zamani wa Everton Keith Wyness akisema klabu hiyo inaweza kupata hadi £70m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 huku Arsenal , Newcastle United na West Ham wakimtaka .(Football Insider) Paris St-Germain hawajakata tamaa katika kumsajili kiungo wa kati wa Barcelona na Uhispania Gavi msimu huu wa joto licha ya kifungu cha kutolewa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 cha 1bn-euro. ( L'Equipe - kwa Kifaransa) Kiungo wa zamani wa West Ham Felipe Anderson anakaribia kukubali dili la kujiunga na Juventus kama mchezaji huru. Mkataba wa winga huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 30 huko Lazio unamalizika mwishoni mwa msimu. ( Fabrizio Romano) Mkufunzi wa Real Betis Manuel Pellegrini hajakutana na maafisa kutoka Roma kuhusu kuchukua nafasi ya ukocha katika uwanja wa Stadio Olimpico huku Mchile huyo mwenye umri wa miaka 70 akitembelea mji mkuu wa Italia hivi majuzi kwa likizo ya kifamilia. (Muchodeporte - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Reuters Inter Milan wanaweza kumnunua fowadi wa Ufaransa Anthony Martial wakati kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 na Manchester United itakapokamilika msimu huu wa joto - ikiwa watashindwa kumsajili mshambuliaji wa Iceland Albert Gudmundsson, 26, kutoka Genoa . (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano) Brighton hawana nia ya kumnunua tena Ansu Fati baada ya uhamisho wake wa mkopo kutoka Barcelona lakini Wolves , Valencia na Sevilla wanawezakuwasilisha ofa kwa mshambuliaji huyo wa Uhispania, 21 msimu huu wa joto. (Sport - kwa Kihispania). Everton itahitaji zaidi ya pauni milioni 40 ili kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Dominic Calvert-Lewin, 27, msimu huu wa joto. (Football Insider) Luton wameonyesha nia yao ya kutaka kumnunua mshambuliaji wa Blackburn na Jamhuri ya Ireland Sammie Szmodics lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Brentford (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Amadou Onana huenda akaondoka Everton msimu huu wa joto, huku The Toffees wakitumai kupokea pauni milioni 50-60 kwa kiungo wa kati wa Ubelgiji, 22. (Football Insider) Vilabu vya Bundesliga vina nia ya kutaka kumnunua mshambuliaji wa Tottenham mwenye umri wa miaka 22 kutoka Jamhuri ya Ireland Troy Parrott, ambaye amekuwa kwa mkopo katika klabu ya Excelsior ya Uholanzi msimu huu. (Football Insider) Beki wa Uingereza Jarrad Branthwaite, 21, anasisitiza kuwa anazingatia zaidi kushinda mechi na Everton na kwamba anapuuza uvumi wote kuhusu mustakabali wake wa muda mrefu, baada ya kuhusishwa na Manchester United (Liverpool Echo) Juventus wamefikia makubaliano kimsingi na Thiago Motta kwa bosi wa Bologna kuwa kocha wao mpya - na kiungo wa kati wa Bologna na Scotland Lewis Ferguson, 24, anaweza kumfuata Turin. (Calciomercato - kwa Kiitaliano) Chanzo cha picha, Getty Images Winga wa Italia Nicolo Zaniolo anataka kurejea Serie A wakati mkopo wake kutoka Galatasaray kwenda Aston Villa utakapomalizika msimu huu, huku Fiorentina na Napoli wakiwa tayari wameulizia kuhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano) Manchester United wameimarisha nia yao ya kumnunua Miguel Gutierrez wa Girona na