text
stringlengths
0
24.2k
label
class label
6 classes
NA VERONICA ROMWALD WATOTO 24 waliozaliwa na matatizo ya usikivu (viziwi) watafanyiwa upasuaji wa kupandikizwa vifaa vya usikivu kila mwaka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Wateja wa Muhimbili, Aminiel Aligaesha alisema hayo mwishoni mwa wiki alipozungumza na MTANZANIA. “Hii ni huduma mpya ambayo Muhimbili tumeianzisha na ilizinduliwa hivi karibuni na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. “Tumepanga kila mwaka kufanya upasuaji katika awamu nne, kila robo tatu ya kwanza ya mwaka tutawafanyia watoto sita,” alisema. Alisema tayari katika robo tatu ya kwanza ya mwaka, Aprili hadi Juni, wamefanyiwa upasuaji watoto sita kwa mafanikio makubwa. “Watoto hao wanaendelea vizuri baada ya upasuaji, sasa hivi madaktari wanaendelea kutoa huduma za kliniki kama kawaida na kufuatilia hali zao. “Hivyo watapanga tena orodha nyingine ya watoto ambao watafanyiwa upasuaji katika awamu inayofuata,” alisema. Inakadiriwa kila mwaka watoto 200 huzaliwa na tatizo la usikivu na hivyo kuhitaji upasuaji awali walikuwa wakipewa rufaa kwenda  India kupata huduma hiyo ya upasuaji. Tangu mwaka 2003 hadi sasa wagonjwa 50 pekee ndiyo walionufaika na mpango wa ufadhili wa serikali.
5afya
  Na Mwandishi wetu, MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Dotto Biteko, amempongeza Rais Dk. John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kuunda kamati maalum kwa ajili ya kuchunguza mchanga wa madini. Akizungumza na MTANZANIA Dar es Salaam jana baada ya Rais Magufuli kukabidhiwa ripoti ya pili, Biteko alisema ripoti zote mbili zimethibitisha kilio cha Watanzania kuhusu kuibiwa rasilimali za madini uliofanywa kwa miaka mingi. “Rais amejibu kilio hiki cha Watanzania, wananchi walikuwa wanaamini na hasa wale wanaozunguka migodi kwamba tulikuwa tunaibiwa. “Ripoti zote mbili zimethibitisha ukweli juu ya kilio hiki na katika hili nampongeza Rais kwa uamuzi wake wa kuunda kamati maalumu ambazo zimetuletea matokeo chanya,” alisema. Hata hivyo Biteko ambaye pia ni Mbunge wa Bukombe, alisema kamati yake inasubiri maelekezo ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, atakapounda kamati ya kufuatilia uchimbaji wa madini ya almasi. “Spika ameahidi kuunda kamati ya kufuatilia suala la uchimbaji wa madini ya almasi kabla ya Bunge hili la Bajeti halijaisha. “Siku zote sisi wabunge na wajumbe wa kamati za Bunge tumekuwa tukifanya kazi chini ya maelekezo ya Spika, hivyo katika hili tunasibiri mwongozo na maelekezo yake,” alisema.
1kitaifa
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeandika historia iliposaini Makubaliano ya Mgawanyo wa Uzalishaji wa Mafuta na Gesi Asilia (PSA) na Kampuni ya RAKGAS ya Ras al Khaimah ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).Mkataba huo wa kwanza wa aina yake katika historia ya mafuta na gesi asilia Zanzibar, unaelezea majukumu, haki, matumizi, mapato na mgawanyo wake baina ya pande hizo mbili.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein alisema mjini hapa mkataba huo unahusisha kitalu cha Pemba – Zanzibar tu ambacho kinajumuisha maeneo yaliyopo nchi kavu na ya baharini.Ulisainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa RAKGAS, Kamal Mohamed Ataya, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta ya Zanzibar (ZPDC), Mwanamkaa Abdulrahman Mohamed na Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati, Salama Aboud Talib.Ulitiwa saini juzi usiku Ikulu ya Zanzibar mjini Unguja, ukishuhudiwa na Rais , Dk Shein na mgeni wake, Mtawala wa Ras Al Khaimah, Shekhe Saud Bin Saqr Al Qasimi ambaye aliwasili Zanzibar juzi jioni kwa shughuli hiyo, pamoja na ziara ya siku mbili visiwani hapa.Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati, Ali Khalil Mirza, mikataba mingine kama hiyo ijayo itahusisha maeneo mengine ya Zanzibar ambayo yamo hatua za matayarisho na taasisi husika.“Kwa mnasaba huo, siku ya leo inaungana na nyingine chache kwenye orodha ya siku muhimu katika kumbukumbu ya nchi yetu. Ni safari ndefu ya kuweka misingi ya kuhakikisha kwamba rasilimali ya Zanzibar ni kwa ajili ya Wazanzibari na kwamba vizazi vilivyopo na vijavyo vitanufaika ipasavyo na manufaa ya rasilimali hiyo itakapopatikana,” alisema Mirza.Akielezea historia fupi ya kazi ya utafutaji mafuta na gesi asilia Tanzania alisema ilianza miaka ya 1950 ambayo kwa Zanzibar, Kampuni ya British Petroleum (BP) na Shell kwa pamoja zilifanya utafiti huo kwa kuchimba visima vya utafiti maeneo ya visiwa vya Unguja na Pemba.Alisema utafiti huo haukukamilika na miaka ya 1962/1963, ulitoa matokeo ya matumaini ya utafiti zaidi kuendelezwa baada ya kugundulika kuwepo kwa miamba ya mafuta na gesi asilia.“Harakati mpya za kuendeleza utafiti wa mafuta na gesi asilia zilianzishwa tena mwaka 2011 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Ras Al Khaimah walipoanzisha mazungumzo ya ushirikiano ukiwemo ushirikiano katika sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia,” alisema katibu.Alisema Novemba 12, 2011, SMZ na Serikali ya Ras Al Khaimah walisaini Hati ya Ushirikiano (MoU) kufanya kazi kwa pamoja na kuleta ufanisi katika maendeleo ya Zanzibar. “Hati hiyo ya Ushirikiano ilikuwa na mambo tisa, moja ya hayo ni “Kuanzisha na kuingia katika makubaliano ya Utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia (Hydrocarbon) ndani ya eneo la mipaka ya Zanzibar,” alisema Mirza.Alisema katika utekelezaji wa ushirikiano huo, serikali hizo mbili ziliunda Kamati Maalumu ya Utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (JISC) yenye lengo la kusimamia utekelezaji wake.Alisema jumla ya vikao saba vilifanyika kati ya Januari 31, 2012 na Agosti 22, 2016. Alisema mwaka 2015, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liliridhia Sheria ya Mafuta Namba 21 ya 2015 ambayo imeipa SMZ mamlaka ya kushughulikia rasilimali za mafuta na gesi asilia wenyewe.Alisema baada ya kukamilika kwa Sera na Sheria, SMZ iliunda Kamati Maalumu ya Majadiliano kwa ajili ya kufanya majadiliano na Kampuni ya RAKGAS kuhusu PSA na baada ya mijadala na mikutano mingi, ndiyo iliyozaa matunda ya mkataba uliosainiwa juzi usiku.Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetumia Mkataba wa PSA kwani unaweza kutoa mfumo mzuri wa kimkataba unaoweza kudhibiti na kutoa uhakika wa kisheria kwa muda wote wa shughuli za mafuta na gesi asilia.Akihutubia baada ya kushuhudia utiaji saini huo, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein alisema tukio la juzi ni kusonga mbele. Alieleza juhudi za serikali zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizokuwapo, ikiwamo kulazimika kutunga sheria muhimu mpya zilizo bora zaidi, madhubuti na zenye kuzingatia maslahi ya pande zote mbili za Muungano.Alimshukuru Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kwa kuhakikisha kabla ya kustaafu, suala la mafuta na gesi linapatiwa ufumbuzi na kuondoa kero ya muda mrefu. Alisema matokeo ya juhudi hizo yatakuwa na manufaa na mchango mkubwa kuendeleza uchumi. Alisema faida yake ni kama mfano wa afya na kiwiliwili, yaani afya inapoimarika na kiwiliwili cha binadamu huimarika na kunawiri.
