id
stringlengths
1
6
url
stringlengths
31
202
title
stringlengths
1
120
text
stringlengths
8
182k
2142
https://sw.wikipedia.org/wiki/Pel%C3%A9
Pelé
Pelé (jina lake halisi ni Edison Arantes do Nascimento; 23 Oktoba 1940- 29 Desemba 2022) alikuwa mchezaji wa mpira wa miguu kutoka Brazili. Anahesabiwa na wengi, kama waandishi wa habari na mashabiki, kuwa mchezaji mzuri zaidi wa wakati wote. Alicheza kama mshambuliaji wa kati. Aliisaidia Brazili kutwaa kombe la dunia 1958, 1962 na baadaye tena mwaka 1970. Aliweka rekodi mwaka 1958 ya kuwa mchezaji mdogo kuliko wote duniani kucheza katika fainali ya kombe la dunia alipocheza akiwa na umri wa miaka 17. Alivuma sana katika miaka ya 1970 duniani kote. Mwaka 1999 alichaguliwa na shirikisho la mpira wa miguu duniani kuwa mchezaji bora wa karne. Kwa mujibu wa shirikisho la mpira wa miguu alikuwa mfungaji bora wa muda wote kwa kufunga magoli 1281 kati ya mechi 1363. Ana wastani wa goli moja kwa kila mechi katika uchezaji wake wote. Katika kipindi cha uchezaji wake alikuwa mchezaji anayelipwa pesa nyingi duniani. Pelé alianza kuichezea Santos akiwa na umri wa miaka 15 na timu ya taifa ya Brazil akiwa na miaka 16.Katika ngazi za kimataifa alishinda kombe la dunia mara tatu 1958,1962 na 1970,akiwa ni mchezaji wa pekee kufanya hivyo.Ni mchezaji wa kibrazili anayeongoza kwa magoli mengi zaidi kwa kufunga magoli 77 kwenye mechi 92.Kwenye ngazi ya klabu ni mfungaji bora wa muda wote katika klabu ya Santos, na aliisaidia kubeba taji la Copa Libertadores kwa miaka ya 1962 na 1963.Kwa mchezo wake wa haraka ,chenga zake na magoli yake ya ajabu yalimpa umaarufu duniani kote.Tangu alipostaafu mwaka 1977,Pelé amekuwa balozi wa mpira wa miguu duniani. Pelé alikuwa na uwezo wa kuupiga mpira kwa mguu wowote ili kuwazidi ujanja wapinzani wake uwanjani.Akiwa bila mpira kwa muda mrefu hurudi nyuma na kufanya kazi ya kukabana kusambaza mipira na kutumia uwezo wake wa kupiga pasi kwa kutoa pasi za zinazozaa mabao na kutumia uwezo wake wa kukokota mpira kuwapita wapinzani.Brazil wanamuheshimu kama shujaa wa taifa kwa mchango wake wa kisoka na sera zilizosaidia katika kupunguza umaskini katika nchi hiyo.Katika uchezaji wake na mpaka kustaafu amepokea tuzo nyingi za timu na za binafsi kwa uwezo wake anapokuwa uwanjani na uvunjaji rekodi wake. Maisha ya awali Pelé alizaliwa mjini Três Corações, Minas Gerais, Brazil, na ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Fluminense Dondinho (mtoto wa João Ramos do Nascimento) na Celeste Arantes.Ni mkubwa kati ya watoto wawili. Alipewa jina la shujaa wa Kimarekani Thomas Edison. Wazazi wake waliamua kuitoa herufi "i" na kumuita "Edson",lakini kulikuwa na makosa kwenye cheti chake cha kuzaliwa kusababisha litumike jina la "Edison" badala ya "Edson".F amilia yake walimpa jina la "Dico". Alipewa jina la "Pelé" alipokuwa shule inaposemekana kuwa alishindwa kutamka jina la golikipa wa timu ya Vasco Da Gama anayeitwa Bilé,alivyozidi kulitamka ndivyo alivyozidi kuchapia. Pelé aliwahi kusema hakujua maana ya jina hilo wala marafiki zake waliompa jina hilo.Lakini jina hilo lilitokana na jina la Bilé lakini kwa Kiebrania maana yake ni maajabu (פֶּ֫לֶא),lakini jina halina maana yoyote kwa KIreno. Pelé alikulia katika hali ya umaskini huko Bauru kwenye mji wa Paulo.Alijikusanyia fedha kidogo alipofanya kazi kwenye duka la chai.Alfundishwa kucheza mpira wa miguu na baba yake lakini hakuweza mara acheze na soksi iliyojazwa na magazeti au magada ya mapera huku akifunga na kamba.Amechezea klabu nyingi za vijana kama Sete de Setembro, Canto do Rio, São Paulinho, na Amériquinha. Pelé aliisaidia Bauru Athletic Club klabu ya vijana (ikifundishwa na Waldemar de Brito) kushinda mataji mawili ya mashindano ya klabu za vijana za São Paulo.Pelé alishindana mashindano ya mpira wa miguu ya ndani ya chumba ambapo aliisaidia timu yake ya Bauru. Pelé aliwahi kukiri kuwa mashindiano hayo yana changamoto kubwa,alisema kuwa kuwa mchezo huo ulikuwa wa haraka kidogo kuliko mpira wa miguu wa kwenye nyasi na kwamba mchezo huo ulihitaji uwezo mkubwa wa kufikiri haraka kwa kuwa kila watu wanakuwa karibukaribu ndani ya uwanja.Pelé anauheshimu sana mchezo huo kwa kuwa ulimpa uwezo mkubwa wa kufikiri papo kwa papo anapokuwa uwanjani.Licha ya hivyo mchezo huo ulimpa uwezo wa kuchezaccredits indoor football for helpin na wakubwa zaidi rika lake alipokuwa na umri wa miaka 14.Katika kila mashindano aliyowahi kucheza alikuwa akichukuliwa kama mdogo asingeweza kucheza lakini kila mashindano yanapoisha yeye ndiye anayekuwa mfungaji bora akiwa na magoli kumi na nne au kumi na tano."Hicho kilinipa kujiamini zaidi", Pelé alisema"Hapo nilijua kuwa nisiwe mwoga kwa chochote kile". Ngazi ya klabu Santos Mwaka 1956, de Brito alimpeleka Pelé Santos,mji wa viwanda na bandari karibu na São Paulo,alienda kwa majaribio kwenye klabu ya Santos FC,akiwaambia mabosi kuwa kijana wa miaka 15 atakuwa mchezaji mkubwa duniani.Pelé alimshangaza kocha Lula wakati majaribio kwenye uwanja wa Estádio Vila Belmiro, na akasaini mkataba na klabu hiyo Juni 1956.Pelé alitangazwa sana kwenye vyombo vya habari kuwa nyota wa baadae.Alianza vizuri Septemba 7 1956 akiwa na umri wa miaka 15 kwenye ushindi wa 7-1 dhidi ya Corinthians Santo Andre akishinda goli la kwanza. Wakati msimu wa 1957 ulipoanza, Pelé alipewa nafasi katika kikosi cha kwanza akiwa na umri wa miaka 16 akawa mfungaji bora wa ligi.Miezi kumi baadaye aliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Brazil.Baada ya kombe la dunia la 1958 na 1962,klabu tajiri za Ulaya kama Real Madrid, Juventus and Manchester United, walijaribu kutaka kumsajili.Mwaka 1958 Iner Milan walimsajili lakini Angelo Moratti ilimbidi akatishe mkataba huo baada ya mwenyekiti wa klabu ya Santos kushambuliwa na shabiki wa Kibrazili.Lakini mwaka 1961 serikali ya Brazil chini ya rais Jânio Quadros ilisema kuwa Pelé ni mchezaji kivutio kwa nchi hivyo haruhusiwi kuhamishwa kwenda nje ya nchi. Pelé alishinda taji kubwa kwa mara ya kwanza akiwa na Santos mwaka 1958 ambapo timu ailishinda taji la Campeonato Paulista; Pelé alimaliza mashindano akiwa mfungaji bora wa magoli 58, rekodi inayoshikiliwa hadi sasa.Mwaka mmoja baaadaye aliisaidia nchi yake kushinda mabao 3-0 dhidi ya Vasco Da Gama kwenye michuano ya Torneio Rio-São Paulo Santos hawakuwa na uwezo wa kushindana kwenye michuano hiyo.Mwaka 1960, Pelé alifunga magoli 33 akiisaidia timu yake kurudi tena kwenye michuano ya Campeonato Paulista na kubeba taji hilo lakini walifungwa kwenye michuano ya Rio-São Paulo baada ya kumaliza wakiwa nafasi ya nane.Kwenye msimu wa 1960, Pelé alifunga magoli 47 na kuisaidia Santos kubeba taji la Campeonato Paulista.Walisonga mbele na kubeba taji la Taça Brasil mwaka huohuo kwa kuwafunga Bahia kwenye fainali.Kwenye fainali,Pelé aliibuka mfungaji bora akiwa na magoli 9. Mwaka 1973 Pele aliitwa mpira wa miguu bora katika Amerika ya Kusini. Ngazi ya kimataifa Mechi ya kwanza ya Pelé kimataifa ilikuwa dhidi ya Argentina waliposhinda 2-1 Julai 7 1957 uwanja wa Maracanã.Kwenye mechi hiyo alifunga goli lake la kwanza akiwa na timu yake ya taifa akiwa na miaka 16 na miezi tisa na anabaki kuwa mchezaji mdogo wa Brazili kuwahi kufinga goli kwenye timu yake ya taifa. Kombe la dunia 1958 Pelé alienda nchini Sweden akiwa na jeraha la goti lakini wenzake walimtetea ili aitwe kwenye kikosi.Mechi yake ya kwanza ilikuwa dhidi ya USSR kwenye mechi ya tatu kwenye mzunguko wa kwanza wa kombe la dunia la mwaka 1958,ambapo alimpa pasi Vavá iliyozaa goli la pili.Alikuwa mchezaji mdogo kuliko wote kwenye michuano na mchezaji mdogo kuwahi kucheza kombe la dunia.Dhidi ya Ufaransa kwenye nusu fainali,Brazili walikuwa wakiongoza 2-1. Kifo Mnamo Desemba 29, 2022, Pelé alifariki akiwa na umri wa miaka 82 katika hospitali ya Israeli ya Albert Einstein huko São Paulo, Brazil. Wakala wake Joe Fraga alithibitisha kifo chake. Pelé alikuwa akitibiwa kansa ya utumbo mkubwa tangu mwaka 2021 na alikuwa amelazwa hospitalini kwa mwezi mmoja uliopita. Marejeo Waliozaliwa 1940 Wachezaji mpira wa Brazil Waliofariki 2022
2145
https://sw.wikipedia.org/wiki/Eastleigh
Eastleigh
Eastleigh ni jina la Eastleigh (Uingereza) ni mji wa Uingereza wa kusini karibu na Southampton katika wilaya ya Hampshire Kutokana na mji huu ni jina la maeneo yaliyowahi kutawaliwa na Uingereza katika sehemu mbalimbali ya dunia: Eastleigh (Nairobi) ni mtaa au eneo la mji mkuu wa Kenya inayopakana na mitaa ya Pangani pia Mathare Valley Eastleigh (Edenvale) ni mtaa wa mji wa Edenvale katika jimbo la Gauteng, Afrika Kusini Jina limetokana na maneno "east" = mashariki na "leigh" kutokana na Kiingereza ya Kale "leah" / "legh" yaani aina ya mti. Makala zinazotofautisha maana
2146
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tanga
Tanga
Tanga ni jina la Mkoa wa Tanga katika Tanzania Wilaya ya Tanga, Tanzania Mji wa Tanga Tanga (Songea) - kata katika mkoa wa Ruvuma, Tanzania Neno "Tanga" linamaanisha pia Tanga (chombo), kitambaa kikubwa kinachokingamishwa kwenye mlingoti wa jahazi Tanga (pesa), sarafu ndogo huko Tajikistan (100 Tanga = 1 Rubel) Tanga (nguo), aina za chupi za wakinamama zinazohitaji kitambaa kidogo sana Tanga (kundinyota) Kuna pia filamu ya Kibrazilia yenye jina la "Tanga" ambamo Tanga ni jina la kisiwa kidogo. Makala zinazotofautisha maana
2150
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Tanga
Mkoa wa Tanga
Mkoa wa Tanga ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania na uko Kaskazini Mashariki mwa nchi, ukipakana na Kenya upande wa Kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki na mikoa ya Morogoro, Manyara na Kilimanjaro wenye Postikodi namba 21000. Mpaka upande wa kusini unafuata mto Mligaji kuutenganisha na mkoa wa Pwani. Makao makuu yako Tanga mjini. Eneo la mkoa Tanga ni kati ya mikoa midogo ya Tanzania ikiwa na msongamano mkubwa wa wakazi ndani ya eneo lake. Msongamano ni mkubwa hasa wilaya ya Lushoto kwenye ardhi yenye rutuba nzuri. Mkoa una eneo la km² 27,348 ambalo linaunganisha sehemu za pwani pamoja na milima ya ndani kama Usambara. Eneo linalofaa kwa kilimo ni km² 17,000. Kuna wilaya 10 ambazo ni Handeni Vijijini, Handeni Mjini, Kilindi, Korogwe Vijijini, Korogwe Mjini, Lushoto, Mkinga, Muheza, Pangani na Tanga Mjini. Hali ya hewa Kwa jumla hali ya hewa ni joto lenye unyevu. Handeni kuna joto kavu zaidi. Milima ya Usambara hakuna joto sana. Miezi ya Desemba - Machi halijoto huko Tanga inafikia sentigredi 30-32 mchana na 26-29 usiku. Wakati wa Mei hadi Oktoba halijota inapoa: ni sentigredi 23-28 mchana na 20-24 usiku. Unyevu iko juu kati ya asilimia 100 na asilimia 65. Maeneo mengi ya mkoa hupokea angalau milimita 750 za mvua kwa mwaka au zaidi. Pwani ni zaidi: takriban milimita 1,100 hadi 1,400 ikipungua sehemu za ndani isipokuwa milima ya Usambara ambako mvua inaweza kuzidi milimita 2000 kwa mwaka. Wakazi Mwaka 2022 wakazi waliohesabiwa katika sensa walikuwa 2,615,597 kutoka 2,045,205 wa mwaka 2012. Makabila makubwa mkoani Tanga ni Wasambaa, Wazigua, Wabondei na Wadigo. Mengine ni Wapare, Wataita, Wambugu, Wasegeju na Wanago. Pia kuna Waarabu wengiwengi wenye asili ya Oman. Wasambaa ndio kabila kubwa lililoko katika milima ya Usambara, Muheza, Korogwe na Lushoto. Kwa jumla ndio asilimia 40 ya wakazi wote wa mkoa. Wazigua ni kabila kubwa huko Handeni na sehemu za Korogwe na Pangani. Wabondei wako hasa Muheza na sehemu za Pangani. Wadigo ndio wengi Tanga yenyewe na sehemu za pwani. Elimu Katika mkoa huu elimu inahitaji kuboreshwa zaidi, hasa maeneo ya vijijini, maana watu wengi wa mkoa huu hufanya shughuli zao za kimila; hali hiyo huwafanya kushindwa kuendelea na shughuli za kimaendeleo katika taifa la Tanzania. Wilaya ya Handeni kuna machimbo ya madini, ila kuhusu elimu ipo nyuma sana kwani mpaka sasa hakuna shule ya sekondari inayotoa huduma ya kidato cha tano na sita. Kama haitoshi shule za watu binafsi hakuna hata moja. Uchumi Wakazi wengi hutegemea kilimo cha riziki pamoja na ufugaji na uvuvi. Mazao ya chakula hasa ni mahindi, muhogo, ndizi, maharagwe na mpunga. Mazao ya biashara ni katani, pamba, kahawa, chai, nazi, tumbaku na korosho. Mifugo ni ng'ombe, mbuzi na kondoo pamoja na kuku. Katani ilikuwa zao la biashara hasa kwa ajili ya Tanga tangu kuingizwa kutoka Mexico zamani za Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hulimwa kote mkoani isipokuwa Lushoto, hasa Muheza na Korogwe kwenye mashamba makubwa. Mashamba hayo yalikuwa ya walowezi, yakataifishwa baada ya uhuru. Tangu kuanguka kwa sekta ya umma yamebinafsishwa tena siku hizi. Zao la katani linategemea sana soko la dunia, umuhimu wake ulirudi nyuma tangu miaka ya 1960. Tanga ilikuwa na viwanda vingi kiasi katika miaka ya 1960 na 1970 lakini karibu vyote vimekwama kutokana na siasa ya Ujamaa na uchumi wake ulioiga mfumo wa nchi za kisoshalisti. Viwanda vichache vilivyobaki havizalishi mali kulingana na uwezo wao. Kilichobaki hasa ni kiwanda cha saruji Tanga. Utalii umeanza kupanuka kidogo, hasa katika eneo la Pangani, Mapango ya Amboni na kituo cha Makumbusho Urithi Tanga. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Tanga Mjini : mbunge ni Ummy Mwalimu (CCM) Bumbuli : mbunge ni January Makamba (CCM) Mlalo : mbunge ni Rashid Abdakkag Shangazi (CCM) Pangani : mbunge ni Jumaa Hamidu Aweso (CCM) Kilindi : mbunge ni Omari Mohamed Kigua (CCM) Mkinga : mbunge ni Dustan Kitandula (CCM) Handeni Vijijini : mbunge ni Mboni Mohamed Mhita (CCM) Muheza : mbunge ni Hamis Mohammed Mwinjuma (CCM) Korogwe Mjini : mbunge ni Pius Kimea (CCM) Korogwe Vijijini : mbunge ni Stephen Hillary Ngonyani (CCM) Lushoto : mbunge ni Handeni Mjini : mbunge ni Omary Abdallah Kigoda (CCM) Tazama pia Mkoa wa Tanga (DOA) - kuhusu mkoa wa zamani chini ya ukoloni wa Kijerumani Orodha ya milima ya mkoa wa Tanga Orodha ya mito ya mkoa wa Tanga Tanbihi Viungo vya nje Tanga Region Socio-Economic Profile (PDF) T
2152
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kijerumani
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani (au: ya Kidachi; kwa Kijerumani Deutsch-Ostafrika -DOA-; kwa Kiingereza German East Africa) ilikuwa jina la koloni la Ujerumani huko Afrika ya Mashariki kati ya miaka 1885 na 1918/1919. Eneo lake lilijumlisha nchi za kisasa za Tanzania bara (yaani bila Zanzibar), Burundi na Rwanda. Ilikuwa koloni kubwa kabisa la Dola la Ujerumani. Eneo, mipaka na wakazi Eneo na mipaka Eneo la koloni lilikuwa na kilomita za mraba 997,000 pamoja na sehemu za maziwa makubwa kama Ziwa Tanganyika na Ziwa Viktoria. Eneo hili lilikuwa karibu mara mbili kuliko eneo la Ujerumani wenyewe kabla ya mwaka 1914. Mipaka iliamuliwa katika mapatano na Uingereza, Ubelgiji na Ureno zilizotawala makoloni ya jirani ya Afrika ya Mashariki ya Kiingereza (leo Kenya na Uganda), Kongo ya Kibelgiji (leo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo), Rhodesia (leo Zambia na Zimbabwe), Nyasaland (leo Malawi) na Msumbiji. Mipaka hii ni pia mipaka ya Tanzania, Rwanda na Burundi hadi leo hii. Katika mapatano baina ya Uingereza na Ujerumani ya Novemba 1886 pande zote mbili ziliahidi kuheshimu utawala wa Sultani wa Zanzibar juu ya visiwa pamoja na kanda la maili 10 kwenye pwani baina ya mto Tana na Mto Minengani (Msumbiji). Pamoja na hayo walielewana kuhusu maeneo ya maslahi yao, wakipatana kuhusu mstari uliokuwa baadaye mpaka baina ya Tanzania na Kenya hadi leo. Katika mkataba wa 1890 kuhusu mipaka katika Afrika Uingereza iliahidi kumshawishi Sultani wa Zanzibar kuuza maeneo yake kwenye pwani la bara pamoja na kisiwa cha Mafia kwa Ujerumani. Upande wa Kenya mstari ulichorwa kuanzia Bahari Hindi kwa mdomo wa mto Umba hadi Ziwa Jipe, halafu kufuata mitelemko ya kaskazini ya mlima Kilimanjaro na kutoka hapa hadi Ziwa Viktoria. Mipaka na Uganda ilifuata latitudo ya kwanza ya kusini ya ikweta hadi mpaka na Kongo. Upande wa Kongo mpaka ulifuata sehemu za chini za bonde la Ufa na katikati ya maziwa kama Kivu na Tanganyika. Upande wa kusini ulifuata mstari kati ya ncha ya kusini ya ziwa Tanganyika hadi mdomo wa Mto Songwe katika Ziwa Nyasa. Eneo lote la ziwa lenyewe lilibaki upande wa Nyasaland ya Kiingereza, halafu mstari kutoka Ziwa Nyasa kwa kufuata mto Ruvuma hadi Rasi ya Delgado kwenye Bahari Hindi. Jinsi ilivyo na mipaka ya kikoloni mistari hii ilikata mara nyingi maeneo ya makabila ya wenyeji. Wakazi Mwaka 1913 takwimu ya Wajerumani ilihesabu wakazi Waafrika 7,645,000, Waasia (Wahindi na Waarabu) 14,898 na Wazungu 5,336, kati yao Wajerumani 4,107. Nusu ya wakazi wote waliishi katika eneo la maziwa makubwa ambako serikali ya kikoloni iliacha maeneo ya Rwanda (wakazi 2,000,000), Burundi (1,500,000) na Bukoba (275,000) kama maeneo lindwa chini ya watawala wa kienyeji waliosimamiwa na afisa mkazi Mjerumani. Historia ya koloni Koloni hilo halikuanzishwa kwa azimio la kisiasa upande wa serikali ya Ujerumani bali lilianzishwa kama mradi wa watu binafsi waliotafuta makoloni katika Afrika. Historia ya koloni ilikuwa na awamu tatu: mwanzo kama maeneo yaliyotawanyika ambako kampuni binafsi (Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki) ilifaulu kushawishi watawala wa kienyeji kutia sahihi kwenye mikataba; kipindi hiki kilianza 1885 hadi kuporomoka kwa utawala wa kampuni mnamo 1890 koloni la Dola la Ujerumani (kwa Kijerumani Deutsches Reich) lililoamua kuchukua mamlaka mkononi mwake kuanzia 1891, ambako Ujerumani iliweza kupanusha utawala wake juu ya maeneo yote mwisho wa utawala wa Kijerumani wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia kuanzia mwaka 1916 wakati jeshi kubwa la Uingereza na Afrika Kusini pamoja na Ubelgiji lilivamia, hadi kusalimu amri kwa jeshi la Schutztruppe kwenye Novemba 1918 Katika mapatano baada ya vita koloni liligawiwa kati ya Uingereza (iliyopata Tanganyika) na Ubelgiji (iliyopata Rwanda na Burundi). Kwa historia ya baadaye ilikuwa na maana ya kwamba walikabidhiwa maeneo ya koloni la Kijerumani la awali si kama mali kamili lakini kama maeneo ya kudhaminiwa kwa niaba ya shirikisho la Mataifa (mtangulizi wa Umoja wa Mataifa (UN). Utangulizi Hadi mnamo mwaka 1880 serikali ya Ujerumani chini ya chansella Otto von Bismarck ilikataa kuanzisha makoloni. Sehemu ya wafanyabiashara Wajerumani walidai koloni. Walisikitika kuona faida za wenzao Waingereza waliopata mara nyingi msaada kutoka kwa wanajeshi na serikali za koloni za Uingereza hasa Asia. Waliona pia faida ya viwanda vya Uingereza vilivyokuwa na soko la kulindwa katika nchi kama Uhindi kwa sababu serikali ya kikoloni ilidai kodi kali kwa bidhaa zisizotoka Uingereza. Bismarck hakuamini ya kwamba koloni lingeleta faida kwa taifa kulingana na gharama kubwa kwa serikali. Lakini wapigania koloni walikuwa na wabunge muhimu kwa serikali na polepole Bismarck alianza kukubali hatua za kwanza. Mwenyewe aliamini mwanzoni ya kwamba itatosha kuwapa wafanyabiashara ulinzi kwa shughuli zao kwa kuwaruhusu matumizi ya bendera ya Ujerumani na kuwa na askari wao wa ulinzi kama wamepatana na viongozi wazalendo katika eneo fulani kuanzisha shughuli huko. Kwa njia hii alifungua mlango kwa harakati iliyoendelea kuwa mchango wa Ujerumani katika mbio wa kugawa dunia, hasa Afrika. Juhudi za Karl Peters Koloni hili lilianzishwa na kijana Mjerumani Karl Peters mwaka 1885 kwa niaba ya "Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki". Peters, aliyewahi kusoma chuo Uingereza, aliona wivu juu ya ukoloni wa Uingereza, akiamini ya kwamba Ujerumani ungestahili nafasi hiyo pia. Hivyo alianza kudai koloni katika mikutano, akaanzisha "Shirika kwa Ukoloni wa Kijerumani" mwaka 1884 iliyokuwa kitangulizi cha kampuni. Shirika hii ilimtuma pamoja na wenzake wawili kwenda Afrika na kutafuta nafasi ya kuanzisha koloni. Kiasili walilenga maeneo mpakani mwa Msumbiji na Zimbabwe ya leo lakini hatimaye waliamua kwenda Afrika ya Mashariki. Peters alifika Zanzibar alipoambiwa na konsuli ya Ujerumani ya kwamba hawezi kuendelea: serikali ya nyumbani iliogopa ugomvi na Uingereza ilikataa mipango yake. Aliamua kuvuka barani hata hivyo akafika Saadani tarehe 10 Novemba 1884 na kufuata njia kando ya mto Wami ili apite kanda la Kizanzibari kwenye pwani na kutembelea machifu na masultani ndani ya bara. Hapo alifaulu kushawishi watawala wa maeneo yaliyojulikana kama Usagara, Nguru, Useguha na Ukami kutia sahihi kwenye mikataba iliyoandikwa kwa Kijerumani ambayo hawakuielewa. Mikataba hii ilisema ya kwamba mtawala alikabidhi kwa kampuni nchi yake pamoja na haki juu ya ardhi na mali yote. Mwaka 1885 Peters alirudi Berlin na kuonyesha mikataba yake kwa magazeti na serikali. Chansela Bismarck alikataa, akacheka mikataba kama karatasi bila maana. Peters alitumia mbinu: akatisha kupeleka mikataba yake kwa mfalme Leopold II wa Ubelgiji aliyekuwa kununua haki zake. Hapa Bismarck aliogopa kilio cha wapenda koloni akakubali kumpa Peters hati ya ulinzi ya tarehe 27 Februari 1885 kwa maeneo yaliyokuwa ya kampuni kufuatana na mikataba. Upanuzi wa eneo la kampuni Upanuzi na ugomvi na Zanzibar Peters na wawakilishi wake walirudi wakaendelea kutafuta machifu waliokuwa tayari kutia saini mikataba yake. Sultani wa Zanzibar alipinga juhudi hizi. Zanzibar ilisimamia pwani ya Afrika ya Mashariki na tangu karne watu wa miji ya pwani walikuwa na mawali wa Sultani. Zanzibar ilidai pia utawala ya bara hadi Ziwa Tanganyika na Kongo, ingawa hali halisi athira yake haikwenda mbali na njia za misafara ambako ndovu na watumwa walipelekwa pwani. Tarehe 27 Aprili 1885 serikali ya Zanzibar ilituma barua Berlin kupinga kazi na madai ya kampuni na kutangaza maeneo ya Tanzania ya leo kama milki yake. Iliongeza pia wanajeshi wake barani zilizokuwa chini ya amri ya mwanajeshi mstaafu Mwingereza Matthews. Hapo serikali ya Berlin ilituma kikosi cha manowari kwenda Bahari Hindi. Mwezi Agosti manowari za Kijerumani chini ya amri ya admirali Eduard von Knorr zilifika mbele ya Unguja zikalenga mizinga yao kwa ikulu ya sultani. Akishauriwa na balozi wa Uingereza, Sultani Bargash alipaswa kutoa tamko kuwa, "Kutokana na madai tunayopelekewa kwa matishio na Kaisari wa Ujerumani, tunatambua ulinzi wa Ujerumani juu ya nchi za Usagara, Nguru, Useguha, Ukami na juu ya wilaya ya Witu. Mipaka yake itaelezwa baadaye na sisi tunatambua ulinzi wa Kaisari juu ya mahali palipotajwa." . Sultani alipaswa pia kutia sahihi mkataba wa biashara na Ujerumani alipokubali haki nyingi kwa Wajerumani katika milki yake. Mwaka 1886 Uingereza na Ujerumani walipatana juu ya "maeneo ya masilahi" yao katika Afrika ya Mashariki; hapa walielewana kuhusu mstari kati ya mdomo wa mto Umba (kati ya Tanga na Mombasa) hadi nukta ambako latitudo ya 1 kusini inakata mwambao wa Ziwa Viktoria Nyanza. Sultani alipaswa kukubali tena. Katika mapatano hayo Sultani alibaki na visiwa vya Unguja, Pemba, Mafia na funguvisiwa ya Lamu pamoja na kanda la pwani barani lenye upana wa maili 10 kati ya mto Ruvuma upande wa Kusini na mto Tana upande wa Kaskazini, halafu miji ya Kismayu, Barawa, Merka na Mogadishu upande wa kaskazini zaidi. . Mkataba kati ya Zanzibar na Kampuni juu ya kofo na pwani Mapatano ya 1886 yaliwapa Wajerumani nafasi ya kuendeleza upanuzi barani nyuma ya kanda la pwani la Kizanzibari na mstari wa mpaka ulichorwa kuanzia mdomo wa mto Umba kupitia mlima Kilimanjaro hadi Ziwa Viktoria. Lakini kwa ajili ya matumizi ya kibiashara suala la mabandari bado lilibaki wazi. Hapo Peters na kampuni yake walianza kujadiliana na Sultani Seyyed Bargash (alitawala 1870 hadi 1888) kuhusu utawala wa pwani katika sehemu ya Tanganyika. Mnamo mwaka 1887 Bargash alikuwa amechoka: alitafuta pesa tu kwa ajili yake binafsi; alikuwa tayari kukodisha utawala wa kanda la pwani ya Tanganyika kwa Wajerumani. Wajerumani walidai kuongezeka haki na Bargash alikufa bila kumaliza mapatano. Lakini mwandamizi wake Sultani Seyyed Khalifa aliwapa Wajerumani walichotaka. Tarehe 15 Agosti 1888 wawakilishi wa kampuni ya Kijerumani walifika kwenye mabandari yote wakatangaza utawala wao kwa niaba ya sultani. Vita ya Abushiri na mwisho wa utawala wa Kampuni tazama Vita ya Abushiri Badiliko hili lilisababisha upinzani na hatimaye ghasia ya wenyeji. Vipengele vya mkataba vilisema mali isiyokuwa na hati za kimaandishi haiwezi kutambuliwa. Wenye mali kama mashamba walitakiwa kununua hati kutoka kwa watawala wapya. Hapo Waswahili wa pwani walijisikia wamesalitiwa na sultani asiyekuwa na haki ya kuchukua mali zao na kuzipa kwa wageni. Mara baada ya kufika kwa Wajerumani kwenye miji ya pwani ghasia ilianza mjini Pangani na kuenea haraka kote pwani kati ya Tanga na Lindi. Kampuni ilikuwa na Wajerumani wachache tu walioshindwa kujitetea. Walipaswa kukimbia au wakauawa. Bagamoyo pekee palikuwa na kikosi cha askari kutoka manowari ikatetewa. Serikali ya Ujerumani iliona lazima kuingia kati na kutuma manowari pamoja na askari waliokandamiza ghasia. Bismarck alitumia mbinu wa kupata kura za bunge alizohitaji kwa ajili ya gharama ya vita hiyo. Alipeleka sheria bungeni kuwa Ujerumani unatoa mark milioni 2 kwa kupambana na biashara ya watumwa na ulinzi wa manufaa ya Kijerumani. Sasa alimtuma afisa wa jeshi mwenye maarifa ya Afrika, Hermann von Wissmann aliyeajiri maafisa na wanajeshi Wajerumani, kwa jumla watu 87 wakaelekea Afrika ya Mashariki. Njiani walipopita Misri waliajiri askari waliostaafishwa Wasudani 650; waliongeza baadaye askari Wazulu 350 kutoka Msumbiji na kuwaunganisha kuwa "kikosi cha Wissmann" kilichofaulu kushinda upinzani wote kwa msaada wa silaha za kisasa na manowari za Ujerumani. Baada ya upinzani wa wenyeji wa pwani mwaka 1889/1890 wakiongozwa na Abushiri na Bwana Heri serikali ya Ujerumani iliamua kutwaa mamlaka kutoka kwa kampuni na kufanya eneo lote kuwa koloni la Dola la Ujerumani badala ya shirika. Koloni la Dola la Ujerumani Maeneo ya kampuni yalikuwa rasmi koloni la serikali tarehe 1 Januari 1891. Koloni lilisimamiwa na gavana. Magavana wa Kijerumani walikuwa wafuatao: 1891–1893: Julius von Soden 1893–1895: Friedrich von Schele 1895–1896: Hermann von Wissmann 1896–1901: Eduard von Liebert 1901–1906: Gustav Adolf von Götzen 1906–1912: Albrecht von Rechenberg 1912–1918: Heinrich Schnee Utawala wa Kijerumani ulikwisha katika Vita Kuu ya Dunia ya Kwanza (1914 - 1918) kutokana na uvamizi wa Uingereza na Ubelgiji. Katika Mkataba wa Versailles mwaka 1919 eneo la koloni la Kijerumani liligawiwa. Sehemu ya Tanganyika ilikabidhiwa kwa Uingereza na maeneo ya Rwanda na Burundi yaliwekwa chini ya Ubelgiji. Utawala Eneo lote la koloni liligawiwa katika mikoa 21 na maeneo matatu yaliyokuwa bado chini ya watawala wenyeji kwa mfumo wa maeneo lindwa. Hadi 1913 mikoa 19 ilikuwa chini ya utawala wa kiraia, yaani chini ya maafisa wa serikali ya kikoloni. Mikoa miwili ya Iringa na Mahenge ilikuwa bado chini ya utawala wa kijeshi yaani hapo walikuwa maafisa wa Schutztruppe waliotekeleza majukumu yote ya serikali. Mikoa chini ya usamimizi wa maafisa Wajerumani wa kiraia ilikuwa: 1. Tanga (DOA) 2. Pangani (DOA) pamoja na ofisi ndogo Handeni 3. Bagamoyo (DOA) pamoja na ofisi ndogo Saadani 4. Daressalam pamoja na ofisi ndogo ya polisi Kisangire 5. Rufiji (DOA), makao makuu Utete 6. Kilwa (DOA) pamoja na ofisi ndogo za Kilindoni, Kibata na Liwale 7. Lindi (DOA) pamoja na ofisi ndogo za Mikindani, Newala und Tunduru 8. Langenburg (DOA) (Tukuyu) pamoja na ofisi ndogo Itaka na Mwakete na kituo cha polisi Muaja 9. Wilhelmstal (DOA) (Lushoto) 10. Morogoro (DOA) pamoja na ofisi ndogo za Kilossa na Kissaki 11. Songea (DOA) pamoja na ofisi ndogo Wiedhafen 12. Moshi (DOA) 13. Arusha (DOA) pamoja na ofisi ndogo Umbulu 14. Kondoa-Irangi (DOA) pamoja na ofisi ndogo Mkalama 15. Dodoma (DOA) pamoja na kituo cha polisi Mpapwa na kituo cha kijeshi Singida 16. Mwanza (DOA) pamoja na ofisi ndogo Shirati na kituo cha kijeshi Ikoma 17. Tabora (DOA) pamoja na ofisi ndogo za Shinyanga na Ushirombo 18. Ujiji (DOA) pamoja na kituo cha kijeshi Kasulo 19. Bismarckburg (DOA) (Kasanga (Ufipa) Mikoa ya kijeshi (jer. Militärbezirke) chini ya usimamizi wa maafisa wa Kijerumani wa kijeshi: 21. Iringa (DOA) pamoja na kituo cha kijeshi Ubena 22. Mahenge (DOA) Maeneo lindwa (jer. Residentur) chini ya watawala wenyeji waliopaswa kufuata ushauri wa afisa mkazi Mjerumani (jer. Resident): Bukoba pamoja na vituo vya kijeshi Usuwi na Kifumbiro, kwa ajili ya watawala wa Wahaya Rwanda, mji mkuu Kigali, kituo cha kijeshi Mruhengeri Burundi, mji mkuu Gitega, pamoja na ofisi ndogo Usumbura (Bujumbura). Tanbihi Marejeo Pugu Hadi Peramiho - kimehaririwa na P. Gerold Rupper, OSB, BPNP, Peramiho 1988, ISBN 9967 67 031 1 Viungo vya nje Iliffe, John: A Modern History of Tanganyika, Cambridge University Press, 10.05.1979, ISBN 978-0-521-22024-8 Afrika ya Mashariki ya Kijerumani Historia ya Tanzania Historia ya Burundi Historia ya Rwanda
2156
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Pili%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Pili ya Dunia
Vita Kuu ya Pili ya Dunia ilikuwa vita iliyodumu kuanzia mwaka 1939 hadi 1945 kati ya Ujerumani, Italia, Japani na mataifa yaliyoshikamana nazo (Romania, Hungaria na Bulgaria) dhidi ya nchi nyingi za dunia (ziliitwa mataifa ya ushirikiano) kati yake hasa Uingereza, Uchina, Urusi na Marekani. Vita Kuu ya Dunia Jina limetokana na vita ya miaka 1914-1918 iliyoona mapambano kati ya Ujerumani na wenzake dhidi ya nchi nyingi. Vita ya 1914/1918 iliitwa "Vita Kuu ya Dunia" kwa sababu mapigano yalienea pande nyingi za dunia, tofauti na vita zilizotangulia. Kwa namna fulani vita iliyoanza 1939 ilikuwa marudio ya vita iliyotangulia. Hivyo imekuwa kawaida kuzitaja vita hizi kama Vita Kuu ya Kwanza na ya Pili ya Dunia. Mwanzo wa vita Vita hii ilianza huko Ulaya tarehe 1 Septemba 1939 kwa mashambulizi ya Wajerumani dhidi ya Poland. Wengine huhesabu mashambulizi ya Japani dhidi ya Uchina tarehe 7 Julai 1937 kuwa mwanzo wa vita. Mwisho wake ulikuwa huko Ulaya tarehe 9 Mei 1945 halafu huko Asia tarehe 2 Septemba 1945. Vita katika Ulaya Wakati Ujerumani iliposhambulia Poland, nchi hiyo ilikuwa na mikataba ya kulindana na Uingereza na Ufaransa. Hivyo ilibidi Uingereza na Ufaransa zitangaze hali ya vita dhidi ya Ujerumani. Serikali za Australia, New Zealand, Nepal, Afrika Kusini na Kanada zilishikamana na Uingereza kwa kutangaza vita dhidi ya Ujerumani. Umoja wa Kisovyeti ilikuwa na mkataba wa siri na Ujerumani ikaweza kuchukua nafasi ya kuteka sehemu kubwa za Poland ya Mashariki. Baada ya uvamizi wa Poland hali kwenye mpaka na Ufaransa ilibaki kimya ingawa vita ilikuwa imeshatangazwa. Uingereza ilipeleka sehemu kubwa ya jeshi lake huko Ufaransa kwa kusudi la kutetea nchi hiyo kama Ujerumani itashambulia. Mwezi Aprili 1940 Waingereza walianza kupeleka wanajeshi Norway wakiwa na shabaha ya kuzuia kupelekwa kwa madini ya chuma kutoka Sweden kwenda Ujerumani kupitia bandari za Norway. Wajerumani walichukua nafasi hiyo kuteka Denmark na Norway na kufukuza Waingereza. Mnamo Mei 1940 Wajerumani walishambulia Ufaransa. Walitumia mbinu ya kupitia Uholanzi, Ubelgiji na Luxemburg zilizowahi kutangaza kwamba hawako upande wowote katika vita. Mapigano hayo yalikwisha haraka: Wajerumani walishinda na kupiga kikosi cha Waingereza pamoja na jeshi la Ufaransa. Lakini Waingereza walifaulu kuokoa wanajeshi wao kutoka Dunkirk kwa meli walipozingirwa na Wajerumani kwa sababu Hitler aliwaamuru kusubiri. Baadaye walisitasita kushambulia Uingereza yenyewe. Mipango yao ilihitaji mbinu za kuvuka bahari. Wakajaribu kuvuruga nguvu ya kijeshi ya Waingereza kwa mashambulizi ya ndege lakini pia hapo Hitler hakuendelea mashambulio dhidi ya wanahewa wa Uingereza na hatimaye kukosa uwezo wa kutosha. Katika shambulizi dhidi ya Ufaransa Waitalia walishiriki upande wa Wajerumani. Mwisho wa mwaka 1940 Waitalia walianza kushambulia Ugiriki na jeshi la Waingereza huko Misri na Malta. Lakini mahali pote walirudishwa nyuma, hadi dikteta Mjerumani Adolf Hitler alipoamua kuwasaidia Waitalia na kupeleka wanajeshi Wajerumani kwenda Afrika ya Kaskazini pamoja na Ugiriki mwaka 1941. Hii ilisababisha pia Wajerumani kuteka Yugoslavia wakiwa njiani kwenda Ugiriki. Vita ya kidunia Mwaka wa 1941 uliona vita kubadilika kutoka vita ya Kiulaya kuwa vita ya kidunia. Wajerumani walishambulia Urusi wakifika hadi kando ya mji mkuu Moscow, lakini walishindwa kuiteka. Walikamata eneo lote la kusini mwa Urusi hadi milima ya Kaukazi na hadi mto Volga. Wajapani walishambulia Marekani pamoja na makoloni ya Waingereza na Waholanzi huko Asia. Hitler alitangaza pia vita dhidi ya Marekani akitaka kuwasaidia Wajapani ingawa Japan haikushambulia Urusi. Katika miaka iliyofuata nguvu ya Ujerumani na Japani ilipungua. Hasa uwezo wa kiuchumi wa Marekani ulizalisha mitambo na silaha kwa mkasi usiopatikana kwa Wajerumani na Wajapan. Ukali wa utetezi wa Warusi ulichosha nguvu za Wajerumani. Kuanzia mwaka 1943 mataifa ya ushirikiano yalianza kusogea mbele pande zote. Warusi walisukuma Wajerumani polepole warudi nyuma. Waamerika na Waingereza walipeleka wanajeshi Italia ya Kusini. Italia ilifanya mapinduzi: dikteta Mwitalia Mussolini aliondolewa madarakani na serikali mpya ilijiunga na mataifa ya ushirikiano. Mwaka 1944 askari wa mataifa ya ushirikiano waliingia Ufaransa wakielekea Ujerumani. Wakati huohuo Warusi walisogea mbele zaidi wakikaribia mipaka ya Ujerumani. Huko Asia Japan ilipoteza sehemu kubwa sana ya meli zake za kivita na Jeshi la Marekani lilikaribia visiwa vya Japani tayari. Mwisho wa vita Mwaka 1945 iliona mwisho wa vita. Mataifa mengi yaliyokuwa mbali, kama Argentina, Peru au Mongolia, yalitangaza pia hali ya vita dhidi ya Ujerumani na Japani. Pia nchi zilizowahi kushikamana na Wajerumani waligeukia mataifa ya ushirikiano. Ujerumani yenyewe ilivamiwa kutoka Magharibi na Mashariki. Warusi walifika mji mkuu wa Berlin na Adolf Hitler alijiua tarehe 30 Aprili 1945; wanajeshi wake walitia sahihi mkataba wa kusalimu amri tarehe 8-9 Mei 1945. Huko Asia Japani iliendelea kupigana na Waamerika walioweza kufikisha ndege zao zilizobeba mabomu hadi Japani yenyewe. Mnamo Agosti 1945 Waamerika walitumia silaha mbili za kinyuklia walizokuwa nazo wakati ule na kuua watu wengi sana huko Hiroshima tarehe 6 Agosti na Nagasaki tarehe 9 Agosti 1945. Siku zilezile Warusi walianza kuwashambulia wanajeshi Wajapani huko Uchina. Haya yote yalisababisha serikali ya Japani kukubali wameshindwa wakatia sahihi mkataba wa kusalimu amri tarehe 2 Septemba 1945. Waliokufa vitani Kwa jumla takriban watu milioni 60 walikufa kutokana na vita hivi. Makadirio hutaja wanajeshi milioni 25 na raia milioni 35. Taifa lililopoteza watu wengi ni Urusi walipokufa kati ya milioni 20-28, idadi kubwa wakiwa raia. Takriban watu milioni 10 waliuawa na Wajerumani au walikufa kutokana na kutendewa vibaya nje ya mapigano, kama vile milioni 6 za Wayahudi, wengine Wapoland, Warusi, Wasinti, walemavu n.k. Umoja wa Mataifa Tokeo mojawapo la vita kuu ya pili ni kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa. Uliundwa mwaka 1945 kama chombo cha kuzuia vita zijazo. Kutokana na historia hiyo mataifa yenye nafasi za kudumu na kura ya veto katika Baraza la Usalama ndiyo mataifa washindi wa vita kuu ya pili: Marekani, Uchina, Ufaransa, Ufalme wa Muungano na Urusi. Kutokana na kura ya veto hawawezi kuondolewa bila kukubali wenyewe hata kama siku hizi Ufaransa na Ufalme wa Muungano si tena nchi muhimu sana duniani. Vita Historia Historia ya Ulaya Historia ya Asia Historia ya Afrika Historia ya Amerika
2161
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mtwara
Mkoa wa Mtwara
Mtwara ni jina la mji na mkoa wa Tanzania wenye postikodi namba 63000 . Mkoa wa Mtwara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Uko katika pembe la kusini-mashariki kabisa la nchi. Umepakana na Mkoa wa Lindi upande wa kaskazini, Bahari Hindi kwa mashariki, Msumbiji katika kusini na Mkoa wa Ruvuma upande wa magharibi. Mpaka wa kusini ni Mto Ruvuma. Ukiwa na km² 16,720 Mtwara ni mkoa mdogo katika Tanzania pamoja na Kilimanjaro. Wakazi Jumla kuna wakazi 1,634,947 waishio humo kadiri ya sensa ya mwaka 2022 (kutoka 1,270,854 wa sensa ya mwaka 2012). Wanawake wanazidi wakiwa asilimia 53 ya wakazi wote kwa sababu wanaume wengi hutoka nje kutafuta kazi. Kati ya makabila ya Mtwara ndio Wamakonde wanaojulikana zaidi kutokana na sanaa yao ya uchongaji wa ubao, hasa mpingo. Utawala Kuna wilaya 5: Mtwara Mjini (pia huitwa "Mikindani"), Mtwara Vijijini, Masasi, Nanyumbu, Newala na Tandahimba. Ndani yake kuna tarafa 21, kata 98 na vijiji 554. Uchumi Mtwara iko kati ya mikoa iliyobaki nyuma miaka mingi kutokana na ugumu wa mawasiliano na barabara isiyopitika kwa sehemu kubwa ya kila mwaka. Historia ya Mtwara inakuja sambamba na kumbukumbu la jaribio la Waingereza la kuanzisha mradi mkubwa wa maendeleo katika eneo hili ulioshindikana kabisa. Kuanzia mwaka 1947 serikali ya kikoloni ilijenga bandari ya Mtwara pamoja na reli. Vilevile Mtwara mjini ilipangwa vizuri na kubwa. Sababu yake ilikuwa mpango wa kuanzisha kilimo cha mashamba makubwa kwa ajili ya karanga hasa zilizohitajika kwa ajili ya mahitaji ya Waingereza ya mafuta ya kupikia. Mradi huo ulishindikana kabisa, pesa nyingi zilipotea hadi mradi ulifutwa kabla ya Tanzania kupata uhuru. Reli iliondolewa tena mwaka 1963. Bandari imebaki ambayo haijaona kazi nyingi lakini bado ina faida ya kuwa na nafasi nzuri sana ya kupokea meli kubwa. Wakati wa mapambano dhidi ya serikali ya ubaguzi wa rangi katika Afrika Kusini mipango mbalimbali ilitungwa kutengeneza njia ya kupeleka bidhaa kutoka bandari ya Mtwara kwenda Songea na kutoka huko Malawi kwa kuvuka Ziwa Nyasa. Baada ya kujengwa kwa daraja juu ya mto Rufiji mwaka 2002 kuna matumaini mpya ya kuwa na barabara inayotumika kati ya Mtwara na Dar es Salaam. Eneo la Mnazi Bay ina gesi inayoweza kutumika kwa mahitaji ya nishati ya eneo lote. Tegemeo kubwa la uchumi kwa mkoa wa Mtwara ni kilimo, hasa ikitegemea zao la korosho kwa wakulima wa wilaya zote za mkoa. Kwa miaka ya karibuni wilaya ya Tandahimba na Masasi ndizo zimekuwa wazalishaji wa kiwango cha juu wa korosho. Pia mfumo wa stakabadhi ghalani umesaidia kwa kiasi fulani kwa miaka ya awali ya uanzishwaji mfumo huo (msimu wa 2008/2009) kwa miaka iliyofuata vyama vya msingi vimeonekana kuelemewa na mfumo huo na kusababisha sintofahamu inayoweza kurekebishwa kwa kuwahusisha wadau wote wa zao la korosho. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Mtwara Mjini : mbunge ni Maftah Abdallah Nachuma (CUF) Mtwara Vijijini : mbunge ni Hawa Ghasia (CCM) Nanyamba : mbunge ni Abdalah Chikota (CCM) Nanyumbu : mbunge ni William Dua Mkurua (CCM) Ndanda : mbunge ni Cecil Mwambe (Chadema) Newala Mjini : mbunge ni Kapteni George Mkuchika (CCM) Newala Vijijini : mbunge alikuwa hayati Rashid Ajali Akbar (CCM) Tandahimba : mbunge ni Katani Ahmad Katani (CUF) Masasi : Rashid Chuachua -->(CCM) Lulindi : Tazama pia Orodha ya mito ya mkoa wa Mtwara Marejeo Viungo vya nje Mtwara Region socioeconomic profile (1997) Mtwara Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census Tanzanian Government Directory Database M
2162
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kongo
Kongo