wanatazamia kushinda Arsenal katika kumsajili beki huyo wa kushoto wa Uhispania, 22, msimu huu. (Mirror, kupitia TeamTalk) Real Madrid wanamtazama kiungo wa River Plate Muargentina Franco Mastantuono, 16, ambaye pia anafuatiliwa na Chelsea na Paris St-Germain . (Fabrizio Romano) Barcelona na Manchester City pia wanavutiwa na Mastantuono, ambaye ana kipengele cha kutolewa cha euro 45m (£38.6m). (Sport - kwa Kihispania) Manchester United wamewasiliana na Palmeiras kuhusu mshambuliaji wa Brazil Thalys, 19, ambaye bado hajacheza kwa mara ya kwanza katika kikosi chake cha kwanza. (TeamTalk) Imetafsiriwa na Yusuf Jumah
2
Chanzo cha picha, Rex Features Kiungo wa kati wa Manchester City Muingereza Kalvin Phillips, 28, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo West Ham, amepangwa kama mmoja wa walengwa wa Fulham msumu ujao. (Football Transfers). Phillips anaweza kujiunga tena na klabu ya kwao Leeds United ikiwa wako tayari kulipa £30-£40m. (Football Insider) Manchester City wanataka kumzawadia Rodri kwa nyongeza ya mshahara ambayo itamfanya kiungo huyo wa kati wa Uhispania, 27, abaki na klabu hiyo katika maisha yake yote ya soka. (Mirror) Chanzo cha picha, Rex Features Arsenal na Chelsea wanavutiwa na Viktor Gyokeres lakini Sporting Lisbon hawatakubali chini ya euro 100m (£85.8m) kwa mshambuliaji huyo wa Uswidi, 25. (Pedro Sepulveda). Atletico Madrid wanavutiwa na kiungo wa kati wa Fulham wa Brazil Andreas Pereira, 28. (Sky Sports) Bodi ya Manchester United itasubiri hadi mwisho wa msimu kufanya uamuzi kuhusu mustakabali wa meneja Erik ten Hag, licha ya shinikizo kwenye nafasi ya Mholanzi huyo. (Times) Chanzo cha picha, Reuters Kipa wa England Aaron Ramsdale anatarajiwa kuondoka Arsenal msimu huu, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 akilengwa na Newcastle United. (Football Insider) Manchester United wana nia ya kumteua kocha wa Bologna Thiago Motta kama mbadala wa Ten Hag. (Gazzetta dello Sport - in Italian) Kocha wa zamani wa Chelsea na Everton Frank Lampard ameibuka kuwa mgombea wa kushtukiza kuchukua mikoba ya kuinoa timu ya taifa ya Canada. (Telegraph) Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool wako kwenye mazungumzo na Trent Alexander-Arnold kuhusu mkataba mpya wa beki huyo wa kulia wa Uingereza, 25. (Football Insider) Dinamo Zagreb wamelipa tangazo la ukurasa mzima katika gazeti la michezo linalouzwa zaidi nchini Uhispania, Marca, katika jaribio la kumshawishi kiungo wa kati wa Croatia Luka Modric, 38, kurejea katika klabu yake ya kwanza iwapo ataamua kuondoka Real Madrid msimu huu. (ESPN) Paris St-Germain wamesitisha mazungumzo ya kuongeza mkataba na kakake mdogo wa Kylian Mbappe Ethan Mbappe, 17, huku mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa kati wa Ufaransa chini ya miaka 16 ukimalizika Juni. (RMC Sport - in French) Chanzo cha picha, Getty Images Sevilla watataka kumuuza mfungaji bora Youssef En-Nesyri, huku mshambuliaji huyo wa Morocco mwenye umri wa miaka 26 akiwa "mlengwa" katika vilabu kadhaa vya Ligi ya Premia. (Marca - in Spanish) Arsenal wameungana na wenzao kama Manchester United na Bayern Munich kumfuata Mikayil Faye wa Barcelona kabla ya kumnunua beki huyo wa Senegal, 19. (Mail).