1kitaifa
NA NORA DAMIAN, KIGOMA WATALII wengi katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyoko mkoani Kigoma, wamevutiwa na vipande vya video ya wimbo wa ‘Leka Dutigite’ ulioimbwa na wasanii wanaotokea Mkoa wa Kigoma ‘Kigoma All Stars’, kutokana na kutumia mazingira ya hifadhi hiyo. Kipande kinachouliziwa zaidi na watalii wanaofika katika hifadhi hiyo ni kile kinachomwonyesha mkali wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’ akiwa anabembea katika mti ulioko katika hifadhi hiyo. Mhamasishaji Utalii Msaidizi katika hifadhi hiyo, Isaya Mkude, alisema watu wengi hasa wazawa wamekuwa wakifika na kutaka waonyeshwe sehemu alipobembea msanii huyo. “Tumeamua kuiita bembea ya Diamond kwa sababu baada ya yeye kubembea imekuwa kivutio kwa watu wengi kuja na kutaka kwenda kupaona na wengine kubembea,” alisema Mkude. Alisema miaka ya nyuma wageni ndio walikuwa wengi wanaotembelea hifadhi hiyo lakini hivi sasa kuna mwamko mkubwa kwa wazawa. Takwimu za mwaka 2014/15 zinaonyesha wazawa waliotembelea hifadhi hiyo ni 527 wakati wageni ni 927. Kwa mwaka 2015/Mei 2016 wazawa ni 374 na wageni ni 645. Gharama ya kuingia katika hifadhi hiyo ambayo ni maarufu kwa wanyama aina ya sokwe ni Sh 10,000 kwa Mtanzania mmoja na Dola 100 kwa mgeni kwa siku.
4burudani
NA KULWA MZEE -DAR ES SALAAM WAKAZI wanne wa Jiji la Dar es Salaam, wamehukumiwa kwenda jela miaka 30 na kuchapwa viboko 12 kila mmoja kwa wizi wa simu nne za kiganjani. Watu hao ambao ni wakazi wa eneo la Boko Magengeni katika Wilaya ya Kinondoni, katika kutekeleza adhabu hiyo watachapwa viboko sita wakiingia gerezani na sita siku wakitoka. Washtakiwa hao walihukumiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicious Mwijage baada ya Jamhuri kuthibitisha makosa yao bila kuacha shaka. Waliohukumiwa ni Donald Nzwenka,  Michael Paschal, Ally Akili na Kurwa Mwakagenda. Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mwijage, alisema washtakiwa kwa pamoja Julai 7, 2013 maeneo ya Boko Magengeni, Dar es Salaam waliiba simu nne aina ya Nokia, Sumsung, Teckno zikiwa na thamani ya Sh 1,300,000. Pia washatakiwa hao waliiba, fedha taslimu Sh 150,000, cheni za dhababu mbili zenye thamani ya Sh 750,000, ambapo mali yote jumla ina thamani ya Sh 2,050,000. Hakimu Mwijage alisema kabla ya wizi huo, washtakiwa walimtishia na jambia Hobokela Mwakijambile, ambaye ndiye mwenye mali hizo. Katika kesi hiyo Jamhuri iliita mashahidi 11 na washtakiwa walijitetea wenyewe. “Baada ya kupitia ushahidi wa pande zote mbili, mahakama ilijiuliza kwamba kosa la kutumia silaha ili lithibitike Jamhuri wana wajibu wa kuthibitisha bila kuacha shaka kwamba washtakiwa kabla ya kutenda awe na kifaa hatari. ” Pia washtakiwa kabla ya kutenda  wawe zaidi ya mmoja na kwamba baada ya tukio hilo walitumia nguvu kwa mtu aliyeporwa,” alisema. Alisema katika shauri hilo, mlalamikaji na mashahidi wengine walieleza usiku wa Julai 7 mwaka huo majambazi walivunja mlango mkuu wa nyumba yao kwa kutumia bomu ambalo lilitambuliwa na polisi kuwa baruti. Ushahidi ulieleza kwamba, washtakiwa waliendelea kuvunja milango mingine na baadae waliingia katika chumba walichokuwa wamekaa mashahidi. Wakiwa katika chumba hicho chenye mwanga, mshtakiwa wa nne alishika panga na alianza kuwapiga nalo kwa kutumia ubapa. “Kwa kuzingatia ushahidi huo, hakuna shaka kwamba mashahidi waliweza kuwatambua hao majambazi kwamba ni washtakiwa katika kesi hiyo. “Kwa kuangalia maelezo yao, waliyotoa Polisi yanaonyesha jinsi walivyoshiriki katika tukio na kwamba washtakiwa ndio walioiba vifaa hivyo kwa kutumia silaha kali,”alisema. Hakimu alisema utetezi wa washtakiwa kwamba walikamatwa maeneo tofauti na kupelekwa Oysterbay Polisi na kupigwa na kunyanyaswa hauaminiki. Mahakama ilisema ushahidi huo hauaminiki na hauwezi kupewa uzito wowote. Alisema utetezi wa kukanusha tu kuhusika katika kosa siku hiyo, haukutikisa kwa namna yoyote ushahidi wa Jamhuri. “Kutokana na hayo, hakuna shaka kwamba washtakiwa walitenda kosa na walitambuliwa ipasavyo. “Nimeridhika Jamhuri imethibitisha kosa bila kuacha shaka dhidi ya washtakiwa, hivyo nawatia hatiani kwa kosa la kutumia silaha kama walivyoshtakiwa,”alisema. Jamhuri katika kesi hiyo iliwakilishwa na Wakili wa Serikali Gloria Mwenda, ambaye alisema washtakiwa ni wakosaji wa mara ya kwanza na akaomba wapewe adhabu kali.
1kitaifa
NA MWAMVITA MTANDA, Kigali LICHA ya aliyewahi kuwa kocha msaidizi wa Simba, Mrundi, Masoud Djuma, kuondoka ndani ya kikosi cha AS Kigali, lakini mashabiki wa soka nchini Rwanda wanataka arejee kuinoa Rayon Sport.  Kabla ya kupata kibarua ndani ya klabu ya Wekundu wa Msimbazi, Simba, Djuma alikuwa akiifundisha Rayon Sports,  ambayo aliiwezesha kutwaa ubingwa. Na baada ya kutemana na Simba, kocha huyo alijiunga na AS Kigali ya hapa ambayo hakudumu nayo, baada ya kutokuwa na maelewano mazuri na watendaji wengine wa benchi la ufundi la timu hiyo. Akizungumza na MTANZANIA, jana, shabiki maarufu wa Rayon Sports, Akizimana Godfrey alisema anaamini Djuma ni kocha mwenye uwezo mkubwa na bado wanamkumbuka kwa kuisaidia Rayon Sport kutwaa ubingwa. Aliutaka uongozi wa klabu hiyo kuangalia uwezekano wa kumrudisha kufanya kazi naye kwa mara nyingine. “Kitu ambacho timu zetu zinashindwa kubaki na Djuma ni kwamba hawaelewi nini anataka, Djuma anataka kupewa nafasi ili afanye kazi yake vizuri.  “Kwa uwezo alionao,  hata akikabidhiwa timu bila msaidizi anaweza kufanya vizuri, ni kocha mzuri na mwenye mbinu za kimataifa,”alisema Akizimana na kuongeza. “Hata kama Rayon inafanya vizuri,lakini bado haijafikia kiwango ilichokuwa nacho Djuma.”