Kongo, Congo, na Kongō ni jina la kutaja mambo mbalimbali: Mto wa Kongo ambao ni kati ya mito mikubwa zaidi ya Afrika na ya dunia; pia eneo la beseni lake (Bonde la Kongo) Nchi mbili katika Afrika ya kati: Jamhuri ya Kongo (mji mkuu Brazzaville), kabla ya uhuru "Kongo ya Kifaransa" Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (mji mkuu Kinshasa), kabla ya uhuru "Kongo ya Kibelgiji" (1908-1960) Ufalme wa Kongo uliokuwa dola kubwa katika Angola ya Kaskazini na Kongo ya Magharibi (1400-1914) BK. Taifa huru la Kongo (1885-1908) Jamhuri ya Kongo (Léopoldville) (1960-1964) Kongo > Bakongo, kabila la Kibantu lenye watu milioni 5 katika Kongo, Angola na Gabon. Kongo > Kikongo, lugha ya Bakongo Mlima wa Kongo katika nchi ya Japani. "Kongo" imekuwa jina la meli za kijeshi huko Japani kutokana na mlima huu. Pia katika Afrika Kongo dia Nlaza (hadi mwishoni mwa karne ya 16), ufalme wa zamani uliomezwa na Ufalme wa Kongo Kongo ya Kireno, hivi sasa Cabinda (Angola) M'banza-Kongo, mji mkuu wa Angola kaskazini-mashariki Kongo ya Kati, zamani jimbo la Bas-Congo, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Kongo ya Kifaransa, jina la zamani la Equatorial Afrika ya Kifaransa (kabla ya 1910); ilihusisha Ubangi-Shari-Chad na Kongo ya Kati Kongo inaweza kuhusu nchi zifuatazo au mikoa: Cabinda, Angola kaskazini, Gabon, Afrika ya Kati, Chad, Rwanda na Burundi Kongo inaweza pia kuhusiswa na makundi ya watu katika Kolombia, Venezuela, Cuba na kwingineko ni sarafu ya nchini Kongo Wanyama Congo African Grey Parrot Congo (chimpanzee), jina la nugu ambao hujifunza kuchora Nyoka wa Kongo, aina ya salamander wa majini Congo, moja ya majina ya kawaida ya Agkistrodon piscivorus, nyoka mwenye sumu na hupatikana mashariki mwa Marekani Conger, aina ya congrid Eles anayepatikana majini Katika muziki na burudani Congo, 1980 riwaya ya Michael Crichton Congo, 1995 filamu yenye msingi kutoka kwa riwaya ya Crichton Congo, mwaka 2001 kumbukumbu ya filamu ya BBC Congo The Movie: The Lost City of Zinj, 1995 Sega Saturn mchezo wa video Kongo, 1932 filamu iliyoongozwa na nyota za filamu Walter Huston, Lupe Velez, na Conrad Nagel Kongo, mhusika katika Monkey Magic (mfululizo wa TV) "Congo", 1997 wimbo wa Mwanzo Kongo Jungle, Donkey Kong michezo ya video. Kongo Bongo, 1983 Arcade na mchezo wa video The Congos, Jamaican reggae duo Katika matumizi mengine Congo (loa), roho katika voodoo ya Haiti CONGO, Mkutano wa mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) Congo, kijiji cha County Fermanagh, Ireland Kaskazini Congo Village, mtaa wa Diego Martin, Trinidad The Congo or The Congo, shairi la Vachel Lindsay HMS Congo (1816), First steamship for the Royal Navy (United Kingdom) Corvette Kongo (1877) ya Japani meli ya vita ya Kongō kutoka ujapani JDS Kongo, kongo darasa Mwangamizi Yawara (Kongo), a martial arts weapon Watu na familia Cheick Kongo (alizaliwa 1975), mpiganaji Kongo Masahiro (alizaliwa 1948), mpinganaji wa Sumo Kid Kongo Powers (alizaliwa 1960), mwimbaji wa gitaa Angalia pia Congo craton, one of the cratons making the African continental crust Misitu ya Kongo Congo Tausi, aina ya ndege Mkongo Congo River, Beyond Darkness, 2005 filamu ya Thierry Michel A Daughter of the Congo, 1930 filamu ya Oscar Micheaux Kakongo, ufalme wa zamani King of the Congo, 1952 mfululizo wa filamu kutoka Columbia Pictures The King of the Kongo, 1929 mfululizo wa filamu kutoka Mascot Pictures Makala zinazotofautisha maana
2165
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilwa%20Kisiwani
Kilwa Kisiwani
Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Kilwa Kilwa Kisiwani ni jina la kijiji kikubwa kwenye Kisiwa cha Kilwa karibu na mji wa Kilwa Masoko katika Mkoa wa Lindi, Tanzania. Ndipo mahali pa mji wa Kilwa ya kihistoria iliyokuwa mji mkubwa kabisa kati ya miji ya Waswahili katika pwani ya Afrika ya Mashariki wakati wa karne ya 14 hadi karne ya 16 BK. Mji muhimu zaidi wa Uswahilini Kuanzia karne ya 11 Kilwa ilikuwa kituo muhimu cha biashara. Kuanzia karne ya 13 na 14 Kilwa ikawa muhimu kuliko Mombasa. Biashara yake ilikuwa dhahabu kutoka Dola la Mwene Mtapa (Zimbabwe), pembe za ndovu, chuma, nazi pamoja na kununua bidhaa kutoka Bara Hindi na Uchina. Sarafu ya dhahabu kutoka Kilwa imepatikana huko Zimbabwe Kuu. Katika karne ya 14 - kati ya 1330 na 1340 BK - mji ulitembelewa na msafiri Mwarabu Ibn Battuta aliyeacha taarifa ya kwanza ya kimaandishi kuhusu mji huo. Majengo makubwa yalijengwa yakiwa magofu yao yamesimama hadi leo kama vile msikiti mkuu, Jumba ya kifalme ya Husuni Kubwa, Boma la Kireno Kilwa na mengine mengi. Kuja kwa Wareno Kuja kwa Wareno katika karne ya 16 ilivuruga biashara ya Waswahili. Kilwa ikarudi nyuma. Katika karne ya 18 na ya 19 ikapata upya nguvu ya kiuchumi kutokana na biashara ya watumwa. Mwisho wa biashara hiyo ulimaliza utajiri wa Kilwa. Kilwa leo Leo hii Kilwa Kisiwani ipo katika eneo la Tanzania lisilotembelewa kwa urahisi. Hata hivyo kisiwa ni kati ya Hifadhi za Kiutamaduni muhimu sana za Tanzania, hata imeandikishwa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia" (World Heritage). Katika wilaya hiyo kuna mahali pengine pa urithi wa dunia, Selous. Tazama pia Orodha ya visiwa vya Tanzania Orodha ya Urithi wa Dunia katika Afrika Kitabu cha Kilwa Tanbihi Marejeo . Volume 1: History and archaeology; Volume 2: The finds. . First published in 1986, ISBN 0-520-05771-6. João de Barros (1552) , Dec. I, Lib. 8, Cap. 6 (p. 223ff) Strong, S. Arthur (1895) "The History of Kilwa, edited from an Arabic MS", Journal of the Royal Asiatic Society, January (No volume number), pp. 385–431. online Viungo vya nje Kilwa katika Historia ya Waswahili (BBC) Kilwa Kisiwani Site Page from the Aluka Digital Library World Monuments Fund Project Page for Kilwa Free resource for tourists on Kilwa Geonames.org Miji ya Tanzania Mkoa wa Lindi Waswahili Visiwa vya Afrika Visiwa vya Tanzania Visiwa vya Bahari ya Hindi Mahali pa Urithi wa Dunia katika Tanzania
2167
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kongo
Jamhuri ya Kongo ni nchi ya Afrika ya Kati. Imejulikana pia kama Kongo-Brazzaville (kutokana na mji mkuu) kwa kusudi la kutoichanganywa na nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Jamhuri ya Kongo imepakana na Gabon, Kamerun, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Angola na Bahari ya Atlantiki. Nchi ilikuwa koloni la Ufaransa hadi tarehe 15 Agosti 1960. Historia Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani na ya Wabilikimo. Katika karne za BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi waliotawala eneo lote na kuendesha biashara katika beseni ya mto Kongo. Baadaye eneo hilo lilikuwa sehemu ya koloni la Afrika ya Kiikweta ya Kifaransa Baada ya uhuru tarehe 15 Agosti 1960 nchi ilitawaliwa na Wakomunisti tangu mwaka 1970 hadi 1991. Kuanzia mwaka 1992 zilifanyika chaguzi kwa mfumo wa vyama vingi, lakini mwaka 1997 vilitokea vita vya wenyewe kwa wenyewe. Rais Denis Sassou Nguesso ametawala miaka 36 kati ya 41 ya mwisho. Watu Sehemu kubwa ya nchi ni misitu, hivyo wakazi wengi (70%) wanaishi mijini upande wa kusini-magharibi wa nchi. Kati yao, 48% ni wa kabila la Wakongo, 20% Wasangha, 17% Wateke, 12% Wam'Bochi. 2% ni Wabilikimo. Nchi ina lugha 62 tofauti, zikiwemo lugha 2 za taifa: Kingala na Kikongo (Kituba). Hata hivyo lugha rasmi ni Kifaransa. Wakazi wengi ni Wakristo (85.9%), wakiwemo Waprotestanti (51.4%) na Wakatoliki (30.1%), ingawa asilimia zinazotajwa hazilingani. Waislamu ni 1.6%, wafuasi wa dini asilia za Kiafrika ni 2.2% na wa Baha'i 0.4%. Tazama pia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Orodha ya lugha za Jamhuri ya Kongo Mto Niger Viungo vya nje Serikali Congolese Government Portal Presidency of the Republic Chief of State and Cabinet Members Taarifa za jumla Country Profile from BBC News Republic of the Congo from UCB Libraries GovPubs Review of Congo by the United Nations Human Rights Council's Universal Periodic Review, May 6, 2009. Humanitarian news and analysis from IRIN – Congo Utalii Congo-Brazzaville.com Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa
2169
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ugali
Ugali
Ugali ni chakula kinacholiwa na jamii za kiafrika. Chakula hiki chenye virutubisho vya wanga hutokana na unga wa nafaka (kama mahindi, mtama, uwele) au muhogo. Ugali hutayarishwa kwa njia ifuatayo: kwanza unachemsha maji kwenye sufuria baada ya kuchemka unachanganya unga kidogo na maji ya baridi pembeni, kisha tia mchanganyiko huo kwenye maji ya moto yaliyo jikoni huku ukikoroga. Utatokea mchanganyiko wa unga na maji ambao unaitwa uji, acha uji huo uchemke kwa muda kisha tia unga kiasi kulingana na uji wako huku ukisonga kwa kutumia mwiko. Endelea kusonga mpaka mchanganyiko ushikamane, mchanganyiko huu ndio hutoa ugali. Kimaeneo kuna aina mbalimbali za ugali kutegemeana na aina za mazao yanayopatikana. Udaga ni ugali unaopikwa kwa kuchanganya unga wa muhogo na ulezi, hupatikana zaidi maeneo ya Musoma kwa Wakuria Ugali huweza kuliwa na mboga ya aina yoyote kama vile mboga majani, sukumawiki, samaki na nyama. Kawaida ugali huliwa kwa mikono mitupu. Tonge la ugali hufinyangwa kwa mkono kisha kuchovya kwenye maziwa au mchuzi wa maharage, samaki, au nyama ya ng'ombe. Ugali, mapishi yake na jinsi unavyoliwa, hufanana kwa kiasi fulani na foufou toka Afrika Magharibi, na polenta toka Italia. Ugali hujulikana kama nshima nchini Zambia au nsima nchini Malawi. Viungo vya nje Video kuhusu jinsi ya kupika ugali Chakula cha Kiafrika de:Ugali en:Ugali it:Ugali ja:ウガリ ru:Угали sv:Ugali
2170
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kinu
Kinu
Kinu ni chombo cha kusaga au kuponda vitu kwa msaada wa mchi vinavyohitaji kusagwa kwa mfano vyakula au madawa. Kwa asili kinu ni kifaa kinachotengenezwa kwa kutumia miti migumu ambapo gogo hutobolewa sehemu ya juu katikati kuelekea chini ambapo upana wa tundu hupungua kuelekea chini tundu hilo hutumika kuwekea vitu vinavyohitaji kusagwa. Kinu hutengenezwa pia kwa kukata jiwe kuwa na umbo linalotakiwa pia kwa metali au kauri. Ili kinu kikamilike huhitaji mchi ambao hutumika kusagia vitu vilivyowekwa ndani ya kinu. Kinu hutumika katika makabila mengi ya Afrika Mashariki, mifano ipo kama kinu cha Warangi. Vifaa
2171
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkesha
Mkesha
Mikesha ni ndege wa familia ya Turdidae ambao ni wadogo na wanono. Spishi za jenasi Neocossyphus na Stizorhina zinaitwa shesiafu pia. Rangi yao kuu ni rangi ya kahawia na madoa meupe na meusi; wengine wana rangi ya machungwa au nyekundu na wengine ni weusi. Hula wadudu hasa lakini wanaweza kula wanyama wadogo wengine, kama koa na nyungunyungu, na hata beri. Wengi wanaweza kuimba vizuri sana. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe na pengine hulawekea matope kwa ndani. Jike huyataga mayai 2-5 yenye vidoa. Spishi za Afrika Alethe castanea, Mkeshamsitu Kishungi-chekundu (Fire-crested Alethe) Alethe diademata, Mkeshamsitu Mkia-mweupe (White-tailed Alethe) Geokichla cameronensis, Mkesha Masikio-meusi (Black-eared Ground Thrush) Geokichla crossleyi, Mkesha wa Crossley (Crossley's Ground Thrush) Geokichla guttata, Mkesha Madoadoa (Spotted Ground Thrush) Geokichla gurneyi, Mkesha Rangi-machungwa (Orange Ground Thrush) Geokichla oberlaenderi, Mkesha wa Ruwenzori (Oberländer's Ground Thrush) Geokichla piaggiae, Mkesha Habeshi (Abyssinian Ground Thrush) Geokichla princei, Mkesha Kijivu (Grey Ground Thrush) Geokichla tanganjicae, Mkesha wa Kivu (Kivu Ground Thrush) Neocossyphus rufus, Shesiafu Mkia-mwekundu (Red-tailed Rufous Thrush au Ant-thrush) Neocossyphus poensis, Shesiafu Mkia-mweupe (White-tailed Rufous Thrush au Ant-thrush) Chamaetylas choloensis, Mkeshamsitu wa Cholo (Thyolo Alethe) Chamaetylas fuelleborni, Mkeshamsitu Kidari-cheupe (White-chested Alethe) Chamaetylas poliocephala, Mkeshamsitu Kidari-kahawia (Brown-chested Alethe) Chamaetylas poliophrys, Mkeshamsitu Koo-jekundu (Red-throated Alethe) Psophocichla litsitsirupa, Mkesha Mgongo-kijivu au Chiru (Groundscraper Thrush) Stizorhina finschii, Shesiafu wa Finsch (Finsch's Rufous Thrush au Flycatcher-thrush) Stizorhina fraseri, Shesiafu Mwekundu (Fraser's Rufous Thrush au Rufous Flycatcher-thrush) Turdus abyssinicus, Mkesha-milima (Abyssinian au African Mountain Thrush) Turdus bewsheri, Mkesha wa Komori (Comoro Thrush) Turdus helleri, Mkesha wa Taita (Taita Thrush) Turdus libonyanus, Mkesha Koo-michirizi (Kurrichane Thrush) Turdus ludoviciae, Mkesha Somali (Somali Thrush) Turdus merula, Mkesha Mweusi (Common Blackbird) Turdus m. aterrimus, Mkesha Mweusi wa Balkani (Balkan Blackbird) Turdus m. cabrerae, Mkesha Mweusi wa Kanari (Canary Islands Blackbird) Turdus m. mauretanicus, Mkesha Mweusi Magharibi (Maghreb Blackbird) Turdus m. merula, Mkesha Mweusi wa Ulaya (European Blackbird) Turdus m. syriacus, Mkesha Mweusi wa Syria (Syrian Blackbird) Turdus olivaceofuscus Mkesha wa Sao Tome (São Tomé Thrush) Turdus olivaceus, Mkesha Kijanikijivu (Olive Thrush) Turdus pelios, Mkesha wa Afrika (African Thrush) Turdus philomelos, Mkesha Mwimbaji (Song Thrush) Turdus roehli, Mkesha wa Usambara (Usambara Thrush) Turdus smithi, Mkesha wa Karuu (Karoo Thrush) Turdus tephronotus, Mkesha Macho-wazi ((African) Bare-eyed Thrush) Turdus viscivorus, Mkesha Mlaberi (Mistle Thrush) Turdus xanthorhynchus, Mkesha wa Principe (Príncipe Thrush) Spishi za mabara mengine Brachypteryx hyperythra (Rusty-bellied Shortwing) Brachypteryx leucophris (Lesser Shortwing) Brachypteryx montana (White-browed Shortwing) Cataponera turdoides (Sulawesi Thrush) Catharus aurantiirostris (Orange-billed Nightingale-thrush) Catharus bicknelli (Bicknell's Thrush) Catharus dryas (Spotted Nightingale-thrush) Catharus frantzii (Ruddy-capped Nightingale-thrush) Catharus fuscater (Slaty-backed Nightingale-thrush) Catharus fuscescens (Veery, Willow Thrush or Wilson's Thrush) Catharus gracilirostris (Black-billed Nightingale-thrush) Catharus guttatus (Hermit Thrush) Catharus mexicanus (Black-headed Nightingale-thrush) Catharus minimus (Grey-cheeked Thrush) Catharus occidentalis (Russet Nightingale-thrush) Catharus ustulatus (Swainson's Thrush or Olive-backed Thrush) Chlamydochaera jefferyi ((Black-breasted) Fruithunter) Cichlopsis leucogenys (Rufous-brown Solitaire) Cochoa azurea (Javan Cochoa) Cochoa beccarii (Sumatran Cochoa) Cochoa purpurea (Purple Cochoa) Cochoa viridis (Green Cochoa) Entomodestes coracinus (Black Solitaire) Entomodestes leucotis (White-eared Solitaire) Geokichla cinerea (Ashy Thrush) Geokichla citrina (Orange-headed Thrush) Geokichla dohertyi (Chestnut-backed Thrush) Geokichla dumasi (Buru Thrush) Geokichla erythronota (Red- au Rusty-backed Thrush) Geokichla interpres (Chestnut-capped Thrush) Geokichla joiceyi (Seram Thrush) Geokichla leucolaema (Enggano Thrush) Geokichla mendeni (Red-and-black Thrush) Geokichla peronii (Orange-sided au Orange-banded Thrush) Geokichla schistacea (Slaty-backed Thrush) Geokichla sibirica (Siberian Thrush) Geokichla spiloptera (Spot-winged Thrush) Geokichla wardii (Pied Thrush) Geomalia heinrichi (Geomalia or Sulawesi Mountain-Thrush) Grandala coelicolor (Grandala) Heinrichia calligyna (Great Shortwing) Heteroxenicus stellatus (Gould's Shortwing) Hylocichla mustelina (Wood Thrush) Ixoreus naevius (Varied Thrush) – pengine katika jenasi Zoothera Myadestes coloratus (Varied Solitaire) Myadestes elisabeth (Cuban Solitaire) Myadestes elisabeth retrusus (Pines Solitaire) – labda imekwisha sasa (miaka 1930 au 1970?) Myadestes genibarbis (Rufous-throated Solitaire) Myadestes lanaiensis (Oloma‘o) Myadestes lanaiensis lanaiensis (Lāna‘i Oloma‘o) – imekwisha sasa (1931-1933) Myadestes lanaiensis rutha (Moloka‘i Oloma‘o) – labda imekwisha sasa (miaka 1980?) Myadestes melanops (Black-faced Solitaire) Myadestes myadestinus (Kāma‘o au Large Kauaʻi Thrush) – imekwisha sasa (miaka 1990) Myadestes obscurus (‘Ōma‘o au Hawaiian Thrush) Myadestes occidentalis (Brown-backed Solitaire) Myadestes palmeri (Puaiohi) Myadestes ralloides (Andean Solitaire) Myadestes townsendi (Townsend's Solitaire) Myadestes unicolor (Slate-coloured Solitaire) Myadestes woahensis (‘Āmaui) – imekwisha sasa (miaka 1850) Nesocichla eremita (Tristan Thrush) Ridgwayia pinicola (Aztec Thrush) – pengine katika jenasi Zoothera Sialia currucoides (Mountain Bluebird) Sialia mexicana (Western Bluebird) Sialia sialis (Eastern Bluebird) Turdus albicollis (White-necked Thrush) Turdus albocinctus (White-collared Blackbird) Turdus amaurochalinus (Creamy-bellied Thrush) Turdus assimilis (White-throated Thrush) Turdus atrogularis (Black-throated Thrush) Turdus aurantius (White-chinned Thrush) Turdus boulboul (Grey-winged Blackbird) Turdus cardis (Japanese Thrush) Turdus celaenops (Izu Thrush) Turdus chiguanco (Chiguanco Thrush) Turdus chrysolaus (Brown-headed Thrush) Turdus daguae (Dagua Thrush) Turdus dissimilis (Black-breasted Thrush) Turdus eunomus (Dusky Thrush) Turdus falcklandii (Austral Thrush) Turdus feae (Grey-sided Thrush) Turdus flavipes (Yellow-legged Thrush) Turdus fulviventris (Chestnut-bellied Thrush) Turdus fumigatus (Cocoa Thrush) Turdus fuscater (Great Thrush) Turdus grayi (Clay-coloured Thrush) Turdus graysoni (Grayson's Thrush) Turdus haplochrous (Unicoloured Thrush) Turdus hauxwelli (Hauxwell's Thrush) Turdus hortulorum (Grey-backed Thrush) Turdus ignobilis (Black-billed Thrush) Turdus iliacus (Redwing) Turdus infuscatus (Black Thrush) Turdus jamaicensis (White-eyed Thrush) Turdus kessleri (Kessler's au White-backed Thrush) Turdus lawrencii (Lawrence's Thrush) Turdus leucomelas (Pale-breasted Thrush) Turdus leucops (Pale-eyed Thrush) Turdus lherminieri (Forest Thrush) Turdus maculirostris (Ecuadorian Thrush) Turdus maranonicus (Maranon Thrush) Turdus maximus (Tibetan Blackbird) Turdus menachensis (Yemen Thrush) Turdus merula (Eurasian Blackbird) Turdus migratorius (American Robin) Turdus mupinensis (Chinese Thrush) Turdus naumanni (Naumann's Thrush) Turdus nigrescens (Sooty Thrush) Turdus nigriceps (Andean Slaty Thrush) Turdus nudigenis (Spectacled au Bare-eyed Thrush) Turdus obscurus (Eyebrowed Thrush) Turdus obsoletus (Pale-vented Thrush) Turdus olivater (Black-hooded Thrush) Turdus pallidus (Pale Thrush) Turdus pilaris (Fieldfare) Turdus plebejus (Mountain Thrush) Turdus plumbeus (Red-legged Thrush) Turdus poliocephalus (Island Thrush) Turdus ravidus (Grand Cayman Thrush) imekwisha sasa (miaka 1930) Turdus reevei (Plumbeous-backed Thrush) Turdus rubrocanus (Chestnut Thrush) Turdus ruficollis (Red-throated Thrush) Turdus rufitorques (Rufous-collared Thrush) Turdus rufiventris (Rufous-bellied Thrush) Turdus rufopalliatus (Rufous-backed Thrush) Turdus sanchezorum (Varzea Thrush) Turdus serranus (Glossy-black Thrush) Turdus simillimus (Indian Blackbird) Turdus subalaris (Eastern Slaty Thrush) Turdus swalesi (La Selle Thrush) Turdus torquatus (Ring Ouzel) Turdus unicolor (Tickell's Thrush) Zoothera andromedae (Sunda Thrush) Zoothera aurea (White's Thrush) Zoothera dauma (Scaly Thrush) Zoothera dixoni (Long-tailed Thrush) Zoothera everetti (Everett's Thrush) Zoothera heinei (Russet-tailed Thrush) Zoothera horsfieldi (Horsfield's Thrush) Zoothera imbricata (Sri Lanka Thrush) Zoothera lunulata (Bassian au Olive-tailed Thrush) Zoothera machiki (Fawn-breasted Thrush) Zoothera major (Amami Thrush) Zoothera margaretae (White-bellied au San Cristobal Thrush) Zoothera marginata (Dark-sided Thrush) Zoothera mollissima (Plain-backed Thrush) Zoothera monticola (Long-billed Thrush) Zoothera neilgherriensis (Nilgiri Thrush) Zoothera salimalii (Himalayan Forest Thrush) Zoothera talaseae (Black-backed au New Britain Thrush) Zoothera terrestris (Bonin (Islands) Thrush) - imekwisha sasa (miaka 1830) Zoothera turipavae (Guadalcanal Thrush) Picha Shore na jamaa Wanyama wa Biblia
2172
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mji%20mkuu
Mji mkuu
Mji mkuu kwa kawaida ni mji wenye makao makuu ya serikali ya nchi fulani. Katika nchi nyingi mji huo ni pia mji mkubwa na muhimu zaidi kushinda miji mingine nchini. Huo ni sehemu yenye maendeleo makubwa sana katika nchi yoyote: ina kila huduma muhimu na miundombinu iliyo bora. Mfano: nchini Tanzania mji mkubwa ni Dar es Salaam, ingawa makao makuu ni Dodoma. Kuna nchi ambako mji mmoja umeteuliwa kuwa mji mkuu katika katiba au kwa sheria fulani. Kumbe kuna nchi nyingine ambako hakuna sheria yoyote lakini makao makuu yanaeleweka yapo mji fulani. Nchi kadhaa zimeteua mji fulani kuwa mji mkuu kwa shabaha ya kubadilisha mwendo wa nchi au kama jaribio la kusahihisha historia yake. Makoloni ya zamani kuanzisha mji mkuu mpya Nchi mbalimbali zilizowahi kuwa koloni zimeamua kuanzisha mji mkuu mpya kwa sababu mji mkuu wa kikoloni uliteuliwa kutokana na mahitaji ya nchi tawala ya zamani si kutokana na mahitaji ya nchi huru yenyewe. Wakati wa ukoloni mara nyingi mji kwenye pwani penye bandari uliteuliwa kuwa mji mkuu. Sababu yake ni ya kwamba kwa ajili ya maafisa wa kikoloni mawasiliano na nyumbani kwao yalikuwa muhimi sana kushinda mawasiliano na sehemu zote za nchi ya koloni yenyewe. Wakati wa ukoloni usafiri ulikuwa kwa meli, hivyo kipaumbele cha mabandari. Katika fikra za kisiasa na za kiuchumi sababu muhimu ya kuwa na koloni ilikuwa nafasi ya nchi tawala kujipatia malighafi katika koloni na kuuza bidhaa zake - yote yalitegemea mabandari. Hasara ya chaguo lile ilikuwa ya kwamba mara nyingi mabandari ni kando kabisa katika nchi zao - watu wengi wako mbali na mji mkuu. Brazil: Hapo Wabrazil wamehamisha mji mkuu kutoka Rio de Janeiro uliyoko pwani na kando ya eneo la Brazil kwenda mji mpya wa Brasilia kuanzia mwaka 1960. Brasilia ilijengwa mahali pasipo mji katika miaka 1956 - 1960 BK. Kwa nia hiyohiyo Tanzania iliamua kuhamisha mji mkuu kutoka Dar es Salaam uliyoko pwani mwa Bahari Hindi kwenda Dodoma iliyoko katikati ya Tanzania. Uhamisho huu umepangwa tangu 1967 na kutangazwa rasmi mwaka 1997; kuanzia mwaka 2016 serikali ya rais John Magufuli ilihamisha hatimaye ofisi kuu za wizara zote kwenda Dodoma. Hata hivyo, kuna bado ofisi nyingi zilizobaki Dar es Salaam. Tazama chini: Nigeria, Côte d'Ivoire Kuhamisha mji mkuu baada ya mapinduzi Uturuki iliamua 1923 kuhamisha mji mkuu kutoka Istanbul kwenda Ankara. Istanbul iliwahi kuwa kwa karne nyingi mji wa Masultani tena mji wa kimataifa; mapinduzi ya 1923 yalimaliza utawala wa sultani na kutangaza Uturuki kuwa jamhuri. Pia Istanbul imekuwa kandokando ya eneo la Uturuki baada ya vita kuu ya kwanza kwa sababu sehemu za magharibi zilikuwa zimepotea na kuchukuliwa na Wagiriki na Wabulgaria. Hivyo Ankara iliteuliwa iliyoko katikati ya Uturuki mpya baada ya vita. Urusi ilihamisha mji mkuu mara mbili. Mwaka 1712 Tsar (mfalme) mrusi Peter aliamua kujenga mji mpya katika pembe la magharibi kabisa ya nchi akahamisha mji mkuu kutoka Moscow kwenda St. Peterburg mpya. Tsar Peter aliona nchi yake ilikuwa imebaki nyuma akitaja kuleta maendeleo kwa kuiga mfano wa Ulaya ya Kati na ya Magharibi. Mji mpya ya St. Peterburg ilipangwa kuwa "dirisha la Urusi la kutazama magharibi". Baada ya mapinduzi ya 1917 Wakomunisti waliamua kufanya Moscow iwe mji mkuu kuanzia mwaka 1918. Sababu yake ni nafasi ya Moscow iliyoko ndani zaidi ya eneo la Urusi yenyewe. Kujenga mji mkuu wa pekee katika nchi za shirikisho Nchi kadhaa zinazofuata muundo wa serikali ya shirikisho zimeamua kujenga mji ulioko katika wilaya au mkoa wa shirikisho ili mji mkuu usiwepo katika eneo la mkoa au dola la shirikisho fulani. Marekani iliteua eneo la Mkoa wa Colombia kuwa mahali pa mji mpya wa shirikisho ulioitwa baadaye kwa jina la raisi wa kwanza "Washington". Mkoa wa Colombia si sehemu ya dola lolote la shirikisho la Marekani. Mji wa Washington D.C. na mkoa wa Colombia ni eneo lilelile. Australia ilijenga mji mkuu mpya kwa sababu miji mikubwa ya Sydney na Melbourne yote yalitaka kuwa mji mkuu wa kitaifa wa Shirikisho la Australia. Mwaka 1908 eneo la Canberra lililokuwa mashambani wakati ule liliteuliwa, ujenzi wa mji mpya ulianza mwaka 1913 na serikali pamoja na bunge ilihamia Canberra mwaka 1927. Dola la shirikisho la New South Wales lilikabidhi "Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho" lililokuwa eneo la pekee chini ya Bunge la Australia moja kwa moja. Nigeria iliamua mwaka 1976 kuhamisha mji mkuu wa kitaifa kutoka Lagos kwenda mahali pa katikati ya nchi. "Eneo la Mji Mkuu wa Shirikisho" limeteuliwa. Mji mpya wa Abuja ndani ya eneo hili ukawa mji mkuu wa Nigeria mwaka 1991. Miji mikuu mbalimbali Afrika Kusini ina miji mikuu mitatu kikatiba: Pretoria ndipo makao makuu ya serikali, Cape Town ndipo makao makuu ya bunge, Bloemfontein ndipo makao makuu ya Mahakama Kuu. Bolivia ina mji mkuu rasmi katika jiji la Sucre, lakini ofisi nyingi za serikali ya kitaifa zimehamia mji mkubwa wa nchi La Paz. Côte d'Ivoire imetangaza 1983 Yamoussoukro kuwa mji mkuu wa taifa lakini hadi leo ofisi za serikali zimebaki Abidjan. Miji mikuu Miji
2173
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jamhuri%20ya%20Kidemokrasia%20ya%20Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (au Kongo-Kinshasa) ni nchi iliyoko Afrika ya Kati; kwa ukubwa wa eneo ni ya pili barani Afrika. Ni tofauti na nchi jirani ya Jamhuri ya Kongo. Jiografia Nchi imepakana na Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Uganda, Rwanda, Burundi, Tanzania, Zambia na Angola. Ina sehemu ndogo ya pwani kwenye Bahari ya Atlantiki. Sehemu hiyo inatenganisha eneo la Cabinda kutoka maeneo mengine ya Jamhuri ya Angola. Eneo lote ni la kilometa mraba 2,345,409 na linafanya Kongo iwe nchi ya 11 duniani kwa ukubwa wa eneo. Historia Historia ya kale Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani na ya Wabilikimo. Katika karne za BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi. Jina la Kongo lahusiana na mto Kongo unaopitia nchi yote. Mnamo karne ya 15, wakati wapelelezi wa kwanza Wareno walipofika kwenye pwani za Afrika, milki kubwa katika nchi ya Kongo ya magharibi pamoja na Angola ya kaskazini ilikuwa Ufalme wa Kongo. Wakati wa uenezaji mkuu ufalme huu ulianza kwenye mwambao wa Atlantiki na kuendelea hadi mto Kwango kwenye mashariki, halafu maeneo kutoka Pointe-Noire (leo: Jamhuri ya Kongo, upande wa kaskazini ya Cabinda) upande wa kaskazini hadi mto Loje (leo: mji wa Ambriz) katika kusini. Mtawala alikuwa na cheo cha Manikongo na ufalme uligawiwa kwa majimbo sita. Baada ya kufika kwa Wareno wafalme na matabaka ya juu walikuwa Wakristo. Ufalme uliporomoka kutokana na vita vilivyosababishwa na biashara ya watumwa na kuingilia kwa wafanyabiashara ya watumwa katika siasa ya ndani. Hata hivyo, nasaba za watawala waliotumia cheo cha "Awenekongo" waliendelea kukaa katika mji mkuu wa kale M'banza-Kongo (iliyobadilishwa jina kuitwa San Salvador) hadi mwaka 1914 ambako Wareno walifuta mabaki ya uhuru na kufanya eneo lililobaki sehemu kamili ya koloni lao la Angola. Upande wa kusini, kuanzia karne ya 17, kulikuwa na ufalme ulioitwa Dola la Kazembe. Koloni binafsi la mfalme kuwa koloni la Ubelgiji Nchi jinsi ilivyo ilianzishwa kama Dola huru la Kongo likiwa mali binafsi ya mfalme Leopold II wa Ubelgiji. Historia yake ni ya aibu na ya ukatili kupindukia. Utawala wa mfalme ulionekana kuwa wa kinyama na upinzani dhidi yake ulikua katika nchi nyingi za dunia. Hatimaye alipaswa kukabidhi koloni lake binafsi mikononi mwa serikali ya Ubelgiji iliyomlipa fidia kwa mali aliyoacha. Kati ya mwaka 1908 hadi 1960 ilikuwa koloni la Ubelgiji kwa jina la Kongo ya Kibelgiji baada ya kuhamishiwa mikononi mwa serikali ya Ubelgiji. Katika miaka 1925 hadi 1946 maeneo ya Rwanda na Burundi yalitawaliwa kama sehemu za Kongo ya Kibelgiji. Siasa ya wakoloni Wabelgiji walijitahidi kuboresha hali ya maisha ya wenyeji baada ya miaka mibaya ya Leopold II. Nia ilichelewa kuonekana hali halisi kwa sababu utaratibu wa kulazimisha Waafrika kufanyia kazi kampuni na shirika kubwa iliendelea hata bila idhini ya serikali mpya ukadai vifo vingi. Kwenye uwanja wa elimu, matibabu na mawasiliano jitihada za siasa mpya zilionekana zaidi. Kongo ilikuwa kati ya nchi chache ambako lugha za kienyeji zilifundishwa shuleni kwa sababu shule nyingi ziliendshwa na wamisionari. Kwa upande mwingine ubaguzi wa rangi uliwaruhusu Waafrika wachache sana kufikia ngazi za juu za elimu. Makampuni makubwa ya migodi kama vile "Société Générale" na "Union Minière du Haut Katanga" yalichimba madini hasa katika jimbo la Katanga. Makampuni haya yalikuwa na athira kubwa. Katanga ilikuwa maarufu kwa shaba iliyochimbwa huko. halafu pia kwa uranium iliyotumiwa kwa mabomu ya kwanza ya kinyuklia ya Marekani mwaka 1945. Upinzani Baada ya unyama wa miaka ya Leopold II upinzani dhidi ya utawala wa kikoloni ulikuwa hafifu. Kuanzia miaka ya 1920 Wakongo wengi walionyesha upinzani huo katika mahudhurio katika madhehebu mapya ya wafuasi wa Simon Kimbangu yaliyopigwa marufuku na Wabelgiji kuanzia mwaka 1926. Tangu mwaka 1950 upinzani uliongezeka na kuonyesha pia uso wa kisiasa. Wabelgiji ambao hawakujiandaa kwa madai hayo yalipaswa kukubali uchaguzi wa halmashauri za vijiji na miji mwaka 1957. Mwaka 1958 vyama vya kisiasa vilikubaliwa. Harakati mbili muhimu kati ya hivi zilikuwa Abako (Alliance de Bakongo) chini ya Joseph Kasavubu na MNC (Mouvement National Congolais) chini ya Patrice Lumumba. Mwaka 1959 mkutano wa wanasiasa Wakongo ulidai uhuru wa nchi. Mwisho wa koloni na uhuru Wabelgiji walijaribu kuchelewesha harakati hizo lakini baada ya kutambua matatizo serikali ya Ubelgiji ilitangaza mnamo Januari 1960 kuwa uchaguzi utaendeshwa haraka na baada ya miezi sita Wabelgiji watakabidhi nchi kwa wenyeji. Chama cha Patrice Lumumba kilishinda kwa kura nyingi naye akawa kiongozi wa kwanza wa nchi huru kama waziri mkuu. Koloni la Kongo ya Kibelgiji lilipata uhuru tarehe 30 Juni 1960. Kati ya 27 Oktoba 1971 na 17 Mei 1997, chini ya utawala wa dikteta Mobutu, nchi ilijulikana kwa jina la "Zaire". Leo hii ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mikoa Nchi imegawiwa katika mikoa 26 kadiri ya Katiba mpya (2006) na utekelezaji wake wa mwaka 2015. Watu Mwaka 2017 wakazi walikuwa 81,339,988: idadi hiyo ni ya 4 kati ya nchi zote za Afrika, baada ya Nigeria, Ethiopia na Misri. Wakazi asilia ni Wabilikimo, ambao kwa sasa ni 600,000. Kumbe walio wengi ni Wabantu. Lugha Kifaransa ni lugha rasmi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ilikuwa lugha ya utawala ya koloni ikaendelea kutumiwa kama lugha isiyoelekea upande wowote kati ya makabila, lugha na tamaduni za nchi hii. Lugha ya Kiholanzi iliyotumiwa na Wabelgiji pamoja na Kifaransa katika utawala haitumiki tena. Kwa jumla kuna takriban lugha 242, hasa lugha za Kibantu, zinazozungumzwa nchini (angalia orodha ya lugha). Kati yake, lugha 4 zinatambuliwa kama lugha za kitaifa, nazo ni: Kikongo (Kituba), Kingala (Kongo), Kiluba (Tshiluba) na Kiswahili. Wakati wa ukoloni lugha hizo nne za kitaifa ziliwahi kutumiwa kieneo katika shule za msingi. Kingala kilikuwa lugha rasmi ya jeshi la kikoloni lililoitwa "Force Publique" chini ya utawala wa Ubelgiji likaendelea kuwa lugha ya jeshi la jamhuri baada ya uhuru. Tangu mapinduzi ya 1997 sehemu za jeshi, hasa mashariki, hutumia pia Kiswahili. Takriban 47% wanatumia Kifaransa kama lugha ya kwanza au lugha ya pili. Dini Wananchi wengi (zaidi ya 90%) wanajihesabu Wakristo wa madhehebu mbalimbali; kati yao asilimia 29.7 ni Wakatoliki. Waislamu ni asilimia 10-12. Wafuasi wa dini asilia za Kiafrika ni 3%. Tazama pia Orodha ya miji ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Marejeo Clark, John F., The African Stakes of the Congo War, 2004. . Drummond, Bill and Manning, Mark, The Wild Highway, 2005. Edgerton, Robert, The Troubled Heart of Africa: A History of the Congo. St. Martin's Press, December 2002. Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. The Dark Side of Globalization. The Vicious Cycle of Exploitation from World Market Integration: Lesson from the Congo, Working Papers in Economics and Statistics 31, University Innsbruck 2007. Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. [http://vkc.library.uu.nl/vkc/seh/research/Lists/Events/Attachments/6/Paper.ExenbergerHartmann.pdf Doomed to Disaster? Long-term Trajectories of Exploitation in the Congo] , Paper to be presented at the Workshop "Colonial Extraction in the Netherlands Indies and Belgian Congo: Institutions, Institutional Change and Long Term Consequences", Utrecht 3–4 December 2010. Gondola, Ch. Didier, "The History of Congo", Westport: Greenwood Press, 2002. Joris, Lieve, translated by Waters, Liz, The Rebels' Hour, Atlantic, 2008. Justenhoven, Heinz-Gerhard; Ehrhart, Hans Georg. Intervention im Kongo: eine kritische Analyse der Befriedungspolitik von UN und EU. Stuttgart: Kohlhammer, 2008. (In German) ISBN 978-3-17-020781-3. Kingsolver, Barbara. The Poisonwood Bible HarperCollins, 1998. Larémont, Ricardo René, ed. 2005. Borders, nationalism and the African state. Boulder, Colorado and London: Lynne Rienner Publishers. Lemarchand, Reni and Hamilton, Lee; Burundi: Ethnic Conflict and Genocide. Woodrow Wilson Center Press, 1994. Mealer, Bryan: "All Things Must Fight To Live", 2008. ISBN 1-59691-345-2. Melvern, Linda, Conspiracy to Murder: The Rwandan Genocide and the International Community. Verso, 2004. Miller, Eric: "The Inability of Peacekeeping to Address the Security Dilemma", 2010. ISBN 978-3-8383-4027-2. Mwakikagile, Godfrey, Nyerere and Africa: End of an Era, Third Edition, New Africa Press, 2006, "Chapter Six: Congo in The Sixties: The Bleeding Heart of Africa", pp. 147 – 205, ISBN 978-0-9802534-1-2; Mwakikagile, Godfrey, Africa and America in The Sixties: A Decade That Changed The Nation and The Destiny of A Continent, First Edition, New Africa Press, 2006, ISBN 978-0-9802534-2-9. Nzongola-Ntalaja, Georges, The Congo from Leopold to Kabila: A People's History, 2002. O'Hanlon, Redmond, Congo Journey, 1996. O'Hanlon, Redmond, No Mercy: A Journey into the Heart of the Congo, 1998. Prunier, Gérard, Africa's World War: Congo, the Rwandan Genocide, and the Making of a Continental Catastrophe, 2011 (also published as From Genocide to Continental War: The Congolese Conflict and the Crisis of Contemporary Africa: The Congo Conflict and the Crisis of Contemporary Africa). Renton, David; Seddon, David; Zeilig, Leo. The Congo: Plunder and Resistance, 2007. ISBN 978-1-84277-485-4. Reyntjens, Filip, The Great African War: Congo and Regional Geopolitics, 1996–2006 , 2009. Rorison, Sean, Bradt Travel Guide: Congo  — Democratic Republic/Republic, 2008. Schulz, Manfred. Entwicklungsträger in der DR Kongo: Entwicklungen in Politik, Wirtschaft, Religion, Zivilgesellschaft und Kultur, Berlin: Lit, 2008, (in German) ISBN 978-3-8258-0425-1. Stearns, Jason: Dancing in the Glory of Monsters: the Collapse of the Congo and the Great War of Africa, Public Affairs, 2011. Tayler, Jeffrey, Facing the Congo, 2001. Turner, Thomas, The Congo Wars: Conflict, Myth and Reality, 2007. Van Reybrouck, David, Congo: The Epic History of a People, 2014 Wrong, Michela, In the Footsteps of Mr. Kurtz: Living on the Brink of Disaster in Mobutu's Congo. Osman, Mohamed Omer Guudle(November,2011) Africa: A rich Continent where poorest people live, The Case of DR Congo and the exploitation of the World Market Viungo vya nje Chief of State and Cabinet Members Country Profile from the BBC News Democratic Republic of the Congo from UCB Libraries GovPubs'' The Democratic Republic of Congo from Global Issues Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa Jumuiya ya Afrika Mashariki K
2175
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mara
Mkoa wa Mara
Mkoa wa Mara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 31000.. Umepakana na mikoa jirani ya Mwanza na Shinyanga upande wa kusini, Arusha upande wa kusini-mashariki, Kagera kwa njia ya Ziwa Nyanza (au Viktoria) na Kenya upande wa mashariki. Jina linatokana na lile la mto Mara. Musoma ndio makao makuu ya mkoa. Idadi ya wakazi ilikuwa 2,372,015 wakati wa sensa ya mwaka 2022, kutoka 1,743,830 wa sensa ya mwaka 2012 , na 1,368,602 wa sensa ya 2002. Kuna wilaya zifuatazo katika mkoa wa Mara: Bunda, Serengeti, Tarime, Rorya, Butiama, Musoma mjini na Musoma vijijini. Sehemu kubwa ya Hifadhi ya Wanyama ya Serengeti iko ndani ya Mkoa wa Mara. Makabila Makabila ya Mara ni mengi kuliko mikoa yote ya Tanzania, kama vile Waluo, Wajita, Waruri, Wazanaki, Wakuria, Wakabwa, Wakiroba, Wasimbiti, Wangoreme, Wakwaya, Waikoma, Wanata, Waisenye, Waikizu, Wasizaki, Wasukuma, Wataturu na makabila madogo kama Wanandi, Wakisii au Wamaragori. Kuna jumla ya makabila 30 yanayodai kujitegemea. Jamii zinazosahaulika huunganishwa katika kundi la Suba (Wategi, ambao pia huitwa Abhathegi maarufu kama Abhagirango, Waugu (Ugu), Warieri, Wakine, Wasweta na Waganjo, Wagire, Wakiseru, Wakamageta na Waturi). Baadhi ya jamii hizi zilimezwa na mila, lugha na desturi za Waluo zikaitwa Suba-Luo katika kipindi cha utawala wa DC Engram aliyekuwa wilaya ya Mara Kaskazini (North Mara). Baadhi ya jamii kwa upande wa Kenya iliyotawaliwa na Waingereza katika Wilaya za Kuria na South Nyanza huitwa Suna, Wagwasi, Ungoe, Kajulu na Kadem. Hata hivyo habari hizi bado zinafanyiwa utafiti kuangalia muingiliano wa lugha na tofauti za kilahaja kati ya jamii moja na nyingine hasa zilizopo Tanzania. Itakumbukwa jamii nyingi ziliingia upande ulioitwa South Nyanza kabla ya nchi za Afrika Mashariki kupata uhuru. Zipo tafiti nyingi siku hizi ambazo zinajaribu kubainisha makundi ya jamii hizo lakini muingiliano bado haujapata ufafanuzi makini. Kimsingi Mkoa wa Mara una jamii hizo zipatazo 30 lakini lugha kuu ni saba tu na nyingine ni lahaja kutokana na makundi ya lugha hizi: Luo, Kuria, Sukuma, Suba, Shashi, Zanaki na Taturu. Yapo makundi ya Wanata, Waisenye na Wataturu, Wazanaki (kundi lake: Kabwa, Kirobha, Wasimbiti, Wairienyi, Waikizu, Wangoreme), Luo (Wakowak, Wakamoti), Wakuria (Nyebhasi, Nyamongo, Wanchari, Wasweta, Wakenye, Warenchoka, Watimbaru, Waregi, hadi 14/15), Sukuma, Nyantuzu na Shashi (Wajita, Wakwaya, Waruri, Wakerewe, Wakara). Jamii zote humezwa katika makundi saba ya lugha kuu lakini kila jamii inajitofautisha kwa lahaja yake. Ni jamii za Kibantu peke yake zinazoweza kuwasiliana na kuelewana kukiwa na tofauti kidogo katika matamshi ya maneno. Ukichunguza zaidi, wakazi wa asili wa Mkoa wa Mara ni makabila makuu mawili yenye uhusiano wa karibu sana, yaani Wakurya (na vikabila kadhaa: Wakurya ni jina ‘linalobeba’ mengi ya yale yanaoyoitwa 'makabila' mkoani Mara, ambayo tafsiri yake halisi ni 'vikabila') na Wajita (hawa nao wana vikabila kadhaa). Pia, Wakurya-Waghusii si 'Bantu halisi' bali ni mchanganyiko kati ya Wabantu na Waniloti. Katika makabila ya Kibantu, yaliyoathiri damu ya Wakurya ni pamoja na: Wasukuma (kwa mfano, baadhi ya koo za Kizanaki, zilichanganya damu sana na Wasukuma) Wachaga (kwa mfano, Wakerobha au Wakiroba, walichanganya damu sana na wahamiaji toka Machame na Marangu kwa Wachaga - na hadi leo Machame na Marangu ni majina ya vitongoji huko kwa Wakiroba Mkoa wa Mara!) Wakikuyu (kwa mfano, baadhi ya Wakurya wa North Mara wana asili ya Wakikuyu au 'Abhaghekoyo'). Pia Wakikuyu wanachanga majina mengi na Wakurya - kama Nyambura, Murughi, Mwita, n.k. na hata lugha zinafanana kwa kiasi kikubwa). Pia, kama makabila, Wakurya-Waghusii, Wakikuyu, na Wameru wa Kenya wana uhusiano wa karibu na asili moja. Makabila mengine yanayohusiana nao ni Wagisu (Uganda) na Waluya (Kenya). Kuna wakati ambapo makundi hayo yote yalikuwa kabila moja, lakini wakatengana kwa kuhamia sehemu za mbali, wakawa makabila tofauti tunayoyajua leo. Waniloti waliochanganya damu na Wakurya ni pamoja na: Wamasai (baadhi ya koo za Wakurya wa leo zilitoka Umasai). Wajaluo (hasa kutokana na kuona kwani, tokea ujio wa Waniloti Mkoani Mara, watu hawa ni majirani), Wakalenjin (hasa kutokana na uhamiaji na wote kuwa na mila za wafugaji). Kwa hiyo, dhana ambayo imejengeka sana vichwani mwa watu kwamba Mara kuna makabila mengi, kwa kiasi kikubwa ni potofu. Ukiangalia kwa undani hata lugha na mila zilizopo, utaona kwamba hata hao kina yego/mbani (Wajita, Wakwaya, Wakara, Waruri, Wakerewe, n.k.) ni 'vikabila' tu vya kabila kubwa la Wajita. Ukiachia Wajaluo (au 'Jakowiny Luo'), mkoani Mara pia kuna Wataturu na Wanandi. Wanandi ni moja kati ya 'vikibila' vya Wakalenjin. Hata hivyo, idadi ya watu wa makabila haya ni ndogo ukilinganisha na ile ya 'Wakurya-Waghusii' na Wajita (ikiwa na maana ya kabila kubwa linalojumuisha pia Wajita, Wakwaya, na Waruri). Pia Mara, Wakurya hawaishi tu Tarime, bali huishi wilaya zote 6 za Mkoa wa Mara: Tarime, Rorya (hao ni Wakurya wa North Mara), Musoma Vijjini, Musoma Mjini, Bunda, na Serengati (hao ndio Wakurya wa South Mara). Abhaghusii (wanaoishi jimbo la Nyanza, Kenya) ni sehemu ya Wakurya wa 'North Mara'. Kwa hiyo, wanahistoria wanatakiwa kuliweka hili sawa. Wazungu walichorekodi ni majina ya vikabila (au koo kubwa), kwani hata leo ukienda Mara, ukauliza swali lako kizembe, si ajabu usikute mtu atayekujibu kwamba anaitwa Mkurya: wote watakuambia, mimi Mzanaki, Mkiroba, Mtimbaru, n.k. Wengine watasema, mimi Mmjita, Mkwaya, Mruri, nk. Kwa wakereketwa wa historia, Wakiroba (kikabila cha Wakurya-Wakisii) na Wakwaya (kikabila cha Wajita) ndiyo makabila ya asili ya inayoitwa leo hii Musoma mjini. Makundi haya mawili, pamoja na kuwa makibali tofauti, yana uhusiano wa muda mrefu wa karibu sana. Hupendana sana, na hata vita walipigana kwa kushirikiana! Pia Wakurya na Wajita, uhusiano wao wa karibu, na hata kushabihiana kwa lugha zao (kwa makabila haya makubwa mawili ya Mkoa wa Mara, hakuna anayeweza akamsengenya mwenzie, na asijue anasema nini), si jambo lililoanza juzi. Mababu wanatuambia hawa watu wote wamehamia Mara, wakitokea maeneo ambayo kwa sasa yako katika nchi zinazojulikana kama Misri na Libya (hata Wajaluo nao, walikujua toka huko). Wakati wa msafara, waligawanyika makundi matatu: • Moja likapita mashariki mwa Ziwa Victoria. Hili lilikuwa ndilo kundi kuu. Koo nyingi za Kikurya zilipita huko. Katika nyakati tofauti, zilitengana na Wagisu (Uganda), Waluya, Wameru, Wakikuyu (Kenya). • Moja likapita magharibi mwa Ziwa Victoria. Koo nyingi za Wajita, pamoja na baadhi ya koo za Wakurya (kama Abhashanake) walipita huko. • Moja likapita katikati ya Ziwa Victoria. Hili kundi lilikuwa dogo zaidi. Lilijumuisha zaidi koo chache za Kijita, kama vile Wakerewe. Hakuna historia ya vita kati ya Wakurya na Wajita, bali wameishi kwa kuelewana na kusaidiana. Hata hivyo, koo za Kikurya hupenda sana kupigana – na haya tunayaona hadi leo hii. Pia tukumbuke: Wabantu ni familia moja, na Waafrika ni ’kabila’ moja kubwa, na binadamu wote, bila kujali rangi zetu, tumetoka kwa Muumba mmoja na tuna asili moja – ni watoto wa Adamu na Eva (Waarabu humwita Hawa), kwa wale wanaoamini dini; au ni watoto wa Mwafrika kwa wale wanaoamini sayansi. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Bunda Mjini : mbunge ni Esther Bulaya (Chadema) Bunda Vijijini : mbunge ni Boniface Mwita Getere (CCM) Butiama : mbunge ni Nimrod Mkono (CCM) Musoma Mjini : mbunge ni Vedastus Mathayo Manyinyi (CCM) Musoma Vijijini : mbunge ni Prof. Sospeter Muhongo (CCM) Mwibara : mbunge ni Kangi Lugola (CCM) Rorya : mbunge ni Lameck Airo (CCM) Serengeti : mbunge ni Mwalimu Marwa Ryoba (Chadema) Tarime Vijijini : mbunge ni John Heche (Chadema) Tarime Mjini : mbunge ni Ester Matiko (Chadema) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Mara Orodha ya mito ya mkoa wa Mara Marejeo Viungo vya nje Tanzanian Government Directory Database M