2
Chanzo cha picha, Getty Images Paris St-Germain wako tayari kulipa pauni milioni 111.5 ili kumsajili mshambuliaji wa tumu ya taifa ya Nigeria Victor Osimhen, 25, kutoka Napoli msimu huu. (Corriere dello Sport - kwa Kiitaliano) Chelsea wanaendelea kutafuta mshambuliaji mbadala wa Osimhen, huku mchezaji wa kimataifa wa Ukraine na Girona Artem Dovbyk, 26, akiwa kwenye rada za klabu hiyo. (GiveMeSport) Manchester United wanapanga msimu ujao huku Erik ten Hag akiwa meneja wa klabu hiyo kwa muda kutokana na kukosekana kwa mbadala wake. (i news) Manchester City wamekubali dili la kumsajili winga wa Troyes Mbrazil Savio, 19, ambaye yuko Girona kwa mkopo. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Mahitaji ya Manchester United ya kutaka ada ya pauni milioni 34 kwa ajili ya Jadon Sancho yanaweza kukatiza hamu ya winga huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 kutaka kurejea kwa mkopo Borussia Dortmund kuwa wa kudumu. (Sky Sport - kwa Kijerumani) Kocha wa Sporting Lisbon anayenyatiwa na Liverpool Mreno Ruben Amorim, 39, amekiri kuwa "hawezi kukuthibitisha" kuwa atakuwa mkufunzi wa klabu hiyo msimu ujao. (ESPN) Amorim ana kipengele cha kuachiliwa cha pauni milioni 12.8 katika klabu ya Sporting msimu huu wa joto, ambacho kitashuka hadi pauni milioni 8.5 mwaka wa 2025. (Sun) Chanzo cha picha, Getty Images Chelsea haitazingatia ofa za kumnunua beki wa Uingereza Reece James, 24, msimu huu licha ya tetesi zinazomhusisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 na PSG au Real Madrid. (Football Insider) Eddie Howe ameelezea azma yake ya kumbakisha Bruno Guimaraes Newcastle huku Magpies wakijiandaa kuzuia klabu nyingine kumnunua kiungo huyo wa Brazil, 26, kutoka PSG. (Mirror) Manchester City wako tayari kupata hasara kubwa kumuuza kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 28, msimu huu. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Tottenham wanapania kumnunua kiungo wa Leicester City Kiernan Dewsbury-Hall, 25, ambaye anaweza kuruhusiwa kuondoka kwa pauni milioni 25 ikiwa Foxes watashindwa kupanda daraja kurejea Premier League. (Talksport) Mshambulizi asiyetakikana wa Barcelona Ansu Fati, 21, hatarejea Brighton msimu ujao - lakini Wolves, Sevilla na Valencia wote wanafikiria kumnunua mshambuliaji huyo wa Uhispania kwa mkopo. (Sport - kwa Kihispania) Burnley wamekubali mkataba wa kumsaini beki wa Uholanzi chini ya umri wa miaka 21 Shurandy Sambo msimu wa joto mara baada ya mkataba wa mchezaji huyo wa PSV Eindhoven kumalizika. (Fabrizio Romano) Chanzo cha picha, Getty Images Leeds United itaweka kipaumbele usajili wa kudumu wa beki wa Wales Joe Rodon, 26, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo katika klabu hiyo akitokea Tottenham, iwapo watapandishwa daraja hadi Ligi ya Premia. (Football Insider) Beki wa Manchester City na Ureno Joao Cancelo, 29, anataka tu kuichezea Barcelona msimu ujao licha ya vilabu vingine kumtaka. (Sport - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Mshambuliaji wa Ureno Joao Felix anasema mchezaji mwenzake wa kimataifa Bernardo Silva, 29, anataka kuhamia Barcelona, ​​huku kiungo huyo wa kati wa Manchester City akihusishwa na klabu hiyo ya Catalan mara kadhaa hivi majuzi. (Gerard Romero) Liverpool wameanza mazungumzo na mkufunzi wa Sporting Lisbon Ruben Amorim, 39, kuchukua nafasi ya Jurgen Klopp