2michezo
NEW YORK, MAREKANI Rapa na mkali wa filamu nchini Marekani, Nick Cannon, anadaiwa kutoka na dansa Rozonda Thomas, baada ya kuachana na Mariah Carey. Cannon na Rozonda, walionekana juzi wakipigana kisi jijini New York, hivyo kuwafanya mashabiki wa wawili hao wakiwa na maswali mengi. Hata hivyo Rozonda kupitia akaunti yake ya Istagram, aliweka wazi kwamba wawili hao sasa wapo katika uhusiano na kila kitu kitazidi kuwekwa wazi siku hadi siku. “Najua kuna maswali mengi yatakuwa yanaendelea, lakini huu ni ukweli kama inavyoonekana kwenye mitandao ya kijamii, kila kitu kitakuwa wazi siku hadi siku,” aliandika Rozonda
4burudani
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mkoa wa Arusha, Nuru Suleiman ameieleza mahakama kuwa basi lililosafarisha wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent, lilikuwa linamilikiwa na mtu mwingine na si Mkurugenzi wa shule hiyo. Amedai basi hilo limewahi kumilikiwa na watu watatu tofauti na mmiliki wa mwisho alikuwa Swalehe Kiluvia kabla ya Kampuni ya Lucky Vincent. Suleiman ambaye ni shahidi wa pili katika kesi ya makosa ya usalama barabarani ikiwamo kusafirisha watoto bila vibali muhimu inayomkabili Mkurugenzi wa Shule ya Lucky Vincent, Innocent Moshi, Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Arumeru, Desderi Kamugisha, amedai mahakamani hapo leo kuwa gari hilo pia halikuwa na leseni ya kubeba wanafunzi na badala yake lilikuwa na leseni ya kusafirisha abiria kutoka Arusha hadi Mererani. “Baada ya kupokea barua kutoka kwa mpelelezi wa shauri linalohusu ajali hiyo ikinitaka kupata baadhi ya uthibitisho kutoka mamlaka tofauti kwa ajili ya upelelezi ambapo tuliandika barua Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), Idara ya Kazi, Mamlaka ya Mapato (TRA) na Kampuni ya Bima, Zanzibar Insurance,” amedai. Shahidi huyo amedai barua hizo aliandika Mei 8, mwaka huu kwa taasisi hizo ili kufahamu kuhusu uhalali wa bima ya gari hilo, uchunguzi wa leseni ya usafirishaji, mkataba kati ya dereva na mmiliki wa gari pamoja na kutaka kujua iwapo gari hilo limewahi kumilikiwa na mtu mwingine. “Mei 9, mwaka huu tulipata majibu kutoka taasisi hizo ambapo Sumatra ikieleza basi hilo halikuwa na leseni ya kubeba wanafunzi na badala yake lilikuwa na leseni ya kusafirisha abiria kutoka Arusha kupitia Mbuguni kuelekea Mererani, huku likionyesha mmiliki alikuwa ni mwingine anayetambulika kwa jina la Swalehe Kiluvia. “Zanzibar Insurance walisema bima ya mwisho kukatiwa basi hilo ilikatwa na Kiluvia na Lucky Vincent hawakukata, hivyo kuendelea kutumia bima ya mmiliki mwingine, bima hiyo inakuwa siyo halali, huku Idara ya kazi ikitoa majibu kuwa ofisi hiyo haikuwa na mkataba wanaoutambua kati ya dereva wa basi hilo Dismas na shule hiyo,” amedai.  
1kitaifa
RAYMOND MINJA IRINGA Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humfrey Polepole, amewataka viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia chama hicho kutokuwa chanzo cha migogoro na majungu badala yake wawe suluhisho kwa kufuata malengo ya chama ambayo ni kusimamia serikali na kuwaletea watanzania Maendeleo. Ameyasema hayo leo Juni 12 katika semina ya kuwafunda makatibu wa uenzi wa ngazi zote mkoani humo ambapo amesema kuwa chama hicho kimejengwa kwenye misingi bora ya kutumikia wananchi na kuwasikiliza ili kujua shida zao. “Hii ni CCM mpya chini ya mwenyekiti rais John Magufuli na hana utani anataka kazi tu na wale ambao wanaona wameshindwa watupishe maana unapoacha sumu ndani kuna siku itakudhuru tunapogombana wanaoumia ni watanzania waliotupa dhamana ya kusimamia serikali ”amesema. Amesema kuwa kwasasa mlango uko wazi na kwamba endapo kuna mtu anaona atashindwa kupelekana na kasi ya chama hicho chini ya rais Magufuli ni vyema akapisha na kuacha wanaojua kufanya kazi. Pia amewataka viongozi kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa huku akimtaka katibu wa itikadi na uenezi mkoani humo, Ramadhani Baraza kuendelea kuwatumikia wananchi vizuri kwa kueleza mambo mazuri yanayofanywa na serikalia ya CCM.
1kitaifa
Kocha wa Simba Sven Vandenbroeck amewaahidi wa klabu hiyo kabubu safi katika mechezo wao wa leo dhidi ya Kagera. Vandenbroeck ambaye ni kocha mkuu wa mabingwa hao watatezi wa ligi kuu ya soka Tanzania bara amesema maandalizi ni mazuri. “Tumejiandaa vizuri na tunawahakikishia soka safi mashabiki wetu kwenye mchezo wetu wa kesho,” amesema Vandenbroeck. "Tumejiandaa vizuri na tunawahakikishia soka safi mashabiki wetu kwenye mchezo wetu wa kesho."- Kocha Mkuu Sven Vandenbroeck kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Kagera Sugar. #NguvuMoja A post shared by Simba Sports Club (@simbasctanzania) on Feb 17, 2020 at 9:16am PST
2michezo
WAKATI mpiga picha raia wa Marekani John Moore akiibuka mshindi wa picha duniani, wapiga picha wa vyombo vya habari nchini wametakiwa kujielimisha zaidi kuhusu lugha ya picha na kuwa wabunifu.Rai hiyo ilitolewa jana na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul aliyesema kuwa wapiga picha wa Tanzania wanakosa ubunifu na hawajui ipasavyo kutambua lugha za picha, kitu kilichofanya wakashindwa kwenye mashindano hayo ya picha duniani maarufu kwa jina World Press Photo, yanayofanyika kila mwaka.“Haihitaji kuwa na vifaa ya kisasa ili kupiga picha bora, hata simu unaweza kutumia kupiga picha na ikawa bora na kushinda tuzo, kinachotakiwa ni maarifa na ufahamu wa lugha za picha ambazo wengi wanakosa,” alisema Verheul.Alisema kutokana na hilo, wameandaa mafunzo ya siku mbili kwa wapiga picha wa vyombo mbalimbali vya habari na kuwajengea uwezo wa kuwa wabunifu na kuwapa maarifa zaidi juu ya upigaji picha. Mafunzo hayo ya siku mbili yamemalizika jana, Oktoba 25.“ Tumetoa mafunzo kwa wapiga picha ili wajitafakari kuhusu taaluma zao na fursa zilizopo nchini za uandishi wa habari shirikishi, lengo kuu ni kuamsha ubunifu na kukuza taaluma yao,” alisema Balozi huyo wa Uholanzi Picha iliyoshinda mwaka huu ilipigwa Juni 25 mwaka jana ikimuonesha mtoto wa Kihandurai aliyekua akilia wakati yeye na mama yake wakipelekwa kizuizini na maofisa wa mipaka ya Marekani.Mshindi wa pili katika picha duniani ni Pieter Hoopen kutoka Uholanzi ambaye picha yake ilihusu msafara wa wahamiaji wa Marekani ya Kati wakielekea katika mpaka wa Marekani katika kipindi cha mwezi Oktoba na Novemba 2018.Meneja wa maonesho ya picha kutoka kituo cha Alliance Francaise, Sanne Vanderleef alisema jumla ya picha 78, 813 ziliwasilishwa kwenye mashindano hayo nakufanya jumla ya wapiga picha 4,000 kutoka nchi 128 duniani. Alisema baada ya kupitia picha hizo, 140 zilifanikiwa kuingia kwenye maonesho ya mwaka huu.“Picha 140 zilizofanikiwa kushinda zitakuwa kwenye maonesho kuanzia leo (Jana) Oktoba 25 hadi Novemba 14,” alisema na kuongeza kuwa kwa Tanzania maonesho hayo yanafanyika kituo cha utamaduni cha Ufaransa, kilichopo Upanga.Vanderleef alisema maonesho hayo yanafanyika sambamba na warsha za waandishi wa habari kuanzia Novemba 11 na 12, mwaka huu.