2177
https://sw.wikipedia.org/wiki/Roma
Roma
Roma (pia Rumi) ni mji mkuu ("Roma Capitale") wa Jamhuri ya Italia. Pia ni mji mkuu wa mkoa wa Lazio. Roma iko katika sehemu ya magharibi ya kati ya Rasi ya Italia, katika makutano ya mito ya Tiber na Aniene karibu na Bahari ya Mediteranea. Roma ina wakazi 2,860,009 katika 1,285 km2 (496.1 sq mi), Roma ni komune yenye watu wengi zaidi nchini na ni jiji la tatu lenye watu wengi katika Umoja wa Ulaya kwa idadi ya watu ndani ya mipaka ya jiji. Roma mara nyingi inajulikana kama Jiji la Milima Saba kutokana na eneo lake la kijiografia, na pia kama "Mji wa Milele". Roma kwa ujumla inachukuliwa kuwa "chimbuko la ustaarabu wa magharibi na Utamaduni wa Kikristo", na kitovu cha Kanisa Katoliki. Mji wa Vatikano (nchi ndogo zaidi duniani) ni nchi huru ndani ya mipaka ya jiji la Roma, mfano pekee uliopo wa nchi ndani ya jiji. Eneo la Roma Roma uko katikati ya Italia ikiwa mita 20 juu ya UB ndani ya tambarare ya bonde la mto Tiber linalopakana na milima ya Abruzzi, milima ya Sabini na milima ya Albani. Wilaya za jirani ni Viterbo, Rieti, L'Aquila, Frosinone na Latina. Mwanzo wa Roma ulikuwa kwenye vilima saba vilivyo katikati ya mji wa leo vinavyoitwa: Palatino, Aventino, Campidoglio, Quirinale, Viminale, Esquilino na Celio. Hali ya hewa Hali ya hewa hutawaliwa na bahari iliyo karibu. Wastani wa halijoto kwa mwaka ni sentigredi 15,4. Mvua hunyesha wastani wa mm 758 kwa mwaka. Miezi yenye joto ni Juni hadi Agosti ikiwa na wastani wa sentigredi 21 hadi 23,8; ni miezi ya mvua kidogo. Mwezi baridi zaidi ni Januari ikiwa na wastani wa sentigredi 7,9. Historia Historia ya mji inasemekana imeanza rasmi tarehe 21 Aprili 753 KK, lakini majengo ya kwanza ni ya karne ya 10 KK. Katika karne za KK ulikuwa mji mkuu wa ufalme wa Roma, halafu wa Jamhuri ya Roma, hatimaye wa Dola la Roma. Katika miaka 100 KK - 400 BK hivi ulikuwa na wakazi wengi kuliko miji yote duniani. Uenezi wa Ukristo kuanzia mwaka 30 na hasa ujio wa Mtume Petro na Mtume Paulo waliofia dini yao (64-68) huko viliathiri mji huo moja kwa moja. Kuanzia karne ya 7 BK ukawa mji mkuu wa Dola la Papa, halafu wa Ufalme wa Italia na sasa wa Jamhuri ya Italia. Huitwa mara nyingi "Mji wa Milele". Wakazi Roma ilianza kama muungano wa vijiji vidogo vyenye wakazi mia kadhaa. Katika karne ya 1 BK ilikuwa tayari na wakazi milioni moja. Tangu kuondoka kwa makao makuu ya Kaisari na kupungua kwa nguvu ya Dola la Roma Magharibi idadi ya wakazi ilipungua hadi kuwa na takriban 100,000 mnamo mwaka 530. Katika karne zilizofuata Italia pamoja na Ulaya iliona vita na mashambulio ya makabila yasiyostaarabika. Mnamo mwaka 1000 Roma ilikuwa mji mdogo wenye wakazi 20,000 pekee walioishi ndani ya maghofu ya mji mkubwa wa kale. Tangu kuimarika kwa utawala wa mapapa mji ulianza kukua tena; mnamo mwaka 1900 ukawa na wakazi 400,000. Katika karne ya 20 mji ulipanuka sana hadi kufikia idadi ya wakazi wa zamani hata kuipita. Siku hizi asilimia 7.4 ni wageni. Orodha inayofuata inaonyesha makadirio hadi 1858, baadaye ni namba za sensa. Uchumi Roma ndiyo kitovu kimojawapo cha sekta ya viwanda na sekta ya huduma ya Italia. Utalii ni pia muhimu sana kiuchumi, kutokana na watalii 26,100,000 wanaoutembelea kila mwaka: 6.5% za Jumla ya Pato la Taifa zinapatikana ndani ya Roma ambazo ni kushinda miji mingine yote ya Italia. Roma ina makao makuu ya F.A.O. (Food and Agriculture Organisation - Shirika la Chakula na Kilimo) ya Umoja wa Mataifa pamoja na ofisi zote za serikali ya Italia. Tanbihi Viungo vya nje Info-Roma - Info-Rome ni tovuti kuhusu mambo ya kitalii katika mji wa Roma, hasa matukio ya aina mbalimbali, hoteli, maonyesho, nyumba za kumbukumbu na vyakula. some quick facts about Rome Satellite image of Rome at NASA's Earth Observatory Rome Travel Guide Guide about Rome with touristic informations Rome map 360° IPIX PANORAMA Roma Lazio Miji Mikuu Ulaya Miji ya Italia Miji ya Biblia Miji ya pwani ya Mediteranea Miji ya Olimpiki Urithi wa Dunia Mtume Petro Mtume Paulo Kanisa Katoliki
2183
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nyerere
Nyerere
Nyerere inaweza kumaanisha Julius Nyerere aliyekuwa rais wa kwanza wa nchi Tanzania Nyerere (Zanzibar) - kata ya jiji la Zanzibar, Tanzania
2184
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nile
Nile
Mto Nile (pia: Naili; kwa Kiarabu: ‏ ,النيل‎ an-nīl) ni mto mkubwa upande wa mashariki ya bara la Afrika. Mara nyingi hutajwa kuwa pia ni mto mrefu kabisa duniani kushinda mto Amazonas. Kutoka Ziwa la Viktoria Nyanza hadi mdomo wake kwenye Bahari ya Mediteranea Nile inavuka nchi za Uganda, Sudan Kusini, Sudan na Misri kwa urefu wa km 6,650. Beseni la Nile hukusanya maji ya eneo linalojumlisha 10% za eneo la Afrika yote au km² 3,349,000. Takriban watu milioni 250 hukalia beseni hilo. Jina "Nile" au "Naili" ni umbo la Kiingereza la jina la mto lililotokana na lile lililotumiwa na Wagiriki wa Kale: "Neilos" (Νεῖλος). Haijulikani Wagiriki walipata jina hilo kwa njia gani, lakini lilikuwa kawaida nje ya Misri. Wamisri wa Kale waliita mto huu kwa jina Ḥ'pī au Iteru linalomaanisha "mto mkubwa". Wakopti walikuwa na jina la piaro lakini tangu utawala wa Kiroma jina la Kigiriki lilizidi kutumika, na Waarabu waliendelea na jina la Kigiriki pia, hivyo leo hii wananchi wanasema "an-nil". Chanzo cha Nile Nile ina vyanzo viwili, yaani Nile yenyewe (inaitwa pia Nile nyeupe) inayotoka katika Ziwa Viktoria Nyanza na Nile ya buluu inayotoka katika Ziwa Tana. Majina hayo ya "nyeupe" na "buluu" yana asili yake katika mji wa Khartoum ambako mito yote miwili inaunganika ilhali kila mmoja una rangi tofauti kutokana na udongo tofauti uliotia rangi yake kwenye maji hayo. Vyanzo vya Nile ni mito yote inayopeleka maji kwenda Ziwa Viktoria Nyanza katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Uganda na Kenya. Chanzo cha mbali kabisa ni mto wa Luvironza huko Burundi unaoingia katika mto Kagera na kufika Ziwa Viktoria Nyanza. Mkono mwingine wa Nile unaanza Ethiopia ukiitwa Abbai au Nile ya Buluu: unatoka katika Ziwa Tana. Hakuna mapatano kabisa Nile inaanzia wapi. Kawaida ya waandishi Waingereza ni kuhesabu kuanzia Ziwa Viktoria; waandishi wa mataifa mengine huwa wanaweza wakaita tayari mto Kagera kwa jina "Nile ya Kagera". Majina ya Nile Majina ya sehemu ya mto kuanzia Ziwa Viktoria hadi Khartoum ni kama yafuatayo: Nile ya Viktoria kuanzia Jinja inapotoka katika Ziwa Viktoria kwa km 500 hadi Ziwa Albert Nile ya Albert kuanzia Ziwa Albert hadi mpaka wa Sudan Kusini ndani ya Sudan Kusini mto huitwa Bahr al-Jabal (mto wa mlimani) hadi kupokea tawimto la Bahr al-Ghazal kwa sababu ya rangi wakati wa mvua yake kutokana na udongo katika maji jina linakuwa Bahr al-Abyad kuanzia Bahr al-Ghazal hadi Khartoum kuanzia Khartoum jina pekee ni Bahr an-Nil (mto wa Nile) hadi mdomo wake wa delta kwenye Mediteranea. Matumizi wa maji ya Nile Tangu milenia kadhaa maji ya Nile yamekuwa msingi wa maisha yote nchini Misri na pia kwa sehemu kubwa ya nchi ya Sudan. Katika miaka ya 1920 Uingereza kama mtawala mkoloni wa Sudan na Misri ulikuwa na majadiliano juu ya ugawaji wa maji ya mto na kufikia mapatano juu ya matumizi ya maji ya mto Nile ya 1929. Hadi leo Misri inadai ya kwamba mapatanao yale yanakataa ujenzi wa malambo na kuanzishwa kwa miradi ya umwagiliaji inayotumia maji ya Nile bila kibali cha serikali yake. Hapa Misri inadai ya kwamba nchi zote zilizokuwa makoloni ya Uingereza wakati ule zinafungwa na mapatano ya mwaka 1929 na hizi ni pamoja na Sudan, Uganda, Kenya, Tanzania, halafu pia Ethiopia iliyopatana na Uingereza wakati ule. Nchi nyingine hazikubali madai hayo, ila majadiliano juu ya mapatano mapya ya ushirikiano katika beseni la Nile yanaendelea. Tazama pia Delta ya Nile Mito mirefu ya Afrika Mito ya Afrika Mito ya Tanzania Mito ya Uganda Mito ya Ethiopia Mito ya Sudan Kusini Mito ya Sudan Mito ya Misri
2185
https://sw.wikipedia.org/wiki/Bahari%20ya%20Mediteranea
Bahari ya Mediteranea
Bahari ya Mediteranea (pia: Bahari ya Kati) ni bahari ya pembeni ya Atlantiki kati ya mabara ya Afrika, Ulaya na Asia ya Magharibi. Eneo lake ni takriban milioni 2,5 km². Kina chake kirefu ni 5,267 m. Ina kanda ya hali ya hewa ya pekee pamoja na mimea na wanyama. Neno "Mediteranea" limetokana na lugha ya Kilatini likiunganisha maneno ya "medium" (inamaanisha "kati ya, katikati") na "terra" (inamaanisha "bara"). Kwa hiyo neno lenyewe linamaanisha "Bahari katikati ya bara". Katika lugha ya Biblia Kiebrania iliitwa "Bahari ya Magharibi" au "Bahari Kuu"; Waroma wa Kale waliotwala nchi zote zinazopakana na Bahari ya Mediteranea waliita "mare nostrum" yaani "bahari yetu". Waarabu na Waturuki wanaiita "Bahari Nyeupe" (kwa Kituruki: Akdeniz; kwa Kiarabu: البحر الأبيض al-baHr-al-abyaD) Jiografia Bahari ya Mediteranea ni bahari, si ziwa, kwa sababu imeunganishwa na Atlantiki kwa njia ya mlango wa bahari wa Gibraltar. Ina bahari za pembeni zake ambazo ni pamoja na Bahari Nyeusi, Bahari ya Aegean, Bahari ya Tyrrheni na mengine. Bahari Nyeusi inaunganishwa kwa njia ya mlangobahari wa Dardaneli, Bahari ya Marmara na mlangobahari wa Bosporus. Tangu mwaka 1869 kuna pia njia ya maji kati ya Mediteranea na Bahari ya Shamu ambayo ni Mfereji wa Suez. Kuna visiwa vingi sana hasa kati ya Ugiriki na Uturuki. Visiwa vikubwa ni Korsika, Sardinia, Sisilia, Kreta, Rhodos na Kibros. Nchi zinazopakana Leo hii kuna nchi au madola 22 zinazopakana na Bahari ya Mediteraneo: Afrika: Misri, Libya, Tunisia, Algeria na Moroko Asia: Uturuki, Syria, Lebanon, Israel, Kibros (Cyprus, kisiwa), Palestina (Gaza) na Misri Ulaya: Hispania, Ufaransa, Monako, Italia, Malta (funguvisiwa), Slovenia, Kroatia, Bosnia - Herzegovina, Montenegro, Albania, Ugiriki, Uturuki Viungo vya nje Jiografia ya Ulaya Jiografia ya Afrika Bahari Mediteranea Bahari ya pembeni
2194
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jibuti
Jibuti
Jibuti (kwa Kifaransa: Djibouti, kwa Kiarabu: جيبوتي) ni nchi ndogo ya Afrika ya Mashariki kwenye Pembe la Afrika. Imepakana na Eritrea, Ethiopia na Somalia upande wa bara. Kuna pwani ya Bahari ya Shamu na Ghuba ya Aden. Ng'ambo ya bahari iko nchi ya Yemen katika umbali wa km 20 pekee. Jina la nchi linatokana na lile la mji mkuu, Jibuti. Jiografia Hali ya nchi inalingana kwa karibu na ile ya mataifa mengine katika Mashariki mwa Afrika, Jibuti ilipo, ikipakana na Ghuba ya Aden na Bahari ya Shamu, katikati ya Eritrea, Ethiopia na Somalia. Eneo Kwa kilomita 13 Jibuti inapakana na Eritrea, huku kukiwa na urefu wa kilomita 337 za mpaka kati ya Jibuti na Ethiopia, na mpaka wa km 58 na Somalia. Kwa jumla ina mpaka wa km 506. Pia ina pwani ya urefu wa km 314. Jibuti inakaa kaika eneo la kufana, ikiwa karibu na leni zenye shughuli nyingi zaidi duniani la meli na pia karibu na mahali pa uchimbaji mafuta nchini Saudi Arabia. Jibuti pia ni kituo cha reli ya Ethiopia-Jibuti. Hali ya hewa Hali yake ya hewa ni ya joto kiasi, na pia haina mvua (ni jangwa). Miinuko Milima iliyopo katikati ya nchi hugawa tambarare za pwani kutoka plateau. Eneo la chini zaidi ni Ziwa Assal mita 155 chini ya usawa wa bahari na la juu zaidi ni volikano Moussa Ali yenye kimo cha mita 2028. Hakuna shamba la ukulima, unyunyizaji maji, mimea iliyojimeza huko (msitu upo tu katika milima ya Goda, hasa mbuga ya Day Forest). Takribani asilimia 9 ya nchi ni malisho yeliyojimeza (1993 mashariki). Kwa hiyo Jibuti inahesabiwa kuwa sehemu ya nyasi ya Ethiopia, isipokuwa kijisehemu kinachopakana na Bahari ya Shamu ambacho ni baadhi ya Jangwa la Pwani ya Eritrea ambayo inajulikana kuwa njia nzuri ya uhamiaji wa ndege ambao wanaweza kuwindwa. Mazingira Matukio ya kimaumbile ni pamoja na Matetemeko ya ardhi, kiangazi, mawimbi kutoka Bahari ya Hindi ambayo husababisha mafuriko na mvua kubwa. Malighafi ni pamoja na umeme kutoka ardhini (geothermal energy). Eneo hili limekumbwa na uhaba wa maji salama ya kunywa na pia kugeuka kwa eneo hilo kuwa jangwa. Jibuti ni mwanachama wa makubaliano ya kimataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, ueneaji wa jangwa, viumbehai vilivyo hatarini, sheria ya bahari, kulinda ukanda wa ozoni na uharibifu wa mazingira na meli. Historia Nchi ilikuwa koloni la Ufaransa kwa jina la Somalia ya Kifaransa, halafu (1967) Eneo la Kifaransa la Waafar na la Waisa, kutokana na majina ya makabila mawili makubwa zaidi ya eneo hilo. Sababu ya kuanzishwa kwa koloni ilikuwa nia ya Ufaransa ya kuwa na bandari ya mji wa Jibuti karibu na Bab el Mandeb inayotawala mawasiliano kati ya Bahari Hindi na Bahari ya Shamu kuelekea Mfereji wa Suez. Nchi ilipata uhuru tarehe 27 Juni 1977. Hadi leo umuhimu na uchumi wake unategemea bandari, ambapo zinapitia asilimia 95 za bidhaa zinazoingizwa Ethiopia. Nchi hiyo imeunganishwa na Jibuti kwa reli, moja ya zamani, na nyingine mpya iliyokamilika mwaka 2016. Watu Siku hizi wakazi wengi (60%) ni Wasomali, hasa wa kabila la Waisa, halafu Waafar (35%). Asilimia 5 zilizobaki ni Waarabu, Waethiopia na Wazungu (hasa Wafaransa na Waitalia). Lugha rasmi ni Kifaransa na Kiarabu. Kisomali na Kiafar ni lugha za taifa. Upande wa dini, Uislamu unafuatwa na 94% za wakazi na ndio dini rasmi pekee. Asilimia 6 wanafuata Ukristo katika madhehebu mbalimbali, hasa Waorthodoksi wa Mashariki kutoka Ethiopia (3.2%), halafu Wakatoliki (1.4%) na Waprotestanti (chini ya 1%). Tazama pia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Viungo vya nje Serikali Taarifa za jumla Djibouti profile from the BBC News. Mengineyo Key Development Forecasts for Djibouti from International Futures. Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Bahari ya Shamu Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa Pembe ya Afrika
2201
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mbuni
Mbuni
Mbuni ni ndege wakubwa wa familia Struthionidae. Kuna spishi mbili katika jenasi moja, lakini wataalamu wengine wanafikiri ni spishi moja tu. Ndege hao ni wakubwa kuliko wengine wote. Wana miguu mirefu na shingo ndefu na wanaweza kukimbia sana, hata kwa mwendo wa km 65 kwa saa, lakini hawawezi kuruka hewani. Rangi za manyoya ya dume ni nyeusi na nyeupe na rangi ya ngozi yake (shingo na miguu) ni nyekundu, pinki au buluu kufuatana na nususpishi. Manyoya ya jike ni kahawiakijivu na rangi ya ngozi ni sawa na dume. Mbuni wanaishi katika savana, nyika na majangwa ya Afrika, lakini wanafugwa ulimwenguni mwote. Jina la kisayansi la spishi kuu, Struthio camelus, linatoka katika lugha ya Kiyunani: στρουθιον = jurawa na καμηλος = ngamia. Dume la mbuni ana harimi ya majike 2-7 lakini moja tu anatawala. Dume hupanda majike yote ya harimi yake na majike huyataga mayai yao yote katika tago moja ambalo dume amelitengeneza. Jike anayetawala hutaga kwanza na baadaye hutupa mayai ya majike wasio na nguvu sana. Kwa kawaida hubakisha mnamo mayai 20. Majike huyaatamia mayai mchana na dume hufanya usiku, kwa sababu rangi ya jike inafanana na mchanga na rangi nyeusi ya dume haionekani usiku. Utangulizi Mbuni ni ndege wakubwa, huku asili yao ikiwa ni Afrika. Hawa ni ndege wasio na uwezo wa kuruka. Wanapatikana kwenye oda ya Struthioniformes, pamoja na ndugu aitwaye kiwi. Mbuni ni wa pekee sana sababu ya muonekane wake, wa shingo na miguu mirefu pamoja na uwezo wake mkubwa wa kukimbia, karibu ya maili 45 kwa saa. Huu ni mwendokasi mkubwa zaidi kwa ndege yeyote ardhini. Mbuni ndiyo ndege mkubwa kuliko wote wanaoishi duniani, wakiwa pia ndio watagaji wa mayai makubwa kuliko wote pia. Mlo wa mbuni kwa kiasi kikubwa huwa ni mimea, ingawa pia hula wadudu. Mbuni huishi katika makundi ya kutansatanga kati ya ndege watano mpaka hamsini. Wanapotishwa, mbuni hujificha kwa kulala ardhini au kukimbia mbali kama wakizingirwa, hushambulia adui zao kwa miguu yao yenye nguvu. Tabia kujamiiana hutofautiana kutoka maeneo moja mpaka vingine, ambapo mbuni dume hupigaia mbani jike hupigania nafasi ya kuwapata mbuni jike kwa nguvu. Mbuni hufugwa dunia nzima, hasa kutokana na manyoya yake, ambayo hunitia na kutumika kuondolea vumbi. Ngozi yake hutumika kutangenezea mtu mbali mbali huku nyama yake ikilizwa kibiashara. Maelezo Mbuni huwa na uzito wa kilogramu 63-130, luku mbuni dume wakifika mpaka uzito wa kg 155. Manyoya ya mbuni dumu wakubwa huwa kwa kiasi kikubwa meusi huku mkia ukiwa wakubwa huwa na rangi ya kahawia na nyeupe. Vichwa vya mbuni wote huwa havina manyoya. Ngozi za mbuni jike huwa na rangi ya pinki – kijini, huku dume wakiwa na ngozi ya bluu au kijini kutegemeana na nususpishi. Shingo zao ndefu, hukiweka kichwa chao mita 1.8 mpaka 2.75 juu ya ardhi, na macho yao husemwa kuwa ndiyo makubwa kuliko wanyama wote wa ardhini, yakiwa na sm 5, hivyo huweza kuwaona adui zao hata wakiwa mbali sana. Macho yao yanakingwa na mwanga mkali wa jua kutoka juu. Miguu ya mbuni, kama ilivyo kwa ndege wengine, haina manyoya isipokuwa magamba. Ndege hawa wawili huwa na vidole vikubwa viwili huku wengi wakiwa na vine, huku kucha moja ikiwa kubwa, ikifanana na kwato. Mbawa hutanuka kwa upana wa mita 2 hivyi, na hutumika sana kwenye tabia za kujamiiana na kujikinga na jua. Wana manyoya 50-60 hivi ya mkiani. Midomo yao huwa mipana na ncha ya duara kidogo. Tofauti na ndege wengine, mbuni hutoa mkoja tofauti na kinyesi, hivyo kuwa na kibofu. Pia tofauti na ndege wengine tena, huwa na ogani ya kutolea manii inayoweza kutoka nje ya mwili kwa urefu wa inchi 8. Mbuni hukomaa na kuwa na uwezo wa kuzaa wakiwa na miaka miwili/minne watoto wa mbuni hukua kwa kiasi ya sm 25 kwa mwezi. Wakiwa na umri wa mwaka mmoja tu, mbuni huwa na uzito wa kg 45. Mbuni jike huweza kuyatambua mayai yake hata kwenye kiota cha jumuiya. Uzazi Kujamiiana huwa na misimu tofauti kutokana na maeneo. Mbuni dume hupigania nafasi ya kujamiiana na jike wengine, na akishinda basi huwa na uwezo wa kujamiiana na jike wote wa kundi lake lote japo atakuwa na jike wake atakayedumu naye kwa wakati husika. Mbuni dume humvutia mbuni jike, kwa kumchezeachezea na kumpigia mbawa zake, ambaye humfuata na wao huenda faragha kwa ajili ya kujamiiana. Wakifika huko huwafukuza wanyama/mbuni wengine kama wapo na kisha dume kuweza tena, mbuni jike hukaa chini na kuwa tayari kwa kujamiiana. Mbuni jike hutaga mayai yaliyorutubishwa kwenye kiota cha jumuiya, ambacho huwa ni shimo lenye upana wa mita tatu na kina cha sentimeta 30-60. Mbuni dume ndiyo huchimba kiota hiki mayai ya mbuni ndiyo mayai makubwa kuliko yote na huwa na uzito wa kg 1.4, zaidi ya mara 20 ya yai la kuku. Huwa na rangi ya maziwa na wakati mwingine pamoja na madoa madogo. Mayai hutumiwa na mbuni jike wakati wa mchana na kutamiwa na mbuni dume wakati wa usiku . Mayai huanguliwa baada ya siku 35-45, na kisha hapo mbuni jike na dume wote hushirikiana kuwakuza watoto wao. Mbuni weusi huwindwa wakati huu, na mara nyingi mbuni mtoto mmoja tu ndiyo hufanikiwa kukua, huku wengine wakigeuzwa kitoweo na wanyama wengine wala nyama. Mbuni wanaokuzwa na binadamu, huhamisha sana upendo wao, na kuanza kuwapenda sana binadamu wanaowatunza. Spishi Struthio camelus, Mbuni wa Kawaida (Common Ostrich) S. c. australis, Mbuni Kusi in (South African Ostrich): shingo na miguu ya dume buluu kidogo. S. c. camelus, Mbuni Kaskazi (North African Ostrich): shingo ya dume nyekundu. S. c. massaicus, Mbuni Masai (Masai Ostrich): shingo na miguu ya dume pinki. S. c. syriacus, Mbuni Arabu (Arabian Ostrich): imekwisha sasa S. molybdophanes, Mbuni Somali (Somali Ostrich): shingo na miguu ya dume buluu. Spishi za kabla ya historia Struthio anderssoni - spishi kutoka mayai(?) Struthio asiaticus (Asian Ostrich) (Asia ya kati mpaka China, mwanzo wa Pliocene - mwisho wa Pleistocene) Struthio brachydactylus (Ukraine, Pliocene) Struthio chersonensis (Ulaya wa kusini mashariki mpaka Asia ya magharibi ya kati, Pliocene) - spishi kutoka mayai Struthio coppensi (Elizabethfeld, Namibia, mwanzo wa Miocene) Struthio daberasensis (Namibia, mwanzo - kati ya Pliocene) - spishi kutoka mayai Struthio dmanisensis (Dmanisi, Georgia, mwisho wa Pliocene/mwanzo wa Pleistocene) Struthio kakesiensis (Laetoli, Tanzania, mwanzo wa Pliocene) - spishi kutoka mayai Struthio karingarabensis (Afrika ya kusini magharibi na kati, mwisho wa Miocene - mwanzo wa Pliocene) - spishi kutoka mayai(?) Struthio linxiaensis (Yangwapuzijifang, China, mwisho wa Miocene) Struthio oldawayi (Tanzania, mwanzo wa Pleistocene - labda spishi ndogo ya S. camelus) Struthio orlovi (Moldova, mwisho wa Miocene) Struthio wimani (China na Mongolia, mwanzo wa Pliocene) Picha Tanbihi Majina ya ndege kwa Kiswahili Wanyama wa Biblia Struthionidae
2205
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mfumo%20wa%20Jua
Mfumo wa Jua
Mfumo wa Jua (:en:solar system) ni mpangilio wa Jua letu, sayari na sayari kibete zinazolizunguka pamoja na miezi yao, asteroidi, meteoridi, kometi na vumbi la angani, vyote vikishikwa na graviti ya Jua. Utaalamu kuhusu mfumo wa jua hujadiliwa katika fani ya astronomia. Muundo wa mfumo wa Jua Karibu masi yote ni ya Jua lenyewe, likiwa na asilimia 99.86 za masi ya mfumo wake. Kwa hiyo sayari zote kwa pamoja na asteroidi ni asilimia 0.14 tu ya masi ya mfumo kwa jumla. Umbali kati ya Jua na Dunia yetu ni takriban kilomita milioni 150. Umbali huu unaitwa "kizio astronomia" (:en:astronomical unit AU). Sayari ya mbali zaidi ni Neptuni ambayo ipo katika umbali wa vizio astronomia 30 kutoka Jua yaani ipo mara 30 mbali zaidi kutoka Jua kuliko Dunia. Magimba ya nje sana yanazunguka Jua kwa umbali wa vizio astronomia 50 au zaidi. Pamoja na sayari kuna idadi kubwa ya violwa vingine. Vingi ni vipande vidogo vya mwamba vinavyokusanyika katika kanda 3 zenye umbo la mwiringo ambazo ni ukanda wa asteroidi, ukanda wa Kuiper na wingu la Oort. Sayari hupatikana katika vikundi viwili. Mara nyingi zinaitwa "Sayari za ndani" na "Sayari za nje".Sayari nne za ndani ni Utaridi, Zuhura, Dunia na Mirihi ambazo ni ndogo na ni sayari za mwamba kama Dunia. Baada ya obiti ya Mirihi kuna pengo lenye upana wa vizio astronomia zaidi ya tatu na nusu hadi Mshtarii. Katika pengo hili upo ukanda wa asteroidi wenye violwa laki kadhaa pamoja na sayari kibete ya Ceres. Nje ya ukanda wa asteroidi hufuata kundi la sayari za gesi ambazo ni kubwa kushinda sayari za ndani. Sehemu kubwa ya masi yao si mwamba bali ni elementi na kampaundi zinazopatikana duniani kama gesi hasa hidrojeni(H), heliamu(He), Amonia(NH3) na methani(CH4). Gesi hizi zimeganda na kuwa imara kutokana na shinikizo kubwa na baridi kali. Sayari za jua letu Kuna magimba 8 yanayozunguka Jua letu yanayoitwa sayari. Sayari za kwanza kuanzia Utaridi(ing. Mercury) hadi Zohali (ing. Saturn) zinaonekana kwa macho. Tangu zamani zilipewa majina na watu. Sayari za mbali zaidi ziligunduliwa tu baada ya kupatikana kwa darubini. Sayari ambazo zipo katika mfumo wa Jua ni kama zifuatazo: (Namba zinazotaja sifa mbalimbali za sayari zinarejelea kipimo kulingana na tabia za Dunia yetu ambayo ni "1". Kuhusu majina ya sayari kadhaa kuna mkanganyiko katika kamusi na vitabu. Kama huna jina mbadala au umbo tofauti, limewekwa katika mabano kama (jina).) {| class="toccolours" border=1 cellspacing=0 cellpadding=2 style="text-align:center; border-collapse:collapse;" |+align=bottom style="text-align:left;"| * Utaridi ni jina la sayari ya kwanza kutokana na lugha ya Kiarabu na pia katika mapokeo ya Kiswahili tangu kale. Vitabu vingine hutumia neno "Zebaki" ambalo pia lina asili ya Kiarabu likimaanisha metali mojawapo; inaonekana limepatikana kama tafsiri ya jina la Kiingereza la sayari ya kwanza "Mercury" bila kujua historia ya majina ya sayari sita ya kwanza yaliyoingia katika Kiswahili kutoka katika lugha ya Kiarabu. ** Zuhura - Ng'andu ni sayari ambayo hutambulika kwa jina la Kibantu(Ng'andu) pamoja na jina lenye asili ya Kiarabu (Zuhura) *** Tazama makala ya Dunia kwa ajili ya namba halisi. Neno "ardhi" hutumika na waandishi kadhaa badala ya "dunia" wakitaka kutaja sayari ya tatu. |- bgcolor=#ccccff ! Jina la sayari ! Kipenyo kwenye ikwetakwa kulinganisha na kipenyo cha Dunia = 1 ! Masi (Dunia =1) ! Nusukipenyo ya obiti (Dunia =1) ! Muda wa obiti (miaka ya Dunia) ! Kuinama kwa obiti Pembenukta (°) ! Muda wa siku ya sayari(siku za Dunia) ! Miezi |- | Utaridi | align="center" | 0.382 | align="center" | 0.06 | align="center" | 0.387 | align="center" | 0.241 | align="center" |  7.00 | align="center" | 58.6 | align="center" | 0 |- | Zuhura (Ng'andu)<sup>**<sup> | align="center" | 0.949 | align="center" | 0.82 | align="center" | 0.72 | align="center" | 0.615 | align="center" |  3.39 | align="center" | -243 | align="center" | 0 |- | Dunia (Ardhi)*** | align="center" | 1.00 | align="center" | 1.00 | align="center" | 1.00 | align="center" | 1.00 | align="center" |  0.00 | align="center" | 1.00 | align="center" | 1 |- | Mirihi (Murihi, Meriki, Mars) | align="center" | 0.53 | align="center" | 0.11 | align="center" | 1.52 | align="center" | 1.88 | align="center" |  1.85 | align="center" | 1.03 | align="center" | 2 |- | Mshtarii | align="center" | 11.2 | align="center" | 318 | align="center" | 5.20 | align="center" | 11.86 | align="center" |  1.31 | align="center" | 0.414 | align="center" | 92 |- | Zohari (Zohali, pia Zuhali) | align="center" | 9.41 | align="center" | 95 | align="center" | 9.54 | align="center" | 29.46 | align="center" |  2.48 | align="center" | 0.426 | align="center" | 83 |- | Uranus <small> | align="center" | 3.98 | align="center" | 14.6 | align="center" | 19.22 | align="center" | 84.01 | align="center" |  0.77 | align="center" | -0.718 | align="center" | 27 |- | Neptun | align="center" | 3.81 | align="center" | 17.2 | align="center" | 30.06 | align="center" | 164.8 | align="center" |  1.77 | align="center" | 0.671 | align="center" | 14 |- |} Sayari vibete Hadi mwaka 2006 Pluto iliyopo nje ya mzingo wa Neptuni ilihesabiwa kuwa sayari, lakini baada ya azimio la Umoja wa Kimataifa wa Astronomia, Pluto inaitwa sasa "sayari kibete“, si sayari kamili tena. Kwa sasa kuna magimba 5 yanayotambuliwa kama sayari kibete: Ceres Pluto Haumea Makemake Eris Sayari za nyongeza? Katika miaka iliyopita wanaastronomia wamejadili uwezekano wa kuwepo kwa sayari za ziada katika umbali mkubwa. Imetambuliwa ya kwamba muundo wa mfumo wa jua ni mkubwa kuliko wataalamu wa kale walivyofikiri. Tangu kutambuliwa wa ukanda wa Kuiper ambamo Pluto ni sehemu tu inajulikana ya kwamba kuna magimba ya angani mengi yasiyoonekana kwa kirahisi kwa sababu yanapokea na kuakisi nuru kidogo sana kutoka kwenye Jua. Kuhusu magimba ya angani yaliyo mbali zaidi kuliko ukanda wa Kuiper hakuna uhakika bado, lakini tangu mwaka 2012 vipimo vipya vilisababisha kutokea kwa nadharia tete kuhusu sayari ya tisa katika umbali mkubwa sana ambayo haikutazamiwa bado. Mwaka 2017 kilitokea kiolwa cha anga kutoka nje ya mfumo wa Jua letu. Kiolwa hiki kilichoitwa ʻOumuamua kilifika kwa njia isiyolingana na bapa la sayari za mfumo wa Jua, tena kwa kasi kubwa mno hivyo kilionekana si sehemu ya mfumo wetu. Kutokea kwa Mfumo wa Jua Mfumo wa Jua ulianza kutokea zamani sana na wataalamu wanaendelea kujadili nadharia zinazoeleza tabia zake kulingana na kanuni za fizikia. Nadharia zinazokubaliwa na wataalamu wengi ni hivi: Takriban miaka bilioni 4.5 iliyopita kulikuwa na wingu kubwa la molekuli lililozunguka kitovu cha galaksi yetu yaani Njia Nyeupe. Wingu hilo lilifanywa hasa na hidrojeni na heliamu (zaidi ya asilimia 99), pamoja na viwango vidogo vya elementi nzito zaidi. Hidrojeni na heli zilitokea katika mlipuko mkuu ulioanzisha ulimwengu wetu. Elementi nzito zilitokea katika nyota zilizowahi kutangulia na kulipuka kabla ya kuzaliwa kwa Jua letu na kusambaza mata zao kama vumbi ya angani. Ndani ya wingu kubwa kulikuwa na sehemu ambamo molekuli ziliongezeka na hivyo kuunda uga wa graviti iliyoendelea kuvuta mata nyingine, kuongeza tena graviti ya sehemu hizi kadiri zilivyopokea mata zaidi. Miendo ndani ya wingu labda ilianzishwa na mishtuko ya supanova ya karibu. Lakini hii ni nadharia tete tu hadi sasa. Sasa sehemu moja ya wingu kubwa ambako molekuli zinaendelea kukusanyika inaanza kuzunguka kwenye mhimili wake na kuongeza mzunguko huo pamoja na ongezeko la graviti. Graviti hiyo inaendelea kuvuta molekuli za eneo kubwa zaidi hadi diski ya uongezekaji (ing. accretion disk) inatokea. Hapo masi kubwa inaelekea kukusanyika katika kitovu cha diski ambako shinikizo na jotoridi zinaanza kupanda. Kadiri atomi zinavyokazwa na graviti na jotoridi kuwa juu, mchakato wa myeyungano wa kinyuklia unaanza katika kitovu na hapo nyota changa inatokea. Myeyungano wa kinyuklia unasababisha mnururisho unaoelekea nje. Mnururisho huu ni kani yenye mwelekeo kinyume cha graviti. Hapo nyota haikazwi zaidi. Hivyo nyota inaingia katika hali thabiti ya uwiano baina ya graviti inayotaka kukaza mata yake kwenye kitovu na shinikizo la mnururisho linaloelekea kinyume. Ndani ya mata iliyobaki kwenye diski nje ya kiini cha nyota changa kuna sehemu ambapo molekuli zinakazana na kuunda vianzio sayari (ing. planetesimal)''. Viini vikubwa zaidi vinavuta tena viini vidogo na kufanya idadi ya viini kupungua ilhali viini vinaungana. Vinavyobaki hukua na kuongeza masi zake na ndipo chanzo cha sayari zetu. Tabia za sayari zinatokea tofauti kutegemeana na umbali wa Jua. Elementi nzito zaidi zinakusanyika karibu na Jua. Kinyume chake, elementi nyepesi zinasukumwa na upepo wa Jua zinaanza kukusanyika kwa umbali mkubwa zaidi. Kwa hiyo sayari zilizo karibu na Jua kama Utaridi, Zuhura, Dunia na Mirihi ni sayari za miamba, zinafanywa na elementi nzito. Sayari zilizo mbali na Jua kama Mshtarii, Zohali, Uranusi na Neptuni ni sayari za gesi, zinafanywa na elementi nyepesi. Marejeo Viungo vya Nje Astronomia Mfumo wa jua
2206
https://sw.wikipedia.org/wiki/Zuhura
Zuhura
Zuhura (alama: ; pia: Ng'andu; kwa Kiingereza Venus) ni sayari ya pili katika mfumo wa jua na sayari zake. Kati ya sayari zote za jua ndiyo inayofanana zaidi na dunia yetu. Jina la sayari Sayari hii ina majina mawili kwa Kiswahili: Zuhura, kwa matamshi mengine pia "Zuhra", ni jina leye asili ya Kiarabu زُهَرَة zuhara lenye maana asilia ya "mwenye kung'aa". Ng'andu ni jina lenye asili ya Kibantu. Tabia za sayari Kwenye anga la usiku inang'aa kushinda nyota zote isipokuwa mwezi. Kutokana na nguvu ya mwanga wake inaonekana mapema kati ya nyota za kwanza zinazoonekana jioni; vilevile huwa inaonekana kama nyota ya mwisho wakati wa pambazuko. Zuhura ina umbali wa kati ya kilomita milioni 107.5-108.9 kutoka jua. Umbali kutoka dunia yetu hutegemea na mahali pa dunia na Zuhura kwenye mizingo yao ya kuzunguka jua: uko kati ya kilomita milioni 38.3-260.9. Ukubwa wake na pia kemia yake zinafanana sana na dunia ikiwa kipenyo chake ni km 12,103.6 kwenye ikweta. Haina mwezi wowote. Mwaka wa Zuhura (ambao ni muda wa kutimiza obiti moja wa kuzunguka dunia) una siku 224.7 za kidunia. Siku ya Zuhura (ambayo ni muda wa dura moja ya sayari yenyewe) ina siku 243 za kidunia. Zuhura ni sayari yenye mzunguko kufuatana na mwendo wa saa. Hali ya hewa ni ya joto sana, kwa wastani sentigredi 500. Hewa yake ni hasa ya kabonidaioksaidi inayosababisha mawingu mengi yanayozuia sura yake isionekane kwa darubini. Kutokana na halijoto kali hakuna maji. Utafiti Warusi na Wamarekani walifaulu kupeleka vipimaanga mbalimbali hadi Zuhura, vingine vilipita na kupima hewa, vingine vilifika kwenye sura ya sayari na kutuma picha za mazingira hadi kuharibika kutokana na joto kali. Uso wa sayari umefanyiwa utafiti kwa msaada wa rada kutoka vipimaanga Magellan na Pioneer-Venus. Kutokana na matokeo yake ramani ya kwanza ilitokea. Sehemu kubwa ya sayari ni tambarare yenye vilima na mabonde yasiyo marefu. Kutokana na joto kubwa (mnamo 500°C) hakuna maji wala bahari. Kuna sehemu mbili ambako nyanda za juu zinapanda juu ya uwiano wa kawaida na hizi zilifananishwa na kontinenti za Dunia. Karibu na ikweta ya Zuhura iko sehemu inayoitwa "Aphrodite Terra" yenye ukubwa kama Amerika Kusini. Kwenye upande wa mashariki kuna safu za milima na mabonde makubwa pamoja na volkeno. Sehemu ya pili huitwa "Ishtar Terra" yenye ukubwa sawa na Australia kwenye Dunia. Hapa kuna milima ya Maxwell yenye urefu wa mita 10.800 juu ya uwiano wa wastani. Tanbihi Viungo vya nje D. Darling, Encyclopedia of Astrobiology, Astronomy, and Spaceflight Venus profile at NASA's Solar System Exploration site Missions to Venus and Image catalog at the National Space Science Data Center Soviet Exploration of Venus and Image catalog at Mentallandscape.com Venus page at The Nine Planets Transits of Venus at NASA.gov Geody Venus, a search engine for surface features Kuhusu ramani za Zuhura Map-a-Planet: Venus by the U.S. Geological Survey Gazetteer of Planetary Nomenclature: Venus by the International Astronomical Union Venus crater database by the Lunar and Planetary Institute Map of Venus by Eötvös Loránd University Google Venus 3D, interactive map of the planet zuhura
2214
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ungo
Ungo
Ungo ni chombo cha kupepetea vitu hasa nafaka kilichotengenezwa kwa chane za miwale au mimea mingine ya jamii hiyo. Ni pia jina la gamba la juu la kaa. Vifaa Kilimo
2215
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mchuzi
Mchuzi
Mchuzi ni kitoweo cha majimaji kinachopikwa kwa kuchanganya nyama au samaki n.k. pamoja na viungo kama vile binzari, vitunguu, mafuta, chumvi na nyanya. Kuna aina nyingi za mchuzi. Mchuzi wa bata na kuku ni mtamu sana; wachanganywa na viungo na mafuta: ladha yake ni ya pekee. Mchuzi ni msingi wa chakula cha supu. Chakula
2216
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kande
Kande
Kande ni chakula kinachopikwa kwa kuchanganya punje za mahindi na maharagwe au kunde, lakini pia maboga n.k. Ni utamaduni wa baadhi ya makabila, kwa mfano nchini Tanzania Wapare, Wabena n.k. Kande huwa zinalika sana kwenye shule nyingi, hasa za bweni. Chakula cha Kiafrika
2219
https://sw.wikipedia.org/wiki/NASA
NASA
NASA ni kifupi cha Kiingereza cha "National Aeronautics and Space Administration" (Mamlaka ya Marekani ya Usafiri wa Anga). Mamlaka hii ilianzishwa 1958. Wajibu wake ni kusimamia miradi ya serikali ya Marekani ya kuendesha utafiti na uchunguzi wa anga. NASA inasimamia utengenezaji wa roketi za kurusha vyombo vya angani na utengenezaji wa vyombo vya angani vyenyewe. Miradi ya NASA ilianzishwa kutokana na Mshtuko wa Sputnik yaani baada ya Warusi kushtusha dunia kwa kupeleka vyombo vya angani vya kwanza katika mradi wao wa Sputnik. Uliofuatiwa na mradi wa "Vostok" ambao tarehe 12 Aprili 1961 ulimfikisha Yuri Gagarin angani akiwa mtu wa kwanza kwenda angani. Mradi wa kwanza wa NASA ulikuwa Mradi wa Mercury uliotakiwa kuonyesha ya kwamba wanaanga wanaweza kukaa angani kwa muda fulani. Alan B. Shepard Jr. alikuwa Mmarekani wa kwanza angani kwa muda wa dakika 15; John Glenn alikuwa Mmarekani wa kwanza wa kuzunguka dunia tarehe 20 Februari 1962 kwa chombo cha angani "Friendship 7". Mradi huo ulifuatiwa na Mradi wa Gemini kuanzia mwaka 1965 ulionyesha ya kwamba watu wanaweza kukaa angani kwa muda wa siku kadhaa hata kutekeleza shughuli fulani. Gemini iliandaa Mradi wa Apollo uliopeleka watu wa kwanza mwezini. Chombo cha angani "Apollo 11" kilifikisha wanaanga Neil Armstrong na Buzz Aldrin kwenye uso wa mwezi tarehe 20 Julai 1969 na kuwarudisha dunia tena. Tangu mwanzo ule kuna miradi mingi iliyofuata. Viungo vya nje Tovuti ya NASA Marekani Usafiri wa anga-nje Kifupi
2221
https://sw.wikipedia.org/wiki/Korongo
Korongo
Kwa maana tofauti ya neno hilo tazama Korongo (maana) Korongo ni ndege wenye shingo ndefu na miguu mirefu na hunyoosha shingo na miguu wakiruka angani. Yangeyange na makoikoi hupinda shingo yao wakiruka angani. Jina hili hutumika kwa jamii mbili ya ndege: Ciconiidae (storks) Gruidae (cranes) Korongo na jamaa Wanyama wa Biblia
2222
https://sw.wikipedia.org/wiki/Waarabu
Waarabu