huko Anfield. (Foot Mercato - kwa Kifaransa) Barcelona pia walikuwa wanamtaka kocha huyo wa Ureno lakini wamesitisha mpango huo kwani wanafikiri huenda akaelekea Liverpool. (Sport - kwa Kihispania) Manchester United wanafikiria kumnunua mlinzi wa Aston Villa wa Uingereza Ezri Konsa, 26. (Footbal Transfers) Chanzo cha picha, PA Media Atalanta wanasema hawajapokea mawasiliano yoyote ya moja kwa moja kutoka kwa Liverpool kuhusu kiungo wao Mholanzi Teun Koopmeiners huku Reds wakiripotiwa kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (90 min) Liverpool wanataka kumsajili kiungo wa kati wa Uruguay Federico Valverde, 25, kutoka Real Madrid. (Team Talk) Mshambuliaji wa Bologna na Uholanzi Joshua Zirkzee, 22, amekuwa akinyatiwa na Manchester United na Liverpool, lakini amemwambia wakala wake angependelea kuhamia AC Milan. (Mirror) Chanzo cha picha, Reuters Arsenal wanajiandaa kupambana na Manchester United katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Barcelona mwenye umri wa miaka 19 Mikayil Faye. (Calciomercato, via TeamTalk) Manchester United imempa mkataba mpya winga Mwingereza Bendito Mantato mwenye umri wa miaka 16 huku klabu kadhaa maarufu zikimtaka kinda huyo. (Fabrizio Romano) Klabu ya Everton huenda wakapunguziwa pointi kwa mara ya tatu baada ya ripoti ya akaunti zake za hivi punde kutolewa. (Football Insider) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Simba Instagram Klabu mbili kongwe za soka Simba na Yanga kutoka Afrika Mashariki nchini Tanzania, Ijumaa hii April 5 zinakabiliwa na kibarua kizito cha kuwania kutinga hatua ya nusu fainali ya Ligi ya mabingwa Afrika kwa mara ya kwanza, zitakaposhuka dimbani katika ncha mbili tofauti za Afrika; Kaskazini nchini Misri na Kusini nchini Afrika Kusini kuwakabili wenyeji Al Ahly na Mamelodi Sundowns. Hii inaweza kuwa wikiendi ya kukumbukwa zaidi kwa mashabiki wa soka Afrika Mashariki, wakati vigogo wa soka Afrika, Al Ahly wakitafuta kuendeleza historia yao kwa kulibeba taji lao la 12 la Ligi ya mabingwa Afrika Simba ya Tanzania inaweza kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza kutoka Tanzania kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo makubwa zaidi kwa ngazi za vilabu Afrika tangu kubaldilishwa kwa mfumo wa mashindano hayo mwaka 1998. Simba iliwahi kufika nusu fainali ya klabu bingwa Afrika mwaka 1974 katika mfumo wa awali na kutolewa na Ghazil Al Mahalla ya Misri kwa changamoto ya mikwaju ya pentai baada ya matokeo ya jumla ya goli 1-1 Klabu hiyo ya mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam inashuka kwenye mchezo huu ikiwa nyuma kwa goli 1-0 walilofungwa kwenye mchezo wao wa mkondo wa kwanza nyumbani Machi 29, hivyo wanalazimika kuifunga Al Ahly walau magoli 2-0 au ushindi mwingine wowote wa tofauti ya magoli mawili ili kufuzu moja kwa moja kwa hatua inayofuata. Lakini hata ushindi wa goli 1-0 utawapeleka kwenye changamoto ya mikwaji ya penati. Chanzo cha picha, Simba Instagram Mchezo huu wa aina yake unatarajiwa kuvuta hisia za wapenzi wengi wa soka kutokana na matokeo ya hivi karibuni baina ya Simba na Al Ahly. Mara ya mwisho Ahly kupata ushindi mkubwa mbele ya Simba ilikuwa mwaka 2019 waliposhinda 5-0 mjini Cairo huku michezo mingine ya karibuni Simba ikiwa imeshinda mara mbili na kutoka sare mara mbili. Kabla ya Simba kutupa karata yao huko Misri, watani