1kitaifa
LONDON, UINGEREZA WATU nchini Uingereza wameombwa kuwa katika tahadhari baada ya ugonjwa usio wa kawaida unaosambaa kwa kuumwa na kupe kubainika kwa mara ya kwanza nchini humo. Wizara ya Afya imesema hatari iliyopo kwa umma ni ya chini lakini ni muhimu wawe waangalifu kuhusu kupe hasa wanapokuwa kwenye maeneo ya bustani msimu wa joto. Imeelezwa kuwa ugonjwa huo unasababishwa na vimelea ambavyo vinaathiri chembe nyekundu za damu. Tayari mgonjwa wa pili aliyeambukizwa ugonjwa huo ambao ni nadra sana kutokea amegunduliwa. Ugonjwa huo unaosambazwa na kupe unaosababisha ubongo kufura mara nyingi hutokana na maambukizi ya virusi. Dk. Katherine Russell kutoka Wizara ya Afya nchini humo amesema ugonjwa huo ni nadra sana na hivyo basi uwezekano wa maambukizi ni wa chini mno. “Kupe hupatikana sana kati ya msimu wa kuchipua na pukutizi, kwahiyo ni muhimu ikiwa raia watachukua tahadhari ya juu ili kuhakikishi hawaumwi na kupe wanapokuwa nje wakijivinjari. Na pia tafuta ushauri wa daktari unapoanza kusikia vibaya baada ya kuumwa na kupe,” alisema Dk. Katherine. Wizara ya afya imesema imepima mamia ya kupe katika eneo la Devon karibu na anapoishi mgonjwa wa kwanza aliyebainika na ugonjwa huo, lakini wote hawakupatikana nao. Na pia vipimo vya damu kutoka Hampshire katika maeneo karibu na anapoishi mgonjwa mwingine vimeonekana kuwa salama. Wagonjwa wote wanapata matibabu hospitalini na kulingana na Kituo cha Kuzuia Magonjwa Ulaya kimesema ugonjwa huo unasambazwa tu na kupe ambao hupata maambukizi kwa kuumwa na ng’ombe walio na maambukizi na panya buku. Kuna watu 39 waliothibitishwa kupata maambukizi barani Ulaya, nje ya Ulaya, ugonjwa huo mara nyingi hutokea Marekani. DALILI Watu wengi wenye ugonjwa huo ama hawatakuwa wanaonesha dalili au dalili za maambukizi ni za wastani.  Hata hivyo, watu wenye mfumo wa kinga ya mwili dhaifu wanaweza kuumwa sana, wakilalamikia dalili za kama mafua, homa, kuhisi baridi, kuumwa na misuli, uchovu na homa ya nyongo ya njano. Karibia theluthi mbili ya watu wenye maambukizi ya ugonjwa huo hawataonesha dalili, kwa walio na mafua na homa, kuumwa kichwa na uchovu wanaweza kupata ugonjwa wa utando wa ubongo au kufura kwa ubongo na kupooza mwili. Shingo inapokakamaa na kuumwa kichwa, kupata maumivu kwa kuangalia mwanga wa taa, kuzimia, kuwa na mabadiliko ya tabia- kama kuchanganyikiwa ghafla na kuhisi baadhi ya sehemu za mwili zinashidwa kusongea.
3kimataifa
JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Tarime- Rorya, limefanikiwa kuwaua watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi akiwemo aliyewahi kudaiwa kunyang’anywa bunduki aina ya SMG na mwanamke mkazi wa Buriba katika Kata ya Sirari wilayani Tarime.Kamanda wa Polisi wa Tarime-Rorya, Henry Mwaibambe alisema jana katika tukio hilo, zimepatikana bunduki 2; moja AK 47 na goboro, na risasi 5 zikiwa ndani ya magazine.Alisema majambazi hao walikufa Novemba 7, mwaka huu saa nne usiku baada ya majibizano ya risasi walipovamia nyumbani kwa mfanyabiashara wa samaki, David Ogutu maarufu Baba Ouma Kijiji cha Obwere Shirati wilayani Rorya kupora fedha.“Kundi la majambazi hao likiwa limejihami kwa silaha za moto, lilivamia nyumbani kwa mfanyabaishara huyu wa samaki kwa nia ya kufanya uhalifu wa kupora fedha; walifyatua risasi hewani kuwatishia wananchi wasijitokeze kutoa msaada lakini mfanyabiashara huyo alipiga simu kwa askari polisi Kituo cha Shirati waliofika,” alisema Mwaibambe.Aliongeza kuwa, “majambazi hao walipowaona polisi, waliwarushia risasi na kuanza majibizano ya risasi hatimaye polisi kufanikiwa kuwajeruhi majambazi hao watatu… wananchi na polisi walifuatia nyayo na damu iliyoonekana katika eneo la tukio.”Kutokana na mwito wa polisi wa kutaka taarifa zitolewe mapema kuhusu watu watakaoonekana wamejeruhiwa, siku iliyofuata (Novemba 8, mwaka huu), wananchi Mjini Tarime walimwona mtu aliyejitambulisha kwa jina la Kesanta Chacha akiwa na majeraha amejifunika jaketi akipanda gari dogo la abiria kutaka kwenda Sirari.Kamanda Mwaibambe alisema walimtilia shaka na kutoa taarifa kwa polisi kabla gari hilo halijaondoka na kumkamata mkazi huyo wa Kebeyo aliyewahi kupatikana na bunduki AK 47, lakini akaachiwa na mahakama akiwa na umri wa takriban miaka 16.