Waarabu (kwa Kiarabu عَرَبِ, matamshi ya Kiarabu: [ʕarabi]) ni watu ambao lugha mama yao ni Kiarabu wakijitambua vile. Asili ya Waarabu na uenezaji Kiasili walikuwa watu wa Bara Arabu na maeneo jirani katika Syria na Iraki, lakini tangu kuja kwa Uislamu walienea nje ya eneo asilia hasa katika Afrika ya Kaskazini na nchi za Mashariki ya Kati ambako walijichangaya na wenyeji ambao wengi wao wamepokea lugha ya Kiarabu tangu karne nyingi na kujitazama kama Waarabu pia. Kutokana na uhamiaji wako pia katika Afrika ya Mashariki, Visiwa vya Komoro na visiwa vingine vya Bahari Hindi, Amerika, Ulaya Magharibi, Indonesia, Uhindi na Iran. Dini ya Uislamu ilianzia kati ya Waarabu na hivyo Kiarabu ndiyo lugha ya Qurani na maandiko ya Kiislamu, na Waarabu wengi ni Waislamu. Walakini kati ya Waislamu wote Waarabu ni kama asilimia 20 tu. Historia Kihistoria Waarabu walitajwa mara ya kwanza wakati wa karne ya 9 KK kama makabila ya mashariki na kusini mwa Syria na kaskazini mwa Bara Arabu. Waarabu wanaonekana walikuwa chini ya wafalme wa Milki ya Ashuru (911-612 KK), na baadaye chini ya Milki ya Babeli iliyofuata (626-539 KK), Waakhemi (539-332 KK), Waseleukidi na Waparthi. Katika karne ya 3 KK Waarabu wa Nabatea waliunda ufalme wao karibu na Petra katika Yordani ya leo. Makabila ya Kiarabu kama Waghassanidi na Walakhmidi huanza kuonekana katika jangwa la Syria Kusini kuanzia katikati ya karne ya 3 BK wakiunda milki zao zilizoshirikiana na Dola la Roma na Wasasani. Hadi karne ya 7 sehemu ya Waarabu hasa wa magharibi mwa eneo lao walikuwa Wakristo, wengine pia Wayahudi. Baada ya Muhamad, makhalifa wa kwanza (632-661 BK) waliunganisha Waarabu wote chini ya utawala wao wakaendelea kuvamia milki jirani za Dola la Roma na Uajemi ya Wasasani. ote walianza kutumia lugha ya Kiarabu kama lugha ya utawala. Makabila mengi kutoka Bara Arabu yalianza kuhamia nchi zilizovamiwa katika hiyo milki kubwa ya Kiislamu iliyoenea kutoka Moroko na Hispania upande wa magharibi hadi mipaka ya China na Uhindi upande wa mashariki. Katika karne zilofuata, wakazi wengi wa maeneo hayo walianza kuwa Waislamu na kutumia Kiarabu kama lugha ya kidini na ya kielimu; hasa katika sehemu kubwa ya Afrika Kaskazini pamoja na Misri na katika nchi za Asia Magharibi (hasa nchi za leo Syria, Lebanoni, Iraki) wenyeji wengi walianza kutumia Kiarabu kama lugha yao na hivyo kuitwa Waarabu. Kwa karne nyingi Waarabu hao walitawaliwa na Milki ya Osmani. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914-1918) milki hiyo ilivunjwa na kugawiwa kwa maeneo ya nchi za Kiarabu za leo ambazo kwa muda mfupi zilitawaliwa bado kama makoloni au nchi lindwa chini ya Uingereza na Ufaransa. Mwaka 1945 nchi hizo ziliunda Jumuiya ya Nchi za Kiarabu. Nchi za Waarabu Leo hii Waarabu kimsingi hukalia nchi 22 wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu. Nchi hizo zinaenea kwa kilomita za mraba milioni 13 kutoka bahari ya Atlantiki upande wa magharibi hadi Bahari ya Kiarabu katika mashariki na kutoka Bahari ya Mediterranean katika kaskazini hadi Pembe ya Afrika na Bahari ya Hindi katika kusini. Watu wasio Waarabu wakitumia lugha zao za pekee huishi pia katika nchi hizo, wakati mwingine wakiwa wengi. Hawa ni pamoja na Wasomali, Wakurdi, Waberberi, Waafar, Wanubi na wengineo . Uenezaji wa lugha Wakati wa kuzaliwa kwa Mtume Muhamad lugha ya Kiarabu ilitumika Uarabuni tu, nchi ya jangwa na oasisi. Kutoka hapa makabila ya Waarabu Waislamu walivamia nchi jirani ambako wenyeji walitumia lugha mbalimbali. Lugha kadhaa zimeendelea kwa viwango vidogo, vingine vimebaki na nguvu zaidi. Lugha ya Kiaramu iliyowahi kutamalaki katika siasa na uchumi kuanzia Syria hadi Uajemi na zaidi, imebaki kati watu wa vijiji katika maeneo ya kaskazini ya Syria na Iraki, pia kama lugha ya liturgia kanisani. Kikopti iliyokuwa lugha ya Misri imebaki pekee katika liturgia ya kanisa ilhali Wakristo Wakopti wanaongea Kiarabu tu. Kiberber bado inazungumzwa na milioni kadhaa katika Moroko na Algeria. Kikurdi ina nguvu katika milima ya Syria na Iraki kaskazini. Kiajemi (lugha ya Iran) kimefaulu kurudi kama lugha ya kitaifa lakini imepokea karibu asilimia 40 za msamiati wake kutoka Kiarabu; atahri kubwa ya lugha ya Kiarabu inaonekana pia katika lugha nyingine nyingi hadi Kiswahili. Katika nchi zinazoitwa Kiarabu, lugha ya Kiarabu imekuwa lugha ya kila siku ya kuongea na pia ya serikali, biashara na utamaduni hata kwa hao ambao bado wmetunza lugha nyingine kama lugha yao ya kwanza. Dini Kwa upande wa dini, Waarabu huwa na tofauti kati yao. Katika zama za kabla ya Uislamu, Waarabu wengi walifuata dini za kuabudu miungu mingi. Makabila kadhaa yalikuwa yamekubali Ukristo au Uyahudi na watu wachache waliotwa hanif walisemekana kuwa na imani kwa Mungu mmoja. Leo, karibu asilimia 93 za Waarabu ni wafuasi wa Uislamu . Kuna pia Wakristo kama jumuiya ndogo zaidi. Waislamu Waarabu kimsingi ni wa madhehebu ya Wasunni, Washiia, Waibadi na Waalawi. Wakristo wa Kiarabu kwa ujumla hufuata moja ya Makanisa ya Kikristo ya Mashariki, kama yale yaliyo ndani ya makanisa ya Orthodox ya Mashariki, makanisa Katoliki ya Mashariki, au makanisa ya Kiprotestanti ya Mashariki. Kuna pia idadi ndogo ya Wayahudi wa Kiarabu ambao bado wanaishi katika nchi za Kiarabu lakini wengi wao waliondoka kwao wakihamia Israeli au nchi nyingine za Ulaya na Amerika. Sehemu ya Wakristo katika nchi za Kiarabu hawajitambui kuwa Waarabu kwa mfano Wakopti au Waashuri. Marejeo Waarabu Makala zisowekewa maelezo ya vyanzo
2223
https://sw.wikipedia.org/wiki/Korongo%20%28Ciconiidae%29
Korongo (Ciconiidae)
Korongo hawa ni ndege wa familia ya Ciconiidae wenye domo refu na nene (korongo wa familia ya Gruidae wana domo fupi na jembamba zaidi). Wanaitwa kongoti pia, hususa korongo mfuko-shingo. Mabawa yao ni marefu sana, yale ya korongo mfuko-shingo yana m 3.2: marefu kuliko yale ya ndege wote ghairi ya tumbusi wa Andes (Andean condor). Spishi nyingine huishi mahali pa majimaji nyingine mahali pakavu. Hula vyura, samaki, wadudu na nyungunyungu, hata ndege na wanyama wadogo. Korongo hawa hawawezi kutoa sauti. Lakini kwa tago hupiga kelele na domo yao. Spishi wa Afrika Anastomus lamelligerus, Korongo Domo-wazi (African Openbill Stork) Anastomus l. lamelligerus, Domo-wazi wa Afrika (African Openbill Stork) Anastomus l. madagascariensis, Domo-wazi wa Madagaska (Madagascan Openbill Stork) Ciconia abdimii, Korongo Samawati (Abdim's Stork) Ciconia ciconia, Korongo Mweupe au Kuyu (White Stork) Ciconia episcopus, Korongo Shingo-sufu (Woolly-necked Stork) Ciconia e. microscelis, Korongo Shingo-sufu wa Afrika (African Woolly-necked Stork) Ciconia nigra, Korongo Mweusi (Black Stork) Ephippiorhynchus senegalensis, Korongo Domo-ngazi (Saddle-billed Stork) Leptoptilos crumenifer, Korongo Mfuko-shingo, Kongoti au Marabu (Marabou Stork) Mycteria ibis, Korongo Domo-njano (Yellow-billed Stork) Spishi wa mabara mengine Anastomus oscitans (Asian Openbill Stork) Ciconia boyciana (Oriental White Stork) Ciconia maguari (Maguari Stork) Ciconia stormi (Storm's Stork) Ephippiorhynchus asiaticus (Black-necked Stork) Jabiru mycteria (Jabiru) Leptoptilos dubius (Greater Adjutant) Leptoptilos javanicus (Lesser Adjutant) Mycteria americana (Wood Stork) Mycteria cinerea (Milky Stork) Mycteria leucocephala (Painted Stork) Picha Korongo na jamaa Wanyama wa Biblia
2225
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Ruvuma
Mkoa wa Ruvuma
Mkoa wa Ruvuma ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepewa jina kutokana na mto Ruvuma ambao ni mpaka wake wa kusini na Msumbiji. Umepakana na Ziwa Nyasa na Mkoa wa Morogoro upande wa magharibi, mikoa ya Iringa na Lindi upande wa kaskazini na Mkoa wa Mtwara upande wa mashariki. Makao makuu ya mkoa yako Songea mjini. Wilaya Ndani ya mkoa huu kuna wilaya sita ambazo ni (idadi ya wakazi katika mabano): Nyasa (146,160; tangu 2012) Songea Mjini (203,309), Songea Vijijini (173,821), Tunduru (298,279), Mbinga (353,683), Namtumbo (201,639). Wakazi Jumla ya wakazi wote katika Mkoa wa Ruvuma ni 1,848,794 (sensa ya mwaka 2022). Makabila makubwa katika Ruvuma ni Wangoni, Wamatengo, Wayao, Wandendeule, Wamanda, Wanyasa, Wapoto, Wabena na Wandengereko. Karibu na Songea iko monasteri kubwa ya Peramiho ya watawa Wabenedikto na nyingine iko Hanga. Elimu Elimu bado inahitajika, hasa kwa maeneo ya vijijini, maana watu wengi katika mkoa huu hawajaelimika hivyo huleta changamoto katika maendeleo maana taifa huhitaji watu ambao ni wasomi. Miundombinu Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna barabara ya lami kutoka Dar es Salaam kupitia Makambako na Njombe hadi Songea. Barabara kuu kwenda [[Lindi] ni kiwango cha lami kuanzia Songea mjini kupitia Wilaya za Namtumbo, Tunduru, Nanyumbu, Masasi, Mnazimmoja-Lindi, hadi Dar es Salaam. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Songea Mjini : mbunge ni Leonidas Tutubert Gama (CCM) Nyasa : mbunge ni Stella Manyanya (CCM) Tunduru Kaskazini : mbunge ni Ramo Matala Makani (CCM) Tunduru Kusini : mbunge ni Daimu Iddi Mpakate (CCM) Peramiho : mbunge ni Jenista Mhagama (CCM) Madaba : mbunge ni Joseph Kisito Mhagama (CCM) Namtumbo : mbunge ni Edwin Amandus Ngonyani (CCM) Mbinga Mjini : mbunge ni Sixtus Mapunda (CCM) Mbinga Vijijini : mbunge ni Martin Msuha (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Ruvuma Orodha ya mito ya mkoa wa Ruvuma Viungo vya nje Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma Matokeo ya sensa 2002: Ruvuma Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census Tanzanian Government Directory Database Makabila ya Tanzania R
2228
https://sw.wikipedia.org/wiki/The%20Jackson%205
The Jackson 5
The Jackson 5 lilikuwa kundi la muziki wa roki la nchini Marekani lililoundwa na wanamuziki watano; mmojawapo ni Michael Jackson. Nyimbo zilizoimbwa na kundi hili ni kama "The Love You Save", "I Will Be There", "Mamas Pearl" na "Never Can Say Goodbye". Kundi Jackie Jackson Tito Jackson Jermaine Jackson Marlon Jackson Michael Jackson Viungo vya nje Jackson Five documentary katika BBC Radio The Jackson 5 katika Rock and Roll Hall of Fame The Jackson Five katika Vocal Group Hall of Fame Jackson Five Indiana
2229
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siku%20ya%20wapendanao
Siku ya wapendanao
Siku ya wapendanao (kwa Kiingereza: Valentine's Day) ni sikukuu ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Februari ya kila mwaka. Historia yake imeanzia karne ya 3 huko Roma au Terni ambapo alikuwapo padri au askofu Valentinus ambaye akaja kuheshimiwa kama mtakatifu hasa tarehe hiyo. Hadithi zilizosababisha sikukuu kuenea Inasemekana kwamba Kaisari wakati huo alikuwa Claudius II: yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyeoa wala kuwa na familia (kapera). Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa askari. Valentinus alipinga jambo hili na hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme Claudius alipopata habari hizi aliamuru Valentinus akamatwe na kuuawa. Kuna hadithi nyingine ya kuwa akiwa gerezani Valentinus aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza za Valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani; mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya: Kutoka kwa Valentinus wako. Mbali ya hadithi, askofu huyo alijulikana kwa miujiza yake. Huko Terni, mnamo 2011, ilipatikana mifupa ya Sabino e Serapia: mmoja alikuwa Mpagani akida wa jeshi la Roma, mwingine msichana Mkristo motomoto. Kwa ajili yake Sabino aliongokea Ukristo, lakini baada ya muda mfupi aligundua kwamba Serapia ni mgonjwa wa kifua kikuu. Ili asitengane naye, Sabino alimuomba Valentinus, naye alibariki ndoa yao na kuomba mapendo yao yadumu milele. Baadaye walifariki pamoja wamekumbatiana na ndivyo mifupa yao inavyopatikana hadi leo. Toka hapo Valentine anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na sikukuu yake kuadhimishwa kote duniani. Kuna matukio kadha wa kadha kutokana na historia ya siku hiyo ikiwemo kufungwa jela kwa askofu Mt. Valentinus wa Roma kutokana na kuwatesa baadhi ya Wakristo katika Dola la Roma mnamo karne ya 3. Kulingana na tamaduni za kale, Askofu huyo alimponya mtoto kipofu wa mfungwa mwenzake. Ndipo mara nyingi matendo yake yanahusishwa na kitendo kikuu cha upendo: kuna baadhi ya historia zinasema kuwa askofu huyo alimtumia barua mtoto wa yule mfungwa mwenzake aliyemponya upofu, na barua hiyo ilikuwa ni katika hali ya kumuaga akiendea kutimiza kifungo chake na adhabu ya kunyongwa. Historia zinazidi kusema kuwa mwishoni mwa barua hiyo kulikuwa kumesainiwa kwa maneno yaliyosema "Valentinus wako". Lakini pia baadhi ya tamaduni za watu zilizidi kusema kuwa askofu huyo aliwafungisha ndoa wanajeshi wawili ambao walikuwa wamekatazwa kufunga ndoa. Sikukuu Sikukuu za Kimataifa Jinsia
2231
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kigoma
Mkoa wa Kigoma
Mkoa wa Kigoma uko kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 47000. Umepakana na Burundi na Mkoa wa Kagera upande wa Kaskazini, mikoa ya Shinyanga na Tabora upande wa mashariki na Mkoa wa Rukwa upande wa kusini. Magharibi umepakana na Ziwa Tanganyika penye mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Jiografia Mkoa una eneo la km² 45,066 (sawa na 4.8% ya eneo lote la Tanzania) ikiwa km² 8,029 ndizo maji ya ndani (hasa Ziwa Tanganyika) na km² 37,037 ndizo nchi kavu. Takriban robo ya eneo la mkoa wa Kigoma hutumika kwa kilimo na ufugaji, karibu nusu ni misitu. Kwa ujumla eneo la mkoa ni tambarare ya juu inayoanza kwenye mita 800 juu ya UB karibu na Ziwa Tanganyika na kupanda hadi mita 1,750. Mito ya kudumu ndani ya mkoa wa Kigoma ni Malagarasi, Luiche, Ruchugi na Rugufu. Hifadhi za wanyama na za kihistoria Kuna maeneo mawili yenye sokwe: ndipo Hifadhi ya Taifa ya Gombe (alikofanya utafiti wake mwanabiolojia Jane Goddall) na Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Mahale. Pia kuna Pori la Akiba la Moyowosi ambalo makao yake makuu yapo katika kijiji cha Kifura, Wilaya ya Kibondo. Utawala Kuna wilaya nane ambazo ni (idadi ya wakazi katika mabano): Kigoma Mjini (144,852), Kigoma Vijijini (490,816), Kibondo (414,764), Kasulu (628,677), Uvinza (383,640), Buhigwe (254,342) na Kakonko (167,555) . Jumla ya wakazi ni 2.127.930 (sensa ya mwaka 2012). Makao makuu ya mkoa ni Kigoma mjini. Mji wa Ujiji ulioko karibu na Kigoma mjini ndio mji wa kale zaidi katika Tanzania ya Magharibi penye makumbusho ya David Livingstone. Mnamo Machi 2012 zimeongezwa wilaya mpya za Buhigwe, Kakonko na Uvinza. Wakazi Kadiri ya sensa ya mwaka 2022 wakazi walikuwa 2,470,967. Kabila kubwa ni Waha, likifuatwa na Wamanyema, Wabembe na Watongwe. Kuna pia Wavinza, Wanyamwezi, Wasukuma, Wafipa na watu wenye asili ya Kongo, Rwanda na Burundi. Idadi au msongamano wa watu katika maeneo ya mkoa huu imetegemea sana shughuli zinazofanyika kama vile kilimo na uvuvi pamoja na kupatikana kwa nzi aina ya ndorobo: penye ndorobo wengi huwa na watu wachache. Uchumi na mawasiliano Mkoa wa Kigoma bado hauna maendeleo yanayolingana na mazingira yake. Hali ya barabara na mawasiliano mengine ni mbaya. Umbali hadi Dar es Salaam ni km 1316, hadi Mwanza 830, hadi Arusha 1204. Ipo barabara nzuri ya lami kuanzia wilaya ya Kaliua (mkoa wa Tabora) kupitia Uvinza, Malagarasi, Nguruka, Kaziramimba hadi Kigoma mjini, isipokuwa kipande cha kilomita 400 ni cha muramu ambayo nayo inapitika vizuri kama si kipindi cha mvua nyingi za uharibifu. Usafiri muhimu ni reli kutoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora na Dodoma. Isipokuwa reli hii imeshazeeka kutokana na kujengwa zamani za Afrika ya Mashariki ya Kijerumani kabla ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Treni (gari moshi) zake huchelewachelewa kwa kuchukua muda mrefu. Wakati wa mvua inatokea ya kwamba mawasiliano yanavurugika. Uwanja wa ndege wa Kigoma unashughulika na shirika la ndege la Tanzania lenye ndege nne zinazofanya safari kwa sasa nchi nzima na usafiri ni wa uhakika, pia yapo mashirika madogo yanyofanya shughuli zake kama auric air, nyingi zikiwa za kubeba watalii.Shukrani za kipekee zimwendee Rais wa nne(Mh Jakaya Mrisho Kikwete) wa Jamhuri ya Muungano aliepigana kiume kuufungua mkoa wa kigoma kwa njia ya mawasiliano ya barabara. Takribani 85% ya wakazi wote hutegema kilimo, walio wengi kilimo cha kujitegemea tu, tena cha jembe la mkono. Kuongezeka kwa wakimbizi kutoka nchi jirani na kukua kwa makambi kulikuwa tatizo kubwa. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Buyungu : mbunge ni Bilago Samson (Chadema) Kasulu Mjini : mbunge ni Daniel Nsanzugwako (CCM) Kasulu Vijijini : mbunge ni Augustine (CCM) Kigoma Kaskazini : mbunge ni Peter Serukamba (CCM) Kigoma Kusini/Uvinza : mbunge ni Hasna Mwilima (CCM) Kigoma Mjini : mbunge ni Zitto Z. Kabwe (ACT-Wazalendo) Manyovu : mbunge ni Albert Ntabaliba (CCM) Muhambwe : mbunge ni Atashasta Justus Nditiye (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Kigoma Orodha ya mito ya mkoa wa Kigoma Marejeo Viungo vya nje Sensa ya 2002 Kigoma Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census*Serikali ya Tanzania Tanzanian Government Directory Database Mkoa wa Kigoma - Taarifa ya kijamii na kiuchumi K
2234
https://sw.wikipedia.org/wiki/Vita%20Kuu%20ya%20Kwanza%20ya%20Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia
Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ilikuwa vita iliyopigwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918. Mataifa wapiganaji yalikuwa Ujerumani, Austria-Hungaria, Bulgaria na Uturuki (ziliitwa "Mataifa ya Kati", ing. central powers) kwa upande mmoja dhidi ya Ufaransa, Urusi, Uingereza, Italia, Marekani na nchi mbalimbali zilizoshirikiana nazo (zilitwa "Mataifa ya Ushirikiano", ing. allied powers). Vita hii ilianza katika Ulaya ikapanuka haraka hadi Mashariki ya Kati. Kupitia koloni za Ujerumani ilipiganiwa pia Afrika na Asia ya Mashariki ikasababisha kifo cha takriban watu milioni tisa. Sababu na matokeo Sababu yake ilikuwa mashindano makali kati ya mataifa ya Ulaya kuhusu kushika nafasi ya kipaumbele barani Ulaya na duniani kote. Matokeo yake yalikuwa mwisho wa kipaumbele cha Ulaya duniani na kupanda ngazi kwa Marekani, mapinduzi katika nchi mbalimbali, mwisho wa falme za Ujerumani, Austria na Urusi pamoja na mwanzo wa utawala wa kikomunisti katika Urusi, mwisho wa Dola la Austria-Hungaria na wa Milki ya Osmani pamoja na mwisho wa ukoloni wa Kijerumani duniani. Katika Ulaya nchi mpya zilijitokeza kama vile Chekoslovakia, Ufini, Latvia, Estonia, na Yugoslavia pamoja na nchi za zamani zilizotokea tena katika uwanja wa kimataifa ndizo Austria, Hungaria, Lithuania na Poland. Katika Mashariki ya Kati Uturuki ilianzishwa kama nchi mpya, ilhali kipindi kifupi cha ukoloni wa Uingereza na Ufaransa kilianza huko Syria, Iraq na Lebanoni. Shirikisho la Mataifa liliundwa kama chombo cha kwanza kilicholenga kuunganisha nchi zote za Dunia na kuzuia vita mpya. Koloni za awali za Ujerumani na majimbo ya Kiarabu ya Milki ya Osmani zilidhaminiwa kwa Uingereza na Ufaransa kwa niaba ya Shirikisho, hatua iliyoweka maeneo haya chini ya uangalizi wa kimataifa, tofauti na koloni za kawaida. Hali kabla ya vita Sehemu kubwa ya Ulaya iliwahi kuwa na kipindi kirefu cha amani tangu vita kati ya Ufaransa na Ujerumani mnamo 1870-1871. Mataifa ya Ulaya yalikuwa na mfumo wa mikataba na mapatano kati yao yaliyolenga kuhakikisha uwiano wa mataifa. Mataifa makubwa ya Ulaya yalikuwa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Italia pamoja na milki ya Austria-Hungaria. Hali ilikuwa tofauti katika Kusini-Mashariki mwa bara hilo. Hadi nusu ya pili ya karne ya 19 sehemu kubwa ya Balkani ilitawaliwa na Milki ya Osmani iliyokuwa milki ya Kiislamu ya kutawala Wakristo wengi. Milki hii iliendelea kudhoofika wakati wa karne ya 19. Nchi mbalimbali zilijitenga na kupata uhuru, kama vile Ugiriki, Serbia, Bulgaria na Romania. Nchi hizi mpya zilipigana kivita kati yao na Milki ya Osmani hadi mwaka 1912. Mwanzo wa vita Vita Kuu ilianza kutokana na ugomvi kati ya Austria-Hungaria na Serbia. Kutokana na muundo wa mikataba ya kusaidiana kati ya nchi za Ulaya mwanzo huo ulisababisha mfululizo wa hali ya vita kati ya mataifa, na mengine ya Balkani yaliyotafuta uhuru wao. Tarehe 28 Juni 1914 katika mji wa Sarayevo, Bosnia, mwana wa Kaizari wa Austria aliyekuwa mfalme mteule aliuawa pamoja na mke wake na mgaidi Mserbia mwanachama wa kundi la "Mkono Mweusi" lililopinga utawala wa Austria-Hungaria katika Bosnia. Austria iliamuru Serbia ifuate masharti makali katika uchunguzi wa tendo lile. Serbia ilipokataa sehemu ya mwisho ya masharti, Austria ilitangaza hali ya vita dhidi ya Serbia tarehe 28 Julai 1914. Agosti ya 1914 iliona kupanuka kwa vita hiyo: Warusi walikuwa na mkataba wa usaidizi na Serbia wakatangaza hali ya vita dhidi ya Austria-Hungaria. Hapo wakaingia Wajerumani waliokuwa na mapatano ya usaidizi na Austria-Hungaria wakitangaza hali ya vita dhidi ya Urusi. Urusi kwa upande wake ulikuwa na mkataba wa kusaidiana na Ufaransa, kwa hivyo hali ya vita ikajitokeza pia kati ya Ufaransa na Ujerumani. Ujerumani ilishambulia Ufaransa kwa kuingia Ubelgiji na kupigana na jeshi la nchi hiyo. Mashambulio hayo yalisababisha Uingereza kujiunga na vita dhidi ya Ujerumani. Japan iliyokuwa na mkataba wa kusaidana na Uingereza tangu mwaka 1902 iliona nafasi ya kukamata koloni za Ujerumani katika Bahari Pasifiki ikaingia upande wa maadui wa Ujerumani. Kuanzia Oktoba 1914 Milki ya Osmani (Uturuki) ilijiunga na vita kufuatana na mkataba wake wa siri na Ujerumani. Mwaka 1915 Italia ilijiunga na Wafaransa na Waingereza kwa kushambulia Austria-Hungaria iliyotawala bado maeneo katika kaskazini ya rasi ya Italia, ingawa awali ilikuwa na mkataba na dola hilo. Vita katika nchi mbalimbali Vita ilipigwa kwa ukali miaka ya 1914-1918. Wajerumani waliingia ndani ya Ufaransa lakini walikwama kabla ya kufikia jiji kuu la Paris. Kwa muda mrefu mstari wa mapambano ulibaki palepale. Katika Mashariki Wajerumani na Waaustria walifaulu kurudisha mashambulio ya Kirusi na kuteka sehemu za Urusi. Katika Kusini mwa Ulaya Waustria walifaulu kwa shida kubwa kuteka Serbia na Montenegro pamoja na Albania. Mapigano dhidi ya Italia yalikwama kwenye milima ya Alpi. Waosmani walishindwa kwa ujumla katika mashambulio yao dhidi ya Warusi katika eneo la Kaukazi na dhidi ya Waingereza katika Misri. Lakini walifaulu kuzuia Waingereza wasifike Uturuki penyewe. Waingereza walipeleka jeshi katika Irak ya kusini wakafaulu kuwarudisha Waosmani hadi kaskazini ya nchi hii. Vita katika koloni Tazama makala kuu: Vita Kuu ya Kwanza katika Afrika ya Mashariki Vita ilienea haraka baharini na katika koloni za Ujerumani zilizovamiwa na Waingereza, Wafaransa, Afrika Kusini na Japani. Koloni hizo zilikuwepo Afrika na kwenye visiwa vya Pasifiki pamoja na China. Ujerumani ilikuwa na vikosi vya kijeshi katika koloni za Afrika na pia huko Qingdao nchini China. Kwa ujumla koloni zote zisizokuwa na jeshi zilitekwa na mataifa ya ushirikiano bila mapigano. Afrika ya Kusini-Magharibi ya Kijerumani ilivamiwa na Afrika Kusini na jeshi la ulinzi la Kijerumani likajisalimisha mnamo Julai 1915. Kamerun ilivamiwa na Ufaransa na Uingereza kutoka koloni zao za Nigeria na Afrika ya Kati ya Kifaransa. Wajerumani wakajisalimisha katika Februari 1916. Afrika ya Mashariki ya Kijerumani ilikuwa mahali pa mapigano yaliyoendelea kwa miaka yote ya vita. Jeshi la Ulinzi la Kijerumani lililoitwa Schutztruppe chini ya uongozi wa Paul von Lettow-Vorbeck lilifaulu kutetea eneo la koloni dhidi ya mashambulio ya kwanza ya Waingereza kutoka Kenya hadi 1916. Kwenye Novemba 1914 jeshi la askari 8,000 kutoka Uhindi lilishindwa kwenye mapigano ya Tanga. Hadi mwanzo wa 1916 Waingereza walikusanya jeshi kubwa kutoka Afrika Kusini na Uhindi wakafaulu kutwaa sehemu kubwa ya koloni hadi Agosti 1916. Jeshi la Schutztruppe likaendelea kushika sehemu ya kusini ya koloni hadi 1917 ilipopaswa kuhamia eneo la Kireno katika Msumbiji. Waingereza na Wareno walishindwa kulishika kundi la Kijerumani. Mwaka 1918 Lettow-Vorbeck alirudi Tanganyika akaingia Rhodesia ya Kaskazini alipoambiwa na Waingereza mnamo Novemba 1918 ya kwamba vita ya Ulaya ilikwisha tayari. Mwisho wa vita Wakati 1917 mataifa ya Ulaya yalionyesha dalili za uchovu. Katika hali hiyo mabadiliko mawili makubwa yalitokea: Marekani ilijiunga na vita dhidi ya Wajerumani na Urusi ilikuwa na mapinduzi yaliyolazimisha serikali mpya kutia sahihi mapatano ya kumaliza vita dhidi ya Ujerumani iliyoteka maeneo makubwa ya Urusi. Nguvu ya Marekani ilionekana haraka na bahati ya Ujerumani ilipungua sana. Austria-Hungaria ilidhoofishwa vilevile. Mwaka 1918 iliona mwisho wa vita. Jeshi la Kiosmani lilishindwa hadi serikali ya milki kuomba kusimamishwa kwa vita. Mataifa ya ushirikiano yalikaribia mipaka ya Ujerumani na hapo mgomo wa wanamaji ilifuatwa na migomo ya wafanyakazi katika viwanda vikubwa iliyosababisha mapinduzi yaliyoangusha serikali ya Kaisari Wilhelm II. Migomo ya wanajeshi ililazimisha Austria-Hungaria kuomba kusimamisha vita. Milki za Austria na Uturuki zilikwisha zikagawiwa na sehemu zao zilikuwa nchi mpya au nchi zilizoundwa upya. Mkutano wa Paris Mwaka 1919 mataifa washindi walikutana Paris (Ufaransa) wakikubaliana masharti ya kumaliza hali ya vita dhidi ya Mataifa ya Kati. Mikataba mbalimbali iliandaliwa kati ya washindi na kuwekwa mbele ya nchi zilizoshindwa. Mikataba hii ilikuwa: Mkataba wa Versailles na Ujerumani (28 Juni 1919), Mkataba wa Saint-Germain na Austria (10 Septemba 1919), Mkataba wa Neuilly na Bulgaria (27 Novemba 1919), Mkataba wa Trianon na Hungaria (4 Juni 1920), Mkataba wa Sèvres na Milki ya Osmani (Uturuki) (10 Agosti 1920; ukasahihishwa na mkataba wa Lausanne (24 Julai 1923). Mkutano wa Paris ulitoa masharti makali dhidi ya Ujerumani katika Mkataba wa Versailles. Ujerumani uliondolowa makoloni yote yaliyokabidhiwa kwa niaba ya Shirikisho la Mataifa kama maeneo ya kukabidhiwa kwa Uingereza, Ufaransa, Ubelgiji, Japani, Afrika Kusini na Australia. Mkutano wa Paris ulikuwa jaribio la kuunda utaratibu mpya duniani uliotakiwa kulindwa na Shirikisho la Mataifa. Lakini ukosefu wa nguvu kwa upande wa Shirikisho la Mataifa pamoja na kuanza na kupanuka kwa mwendo mpya wa Kifashisti iliyochukua utawala katika Italia na Ujerumani vilishinda nia hiyo. Wataalamu wasio wachache wanasema mwisho wa vita kuu ya kwanza ulipanda tayari mbegu za Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ni kwamba Wajerumani na wakazi wa nchi nyingine zilizoshindwa walijiona wamekosewa haki, lakini pia Waitalia walioshinda kwa gharama kubwa ya damu walijiona wamedanganywa kwa kutotimiziwa ahadi walizopewa ili wasaliti Ujerumani na Austria-Hungaria na kuingia vitani upande wa pili. Hivyo vyama vya mrengo wa kulia viliweza kupata nguvu na hatimaye kupanga kisasi. Vita ya kwanza ya Dunia? Vita hii ilitwa "Vita ya Dunia" kwa sababu mapigano yalisambaa kote duniani. Sehemu kubwa ya mapigano yalitokea Ulaya na Asia ya Magharibi lakini pia katika makoloni ya Afrika, Asia na Pasifiki. Nchi za Amerika hazikuona mapigano kwenye nchi kavu lakini manowari za Ujerumani zilipigana na mataifa ya ushirikiano mbele ya pwani za Marekani na Amerika Kusini. Ilikuwa pia vita ya kwanza iliyopigwa kote duniani ilhali habari zake ziliweza kufika katika muda wa masaa au siku chache kwa mataifa yote kutokana na upatikanaji wa vyombo vya mawasiliano hasa simu za kimataifa na redio. Lakini kwa kweli haikuwa vita ya kwanza ya "Dunia" maana vita ya miaka saba (1756-1762) ilipigwa tayari kwenye mabara yote ya Dunia baina ya nchi zenye koloni, hasa Uingereza, Ufaransa na Hispania. Tazama pia Kampeni za Kivita katika Afrika ya Mashariki (Vita ya Kwanza ya Dunia) Tanbihi Marejeo (translated from the German) , reviewed in (via Highbeam.com) Encyclopaedia Britannica (12th ed. 1922) comprises the 11th edition plus three new volumes 30-31-32 that cover events since 1911 with very thorough coverage of the war as well as every country and colony. partly online and list of article titles full text of vol 30 ABBE to ENGLISH HISTORY online free scans of each page of vol 30-31-32 {{citation|last=Grant|first=R.G.|title=Battle: A Visual Journey Through 5,000 Years of Combat|publisher=DK Publishing|year=2005|isbn=978-0-7566-5578-5}} , Wilson's maneuvering US into war , general military history also published by Harper as "Ludendorff's Own Story, August 1914 – November 1918: The Great War from the Siege of Liège to the Signing of the Armistice as Viewed from the Grand Headquarters of the German Army" (original title Meine Kriegserinnerungen, 1914–1918) cites "Cf. articles signed XXX in La Revue de Deux Mondes'', 1 and 15 March 1920" Deals with technical developments, including the first dipping hydrophones Viungo vya nje A multimedia history of World War I The Heritage of the Great War/ First World War. Graphic color photos, pictures and music, Netherlands The World War I Document Archive Wiki, Brigham Young University Maps of Europe covering the history of World War I at omniatlas.com Your Family History of World War I – Europeana 1914–1918(Crowd-sourcing project) EFG1914 – Film digitisation project on First World War WWI Films on the European Film Gateway World War I British press photograph collection – A sampling of images distributed by the British government during the war to diplomats overseas, from the UBC Library Digital Collections The British Pathé WW1 Film Archive Ramani hai An animated map "Europe plunges into war" An animated map of Europe at the end of the war Vita Historia ya Ulaya Historia
2235
https://sw.wikipedia.org/wiki/R%C3%A9union
Réunion
Réunion (kwa Kifaransa: La Réunion) ni kisiwa cha Afrika na mkoa wa ng'ambo wa Ufaransa (kwa Kifaransa: département d'outre-mer, au DOM) katika Bahari Hindi. Kisheria hali yake ni sawa na mikoa mingine ya Ufaransa hivyo ni pia sehemu ya Umoja wa Ulaya. Eneo lake Reunion iko km 800 upande wa mashariki wa Madagaska. Pamoja na visiwa vya Mauritius na Rodrigues inaunda funguvisiwa la Maskareni. Kisiwa kina eneo la km² 2.512 kikiwa na kipenyo cha km 50 hadi 70. Milima mikubwa ni ya kivolkeno. Upande wa mashariki wa kisiwa ndipo mlima wa "Piton de la Fournaise" wenye urefu wa mita 2611 uliolipuka zaidi ya mara 100 tangu kumbukumbu ya kimaandishi ilipoanzishwa mwaka 1640. Mlipuko wa mwisho hadi leo ulitokea tarehe 4 Oktoba 2005. Mlima wa "Piton des Neiges" ndio mkubwa kisiwani ikiwa na 3070 m juu ya UB. Hali ya hewa Hali ya hewa ni ya joto mwaka wote. Majira ya mvua ndiyo kati ya Desemba hadi Machi. Historia na Utawala Taarifa za kwanza za kimaandishi hudokeza kwamba kisiwa kilikuwa bila ya wakazi. Waarabu waliita "dina margabin" yaani kisiwa cha magharibi. Baharia Mreno Diego Dias alifika tarehe 9 Februari 1513 ambayo ni sikukuu ya Mt. Apolonia katika mapokeo ya Kanisa Katoliki na kukiita kisiwa kwa jina la mtakatifu huyu "Santa Apolonia", jinsi inavyoonekana katika ramani za kwanza. Baadaye Wareno walitumia jina la nahodha maarufu Pedro de Mascarenhas na kujumlisha visiwa vya Reunion, Mauritius na Rodrigues kwa jina la visiwa vya Maskareni. Visiwa hivyo vilikuwa na umuhimu fulani kama vituo vya kupumzika katika safari kati ya Ulaya na Bara Hindi, mabaharia wakitafuta maji ya kunywa, nafasi ya kutengeneza jahazi zao na kuongeza chakula. Lakini hapakuwa na makao ya kudumu kisiwani. Utawala wa Kifaransa Mwaka 1640 Wafaransa walivamia kisiwa na kukitangaza kuwa mali ya Ufaransa. Walikiita "Île Bourbon" kutokana na jina la familia ya wafalme wa Ufaransa. Mwaka 1665 walowezi wa kwanza Wafaransa walianza kujenga nyumba zao. Ufalme ulipoondolewa wakati wa mapinduzi ya Ufaransa kisiwa kimepewa jina jipya la Reunion tarehe 17 Machi 1793. Wakati wa vita vya Napoleoni, Waingereza walivamia kisiwa mwaka 1810 lakini wakakirudisha kwa Wafaransa baada ya vita (1815). Uchumi wa mashamba na watumwa Walowezi Wazungu walianzisha mashamba kwa ajili ya mahitaji ya jahazi zilizopita. Kuanzia mwaka 1718 mazao ya biashara yalilimwa, kwanza kahawa baadaye pia vanilla na hasa sukari. Kwa kusudi hilo watumwa walipelekwa Reunion kutoka Afrika bara, Bara Hindi na Madagaska. Mwaka 1768 kisiwa kilikuwa na wakazi huru 26,284 (hasa Wafaransa) na watumwa 45,000. Ufaransa ulitia sahihi maazimio ya Mkutano wa Vienna mwaka 1815 pamoja na kumaliza biashara ya watumwa lakini biashara hii iliendelea kwa siri na kupanuka hasa kwa wafungwa kutoka Afrika. Idadi ya watumwa iliendela kuongezeka hadi kuondolewa hali ya utumwa tarehe 20 Desemba 1848. Baada ya mwisho wa utumwa walowezi walitafuta wafanyakazi huko Bara Hindi wakachukua Wahindi wasiofika kama watu huru kwa miaka na haki kidogo. Baadaye hata wafanyakazi Wachina walichukuliwa. Mkoa wa Ufaransa Mwaka 1946 Reunion ilipewa cheo cha Mkoa wa Ufaransa, na tangu 1997 imekuwa sehemu ya Umoja wa Ulaya. Mkoa wa Reunion ina wilaya (Kifaransa: arrondissements) nne. Wakazi Wakazi wanaonyesha historia hii katika mchanganyiko wao wa aina za watu na tamaduni kutoka pande mbalimbali wa dunia. Sehemu kubwa ya wakazi ni wajukuu wa watumwa au wafanyakazi wasio huru wa zamani wakionyesha tabia za Wahindi, Waafrika na Wachina. Takriban robo ya wakazi ni wa asili ya Ulaya. Kuna lugha tatu tu ambazo huzungumzwa na wakazi wa Réunion, yaani Kifaransa (lugha rasmi), Kitamil na krioli inayotokana na Kifaransa. Pia kuna wahamiaji kutoka visiwa vya jirani ambao huzungumza lugha za Kichina na za Komori, kama vile Kimaore, Kimwali, Kindzwani na Kingazidja. Vikundi hivi havikai mbali: kuna mchanganyiko wa kila aina. Wakazi wengi hufuata Ukristo wa Kikatoliki, wengine Uislamu na Uhindu. Kuna pia Waprotestanti. Tazama pia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Viungo vya nje Visiwa vya Bahari ya Hindi Visiwa vya Afrika Eneo la ng'ambo la Ufaransa Mikoa ya Ufaransa
2236
https://sw.wikipedia.org/wiki/Agostino%20wa%20Hippo
Agostino wa Hippo
Agostino wa Hippo (Thagaste, leo Souk Ahras nchini Algeria, 13 Novemba 354 – Hippo, leo Annaba, Algeria, 28 Agosti, 430) alikuwa mtawa, mwanateolojia, padri na hatimaye askofu mkuu wa Hippo. Ndiye kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki katika Afrika Kaskazini mwanzoni mwa karne ya 5. Kutokana na maisha, mafundisho na maandiko yake bora, tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa. Mwaka 1298 Papa Bonifasi VIII alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia. Maisha yake Asili Katika sehemu za magharibi za Afrika ya Kaskazini wenyeji walikuwa Waberberi kama mama yake, lakini watu wa mjini, kama baba yake, na wenye mashamba makubwa walikuwa wa asili ya Ulaya wakitumia hasa lugha ya Kilatini. Kwa jumla sehemu hii ya Afrika ilikuwa karibu na utamaduni wa Ulaya ya Magharibi. Mama yake (Monika, anayeheshimiwa kama mtakatifu) alikuwa Mkristo, kumbe baba (Patrisi) alifuata dini ya jadi ya kuabudu miungu mingi kabla hajabatizwa mwishoni mwa maisha yake. Utoto Agostino alizaliwa tarehe 13 Novemba 354 mjini Thagaste katika mkoa wa Numidia. Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Aurelius Augustinus. Wakati ule Ukristo ulikuwa tayari dini iliyokubaliwa katika Dola la Roma; dhuluma dhidi ya Wakristo zilikuwa zimekwisha rasmi mwaka 313 kwa Hati ya Milano iliyotolewa na Konstantino Mkuu ili kuruhusu uhuru wa dini. Alikuwa na wadogo wawili, mmoja mwanamume, Naviji, na mwingine wa kike, ambaye hatujui jina lake, ila kwamba baada ya kufiwa mume wake akawa mmonaki na abesi. Monika alimuathiri sana Augustino na kumlea katika imani ya Kikristo. Mwanae aliweza kuandika kwamba alipokuwa ananyonya maziwa ya mama, alifyonza pia upendo kwa jina la Yesu. Akiwa mtoto alipokea chumvi kama ishara ya kuingia ukatekumeni akabaki daima anavutiwa na Yesu, hata alipozidi kusogea mbali na Kanisa lake. Ujana Wakati wote wa ujana wake alifuata anasa na uzushi, bila kujali machozi ya mama yake. Alipata elimu yake nzuri ya lugha na ya ufasaha wa kuhubiri huko Thagaste, Madaura na hata katika Chuo Kikuu cha Karthago (karibu na Tunis) ingawa hakuwa daima mwanafunzi mzuri, mbali ya kuwa na akili ya pekee. Alimudu kikamilifu Kilatini, lakini si sana Kigiriki. Akiwa huko Karthago, mwaka 373 alisoma kitabu cha maadili cha Sisero ambacho kilibadilisha hisia zake hivi kwamba “matumaini yote ya bure yakawa hayana maana kwangu, nikatamani hekima isiyokufa kwa ari isiyosemeka moyoni mwangu”. Lakini kwa kuamini ukweli haupatikani pasipo Yesu, ambaye hatajwi katika kitabu hicho, alianza kusoma Biblia, ila hakupenda tafsiri ya Kilatini wala yaliyomo, akiyaona tofauti na mtindo wa falsafa inayotafuta ukweli. Hivyo alisogea mbali na dini iliyoonekana kutotia maanani hoja za akili ambayo pamoja na imani ndizo “nguvu mbili zinazotuongoza kwenye ujuzi”. Ndivyo alivyoandika baadaye, akitoa pia kauli mbili za msingi kuhusu kulenga ukweli: “Usadiki ili uelewe”, halafu “uelewe ili usadiki”. Hapo, kusudi asiishi bila Mungu, alijitafutia dini ya kuridhisha hamu yake ya kujua ukweli na ya kuwa karibu na Yesu, akajiunga kwa karibu miaka 10 na Umani. Dini hiyo ilidai kufuata akili na kufafanua sababu ya mabaya kuwepo duniani kutokana na chanzo cha pili cha ulimwengu kilicho kinyume cha Mungu, ikikataa Agano la Kale ili kufuata Ukristo wa kiroho. Augustino alipenda pia maadili ya dini hiyo kwa sababu yalikuwa yanawadai sana baadhi ya waumini tu, yakiwaacha wengine wote wasijali zaidi. Hatimaye Wamani walikuwa wanasaidiana kupanda chati katika jamii. Lakini alipokutana na askofu wao Fausto, alikosa imani nao kwa kuona alivyoshindwa kujibu maswali yake. Kazi baada ya masomo Baada ya kuhitimu masomo, alifundisha Kilatini huko Thagaste (374), halafu namna ya kuhubiri huko Kartago (375-383), akaendelea kufanya hivyo nchini Italia, kwanza Roma (384), halafu Milano (384-386), makao makuu ya Dola, alipopata kazi ya heshima sana. Wakati huo wote aliendelea kuishi bila ndoa na mwanamke aliyemzalia mtoto wa kiume mwenye akili sana, Adeodatus. Akiwa Milano alikutana na watu, hasa Ambrosi askofu wa Milano, waliomvuta awe Mkristo Mkatoliki. Mahubiri bora ya Ambrosi aliyokwenda kuyasikiliza kwanza ili kuzidi kupata mbinu za kutoa hotuba, yalizidi kumgusa moyoni na kumfanya asadiki mamlaka ya Biblia nzima inavyosomwa rasmi na Kanisa. Aliona uzuri na udhati wa masimulizi ya Agano la Kale yakifafanuliwa kiroho kama mifano ya mambo ya Agano Jipya inayomuelekea Kristo, kiini cha yote. Katika barua za Mtume Paulo, Augustino alimtambua Kristo kama mwokozi, si mwalimu tu. Hasa aliguswa na maneno ya Rom 13:13-14 aliyoyasoma kwa kufungua tu kitabu kisha kumsikia mtoto wa jirani akiimba kwa kukariri, “Chukua usome, chukua usome”. Alitambua ameambiwa mwenyewe na Mungu maneno hayo yakimdai aachane na matendo ya mwili akamvae Kristo. Wongofu na ubatizo Kisha kuongoka hivyo tarehe 15 Agosti 386, akiwa na umri wa miaka 32, aliacha kufundisha na hata kuishi na mama mtoto, akatawa kwa muda Cassiciaco karibu na ziwa la Como, akiwa na Monika, Adeodatus na marafiki wachache, akarudi Milano alipobatizwa na Ambrosi pamoja na mwanae na rafiki yake Alipio usiku wa Pasaka ya mwaka 387. Mmonaki Baada ya kubatizwa na kunuia akaishi kitawa Thagaste, alirudi Afrika; njiani, huko Ostia, bandari ya Roma, alifiwa mamaye. Ndoto yake ilikuwa kujitosa katika maisha ya sala na masomo pamoja na marafiki wake. Lakini hiyo ilidumu miaka mitatu tu. Padri na askofu Mwaka 391 bila kutarajia alipewa daraja ya upadri huko Hippo, alipoanzisha monasteri, akigawa muda wake kati ya sala, masomo na mahubiri, halafu mwaka 395 akachaguliwa kuwa askofu msaidizi wa mji huo na mwaka 397 akawa askofu wa jimbo hilo. Ilimbidi akubali matakwa ya Mungu kwake, kwamba ajitoe kwa wengine na kuwashirikisha ujuzi wake ili kuishi kweli kwa ajili ya Kristo. “Kuhubiri mfululizo, kujadili, kusisitiza, kujenga, kuwa tayari kwa yeyote ni jukumu kubwa sana, ni mzigo mzito, ni juhudi ya ajabu”. Ilikuwa kama wongofu wake wa pili. Hapo alitegemeza maskini na mayatima, alisimamia malezi ya wakleri, akiwadai waishi pamoja, akaeneza monasteri za kiume na za kike. Alifanya adhimisho la ekaristi kuwa kiini cha maisha ya jumuia zake. Mahubiri yake mengi yanaonyesha alivyojua kujadiliana na umati akitumia maneno rahisi na ya kawaida na hata ucheshi katika kulinganisha Neno la Mungu na mazingira yao. Kwa tabia yake karimu na pendevu, hisia zake, uvumilivu na utayari wa kusamehe alifanya hata maadui kadhaa kuwa marafiki. Maisha yake ya Kiroho yaliyoongoza uandishi wa kanuni yake kwa watawa yamefuatwa na mashirika mengi ya kiume na ya kike hadi leo. Kwa miaka 35 mpaka kifo chake, mbali na kutimiza majukumu yake mengi, aliendelea kueleza na kutetea imani sahihi ya Kikristo kwa mahubiri, maandishi na vitabu vingi sana (hata vya mitindo mipya) dhidi ya aina zote za uzushi za wakati ule: Wamani, Wadonati, Wapelaji na Waario. Hivyo tangu alipokuwa hai, hakuongoza Kanisa la Afrika Kaskazini tu, bali alitegemeza imani kila mahali. Kwa njia hiyo amekuwa mwalimu muhimu sana katika Ukristo, hasa wa Magharibi (yaani Kanisa Katoliki na katika Uprotestanti uliotokea katika Kanisa hilo. Kwa mfano Martin Luther alimtaja kuwa baba yake wa kiroho pamoja na Mtume Paulo). Augustino alijilisha tunu za Kikristo na kutokeza utajiri wake wa dhati, akibuni mawazo na mifumo ya kulisha vizazi vijavyo. Hata nakala za vitabu vyake ni nyingi sana, zikithibitisha vilivyopendwa na kuenea. Hivyo aliathiri sana ustaarabu wa Magharibi unaozidi kuenea leo duniani kote. Mawazo yote yaliyomtangulia yanakutana katika maandishi yake na kuwa chemchemi ya mafundisho kwa nyakati zilizofuata. Miaka ya mwisho Tarehe 26 Septemba 426 alikusanya waamini ili kuwatambulisha padri Eraklio aliyemchagua kama mwandamizi wake naye aweze kutumia miaka yake ya mwisho katika kusoma kwa dhati zaidi Maandiko matakatifu. Watu walimkubalia kwa shangwe. Miaka minne iliyofuata Augustino alifanya kazi kubwa kwa kumaliza vitabu mbalimbali na kuanza kuandika vingine. Kati ya vile vya wakati huo kuna “Retractationes” (yaani “Kupitia Upya” vile vilivyotangulia), ambamo tunaona unyofu wake kwa kuwa tayari kurekebisha baadhi ya mafundisho aliyowahi kuyatoa. Hivyo mpaka mwisho alionyesha alivyolenga ukweli kuliko yote. Pia miaka hiyo alijadiliana na wazushi hadharani na kurudisha amani iliyohatarishwa na makabila ya kusini yakifaidika na matatizo kati ya Kaisari na jemadari wake Bonifasi. Alimuandikia mpatanishi: “Ni utukufu mkubwa zaidi kuzuia vita vyenyewe kwa neno moja, kuliko kuangamiza watu kwa upanga, na vilevile kusababisha au kudumisha amani kwa amani kuliko kwa vita. Kwa sababu wanaopigana, ikiwa ni watu wema, bila shaka wanalenga amani, ila kupitia damu. Kumbe kazi yako ni kuzuia umwagaji damu”. Hata hivyo, tumaini lilitoweka Bonifasi alipoalika kwa hasira washenzi wa Kijerumani walioitwa Wavandali kutoka Hispania wavamie Afrika. Agostino aliaga dunia akiwa Hippo tarehe 28 Agosti 430, wakati Wavandali walipokaribia kuteka mji wake baada ya kuuzingira miezi mitatu, huku wakibomoa makanisa na nyumba za vijijini na kuua au kukimbiza wakazi, wakiwemo watawa. Baadhi waliteswa na kuchinjwa, wengine walibakwa au kufanywa watumwa. Mbele ya maovu hayo yaliyokomesha ustaarabu wa Kirumi, Augustino alizidi kutafakari fumbo la Maongozi ya Mungu ili kujifariji na kuwatuliza wengine kama alivyofanya miaka 20 ya nyuma, Roma ilipotekwa kwa mara ya kwanza na Wagoti. Aliona ustaarabu huo ulikuwa umechakaa, kumbe Kristo tu hazeeki kamwe na ni wa kutegemewa. Hapo awali, alidhani mtu akiongoka na kubatizwa atafikia kwa urahisi ukamilifu unaoelekezwa na Hotuba ya Mlimani. Miaka ya mwisho alikiri kwamba Yesu tu alitekeleza sawasawa hotuba yake hiyo. Waamini wanahitaji daima kuongoka na kutakaswa naye ili kufanywa wapya. “Nimeelewa kwamba mmoja tu ni mkamilifu kweli… Kumbe Kanisa lote - sisi sote, tukiwa pamoja na Mitume - tunapaswa kusali kila siku: ‘Utusamehe dhambi zetu kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea’”. Ndio wongofu wake wa tatu, uliomfanya amalizie maisha yake kwa unyenyekevu wa hali ya juu. Katika ugonjwa wa mwisho aliomba Zaburi za toba ziandikwe kwa herufi kubwa na kubandikwa ukutani aweze kuzisoma kutoka kitandani huku akijiaminisha kwa Mungu kwa machozi mengi usiku na mchana. Ili kujiandaa zaidi kufa, siku 10 za mwisho hakuruhusu mtu kumtembelea, ila waliomletea chakula na dawa. Kazi na mafundisho yake Katika historia yote Augustino ni kati ya watu wenye akili kubwa zaidi, iliyopenya masuala yoyote, pamoja na ubunifu wa ajabu na moyo mpana. Aliunda upya teolojia ya mapokeo akiitia chapa yake mwenyewe. Kati ya mababu wa Kanisa, ndiye aliyetuachia maandishi mengi zaidi, kuanzia yale maarufu sana yanayoitwa "Maungamo", kwa kuwa humo miaka 397-400 aliungama sifa za Mungu na ukosefu wake mwenyewe kwa kusimulia alivyoishi hadi miaka ya kwanza baada ya kuongoka. Kila wakati ulifurahia zaidi kitu fulani katika Augustino. Siku hizi anapendwa hasa kwa unyofu wake katika kujichunguza na kutoa siri zake, akikiri makosa yake na kuyageuza yawe sifa kwa Mungu. Uzingatifu wake wa fumbo la nafsi yake ambamo fumbo la Mungu limefichama, ni mzuri ajabu kiasi cha kubaki hata leo kilele cha kujitafiti kiroho. Aliandika: “Usiende nje, rudi ndani mwako; ukweli unakaa katika utu wa ndani; na ukiona umbile lako ni geugeu, panda juu yako. Lakini kumbuka, unapopanda juu yako, unapanda juu ya roho inayofikiri. Basi, ufikie pale mwanga wa akili unapowaka”. Tena: “Naona ni lazima wanadamu warudishiwe tumaini la kupata ukweli”. Posidi, mtu wa kwanza kuandika habari za maisha ya Augustino (kwa Kilatini, “Vita Augustini”), alisema “waamini wanamkuta daima hai” katika vitabu vyake. Kweli havionyeshi imepita miaka 1600 tangu viandikwe: humo anaonekana kama rafiki yetu wa wakati huu anayesema nasi kwa imani isiyozeeka. Augustino mwenyewe aliviorodhesha 1,030, ambavyo si vyote. Kazi yake kubwa haikuwa kuandika maelezo juu ya vitabu na maneno ya Biblia yenyewe alivyofanya Origene, bali kuingiza Biblia katika mazingira ya kiroho, ya kijamii na ya kisiasa ya wakati wake. Hapo, akitegemea mamlaka ya imani inayodhihirishwa na Biblia, maandiko ya Kimungu yasiyoweza kukosea yakisomwa katika mapokeo ya Kanisa lililoorodhesha vitabu vinavyoiunda, aliuliza maswali na kutoa majibu yaliyo muhimu mpaka leo. Akilinganisha imani na akili, Augustino alichunguza hasa fumbo la Mungu (Ukweli mkuu na Upendo wa milele, unaohitajiwa na roho ili kupata amani) na la binadamu (ambaye ni sura na mfano wa Mungu). Huyo katika roho yake isiyokufa, bado ana uwezo wa kuinuka hadi kwa Mungu, ingawa uwezo huo umeharibiwa na dhambi na unahitaji kabisa kurekebishwa na neema. Teolojia yake kuhusu Utatu inaendeleza ile ya mapokeo na kuathiri Kanisa lote la Magharibi. Augustino anaweka wazi kuwa Nafsi tatu ni sawa lakini hazichanganyikani; tena anajaribu kuufafanua Utatu kwa kutumia saikolojia (mfano wa kumbukumbu, akili na utashi). Kitabu muhimu zaidi kuhusu Utatu (kwa Kilatini kinaitwa “De Trinitate”) alikiandika miaka 399-420. Kilichukua muda mrefu kwa kuwa alisimamisha uandishi wake miaka minane “kwa sababu ni kigumu mno na nadhani wachache tu wanaweza kukielewa; basi kuna haraka zaidi ya kuwa na vitabu vingine tunavyotumaini vitafaidisha wengi”. Hivyo alielekeza nguvu zake kutunga vitabu vya katekesi kwa wasio na elimu (hasa “De Catechizandis Rudibus”). Akijibu hoja za Wadonati, ambao walitaka Kanisa la Kiafrika na kuchukia mambo ya Kilatini, alikubali kurahisisha lugha hata kufanya makosa ya kisarufi kusudi wamuelewe zaidi akifafanua umoja wa Kanisa ulivyo muhimu kwa mahusiano na Mungu na kwa amani duniani. Hasa hotuba zake, zilizoandikwa na wengine wakati alipokuwa anazitoa kwa watu akiongea nao kirahisi, zimechangia kueneza ujumbe wake. Tunazo bado karibu 600, lakini zilikuwa zaidi ya 3,000. Pia alifafanua upya imani kuhusu umwilisho wa Mwana wa Mungu, akiwahi kutumia misamiati iliyokuja kupitishwa na Mtaguso wa Kalsedonia (451): uwepo wa hali mbili (ya Kimungu na ya kibinadamu) katika nafsi moja. Lengo la umwilisho lilikuwa wokovu wa watu, hivyo hakuna anayeweza kuokoka bila Kristo aliyejitoa sadaka kwa Baba, “akitakasa, akifuta na kutangua makosa yote ya binadamu, akiwakomboa kutoka mamlaka ya shetani”. Dhambi na neema Katika suala la neema na dhambi ni Agostino aliyefundisha kwamba ubinadamu umerithi dhambi ya asili kutoka kwa Adamu. Uhuru wa asili umepotezwa na dhambi hiyo, na hali hii imerithiwa na watu wote baadaye. Lakini kwa neema yake Mungu hufunua upendo wake kwao. Alisisitiza kwamba si binadamu anayemtafuta Mungu, bali Mungu ndiye anayemhurumia mwanadamu mwenye dhambi. Utakaso unaopatikana kwa imani unasababisha ondoleo kamili la dhambi zote kabisa. Halafu mwamini anazidi kufanywa mpya kwa mchakato utakaokamilishwa na ufufuko wa siku ya mwisho. Mchakato huo wote ni kazi ya neema ya Mungu: bila hiyo, binadamu hawezi kuongoka, kukwepa dhambi na kufikia utimilifu wa wokovu. Hayo yote ni zawadi tu ya Mungu, kama vilivyo pia udumifu na stahili za mtu. Sisitizo hilo la kwamba neema ni dezo, lilimuongoza Augustino kufundisha juu ya uteule, neema ambayo hakuna anayeweza kuikataa na ambayo inafikisha kwa hakika mbinguni. Kwa nini Mungu hawapi wote neema hiyo ni fumbo ambalo tuliinamie tu, kwa sababu hatuwezi kabisa kulielewa. Kwa vyovyote haiwezekani kumlaumu Mungu kwa ajili hiyo, eti si haki. Mawazo hayo yalikuja kukaziwa zaidi tena na watu kama Martin Luther, Yohane Kalvini na Janseni, namna iliyokataliwa na Kanisa Katoliki. Mji wa Mungu Juu ya uhusiano kati ya serikali na kanisa Augustino katika miaka 413-426 aliandika kitabu "De Civitate Dei" (maana yake kwa Kilatini ni: Mji wa Mungu. Badala ya "mji" tungeweza kutafsiri pia: "eneo au kikundi cha watu au utawala"). Alieleza kwamba iko "miji" miwili: mji wa Mungu (yaani Yerusalemu wa mbinguni, au Kanisa) na mji wa dunia hii, yaani taratibu za kisiasa. Katika "mji wa dunia hii" hali hubadilika. Hakuna taratibu za kudumu. Agostino alifahamu taratibu za Waroma Wapagani waliotazama Makaisari wao kuwa miungu, na vilevile habari za demokrasia ya Kigiriki ya kale. Akafahamu habari za mji mkubwa wa Roma ulioitwa "mji wa milele" lakini ulichomwa moto na maadui katika siku zake jinsi ilivyoanguka zamani miji ya Babeli na Yerusalemu. Pamoja na "mji" huo alisema upo "mji" wa pili ndio mji wa Mungu ambao ni mji wa upendo na undugu wenye neema yake. Miji yote miwili iko pamoja ingawa zina taratibu tofauti. Mkristo ni raia wa miji yote miwili. Huitwa kuwa mwaminifu pande zote mbili. Lakini ajue kwamba mji wa dunia hii hauna shabaha ya kudumu. Umeingiliwa na dhambi. Kumbe mji wa Mungu utadumu. Umepewa lengo la kudumu, unashiriki enzi ya Mungu. Ndiyo sababu inafaa serikali isikie mawazo ya Kanisa, kwani ni kwa njia ya Kanisa kwamba Mungu ameamua kufunua mapenzi yake. Mkristo anaweza kushiriki katika taratibu za kisiasa akijua ya kwamba mawazo na mipango yote ya siasa havidumu. Utakaodumu ni utaratibu wa Mungu tu. Ni kutokana na mafundisho hayo pia kwamba Kanisa la Magharibi lilijifunza umuhimu wa kuwa na msimamo imara mbele ya serikali mbalimbali kama ulivyojitokeza katika historia ndefu ya Kanisa, ingawa Agostino alijua jinsi Kaisari Theodosi alivyotubu kanisani baada ya askofu Ambrosi wa Milano kumtenga kwa sababu aliwatuza wanajeshi wa serikali yake walioua watu wengi ovyo walipotuliza fujo lililotokea katika mji wa Thesalonike. Watu wengi pamoja na Askofu walisikitikia tendo hilo. Baadaye Theodosi alipotaka kuingia katika ibada, Askofu huyo alimtangaza ametengwa kwa sababu ya kumwaga damu ya Wathesalonike, hivyo hawezi kushiriki meza ya Bwana. Kaisari akakubali kosa mbele ya umati. Hata baadaye viongozi wa Kanisa la magharibi wakafuata mara nyingi mfano wa Ambrosio na mafundisho ya Agostino. Mafundisho hayo yaliathiri mawazo na fikra za Wakristo kwa karne nyingi za baadaye. Tunaweza kuona aina mbili za matokeo ya urithi huo. Kwa upande mmoja Kanisa lilijaribu kutawala jamii na serikali katika nchi za Ulaya. Lilidai sheria zote za serikali zifuate taratibu za Kanisa. Viongozi wa serikali walitakiwa kusimikwa na wale wa Kanisa. Hoja hiyo huitwa "Uklerikali" (clericalism). Nguvu ya kisiasa ya Kanisa ilifikia kilele chake mwanzoni mwa karne ya 13 wakati wa Papa Inosenti III, halafu ilizidi kupungua hadi kupingwa kabisa na mapinduzi mbalimbali ya Ulaya na Amerika (kuanzia mapinduzi ya Ufaransa 1789). Siku hizi wazo hili halipo tena lakini zamani lilileta matatizo mengi, kama vile ugandamizaji wa madhehebu tofauti na ya mtawala, na hata vita vya kidini. Agostino aliingiza pia hoja ya "vita halali" katika Ukristo uliowahi kukataa ukatili na vita kama dhambi dhidi ya Mungu. Agostino alieleza kwamba wakati mwingine vita ni halali, na kama ni halali ni wajibu wa Mkristo pia. Maelezo hayo yalitumiwa baadaye na watawala na wanasiasa Wakristo kwa kutetea vita vya kila aina. Lakini sehemu nyingine ya urithi huo imebaki: kazi ya Kanisa ya kuzitetea haki za binadamu, hata dhidi ya serikali inayoweza kuzigandamiza. Kwa mfano makanisa ndiyo yaliyopinga sana siasa ya ubaguzi wa rangi Marekani na Afrika ya Kusini, hata dhidi ya serikali zilizoutetea. Vilevile ni makanisa yanayotetea haki za wakimbizi katika nchi nyingi hata kama serikali zimeshachoka mzigo wa kupokea wageni maskini kutoka nchi jirani. Mwishoni tusifiche sehemu ya urithi wa Agostino iliyokuwa ngumu zaidi mpaka leo. Katika mikoa ya Afrika Kaskazini walikuwepo Wakristo wengi waliojitenga na Kanisa kubwa na kuanzisha madhehebu ya Wadonato. Agostino alijadiliana nao miaka mingi akijaribu kuwavuta warudi tena. Mwaka 411 B.K. serikali ya Kiroma ilitafuta shauri la Agostino katika suala la Wadonato kule Karthago na Numidia (Tunisia na Algeria). Serikali ilitaka kuwe na umoja wa kidini kati ya wananchi. Pia wapinzani wa utawala wa Roma huko Afrika Kaskazini walijiunga na Kanisa la Wadonato. Basi Agostino aliona kwamba Wadonato wameshika mafundisho ya uongo, akaogopa wataongoza waumini wao jehanamu. Akaona Kanisa lisiache wafundishe uongo (alivyoelewa mwenyewe), akaona vema kutumia nguvu ya serikali walazimishwe kurudi katika Kanisa kubwa. Mwenyewe hakukubali adhabu ya kifo kwa "wazushi" hao, lakini serikali ilichukua kibali chake cha kuingilia kati kama msingi wa kuwatesa vikali na kuwaua wengi. Wadonato walipoteswa hivi na serikali, Agostino akanyamaza, hakupinga. Mateso hayo ya Wakristo Wadonato chini ya serikali ya Kikristo mbele ya macho ya Kanisa Katoliki yaliendelea muda mrefu yakawa mwanzo wa mwisho wa Ukristo Afrika Kaskazini. Miaka mia mbili baadaye wanajeshi wa Waarabu Waislamu wakaingia huko, wakakuta Ukristo uliodhoofishwa (pia kutokana na dhuluma za Wavandali Waario dhidi ya Wakatoliki). Baada ya muda mfupi wenyeji wengi sana wa sehemu hizo wakaacha Ukristo wakajiunga na Uislamu. Tukiangalia hali ya Misri tunaona tofauti: huko Wakristo wakashika imani yao katika karne zote ingawa kwa matatizo makubwa chini ya serikali ya Kiislamu. Lakini katika sehemu ya Afrika Kaskazini-Magharibi nguvu za ndani za Ukristo zilivunjika wakati wa mateso hayo makali ya Wadonato (halafu ya Wakatoliki) kwa mikono ya Wakristo wenzao. Tatizo halikuishia Afrika Kaskazini. Agostino katika kitabu chake kimojawapo alitetea siasa ya ugandamizaji wa wazushi bila kuruhusu wauawe. Katika karne zilizofuata maandiko hayo yaliongoza sera ya Kanisa la magharibi dhidi ya wazushi kote Ulaya. Kanisa lilikubali wazo la kwamba wazushi wanapaswa kugandamizwa. Basi kwa karne nyingi Kanisa la magharibi likaendelea kuwagandamiza na kuwatesa Wakristo wasiokubali mafundisho yake au uongozi wake. Watu wakateswa, kuchomwa moto na kufungwa gerezani, yote hayo kwa idhini ya Kanisa. Hata madhehebu ya Uprotestanti kama Walutheri, Waanglikana na Wareformati yalitenda hivihivi baada ya kuwa dini rasmi ya serikali katika maeneo yao. Walifuata mfano uliowekwa wakati wa mgongano kati ya Kanisa kubwa na Wadonato huko Afrika Kaskazini katika karne ya 5. Bila shaka Agostino hakutegemea matokeo hayo lakini hata habari hizi za kuhuzunisha ni sehemu ya urithi wa mtu huyo ambaye kwa mengine tunamkumbuka kama mwalimu mkubwa wa Ukristo mzima. Sala zake Wewe Bwana ni mkuu na unastahili kabisa sifa. Uweza wake ni mkuu na hekima yako haina mipaka. Mtu anataka kukusifu, yeye aliye sehemu ndogo ya viumbe vyako vyote, yeye anayetembea akielekea kifo, ushahidi wa dhambi yake, wa kwamba wewe unapinga wenye kiburi. Hata hivyo mtu, sehemu ndogo ya viumbe vyako vyote, anataka kukusifu. Wewe unamchochea aonje furaha ya kukusifu, kwa kuwa umetuumba kwa ajili yako, na moyo wetu hautulii mpaka ustarehe ndani mwako. Ee upendo wenye kuwaka daima usiweze kuzimika kamwe, Mungu wangu uniwashe moto! Unijalie mimi, mimi pia, Bwana wangu mpenzi, nikujue, nikupende na kukufurahia. Nisipoweza kufanya hayo kikamilifu katika maisha haya, unijalie walau kusonga mbele kila siku hata niweze kufikia kuyafanya kwa ukamilifu. Acha nikufahamu zaidi na zaidi hata ukamilifu. Acha nikupende kila siku zaidi na zaidi hata ukamilifu; furaha yangu iwe kubwa kwa yenyewe, na kamili ndani yako. Wewe ni nini kwangu? Uniwie huruma, niweze kusema. Mimi ni nini kwako, hata uniagize nikupende, halafu nisipokutii unanikasirikia na kunitishia maafa makubwa? Je, kutokupenda si balaa kubwa tayari? Lo, kwa huruma yako, Bwana Mungu wangu, uniambie wewe ni nini kwangu. “Uiambie nafsi yangu, Mimi ni wokovu wako”. Sema hivyo, nami nitasikiliza. Tazama, moyo wangu unakusikiliza, Bwana; uuweke tayari ukaniambie, “Mimi ni wokovu wako”. Nitafuata sauti ya neno lako hilo hata nikufikie. Usinifiche uso wako: nife nisije kufa, bali niuone uso wako. Unijalie nifanye unachoagiza, halafu uniagize unachotaka. Nimechelewa kukupenda, Uzuri wa kale na mpya daima; nimechelewa kukupenda. Tazama, wewe ulikuwa ndani mwangu, nami nilikuwa nje na kukutafuta huko. Mimi, mbaya, nilikuwa ninaparamia vitu vizuri ulivyoviumba. Wewe ulikuwa nami, lakini mimi sikuwa nawe. Vilikuwa vikinishika mbali nawe viumbe vile ambavyo kama visingekuwa ndani yako hata kuwepo visingekuwepo. Uliniita, ukanipigia kelele, ukashinda uziwi wangu. Uliniangaza, ukanimulikia kama umeme angani, hatimaye ukaponya upofu wangu. Ulinipulizia harufu yako nami nikainusa, na sasa nakuonea shauku. Nimekuonja na sasa nakuonea njaa na kiu. Umenigusa nami sasa nawaka tamaa ya kupata amani yako. Sasa nakupenda wewe tu, nakufuata wewe tu, nakutafuta wewe tu, niko tayari kukutumikia wewe tu, kwa kuwa wewe tu unatawala kwa haki, natamani kuwa chini ya uwezo wako. Naomba kitu hiki tu kutokana na hisani yako kuu: kwamba unigeuzie kabisa kwako, usiruhusu chochote kunizuia nisielekee kwako. Maandishi yake makuu Maandishi kuhusu maisha yake Confessiones (Maungamo) 397-398 - anamoeleza maisha yake pamoja na njia yake ya imani. Ni kitabu ambacho baada ya Biblia kilisomwa zaidi katika Karne za Kati Retractationes (Masahihisho) 426-428 - anamopitia maandiko yake ya awali akitaja mifano jinsi alivyobadilisha mawazo na hoja zake Maandishi juu ya falsafa na teolojia De Musica (kuhusu muziki) De civitate Dei (Mji wa Mungu) 413 - 426 De Trinitate (Kuhusu Utatu) 400-416 - andiko lake kubwa lenye vitabu 15 De doctrina christiana (kuhusu mafundisho ya kikristo) 397-426 De libero arbitrio (kuhusu nia huru) De beata vita (kuhusu maisha mema) -- kuhusu raha na kumjua Mungu De magistro (juuy a mwalimu) -- mafundisho kuhusu umuhimu wa lugha De vera religione (kuhusu dini ya kweli) -- kuhusu imani ya kikristo Soliloquia (mazungumzo na nafsi) -- kuhusu uwezo wa akili ya kujijua De immortalitate animae(kuhusu roho isiyokufa) Tazama pia Watakatifu wa Agano la Kale Orodha ya Watakatifu Wakristo Orodha ya Watakatifu wa Afrika Orodha ya Watakatifu Wafransisko Mababu wa Kanisa Tanbihi Marejeo kwa Kiswahili MT. AUGUSTINO, Kanuni– tafsiri ya Mapadri Waaugustino – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1992 – ISBN 9976-67-059-1 M. CULLEN, O.S.A., Maungamo ya Mtakatifu Augustino kwa Muhtasari – tafsiri ya E. Msigala, O.S.A. - ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda – ISBN 9976-63-643-1 M. CULLEN, O.S.A., Mtakatifu Monika: Mlinzi wa Akina Mama Wakristu – tafsiri ya E. Msigala, O.S.A. - ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 2002 – ISBN 9976-63-641-5 U. D. KINYERO, O.S.A., Mt. Agustino wa Hippo - Wasifu M. CULLEN, O.S.A., Watakatifu Monika na Augustino - ed. Shirika la Mt. Augustino Tanzania, 2013 Vyanzo vingine g Saint Augustine, pages 30, 144; City of God 51, 52, 53 and The Confessions 50, 51, 52 Règle de St. Augustin pour les religieuses de son ordre; et Constitutions de la Congrégation des Religieuses du Verbe-Incarné et du Saint-Sacrament (Lyon: Chez Pierre Guillimin, 1662), pp. 28–29. Cf. later edition published at Lyon (Chez Briday, Libraire,1962), pp. 22–24. English edition, (New York: Schwartz, Kirwin, and Fauss, 1893), pp. 33–35. Pagels, Elaine Adam, Eve, and the Serpent: Sex and Politics in Early Christianity Vintage Books (Sep 19 1989) ISBN 0-679-72232-7 Viungo vya nje Augustine of Hippo edited by James J. O'Donnell – texts, translations, introductions, commentaries, etc. St. Augustine at the Christian Classics Ethereal Library Aurelius Augustinus at "IntraText Digital Library" – texts in several languages, with concordance and frequency list Augustinus.it – Latin and Italian texts Sanctus Augustinus at Documenta Catholica Omnia – Latin City of God, Confessions, Enchiridion, Doctrine audio books* St. Augustinus | Augustine of Hippo – a site dedicated to the life and teaching of the doctor of the Catholic Church. Augustine of Hippo at EarlyChurch.org.uk – extensive bibliography and on-line articles Order of St Augustine Blessed Augustine of Hippo: His Place in the Orthodox Church Waliozaliwa 354 Waliofariki 430 Wanafalsafa wa Algeria Wanateolojia wa Algeria Watakatifu wa Algeria Mababu wa Kanisa Walimu wa Kanisa Maaskofu Wakatoliki Wamonaki Waaugustino Watawa waanzilishi
2237
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wavandali
Wavandali
Wavandali walikuwa kabila kubwa la Kigermanik la mashariki ambao katika karne tano za kwanza BK walihama kutoka sehemu za Poland ya leo hadi Afrika ya Kaskazini wakiunda Ufalme wao katika maeneo ya Algeria na Tunisia ya leo, pamoja na kutawala visiwa vya Mediteraneo magharibi. Historia Inaonekana ya kwamba walianza kuondoka kwao Ulaya ya mashariki kutokana na uvamizi wa Wahunni. Mwaka 406 BK walivuka mto wa Rhine wakaingia Gallia (leo Ufaransa), mwaka 409 wakavamia Hispania. Kutoka Hispania ya Kusini walivuka bahari ya Mediteraneo mwaka 429 na kuingia Afrika ya Kaskazini iliyokuwa jimbo la Dola la Roma. Kuna taarifa ya jemadari Mroma wa wakati ule ya kwamba walikuwa jumla ya wanaume wenye silaha kati ya 15,000 hadi 20,000, kwa hiyo pamoja na familia zao takriban watu 80,000. Wavandali waliteka Afrika ya Kaskazini yote iliyokuwa jimbo tajiri sana katika Dola la Roma likilimwa sehemu kubwa ya ngano kwa ajili ya mahitaji ya Italia. Mwaka 430 waliteka mji wa Hippo, maarufu kutokana na askofu wake Agostino, ambao ukawa makao makuu ya mfalme wao Genseriki. Mwaka 439 waliteka pia mji wa Karthago na mfalme akaufanya mji wake mkuu. Uvamizi wa Karthago uliwapatia Wavandali pia jahazi nyingi za kijeshi za Waroma. Hali hiyo iliwawezesha kushambulia hata mji wenyewe wa Roma mwaka 455, lakini hawakukaa, ila baada ya kuuvamia na kuuharibu walirudi Afrika. Ufalme wa Wavandali ulidumu karibu karne moja. Wakati wa madhehebu ya Waario, walitesa vikali Wakristo wenzao Wakatoliki. Katika karne ya 6 Kaisari Justiniani I wa Bizanti (Roma ya Mashariki) alimaliza utawala wao akivamia Afrika ya Kaskazini na kuirudisha katika Dola la Roma tangu mwaka 534. Marejeo Blume, Mary. "Vandals Exhibit Sacks Some Cultural Myths", International Herald Tribune, August 25, 2001. Christian Courtois: Les Vandales et l'Afrique. Paris 1955 Clover, Frank M: The Late Roman West and the Vandals. Aldershot 1993 (Collected studies series 401), ISBN 0-86078-354-5 Die Vandalen: die Könige, die Eliten, die Krieger, die Handwerker. Publikation zur Ausstellung "Die Vandalen"; eine Ausstellung der Maria-Curie-Sklodowska-Universität Lublin und des Landesmuseums Zamość ... ; Ausstellung im Weserrenaissance-Schloss Bevern ... Nordstemmen 2003. ISBN 3-9805898-6-2 John Julius Norwich, Byzantium: The Early Centuries F. Papencordt's Geschichte der vandalischen Herrschaft in Afrika Guido M. Berndt, Konflikt und Anpassung: Studien zu Migration und Ethnogenese der Vandalen (Historische Studien 489, Husum 2007), ISBN 978-3-7868-1489-4. Hans-Joachim Diesner: Vandalen. In: Paulys Realencyclopädie der class. Altertumswissenschaft (RE Suppl. X, 1965), S. 957-992. Hans-Joachim Diesner: Das Vandalenreich. Aufstieg und Untergang. Stuttgart 1966. 5. Helmut Castritius: Die Vandalen. Etappen einer Spurensuche. Stuttgart u.a. 2007. Ivor J. Davidson, A Public Faith, Chapter 11, Christians and Barbarians, Volume 2 of Baker History of the Church, 2005, ISBN 0-8010-1275-9 L'Afrique vandale et Byzantine. Teil 1. Turnhout 2002 (Antiquité Tardive 10), ISBN 2-503-51275-5. L'Afrique vandale et Byzantine. Teil 2, Turnhout 2003 (Antiquité Tardive 11), ISBN 2-503-52262-9. Lord Mahon Philip Henry Stanhope, 5th Earl Stanhope, The Life of Belisarius, 1848. Reprinted 2006 (unabridged with editorial comments) Evolution Publishing, ISBN 1-889758-67-1. Evolpub.com Ludwig Schmidt: Geschichte der Wandalen. 2. Auflage, München 1942. Pauly-Wissowa Pierre Courcelle: Histoire littéraire des grandes invasions germaniques. 3rd edition Paris 1964 (Collection des études Augustiniennes: Série antiquité, 19). Roland Steinacher: Vandalen - Rezeptions- und Wissenschaftsgeschichte. In: Hubert Cancik (Hrsg.): Der Neue Pauly, Stuttgart 2003, Band 15/3, S. 942-946, ISBN 3-476-01489-4. Roland Steinacher: Wenden, Slawen, Vandalen. Eine frühmittelalterliche pseudologische Gleichsetzung und ihr Nachleben bis ins 18. Jahrhundert. In: W. Pohl (Hrsg.): Auf der Suche nach den Ursprüngen. Von der Bedeutung des frühen Mittelalters (Forschungen zur Geschichte des Mittelalters 8), Wien 2004, S. 329-353. Uibk.ac.at Stefan Donecker; Roland Steinacher, Rex Vandalorum - The Debates on Wends and Vandals in Swedish Humanism as an Indicator for Early Modern Patterns of Ethnic Perception, in: ed. Robert Nedoma, Der Norden im Ausland - das Ausland im Norden. Formung und Transformation von Konzepten und Bildern des Anderen vom Mittelalter bis heute (Wiener Studien zur Skandinavistik 15, Wien 2006) 242-252. Uibk.ac.at Victor of Vita, History of the Vandal Persecution ISBN 0-85323-127-3. Written 484. Walter Pohl: Die Völkerwanderung. Eroberung und Integration. Stuttgart 2002, S. 70-86, ISBN 3-17-015566-0. Westermann, Grosser Atlas zur Weltgeschichte Yves Modéran: Les Maures et l'Afrique romaine. 4e.-7e. siècle. Rom 2003 (Bibliothèque des Écoles françaises d'Athènes et de Rome, 314), ISBN 2-7283-0640-0. Makabila ya Wagermanik Historia ya Algeria Historia ya Tunisia Historia ya Hispania
2238
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tunisia
Tunisia
Tunisia (kirefu: Jamhuri ya Tunisia - kwa Kiarabu الجمهرية التونسية, al-Jumhūrīya at-Tūnisīya) ni nchi ya Afrika ya Kaskazini inayopakana na Bahari ya Mediteranea, Libya na Algeria. Nchi imegawanyika katika mikoa 6 tena katika wilaya 24. Mji mkuu ni Tunis (wakazi 1,066,961) ulioko mahali pa Karthago ya kale. Historia Tunisia iliwahi kutawaliwa na Wafinikia walioanzisha huko mji wa Karthago. Baada ya hao kushindwa na Roma ya Kale, ilikuwa jimbo la Afrika katika Dola la Roma. Kisha eneo lake likatawaliwa kwa awamu na Wavandali, Waarabu, Wahispania, Waturuki na Wafaransa. Tarehe 20 Machi 1956 ilipata uhuru. Watu Wakazi karibu wote (98%) wanajiita Waarabu na hutumia lugha ya Kiarabu ambacho ndicho lugha rasmi. Hata hivyo damu yao ni mchanganyiko hasa wa ile ya Waberber, Waarabu na Waturuki. Takriban watu 200,000, hasa kusini, wanaendelea kuzungumza Kiberber ambacho ni lugha asili ya wenyeji lakini Waberber wengi wamezoea kutumia Kiarabu. Katika elimu na biashara Kifaransa kinatumika pia sana. Upande wa dini, Uislamu unafuatwa na asilimia 99 za wakazi, nao ndio dini rasmi, lakini theluthi moja kati yao, na nusu kati ya vijana, wanajitambulisha kama wasio na dini, kiwango kikubwa kuliko nchi zote za Kiarabu. Waliobaki ni Wakristo, hasa Wakatoliki, na Wayahudi wachache. Tazama pia Orodha ya miji ya Tunisia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Viungo vya nje Government of Tunisia (official website). Tunisia profile from BBC News. Nchi za Kiarabu Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa
2239
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Kiswahili
Historia ya Kiswahili
Historia ya Kiswahili imeanza takriban miaka 1000 iliyopita kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Neno Swahili lina asili ya Kiarabu: Sahil ina maana ya pwani; sawahil ’’as-sawāhilī’’ (السواحلي) ni wingi wake kwa kumaanisha yote yanayohusiana na pwani, watu au utamaduni wa eneo la pwani. Lugha ya Wabantu iliyoenea kwa njia ya biashara Utafiti umeonyesha kwamba vyanzo vya Kiswahili vilikuwa katika lugha za jamii ya wakulima Wabantu waliofika kwenye pwani za Bahari Hindi; wataalamu hutofautiana wakiona asili hiyo ama kwenye mpaka wa Kenya na Somalia au Kenya na Tanzania za leo. Wasemaji wa kwanza walikuwa karibu na wasemaji wa Kipokomo, Kimijikenda na Kikomori. Mababu hao wa Waswahili wa baadaye waliunda vijiji kwenye pwani ilhali chakula chao kilikuwa hasa samaki na kome. Walijifunza kusafiri baharini wakaanza kushiriki katika biashara iliyoendelea kwenye pwani za Bahari Hindi tangu miaka kabla ya Kristo. Mfumo wa upepo wa monsuni unawezesha safari za mbali kwa kutumia vyombo sahili kwa kufuata upepo kutoka kaskazini kuelekea kusini, kusubiri huko hadi kugeuka kwa upepo na kurudi tena. Mnamo mwaka 800 BK Unguja Ukuu (kusini mwa mji wa Zanzibar) ilikuwa kitovu cha biashara ya kimataifa kwenye maeneo ya Tanzania ya leo. Utamaduni wa Kiislamu kwenye pwani Pamoja na wafanyabiashara kutoka nchi za Kiislamu kufika kusini, watu wa pwani walisafiri wenyewe hadi Uarabuni na Bara Hindi; hapo waliweza kujiunga na Uislamu ambako kulileta faida mbalimbali: walikingwa zaidi wasikamatwe kuwa watumwa (iliyokuwa vigumu zaidi ukiwa Mwislamu), walikubaliwa kama washirikiki katika mfumo wa biashara iliyokingwa na sheria za Kiislamu. Vilevile wafanyabiashara kutoka kaskazini walikuwa salama zaidi wakikaa miezi kadhaa kwenye miji iliyotokea ikifuata desturi za Kiislamu. Misikiti ilianza kujengwa kwenye makazi ya pwani na vijiji vilibadilika kuwa miji. Kiswahili kilienea kama lugha ya miji na bandari za biashara ya kimataifa kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Lahaja za Kiswahili ziliendelea tofauti kiasi kutokana na athira ya lugha za majirani tofauti kwenye kanda ndefu ya pwani; wataalamu wanaona makundi ya lahaja za kaskazini (pwani za Kenya na Somalia) na lahaja za kusini (pwani za Tanzania na Msumbiji). Kufuatana na biashara na dini lahaja zote zilipokea maneno ya Kiarabu kwa viwango tofauti; katika Kiswahili sanifu cha kisasa chenye asili katika lahaja ya Unguja kiasi hicho hukadiriwa takriban theluthi moja ya maneno yote. Kuna masimulizi kuhusu vyanzo vya miji kama vile Kilwa, Lamu ambamo miji hiyo ilianzishwa na wakimbizi kutoka Uajemi, hasa kutoka Shiraz, waliooa wenyeji. Hadi leo wenyeji wengine wa pwani na funguvisiwa la Zanzibar hujiita "Washirazi". Siku hizi wataalamu wengi hukubaliana kwamba masimulizi hayo si taarifa ya kihistoria ila visasili. Hata hivyo, utafiti wa DNA ya mifupa ya watu 80 iliyopatikana kwenye makaburi ya miji ya Waswahili kuanzia kisiwa cha Manda, Faza na Mtwapa huko Kenya hadi Kilwa, Songo Mnara na Lindi kusini mwa Tanzania, umeonyesha kwamba sampuli nyingi zilizochunguzwa zilitokana na watu waliozaliwa na mababu wa mchanganyiko kati ya wanaume Waajemi (kutoka Iran) na wanawake Waafrika. Utamaduni mpya ulijitokeza uliokuwa wa Kiafrika na wa Kiislamu ukajielewa kuwa sehemu ya dunia ya Uislamu. Hivyo Kiswahili kilizaliwa kuwa lugha ya Kibantu kilichopokea maneno mengi ya asili ya nje. Lugha iliandikwa kwa herufi za Kiarabu tangu karne ya 13 BK. Kwa bahati mbaya leo hatuna tena maandiko ya kale sana, kutokana na hali ya hewa kwenye pwani isiyosaidia kutunza karatasi na kurasa zenyewe zinaweza kuoza kutokana na unyevu hewani pamoja na wadudu wengi walioko katika mazingira ya pwani. Lakini maandiko ya kale yanayopatikana kutoka karne ya 17 huonyesha ya kwamba tenzi na mashairi vinafuata muundo uliotangulia maandiko yenyewe kwa karne kadhaa. Sehemu kubwa ya maandiko ya kale ni tenzi yaani mashairi yenye aya maelfu. Tenzi ndefu kabisa inahusu kifo cha Mtume Muhamad ikiwa na aya 45,000. Kiswahili kimepokewa kwa urahisi na wenyeji kwa sababu walikosa lugha ya pamoja kati yao, lugha za Kibantu ziko karibu sana na athira ya Kiarabu ilikuwa kilekile kote pwani. Haya yote yalisaidia kujenga umoja wa Kiswahili katika eneo kubwa la pwani ya Afrika ya Mashariki. Kiajemi pia kilichangia maneno mbalimbali, kama vile "bibi" na "cherehani". Kufika kwa Wareno huko Afrika ya Mashariki kuanzia mwaka 1500 kulileta athira mpya ikiwa maneno kadhaa ya Kireno yameingia katika Kiswahili kama vile "bendera", "gereza" na "meza". Kuwepo kwa wafanyabiashara Wahindi katika miji mikubwa ya pwani kuliingiza pia maneno ya asili ya Kihindi katika lugha kama vile "lakhi", "gunia" n.k. Athira ya lugha za Kihindi iliongezeka kiasi baada ya Waingereza kutumia Wahindi wengi kujenga reli ya Uganda. Lugha ya biashara Kiswahili kilitumika kama lugha ya biashara baina ya watu wa pwani na bara katika kanda ndefu sana kutoka Somalia hadi Msumbiji wa Kaskazini. Wafanyabiashara Waswahili waliendeleza biashara ya misafara hadi Kongo. Kiswahili kiliendelea kuenea kwenye njia za misafara hii. Kila msafara ulihitaji watu mamia hadi maelfu wa kubeba mizigo ya biashara kutoka pwani hadi pale msafara ulipolenga hata Ziwa Tanganyika. Watu hawa wote walisambaza matumizi ya Kiswahili katika sehemu za ndani. Lakini katika maeneo fulani biashara hii ilijenga pia kizuizi. Watu kama Waganda waliona Kiswahili ni lugha ya Waislamu tena lugha ya biashara ya watumwa; hivyo hadi leo ni wagumu kukubali Kiswahili. Wamisionari Wakristo wa awali, kama Ludwig Krapf, Edward Steere na A.C. Madan, walifanya utafiti wa lugha na kutunga kamusi na sarufi za kwanza pamoja na kuunda mfumo wa kuandika Kiswahili kwa herufi za Kilatini. Kiswahili wakati wa ukoloni Karne ya 19 ilileta utawala wa kikoloni. Wakoloni walitangulia kufika katika bandari za pwani wakatumia mara nyingi makarani, askari na watumishi kutoka eneo la pwani wakijenga vituo vyao barani. Watu hao walieneza Kiswahili pande za bara. Wajerumani waliamua kutumia Kiswahili kama lugha ya utawala katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hapo walitumia kazi ya utafiti iliyofanywa na wamisionari. Utawala wa kikoloni ulirahisisha mawasiliano kati ya wenyeji. Reli zilijengwa na wafanyakazi kutoka makabila mbalimbali walishirikiana. Waafrika walilazimishwa kulipa kodi kwa wakoloni, hivyo walitafuta kazi ya ajira. Hasa katika mashamba makubwa yaliyolima mazao ya biashara pia katika migodi ya Kongo watu wa makabila mengi walichanganyikana wakitumia hasa Kiswahili kati yao. Kwa namna hiyo lugha ilienea zaidi. Waingereza baada ya kuchukua Tanganyika kutoka kwa Wajerumani waliendela kutumia Kiswahili kama lugha ya utawala. Kuanzia mwaka 1930 waliunda kamati yenye shabaha ya kuunganisha lahaja mbalimbali na kuunda Kiswahili cha pamoja kwa ajili ya Afrika ya Mashariki (Inter-territorial Language (Swahili) committee for the East African Dependencies). Mwenyekiti alikuwa Frederick Johnson, makatibu R. K. Watts, P. Mzaba na Seyyid Majid Khalid Barghash. Kamati hiyo iliamua kutumia lahaja ya Kiunguja kuwa msingi wa Kiswahili cha pamoja kilichoendela kufundishwa shuleni. Leo hii ni Kiswahili rasmi kinachofunzwa na wanafunzi na kuandikwa magazetini na vitabuni. Miaka ya ukoloni ilisababisha pia kupokelewa kwa maneno mapya katika Kiswahili. Kijerumani kiliacha maneno machache kama "shule" (Kijerumani Schule) na "hela" (Heller) lakini maneno mengi sana ya asili ya Kiingereza yalipokelewa. Kiswahili kimeonyesha uwezo mkubwa wa kupokea maneno kutoka lugha tofauti sana, kikitumia maneno haya kufuatana na sarufi ya Kibantu ya Kiswahili. Lugha ya kimaandishi Tofauti na lugha nyingi za Afrika, Kiswahili kiliandikwa tangu karne kadhaa kwa herufi za Kiarabu. Mwandiko wa Kiarabu huwa na herufi kadhaa kwa sauti ambazo haziko katika lugha za Kibantu, vilevile kuna sauti kama "p" au "g" ambazo hazina herufi kwa Kiarabu. Ilhali miji ya Waswahili kwenye eneo kubwa kutoka Somalia hadi Msumbiji ilijitegemea, hapakuwa na tahajia sanifu. Jedwali ifuatayo inaonyesha matumizi iliyokuwa kawaida mara nyingi. Kiswahili leo Katika Tanzania Kiswahili kimekuwa lugha rasmi ya serikali na taifa. Shule za msingi hutumia Kiswahili lakini shule za sekondari na vyuo bado zinaendelea kufundisha kwa Kiingereza. Tarehe 15 Februari 2015 rais Jakaya Kikwete alitangaza mpango wa kubadilisha lugha ya elimu nchini kwa kutumia Kiswahili kwenye ngazi zote hadi shule za sekondari na chuo kikuu. Kenya imetangaza Kiswahili kuwa lugha ya taifa lakini inaendelea kutumia Kiingereza katika shughuli za serikali. Watu wa matabaka ya juu mara nyingi hupendelea kutumia Kiingereza wakiona ni lugha bora. Lakini tangu 1986 wanafunzi wote wanatakiwa kujifunza Kiswahili katika shule za sekondari. Tatizo mojawapo ni kuwepo wa makabila makubwa kama Wakikuyu au Waluo wenye wasemaji wengi sana katika eneo moja, hali isiyosaidia kujifunza lugha tofauti. Pia kaskazini na magharibi mwa Kenya wenyeji wengi si wasemaji wa lugha za Kibantu nao hawaoni Kiswahili ni lugha rahisi. Uganda inatumia Kiswahili kama lugha ya polisi na jeshi, hali ambayo haikuongeza upendo wa Waganda kwa lugha kutokana na historia ya Uganda ya kuwa na vita na serikali za kijeshi. Lakini kinasikika pia kama lugha ya biashara masokoni. Pamoja na kwamba Waganda walikichukulia Kiswahili kama lugha ya kitumwa lakini pia lugha hii ilionekana kuwa na ustaarabu wa Kiarabu zaidi, yaani Uislamu. Lugha ya Kiswahili ilitumika katika kueneza dini hiyo. Mashariki mwa Kongo Kiswahili kimeenea sana: ni moja kati ya lugha nne za kitaifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kwenye visiwa vya Ngazija (Comoros) kuna lahaja mbalimbali za Kiswahili zinazotumika na wananchi. Tazama pia Asili ya Kiswahili Uenezi wa Kiswahili Tanbihi Marejeo Shihabdin Chiraghdin et Mathias E. Mnyampala. Historia ya Kiswahili. Oxford University Press, 1977. Nurse, D. and Hinnebusch, T. J. 1993. Swahili and Sabaki: A Linguistic History. Berkeley and Los Angeles: University of California Press. en:Swahili_language#The_rise_of_Swahili_to_regional_prominence Swahili Historia
2240
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lahaja%20za%20Kiswahili
Lahaja za Kiswahili
Kiswahili kimepatikana kwa namna au lahaja mbalimbali. Wakati wa ukoloni wa Uingereza azimio lilitolewa kutumia Kiswahili cha Unguja kuwa Kiswahili rasmi katika Tanganyika, Kenya na Zanzibar. Waingereza walikitumia pia kama lugha ya polisi na jeshi katika Uganda. Kati ya lahaja za Kiswahili ni zifuatazo: Kiunguja: kisiwani Unguja (Tanzania) - kimekuwa msingi wa Kiswahili Sanifu. Kihadimu (Kimakunduchi): kusini mashariki mwa kisiwa cha Unguja (Tanzania) Kimrima: eneo la Pangani, Vanga, Dar es Salaam, Rufiji na Mafia kisiwani (Tanzania) Kimgao: eneo la Kilwa (Tanzania) Kipate: eneo la Pate, visiwa vya pate (Kenya) Kipemba: kisiwani Pemba (Tanzania) Kimvita: eneo la Mvita au Mombasa (Kenya). Zamani ilikuwa lahaja kubwa ya kisomi ikitungiwa mashairi kuliko Kiunguja. Kingozi: kisiwa cha lamu na viungani mwake (Kenya) Kibajuni: magharibi mwa visiwa vya pate (Kenya) Chimbalanzi: barawa kusini mwa juba (Somalia) Kitikuu: katikati mwa kisiwa cha pate (Kenya) Kiamu: eneo la Lamu (Kenya) Kijomvu: eneo la Jomvu (Kenya) Kingwana: Kiswahili cha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Kisiu: eneo la Siu (pwani ya kaskazini ya Kenya) Kivumba: kisiwa cha Vumba na kaskazini kwa Tanga (Tanzania) Kimtang'ata: Mtang'ata, mkoa wa Tanga (Tanzania) Kimafia (Kingome): Mafia (Tanzania) Shikomor: Kiswahili cha Komoro Shimaore: Shikomor cha Mayotte (Mahore) Shindzuani: Shikomor cha Anjouan (Komoro) Shingadzija: Shikomor cha Komoro Kuu Kimwani: kaskazini mwa Msumbiji na visiwa vya Kerimba Chichifundi: kusini mwa PWANI Kwale,Kenya (kando ya fuo za bahari. hususan Gazi, Munje, Funzi, Bodo, Shimoni, Wasini, Mkwiro na Vanga) Chimiini: eneo la Barawa, kusini mwa Somalia Kiswahili.