wao Yanga watakuwa wageni wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambayo ni mabingwa wa kombe hilo mwaka 2016 ambapo sare ya magoli ya aina yoyote au ushindi utaivusha Yanga na kutinga nusu fainali ya kwanza ya mashindano ya Afrika. Hatua kubwa ambayo Yanga iliwahi kufikia ni robo fainali mwaka 1969 na mwaka 1970 katika mfumo wa zamani wa mashindano hayo. Mara zote mbili ilitolewa na Asante Kotoko ya Ghana. Chanzo cha picha, Young Africans/Instagram Pia Yanga ilifika hatua ya nane bora mwaka 1998 wakati ulipoanzishwa mfumo mpya wa ligi ya mabingwa Afrika. Mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa jijini Dar es Salaam ulimalizika kwa sare ya 0-0 huku Mamelodi wakionekana kuwa na nafasi kubwa ya kusonga mbele kutokana na rekodi yao nzuri wanapocheza nyumbani. Kwa msimu huu Mamelodi Sundowns hawajaruhusu bao lolote wakiwa nyumbani huku Yanga hawajapata ushindi wa aina yoyote ugenini. Yanga inahitaji sare yoyote ya magoli ili kusonga mbele kwa kunufaika na kanuni ya goli la ugeni. Chanzo cha picha, Young Africans/ Instagram Hata hivyo, Yanga imekuwa na matokeo bora ya michezo ugenini katika michezo ya Afrika hususan msimu uliopita. Miongoni mwa matokeo bora ya ugenini ni ushindi wa 1-0 katika mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger japo waliuokosa ubingwa kwa sababu ya kanuni ya goli la ugenini baada ya kukubali kichapo cha 2-1 jijini Dar es Salaam katika mchezo wa mkondo wa kwanza. Kukosekana kiungo mshambuliaji wa Yanga Rai awa Ivory Coast, Pacome Zouzoua ilikiwa pengo kubwa kwenye mchezo wa nyumbani kwa upande wa Yanga huku akitarajiwa kuanza kwenye mchezo huo wa mkondo wa pili. Timu pekee kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kuwahi kutwaa ubingwa Ligi ya mabingwa Afrika,TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo itasafiri mpaka Angola kupambana na Petro de Luanda baada ya sare ya 0-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliofanyika mjini Lubumbashi. Mazembe wanahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya magoli ili kusonga mbele.
2
Chanzo cha picha, Getty Images Newcastle United wanahofia huenda wakahitaji kumuuza kiungo wa Brazil Bruno Guimaraes, 26, ili kukidhi sheria za kifedha za Ligi ya England. Miamba wa Ufaransa Paris St-Germain wanaongoza katika mbio hizo, huku Manchester United na Arsenal pia wakiwa na hamu. (Sun) Tottenham pia wameungana na Arsenal katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, 24, iwapo Newcastle italazimika kuuza wachezaji wake muhimu msimu huu wa joto. (Football Insider) Lakini Isak amesisitiza kujitolea kwake kwa Newcastle huku kukiwa na nia ya wapinzani wa klabu yake ya Ligi ya Premia. (inews) Chanzo cha picha, Reuters Newcastle itapatia kipaumbele usajili wa mabeki wawili wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa baada ya Mholanzi Sven Botman, 24, na Muingereza Jamaal Lascelles, 30, kukabiliwa na majeraha ya muda mrefu. (Football Insider) Mshambuliaji wa Uswidi Viktor Gyokeres, 25, yuko juu kwenye orodha ya washambuliaji wa Arsenal, lakini Sporting Lisbon wanatarajia kipengele cha kuachiliwa kwa mchezaji huyo cha euro 100m (£85.6m) kuchochewa ili aondoke. (Caught Offside) Kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 28, atalazimika kukatwa mshahara mkubwa ikiwa anataka kondoka Manchester City na kurejea