1kitaifa
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA SERIKALI imetangaza kuwapandisha vyeo watumishi wa umma 193,166 kuanzia Mei Mosi. Hayo yalielezwa jana bungeni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika wakati akitoa kauli kuhusu upandishwaji vyeo kwa watumishi wa umma. Mkuchika alipewa nafasi hiyo na Spika wa Bunge, Job Ndugai mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu. Alisema watumishi hao watakaopandishwa vyeo ni wenye utendaji kazi mzuri ambao wanakaribia kustaafu, watumishi waliokaa katika vyeo walivyonavyo kwa muda usiopungua miaka minne na kukasimiwa kwenye ikama ya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18. Mkuchika aliwataka waajiri wote kuhakikisha wanawapandisha vyeo watumishi stahiki kwa wakati na kwa kuzingatia TANGE (Seniority List) ya taasisi husika, sifa za kimuundo na kuwepo kwa nafasi iliyoidhinishwa kwa mujibu wa matokeo ya tathimini ya utendajikazi. “Waajiri na maofisa watakaotekeleza zoezi hili kinyume na maelekezo yaliyotolewa na Serikali kuhusu upandishaji vyeo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma,” alisema. Alisema upandishwaji vyeo ulihairishwa Mei mwaka 2016 kupisha uhakiki wa watumishi hewa na mishahara batili pamoja na vyeti vya utumishi wa umma. “Baada ya kukamilika kwa mazoezi tajwa, Mheshimiwa Rais Dk. John Magufuli aliridhia upandishaji vyeo watumishi kwa awamu,” alisema. Mkuchika alisema awamu ya kwanza iliyoanza Novemba Mosi mwaka juzi, ilihusisha upandishaji na uidhinishaji wa taarifa za watumishi 59,967 ambao taarifa zao za kupandishwa vyeo zilikuwemo katika Mfumo wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS), lakini zilikuwa hazijaidhinishwa wakati wa usitishaji tajwa Mei mwaka 2016. Alisema kuwa awamu ya pili iliyoanza Aprili Mosi mwaka jana, ilihusisha watumishi zaidi ya 53,553 ambao walipandishwa vyeo, lakini taarifa zao zilikuwa hazijaingizwa kwenye mfumo wa HCMIS. Mkuchika alisema uidhinishaji wa taarifa za watumishi 113,520 katika makundi hayo mawili kupitia mfumo wa HCMIS umekamilika. “Baada ya kukamilika upandishaji vyeo watumishi wa umma wapatao 113,520, Serikali imewaelekeza waajiri kuendelea na upandishaji vyeo kwa watumishi 193,116 waliokasimiwa ikama na bajeti ya mishahara kwa mwaka wa fedha 2017/18 kuanzia Mei mwaka huu,” alisema Mkuchika
1kitaifa
Na ESTHER MNYIKA-DAR ES SALAAM SERIKALI imeitaka Kampuni ya M/s China Civil Engineering Construction Corparation (CCECC) kukamilisha mradi  wa ujenzi wa barabara za juu  ‘interchange’ katika makutano ya Ubungo ndani ya miaka ya mitatu.  Mkataba uliofikiwa unamtaka Mkandarasi ambayo ni Kampuni ya CCECC kutoka China kuanza ujenzi huo mara moja na ujenzi huo ambao unatarajiwa kutumia takriban miezi 30  kukamilika   Mtendaji Mkuu  wa Wakala wa Barabara Tanzania  (TANROADS), Patrick Mfugale aliyesema hayo Dar es Salaam jana baada ya kusaini mkataba na kampuni hiyo ya  ujenzi wa barabara za juu   katika makutano ya Barabara ya Sam Najoma, Morogoro na Mandela. “Zaidi ya Sh bilioni 177.4 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo ambao utakawekewa jiwe la msingi Machi mwaka huu. “Hakikisheni mnaanza ujenzi mara moja kwa sababu Serikali imeshakamilisha taratibu zote na tayari Sh bilioni 2.1 zimelipwa kwa ajili ya fidia kwa wananchi walioguswa na mradi huo,”  alisema Mfugale. Alisema ujenzi wa Ubungo interchange unatekelezwa  kwa fedha ya mkopo kutoka Benki ya Dunia  kwa ajili ya   uboreshaji miundombinu ya usafiri Dar es Salaam.
1kitaifa
UTUMIKISHWAJI wa watoto wa kike ili kusaidia familia, umaskini, mazingira magumu kwenye shule, mimba za utotoni ni miongoni mwa sababu zinazowafanya wasichana kuacha shule katika wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.Akizungumza wakati wa mahojiano jana, Mratibu wa Programu wa Shirika lisilokuwa la kiserikali la Marafiki wa Elimu Dodoma (MED), Luhaga Makunja alisema kuna idadi kubwa ya wasichana wanaoacha shule kutokana na sababu mbalimbali. Alisema shirika hilo lilikuwa likitekeleza mradi wa kutatua changamoto za unyanyasaji wa kijinsia katika elimu ya msichana ambapo eneo la mradi lilikuwa kata nne za Chibelela, Mapanga, Mtitaa, Mwitikila na Chipanga. Alisema mradi huo ulilenga watoto wetu umri kuanzia tisa hadi 19 ambao wako shuleni.“Ukatili mkubwa tuliouona ulikuwa ni kuachishwa masomo kutokana na mimba za utotoni,” alisema. Alisema kulingana na takwimu walizopata kutoka Idara ya Elimu wasichana 3,179 walioanza shule 2013 miongoni mwao 1,238 hawakumaliza kidato cha nne mwaka 2017 ambapo ni asilimia 39 sababu kubwa ikiwa ni mimba za utotoni. Makunja alisema tulikuwa na wasichana kutumikishwa kazi za majumbani ambapo wasichana wamekuwa wakiachishwa shule na kwenda mijini kufanya kazi za ndani kusaidia familia.“Bado kuna mila na desturi ambazo hazioni thamani ya mwanamke kwenye elimu hata inapofikia umri wa mtoto kuandikishwa shule suala la kusoma linaokana sio muhimu,” alisema. Makunja alisema umasikini, utumikishwaji wa watoto kusaidia familia, mazingira magumu shuleni kutokana na umbali kutoka makazi Hadi shuleni inaonekana ni kikwazo cha elimu kwa mtoto wa kike.“Kuna wanafunzi wanalazimika kwenda kupanga vijijini ili wawe karibu na shule, wanakosa ulinzi wa wazazi na kujikuta wakiingia kwenye ngono na hivyo wengi hujikuta wakikatisha masomo kutokana na ujauzito,” alisema. Pia alisema mazingira magumu ya nyumbani hupelekea watoto kufika shule wakiwa hawajala huku akitembea umbali mrefu kufika shuleni.“Anatoka nyumbani hajala anakaa muda mrefu na njaa, hata masomo haelewi vizuri anajua atafeli tu alishakata tamaa anaona amalize tu shule,” alisema. Makunja alisema ukosefu wa mabweni na chakula unasababisha watoto kutoshawishika kwenda shuleni.Alisema kumekuwa na mtazamo hasi wa wazazi na walimu juu ya elimu kwa wasichana. “Jitihada kubwa zinahitajika kuhakikisha elimu inatolewa ili kupunguza unyanyasaji wa kijinsia unaosababisha wasichana kukosa elimu,” alisema. Pia alisema wasichana wengi walikuwa hawashiriki katika maamuzi hata kwenye mipango ya shule na vijiji.
1kitaifa
WAZIRI wa Kilimo Japhet Hasunga ametembelea na kujionea maandalizi ya Maadhimisho ya 27 ya Sikukuu ya Wakulima maarufu kama Nanenane.Maadhimisho hayo yana lengo la kuwatambua na kuwaenzi wadau wakuu wa sekta ya kilimo ambao ni wakulima, wafugaji, wavuvi, wanaushirika, wasindikaji wa mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na maliasili kwa mchango wao mkubwa wanaoutoa katika kuendeleza uchumi wa nchi.Hasunga pamoja na mambo mengine akiwa katika Banda la Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), aliutaka uongozi wa taasisi hiyo kuongeza juhudi za utoaji elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi ya mifuko maalumu ya kuhifadhia nafaka ya PIC’S.Alisema NFRA inapaswa kutoa elimu hiyo ili iwafikie wakulima wengi kwani kufanya hivyo itarahisisha huduma za uhifadhi wa mahindi ya wakulima, ambao kwa muda mrefu wamekumbwa na kadhia ya kushindwa kuhifadhi mahindi kwa ufasaha.Pamoja na NFRA kutoa elimu kwa wakulima kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na televisheni, pia alisisitiza kuwa NFRA inapaswa kuongeza uwezekano wa kuwafikia wakulima wengi zaidi. Mwaka huu sherehe za Nanenane zinafanyika kitaifa mjini Bariadi katika Viwanja vya maonesho ya kilimo Nyakabindi katika Mkoa wa Simiyu. Waziri huyo aliupongeza uongozi wa mikoa ya Simiyu, Shinyanga na Mara kwa juhudi zao za kufanikisha kuingiza uwanjani huduma za msingi ambazo ni maji na umeme. Alisema jukumu hilo kwa serikali na wadau wa sekta binafsi ni kuendeleza viwanja hivyo vya Nyakabindi kwa kujenga mabanda ya maonesho ya kudumu, kuboresha huduma muhimu za kijamii ili kuwe na maonesho endelevu yenye sura ya kitaifa na Kimataifa.