2242
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kidachi
Kidachi
Kidachi ni neno la Kiswahili cha zamani linalosikika hadi leo katika sehemu za Tanzania kwa ajili ya lugha ya Kijerumani au tabia za Wajerumani. Neno limetokana na "Deutsch" (tamka: doitsh) ambalo ni jinsi Wajerumani wenyewe wanavyojiita. Kidachi, Mdachi/Wadachi na Udachi yalikuwa maneno ya Kiswahili cha kawaida kutokana na utawala wa Kijerumani katika Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Tangu mwisho wa ukoloni wa Wajerumani mwaka 1918 na kuja kwa Waingereza wasemaji wa Kiswahili wamezoea zaidi kuwataja "Wadachi" kwa kutumia jina lenye asili ya Kiingereza, yaani Kijerumani, Mjerumani/Wajerumani na Ujerumani. Mara nyingi maneno yenye "-dachi" huchanganywa na neno la Kiingereza "Dutch" linalomaanisha Waholanzi. Kidachi kimeathiri kwa kiasi fulani lugha ya Kiswahili cha Tanzania bara kama vile kukikopesha maneno mbalimbali, kwa mfano: shule, hela n.k. Kiswahili
2248
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Rukwa
Mkoa wa Rukwa
Mkoa wa Rukwa ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 55000. Unapakana na mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi upande wa kaskazini, mkoa wa Mbeya upande wa mashariki, Zambia kusini na upande wa magharibi Ziwa Tanganyika lililo mpaka na Kongo pia. Makao makuu ya mkoa ni Sumbawanga. Kabla ya kumegwa mwaka 2012 eneo la mkoa lilikuwa takriban km² 70,000. Kwa sasa lina kilomita ya mraba 22,792. Kusini mwa mkoa liko ziwa Rukwa ambalo ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki. Wilaya Wilaya nne zilikuwa (idadi ya wakazi katika mabano): Sumbawanga Mjini (147,483), Sumbawanga Vijijini (373,080) Wilaya ya Nkasi (208,497) Mwaka 2012 ilianzishwa Wilaya ya Kalambo. Mwaka 2014 ilianzishwa Wilaya ya Lyamba lya Mfipa. Wilaya ya Mpanda ilikuwa sehemu ya Rukwa ikaendelea kuwa kiini cha mkoa mpya wa Katavi kuanzia mwaka 2012. Wakazi Kulikuwa na wakazi 1,540,519 (sensa ya mwaka 2022), kwa asilimia kubwa waumini wa Kanisa Katoliki. Kabila kubwa zaidi mkoani ndio Wafipa walioko hasa katika wilaya za Sumbawanga na Nkansi. Kati ya makabila mengine kuna Wamambwe-Lungu, Wawanda na Wanyamwanga katika wilaya ya Sumbawanga; kuna pia Wasukuma, Wanyamwezi na Wamasai. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Sumbawanga Mjini : mbunge ni Aeshi Hilaly (CCM) Nkansi Kaskazini : mbunge ni Ally Keisy (CCM) Nkansi Kusini : mbunge ni Deuderit Mipata (CCM) Kwela : mbunge ni Deus Sangu (CCM) Kalambo : mbunge ni Kandege Sinkamba (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Rukwa Orodha ya mito ya mkoa wa Rukwa Tanbihi Viungo vya nje Tovuti ya Mkoa wa Rukwa Matokeo ya sensa 2002: Makabila na lugha za Tanzania: R
2250
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Shinyanga
Mkoa wa Shinyanga
Mkoa wa Shinyanga ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye msimbo wa posta 37000. Mkoa umepakana upande wa kaskazini na mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera, upande wa kusini na Mkoa wa Tabora. Mkoa wa Kigoma uko upande wa magharibi, na mkoa wa Simiyu upande wa mashariki. Makao makuu yako mjini Shinyanga. Baada ya kumegwa upande wa mashariki na kuzaa mkoa wa Simiyu, Shinyanga ina wakazi 2,241,299 kufuatana na sensa ya mwaka 2002 kutoka wakazi 1,534,808 wa sensa ya mwaka 2012. Utamaduni Makabila ya Shinyanga hasa ni Wasukuma, Wanyamwezi na Wasumbwa. Wilaya Mkoa wa Shinyanga una wilaya 5: Kahama Mjini, Kahama Vijijini, Kishapu, wilaya ya Shinyanga Vijijini na wilaya ya Shinyanga Mjini. Wilaya tano zimepelekwa kwenda mikoa mipya ya Simiyu na Geita., Wakazi wa Mkoa wa Shinyanga hujishughulisha na uchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu na almasi. Kuna migodi mikubwa ya uchimbaji wa madini ya almasi katika mgodi wa Mwadui na dhahabu katika migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi. Mgodi wa almasi wa Williamson Mgodi wa Williamson Diamond, ulioko katika Mkoa wa Shinyanga kilomita 160 kusini mwa jiji la Mwanza, ni moja ya mabomu saba yanayoendeshwa na Petra Diamonds. Mgodi huo kwa 75% inamilikiwa na almasi ya Petra na 25% na Serikali ya Tanzania. Williamson ni mgodi wazi wa shimo ulioenea juu ya eneo la hekta 146. Mgodi huo umekuwa ukifanya kazi kwa miaka 70. Bado ina rasilimali muhimu ya almasi bado inapaswa kuchimbwa. Mpango wa sasa wa mgodi kwa Williamson ni kwa miaka 18. Maisha yanayowezekana ya mgodi ni zaidi ya miaka 50. Mgodi huo umetajwa kwa jina la Dk John Williamson, mtaalamu wa jiolojia wa Canada, ambaye aligundua mnamo 1940 kama amana ya msingi ya kiuchumi ya almasi. Dk Williamson alisimamia mgodi huo hadi kifo chake mnamo 1958. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Kahama Mjini : mbunge ni Jumanne Kishimba (CCM) Kishapu : mbunge ni Suleiman Nchambi (CCM) Msalala : mbunge ni Ezekiel Maige (CCM) Shinyanga Mjini : mbunge ni Patrobas Katambi (CCM) Solwa : mbunge ni Ahmed Ally Salum (CCM) Ushetu : mbunge ni Elias Kwandikwa (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Shinyanga Orodha ya mito ya mkoa wa Shinyanga Tanbihi Viungo vya nje Shinyanga Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census Tanzanian Government Directory Database Shinyanga Investment profile Taarifa ya hali ya kilimo - Mkoa wa Shinyanga S
2251
https://sw.wikipedia.org/wiki/Idhaa%20ya%20Kiswahili%20ya%20Radio%20Tehran
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Tehran
Idhaa ya Kiswahili Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni huduma ya matangazo ya "Islamic Republic of Iran Broadcasting" (IRIB) ambayo ni redio ya taifa ya Iran (Uajemi) kwa lugha ya Kiswahili. IRIB inarusha matangazo kwa lugha mbalimbali kama vile Kirusi, Kiarabu, Kiingereza, Kifaransa Kichina na mengine. Kwa lugha ya Kiswahili ilianza kurusha matangazo yake kwa mara ya kwanza siku ya Ijumaa usiku ya tarehe 30 Desemba mwaka 1994. Kwa wakati huo matangazo ya Radio Tehran yaliyokuwa yakirushwa kwa ajili ya nchi za mashariki na katikati mwa Afrika, yalianza yakiwa na wafanyakazi wachache ambao ni Sayyid Muhammad Ridha Shushtari, Sayyid Hashim Shushtari ambaye kwa sasa ni marehemu, Muhammad Baraza, Leyla Kimani, Abdul Fatah Mussa, Ahmed Rashid, Nargis Jalalakhan na Said Kambi. Watangazaji wengine wa idhaa hii ni Asmahan Ghanima Mohammad, Salum Bendera, Mubarak Henia, Sudi Ja'afar Shaban na Hussein Hassan Kamau. Lengo la kuasisiwa Idhaa ya Kiswahili Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kufikisha sauti ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran kwa wananchi waliodhulumiwa wa bara la Afrika, kuelimisha na kufichua njama za ubeberu wa kimataifa dhidi ya bara hilo. Kuanzia tarehe 26 Aprili mwaka 1997 Radio Tehran ilianza kutangaza kwa muda wa saa moja kuanzia saa mbili na nusu usiku kwa saa za Afrika Mashariki, na matangazo hayo kurejewa siku ya pili yake kuanzia saa 12:30 asubuhi kwa majira ya Afrika Mashariki sawa na saa 11:30 asubuhi kwa majira ya Afrika ya Kati. Mnamo tarehe 23 Mfunguo Tatu (Dhulhijja) 1418 Hijria iliyosadifiana na tarehe 21 Aprili 1998 Milaadia, matangazo ya Radio Tehran yalianza kurushwa hewani kwa muda wa masaa matatu katika nyakati za usiku, asubuhi na machana. Saa moja ilikuwa ni marudio ya matangazo ya asubuhi, ambayo yalikuwa yakisikika kuanzia saa saba kamili hadi saa nane kamili mchana kila siku kwa majira ya Afrika Mashariki. Kwa hivi sasa Idhaa imeongeza wafanyakazi wake ambapo matangazo ya mchana nayo sasa yanasikika kwa njia ya moja kwa moja kuanzia saa 5:30 hadi 6:30 mchana kwa saa za Afrika Mashariki. Inarusha matangazo yake kwa ajili ya nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Congo, mashariki mwa Zambia, kaskazini mwa Malawi na Msumbiji pamoja na Afrika Kusini. Inarusha pia matangazo yake kwa ajili ya nchi za Mashariki ya Kati hususan za Ghuba ya Uajemi na ina waandishi wake katika maeneo ya Afrika Mashariki na Kati kama vile Kenya, Tanzania, Uganda, Burundi na Kongo. Matangazo ya IRIB yanalenga kusambaza habari juu ya Iran na utamaduni wake. Yanalenga kusambaza mitazamo ya Kiislamu na mafundisho ya Ahlul Baiti (as) inayolingana na siasa ya Iran. Matangazo ya IRIB pia yananawabaishia Walimwengu ubeberu wa Marekani na madola ya Kimagharibi dhidi ya mataifa mengine na ukandamizaji wa utawala haramu wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina. Viungo vya Nje http://kiswahili.irib.ir/ Redio ya kimataifa Uajemi Kiswahili
2253
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Pwani
Mkoa wa Pwani
Mkoa wa Pwani ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 61000. Mkoa umepakana upande wa Kaskazini na Tanga, upande wa mashariki na Dar-es-Salaam na Bahari Hindi, upande wa kusini na mkoa wa Lindi na upande wa magharibi na mkoa wa Morogoro. Makao makuu ya mkoa yako Kibaha. Eneo na wakazi Mkoa huu unalo eneo la km² 32,407, ukiwa na idadi ya wakazi wapatao 2,024,947 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 kutoka 1,098,668 (2012). Mkoa huu wenyeji wake ni watu wa makabila ya Wakwere, Wazaramo, Wandengereko na Wanyagatwa. Wilaya ya Rufiji imegawanyika sehemu mbili, visiwani na bara: wenyeji wa visiwani ni wa kabila la Wanyagatwa na walio bara ndio Wandengereko. Wenyeji wa visiwani wanajishughulisha sana na uvuvi, kilimo cha mnazi na kupika chumvi, Wandengereko wanajishughulisha sana na mazao ya vyakula kama vile mpunga, mahindi n.k. Wilaya Mkoa wa Pwani una wilaya nane ndizo (idadi ya wakazi katika mabano): Bagamoyo (230,164), Chalinze Kibaha Mjini (132,045), na Kibaha Vijijini, Kisarawe (95,614), Mkuranga (187,428), Mafia (40,801). Rufiji (103,174) Kibiti (133,727). Mkoa huu una jumla ya majimbo ya uchaguzi yanayofikia (9) ambayo yanajumuisha Bagamoyo, Chalinze, Kibaha, Kibaha Vijijini, Kibiti, Kisarawe, Mafia, Mkuranga na Rufiji Utalii Mkoa huu ni maarufu sana kwa shughuli za kiutalii hususani katika mji wa Bagamoyo. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Chalinze : mbunge ni Ridhwan Kikwete (CCM) Bagamoyo : mbunge ni Shukuru Kawambwa (CCM) Kibaha Mjini : mbunge ni Sylvester Francis Koka (CCM Kibaha Vijijini : mbunge ni Hamoud Abuu Jumaa (CCM) Kisarawe : mbunge ni Selemani Said Jafo (CCM) Mafia : mbunge ni Mbaraka Kitwana Dau (CCM) Mkuranga : mbunge ni Abdallah Hamis Ulega (CCM) Kibiti : mbunge ni Ally Seif Ungando (CCM) Rufiji : mbunge ni Mohamed Omary Mchengerwa (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Pwani Orodha ya mito ya mkoa wa Pwani Tanbihi Viungo vya nje Tovuti rasmi ya Mkoa wa Pwani, Tanzania Matokeo ya sensa 2002 kwa ajili ya mkoa wa Pwani Habari za Pwani kwenye kurasa za Tume ya Uchagizi P
2255
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Manyara
Mkoa wa Manyara
Mkoa wa Manyara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 27000. Umepakana na mikoa ya Arusha na Kilimanjaro upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa mashariki, Mkoa wa Dodoma upande wa kusini na mikoa ya Singida na Shinyanga upande wa magharibi. Mkoa wa Manyara umetengwa na Mkoa wa Arusha mwaka 2002 kwa azimio la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiwa na eneo la km² 46,359. Babati ndiyo makao makuu ya mkoa. Wakazi Jumla ya wakazi mkoani ilikuwa 1,892,502 katika sensa ya mwaka 2022. Idadi hiyo imepatikana katika wilaya zifuatazo (idadi ya wakazi katika mabano mwaka 2002): Babati (303,013), Hanang (205,133), Mbulu (237,882), Simanjiro (141,676) na Kiteto (152,757). Sensa zinaonyesha kwamba ni kati ya mikoa ya Tanzania yenye ongezeko kubwa la wakazi. Pia ni kati ya mikoa yenye maambukizi machache zaidi ya Ukimwi. Wenyeji wa mkoa huu ni pamoja na Wairaqw, Wamasai, Wambugwe, Wafyomi na Wabarbaig wakijihusisha na shughuli za kilimo na ufugaji kama njia ya kuingiza kipato chao cha kila siku. Wilaya Kuna wilaya zifuatazo: Babati, Mbulu, Hanang, Simanjiro and Kiteto. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi 7 yafuatayo: Babati Mjini : mbunge ni Pauline Gekuli (CCM) Babati Vijijini : mbunge ni Jitu Vrajilal Soni (CCM) Hanang’ : mbunge ni Samwel Hhayuma (CCM) Kiteto : mbunge ni Emmanuel Papiani (CCM) Mbulu Mjini : mbunge ni Zacharia Paulo Issaay (CCM) Mbulu Vijijini : mbunge ni Flatei Massay (CCM) Simanjiro : mbunge ni James Kinyasi Ole Millya (CCM) Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Manyara Orodha ya mito ya mkoa wa Manyara Tanbihi Viungo vya nje Tovuti ya Mkoa wa Manyara Manyara Matokeo ya sensa ya 2002* Serikali ya Tanzania Ijue mikoa ya Tanzania Mikoa ya Tanzania
2257
https://sw.wikipedia.org/wiki/Korongo%20%28Gruidae%29
Korongo (Gruidae)
Korongo hawa (pia mana) ni ndege wa familia ya Gruidae wenye domo fupi na jembamba kuliko lile la korongo wa familia ya Ciconiidae. Spishi nyingi hufanya mikogo ya kubembeleza jike wakitoa sauti kubwa. Huugana kwa maishi yao yote. Spishi za nchi za halijoto wastani huhama kila mwaka kabla ya wakati wa baridi. Korongo hawa hupenda kuwa pamoja na huhama kwa makundi makubwa. Hula kila kitu kinachopatikana, kama panya, watambaazi, amfibia au samaki, hata nafaka na matunda madogo. Spishi za korongo zinatokea mabara yote ghairi ya Amerika ya Kusini. Spishi za Afrika Balearica pavonina, Korongo-taji Mweusi (Black Crowned Crane) Balearica regulorum, Korongo-taji Kijivu au Ndege-chai (Grey Crowned Crane) Grus carunculata, Korongo Ndevu au Bwenzi (Wattled Crane) Grus grus, Korongo Paji-jeusi (Eurasian or Common Crane) Grus paradisea, Korongo Buluu (Blue Crane) Grus virgo, Korongo Tumbo-jeusi (Demoiselle Crane) Spishi za mabara mengi Antigone antigone (Sarus Crane) Antigone canadensis (Sandhill Crane) Antigone rubicunda (Brolga) Antigone vipio (White-naped Crane) Grus americana (Whooping Crane) Grus japonensis (Red-crowned Crane) Grus monacha (Hooded Crane) Grus nigricollis (Black-necked Crane) Leucogeranus leucogeranus (Siberian Crane) Picha Korongo na jamaa
2259
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Mwanza
Mkoa wa Mwanza
Mkoa wa Mwanza ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania, wenye postikodi namba 33000. Umepakana na Geita upande wa magharibi, Shinyanga na Simiyu upande wa kusini na Mara upande wa mashariki. Ziwa la Viktoria Nyanza liko kaskazini. Makao makuu ya mkoa yapo Mwanza mjini. Mkoa una wakazi 3,699,872 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 . Wilaya Kabla ya kumegwa na kuzaa mkoa mpya wa Geita, mkoa wa Mwanza ulikuwa na wakazi 2,942,148 (sensa ya mwaka 2002) katika wilaya 8 ukiwa na eneo la 19,592 km2. Wilaya ndizo Ukerewe, Magu, Sengerema, Geita, Misungwi, Kwimba, Nyamaganga na Ilemela. Jiji la Mwanza ndani yake lina wilaya za Nyamagana na Ilemela. Wakazi Makabila makubwa ya Mwanza ndio Wasukuma na Wazinza upande wa bara, halafu Wakerewe na Wakara visiwani. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Buchosa : mbunge ni Dk. Charles Tizeba (CCM) Ilemela : mbunge ni Angelina Mabula (CCM) Kwimba : mbunge ni Mansoor Hirani (CCM) Magu : mbunge ni Kiswaga Boniventura (CCM) Misungwi : mbunge ni Charles Kitwanga (CCM) Nyamagana : mbunge ni Stanslaus Mabula (CCM) Sengerema : mbunge ni William Ngeleja (CCM) Sumve : mbunge ni Richard Mganga Ndassa (CCM) Ukerewe : mbunge ni Joseph Mkundi (CCM) Tazama pia Orodha ya mito ya mkoa wa Mwanza Tanbihi Viungo vya nje Tovuti rasmi ya Mkoa wa Mwanza Mji wa Mwanza, habari za uchumi, utamaduni na mengi mengine Matokeo ya Sensa 2002 kwa Mwanza* Serikali ya Tanzania Wasukuma M
2266
https://sw.wikipedia.org/wiki/Heroe
Heroe
Heroe ni ndege wa jenasi Phoenicopterus, jenasi pekee ya familia ya Phoenicopteridae. Ndege hawa hukaa kwa maji ya chumvi kwa makundi makubwa. Wana miguu mirefu na shingo ndefu na nyembamba. Wakiruka angani hunyosha shingo. Urefu wao ni kati ya futi 3 na 5. Hula vijimea (algae) na nduvi ndogo ambazo huzikamata na domo lao zungu linalotumika kama chujio. Tago lao ni kifungu cha matope kwa tundu fupi ambalo ndani lake yai moja linatagwa. Spishi za Afrika Phoeniconaias minor, Heroe Mdogo (Lesser Flamingo) Phoenicopterus roseus, Heroe Mkubwa (Greater Flamingo): anatokea Asia na Ulaya pia. Spishi za Amerika Phoenicoparrus andinus (Andean Flamingo) Phoenicoparrus jamesi (James's Flamingo) Phoenicopterus chilensis (Chilean Flamingo) Phoenicopterus ruber (American Flamingo) Picha Majina ya ndege kwa Kiswahili
2269
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kilimanjaro
Mkoa wa Kilimanjaro
Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 25000. Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kupita yote barani Afrika, umo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Jina la mlima huu ndilo limeupatia mkoa jina lake. Mkoa wa Kilimanjaro umepakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa kusini na mikoa ya Manyara na Arusha upande wa magharibi. Wakazi Mkoani Kilimanjaro kuna wakazi wapatao 1,861,934 (sensa ya mwaka 2022). Makabila makubwa mkoani humo ni Wachagga, Wagweno na Wapare, ambapo pia kuna makabila mengine madogomadogo kama Wamasai na Wakamba. Makao makuu ya mkoa huu ni Moshi. Katika sekta ya elimu wakazi wameendelea kidogo kwa maeneo ya mjini, lakini katika sehemu za vijijini elimu bado inatetereka kwa kiasi kikubwa, maana teknolojia ya utandawazi katika eneo kubwa haijashamiri. Wilaya Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 7 ambazo ni: Hai, Mwanga, Moshi mjini, Moshi vijijini, Rombo na Same na ile mpya ya Siha. Majimbo ya bunge Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: Hai Siha Moshi Mjini Mwanga Same Mashiriki Same Magharibi Moshi Vijijini Vunjo Rombo Tazama pia Orodha ya milima ya mkoa wa Kilimanjaro Orodha ya mito ya mkoa wa Kilimanjaro Marejeo Viungo vya nje Matokeo ya sensa 2002 ya Tanzania kwa Mkoa wa Kilimanjaro K
2270
https://sw.wikipedia.org/wiki/Unguja
Unguja
Unguja ni kisiwa kikubwa katika Bahari Hindi mkabala wa mwambao wa Afrika ya Mashariki karibu na Dar es Salaam. Unguja ndicho kisiwa kikuu cha funguvisiwa la Zanzibar ambavyo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Unguja ina eneo la takriban km² 1.658 ikiwa na wakazi 869,721 (2012). Mji mkuu ni Jiji la Zanzibar kwenye pwani ya magharibi mkabala wa bara. Kisiwani Unguja kuna mitatu kati ya mikoa 31 ya Tanzania ambayo ni Unguja Kaskazini, Unguja Kusini na Unguja Mjini Magharibi. Tazama pia Usultani wa Zanzibar Kilwa Mji Mkongwe (Stone Town) Funguvisiwa la Zanzibar Kiunguja Orodha ya visiwa vya Tanzania Viungo vya nje Zanzinet: Unguja Island Zanzibar Yetu Zanzibar Visiwa vya Tanzania Waswahili Visiwa vya Afrika Visiwa vya Bahari ya Hindi
2271
https://sw.wikipedia.org/wiki/Zanzibar%20%28maana%29
Zanzibar (maana)
Zanzibar ni neno linalotaja Kijiografia Funguvisiwa la Zanzibar kwenye mwambao wa Afrika ya Mashariki hasa visiwa vikubwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo Nje ya Tanzania kisiwa cha Unguja mara nyingi huitwa "Zanzibar" Kihistoria Usultani wa Zanzibar iliyoanzishwa baada ya kifo cha Sultani Sayyid Said na kugawiwa kwa Usultani ya Omani mwaka 1856 wakati mwanaye Sayyid Majid alipokuwa sultani wa kwanza wa Zanzibar akitawala funguvisiwa ya Zanzibar pamoja na pwani la Afrika ya Mashariki kati ya Mogadishu (leo mji mkuu wa Somalia) na Rasi ya Delgado (leo Msumbiji ya Kaskazini karibu na mto wa Ruvuma). Kisiasa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Zanzibar ilipata uhuru kwa njia ya mapinduzi mwaka 1963 na iliungana na Tanganyika mwaka 1964 hivyo kuunda Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na waasisi walikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume. Zanzibar ina jumla ya mikoa mitano ambayo ni: Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba Jiji la Zanzibar ambalo ni mji mkubwa wa Unguja na mji mkuu wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar Jina la filamu, vitabu, hoteli n.k. zilizotajwa kufuatana na neno lenyewe kama vile Jamhuri ya Zanzibar, funguvisiwa la Zanzibar, jiji la Zanzibar n.k. Kuhusu maana ya neno lenyewe taz. "Etimolojia ya Neno Zanzibar" . Zanzibar Tanzania
2273
https://sw.wikipedia.org/wiki/Zanzibar%20%28Jiji%29
Zanzibar (Jiji)
Jiji la Zanzibar ni mji mkubwa wa kisiwa cha Unguja na mji mkuu wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Pia ni wilaya katika Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi wa Tanzania. Jiji lina wakazi 206,292 (sensa ya mwaka 2002). Jina Makala kuu: Etimolojia ya Neno Zanzibar Mji Mkongwe Kitovu cha historia yake ni Mji Mkongwe (Stone Town) ulioandikishwa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia" (World Heritage). Nyumba za Mji Mkongwe zilijengwa tangu mwaka 1830 wakati Sultani Sayyid Said alipohamisha mji mkuu wake kutoka Omani kuja Unguja. Kati ya majengo maarufu ni Beit al Ajaib (yaani Jumba la Maajabu lililobomoka tarehe 24 Desemba 2020), boma la kale, Kanisa Kuu la Kianglikana lililojengwa mahali pa soko la watumwa na hasa nyumba nyingi za kihistoria za ghorofa zilizojengwa na famila za tabaka la matajiri Waarabu zenye milango yenye mapambo mazuri. Mji Mkongwe unapokea watalii wengi kila mwaka. Mji wa kisasa umekua sana ng'ambo ya Mji Mkongwe. Tazama Pia Jamhuri ya Watu wa Zanzibar Picha Marejeo Viungo vya nje Historia na utamaduni wa Zanzibar UNESCO Stone Town Site Stone Town Conservation and Development Authority Zanzibar Urban District Homepage for the 2002 Tanzania National Census Stranger in Paradise: Searching for a Place to Call Home in Stone Town by Christopher Vourlias, World Hum, June 15, 2009 Zanzibar Stone Town & Hotels A travel guide website containing pictures and information about Stone Town as well as a selection of Stone Town Hotels. Stone Town sites and attractions Miji ya Tanzania Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi Zanzibar Waswahili
2275
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Mjini%20Magharibi
Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi
Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 71000. Mikoa mitatu kati yake iko katika kisiwa cha Unguja. Mkoa huu una wilaya mbili ambazo ndizo mjini yaani Jiji la Zanzibar na Unguja Magharibi. Mkoa una wakazi 893,169 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 . Walikuwa 593,678; Mjini wako 223,033 na Magharibi 370,645 (sensa ya mwaka 2012). Marejeo Tazama pia Orodha ya mito ya mkoa wa Unguja Mjini Magharibi Viungo vya nje U Zanzibar
2276
https://sw.wikipedia.org/wiki/Etimolojia%20ya%20neno%20Zanzibar
Etimolojia ya neno Zanzibar
Etimolojia ya neno "Zanzibar" inaonyesha ya kuwa ni jina la kale sana. Hakuna hakika kabisa kuhusu asili ya neno hilo. Etimolojia ni elimu ya asili ya maneno na uhusiano yake na maneno mengine. Asili za Kiarabu na Kiajemi Zanzibar ina uhusiano na maneno mawili ya Kiarabu. Neno la kwanza ni "zanj- ﺯﻧﺞ" lililomaanisha watu weusi au nchi ya watu weusi. Katika historia kuna kipindi cha vita ya Wazanj waliokuwa watumwa Waafrika katika Irak karibu na mji wa Basra walioasi dhidi ya mabwana wao Waarabu kati ya 869 and 879 BK wakijaribu kujipatia uhuru. Neno "zanj" linaandikwa "zang زنگ" kwa Kiajemi na zamani taarifa nyingi za Wazungu zilitumia umbo la "Zanguebar" kwa matamshi ya Kiajemi wakitaja Zanzibar. Neno la pili ni "bar - ﺑﺮ " linalomaanisha "nchi kavu" - ni asili ya neno la Kiswahili "bara". Historia ya jina Bila shaka wakazi asilia walikuwa na jina au majina yao kwa ajili ya mwambao wa Afrika ya Mashariki na visiwa. Lakini hatuna ushuhuda kuhusu majina yale yaliyotumiwa karne nyingi zilizopita. Katika taarifa ya wasafiri na wataalamu Wagiriki na Waarabu tunakuta majina yanayofanana na Zanzibar. Ptolemaio (aliishi mnamo mwaka 200 BK) alitaja rasi ya "Zingis" au "Zingisa" ((Ζίγγις ή Ζήγγισα) ambayo inaaminiwa kuwa Zanzibar; wasafiri wa baadaye walitumia jina tunalojua kutoka kwa Waarabu, kwa mfano Marco Polo aliyetaja "Zamzibar". Hatujui kama wale wageni walitumia jina walilopokea kutoka wenyeji. Azania, Zanj na Zanguebar Kwa mahitaji yetu inatosha kusema ya kwamba kuna jina la kale kwa ajili ya mwambao wa Afrika ya Mashariki lililowahi kutajwa kwa umbo tofauti katika karne za kale kama vile Zingis, Zingium, Azania, au nchi (=bar) ya „Zanj“ (kiarabu) au ya „Zangi“ (kiajemi). Wajemi na Waarabu wote walitaja pia watu weusi kwa neno hili. „Zangibar“ au „zanjbar“ ni „nchi ya watu weusi“. Wareno walianza baadaye kutofautisha kati ya bara na kisiwa wakiandika jina la kisiwa mbele ya pwani la „Zanguebar“ kama „Zanzibar“ yaani kwa namna inayolingana zaidi na matamshi ya Kiarabu lakini waliendelea kusema "Zanguebar" wakimaanisha bara. Tazama pia Makala kuhusu maana mbalimbali ya neno Zanzibar Marejeo Zanzibar Kiswahili
2306
https://sw.wikipedia.org/wiki/Pemba
Pemba
Pemba ni neno linalomaanisha Kisiwa cha Pemba ambacho ni sehemu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar katika Tanzania Pemba (Tarime) ni kata ya wilaya ya Tarime katka Mkoa wa Mara, Tanzania Pemba (Msumbiji) (zamani: "Porto Amelia"), mji wa mwambao wa Msumbiji na makao makuu ya mkoa wa Cabo Delgado Pemba (Zambia) ni wilaya na mji katika Jimbo la Kusini takriban 300 km kusini ya Lusaka Makala zinazotofautisha maana
2307
https://sw.wikipedia.org/wiki/Pemba%20%28kisiwa%29
Pemba (kisiwa)
Makala hii inahusu Kisiwa cha Pemba. Jina Pemba linatumika pia kwa ajili ya Pemba katika Msumbiji na Pemba wilaya pamoja na mji huko Zambia. Pemba ni kisiwa kilichopo takriban 50 km kaskazini ya Unguja katika Bahari Hindi. Visiwa vyote viwili ni sehemu za Jamhuri ya Watu wa Zanzibar katika Tanzania. Umbali na Tanganyika au Tanzania bara ni 50 km. Pemba pamoja na visiwa vidogo karibu nayo ina wakazi 360,797 katika eneo la 980 km². Miji muhimu ya Pemba ndiyo Chake Chake, Mkoani na Wete. Pemba kuna mikoa miwili kati ya mikoa 26 ya Tanzania ambayo ni Mkoa wa Pemba Kaskazini yenye wilaya za Wete na Micheweni. Mkoa wa Pemba Kusini yenye wilaya za Mkoani na Chake Chake. Uchumi wa Pemba ni hasa kilimo pamoja na uvuvi. Mazao ya sokoni hulimwa hasa karafuu. Katika utamaduni wa Pemba kuna desturi ya kipekee katika Afrika ndiyo mchezo wa ng'ombe iliyorithiwa na Wareno walipokuwa na athari kisiwani karne zilizopita. Viungo vya nje zanzinet.org Takwimu ya Zanzibar Wapicha Visiwa vya Bahari ya Hindi Visiwa vya Tanzania Zanzibar Visiwa vya Afrika Waswahili
2310
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mchezo%20wa%20ng%27ombe
Mchezo wa ng'ombe
Mchezo wa ng'ombe ni desturi inayojulikana hasa katika nchi za Hispania na Ureno, pia katika maeneo ya jirani ya Ufaransa kusini na katika koloni za zamani za Hispania huko Amerika ya Kilatini kama Meksiko. Imekuwa pia mila ya pekee kwenye Kisiwa cha Pemba, Tanzania. Kila mahali ni mashindano kati ya wanadamu na fahali wa ng'ombe lakini kuna taratibu tofautitofauti. Mchezo wa ng'ombe katika Hispania Katika mchezo wa Hispania fahali anauawa uwanjani. Mchezo unafanywa katika uwanja wa pekee unaoitwa Plaza de Toros. Wale wanoshindana na ng'ombe dume wanaitwa "torero"; mkuu wao atakayemwua kwa pigo la upanga wake ni "matador". Matador anatangulia kucheza na fahali kwa kumkasirisha kwa kitambaa chekundu na kutoroka akishambuliwa. Wasaidizi wake wanapita kwa farasi na kumdunga fahali kwa mikuki midogo kwa kusudi la kumdhoofisha. Mwishoni ng'ombe anauawa na matador kwa upanga. Muda wa mchezo ni kama dakika 20 kwa kila mnyama. Ilhali Wahispania wanaua ng'ombe wa dume Aareno wanawachezea tu hadi kuwaangusha chini bila kuwaua. Asili za Roma ya Kale Historia ya desturi hii inarudi nyuma hadi zamani za Dola la Roma watu walipopenda kuwa na maonyesho ya mapambano ya wanyama pori, ama ya wenyewe kwa wenyewe au zaidi ya watu dhidi ya wanyama hawa. Maonyesho haya yalifanyika katika uwanja wa mji kwa mfano uwanja wa Koloseo huko Roma. Desturi hii imepotea kila sehemu ya eneo la kale la Dola la Roma kwa sababu ilipingwa na kanisa la kikristo isipokuwa Hispania na Ureno. Mchezo wa ng'ombe Pemba kisiwani Pemba ndipo mahali pa pekee katika Afrika penye desturi hii ya mchezo wa ng'ombe. Hii ni kutokana na athira ya Ureno kwenye mwambao wa Afrika ya Mashariki miaka 400 iliyopita. Mara Wareno walikuwa na kituo huko Chake Chake, mara walikuwa na mapatano ya usaidizi na Pemba, mara waliuachia utawala Sultani wa Mombasa. Haijulikani jinsi walivyoacha desturi hii Pemba. Kuhusu mchezo huu amesema Abdullah Amur Suleiman (http://groups.msn.com/SitiBintiSaad/mchezowangombebullfight.msnw ): Viungo vya Nje Abdullah Amur Suleiman akieleza mchezo huu wa kitaifa Picha za mchezo wa ng'ombe Pemba Pemba Michezo
2315
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20ya%20kupangwa
Lugha ya kupangwa
Lugha ya kupangwa ni aina ya lugha ya kuundwa. Kwa kawaida, msemo lugha ya kupangwa unatumika kwa lugha zile ambazo ziliundwa kwa ajili ya utumiaji wa kawaida baina ya watu. Kumbe kuna lugha iliyotengenezwa ambayo si lugha ya kupangwa, kama vile lugha za uzushi na lugha za siri. Lugha ya kupangwa inayozungumzwa zaidi ni Kiesperanto. Lugha
2318
https://sw.wikipedia.org/wiki/Taasisi%20ya%20Taaluma%20za%20Kiswahili
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) ni idara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania. Taasisi hii ni miongoni mwa taasisi kongwe za lugha nchini Tanzania. Madhumuni yake yakiwa ni kusimamia usanifishaji na maendeleo ya lugha ya Kiswahili. Hadi mnamo mwaka 2009 taasisi hii ilijulikana zaidi kwa jina la TUKI au "Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili". Historia yake Ilianzishwa mnamo mwaka 1930 kama Inter-territorial Language (Swahili) committee ya Nchi za Afrika ya Mashariki, baadaye ikaitwa Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki. Mnamo mwaka 1964 kamati ilifanywa kuwa Sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaamu. Baadaye ikaitwa Chuo cha Uchunguzi wa Lugha ya Kiswahili. Tangu 1970 kimepewa jina la Taasisi ya Uchunguzi wa Lugha ya Kiswahili. Mwaka 2009, TUKI iliungana na iliyokuwa Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuunda Taasisi kubwa zaidi inayoitwa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili - TATAKI Majukumu Mwanzoni, Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili ni taasisi ya utafiti ilipewa jukumu la kutafiti nyanja zote za lugha ya Kiswahili, fasihi na utamaduni, na kuchapisha matokeo ya utafiti huo. Hivyo pamoja na BAKITA (Baraza la Kiswahili Tanzania) TUKI ndiye mlinzi wa usanifu wa lugha ya Kiswahili katika Tanzania. Baada ya kuungana na Idara ya Kiswahili, sasa TATAKI inafundisha Isimu, Fasihi na Historia ya Lugha ya Kiswahili katika Shahada za Awali, Mahiri na Uzamivu. Kazi yake Kutafiti na kuchapisha matokeo ya utafiti katika nyanja mbalimbali za Lugha, Isimu na Fasihi ya Kiswahili, TATAKI inasimamia Tafsiri na Ukalimani. Inafundisha Kiswahili kama lugha ya pili hasa kwa wageni kutoka nje ya ulimwengu wa Waswahili na kuendeleza utungaji wa Kamusi mbalimbali zinazohusiana na Kiswahili. Kati ya kamusi hizi ni Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Kamusi ya Kiingereza -Kiswahili, Kamusi ya Kiswahili - Kiingereza, Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha, Kamusi Awali ya Sayansi na Tekinologia Kamusi ya Sheria Kamusi ya Biashara na Uchumi Kamusi ya Tiba Kamusi Asisi ya Kiingereza - Kiswahili - Kiarabu Kamusi ya Biolojia Fizikia na Kemia TUKI imehariri toleo la Kiswahili la "Historia Kuu ya Afrika" iliyotungwa na kamati ya wataalamu ya UNESCO. Viungo vya nje Tovuti ya TUKI Kiswahili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kifupi
2324
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Pemba%20Kusini
Mkoa wa Pemba Kusini
Mkoa wa Pemba Kusini mi mojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 74000. Uko katika sehemu ya kusini ya Kisiwa cha Pemba ambacho ni sehemu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Makao makuu ya mkoa yako Chake Chake. Mkoa una wilaya mbili tu, Mkoani na Chake Chake Mkoa una wakazi 271,350 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 . Katika sensa ya mwaka 2012 ulikuwa na wakazi wapatao 195,116. Tazama pia Orodha ya mito ya mkoa wa Pemba Kusini Tanbihi Viungo vya nje Mkoa wa Pemba Kusini katika sensa ya 2012 P Zanzibar
2325
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Pemba%20Kaskazini
Mkoa wa Pemba Kaskazini
Mkoa wa Pemba Kaskazini ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania yenye postikodi namba 75000 . Uko katika sehemu ya kaskazini ya Kisiwa cha Pemba ambacho ni sehemu ya Zanzibar katika Muungano wa Tanzania. Mkoa una wakazi 272,091 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 . Makao makuu ya mkoa yako wilayani Wete. Mkoa una wilaya mbili tu, Wete na Micheweni. Tazama pia Mkoa wa Pemba Kusini Orodha ya mito ya mkoa wa Pemba Kaskazini Tanbihi P Mkoa wa Pemba Kaskazini Zanzibar
2326
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kaskazini
Mkoa wa Unguja Kaskazini
Mkoa wa Unguja Kaskazini ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 73000. Uko Unguja ambayo ni kisiwa kikubwa cha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Makao makuu ya mkoa yako Mkokotoni. Kuna wilaya mbili ambazo ni Kaskazini Unguja 'A' (105,780 mwaka 2012) na Kaskazini Unguja 'B' (81,675 mwaka 2012). Eneo la mkoa ni km² 470 ambako kuna jumla ya wakazi 257,290 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022. Wengi wanajishughulisha na uvuvi na kilimo. Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna kilimo cha karafuu. Upande wa magharibi utalii umeanza kuwa muhimu. Eneo la Ras Nungwi ni sehemu moja yenye mahoteli ya watalii wa nje. Kisiwa cha Tumbatu ni sehemu ya mkoa huu. Miji ya mkoa ndiyo Mkokotoni, Mahonda na Gamba. Tazama pia Orodha ya mito ya mkoa wa Unguja Kaskazini Tanbihi Viungo vya nje Dira mikoani: Kaskazini Unguja U Zanzibar
2327
https://sw.wikipedia.org/wiki/Tikisa
Tikisa
Tikisa au vibikula ni ndege wa jenasi Motacilla na Dendronanthus katika familia ya Motacillidae. Wana mkia mrefu ambao wanautikisa mara kwa mara. Ndege hao ni wadogo na wembamba na spishi kadhaa zina rangi nzuri. Hukamata wadudu ardhini na hutaga mayai 4-8 ndani ya kikombe cha nyasi ardhini. Spishi za Afrika Motacilla aguimp, Tikisa-majumba (African Pied Wagtail) Motacilla a. aguimp, Tikisa-majumba Kusi (Southern Pied Wagtail) Motacilla a. vidua, Tikisa-majumba wa Kawaida (African Pied Wagtail) Motacilla alba, Tikisa Mweupe (White Wagtail) Motacilla a. alba, Tikisa Mweupe wa Ulaya (European White Wagtail) Motacilla a. subpersonata, Tikisa wa Maroko (Moroccan White Wagtail) Motacilla a. yarellii, Tikisa Mweupe wa Uingereza (Pied Wagtail) Motacilla bocagii, Tikisa Mkia-mfupi wa Sao Tome (São Tomé Shorttail) Motacilla capensis, Tikisa Kusi (Cape Wagtail) Motacilla c. capensis, Tikisa Kusi (Cape Wagtail) Motacilla c. simplicissima, Tikisa wa Kati (Central African Wagtail) Motacilla c. wellsi, Tikisa Mashariki (East African Wagtail) Motacilla cinerea, Tikisa Kijivu (Grey Wagtail) Motacilla citreola, Tikisa Manjano (Citrine Wagtail) Motacilla clara, Tikisa-milima (Mountain Wagtail) Motacilla flava, Tikisa Njano (Yellow Wagtail) Motacilla f. beema, Tikisa wa Sykes (Sykes's Wagtail) Motacilla f. cinereocapilla, Tikisa Kichwa-kijivu (Ashy-headed Wagtail) Motacilla f. feldegg, Tikisa Kichwa-cheusi (Black-headed Wagtail) Motacilla f. flava, Tikisa Kichwa-buluu (Blue-headed Wagtail) Motacilla f. flavissima, Tikisa Utosi-njano (Yellow-crowned Wagtail) Motacilla f. iberiae, Tikisa wa Hispania (Iberian Yellow Wagtail) Motacilla f. leucocephala, Tikisa Kichwa-cheupe (White-headed Wagtail) Motacilla f. lutea, Tikisa Kichwa-njano (Yellow-headed Wagtail) Motacilla f. pygmaea, Tikisa wa Misri (Egyptian Yellow Wagtail) Motacilla f. thunbergi, Tikisa wa Thunberg (Dark-headed Wagtail) Motacilla flaviventris, Tikisa wa Madagaska (Madagascar Wagtail) Spishi za Asia Dendronanthus indicus (Forest Wagtail) Motacilla alba (White Wagtail) Motacilla a. alboides (Himalayan White Wagtail) Motacilla a. baicalensis (Baikal White Wagtail) Motacilla a. dukhunensis (Indian Pied Wagtail) Motacilla a. leucopsis (Amur Wagtail) Motacilla a. lugens (Black-backed Wagtail) Motacilla a. ocularis (Eastern White Wagtail) Motacilla a. personata (Masked Wagtail) Motacilla flava (Yellow Wagtail) Motacilla f. leucocephala (White-headed Yellow Wagtail) Motacilla f. melanogrisea (Turkestan Black-headed Wagtail) Motacilla f. plexa (North Siberian Yellow Wagtail) Motacilla f. simillima (Bering Sea Yellow Wagtail) Motacilla grandis (Japanese Wagtail) Motacilla maderaspatensis (White-browed Wagtail) Motacilla samveasnae (Mekong Wagtail) Motacilla tschutschensis (Eastern Yellow Wagtail) Motacilla t. angarensis (South Siberian Yellow Wagtail) Motacilla t. macronyx (Southeast Siberian Yellow Wagtail) Motacilla t. taivana (Green-crowned Yellow Wagtail) Motacilla t. tschutschensis (Beringian Yellow Wagtail) Picha Shomoro na jamaa
2328
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Unguja%20Kusini
Mkoa wa Unguja Kusini
Mkoa wa Unguja Kusini ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 72000 na uko kwenye kisiwa cha Unguja. Makao makuu yako Koani. Eneo la mkoa ni km² 854 likiwa na wakazi 195,873 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 . Mwaka 2012 walikuwa 115,588 katika wilaya mbili ikiwa Wilaya ya Kati ina wakazi 73,346 na Wilaya ya Kusini ina wakazi 39,242. Wakazi wa eneo hili la kisiwa cha Unguja, mbali na kujishughulisha na uvuvi kwenye Bahari ya Hindi, ni maarufu pia kwa kilimo cha zao la karafuu, zao linalokifanya Kisiwa cha Zanzibar kujulikana zaidi kama kisiwa cha viungo. Viungo vya nje U Zanzibar
2336
https://sw.wikipedia.org/wiki/Joseph%20Hill
Joseph Hill
Joseph Hill (22 Januari 1949 – 19 Agosti 2006) alikuwa mtunzi na mwimbaji wa Reggae toka nchini Jamaika. Alianza muziki katika kundi lijulikanalo kama The Soul Defender lililokuwa na makazi yake kitongoji cha St Catherine. Baadaye akaanzisha kundi la Culture akiwa na Telford Nelson na Albert Walker. Mwaka 1977 walitoa wimbo uliovuma sana uitwao Two Sevens Clash ambao ulizungumzia herufi mbili za 7 katika mwaka 1977. Hadi sasa Joseph Hill na wenzake wametoa album 22. Falsafa ya nyimbo za Joseph Hill ni ya kimapinduzi na kiroho inayopinga utumwa na ukosefu wa maadili na ucha mungu. Joseph Hill ni muumini wa imani na utamaduni wa Kirastafari. Katika wimbo wake wa wa PAY DAY anauliza ni lini watu walioumizwa na utumwa watalipwa. Pia amepinga aina zote za ukoloni na kumzumgumzia Chistopher Columbas kama muongo kwa kusema kwamba amegundua visiwa vya Jamaika ambavyo vilikuwapo tayari na watu. Joseph Hill pia anaenzi kitabu Bibilia anachoamini kuwa ni kitakatifu na amekuwa akitumia mistari na manabii toka kwenye Biblia kwenye nyimbo zake, kwa mfano wimbo wake kuhusu nabii Eliya. Viungo vya nje Tovuti ya kundi la Culture Waliozaliwa 1949 Waliofariki 2006 Wanamuziki wa Jamaika
2338
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa%20wa%20Kaskazini-Mashariki%20%28Kenya%29
Mkoa wa Kaskazini-Mashariki (Kenya)
Kaskazini-Mashariki ulikuwa mmoja kati ya mikoa 9 ya Kenya. Eneo lake lilikuwa km² 127 000 na wakazi 962,143 (sensa ya 1999). Wakati wa ukoloni eneo hilo liliitwa "Northern Frontier District" (Eneo la mpakani wa kaskazini) likitawaliwa pekee na sehemu kubwa ya Kenya. Wakazi walio wengi ni Wasomalia kwa lugha na utamaduni; kuwepo kwao ndani ya Kenya badala ya Somalia ni urithi wa mipaka ya kikoloni. Wengine ni Waborana, Warendille na Waturkana. Kuna pia makambi makubwa ya wakimbizi Wasomalia, hasa karibu na Daadab. Hali ya hewa Eneo hili ni kavu sana. Mbali na bonde la mto Tana na maeneo mengine madogo, mkoa haufai kwa kilimo. Wakazi walio wengi hujipatia riziki kutokana na ufugaji. Utawala Mkoa wa Kaskazini-Mashariki ulikuwa na wilaya nne: Garissa -- makao makuu Garissa Ijara -- makao makuu Ijara Wajir -- makao makuu Wajir Mandera -- makao makuu Mandera K
2339
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ali%20Farka%20Toure
Ali Farka Toure
Ali Farka Touré ni mmoja wa wanamuziki mahiri barani Afrika. Alizaliwa jijini Bamako nchini Mali mwaka 1939. Jina lake hasa ni Ali Ibrahim Touré. Muziki wa Ali Farka Touré ni mchanganyiko wa muziki wa asili wa Mali na muziki wa Amerika ya Kaskazini hasa blues. Touré alizaliwa katika kijiji cha Kanau katika ukingo wa mto Niger, kaskazini magharibi mwa nchi ya Mali. Mama yake alikuwa na watoto kumi ambapo ndugu zake wote walifariki wakiwa wachanga. Jina la "Farka" ni jina la utani ambalo alipewa na wazazi wake likimaanisha mnyama punda kutokana na kuwa na msimamo mkali na kiburi. Muziki wa Touré una nguvu kama za miujiza. Wapenzi wake dunia nzima wamelogwa na upigaji wake wa gitaa. Mara nyingi nyimbo zake amekuwa akiimba kwa lugha za Kisonghai, Kifula, na Kitamasheck. Albamu yake iitwayo Talking Timbukuta, ambayo aliitoa kwa kushirikiana na mwanamuziki Ry Cooder, iliuzwa na kumpatia umaarufu mkubwa hasa katika soko la muziki la nchi za Magharibi. Mwaka 2005 alitoa albamu ya In the Heart of the Moon akishirikiana na mwanamuziki Toumani Diabaté. Albamu hii ilimpatia tuzo ya Grammy. Pamoja na muziki, Ali Farka Touré alikuwa akijihusisha na masuala ya kisiasa. Mwaka 2004 alichaguliwa kuwa meya wa mji wa Niafunké. Ali Farka Touré alifariki dunia 7 Machi 2006 baada ya kuugua ugonjwa wa kansa. Albamu 1976 - Farka 1987 - Ali Farka Touré 1990 - The River (World Circuit) 1992 - The Source (World Circuit) 1994 - Talking Timbuktu (World Circuit) 1996 - Radio Mali (World Circuit) 1999 - Niafunké (World Circuit) 2004 - Red/Green - 2004 (World Circuit; remastered original albums from 1979 and 1988) 2005 - In The Heart Of The Moon Filamu Ali Farka Touré: Ça coule de source (2000). Filamu imetengenezwa na Yves Billon and Henry Lecomte. Viungo vya nje Historia fupi Historia fupi Historia fupi Historia fupi iliyoandikwa na Lucy Duran Waliozaliwa 1939 Waliofariki 2006 Wanamuziki wa Mali
2340
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rupia
Rupia
Rupia ni jina la pesa inayotumika leo huko India na katika nchi mbalimbali za Asia. Ni pia jina la pesa iliyowahi kutumika Afrika ya Mashariki na nchi mbalimbali. Jina na historia Neno "rupia" limetokana na lugha ya Kihindi cha kale "rūp" au "rūpā" linalomaanisha "fedha". Katika lugha ya Sanskrit "rupyakam" (रूप्यकम्) inamaanisha sarafu ya fedha. Hii ni asili ya "Rūpaya" iliyotumika katika India kama sarafu yenye gramu 11.66 za fedha tangu mwaka 1540. Rupia moja ilikuwa na Anna 16, Paisa 64 au Pai 192. Pesa ya kisasa Leo hii nchi zifuatazo zinatumia jina la Rupia (Rupiah, Rupee: ₨) kwa pesa zao: India Indonesia Maldivi Mauritius Nepal Pakistan Shelisheli Sri Lanka Pesa ya kihistoria Rupia ilikuwa pesa ya nchi na maeneo yafuatayo: Afrika ya Mashariki ya Kijerumani (DOA) kwa jina la "Rupie ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani" Afrika ya Mashariki ya Kiingereza Zanzibar Kwenye eneo la India ya leo katika makoloni ya nchi zifuatazo: Denmark, Ufaransa na Ureno, pia katika madola mbalimbali ya Kihindi kabla ya ukoloni na kabla ya uhuru kama vile Hyderabad. Katika nchi jirani za India kama vile Bhutan, Burma, Sri Lanka, Afghanistan Katika maeneo ya Ghuba ya Uajemi Somalia ya Kiitalia Indonesia wakati wa uvamizi wa Japan (1940-1945) Picha Pesa
2341
https://sw.wikipedia.org/wiki/Afrika%20ya%20Mashariki%20ya%20Kiingereza
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza
Afrika ya Mashariki ya Kiingereza (kwa Kiingereza British East Africa Protectorate) lilikuwa jina la eneo la Kenya lililowekwa chini ya utawala wa ulinzi wa Uingereza kuanzia mwaka 1895 hadi 1920 BK kama mtangulizi wa koloni la Kiingereza la Kenya. Historia Wakati wa mashindano ya kugawa Afrika kati ya madola ya Ulaya, Kampuni ya Kifalme ya Kiingereza kwa Afrika ya Mashariki ilianza shughuli zake katika eneo hili kwa kibali cha sultani wa Zanzibar kuanzia mwaka 1888. Kampuni hiyo ilitakiwa kuwa na mamlaka juu ya eneo hili kwa kusudi la kufanya biashara, lakini uwezo wake haukutosha kutimiza shughuli, hasa maandalizi ya kujenga reli ya Uganda kati ya Mombasa na Kampala. Baada ya kuazimia kujenga reli, Uingereza iliona haja ya kulinda eneo la reli hiyo: ndipo ikatangaza eneo lote kati ya Mombasa na Uganda kuwa chini ya ulinzi wake kuanzia tarehe 1 Julai 1895. Huo ndio mwanzo wa Afrika ya Mashariki ya Kiingereza ambaye baadaye iliitwa Kenya. Eneo hilo baadaye lilipanuliwa zaidi hadi kukutana na maeneo yaliyokuwa chini ya utawala wa Italia (Somalia) na Ethiopia upande wa Kaskazini, utawala wa ushirikiano wa Misri na Uingereza (Sudan). Upande wa kusini mpaka ulifuata mapatano na Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Mpaka na eneo chini ya utawala wa ulinzi wa Uganda ulisahihishwa mwaka 1905; hadi wakati ule sehemu kubwa ya eneo la Kenya ya Magharibi ya leo ilihesabiwa kuwa upande wa Uganda. Baada ya vita kuu ya kwanza hali ya eneo ilibadilishwa kuwa koloni la Kenya kuanzia 1920. Historia ya Kenya
2343
https://sw.wikipedia.org/wiki/Siti%20Binti%20Saad
Siti Binti Saad