Leeds United msimu huu wa joto. (Mirror) Chanzo cha picha, Getty Images West Ham haina mpango wa kubadilisha mkataba wa mkopo wa Phillips kuwa wa kudumu katika klabu hiyo. (Football Insider) Manchester United wameanza majadiliano kuhusu kumsajili beki wa Nice mwenye umri wa miaka 23 Melvin Bard, huku wakilenga kusajili beki mpya. (Evening Standard) Beki wa Wolves Muingereza Max Kilman, 26, pia yuko kwenye orodha ya wachezaji wanaowania uhamisho wa majira ya kiangazi ya Manchester United. (Times - usajili unahitajika) Chanzo cha picha, Getty Images Leicester City wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Muingereza Eddie Nketiah mwenye umri wa miaka 24 lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Crystal Palace na Brentford. (Football Transfers) Arsenal, Liverpool na Manchester United ni miongoni mwa klabu za Ligi Kuu ya England zinazomuwania beki wa Bayer Leverkusen Jeremie Frimpong. Mholanzi huyo, 23, atapatikana kwa £35m msimu wa joto. (Football Insider) Newcastle wanavutiwa na kiungo wa kati wa Real Madrid Muhispania Dani Ceballos, 27. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Liverpool na Bayern Munich wanatathmini upya mipango yao baada ya kocha Xabi Alonso kuamua kusalia Bayer Leverkusen, huku Barcelona wakitazamia kukamilisha dili la kumnunua kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim kama mbadala wa Xavi anayeondoka. (Independent) Hata hivyo, bodi ya Barcelona inataka kumshawishi Xavi kuondoka na inamtaka abaki Nou Camp. (Athletic - Usajili unahitajika) Arsenal wamewasiliana na Bayern Munich kuhusu uhamisho wa kiungo wao wa kati wa Ujerumani Joshua Kimmich, lakini wameambiwa mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 hautajadiliwa hadi msimu wa joto. (Football transfers) Chanzo cha picha, Getty Images Arsenal pia wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kumsajili kiungo wa kati wa Real Sociedad Mhispania Martin Zubimendi, 25, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Bayern Munich. (Caught offside) Manchester City na Liverpool wanatarajia juhudi zao za kumsajili kiungo wa kati wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Florian Wirtz, 20, yatatatizwa na uamuzi wa Xabi Alonso kusalia na katika klabu hiyo ya Bundesliga. (HITC) Manchester United imewajumuisha wachezaji Jarrad Branthwaite,21, wa Everton, Aaron Anselmino ,19, wa Boca Juniors na mchezaji wa kimataifa wa Senegal Mikayil Faye kwenye orodha yao ya kuimarisha safu ya ulinzi msimu huu. (Mail) Jadon Sancho, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Borussia Dortmund, anaweza kupata fursa nyingine Manchester United ikiwa klabu hiyo itamteua Jason Wilcox wa Southampton kama mkurugenzi wao wa soka. Wilcox alifanya kazi na mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 katika chuo cha soka cha Manchester City. (Manchester Evening News) Chanzo cha picha, Getty Images Manchester United wana nia ya kumteua meneja wa Ipswich Kieran McKenna kama kocha wao mpya. Raia huyo wa Ireland Kaskazini, 37, aliwahi kufanya kazi katika klabu hiyo kama kocha msaidizi chini ya Jose Mourinho na Ole Gunnar Solskjaer. (Football Insider) Real Madrid ingependa kumsajili beki wa kati wa Lille Leny Yoro, 18, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Manchester United, Liverpool na Chelsea - msimu huu baada ya Mfaransa