1kitaifa
BENJAMIN MASESE-MWANZA SERIKALI imepokea injini mbili kutoka Korea Kusini ambazo zitafungwa kwenye meli mpya ya MV Mwanza, huku ikizindua pia safari za ndege kusafirikisha minofu ya samaki kwenda nchini Uholanzi ambapo Shirika la ndege la Rwanda litakuwa likiisafirisha. Mbali na kuzindua usafirishaji huo wa samaki, pia imetangaza kwamba sasa uwanja wa ndege wa Mwanza unakuwa wa kimataifa. Meli Akizungumza jijini Mwanza jana baada ya kuzindua safari za ndege na kupokea injini hizo, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Isaack Kamwelwe, meli inayotengenezea jijini Mwanza itakuwa ikifanya za Mwanza-Bukoba na nchi jirani za Kenya na Uganda Alisema meli hiyo inayogharimu Sh bilioni 159 inatarajia kukamilika na Januari 2021 na kuwataka wakandarasi  ambao ni  Gas Entec Co. Ltd, Kangnam Corporation zote kutoka Korea ya Kusini zikishirikiana na Suma JKT ya Tanzania kuhakikisha zinakamilisha shughuli hiyo  kama mkataba unavyoelekeza.  “Meli hii itakuwa kubwa kuliko meli zote katika ukanda huu wa maziwa makuu, itakuwa na mita 92.6, kimo chake kitakuwa mita 11.2, upana mita 17 na uzito wa tani 3,500 kwa takwimu hizo ndio itakuwa meli kubwa kuliko zote na itakuwa inatumia masaa saba kutoka Mwanza hadi Bukoba,”alisema. Akitoa ufafanuzi wa injini hizo, Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Huduma za Meli Tanzania (MSCL), Erick Hamisi, alisema injini hizo zimenunuliwa kwa Dola za Marekani 39,000,000 sawa na Sh bilioni 89.764  na kila moja ina tani 35 na uwezo wa kuzaliza KW 2,380. Alisema uwezo huo wa injini utaiwezesha meli hiyo kusafiri kwa saa sita kutoka Mwanza hadi Bukoba na kwamba hadi sasa wakandarasi hao wamelipwa Sh bilioni 55.618 sawa na asilimia 64 ya gharama zote. “Kila injini itakuwa na uwezo wa kutumia mafuta lita 9,300 kutoka Mwanza hadi Bukoba, hivyo kwa injini mbili zitatumia lita 18,600  kwa kusafirisha abiria 1200, tani 400 za mizigo na magari madogo 20 lakini meli hii  itakuwa na madaraja sita, daraja la uchumi abiria 834, daraja la biashara abiria 200, darala la pili la kulala abiria 100, darala la kwanza abiria 60 na daraja la hadhi ya juu abiria wanne, mwisho ni VIP abiria wawili. Safari za ndege Katika hatua nyingine Kamwelwe alizindua safari za Mwanza hadi hadi Uholanzi katika kwa kutumia shirika la Ndege ya Rwanda ambapo  jana ilisafirishwa tani  nane za minofu ya samaki huku akifafanua kwamba kila wiki kutakuwa na safari moja. Kutokana na safari hizo, amewaagiza wakuu wa mikoa ya Mwanza, Mara, Simiyu na Kagera kuunda mtandao wa pamoja wa kuhakikisha samaki wote wanaletwa kwenye viwanda ili kurahisisha upatikanaji wa minofu hiyo na kufikishwa uwanja wa kimataifa wa Mwanza.
1kitaifa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema vyombo huru vya habari ni muhimu kwa amani, haki, maendeleo endelevu na haki za binadamu. Maudhui  ya mwaka huu ni “Vyombo vya Habari kwa Demokrasia: Tasnia ya Habari na Uchaguzi katika Nyakati za Upotoshwaji wa Taarifa.” Guterres amesema, “hakuna demokrasia iliyo kamilifu bila kupata taarifa kwa uwazi na za kuaminika. Ni msingi wa kujenga taasisi za haki za zisizo na upendeleo, na kuwawajibisha viongozi na kila wakati kueleza mamlaka ukweli.” Ameongeza kuwa taarifa za uwazi na za kuaminika ni ni muhimu zaidi wakati wa msimu wa uchaguzi, ambayo ndio maudhui ya sik uya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani mwaka hu una kwamba , “taarifa sahihi na si za uongo zinapaswa kuongoza watu wakati wanachagua wawakilishi wao.” Hata hivyo amesema wakati teknolojia imebadili jinsi tunapokea na kubadilishana taarifa, wakati mwingine inatumika kudanganya maoni ya umma au hata kuchochea ghasia na chuki.
3kimataifa
Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimelituhumu Bunge kwa madai ya kuvunja sheria kwa kuomba fedha za ziada nje ya bajeti yake iliyoidhinishwa bila kupitisha maombi hayo bungeni kama katiba inavyotaka. Chadema imesema Bunge limevunja katiba, ibara ya 137 (3), (a) na (b) huku wakidai pia Waziri wa Fedha amevunja ibara ya 136 na 137 (3) kwa kutoa fedha za ziada nje ya bajeti iliyopitishwa. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji, alisema kati ya Juni 21 na Agosti 15, mwaka huu, Katibu wa Bunge aliandika barua tatu tofauti akiomba zaidi ya Sh bilioni 9 kwa Waziri wa Fedha na kwa Katibu Mkuu Hazina kugharimia bajeti ya ziada. “Tangu wakati huo hadi Agosti 15, Serikali ilishatoa shilingi bilioni 7 kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina bila kufuata masharti ya katiba na inategemewa itaendelea kutoa shilingi bilioni 2.5 kulipia gharama za posho ya jimbo ya Juni ambayo haijalipwa kwa ukamilifu,” alisema Dk. Mashinji. Alisema fedha zilizotolewa kama bajeti ya ziada zilitumika kulipa posho za jimbo, kujikimu, vikao, saa za ziada kwa watumishi na posho ya kamati maalumu kwa kipindi cha Mei hadi Juni. “Katiba inamtaka waziri kuwasilisha bungeni maombi ya bajeti ya ziada na baada ya Bunge kuyakubali, atawasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali kuidhinisha matumizi ya fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali. “Hatutaki kuamini kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amehusika kuidhinisha malipo haya, maana hata kwenye mawasiliano yaliyopo hajawahi kupewa nakala,” alisema. Alisema Bunge likiwa kama mhimili unaojitegemea, linapaswa kujiendesha bila kuwa tegemezi kwani ndilo linalopitisha bajeti yake na ya Serikali. Alisema katika mwaka wa fedha wa 2016/17 Bunge liliidhinisha Sh bilioni 92.7 kwa matumizi ya kawaida, Sh bilioni 23.80 mishahara, Sh bilioni 68.27 matumizi mengineyo na Sh bilioni 7 miradi ya maendeleo. “Bunge ni taasisi ambayo kalenda yake na idadi ya wajumbe vinafahamika, hivyo wanapopitisha bajeti wanakuwa wakijua ni kiasi gani kitahitajika katika mwaka husika wa fedha. “Tukianza kupuuza katiba, maana yake tunarudi kwenye hali ya kuangalia nani ana nguvu na ataamua nini kukicha,” alisema. Dk. Mashinji alisema pia uendeshaji wa shughuli za Bunge umekuwa ukiichanganya jamii na alitahadharisha kuwapo hatari ya kutengeneza nchi isiyofuata na kuzingatia taratibu. “Kuna udhaifu mkubwa katika uongozi wa Bunge ukiongozwa na Spika. Kiongozi jasiri ahitaji kuongea kwa sauti kali, kutumia nguvu kubwa ama ubabe bali ni yule anayefuata taratibu tulizojiwekea. “Ajipe muda kutafakari je, uongozi wake unaleta hali ya utengamano ama utavuruga jamii… kipimo cha uimara wa kiongozi ni kusimamia katiba,” alisema Dk. Mashinji. Chadema imeitaka Serikali na Bunge kutoa majibu ya kina kuhusu ukiukwaji na uvunjwaji wa katiba na wale wote waliohusika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria. “Tunaamini kuwa haya yanaweza kumalizika kama tutakuwa na katiba mpya iliyotokana na maoni ya wananchi, tutatumia njia za kidemokrasia na kidiplomasia kuhakikisha tunapata mwafaka wa katiba mpya. Endapo hazitazaa matunda tutaomba wananchi wafanye maamuzi,” alisema. Kutokana na madai hayo ya Chadema MTANZANIA lilimtafuta Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila ili kupata ufafanuzi, lakini simu yake ya mkononi iliita bila kupokewa.