Siti binti Saad (alizaliwa Fumba, Zanzibari, 1880 akapewa jina la 'Mtumwa' kwa vile alizaliwa kipindi cha utumwa wa Kiarabu. Jina la Siti alipewa na kabaila mmoja wa Kiarabu) alikuwa mwimbaji wa Zanzibar. Baba yake bwana Saadi alikuwa ni Mnyamwezi kutoka Tabora na mama yake alikuwa Mzigua toka Tanga, lakini wote wawili walizaliwa Zanzibar. Hali ya maisha ya familia yao ilikuwa ni duni sana na walijishughulisha zaidi katika shughuli za kilimo na ufinyanzi kazi ambazo Siti alijifunza na kuzimudu vizuri pia. Kama Waswahili wasemavyo "kuzaliwa masikini si kufa masikini", Siti alibarikiwa kuwa na kipaji cha pekee cha uimbaji. Kipaji hiki kilimsaidia sana tangu siku za awali ya maisha yake kwani alitumia uimbaji wake kuuza vyungu vya mama yake alivyokuwa akimsaidia kuvitembeza. Siti alipoimba sauti yake iliweza kupaa na kusafiri kwa umbali wa maili nyingi na hii ndio ilikuwa ishara ya watu kujua kwamba vyungu vya kina Mtumwa vinapita leo. Alifananishwa kuwa na mapafu yenye nguvu kama ya simba kutokana na alivyoweza kupaza sauti yake mbali na bila kuachia pumzi. Kutokana na wakati huo elimu kwa watoto wa kike kutotiliwa mkazo, Siti hakuwahi kwenda shule wala kuhudhuria mafunzo ya Kurani. Hivyo mnamo mwaka 1911 aliona ni bora ahamie mjini ili kuboresha maisha yake zaidi. Ujio wake wa mjini ulikuwa wa neema kwani alikutana na bwana mmoja wa kundi la muziki wa Taarabu la "Nadi Ikhwani Safaa" aliyeitwa Muhsin Ali. Katika kipindi hicho, hilo ndilo lilikuwa kundi pekee la muziki wa taarabu lililoanzishwa na Sultani mpenda starehe na anasa bwana Seyyid Barghash Said. Kundi hili lilikuwa ni la wanaume peke yao, wanawake hawakuruhusiwa kujiunga na vikundi vya muziki kwa vile ilikuwa ikichukuliwa kama ni uhuni. Bwana Muhsin alikiona kipaji cha pekee cha Siti na hivyo akajitolea kumfundisha kuimba kwa kufuata vyombo vya muziki na lugha ya kiarabu. Baada ya hapo alikwenda kumtambulisha kwa wanamuziki wenzie wa "Nadi Ikhwani Safaa" ambao bila kusita wakaanza kufanya naye maonyesho mbalimbali katika jamii. Walipata mialiko mingi hasa kutoka kwa Sultani na matajiri wengine wa Kiarabu, pia katika harusi na sherehe zingine mbalimbali, inasemekana ulifika wakati ambapo sherehe ilishindwa kufana kama Siti binti Saadi hakuwepo kutumbuiza. Siti alikuwa ni moto wa kuotea mbali na jina lake lilivuma kwa haraka sana hadi nje ya mipaka ya nchi na bara la Afrika. Na punde Siti alianza kufananishwa na 'Umm Kulthum', mwimbaji mahiri wa kike aliyetamba wakati huo kutoka Misri. Kama nilivyosema moto wa Siti ulikuwa si wa kuusogelea karibu, mwaka 1928 kampuni ya kurekodi muziki ya Columbia and His Master's voice yenye makazi yake Mumbai India ilisikia umaarufu wa Siti binti Saadi na hivyo ikamwalika yeye pamoja na kundi lake kwenda kurekodi kwa lugha ya Kiswahili ili kujaribu kama muziki wake utauzika. Kampuni ile haikuweza kuamini jinsi muziki ule ulivyouzika kwa kasi kubwa kwani wastani wa santuri 900 ziliweza kuuzika katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo, na hadi kufikia 1931 santuri 72,000 zilikuwa zimeuzwa. Kutokana na kusambaa kwa santuri hizi, umaarufu wa Siti ulizidi mara dufu na watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia walizuru Zanzibari kumwona. Mambo yalizidi kuwa mazuri kwa Siti hadi ikafikia hatua kampuni ya kurekodi ya Columbia kuamua kujenga studio ya kurekodi muziki palepale Zanzibar maalumu kwa ajili ya Siti binti Saadi. Hatua hiyo ya hadi kujengewa studio iliwaumiza wengi wenye wivu, hivyo wakaanza kumtungia nyimbo za kumkejeli ili kumshusha na hasa walitumia kigezo kwamba hana uzuri wa sura, nyimbo nyingi ziliimbwa lakini huu ndio uliovuma sana: Siti binti Saadi kawa mtu lini, Kaja mjini na kaniki chini, Kama si sauti angekula nini? Na yeye kwa kujua hila za wabaya wake, akaona isiwe taabu akajibu shambulio namna hii: Si hoja uzuri, Na sura jamali, Kuwa mtukufu, Na jadi kebeli, Hasara ya mtu, Kukosa akili. Kwa kujibu shambulio hilo kwa namna yake aliwafunga midomo wale wote waliokuwa wakimkejeli. Siti pia alikuwa ni mwanamke wa kwanza mwanaharakati katika kipindi chake kwa kuwatetea wanawake na wanyonge kwa ujumla, kwani katika kipindi chake watu matajiri walikuwa wakiwaonea masikini na walipofikishwa mbele ya haki waliweza kutoa hongo na kuachiwa huru halafu wewe uliyeshitaki ndiye unayefungwa. Utunzi wake wa wimbo wa Kijiti ulimpatia sifa kubwa kwani ulikuwa ukielezea kisa cha kweli kilichomkuta mwanamke mmoja mgeni kutoka bara, mwanamke huyu alipofika alikutana na Tajiri mmoja ambaye alijifanya amempenda, hivyo akamchukua na kulala naye halafu baadaye akamuua. Tajiri yule alishitakiwa na bahati nzuri walikuwepo mashahidi wawili walioshuhudia tukio lile, lakini kwa vile ni Tajiri alitoa pesa na kesi ikawageukia wale mashahidi na kufungwa. Siti akatoa wimbo huu: Tazameni tazameni, Eti alofanya Kijiti, Kumchukua mgeni, Kumcheza foliti, Kenda naye maguguni, Kamrejesha maiti. Siti aliendelea kumwambia katika nyimbo zake kwamba asijethubutu kwenda Dar es Salaam kwa maana watu wenye hasira wanamsubiri na wameapa kwa ajili yake. Siti aliendelea na shughuli yake ya muziki hadi uzeeni, muda mfupi kabla ya kifo chake alikutana na mwandishi maarufu na mwanamashairi Shaaban Robert ambaye alimhoji na kuweza kuandika wasifu wake katika kitabu alichokiita " Wasifu wa Siti binti Saadi." Wasifu huu unaonekana kuwa ndio bora zaidi uliowahi kuandikwa katika fasihi ya Tanzania. Kitabu hiki kinatumika kufundishia shule za sekondari za Tanzania. Tarehe 8 Julai 1950 Siti binti Saadi alifariki dunia na kuacha pengo kubwa katika fani ya Taarabu. Ingawa pengo hilo haliwezi kuzibika lakini kuna watu wengi walioweza kuibuka na umaarufu wa kuimba taarabu kupitia kwake, mfano hai ni Bi Kidude. Hata baada ya kifo chake jina lake bado linatumika sana kama kielelezo cha ushujaa wake, Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA), kimetumia jina lake kulipa jina gazeti la chama chao "Sauti ya Siti". Hadi leo hii Siti hutumika kama kipimo cha kufundishia uimbaji wa Taarabu. Na anakumbukwa katika historia yake ya kuwa mwanamke wa kwanza Afrika mashariki kurekodi muziki katika santuri. Viungo vya nje wasifu ya Siti binti Saad Waliozaliwa 1880 Waliofariki 1950 Wanamuziki wa Tanzania Wanawake wa Zanzibar
2345
https://sw.wikipedia.org/wiki/Rwanda
Rwanda
Kwa maana nyingine za jina hili angalia Ruanda Rwanda (zamani pia "Ruanda") ni nchi ya Afrika ya Mashariki isiyo na pwani kwenye bahari yoyote. Imepakana na Uganda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Burundi na Tanzania. Rwanda ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa na wa Umoja wa Afrika. Jiografia Rwanda huitwa nchi ya vilima elfu (kwa Kinyarwanda: Igihugu cy'Imisozi Igihumbi; kwa Kifaransa: Pays de Mille Collines): ndivyo sehemu kubwa ya eneo lake inavyoonekana, hasa magharibi. Ni nyanda za juu na milima; sehemu kubwa ni mita 1500 juu ya UB. Milima kaskazini mwa nchi inapanda hadi mita 4507 juu ya UB. Kutokana na urefu huo hali ya hewa haina joto kali. Mpaka na Kongo ni hasa Ziwa Kivu ambalo ni mojawapo kati ya maziwa ya bonde la ufa la Afrika ya Mashariki. Mpakani kwa Kongo na Uganda ndiyo milima ya kivolkeno ya Virunga. Huko kuna mazingira ya pekee duniani yenye sokwe wa milimani. Wako hatarini kuangamizwa kutokana na uwindaji na upanuzi wa mashamba unaopunguza mazingira wanamoishi. Miji Miji mikubwa zaidi ndiyo: Kigali wakazi 745.261, Butare wakazi 89.800, Gitarama wakazi 87.613, Ruhengeri wakazi 86.685 na Gisenyi wakazi 83.623.(namba za Januari 2005) Kigali ni mji mkuu wenye kiwanja cha ndege cha kimataifa na mahoteli makubwa. Gisenyi ni mji kwenye ncha ya kaskazini ya Ziwa la Kivu mpakani kwa Kongo ukiwa jirani na mji wa Goma. Kuna usafiri wa mashua kwenda Kibuye na Cyangugu. Kibuye ni mji mdogo ufukoni mwa Ziwa la Kivu. Una wavuvi wengi, kituo cha watalii na nyumba za kihistoria za wamisionari. Hadi mwaka 1994 Watutsi 250,000 waliishi katika wilaya ya Kibuye, lakini tangu uangamizaji wa Watutsi katika vita vya wenyewe kwa wenyewe wamebaki 8000 pekee. Butare ni kitovu cha utamaduni kusini mwa nchi chenye chuo kikuu. Wakazi Wakazi wa Rwanda ni zaidi ya milioni 11. Banyarwanda milioni 2 wako Uganda na wengi zaidi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Makabila Kwa kawaida vikundi vitatu hutajwa kuwa wakazi wa Rwanda ndio Wahutu, Watutsi, Watwa. Lakini kuna tofauti kali kati ya mawazo kama vikundi hivyo ni makabila, mataifa ya pekee au matabaka ya kijamii. Hali halisi wanatumia lugha ileile ya Kinyarwanda na wanafuata utamaduni uleule. Wanahistoria wengi wanasema ya kuwa Watwa walikuwa wakazi wa kwanza wakiwa wawindaji, Wahutu ndio wakulima wa Kibantu waliopatikana kwa uenezi wa Wabantu katika Afrika ya Kati na mababu wa Watutsi waliingia kama wafugaji kutoka kaskazini. Watutsi walikuwa tabaka la kikabaila, pia mfalme alikuwa Mtutsi. Lakini wengine wanaamini ya kwamba vikundi vyote vitatu vilijitokeza nchini si kama tokeo la uhamiaji mbalimbali lakini zaidi kama matabaka yaliyotofautiana kikazi: wakulima, wavindaji na wafugaji waliokuwa pia askari wa mfalme. Wakati wa ukoloni Wabelgiji walihesabu mwaka 1931 wakazi wa nchi kama ifuatavyo: 84 % Wahutu, 15 % Watutsi na 1 % Watwa. Kabla ya uhuru vilitokea kwa mara ya kwanza vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya makabila mawili makubwa viliyosababisha kupungua kwa Watutsi kutokana na mauaji na zaidi kwa Watutsi kukimbilia nchi jirani. Mnamo 1990 asilimia ya Watutsi ilikadiriwa kuwa 9 - 10 %. Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka ya 1990 vilileta uangamizaji mkubwa wa Watutsi. Kati ya asilimia 75 hadi 90 za wakazi Watutsi waliuawa katika wiki chache za mwaka 1994. Baada ya mwisho wa vita Watutsi wengi ambao wenyewe au wazazi wao walikuwa wamekimbilia Uganda na Tanzania walirudi tena Rwanda. Demografia Kwa wastani kuna wakazi 300 kwa kilomita ya mraba ambayo ni msongamano mkubwa kabisa katika Afrika. Karibu nusu ya wakazi ni watoto hadi umri wa miaka 14. Wastani wa muda wa maisha ni miaka 40 pekee. Vita vimesababisha idadi kubwa ya wagonjwa wa UKIMWI. Lugha Lugha ya taifa, lugha rasmi na lugha ya mama kwa Wanyarwanda wote ni Kinyarwanda ambayo ni lugha ya Kibantu, mojawapo ya Niger-Kongo. Mijini na sokoni Kiswahili kinatumika pia lakini si lugha asilia ya Rwanda. Lugha rasmi tangu enzi za ukoloni ni Kifaransa. Tangu mwaka 1994 serikali mpya, iliyoongozwa na Watutsi walioishi miaka mingi Uganda, imetumia pia Kiingereza kama lugha rasmi ya tatu. Dini Tazama makala Uislamu nchini Rwanda Kadiri ya sensa ya mwaka 2012 wakazi wengi ni Wakristo, hasa Waprotestanti (49.5%) na Wakatoliki (43.7%). Waislamu ni 2%. Kwa sasa serikali inazidi kufungia maabadi. Miezi saba ya kwanza ya mwaka 2018, imefungia tayari makanisa 8,000. Historia Tazama makala "Historia ya Rwanda" Rwanda ilikuwa ufalme tangu karne ya 16 kwa jina la Rwanda Rugali. Mwanzo wa karne ya 20 ilikuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na sababu ya mzozo kati ya Ujerumani na Ubelgiji. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Rwanda ikawa chini ya Ubelgiji kama eneo lindwa. Uhuru katika mwaka 1961 ulifika pamoja na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya Wahutu na Watutsi. Uhusiano kati ya vikundi hivi viwili uliendelea kuwa vigumu. Kuuawa kwa rais Juvenal Habariyama mwaka 1994 kulisababisha mauaji ya watu karibu milioni moja (walau 600,000) kati ya Watutsi, Watwa pamoja na Wahutu wasio na msimamo mkali. Kikundi cha RPF chini ya Paul Kagame kiliingia kati na kuchukua madaraka. Tangu ushindi wake wa kijeshi mwaka 1994 RPF ilianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Mwaka 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza. Rwanda pamoja na Burundi zilijiunga na Kenya, Uganda na Tanzania kama wanashirika wa Jumuia ya Afrika Mashariki kwa maendeleo muhimu katika elimu, afya, uchumi na mambo mbalimbali. Mwaka 2017 bunge la Rwanda liliamua kufanya Kiswahili kuwa moja ya lugha rasmi nchini. Vita vya Kongo vilivyokuwa na majeshi ya mataifa mbalimbali (Kivu Conflict) vilimalizika mwaka 2012. Siasa Serikali Rais na mkuu wa dola ndiye jenerali Paul Kagame (RPF). Waziri Mkuu ni Anastase Murekezi. Ugatuzi Kuanzia mwaka 2006 kuna mikoa mitano inayogawanyika katika wilaya kadhaa: Tazama pia Orodha ya Marais wa Rwanda Orodha ya Wafalme wa Rwanda Orodha ya Mawaziri Wakuu wa Rwanda Orodha ya viongozi Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Marejeo Viungo vya nje Serikali The Republic of Rwanda (official government site). Chief of State and Cabinet Members Taarifa za jumla Rwanda from UCB Libraries GovPubs. Rwanda profile from the BBC News. Utalii Rwanda Tourism (official Rwanda Tourism Board site). Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa Jumuiya ya Afrika Mashariki
2347
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi
Malawi
Makala hii inahusu nchi ya Malawi. Kwa maana mbalimbali za neno taz. Malawi (maana) Malawi (wakati wa ukoloni iliitwa Unyasa au Nyasaland) ni nchi ya bara la Afrika iliyopo kusini-mashariki, ikipakana na Tanzania, Msumbiji na Zambia. Jina la nchi limeteuliwa kutokana na ufalme wa kihistoria wa Maravi. Jiografia Sehemu kubwa ya eneo lake ni ziwa linaloitwa na majirani "Ziwa Nyasa" au "Niassa", lakini "Ziwa Malawi" hapa nchini. Kati ya Malawi na Tanzania kuna mzozo kuhusu eneo la ziwa ambao unazidi kufanyiwa kazi. Historia Wakazi wa kwanza wa Malawi walikuwa wawindaji-wakusanyaji Wasan. Katika karne ya 10 BK walifika Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi. Wengi walizidi kuelekea kusini, lakini wengine walihamia nchini. Hakuna habari za kimaandishi kabla ya kufika kwa Wazungu. Tangu karne ya 16 ufalme wa Wamaravi ulikuwepo upande wa kusini wa ziwa. Wamaravi walipanua utawala wao. Lakini katika karne ya 19 walishambuliwa sana na Wayao walioendesha biashara ya watumwa wakiwakamata katika eneo la ziwa na kuwapeleka hadi pwani ya Bahari Hindi kama vile Kilwa. Mwaka 1859 Mwingereza David Livingstone alifika ziwani. Wamisionari walimfuata, hasa Wapresbiteri kutoka Uskoti, waliotafuta wafuasi wa Ukristo na kumpambana na wafanyabiashara ya utumwa. Mwaka 1891 serikali ya Uingereza iliweka nchi upande wa magharibi na kusini kwa ziwa chini ya ulinzi wake ikawa „Nyassaland Protectorate“, halafu tangu 1907 koloni la Unyasa. Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Waingereza waliogopa kushambuliwa kutoka Afrika ya Mashariki ya Kijerumani wakachukua hatua za kudai huduma za nyongeza kutoka kwa wananchi. Hii ilisababisha ghasia ya John Chilembwe dhidi ya wakoloni. Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia Waingereza waliunganisha Unyasa na Rhodesia (leo Zambia na Zimbabwe) kuwa Shirikisho la Afrika ya Kati mwaka 1953. Shirikisho hilo halikudumu hadi mwisho wa ukoloni kutokana mielekeo tofautitofauti katika sehemu tatu za shirikisho. Katika Unyasa daktari Hastings Kamuzu Banda alijitokeza kuwa mwanasiasa aliyependelewa na wananchi wengi, akawa waziri mkuu wakati wa Unyasa kupata madaraka ya kujitawala katika mambo ya ndani na baadaye rais wa kwanza wa taifa. Mwaka 1964 Unyasa (Nyassaland) ilikuwa nchi huru kabisa lakini bado sehemu ya Jumuiya ya Madola chini ya malkia wa Uingereza kwa miaka miwili ya kwanza. Mwaka 1966 Banda alitangaza kura ya katiba mpya iliyopokewa na wananchi. Nchi ilipata jina la Malawi na chama cha Malawi Congress Party kikawa chama pekee. Banda aliendelea kutawala, akatangazwa kuwa rais kwa muda wote wa maisha yake mwaka 1971. Mabadiliko ya kimataifa baada ya kuporomoka kwa Ukomunisti na ukuta wa Berlin miaka 1989/1990 yalileta shinikizo kote Afrika dhidi ya serikali zilizofuata mtindo wa chama kimoja. Shinikizo hilo lilimkuta Banda mzee na mgonjwa ilhali watu wa familia yake wakitawala kupitia yeye. Hali ya uchumi ilikuwa duni, rushwa na magendo juu. Mwaka 1993 serikali yake ililazimishwa kukubali kura ya wananchi wote walioamua kumaliza mfumo wa chama kimoja na kuanzisha kipindi kipya. Uchaguzi huru wa mwaka 1994 ulimaliza utawala wa MCP ukamfanya Bakili Muluzi wa United Democratic Front (UDF) ndiye rais aliyechaguliwa mara ya pili 1999. Katika uchaguzi wa mwaka 2004 alishinda tena mgombea wa UDF, ndiye Bingu Mutharika aliyeapishwa kuwa rais wa Malawi tarehe 24 Mei 2004 huko Blantyre. Siasa Malawi ilikuwa na siasa ya chama kimoja chini ya rais wa kwanza Hastings Kamuzu Banda tangu kupata uhuru mwaka 1964 na masahihisho ya katiba 1966. Tangu kura ya wananchi mwaka 1993 Malawi imeanzisha mfumo wa vyama vingi vya kisiasa. Kutokana na katiba ya 1995 rais wa taifa anayechaguliwa na wananchi ndiye mkuu wa dola pia mkuu wa serikali. Makamu wa rais anachaguliwa pamoja naye lakini rais ana haki ya kumteua makamu wa pili asiyetoka katika chama chake. Mawaziri huteuliwa ama kati ya wabunge au nje ya bunge. Wabunge 193 wanachaguliwa moja kwa moja na wananchi kwa muda wa miaka mitano. Mahakama zinafuata mtindo wa Uingereza. Majaji huteuliwa kwa muda wa maisha; wanatakiwa kuwa huru na kutoathiriwa na siasa. Utawala hutekelezwa katika mikoa mitatu ya nchi zinazogawiwa katika wilaya 28. Wakuu wa mikoa na wilaya huteuliwa na serikali kuu. Mnamo Novemba 2000 palitokea uchaguzi wa kwanza wa ngazi ya chini mjini na vijijini. Utawala Serikali za mitaa zimeundwa na wilaya 28 katika maeneo matatu (Kaskazini, Kati na Kusini) yanayotawaliwa na Watawala wa Maeneo na Wakuu wa Wilaya ambao wanachaguliwa na serikali kuu. Chini ya ngazi ya wilaya kuna tarafa na vijiji vinavyoitwa maeneo madogo ya machifu. Uchaguzi wa kwanza wa Serikali za mitaa katika historia ya mfumo wa vyama vingi ulifanyika mnamo 21 Novemba 2000. UDF ilishinda asilimia 70 ya viti hivi katika uchaguzi huu. Wilaya ni hizi zifuatazo: Balaka, Blantyre, Chikwawa, Chiradzulu, Chitipa, Dedza, Dowa, Karonga, Kasungu, Likoma, Lilongwe, Machinga, Mangochi, Mchinji, Mulanje, Mwanza, Mzimba, Nkhata Bay, Nkhotakota, Nsanje, Ntcheu, Ntchisi, Phalombe, Rumphi, Salima, Thyolo, Zomba. Watu Wakazi wengi ni wa makabila ya Wabantu na wanatumia lugha za Kibantu, hasa Kichewa (zaidi ya 57%), lakini lugha rasmi ni Kiingereza. Upande wa dini, kadiri ya sensa ya mwaka 2018, wakazi wengi ni Wakristo (77.5%, kati yao Wakatoliki 17.2%), wakifuatwa na Waislamu (13.8%). Ushiriki katika Mashirika ya Kimataifa ACP, AU, AfDB, Jumuia ya Madola, CCC, ECA, Economic Commission for Africa FAO, Food and Agriculture Organization G-77, IBRD, ICAO, ICCt, ICFTU, ICRM, IDA, IFAD, IFC, IFRCS, ILO, IMF, International Monetary Fund IMO, Intelsat, Interpol, IOC, ISO (correspondent), ITU, NAM, OPCW, SADC, Southern African Development Community UNO, United Nations Organization UNCTAD, United Nations Conference on Trade and Development UNESCO, UNIDO, UNMIK, UPU, WFTU, WHO, World Health Organization WIPO, WMO, WToO, WTrO Tazama pia Orodha ya lugha za Malawi Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Viungo vya nje Government of the Republic of Malawi Official website Malawi Democrat Newspaper Lilongwe based Chief of State and Cabinet Members Malawi from UCB Libraries GovPubs Malawi profile from the BBC News Nation Malawi daily Blantyre-based newspaper Nyasa Times Online based in United Kingdom and Blantyre The Daily Times daily Blantyre-based newspaper Human Development Report 2007/2008 Maravi Post Global Lives Project video recording of 24 hours of daily life of Edith Kaphuka in Ngwale Village, Malawi Key Development Forecasts for Malawi from International Futures Love Support Unite Foundation UK-based charity organising volunteers in Malawi Malawi Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Jumuiya ya Madola Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
2351
https://sw.wikipedia.org/wiki/Msumbiji
Msumbiji
Msumbiji (pia Mozambik, kwa Kireno: Moçambique) ni nchi ya Afrika ya Kusini-Mashariki. Msumbiji iko ufukoni mwa Bahari Hindi ikipakana na Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, Afrika Kusini na Eswatini. Upande wa mashariki kuna kisiwa cha Madagaska ng'ambo ya mlango bahari wa Msumbiji. Jina la nchi limetokana na Kisiwa cha Msumbiji (kwa Kireno: Ilha de Moçambique) kilichokuwa boma na makao makuu ya Ureno kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki. Sikukuu ya Taifa ni tarehe 25 Juni, ulipopatikana na uhuru mwaka 1975. Jiografia Tambarare ya pwani ni sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, lakini kwenda kaskazini upana wake unapungua. Nyuma ya tambarare nchi inapanda hadi kufika uwiano wa tambarare ya juu ya Afrika ya Kusini. Milima mirefu zaidi inajulikana kama Inyanga yenye mita 2500 juu ya UB: iko katika jimbo la Tete inayopakana na Zimbabwe, Zambia na Malawi. Mito iko mingi, mkubwa zaidi ukiwa ndio Zambezi, halafu Ruvuma mpakani kwa Tanzania, Save na Limpopo. Ziwa la Nyassa ni sehemu ya mpaka na Malawi. Umbo la eneo la nchi ni refu sana: ni kilomita 2000 kutoka mpaka wa Tanzania upande wa kaskazini hadi Maputo iliyoko karibu na Uswazi na Afrika Kusini. Pwani ya Bahari Hindi ina urefu wa km 2.470. Miji mikubwa zaidi ni Maputo (wakazi 1.191.613), Matola (wakazi 543.907) na Beira (wakazi 530.706). Historia Wakazi wa kwanza wa Msumbiji huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani. Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi ambao walimeza wakazi wa kwanza inavyothibitishwa na DNA. Haijulikani ni lini ya kwamba wafanyabiashara Waarabu walianza kufika ufukoni na kujenga vituo na miji yao. Lakini utamaduni wa Waswahili ulifika hadi sehemu za mwambao wa Msumbiji. Hadi leo aina ya Kiswahili inazungumzwa kwenye visiwa vya Kirimba. Mto wa Zambezi ilitumika kama njia ya mawasiliano na biashara kati ya Ufalme wa Mwene Mtapa (Zimbabwe) na wafanyabiashara wa pwani. Taarifa za kimaandishi zinaanza na kufika kwa Wareno. Mwaka 1498 Vasco da Gama alifika akiwa njiani kuelekea Bara Hindi. Baadaye Msumbiji ikawa koloni la Wareno hadi mwaka 1975 vita vya ukombozi vya miaka 1964-1974 vilipomalizika kwa ushindi. Hata hivyo vilifuata vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka 1977-1992. Watu Nchini Msumbiji kuna makabila mengi sana, kama vile Wamakua, Wanyungwe, Wayao, Wamakonde na Watsonga. Kila kabila lina lugha yake, lakini lugha rasmi ni Kireno, ambacho kinaweza kuzungumzwa na 50.3% za wakazi, ingawa ni lugha ya nyumbani kwa 16.6% tu. Upande wa dini, sensa ya mwaka 2017 ilikuta 59.2% ni Wakristo (hasa Waprotestanti na Wakatoliki, ambao ni 28.4%) na 18.9% ni Waislamu. 7.3% wanafuata dini asilia za Kiafrika au nyingine. Kumbe 13.9% hawana dini yoyote, kufuatana na kampeni ya Ukomunisti ya miaka 1979-1982. Tazama pia Mikoa ya Msumbiji Orodha ya lugha za Msumbiji Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Marejeo Abrahamsson, Hans Mozambique: The Troubled Transition, from Socialist Construction to Free Market Capitalism London: Zed Books, 1995 Cahen, Michel Les bandits: un historien au Mozambique, Paris: Gulbenkian, 1994 Gengenbach, Heidi. Binding Memories: Women as Makers and Tellers of History in Magude, Mozambique. Columbia University Press, 2004. Entire Text Online Mwakikagile, Godfrey, Africa and America in The Sixties: A Decade That Changed The Nation and The Destiny of A Continent, First Edition, New Africa Press, 2006, ISBN 978-0-9802534-2-9 Mwakikagile, Godfrey, Nyerere and Africa: End of an Era, Third Edition, New Africa Press, 2006, "Chapter Seven: "The Struggle for Mozambique: The Founding of FRELIMO in Tanzania," pp. 206–225, ISBN 978-0-9802534-1-2 Newitt, Malyn A History of Mozambique Indiana University Press. ISBN 1-85065-172-8 Pitcher, Anne Transforming Mozambique: The politics of privatisation, 1975–2000 Cambridge, 2002 Varia, "Religion in Mozambique", LFM: Social sciences & Missions No. 17, December 2005 Viungo vya nje Serikali Serikali ya Msumbiji Republic of Mozambique Official Government Portal Instituto Nacional de Estatística National Statistical Office Chief of State and Cabinet Members Habari News From Mozambique from Notícias Moçambique Taarifa za jumla Mozambique Country Report Country Profile from BBC News Mozambique from UCB Libraries GovPubs Key Development Forecasts for Mozambique from International Futures Asasi zisizolenga faida UNICEF Mozambique UNICEF Mozambique Hungarian Peacekeepers in Africa and a Hungarian Perspective on the UN Mission in Mozambique Utalii Niassa Reserve Niassa National Reserve official website Msumbiji - taswira Afya The State of the World's Midwifery – Mozambique Country Profile Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Jumuiya ya Madola Nchi zinazotumia Kireno Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
2353
https://sw.wikipedia.org/wiki/Culture
Culture
Culture ni kundi la muziki ya reggae kutoka nchi ya Jamaika lililoanzishwa mwaka wa 1976. Jina la mwanzoni la kundi hilo lilikuwa ni "African Disciples". Kundi la Culture linaaminika kuwa ni kati ya makundi wanaopiga muziki halisi ya reggae yenye mafunzo na busara. Waanzilishi wa kundi hilo ni Joseph Hill, mwimbaji mwongozaji, Kenneth Dayes, mwitikiaji, na Albert Walker, mwitikiaji. Wimbo wao wa "Two Sevens Clash" uliorekodiwa mwaka wa 1977 katika studio ya Joe Gibbs, na uliwapatia umaarufu mkubwa na kuwaweka kwenye ramani ya muziki ya reggae duniani. Albamu za Culture Two Sevens Clash Harder Than the Rest Lion Rock Nuff Crisis Good Things Culture at Work Culture in Culture Three Sides to My Story International Herb Wings of a Dove Too Long in Slavery Trod On One Stone Baldhead Bridge Trust Me 17 Chapters of Culture Ras Portraits Cultural Livity: Culture Live '98 (Live) Production Something Obeah Peace and Love Cumbolo Culture in Dub: 15 Dub Shots Stoned Payday Peace and Love Humble African Live in Africa 2002 Healing of the Nations World Peace Humble African Live in Africa 2002 Healing of the Nations World Peace Rounder 2003 Viungo vya nje Tovuti ya Culture Wanamuziki wa Jamaika
2355
https://sw.wikipedia.org/wiki/True%20Jesus%20Church
True Jesus Church
True Jesus Church ni kanisa la kujitegemea la Ukristo wa Kiprotestanti lililo na asili huko Beijing, Uchina, mwaka 1917. Kanisa hilo linaamini teolojia ya "Mungu Mmoja wa Kweli". Mwenyekiti wa sasa wa TJC International Assembly aliyechaguliwa ni mhubiri Yong-Ji Lin. Uenezi Kwa sasa, kuna wanachama takriban milioni 1.5 hadi 3 katika nchi sitini na tano za mabara sita. Idadi kubwa wako ndani ya Uchina ambako si rahisi kuhakikisha idadi kamili kwa sababu TSC ni kati ya makanisa na vikundi vya Kikristo vilivyopigwa marufuku na serikali ya nchi hiyo. Tovuti za TJC katika nchi mbalimbali zinataja Wakristo 70,000 hadi 80,000 katika "nchi huru", wengi wao wakiwa na asili ya Kichina. Historia Kanisa lilianzishwa wakati wa kustawishwa kwa harakati za Kipentekoste nchini Uchina mwanzo wa karne ya 20. Harakati hizi zilianzia Marekani wakati wa mkutano wa kwanza wa Kipentekoste katika Azusa Street Revival huko Los Angeles iliyoongozwa na William J. Seymour miaka [1906]]-1908. Toka huko tapo hilo lilienea hadi Uchina. Kulikuwepo moja ya nyumba tatu za Kichina zilizotengenezwa kabla ya Chama cha Kikomunisti cha Uchina kuchukua mamlaka mwaka 1949. Kanisa lina lengo la kuhubiri injili kwa kila nchi kabla ya kurejea kwa Yesu Kristo. Tangu mwaka 2002 lilianza kuwasiliana na kikundi cha kikristo huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kilichojiunga nalo mnamo mwaka 2004. Mafundisho Wanajieleza kwamba Yesu Kristo alianzisha Kanisa moja la kimitume lililopeleka Injili katika nchi mbalimbali. Lakini Kanisa hilo likavurugika na kupatwa na imani potovu na uzushi hadi mwaka 1917 Mungu alipoamua kulifufua kwa nguvu ya Roho Mtakatifu na ndio mwanzo wa TJC. Kati ya imani nyingine za pekee ni hizi zifuatazo: Atakayebatizwa lazima akubali TJC ni Mwili wa Kristo. Wakanusha mafundisho ya Utatu wa Mungu wakisema "Yesu yu Mungu wa kweli". Wanakataza ibada za Jumapili wakidai siku ya Jumamosi ndiyo siku takatifu ya Sabato iliyoamriwa na Mungu. Hawasheherekei sikukuu za Krismasi na Pasaka kwa sababu wanaamini zina asili za kipagani na ni mifano ya imani ya Kikristo ya asili kuingiliwa na uzushi. Wanaangalia desturi ya kuosha miguu kama sakramenti iliyoamriwa na Yesu. Mafundisho mengine yanafanana na yale ya Wapentekoste, kama vile kusema kwa lugha za roho au kubatizwa kwa jina la Yesu kwa kuzamishwa chini ya maji, tena maji ya kutiririka. Imani kuu kumi za kanisa ni: Roho Mtakatifu: "kupatwa na Roho Mtakatifu ambayo huthibitishwa na uwezo wa kuongea pepo, ni hakikisho yetu ya kurithi ufalme mbinguni." Ubatizo: "Kubatizwa kwa maji ni sakramenti ya kutubu dhambi na kuzaliwa tena. Ubatizo unafaa kufanywa kwenye maji ya kawaida kama vile kwenye mto, kisima au ziwa. Mbatizaji, ambaye pia amebatizwa vilevile na kwa Roho Mtakatifu, hutimiliza ubatizaji kwa jina la Mwana Yesu Kristu. Kichwa cha Mbatizwaji hutumbUkizwa kwenya maji kukamilisha ubatizo." Kutakaswa: "Sakramenti ya kunawa miguu huwezesha binafsi kuwa na shirika na Bwana Yesu. Pia hutukumbusha mara kwa mara ni lazima tuwe na upendo, utakatifu, unyeyekevu, msamaha na utumishi. Yeyote aliyepata ubatizo wa maji ni lazima aoshwe miguu kwa jina la Yesu Kristo. Kunawishwa miguu yaweza kufanywa inapohitajika." Komunio Takatifu: "Komunio Takatifu ni sakramenti ya kusheherekea kifo cha Mola Yesu Kristu. Inatueneza kupata mwili na damu ya mwokozi wetu na kuwa na umoja naye ili tuweze kupata uzima wa milele na kufufuliwa siku ya mwisho. Sakramenti hii ina haja ya kufanywa kila iwezekanapo. Katika sakramenti hii hutumiwa mkate na divai." Sabato: "Siku ya sabato, ambayo ni siku ya saba kwenye wiki (Jumamosi), ni siku takatifu, iliyobarikiwa na kusahihishwa na Mungu Baba. Siku hii hubudiwa kwa ajili ya ukumbusho wa maumbo na pia ukombozi na Mungu Baba, na tarajio la pumziko la milele daima kwenye maisha yatakayokuja." Yesu Kristo: "Yesu Kristo, Neno aliyefanyika mwili, akafa msalabani kwa msamaha wa wenye dhambi, akafufuka siku ya tatu akapaa juu mbinguni. Yeye ndiye mwokozi wa binadamu, Muumba wa mbingu na nchi na ndiye Mungu wa kweli." Biblia Takatifu (Maandiko Matakatifu): "Biblia Takatifu, ina Agano la Kale na Agano Jipya ambayo imewezeshwa na Mungu na yenye Maandiko Matakatifu ya kweli kwa maisha ya Mkristo." Wokovu: "Wokovu unatolewa kwa neema ya Mungu kupitia imani. Waaminio lazima wamwamini Roho Mtakatifu ili kupata utakatifu, kwa kumheshimu Mungu, na kwa upendo wa watu" Kanisa: "Kanisa, lililetwa na Bwana Yesu Kristo, kupitia Roho Mtakatifu kipindi cha 'nyakati za mwisho', ni kanisa la kweli lililorejeshwa nyakati za ki'Apostoliki." Hukumu ya mwisho: "Kuja kwa Yesu kwa mara ya pili itakuwa siku ya mwisho wakati akishuka kutoka mbinguni kuhukumu: walio na haki watapokea uzima wa milele wasio na haki watahukumiwa milele" Hoja ya msingi Ingefaa ueleweke ukweli wa msimamo wa TJC kulingana na Biblia wanapodai kwa miaka mia kadhaa duniani halikuwepo tena Kanisa la kweli, wakati Yesu aliahidi, "Nipo pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari" (Mathayo 28:20). Tena "Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, wala milango ya kuzimu haitalishinda" (Mathayo 16:18). Uprotestanti
2360
https://sw.wikipedia.org/wiki/Umoja%20wa%20Afrika
Umoja wa Afrika
Umoja wa Afrika (UA) (kwa Kiingereza: African Union (AU); Kifaransa: Union Africaine (UA); Kihispania: Unión Africana (UA) ; Kireno: União Africana (UA) ) ni muungano wa nchi 55 za Afrika ulioanzishwa mnamo Julai 2002. Umoja huu unaendeleza kazi za Umoja wa Muungano wa Afrika (kwa Kiingereza: Organisation of African Union - OAU) uliokuwepo 1963 hadi 2002. Nia ya umoja huu ni kujenga muundo na mfumo wa kisiasa, wa kiuchumi, na wa kijamii ili kufikia wakati ambapo bara la Afrika litakuwa na bunge moja, benki moja, jeshi moja, rais mmoja, sarafu moja, n.k. Dhumuni kubwa la umoja huu ni kuunganisha nguvu za mataifa ya Afrika ili kuweza kutatua matatizo yanayokabili bara hili kama vile vita, njaa, Ukimwi, n.k. Nchi wanachama Umoja wa Afrika ina nchi wanachama 55, yaani nchi zote za bara la Afrika (baada ya kurudi kwa Moroko, iliyokuwa imejiondoa mwaka 1985 kwa sababu UA ilitambua Sahara ya Magharibi kuwa nchi huru wakati Moroko inadai ni eneo la majimbo yake ya kusini). Mkutano wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika ulifanyika mwaka 2004 huko Afrika Kusini. Mikutano mikuu ya UA Durban (Afrika Kusini): 9-11 Julai 2002. Maputo (Msumbiji): 10-11 Julai 2003. Sirte (Libya), mkutano wa dharura: Februari 2004. Addis Ababa (Ethiopia): 6-8 Julai 2004. Abuja (Nigeria): 24-31 Januari 2005. Sirte (Libya): 28 Jun. - 5 Julai 2005. Khartoum (Sudan): 16-24 Januari 2006. Viongozi Thabo Mbeki 9 Julai 2002 10 Julai 2003 Afrika Kusini Joaquim Chissano 10 Julai 2003 6 Julai 2004 Msumbiji Olusegun Obasanjo 6 Julai 2004 24 Januari 2006 Nigeria Denis Sassou-Nguesso 24 Januari 2006 24 Januari 2007 Jamhuri ya Kongo John Kufuor 30 Januari 2007 31 Januari 2008 Ghana Jakaya Kikwete 31 Januari 2008 2 Februari 2009 Tanzania Muammar al-Gaddafi 2 Februari 2009 31 Januari 2010 Libya Bingu wa Mutharika 31 Januari 2010 31 Januari 2011 Malawi Teodoro Obiang Nguema Mbasogo 31 Januari 2011 29 Januari 2012 Guinea ya Ikweta Yayi Boni 29 Januari 2012 27 Januari 2013 Benin Hailemariam Desalegn 27 Januari 2013 30 Januari 2014 Ethiopia Mohamed Ould Abdel Aziz 30 Januari 2014 30 Januari 2015 Mauritania Robert Mugabe 30 Januari 2015 30 Januari 2016 Zimbabwe Idriss Déby 30 Januari 2016 30 Januari 2017 Chad Alpha Condé 30 Januari 2017 28 Januari 2018 Guinea Paul Kagame 28 Januari 2018 10 Februari 2019 Rwanda Abdel Fattah el-Sisi 10 Februari 2019 10 Februari 2020 Misri Cyril Ramaphosa 10 Februari 2020 madarakani Afrika Kusini Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya UA ni N. Dlamini-Zuma. Spika wa Bunge la Umoja wa Afrika ni Roger Nkodo Dang. Tanbihi Viungo vya nje Tovuti ya Umoja wa Afrika Afrika Mashirika ya kimataifa Muungano wa Afrika
2364
https://sw.wikipedia.org/wiki/Shelisheli
Shelisheli
Shelisheli ni funguvisiwa na jamhuri katika Bahari Hindi, mashariki kwa mwambao wa Afrika Mashariki na kaskazini kwa Madagaska. Jiografia Shelisheli ina visiwa 115; 32 kati ya hivyo ni visiwa vikubwa kidogo vyenye milima, vingine ni vidogo na huitwa "Visiwa vya nje". Kisiwa kikubwa zaidi ni Mahé na mji mkuu Victoria uko huko. Wakazi wengi huishi Mahe pamoja na visiwa vya karibu, hasa Praslin na La Digue. Visiwa hivyo vina milima inayofikia hadi mita 900 juu ya UB. Mkubwa ni Morne Seychellois wenye mita 905 juu ya UB. Hali ya hewa ni ya kitropiki ikiwa halijoto iko kati ya 24 °C na 30 °C. Kiasi cha mvua ni kati ya mm 2.880 huko Victoria na mm 3.550  mlimani. Historia Hakuna hakika kuhusu wakazi wa kwanza. Inaaminika ya kwamba ndio mabaharia na wafanyabiashara Waarabu. Taarifa ya kwanza imepatikana kutoka kwa Wareno waliozunguka hapa kuanzia mwaka 1505. Kwa karne moja na nusu meli au jahazi zilipitia Shelisheli tu kwa kusudi la kuchota maji ya kunywa au kukusanya matunda bila ya kuanzisha makao ya kudumu. Majambazi wa baharini walipenda kujificha Shelisheli. Ndio Ufaransa uliojenga vituo vya kwanza vya kudumu mwaka 1756. Wafaransa waliita visiva "Seychelles" kwa heshima ya waziri wao wa siku zile Jean Moreau de Sechelles. Walowezi wao walianzisha mashamba makubwa ya mazao ya biashara wakitumia watumwa kutoka Madagaska na Afrika bara kwa ajili ya kazi yenyewe. Tangu mwaka 1814 visiwa vilikuwa chini ya Uingereza. Waingereza walivumilia walowezi na utamaduni wa Kifaransa visiwani. Kwanza Shelisheli zilikuwa zikitawaliwa pamoja na Mauritius, lakini mwaka 1903 visiwa vilipewa cheo cha koloni mbali na Mauritius. Mwaka 1970 Shelisheli walipata uhuru. Katiba ya kwanza ilifuata mfano wa Uingerezeza lakini mwaka 1979 katiba mpya ilileta mfumo wa chama kimoja. Tangu 1993 katiba ilisahihishwa tena ikiruhusu vyama vingi vya kisiasa. Chama kilichopata kura nyingi ndicho SPPF (Seychelles People's Progressive Front). Wakazi Wakazi kwa jumla (93.2%) ni machotara wenye mchanganyiko wa damu ya Afrika bara, Ulaya na Asia. Licha ya hao kuna vikundi vidogo vya Wahindi (6%), Wazungu (5%) na Wachina (0.5%) halisi. Lugha rasmi ni tatu: Kiingereza (5.1%), Kifaransa (0.7%) na Kiseselwa, aina ya Krioli ambayo imetokana na Kifaransa na ndiyo lugha ya kawaida (91%). Upande wa dini, wakazi wengi ni Wakristo, hasa Wakatoliki (76.2%), halafu Waprotestanti (13.0%), wengine wachache ni Wahindu (2.4%), Waislamu (1.6%) n.k. Uchumi Biashara ya Shelisheli inategemea hasa utalii unaoingiza 70% ya pato la taifa. Asilimia 30 hivi za wafanyakazi wote wamo katika utalii. Pamoja na utalii, uvuvi na kilimo ni muhimu pia. Tazama pia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa Demografia ya Afrika Tanbihi Viungo vya nje Serikali SeyGov, main government portal State House, Office of the President of the Republic of Seychelles Central Bank of Seychelles, on-shore banking and insurance regulator Seychelles International Business Authority (SIBA), regulator of off-shore financial sector Seychelles Investment Bureau, government agency promoting investment in the Seychelles National Bureau of Statistics, government agency responsible for collecting, compiling, analysing and publishing statistical information Serikali ya Shelisheli mtandaoni US Department of State, Background Note: Seychelles Dini GigaCatholic Taarifa za jumla Seychelles from UCB Libraries GovPubs Seychelles from BBC News Island Conservation Society, a non-profit nature conservation and educational non-governmental organisation Nature Seychelles, a scientific/environmental non-governmental nature protection association The Seychelles Nation, the largest circulation local daily newspaper Seychelles Bird Records Committee Seychelles.travel, Government tourism portal Air Seychelles, Seychelles national airline ADST interview with U.S. Ambassador to the Seychelles David Fischer Private website with tips and images Shelisheli Nchi za Afrika Umoja wa Afrika Visiwa vya Afrika Visiwa vya Bahari ya Hindi Nchi za visiwa Jumuiya ya Madola Nchi zinazotumia lugha ya Kifaransa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
2365
https://sw.wikipedia.org/wiki/Haile%20Selassie
Haile Selassie
Haile Selassie (kwa Kige'ez: ቀዳማዊ ኃይለ ሥላሴ, qädamawi haylä səllasé, [ˈhaɪlə sɨlˈlase]; 23 Julai 1892 – 27 Agosti 1975) alikuwa Kaisari au Negus Negeste wa Ethiopia. Kabla ya kuwa mfalme aliitwa Ras Tafari Makonnen. Jina lake la kifalme lina maana ya "Utukufu wa Utatu (Mtakatifu)". Pia anafahamika kwa jina la Simba wa Yuda, Mfalme wa wafalme. Alikuwa Mkristo, tena shemasi wa madhehebu ya Kanisa la Kiorthodoksi la Ethiopia. Maisha Maisha ya awali Alizaliwa katika kijiji kiitwacho Ejersa. Baba yake alikuwa kabaila Mwethiopia aliyeitwa Ras Makonnen akawa gavana wa Harar, familia yake ikiwa na watoto 11. Gavana wa mikoa Ras Tafari Makonnen alikuwa bado kijana alipopewa cheo cha gavana wa Sidamo mwaka 1907. Mwaka 1911 akarithi nafasi ya gavana wa Harar. Wakati wa ugomvi kuhusu Negus Mwislamu Lij Iyasu (1913-1916) alisimama awali upande wa mfalme lakini alifaidika zaidi na uasi uliompindua Negus. Makabaila waliomwondoa Iyasu mwaka 1916 walimteua shangazi yake Zauditu, aliyekuwa binti wa Negus Negesti marehemu Menelik II, kuwa malkia, wakaamua pia Ras Tafari awe mwangalizi wake. Mtawala na Negus Negeste Kwa njia hiyo Ras Tafari akawa kiongozi muhimu zaidi nchini. Mwaka 1928 Zauditu akampa cheo cha negus chini yake mwenyewe. Baada ya kifo cha Zauditu (1930) Ras Tafari akapokea taji na cheo cha Negus Negeste (au mfalme wa wafalme) wa Ethiopia akajiita Haile Selassie. Baada ya kupokea taji akafanya ziara Ulaya. Mwokozi wa Rastafari Habari zake zikaenea kote duniani zikasababisha kutokea kwa dini mpya ya Rastafari iliyopokea jina kutoka kwake, ingawa mwenyewe alibaki mwamini wa Kanisa la Orthodoksi, akiwa na daraja ya ushemasi. Watu weusi kisiwani Jamaika, waliokuwa wajukuu wa watumwa wenye asili ya Afrika, walisikia kwa mara ya kwanza ya kwamba Mwafrika anaheshimiwa na wafalme wa Ulaya, wakaona yeye ni mwokozi wa Mungu aliyerudi duniani kwa ajili ya watu weusi. Haile Selassie alifukuzwa katika Ethiopia mwaka 1936 Italia ilipovamia Ethiopia, akarudi 1941 kwa msaada wa Uingereza iliyoondoa Waiitalia nchini katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Sifa na kasoro za utawala wake Utawala wa Haile Selassie uliingiza Ethiopia katika Chama cha Mataifa ikiwa nchi ya kwanza ya Afrika kujiunga nacho. Baadaye ulimpa nafasi kubwa katika harakati ya uhuru wa Afrika na makao makuu ya Umoja wa Afrika yalijengwa Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia. Katika siasa ya ndani alishindwa kuendeleza nchi yake. Alikosa nguvu na nia ya kumaliza utawala wa kikabaila nchini uliosababisha umaskini mkali kati ya wakulima waliopaswa kuwaachia wakabaila sehemu ya mazao. Hivyo kimataifa Haile Selassie aliheshimiwa sana lakini ndani ya nchi maendeleo yalikwama, wanafunzi na wasomi wakikasirikia na wakulima maskini wakifa njaa mara kwa mara. Mapinduzi ya 1974 na kifo Njaa kubwa ya miaka 1972–1973 katika majimbo ya Wollo na Tigray ikafuatwa na mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 1974. Kamati ya kijeshi ya Derg ikamkamata tarehe 12 Septemba 1974. Kifo chake kikatangazwa tarehe 28 Agosti 1975 na haieleweki kama aliuawa au alikufa kutokana na ugonjwa. Baada ya kuondolewa kwa Derg mabaki ya maiti ya Kaisari yalipatikana mwaka 1992 chini ya sakafu ya choo cha jumba la kifalme alikokamatwa. Tarehe 5 Novemba 2000 mabaki hayo yalipewa mazishi ya kifalme katika kanisa kuu la Kiorthodoksi la Addis Ababa. Waliozaliwa 1892 Waliofariki 1975 Mashemasi Wafalme wa Ethiopia Viongozi wa Afrika
2367
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kenyatta
Kenyatta
Kenyatta ni jina la: Jomo Kenyatta Uhuru Kenyatta Majina ya ukoo
2368
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kampala
Kampala
Kampala ni mji mkuu wa Uganda, pia mojawapo ya wilaya za nchi. Iko karibu na ziwa kubwa la Nyanza Viktoria, mita kama 1,189 juu ya UB. Kampala ni mji mkubwa wa Uganda ikiwa na wakazi 1,208,544 (2002). UNDIO, UNEP, Benki ya Uchumi na East Africa Development Bank (EADB) zina ofisi hapa. Jina Jina la Kampala limetokana na msemo wa Kiganda "Kasozi K'Empala" wenye maana ya "kilima cha swala" kwa sababu wafalme wa Buganda walipenda kuwinda katika eneo hili. Historia Kampala ni mji ulioanza kukua sehemu za vilima mbalimbali upande wa kaskazini wa Entebbe. Kitovu cha kwanza kilikuwa nyumba ya kifalme kwenye kilima cha Kasubi iliyojengwa na Kabaka Mutesa I wa Buganda mnamo mwaka 1882. Baada ya kifo chake Mutesa ikawa kaburi la kifalme. Ikulu mpya ya Kabaka Mwanga II ikajengwa karibu kwenye kilima cha Mengo. Mwaka 1890 mwakilishi wa Kampuni ya Kifalme ya Uingereza kwa Afrika ya Mashariki (IBEA, kifupi kwa Imperial British East Africa Company), Frederick Lugard aliingilia vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya Waganda Waprotestanti, Wakatoliki na Waislamu, akajenga boma juu ya kilima kilichoitwa "Kampala" kikawa kitovu cha makao ya Wazungu katika mji mpya. Wamisionari wakapewa na Kabaka nafasi ya kujenga makanisa na nyumba zao kwenye vilima mbalimbali: Namirembe ikawa kilima cha Waanglikana, Rubaga kilima cha Wakatoliki. Waislamu walikuwa na eneo lao hasa kwenye kilima cha Kibuli. Maeneo hayo yote yaliunganika pamoja kuwa mji wa Kampala. Kati ya 1900 hadi 1905 Kampala ikawa makao makuu ya utawala wa kikoloni wa Uingereza uliohamishwa baadaye kwenda Entebbe. Baada ya uhuru ikawa mji mkuu wa kitaifa wa Uganda. Utawala wa Idi Amin na vita vya kumpindua 1979 uliharibu mengi, kwanza tabaka la wafanyabiashara Wahindi pamoja na nguvu ya kiuchumi, baadaye pia majengo. Tangu kufufuka kutoka nyakati mbaya za udikteta na vita, Kampala imeanza kukua tena. Wakazi Makerere Kampala ina Chuo Kikuu katika mtaa wa Makerere kilichokuwa chuo kikuu cha kwanza katika Afrika ya Mashariki na mahali pa mafunzo kwa viongozi wengi wa Kiafrika upande wa siasa, utamaduni na uchumi. Marejeo Viungo vya nje Tovuti rasmi Miji ya Uganda Miji Mikuu Afrika Ziwa Viktoria Africa Wiki Challenge 2021 in Tanzania
2369
https://sw.wikipedia.org/wiki/Italia
Italia