huyo kuiambia klabu yake kuwa anataka changamoto mpya. ( Athletic- Usajili unahitajika) Tottenham huenda ikalazimika kumuuza mlinzi wa Brazil Emerson Royal, 25, ili kusaidia fedha za uhamisho wao katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images Kiungo wa kati wa Leeds United na England chini ya umri wa miaka 21 na beki wa kulia Archie Gray, 18, anatazamwa na Real Madrid na Bayern Munich pamoja na timu nyingi za Ligi kuu ya England. (HITC) Beki wa Barcelona na Uhispania Marcos Alonso, 33, yuko kwenye mazungumzo ya ya ngazi ya juu na Atletico Madrid kuhusu kujiunga kwa uhamisho wa bila malipo msimu huu wa joto. (Cadena Ser - kwa Kihispania) Birmingham wako kifua mbele, kumsajili beki wa Queen's Park wa chini ya miaka -18, Darryl Carrick, baada ya kumfuatilia kiungo huyo wa kati wa Scotland mara kadhaa msimu huu. (Team Talk) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
Chanzo cha picha, Getty Images Newcastle wanatarajiwa kurejelea azma yao ya kumnunua mlinda lango wa Arsenal Muingereza Aaron Ramsdale, 25, msimu huu wa joto huku wakimlenga kipa mwenye umri mdogo zaidi. (Mail) Newcastle wanajiandaa kupokea ofa kutoka kwa Arsenal na Tottenham, ambazo huenda zikagharimu pauni milioni 100, kwa mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, 24, huku vilabu vikitazamia kuchukua fursa ya hitaji la Magpies kutafuta fedha za kuwaruhusu kurejesha kikosi chao ndani ya sheria za usawa wa kifedha. (Sun) Tottenham na Newcastle wameambiwa watalazimika kulipa zaidi ya pauni milioni 50 iwapo wanataka kumsajili kiungo wa zamani wa England wa chini ya miaka 21 Morgan Gibbs-White, 24, kutoka Nottingham Forest, ambaye huenda akalazimika kumuuza kwa sababu ya matatizo yao ya kifedha. (Football Insider) Chanzo cha picha, Getty Images West Ham italazimika kulipa pauni milioni 60 kama wanataka kumsajili kiungo wa kati wa Everton na Ubelgiji Amadou Onana, 22. (Football Insider) Manchester City wanatarajiwa kumweka kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 28, kwa uhamisho wa kudumu msimu wa joto kwa bei ya pauni milioni 30. (Mail) Liverpool, Tottenham na AC Milan wako tayari kupigania saini ya beki wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo, 26, kwa uhamisho wa bure msimu huu wa joto. (Sun) Real Madrid wanatathmini uwezekano wa kumsajili beki wa kulia wa Chelsea na England Reece James lakini wanatarajia dili lolote kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kuwa gumu kwa sababu amesalia na miaka minne kumaliza mkataba wake. (Fichajes - kwa Kihispania) Chanzo cha picha, Getty Images Beki wa Barcelona na Uhispania Marcos Alonso, 33, anatarajiwa kuondoka bila malipo msimu huu wa joto, huku kiungo wa kati wa Uhispania na beki wa pembeni Sergi Roberto pia akaondoka bila malipo. (Fabrizio Romano) Nyota wa zamani wa Barcelona na Paris St-Germain Neymar, 32, anapanga kurejea kwao Brazil na Santos mnamo 2025 mkataba wake na klabu ya Al-Hilal ya Saudi Arabia utakapomalizika. (Goal) Barcelona wamesitisha mpango wa kumnunua Estevao Willian, 17 wa Palmeiras na Brazil ambaye amepewa jina la 'Messinho', katika hatua inayotoa nafasi kwa Chelsea na Paris St-Germain kumsajili. (Sport - kwa Kihispania) Imetafsiriwa na Ambia Hirsi
2
README.md exists but content is empty. Use the Edit dataset card button to edit it.
Downloads last month
6
Edit dataset card