Jamhuri ya Italia (kwa Kiitalia: Repubblica Italiana) ni nchi ya Ulaya Kusini inayoenea katika sehemu kubwa ya Rasi ya Italia na baadhi ya visiwa vya jirani kwenye Bahari ya Kati. Eneo lake ni km² 302,072.84 ambalo lina wakazi 59,236,213 (31-12-2020): ni nchi ya 23 duniani kwa wingi wa watu, lakini ya 8 au 9 kwa uchumi. Mtu anayetokea katika nchi hii ya Italia kwa Kiswahili huitwa Mwitalia. Imepakana na Ufaransa, Uswisi, Austria na Slovenia. Nchi huru mbili ndogo zinazozungukwa na eneo la Italia pande zote ni San Marino na Vatikano. Makao makuu ni jiji la Roma, lenye umuhimu mkubwa katika historia ya dunia nzima. Jiografia Umbo la jamhuri, kama lile la rasi yake, linafanana na mguu linalozungukwa na maji ya Mediteraneo pande tatu. Milima ya Appennini inaunda uti wa mgongo wake, wakati ile ya Alpi, ambayo ni mirefu zaidi, inaunda kwa kiasi kikubwa mpaka kati ya Italia na nchi nyingine za Ulaya. Mlima mrefu zaidi, ukiwa na mita 4,810 juu ya usawa wa bahari, unaitwa Monte Bianco (Mlima Mweupe) na uko mpakani kwa Ufaransa. Visiwa viwili vikubwa vya Sisilia na Sardinia ni sehemu za Italia pamoja na visiwa vingi vidogovidogo, vile vya Pelagie vikiwa upande wa Afrika. Italia ina volkeno 14, ambazo 4 kati yake ziko hai: ile ndefu zaidi kuliko zote za Ulaya (mita 3,329) inaitwa Etna na iko mashariki mwa Sisilia. Italia inaongoza Ulaya kwa wingi wa matetemeko ya ardhi. Mto mrefu zaidi unaitwa Po na una urefu wa kilomita 652. Mito mingine mirefu ni Adige, Tevere, Adda, Oglio, Tanaro, Ticino, Arno, Piave, Reno, Sarca-Mincio n.k. Maziwa makubwa zaidi ni: Garda (km2 367.94), Ziwa Maggiore (212.51, likiingia Uswisi), Ziwa la Como (145.9), Trasimeno (124.29) na Ziwa la Bolsena (113.55). Kutokana na urefu mkubwa wa Italia toka kaskazini hadi kusini, hali ya hewa ni tofauti sana, kuanzia baridi kali sana hadi joto kali sana. Mikoa Historia Akiolojia imethibitisha uwepo wa Homo neanderthaliensis miaka 128,000-187,000 hivi iliyopita. Homo sapiens sapiens alifika miaka 40,000 hivi iliyopita. Kufikia milenia ya 1 KK wakazi wengi walikuwa wa jamii ya Kizungu na kutumia lugha za Kihindi-Kiulaya. Peninsula ya Italia iliunganishwa mara ya kwanza na Jamhuri ya Roma (509-27 KK), lakini hiyo ilipoenea Ulaya kusini na magharibi, Afrika ya Kaskazini na Asia ya Magharibi ikawa na sura ya kimataifa kama Dola la Roma. Umoja ulipotea kuanzia uvamizi wa jiji la Roma uliofanywa na Wagermanik (476 BK) na hasa baada ya ufalme wa Karolo Mkuu aliyetawala sehemu ya kaskazini tu. Juhudi za kuurudisha umoja zilifanywa hasa katika karne ya 19, ambapo Ufalme wa Sardinia uliteka sehemu kubwa ya Italia (hasa miaka 1860, 1866 na 1870) na kubadilika kuwa Ufalme wa Italia wenye makao makuu Roma. Baada ya vita vikuu vya pili iligeuka Jamhuri yenye katiba inayotia mamlaka kuu mikononi mwa bunge. Ni kati ya nchi sita zilizoanzisha Umoja wa Ulaya mwaka 1957 ikaendelea kuunga mkono ustawi wake hadi uanzishaji wa pesa ya pamoja (Euro). Maendeleo Italia ni kati ya nchi zilizoendelea, ikiwa na nafasi ya nane kwa nguvu ya uchumi duniani, hivyo ni mwanachama wa G7, G8 na G20. Sanaa na utalii Italia ndiyo nchi inayongoza duniani kwa kuwa na mahali pengi (51) pa kimaumbile na pa kihistoria palipoingizwa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia". Kwa sababu hiyo pia inashika nafasi ya 5 kati ya nchi zote zilizo lengo la utalii. Watu Wananchi wana sifa za pekee kati ya Wazungu wote, hata upande wa DNA, kutokana na jiografia na historia ya rasi. Ni kati ya nchi ambamo watu wanatarajiwa kuishi miaka mingi zaidi, lakini pia ni kati ya nchi ambapo uzazi ni mdogo zaidi: wanaokufa ni wengi kuliko wanaozaliwa. Kutokana na umati wa Waitalia waliohama nchi hiyo karne za nyuma, sasa zaidi ya watu milioni 60 nje ya Italia wana asili ya nchi hiyo, mbali na raia zaidi ya milioni 4 wanaoishi nje. Lugha rasmi ni Kiitalia, inayotegemea zaidi lahaja za Italia ya Kati, lakini siku hizi inatumiwa na wananchi walio wengi hata katika mikoa mingine, ambayo kwa jumla ni 20. Upande wa dini, wengi wao (81.2%) ni Wakristo wa Kanisa Katoliki, wakifuatwa na Waorthodoksi (2.8%, wengi wao wakiwa wahamiaji, hasa kutoka Romania) na Waprotestanti (1.1%, wengi wao wakiwa Wapentekoste). Uhamiaji mwingi wa miaka ya mwisho wa karne ya 20 umeleta pia Uislamu (3.7%) na dini nyingine. Dini zote zinaachiwa uhuru na, tofauti na nchi nyingi za Ulaya, waumini wake wanajitahidi kiasi kufuata ibada (29% kila wiki). Watu maarufu Fransisko wa Asizi Marko Polo Dante Alighieri Katerina wa Siena Bernardino wa Siena Kristofa Columbus Amerigo Vespucci Yohane wa Verrazzano Nikola Machiavelli Leonardo wa Vinci Michelangelo Raffaello Sanzio Karolo Borromeo Papa Pius V Galileo Galilei Amedeo Avogadro Alessandro Volta Giuseppe Verdi Giuseppe Garibaldi Yohane Bosco Antonio Meucci Papa Pius X Maria Montessori Guglielmo Marconi Benito Mussolini Enrico Fermi Papa Yohane XXIII Papa Paulo VI Pio wa Pietrelcina Carlo Rubbia Tazama pia Mikoa ya Italia Orodha ya miji ya Italia Orodha ya nchi kufuatana na wakazi Tanbihi Marejeo Viungo vya nje Online resources about Italy at UCB Libraries GovPubs Italian Higher Education for International Students Italian National and Regional parks Italian tourism official website Nchi za Ulaya Italia Nchi za G7 Nchi za G8 Nchi za G20 Nchi za Umoja wa Ulaya Mkataba wa Schengen Umoja wa Forodha wa Ulaya Maeneo ya Biblia
2373
https://sw.wikipedia.org/wiki/Gideon%20Byamugisha
Gideon Byamugisha
Gideon Byamugisha ni kasisi Mwanglikana wa Uganda na mchungaji wa kwanza Mwafrika aliyetangaza wazi ya kwamba ameambukizwa UKIMWI. Maisha Alizaliwa Buranga Ndorwa, Wilaya ya Kabale, Uganda wa Magharibi tarehe 29 Agosti 1959 akasomea ualimu kwenye Chuo Kikuu cha Makerere akamaliza kwa digrii mwaka 1985. Akaendelea kusoma digrii ya theolojia huko Nairobi akapokelewa katika utumishi wa Kanisa la Kianglikana Uganda mwaka 1991. Mwaka uleule mke wake alikufa kutokana na UKIMWI. 1992 alipokea baraka ngazi ya ukasisi akapewa jukumu la kufundisha chuo cha theolojia Mukono (sasa: Chuo Kikuu cha Kikristo cha Uganda). Wakati ule alifuata ushauri kutafuta upimaji wa damu yake ahakikishe hana UKIMWI. Alipopimwa akaonekana kuwa na viini vya HIV vilevile. Aliambiwa matokeo dakika chache tu kabla ya kuwa na somo chuoni. Aliamua kuwaambia wasikilizaji wake wakiwa na walimu wenzake ya kuwa amepatikana na HIV. Tangazo hili lilipokelewa kwa mshangao kwani katika utamaduni wa kiafrika na zaidi katika utamaduni wa kidini wa Afrika haikuwahi kutokea ya kwamba kiongozi wa kidini anasema waziwazi kuwa ameambukizwa UKIMWI. Kinyume chake mara nyingi wahubiri walitumia mfano wa UKIMWI kuonyesha ya kuwa ni adhabu kutoka Mungu na dalili ya dhambi. Gideoni Byamugisha aliitwa na kanisa lake kuanzia mwaka 1993 kusaidia katika mradi wa UKIMWI wa kanisa. 1995 - 2002 aliongoza idara wa HIV/UKIMWI ya dayosisi ya Kianglikana ya Namirembe. Mwaka 1995 alifunga ndoa mara ya pili akimwoa Pamela aliyekuwa mjane wakati ule kutokana na UKIMWI akipatikana mwenyewe na viini vya HIV. Wanalea watoto wao kutoka ndoa zote mbili za awali pia wakamzaa mtoto wa pamoja asiye na HIV kutokana na tibu la madawa ya ARV. Siku hizi (2005) Byamugisha anafanya kazi na shirika la Word Vision International pia pamoja na kasisi Jape Heath kutoka Afrika Kusini ameunda "Umoja wa viongozi wa kidini wa Afrika wanaoishi na UKIMWI" (ANERELA African Network of Religious Leaders living with HIV/AIDS). Viungo vya nje Samaritan Strategy Africa (Kiingereza) ANERELA Watch a film on Gideon Byamugisha Waliozaliwa 1959 Watu wa Uganda Ukimwi
2375
https://sw.wikipedia.org/wiki/Chuo%20Kikuu%20cha%20Makerere
Chuo Kikuu cha Makerere
Chuo Kikuu cha Makerere ni chuo kikuu cha kwanza cha Afrika ya Mashariki na chuo kikuu kikubwa cha Uganda. Kimeanzishwa wakati wa ukoloni mwaka 1922 kama shule ya ufundi kwa wanafunzi 14. Kozi za kwanza zilikuwa pamoja na useremala, ujenzi na umekanika. Shule ikawa chuo na kozi zikaongezeka kwa masomo ya utabibu, kilimo, maradhi ya wanyama na ualimu. Kuanzia mwaka 1937 chuo kilianza kozi za stashahada mbalimbali. Mwaka 1949 Makerere ikawa chuo kishiriki cha Chuo Kikuu cha London kikitoa shahada ya kwanza ya ngazi ya chuo kikuu. Mwaka 1963 ikawa sehemu ya Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki pamoja na kampasi za Dar es Salaam na Nairobi. Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki kimegawiwa mwaka 1970 kutokana na kufifia kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Makerere ikawa Chuo Kikuu cha kitaifa cha Uganda. Chuo cha Viongozi Makerere ilikuwa chuo waliposoma viongozi wengi wa Afrika, wakiwa pamoja na marais wa zamani Milton Obote (Uganda), Julius Nyerere na Benjamin Mkapa (Tanzania) na Mwai Kibaki (Kenya). Baada ya uhuru Makerere ilikuwa pia mahali pa majadiliano na mafunzo ya utamaduni wa Kiafrika. Waandishi na walimu muhimu wa Kiafrika walianzisha mafunzo yao au walifundisha kwa muda fulani Makerere kama vile Nuruddin Farrah, Ali Mazrui, David Rubadiri, Okello Oculi, Ngugi wa Thiongo, John Ruganda, Paul Theroux na Peter Nazareth. Idara Makerere ina idara 22 zinazohudumia wanafunzi 30,000 hivi, wakiwemo 3,000 wa kozi za shahada za ngazi ya juu. Vitivo Kitivo cha Kilimo Kitivo cha Fani Kitivo cha Elimu Misitu na Hifadhi la Mazingira Kitivo cha Sheria Kitivo cha Uganga Kitivo cha Sayansi Kitivo cha Sayansi Jamii Kitivo cha Teknolojia Kitivo cha Elimu ya Maradhi ya Wanyama Taasisi Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Taasisi ya Sayansi ya Kompyuta Taasisi ya Uchumi Taasisi ya Mazingira na Mali Asili Taasisi ya Uchunguzi wa Kijamii Taasisi ya Takwimu na Saikolojia Vyuo Chuo cha Ualimu Chuo cha Sanaa Chuo cha Sayansi za Maktaba na Habari Chuo cha Biashara Chuo cha Mafunzo baada ya Digrii ya Kwanza Idara Idara ya Teknolojia ya Kompyuta na Habari Kampasi Makerere - Kikara Makerere - Kabanyoro Makerere - Katumani Wanafunzi waliopitia Chuo Kikuu cha Makerere John Sentamu, Askofu Mkuu wa York, askofu mkuu Mwafrika wa kwanza katika Kanisa la Uingereza Okello Oculi, mwandishi, mshairi Peter Nazareth, mwandishi David Rubadiri, mwandishi na mshairi wa Malawi Benjamin Mkapa, alikuwa rais wa Tanzania Joseph Kabila, rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Specioza Kazibwe, mwanamke wa kwanza kuwa makamu wa rais wa Uganda (1994-2003) Julius Nyerere, alikuwa rais wa Tanzania Milton Obote, alikuwa rais wa Uganda Sir Frederick Edward Mutesa II, alikuwa Kabaka wa Buganda Mwai Kibaki, alikuwa rais wa Kenya (alikuwa pia mwalimu Makerere) Ngugi wa Thiongo, mwandishi (alikuwa pia mwalimu Makerere) Jaramogi Oginga Odinga, mwanasiasa na makamu wa rais wa Kenya (1964-1966) Okot p'Bitek, mshairi na mwandishi (alikuwa pia mwalimu Makerere) Chege Joseph Macharia, mwalimu wa Kiswahili Don Gasangwa, siasa ya Eacu Helen Akwi, mwandishi wa hadithi Viungo vya nje Tovuti rasmi Kampala Vyuo vikuu vya Uganda
2377
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ngugi%20wa%20Thiongo
Ngugi wa Thiongo
Ngũgĩ wa Thiong'o (amezaliwa 5 Januari 1938) ni mwandishi Mkenya aliyeandika kwa Kiingereza lakini siku hizi anatumia lugha ya Gikuyu. Maandishi yake ni pamoja na riwaya, tamthilia, hekaya, insha na uhakiki. Ameanzisha gazeti la lugha ya Gikuyu Mũtiiri. Tangu mwaka 1982 ameishi nje ya Kenya akifundisha kwenye vyuo vikuu mbalimbali kama Yale, New York na Irvine/California. Masomo Ngugi amezaliwa Kenya katika kijiji cha Kamiriithu karibu na Limuru, wilaya ya Kiambu katika jamii ya Wagikuyu akabatizwa James Ngugi. Alikuwa mtoto wa tano wa mke wa tatu wa baba yake Thiong'o wa Nducu. Baba alikuwa mkulima aliyepotea shamba lake kutokana na Waingereza kuteka na kutwaa Nyanda za Juu za Kenya. James alisoma shule za wamisionari za Kamaandura (Limuru), Karinga (Mangu) na Alliance High School (Kikuyu). Katika miaka ile akawa Mkristo. Wakati alikisoma shule familia yake iliathiriwa na vita ya Maumau ikawa kaka yake aliuawa na mama yake aliteswa. Baada ya kumaliza Alliance High akasoma Makerere akahitimu kupata digrii ya Kiingereza mwaka 1963. Akafunga ndoa na Nyambura mwaka 1961 akazaa naye watoto sita katika miaka iliyofuata. Mwaka 1962 aliandika tamthilia yake ya kwanza "The Black Hermit". Baada ya digrii alirudi Nairobi alipofanya kazi ya uandishi wa gazeti. Riwaya za kwanza 1964 akachukua nafasi ya masomo huko Chuo Kikuu cha Leeds. Hapo Uingereza alitunga riwaya ya "WEEP NOT, CHILD" (1964) akiwa mwandishi wa kwanza kutoka Afrika ya Mashariki aliyetunga riwaya kwa Kiingereza. Alisimulia hadithi ya kijana Njoroge mwenye ndoto ya kuendeleza elimu yake lakini anakwama kati ya ndoto zake na hali halisi ya maisha ya Kiafrika chini ya ukoloni. Aliendelea kwa "THE RIVER BETWEEN" (1965) akichora picha ya kijiji kilichopasuliwa kati ya wakristo na wafuasi wa dini ya asili. 1967 alitumia historia ya vita ya Maumau na maarifa ya familia yake kwa ajili ya riwaya ya "A GRAIN OF WHEAT". Mwaka uleule baada ya kuchukua digrii ya pili alirudi Kenya akifundisha Chuo Kikuu cha Nairobi 1967-1969. Aliondoka kwa sababu alipinga kuingia kwa siasa ya serikali katika mambo ya chuo. Baada ya mwaka moja huko Makerere alipata nafasi ya kufundisha Marekani kwenye Chuo Kikuu cha Evanston (1970-71). Mwaka 2013 akatunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) nchini Tanzania. Profesa wa fasihi Nairobi 1973 alirudi Nairobi kama Profesa wa Kiingereza na mwenyekiti wa idara ya fasihi. Idara hii ilianzishwa kutokana na upinzani wa Ngugi na wenzake dhidi ya hali ya Kiingereza kuwa nguzo kuu ya elimu katika Afrika. Katika makala 'On the Abolition of the English Department' aliyoandika 1968 pamoja na Taban lo Liyong na Henry Owuor-Anyumba, aliwahi kuuliza "Tukihitaji kutazama historia ya utamaduni mmoja kwa undani kwa ajili ya masomo yetu, kwa nini tusichague utamaduni mmoja wa Kiafrika na kuupa kipaumbele ili tulinganishe tamaduni mbalimbali nao?" Kutokana na msimamo huo aliendelea kutafiti fasihi ya simulizi ya makabila ya Kenya, hasa ya Wagikuyu na fasihi ya Kiswahili. Katika miaka hii huko Nairobi Ngugi aliamua hawezi kuwa tena mkristo. Mwaka 1976 akabadilisha jina lake kutoka James Ngugi kuwa Ngugi wa Thiong'o. Fasihi simulizi na gereza Kazi yake ya kifasihi ilimpeleka katika mzozo na serikali. Kuanzia mwaka 1976 Ngugi alishirikiana na wanakijiji Wagikuyu karibu na Limuru kuanzisha maagizo ya tamthilia katika lugha yao. 1976 riwaya yake ya "PETALS OF BLOOD" ilichora picha ya watawala wapya Waafrika jinsi walivyochukua nafasi ya wakoloni wa awali wakidharau na kukandamiza wananchi. Mwaka uleule aliandika tamthilia ya "Ngaahika Ndeenda" (Nitaolewa nitakapopenda). Wakubwa katika serikali walikuwa na wasiwasi wakiogopa mwelekeo wa kimarxist wa Ngugi hasa alipotoka katika Chuo Kikuu na kuingia kati ya wananchi wa kawaida kwa njia ya maigizo yake katika lugha ya Gikuyu. Makamu wa Rais wa Kenya Moi aliamua kumkamata Ngugi kwa misingi ya sheria ya usalama wa kitaifa wakati Rais Jomo Kenyatta mwenyewe tayari alikuwa amedhoofika kutokana na uzee na ugonjwa. Ngugi alikaa mwaka mmoja katika gereza la Kamiti akaandika riwaya ya kwanza kwa Gikuyu "Caitaani mũtharaba-Inĩ" (Shetani msalabani) akitumia karatasi ya choo. Baada ya kuachichwa huru hakuruhusiwa kurudi kazini kwenye Chuo Kikuu. Mwaka 1982 aliondoka Kenya kwenda London. Maandishi ya baadaye Ngugi ameendelea kutumia Gikuyu pekee kwa ajili ya riwaya lakini amefundisha na kutunga insha kwa Kiingereza. Kati ya maandiko yaliyofuata ni "Detained" (Daiari ya gerezani - 1981); "Decolonizing the Mind: The Politics of Language in African Literature" (Kuondoa ukoloni rohoni - siasa ya lugha katika fasihi ya Afrika 1986) alimodai waandishi Waafrika watumie lugha zao za kienyeji badala la lugha za Kiulaya; Matigari (1987) alimotumia hadithi ya kiutamaduni wa Gikuyu. Mwaka 2004 Ngugi alirudi mara ya kwanza Kenya lakini alipata maarifa mabaya akishambuliwa na wahuni na kuibiwa mali mke wake akibakiwa. Shabaha muhmu wa ziara yake ilikuwa kutangaza riwaya yake mpya kwa Gikuyu "Muroogi wa Kigogo". Kiini cha imani ya Ngugi ni ya kwamba kwa kutumia lugha za kienyeji pekee waandishi waafrika watafikia wanachi wa kawaida na kushinda ukoloni mamboleo rohoni. Tatizo alilo nalo hapo ni ya kwamba lugha za kienyeji zinarudi nyuma haraka katika mazingira ya kisasa hata zikiendelea kuzungumzwa na kusikilizwa kwa redio si lazima zinasomwa pia. Tuzo na heshima 1973: Lotus Prize for Literature 2001: Nonino International Prize for Literature 2009: Shortlisted for the Man Booker International Prize 2012: National Book Critics Circle Award (finalist Autobiography) for In the House of the Interpreter 2014: Nicolás Guillén Lifetime Achievement Award for Philosophical Literature 2016: Park Kyong-ni Prize Shahada za heshima University of Auckland, Honorary doctorate of Letters (LittD), 2005 University of Dar es Salaam, Honorary doctorate in Literature, 2013 University of Bayreuth, Honorary doctorate (Dr. phil. h.c.), 2014 Yale University, Honorary doctorate (D.Litt. h.c.), 2017 Maandishi Vitabu vya hadithi Weep Not, Child, (1964) The River Between, (1965) A Grain of Wheat, (1967, 1992) Petals of Blood (1977) Caitaani mutharaba-Ini (Devil on the Cross, 1980) Matigari ma Njiruungi, 1986 (Matigari, translated into English by Wangui wa Goro, 1989) Mũrogi wa Kagogo (Wizard of the Crow, 2004) Mkusanyiko wa hadithi fupi A Meeting in the Dark (1974) Secret Lives, and Other Stories, (1976, 1992) Tamthiliya The Black Hermit (1963) This Time Tomorrow (three plays, including the title play, "The Rebels", and "The Wound in the Heart") (c. 1970) The Trial of Dedan Kimathi (1976) Ngaahika Ndeenda: Ithaako ria ngerekano (I Will Marry When I Want) (1977, 1982) (with Ngugi wa Mirii) Insha Homecoming: Essays on African and Caribbean Literature, Culture, and Politics (1972) Writers in Politics: Essays (1981) ISBN 978-0-85255-541-5 (UK) Decolonising the Mind: The Politics of Language in African Literature (1986) Moving the Centre: The Struggle for Cultural Freedom (1993) Penpoints, Gunpoints and Dreams: The Performance of Literature and Power in Post-Colonial Africa (The Clarendon Lectures in English Literature 1996), Oxford University Press, 1998. Kumbukumbu Detained: A Writer's Prison Diary (1981) Dreams in a Time of War: a Childhood Memoir (2010) In the House of the Interpreter: A Memoir (2012) Birth of a Dream Weaver: A Memoir of a Writer's Awakening (2016) Kazi nyingine Education for a National Culture (1981) Barrel of a Pen: Resistance to Repression in Neo-Colonial Kenya (1983) Mother, Sing For Me (1986) Writing against Neo-Colonialism (1986) Something Torn and New: An African Renaissance (2009) "Queries over Ngugi's appeal to save African languages, culture", Daily Nation, Lifestyle Magazine, 13 June 2009. Vitabu vya watoto Njamba Nene and the Flying Bus (Njamba Nene na Mbaathi i Mathagu, 1986) Njamba Nene and the Cruel Chief (Njamba Nene na Chibu King'ang'i, 1988) Njamba Nene's Pistol (Bathitoora ya Njamba Nene, 1990) Tanbihi Viungo vya nje Tovuti rasmi Ngũgĩ wa Thiong'o Biografia na orodha ya vitabu vyake Fasihi ya Afrika Waandishi wa Kenya Fasihi ya Kiingereza
2378
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ngugi
Ngugi
Ngugi ni jina la mwanaume katika lugha ya Gikuyu ya Kenya. Ngugi anayejulikana hasa ni mwandishi Ngugi wa Thiongo.
2379
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilwa%20Kivinje
Kilwa Kivinje
Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Kilwa Kilwa Kivinje ni mji mdogo katika Wilaya ya Kilwa ufukoni wa Bahari Hindi. Kiutawala ni sehemu ya kata ya Kivinje Singino. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, mji ulilikuwa na wakazi wapatao 15,061. Msimbo wa posta ni 65402. Historia Wakati wa utawala wa Zanzibar ilikuwa makao ya liwali ya Sultani kwa ajili ya pwani la kusini la Tanganyika ikichukua nafasi ya Kilwa Kisiwani kama bandari muhimu katika sehemu hii ya pwani la kusini. Kivinje ilikuwa lengo la misafara ya watumwa katika kusini ya Tanzania. the mainland port of Kilwa Kivinje supplanted Kisiwani as the terminus of the southern slave caravan. Bandari yake ya mchanga ilifaa kwa maboti madogo ya ubao waliobeba watumwa Zanzibar. Kuna makadirio ya kwamba watumwa 20,000 walipita Kivinje kila mwaka. Mnamo mwaka 1850 Kivinje ilikuwa mji wa wakazi 12-15,000 pamoja na wanfanyabiashara wenye asili ya Uhindini. Baada ya Sultani wa zanzibar kupiga biashara ya watumwa marufuku Kivinje ilijulikana kwa kuendelea na biashara hii kwa siri. Zanzibar ilimkamata sulatani wa mwisho wa Kivinje na kumtuma nje ya mji. Ilikuwa makao makuu ya wilaya tangu zamani ya ukoloni wa Kijerumani. Wakati wa vita ya Abushiri iliona mapigano dhidi ya Wajerumani na wawakilishi wa Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki waliuawa tar. 22 Septemba 1888. Mei 1890 Wajerumani walirudi chini ya meja Hermann von Wissmann wakateka mji bila upinzani. Wakati wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani Kilwa Kivinje ilikuwa makao makuu ya mkoa wa nane iliyoenea kati ya Rufiji na Lindi. Utawala wa Kijerumani kilikwisha tar. 7 Septemba 1916 siku ambako Wajerumani waliobaki mjini walijisalimisha mbele ya kikosi cha wanamaji Waingereza. Mji uliendelea kuwa makao makuu ya wilaya chini ya Waingereza. Hali ya mji leo Tangu kuondoka kwa makao makuu ya wilaya mji umerudi nyuma. Nyumba za ghorofa za wafanyabiashara hazitumiki tena zimeanza kuporomoka. Boma la Kale la Wajerumani bado linatumika. Hospitali ya wilaya imebaki Kilwa Kivinje. Bandari ndogo inafaa kwa jahazi tu. Eneo la kihistoria lina magofu ya majengo ya Waswahili ya enzi za kati na baadhi ya majengo ya kiswahili yaliyosalia kutoka mwishoni mwa karne ya 19. Makazi haya yanachukuliwa kama kimbilio la wenyeji wa awali kutoka Kilwa Kisiwani ambao walikuwa wakimbizi kutoka kwa Vasco da Gama ambae alikuwa akiwafukuza mji huo mnamo 1505 na pia kuwachukua kama wakimbizi waliokimbia maharamia wa Madagaska mnamo 1822. Viungo vya nje Taarifa ya serikali ya Ujerumani juu ya uasi mjini Kilwa (1888) Picha za kilwa Kivinje wakati wa Wajerumani, pamoja na Boma (Kaiserliches Bezirksamt), Boma na Hospitali (Gruppe von Menschen vor der Boma und dem Hospital von Kilwa-Kivinje), Kikosi cha askari(Station Kilwa), Posta (Kais. Post, Akazienstrasse), Nyumba ya wanfanyabiashara de Souza (Haus der Firma de Souza jr. Dias & Co;) Marejeo Wilaya ya Kilwa Kata za Mkoa wa Lindi Miji ya Tanzania Waswahili
2380
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wilaya%20ya%20Kilwa
Wilaya ya Kilwa
Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Kilwa Wilaya ya Kilwa iko katika Mkoa wa Lindi, takriban kilometa 220 kusini mwa Dar es Salaam. Kilwa imepakana na Mkoa wa Pwani upande wa kaskazini, Bahari ya Hindi upande wa mashariki, wilaya ya Lindi Vijijini upande wa kusini na wilaya ya Liwale upande wa magharibi. Wakati wa sensa ya nwaka 2012, wilaya hii ilikuwa na wakazi 190,744 (mwaka 2002 waliohesbiwa 171,850 ). Makao makuu ya wilaya ni Kilwa Masoko. Historia Wilaya hii ina sehemu za kihistoria ambazo ni hasa Kilwa Kisiwani - ambayo ni mfano bora wa miji ya Waswahili wa kale uliojulikana kimataifa tangu karne ya 13 BK Kilwa Kivinje - iliyokuwa makao makuu ya eneo chini ya masultani wa Zanzibar na wakati wa ukoloni Songo Mnara - maghofu ya mji wa Waswahili wa kale Uchumi Wakazi wengi hutegemea kilimo na uvuwi. Mazao yanayolimwa hasa ni pamoja na muhogo, mahindi, mtama na mpunga. Hata hivyo uzalishaji wa chakula hautoshelezi mahitaji ya wakazi. Sababu za upungufu ni kuongezeka kwa watu pamoja mitindo ya kilimo cha kimila ambako mashamba ni madogo, kwa wastani ekari 2, yakilimwa kwa mkono tu. Sehemu kubwa za wilaya kuna ardhi isiyo na rutba kubwa ambayo haushiki maji vizuri. Penye udongo mweusi mzuri karibu na Makangaga, Liwiti, Matandu, na Mbwemkuru inawezekana kulima mpunga. Kuna maeneo katika Milima ya Matumbi ambako miti ya matunda kutunzwa, hasa minazi na michungwa. Karibu na Likawage, Nanjirinji, Nainokwe, Njinjo na Singino Hill watu wanavuna pia korosho. Upatikanaji wa inzi za tsetse ni kizuizi kwa ufugaji. Kuna pia majaribio ya kupana vchaka vya Jatropha curcas kama zao la nishati. Gesi asilia huzalishwa kwenye Kisiwa cha Songosongo. Gesi hii inapelekwa hasa Dar es Salaam kwa uzalishaji wa umeme; lakini kuna pia kituo cha umeme kinachoendedhwa na gesi ya Songosongo kilichopo kwenye kata ya Somanga kikihudumia wilaya hii. Utawala Wilaya hii ina kata zifuatazo (idadi ya wakazi 2012 katika mabano): Chumo (13,879), Kandawale (5,040), Kibata (8,730) Kijumbi (14,426), Kikole (4,294), Kilwa Kivinje Singino (19,376), Kilwa Masoko (13,601) Kipatimu (14,606), Kiranjeranje (9,752), Lihimalyao (10,434), Likawage (3,569 Mandawa (13,192), Miguruwe (3,381), Mingumbi (9,948), Miteja (6,157), Mitole (3,352), Nanjirinji (7,491), Njinjo (8,904), Pande Mikoma (11,569), Songosongo (3,062), Tingi (6,782), Kata za Namayuni na Somanga zilianzishwa baada ya sensa ya 2012 kwa hiyo hakuna namba za kulingana. Tanbihi Viungo vya nje Sensa ya Tanzania ya 2002 K
2381
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kilwa%20Masoko
Kilwa Masoko
Kwa matumizi mengine ya jina hili tazama Kilwa [[Picha: Kilwa Masoko ni mji mdogo katika Tanzania ikiwa makao makuu ya Wilaya ya Kilwa tangu miaka ya 1960. Iko barani ikitazama Kilwa Kisiwani. Mji ni wa kisasa. Kuna uwanja mdogo wa ndege pia bandari ndogo yenye kituo cha forodha. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 13,601 Msimbo wa posta ni 65408 walioishi humo. Marejeo Wilaya ya Kilwa Kata za Mkoa wa Lindi
2382
https://sw.wikipedia.org/wiki/Wilaya%20ya%20Pangani
Wilaya ya Pangani
Wilaya ya Pangani ni kati ya wilaya za Mkoa wa Tanga katika Tanzania yenye Postikodi namba 21300. Imepakana na wilaya ya Muheza upande wa Kaskazini, Wilaya ya Handeni upande wa magharibi, wilaya ya Bagamoyo (Mkoa wa Pwani) upande wa kusini na Bahari Hindi upande wa mashariki. Makao makuu ya wilaya yako Pangani mjini. Wilaya ina wakazi 54,025 (2012) katika tarafa 4, kata 14 na vijiji 33. Ina shule za msingi 35, shule za sekondari 10 na zahanati 16. Eneo la wilaya ni kama kanda linalofuata ufuko wa Bahari Hindi. Mji wa Pangani upo mdomoni mwa mto Pangani unaoingia ndani ya nchi kavu kwa umbo la mlango mpana. Maeneo yaliyo karibu zaidi na bahari yenye ardhi ya rutuba kuna kilimo cha korosho, nazi, mihogo, mahindi, viazi vitamu na ndizi. Maeneo ya ndani zaidi pasipo rutuba sana kuna mashamba ya katani na mahindi. Kihistoria mazingira ya Pangani ni kati ya maeneo ya utamaduni wa Uswahilini; kabla ya ukoloni kulikuwa na mashamba ya Waarabu waliotumia watumwa na tangu kufika kwa ukoloni wa Kijerumani mashamba makubwa ya katani yalianzishwa. Wilaya hii ilikuwa pia nyumbani ya Abushiri ibn Salim al-Harthi na chanzo cha vita ya Abushiri dhidi ya utawala wa Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki. Tazama pia Mkoa wa Pangani Marejeo na Viungo vya Nje Taarifa (profile) ya wilaya ya Pangani mnamo mwaka 2011 P
2383
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Rwanda
Historia ya Rwanda
Historia ya Rwanda inahusu eneo la Afrika Mashariki ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Rwanda. Historia ya kale Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani. Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi. Rwanda ilikuwa eneo penye utawala wa kifalme tangu karne nyingi kabla ya kufika kwa ukoloni. Mwanzo wake ni katika eneo la Ziwa la Muhazi. Watawala wenye cheo cha "mwami" kutoka kikundi cha wafugaji (Watutsi) walisambaza eneo lao tangu miaka ya karne ya 16 BK hadi kufika eneo la leo. Wafugaji wa ng'ombe Watutsi walikalia nchi pamoja na wakulima wa Kihutu na wavindaji Watwaa. Ukoloni wa Kijerumani Ukoloni ulichelewa kufika Rwanda; mwaka 1890 Ujerumani na Uingereza walipatana ya kuwa Rwanda na Burundi ni sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Lakini ilikuwa mwaka 1908 tu ya kwamba Wajerumani walimtuma afisa wa kudumu aliyekaa Rwanda kama mwakilishi wa serikali ya Ujerumani. Mwaka 1916 Ubelgiji na Uingereza walivamia Rwanda katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baadaye ikawa chini ya Ubelgiji pamoja na Burundi kama "Rwanda-Urundi" katika hali ya eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa. Ukoloni wa Ubelgiji Utawala wa Wabelgiji ilikuwa ya moja-kwa moja na kali zaidi kuliko Wajerumani. Wabelgiji walijaribu kutoa faida ya kiuchumi wakilazimisha wenyeji kupanda mikahawa na kutekeleza kazi za serikali ya kikoloni. Katika utawala wao Wabelgiji walitumia zaidi Watutsi wakiwapa nafasi za elimu na kuwatumia katika shughuli za serikali. Wataalamu wengine huamini ya kwamba siasa hii ilisababisha kukua kwa chuki dhidi ya Watutsi kwa upande wa wakulima Wahutu iliyoleta kumwaga kwa damu baadaye. Katika miaka ya 1950 ilionekana ya kwamba ukoloni unaelekea mwisho wake. Uhusiano kati ya Wahutu na Watutsi ukawa vigumu kwa sababu Wabelgiji walibadilisha siasa yao yakupendelea Watutsi wakidai haki zaidi kwa ajili ya Wahutu wliokuwa wengi. Ni hasa wamisionari wa katoliki Mapadre Weupe waliosimama upande wa Wahutu wakiona ndio wagandamizwa. Mwami Mutara Rudahigwa aliyejiita pia Charles alijaribu kuleta upatanishi kati ya vikundi katika nchi. Mwaka 1954 aligawa nchi ya kifalme kati ya Wahutu na Watutsi. Lakini alikuwa na wapinzani Watutsi waliomwua mwaka 1959. Mtoto wake Mwami Kigeri V aliwekwa kwenye kiti chake. Tendo hili lilisababisha ghasia na vurugu nchini kwa sababu Wahutu walidai kuwa na neno katika mabadiliko ya serikali. Mwezi wa Novemba 1959 Mwami Kigeri V. alilazimishwa kuondoka nchini akikimbilia Uganda. Watutsi wenye siasa kali walijaribu kumwua kiongozi wa Mouvement Democratique Republicain (MDR) chama kikubwa cha Wahutu. Wahutu walijibu kwa kuwashambulia na kuua Watutsi. Wabelgiji walitumia wanajeshi wao kupoza hali nchini. Katika uchaguzi wa kwanza wa halmashauri ya tarafa na miji kabla ya uhuru ndicho chama cha Parmehutu kilichopata kura nyingi. Viongozi wa Parmehutu walitangaza serikali mpya mwaka 1961. Uchaguzi wa Bunge ulileta kura ya 77% kwa ajili ya chama cha Parmehutu kilichomchagua kiongozi wake Grégoire Kayibanda kuwa Rais. Uhuru Tarehe 1 Julai 1962 Rwanda ilipata uhuru wake wa kisiasa. Wakati huu zaidi ya Watutsi 350,000 wameshakuwa wakikimbilia nchi jirani. Mwaka uliofuata vikundi vya Watutsi kutoka nchi hizi za jirani walijaribu kushambulia utaratibu mpya. Iliyofuata ilikuwa uangamizaji wa kwanza wa Watutsi; zaidi ya 100,000 waliuawa na Wahutu. Hata katika miaka iliyofuata mauaji dhidi ya Watutsi yaliendelea. Wanasiasa Wahutu walizoea kuwaita Watusi ndio "Wadudu". Kila kitu kilichokuwa si sawa kilielezwa ni kosa la Watutsi waliokuwa raia bila haki. Idadi kubwa ya Watutsi walikimbilia Burundi, Uganda na Tanzania. Mwaka 1973 Generali Habariyama alimpindua rais Kayibanda na kuanzisha serikali ya kijeshi akijaribu kupatanisha vikundi ndani ya taifa. Lakini hata mwaka uliofuata 1974 mauaji ya Watutsi yalitokea tena. Mnamo 1990 ilikuwa wazi ya kwamba Rwanda ilikuwa na hali ngumu. Kwa upande moja nchi za nje zilisukuma serikali za Afrika kuruhusu kura huru za kisiasa; katika Rwanda ongezeko la wakazi lilileta msongamano mkubwa na uhaba wa ardhi ya kilimo. Uchumi ilikuwa duni. Wakati huohuo wapinzani Wahutu walikusanyika nje ya nchi ny kudai demokrasia. Na kati ya watoto wa Watutsi waliokuwa walitoka nchini sauti zikasikika zilizodai warudi tena. Habyarimana alijaribu kutafuta suluhisho akanza kujadiliana na Watutsi wa nje lakini alikuta pia upinzani kwa upande wa Wahutu wakali waliochukia uelewano wa Watutsi. RPF inajaribu kurudi Rwanda kutoka Uganda Mnamo Oktoba 1990 Watutsi waliokaa Uganda walianzisha chama cha RPF (Rwanda Patriotic Front) wakiwa na wafuasi wahutu wachache wakavamia Rwanda kwa silaha. Kiongozi wao alikuwa Paul Kagame aliyeondoka Rwanda akiwa mtoto wa miaka minne. Alikuwa amejiunga na jeshi la Yoweri Museveni na kupanda ngazi katika jeshi la Uganda hadi kuwa mkuu wa huduma ya usalama ya kijeshi ya Uganda. Walitaka kulazimisha serikali ibadilishe hali ya Watutsi kuwa raia bila haki. Lakini uvamizi huu ulisababisha kuongezeka kwa ukali dhidi ya Watutsi ndani ya Rwanda na siasa kali kwa upande wa viongozi Wahutu. Kikundi cha kihutu cha Interahamwe na kupewa silaha. Maelfu ya Watutsi Warwanda waliuawa. Vita kati ya wapinzani kutoka Uganda na jeshi la serikali iliendelea mpakani hadi pande zote mbili zilikutana huko Arusha na kupatana koma kwa vita 1992 chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika. Sehemu ya viongozi Warwanda walijiandaa kutafuta utaratibu mpya lakini wengine walifanya mipango ya kumaliza swali la Watutsi kabisa wakipanga kuua Watutsi wote nchini. Kifo cha Habariyama na mauaji ya kizazi ya milioni moja Tarehe 6 Aprili 1994 rais Habariyama alirudi nchini kutoka safari ya Tanzania. Ndege yake ilipigwa risasi kabla ya kutelemka ikaanguka chini akafa. Haipingiki kwamba Watutsi wakali (RPF) ndio waliomwua. Tendo hili lilikuwa mwanzo wa mauaji ambayo hayakuwahi kutokea Afrika. Viongozi wa Interahamwe, wa jeshi la kitaifa na vikundi vikali vya Kihutu walitekeleza mipango ya kukusanya Watutsi kila mahali na kuwaua. Haiwezekani kuwa na idadi kamili lakini makadirio ya chini yanataja Watutsi 750.000 na Wahutu wasio wakali zaidi ya 600000 waliuawa na Interahamwe na wanajeshi wa serikali ya Kihutu. Watu walikimbilia na kutafuta hifadhi makanisani lakini hata huko walichinjwa bila huruma. Wahutu waliokataa kushiriki katika mauaji waliuawa pia. RPF chini ya uongozi wa Paul Kagame iliamua kutumia nguvu zote kwa kulipiza kisasi kwa kuwaua Wahutu wenye msimamo mkali na wengine wengi kufungwa maisha katika jela zenye hali mbaya sana, akilenga kulipiza kisasi cha mauaji. Kwa miezi miwili mauaji na vita vilikwenda sambamba hadi RPF iliposhinda mnamo Julai 1994 na kuchukua madaraka ya serikali. Jeshi, Waparmehutu na serikali ya kihutu walikimbilia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakiwalazimisha wakazi wengi kuongozana nao hali iliyosababisha kutokea kwa makambi ya wakimbizi makubwa sana katika Kongo ya mashariki yaliyokuwa na idadi ya wahutu milioni mbili. Walio wengi wamerudi baada ya kuimarika kwa serikali mpya. Rwanda mpya Tangu ushindi wa kijeshi mwaka 1994 RPF walianzisha serikali ya umoja wa kitaifa. Rais alikuwa Pasteur Bizimungu mwanasiasa Mhutu aliyeshikamana na RPF, Kagame akiwa makamu wake. Baada ya kupinduliwa kwa Bizimungu mwaka 2000 Kagame akawa Rais. Mwaka 2003 palitokea uchaguzi wa kwanza. Jeshi la Rwanda limeendelea kuwa na vita ndani ya Kongo ikipigana na mabaki ya Interahamwe walioshambulia Rwanda mara kwa mara kutoka Kongo. Ndani ya Rwanda mahakama za vijijini zinazoitwa "gachacha" zimejaribu kutoa hukumu juu ya wauaji wa mwaka 1994. Rais D. Gasangwa wa Eacu alisisitiza kwamba ilikuwa "Ethnic cleansing", si Holocaust kama ilivyoandikwa na Wazungu wa magazeti ya Ulaya. Watu karibu 600,000 waliuawa Rwanda, na Mkoa wa Kivu, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Utengamano wa siasa mpya lazima utatupa nafasi ya kujenga nchi mpya. Rwanda Historia ya Afrika
2384
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ceuta
Ceuta
Ceuta (tamka: the-uta; kwa Kiarabu: سبتة sabta) ni mji wa Kihispania kwenye pwani ya Mediteranea ambao upande wa bara unazungukwa na eneo la Moroko. Ceuta iko karibu na mji wa Tetouan upande wa Moroko. Umbali na Hispania ni km 21 kuvuka mlango wa bahari wa Gibraltar. Pamoja na mji wa Melilla ni sehemu ya Hispania na Umoja wa Ulaya kisiasa , lakini kijiografia ni sehemu ya Afrika. Moroko inadai ni sehemu ya eneo lake la kitaifa. Watu Ceuta ina wakazi 75.276 katika eneo la km² 18.5. Karibu nusu ni Wazungu/Wakristo na nusu ya pili ni Waberber-Waarabu/Waislamu. Historia Ceuta inaaminika iliundwa na Karthago katika karne ya 5 KK. Jina la Kigiriki la mji imekuwa "Επτά Αδελφοί" (hepta adelphoí - ndugu saba). Tangu Waroma walipochukua utawala wa Afrika ya Kaskazini mji ulijulikana kwa jina la "Septem Fratres" (ndugu saba). Jina hili limeendelea hadi leo, mji ukiitwa "sabta" kwa Kiarabu au kwa matamshi ya Kihispania "Ceuta". Kuanzia karne ya 5 BK mji ulitawaliwa na Wavandali. Mwaka 710 Waarabu Waislamu walifika wakipita Ceuta kuvamia Hispania. Hadi karne ya 14 mji ulikuwa chini ya watawala Waislamu ama Waarabu au Waberberi. Kati ya Wakristo waliofia dini yao huko wanakumbukwa watakatifu Danieli mfiadini na wenzake (1226). Mwaka 1415 Wareno waliteka Ceuta wakaitawala hadi mwaka 1668. Baada ya vita kati ya Ureno na Hispania mji ulikabidhiwa kwa mfalme wa Hispania. Tangu mwaka 1668 Ceuta imekuwa sehemu ya Hispania. Ndani ya Hispania imekuwa Mji wa kujitawala (kwa Kihispania: ciudad autónoma) tangu 1995. Miji ya Hispania
2385
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kabla%20ya%20Kristo
Kabla ya Kristo
Kabla ya kuzaliwa kwake Yesu Kristo (kifupi: KK) ni namna mojawapo ya kutaja miaka. Hesabu hii imekuwa njia ya kuhesabu miaka inayotumika zaidi duniani siku hizi. Kila mwaka huhesabiwa kuanzia ule uliodhaniwa kuwa mwaka wa kuzaliwa kwake Yesu Kristo. Miaka iliyofuata kuzaliwa kwake hutajwa kwa kuongeza Baada ya Kristo au kifupi: BK. Kuhusu historia ya hesabu hii tazama: Historia ya Hesabu "Kabla ya / Baada ya Kristo" Kalenda Yesu Kristo
2387
https://sw.wikipedia.org/wiki/Ella%20Fitzgerald
Ella Fitzgerald
Ella Fitzgerald (25 Aprili 1917 – 15 Juni 1996) alifahamika kama muimbaji wa kike wa muziki wa Jazz (Lady of songs). Ella Fitzgerald au mama Ella sauti yake ilikuwa ni muhimu sana kwenye muziki wa Jazz na hata mitindo mingine ya muziki katika karne ya ishirini. Ella Fitzgerald alizaliwa 25 Aprili 1917 mjini Newport News (Va- Marekani). Ella ameshirikiana na wanamuziki wengi mojawapo ni Louis Armstrong "Satchimo" huyu alikuwa ni mpiga tarumpeta mashuhuri. Mama Ella alizama zaidi katika mtindo wa Swing Jazz. Kati ya nyimbo alizowahi kuimba ni: That old black magic; Can't we be friends?; Love is the thing so they say; It's a blue wold; Dedicated to you; If you ever should live na Sugar blues. Alifariki mwaka 1996. Waliozaliwa 1917 Waliofariki 1996 Wanamuziki wa Marekani
2388
https://sw.wikipedia.org/wiki/Simba%20Wanyika
Simba Wanyika
Simba Wanyika ilikuwa bendi nchini Kenya iliyoundwa mwaka wa 1971 na ndugu kutoka Tanzania, Wilson Kinyonga na George Kinyonga. Bendi hii ilivunjika mwaka wa 1994. Simba Wanyika na bendi zingine mbili zilizotoka kwayo, Les Wanyika na Super Wanyika Stars, zilikuwa bendi mashuhuri sana nchini Kenya. Muziki wao uliotokana na sauti ya gitaa, ikiongozwa na mpiga gitaa wa Soukous, Dr Nico,ikichanganywa na maneno matamu ya muziki wa rumba na kuimbwa kwa Kiswahili. Simba wa nyika tafsiri yake kwa Kiingereza ni "Lions of the Savannah". Wilson Kinyonga na George Kinyonga walianza muziki katika mji wao wa nyumbani wa Tanga nchini Tanzania walipojiunga na Jamhuri Jazz Band mwaka wa 1966. Walihamia Arusha mwaka wa 1970 na kuunda bendi ya Arusha Jazz na ndugu yao mwingine, William Kinyonga. Katika kipindi hiki, wanamuziki walikuwa wakisafiri watakavyo kati ya Kenya na Tanzania, na muziki wa Kenya ukashawishika sana na muziki wa rumba wa Tanzania. Mwaka wa 1971 ndugu hawa walihamia nchini Kenya na kuanzisha Simba Wanyika. Bendi ilitumbuiza katika vilabu vya usiku na baa mbalimbali katika jiji la Nairobi, nakupata wafuasi wengi mno, na katikati ya miaka ya 1970, walikuwa wanajulikana kote Kenya, kwa ajili ya nyimbo kama "Mwongele" na "Wana Wanyika". Kutekelezwa kwa vikwazo baina ya mpaka wa Kenya-Tanzania ilisababisha watu kukua kwa muziki na kuelekea katika mtindo wa uliokuwa unajitokeza wa benga nchini Kenya. Simba Wanyika waliendelea kucheza rumba, na walikuwa bado maarufu wakati bendi ilipogawanyika katika miaka ya 1970 wakati mpiga gitaa Omar Shabini alichukua baadhi ya wanamuziki wake na kutengeneza Les Wanyika. Mwaka wa 1980, George Kinyonga pia alijiondoa katika Simba Wanyika, akachukua wanamuziki zaidi na kuunda bendi ya Orchestra Jobiso. Lakini baadaye alirudi Simba Wanyika huku bado akifanya miradi za upande na Jobiso. Simba Wanyika baadaye walibadilisha jina lao hadi "Simba Wanyika Original" ili kuzuia mkanganyiko na Les Wanyika na kundi lilojigawa kutoka kwao la Super Wanyika Stars. Simba Wanyika ilirudia umaarufu wake katika katikati ya miaka ya 1980 wakitoa nyimbo zilizoptata umaarufu na baadaye kuzuru Ulaya mwaka wa 1989. Bendi ilivunjika mwaka wa 1994 lakini bendi kadhaa zilizotokana nayo bado ziko hai. Angalia Pia Muziki wa Kenya Muziki wa Tanzania Viungo vya nje Muziki wa VIKUNDI vya "WANYIKA" Simba Wanyika: Bendi ya Afropop Video ya Simba Wanyika 1968 Rumba Makundi ya muziki ya Tanzania Makundi ya muziki ya Kenya
2391
https://sw.wikipedia.org/wiki/Nyasa%20%28ziwa%29
Nyasa (ziwa)
Ziwa Nyasa (katika Malawi: Lake Malawi; katika Msumbiji: Niassa) ni kati ya maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki likiwa na nafasi ya tatu baada ya Viktoria Nyanza na Ziwa Tanganyika. Eneo la Ziwa Eneo la ziwa ni km² 29,600. Lina urefu wa km 560 na upana wa km 50-80, likienea kutoka kaskazini kuelekea kusini. Vilindi vyake vinafikia hadi mita 704 chini ya uwiano wa maji yake. Ziwa Nyasa linapatikana kati ya nchi za Malawi, Msumbiji na Tanzania. Katika ziwa hilo kuna mito mbalimbali inayoingiza maji yake humo kama vile mto Lufilyo, mto Mbaka, mto Kiwila, mto Songwe n.k. Kusini mwa ziwa unatoka Mto Shire unaopeleka maji kwenye Mto Zambezi na hatimaye Bahari Hindi. Kijiolojia ziwa ni sehemu ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki. Ziwa Nyasa linajulikana kuwa na aina nyingi za samaki (zaidi ya 1500). Aina chache tu zinavuliwa kama chakula, lakini aina mbalimbali zinakamatwa na kuuzwa nje ya Afrika kwa wapenzi wa samaki wa rangi. Suala la mipaka ziwani Malawi lina ufuko mrefu ziwani upande wa magharibi na kusini, ilhali Tanzania inapakana na kaskazini mwa ziwa na kwenye ufuko wa mashariki, ikifuatwa na Msumbiji. Kuna ugomvi kati ya Malawi na Tanzania kuhusu mipaka ndani ya ziwa. Mpaka baina ya Malawi (zamani: Nyassaland) na Msumbiji ulipangwa wakati wa ukoloni. Lakini kuna mzozo kuhusu robo ya kaskazini-mashariki inayodaiwa na Tanzania kuwa ni eneo lake, ilhali Malawi inaidai pia. Malawi imedai ya kwamba maji yote hadi ufukoni upande wa Tanzania ni sehemu ya eneo lake la kitaifa. Tanzania imedai ya kwamba mpaka uwe katikati ya ziwa kufuatana na desturi za kimataifa. Sababu ya mzozo ni maelewano ya kikoloni. Wakati wa kuanzishwa kwa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani lakini kabla ya serikali ya Ujerumani kuchukua koloni mkononi mwake, serikali za Uingereza na Ujerumani zilipatana kuhusu mipaka ya "eneo chini ya athira ya Ujerumani" ("German sphere of influence") kwa kutaja mpaka ulifuata ufuko wa Ziwa Nyasa. Leo inajadiliwa baina ya wanasharia wa kimataifa kama maneno haya yalitaja mipaka halisi ya kiutawala au kama yalikuwa tu mapatano ya awali kuhusu "maeneo chini ya athira" ya nchi husika. Baada ya mwaka 1919 Uingereza ilitawala Tanganyika pamoja na Malawi (Nyassaland), hivyo hakukuwa na shida. Kabla ya uhuru, wakati wawakilishi wa TANU walichaguliwa tayari kuwa wabunge katika bunge la kikoloni (legislative council) na Julius Nyerere alikuwa waziri mkuu wa Tanganyika tangu 1960, mbunge Chifu Mhaiki alitaka serikali iangalie upya haki za Tanganyika kwa maji ya ziwa. Tarehe 12 Oktoba 1960 waziri mkuu Nyerere alijibu: "Hakuna shaka lolote kuhusu mpaka huu. Tunajua kwamba hakuna tone la maji kwenye Ziwa Nyasa ni mali ya Tanganyika kufuatana na mapatano haya. Hali halisi tungedai serikali jirani ibadilishe mipaka kwa manufaa ya Tanganyika." . Chifu Mhaiki alirudia swali lake alipokuwa mbunge katika Bunge la Kitaifa baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1962 na safari hii waziri mkuu Rashidi Kawawa alijibu tena kwamba hakuna sehemu ya Ziwa Nyasa iliyokuwa ndani ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, kwamba Uingereza haikubadilisha mipaka hii na kwamba hata kama kuna hasara kwa Tanganyika serikali haiwezi kuanza majadiliano juu ya swali hili na Uingereza au serikali ya Nyasaland kabla ya uhuru wa nchi hii jirani. Tarehe 3 Januari 1967 serikali ya Tanzania iliandika mara ya kwanza kwa serikali ya Malawi na kuifahamisha kwamba iliona mpaka baina ya nhci hizi ilifuata mstari wa kati wa Ziwa Nyasa. Malawi ilithibitisha kupokelewa kwa barua hii bila kuijibu rasmi. Hata hivyo rais Banda wa Malawi alikataa madai ya tanzania mbele ya bunge lake. Polisi ya Malawi ilijaribu kutawala wavuvi na feri za Tanzania ziwani. Mzozo huu ulisababisha risasi kufyatuliwa hadi kutulia mwaka 1968. Hadi leo hakuna mapatano rasmi lakini nchi zote mbili zinaendelea kudai bila kutumia nguvu. Hali halisi Malawi imeheshimu dai la Tanzania, haijasumbua tena wavuvi wala feri za jirani ndani ya robo ya kaskazini-mashariki ya ziwa. Mzozo ulifufuka tena tangu mwaka 2012 baada ya Malawi kutoa vibali vya upelelezi wa gesi na mafuta chini ya ziwa, tendo linalopingwa na Tanzania. Marejeo Ziwa Nyasa Maziwa ya Tanzania Maziwa ya Malawi Maziwa ya Msumbiji Maziwa ya Afrika
2395
https://sw.wikipedia.org/wiki/Malawi%20%28maana%29
Malawi (maana)
Malawi ni neno linaloweza kumaanisha Malawi, nchi ya Afrika ya Kusini-Mashariki Malawi kama jina la Ziwa Nyassa Malawi kama matamshi ya ufalme wa Marawi uliokuwa na nguvu katika kusini ya nchi kati ya karne 16. - 19. BK Makala zinazotofautisha maana
2396
https://sw.wikipedia.org/wiki/Mafia
Mafia
Mafia ni neno la kumaanisha Kisiwa cha Mafia katika Tanzania Wilaya ya Mafia katika Tanzania inayojumuisha kisiwa cha Mafia pamoja na visiwa vidogovidogo karibu nacho Mafia (jinai) ni shirika la jinai la Kiitalia limepatikana pia Marekani Makala zinazotofautisha maana