1kitaifa
VYAMA vya siasa nchini vimetakiwa kutekeleza matakwa ya sheria ya msajili wa vyama vya siasa ambayo inavitaka vyama hivyo kuzingatia uwepo wa Muungano katika katiba za vyama vyao ikiwa ni moja ya tunu ya taifa.Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu ya miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mohamed Ali Ahmed alisema muungano ndiyo utambulisho wa taifa la Tanzania. Alisema sheria ya vyama vya siasa imetambua umuhimu wa kuwepo kwa muungano katika katiba za vyama hivyo kwa ajili ya kupata viongozi ambao watafahamu umuhimu wa muungano.Alisema marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2019 kifungu cha 6 (5) unavitaka vyama vya siasa vyenye usajili nchini katika maandalizi ya katiba zao na sera kuzingatia suala la muungano kama kipaumbele cha kwanza. Aidha katika marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2019 pia umevitaka vyama vilivyopata usajili kuyatambua Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 kuwa ndiyo yaliyowakomboa wananchi wa Zanzibar na wazalendo kushika hatamu ya kuongoza dola. ‘’Katika marekebisho ya sheria ya msajili wa vyama vya siasa suala la kuyaenzi Mapinduzi ya Zanzibar limetambuliwa rasmi kwa lengo la wanachama na wananchi kwa ujumla kuyatambua kwa mujibu wa sheria,’’alisema.Mambo mengine ya msingi ambayo yametakiwa kutambuliwa na kuingizwa katika katiba na sera za vyama vya siasa ni mwenge wa uhuru, demokrasia na utawala bora. Akifafanua zaidi kuhusu Mwenge wa Uhuru, alisema upo kwa ajili ya kujenga umoja na mshikamano wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ndiyo maana hutembezwa nchini kote. Alisema Mwenge wa Uhuru hata muundo wake umewekwa alama ya Adamu na Hawa ambayo ni nembo rasmi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukionesha ushirikiano wa pamoja.
1kitaifa
  Na UPENDO MOSHA-ROMBO KIFO cha Mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), jijini Dar es Salaam, aliyeuawa kwa kupigwa risasi juzi, Akwilina Akwilini, kimezua simanzi nyumbani kwao, Kijiji cha Marangu Kitowo, Kata ya Olele, Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro, huku wazazi wake wakitoa ujumbe mzito kwa Serikali. Kutokana na hali hiyo wameitaka Serikali itoe maelezo ya kina kuhusu mauji ya ovyo ya raia wasiokuwa na hatia sambamba na kutaka uchunguzi huru na waliohusika na mauji ya mtoto wao wachukuliwe hatua za kisheria. MTANZANIA ilifika nyumbani kwao marehemu jana na kutembelea maeneo mbalimbali ya kijiji hicho, alishuhudia watu walivyokuwa na simanzi na jinsi walivyokuwa wakizungumzia kifo hicho. Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwake, mama mzazi wa marehemu, Constansia Akwilini, alisema familia yake imepokea tukio hilo kwa mshtuko wa aina yake. “Huu ni msiba uliogusa moyo wangu sana na familia yetu kwa ujumla nashindwa nikuelezeeje. “Kitendo hiki hakipaswi kufumbiwa macho, haya ni mauaji ya ovyo ya raia wasiokuwa na hatia na yanapaswa kupingwa kwa nguvu zote ili kulinda amani na usalama wa nchi yetu. “Kifo hiki kimeacha pengo kubwa katika familia yetu kwa sababu huyo ndiye mtoto pekee tuliyekuwa tukimtegemea katika familia yetu kwa siku zijazo kwa sababu ndiye aliyekuwa na mwelekeo wa kusoma,” alisema Constansia huku akitokwa na machozi. Kwa mujibu wa mama huyo, Akwilini alifikia hatua hiyo kielimu kutokana na ufadhili wa shangazi yake na kwamba alikuwa ni mtoto wa sita kuzaliwa kati ya watoto wanane wa familia hiyo. BABA MZAZI ATOA NENO Akizungumzia historia ya marehemu baba mzazi wa marehemu, Akwilini Shirima, alisema Akwilina alizaliwa Aprili Mosi, mwaka 1996, katika Kijiji cha Marangu Kitowo, Kata ya Olele, wilayani Rombo. Alipata elimu yake ya msingi katika Shule ya Msingi Kitongoria na kuhitimu mwaka 2009. Baada ya hapo, Akwilina alijiunga na shule moja ya sekondari iliyoko mkoani Iringa ambako alihitimu mwaka 2014. Baadaye, alichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Embauwai, iliyoko Wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha. Kwa mujibu wa mzazi huyo, Akwilina hakumaliza kidato cha sita shuleni hapo kwani baada ya afya yake kudhoofika mara kwa mara kutokana na hali ya hewa ya Ngorongoro, alihamia mkoani Iringa ambako alihitimu kidato cha sita, mwaka 2016 Kuanzia Oktoba mwaka jana hadi alipofikwa na mauti, Februari 16, mwaka huu, alikuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), akisomea shahada ya kwanza ya ugavi na ununuzi. TABIA YA MAREHEMU  Akizungumzia tabia ya binti yake huyo, Akwilini alisema mtoto wake alikuwa ni mtu mwenye misimamo ya kimaisha na alipenda kuzungumza na kucheka na kila mtu. “Watu wanasema mtu akishakufa ndiyo tunamzungumzia vizuri, lakini mwanangu alikuwa ni mcheshi, asiyependa kugombana na watu. “Alipenda kazi na kusoma na pia alikuwa na misimamo ya kimaisha na niliamini kama angefanikiwa kuishi zaidi, angetusaidia kuondokana na umasikini kwa sababu ndiye mtoto pekee aliyesoma kati ya watoto wangu wanane,” alisema. DADA WA MAREHEMU Naye dada wa marehemu, Teddy Akwilini, alisema alizungumza na mdogo wake, Februari  12 na 15, mwaka huu ambapo walizungumzia masuala ya maisha na kuwaahidi kwenda Rombo kuwatembelea, Julai mwaka, huu baada ya kufunga chuo. “Aliniambia anatamani sana kuja nyumbani na kasema Julai angekuja kutuona maana alikuwa amewakumbuka baba na mama. “Nakumbuka aliniambia alikuwa akitafuta sehemu ya kufanyia masomo yake kwa vitendo, lakini inaniuma sana, kwamba amefariki bila kutuona na atakuja akiwa kwenye jeneza. “Mimi ndiye mtoto wa kwanza katika familia yetu na kwa bahati mbaya mimi na wengine hakutubahatika kusoma zaidi ya darasa la saba kutokana na ufukara wa familia yetu. “Kwa hiyo, kifo cha mdogo wangu ni pigo kubwa sana tena sana katika familia yetu kwa sababu kila mmoja alikuwa akimtegemea na tulikuwa tukimwombea kila siku kwani alikuwa na ndoto nyingi za kutubadilisha kamaisha,” alisema dada huyo huku akibubujikwa na machozi. MAJIRANI WAZUNGUMZA Mmoja wa majirani wa Akwilina, Dismas Shirima, alisema marehemu alikuwa ni mtu wa watu na alikuwa ni mtu wa kupenda kuwasaidia ndugu zake. Kwa upande wake, jirani mwingine, Fausta Focus, alisema marehemu alikuwa ni mfano wa kuigwa kijijini hapo kutokana na tabia yake ya kupenda kujitolea katika shughuli mbalimbali za kijamii. SERIKALI KUGHARIMIA MAZISHI Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema wizara yake itagharimia mazishi ya mwanafunzi huyo aliyeuawa kwa kupigwa risasi Februari 16 mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Profesa Ndalichako alisema yeye pamoja na katibu mkuu wa wizara yake, watasimamia shughuli zote za msiba huo. “Serikali imepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mwanafunzi huyu na alikuwa miongoni mwa wanafunzi wa kike waliojipambanua  kwa kujua umuhimu wa elimu, alihakikisha anasoma kwa bidii kwa manufaa yake na familia yake, lakini pia alikuwa miongoni mwa wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu. “Kifo chake kimeleta simanzi kwa wananchi wote na Serikali kwa ujumla alikuwa katika majukumu yake ya kawaida akipeleka barua yake ya mafunzo kwa vitendo Bagamoyo ndipo umauti ukamkuta,” alisema Profesa Ndalichako. Kutokana na tukio hilo, Profesa Ndalichako alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua stahiki kwa wahusika. Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusuph Masauni, alisema Serikali haiwezi kuyaacha matukio hayo yapite kama yalivyo, hivyo imeyachukulia kwa uzito unaostahili. Masauni alisema uchunguzi wa tukio hilo utafanyika haraka iwekezanavyo, kwa weledi na utaalamu ili haki itendeke. “Tutafanya uchunguzi na kuwachukulia hatua kali za kisheria wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo, Serikali tunasikitishwa na kifo cha mwanafunzi huyu, pia na kujeruhiwa raia,” alisema Masauni. Alisema uchunguzi huo utakuwa mpana na utakuwa fundisho kwa kuwachukulia hatua kali za kisheria. ASKARI SITA WASHIKILIWA Baada ya tukio hilo la kuuawa kwa mwanafunzi huyo Jeshi la Polisi limtangaza kuwashikilia askari wake sita ambao wanadaiwa kuhusika na tukio hilo la mauaji ya mwanafunzi huyo. Mwanafunzi huyo, aliuawa juzi jioni kwa risasi wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), waliokuwa wakielekea kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Jimbo la Kinondoni, jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro  Mambosasa, alisema mbali na kuwashikilia askari hao, pia wamewakamata wafuasi 40 wa Chadema. Pia, alisema wanaendelea kuwatafuta viongozi wa chama hicho, walioshiriki kushawishi maandamano hayo. “Februari 16, mwaka huu, Chadema walikuwa na mkutano wa kufunga kampeni katika Viwanja vya Buibui, Mwananyamala ambapo Mwenyekiti wao Mbowe, alisikika akikatisha mkutano na kuhamasisha wafuasi wao kuingia Kinondoni ili kumshinikiza mkurugenzi awape barua za viapo vya mawakala wa chama hicho. “Pia Mbowe alisikika akiwatukana viongozi wakuu wa nchi akiwa jukwaani, suala hili linaendelea na uchunguzi wake. “Kadiri wanachama hao walipokuwa wakisogea mbele, idadi ya waandamanaji iliongezeka na walipofika Barabara ya Kawawa, maeneo ya Mkwajuni, walifunga barabara ya mabasi ya mwendo kasi na ya kawaida na kusababisha msongamano mkubwa wa magari. “Polisi walifika katika eneo la tukio na kuzuia maandamano hayo, lakini ghafla wafuasi wa Chadema walianza kuwashambulia askari kwa mawe na chupa, fimbo na silaha zingine za jadi na kuwajeruhi askari wawili. “Katika harakati za kujihami na mashambulizi  yaliyozidi, polisi walitumia silaha za kutuliza ghasia, lakini nazo zilionekana kushindwa kuwatawanya waandamaji hao, ndipo walipiga risasi za moto hewani na kufanikwa kuwakamata watuhumiwa 40 na kutawanya maandamano hayo. “Siku hiyo hiyo, saa 1:30 usiku, polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ilipata taarifa za kiintelijensia, kwamba katika purukushani hizo, kuna mwanamke mmoja alipoteza maisha na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala. “Pamoja na kuendelea na uchunguzi wa kifo cha mwanafunzi huyo, tumepata taarifa zingine, kwamba watu wawili walijeruhiwa maeneo ya miguuni na kitu chenye ncha kali ambao ni Erick John (24) na Innocent Mushi (23),” alisema Kamanda Mambosasa. JPM AAGIZA UCHUNGUZI Rais Dk. John Magufuli, amesikitishwa na kifo cha mwanafunzi huyo na kutoa pole kwa familia, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huo. “Nimesikitishwa sana na kifo cha mwananafunzi Akwilina Akwilini wa chuo cha NIT, natoa pole kwa familia, ndugu, wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba huo. “Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliosababisha tukio hili,” aliandika Rais Magufuli katika ukurasa wake wa twitter. MTANDAO WA WANAFUNZI Wakati huo huo, Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), umesema utafungua kesi ya madai dhidi ya Jeshi la Polisi nchini kutokana na kifo cha mwanafunzi Akwilina. Akizungumza jana waandishi wa habari, Mwenyekiti wa TSNP, Abdul Nondo, alisema watafungua kesi hiyo kwa kushirikiana na wanasheria wa taasisi mbalimbali ili iwe fundisho kwa askari wengine. Alisema kwamba, sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma Saidizi, sura ya 332, kifungu cha 29, kinaeleza mazingira ambayo polisi wanatakiwa kutumia nguvu kutuliza ghasia. “Kama mwanafunzi huyu asiye na hatia ameuawa kwa mazingira ya namna hii, TSNP tunaona kuwa hili ni shambulizi dhidi ya wanafunzi nchini bila sababu yoyote. “Tunataka hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya askari polisi waliotenda unyama huu na kukatisha haki ya kusoma na ya kuishi kwa mwanafunzi mwenzetu. “Polisi, wamekiuka maadili ya kazi yao katika kulinda amani, Jeshi la Polisi, lijitathmini upya na kujipima namna linavyoenenda na kama lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa raia,” alisema Nondo. Mtandao huo pia umemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba kujiuzulu ili kuonyesha uwajibikaji. “Tumeshuhudia watu wakipigwa risasi, kutekwa, miili kuokotwa kandokando ya bahari na haya yote yanatokea pasipokuwapo kwa uchunguzi wa kina. “Tanzania tumekuwa na chunguzi nyingi zinazoendelea na hadi sasa hazina majibu. Hivyo basi, sisi hatuamini kama uchunguzi pekee ndiyo utakuwa chachu ya kukomesha matendo yanayoendelea nchini. “Ni muda muafaka sasa, waziri husika (Dk. Nchemba), kujiuzulu kama njia ya kuonyesha uwajibikaji kama alivyowahi kujiuzulu, Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani. “Lakini niwaambie kwamba, kama matukio ya aina hii yataendelea, basi tutaitisha maandamano ya wanafunzi ya vyuo vyote nchini kulalamikia uvunjwaji wa haki za binadamu,” alisema Nondo. Naye Mwalikishi wa Klabu za Haki za Binadamu nchini, Alfahad Thabo, alisema hivi sasa wana mashaka na usalama wao kwa sababu vitendo hivyo vimekuwa vikijirudia mara kwa mara. ACT  WAMVAA MWIGULU Nayo ngome ya Vijana wa Chama cha ACT Wazalendo, imemtaka Dk. Mwigulu ajiuzulu kutokana na kuongezeka kwa matukio ya mauaji nchini. Pia, ngome hiyo imewataka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro na Kamanda Mambosasa, nao wajiuzulu. Aidha ngome hiyo imewataka viongozi wote wa vyama vya upinzani kushirikiana na kuitisha maandamano nchi nzima ili kupinga mauaji, utekaji watu na ubakwaji wa demokrasia. Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Ngome hiyo, Likapo Likapo, alisema wamefikia hatua hiyo kutokana na kuongezeka kwa matukio ya mauaji, utekaji na kupotea kwa watu huku jeshi hilo likishindwa kutoa taarifa za kina. CHADEMA WATUPA MZIGO Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema, Kigaila Benson aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mtu wa kwanza aliyesababisha kifo cha Akwilina ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Kinondoni, Aron Kagurumjuli kwa kukataa kutoa viapo kwa mawakala wao. Kigaila alisema polisi siku hiyo walilenga kuwapiga risasi viongozi wakuu wa chama hicho kwa sababu majeruhi wote wanne ambao wako hospitali ni walinzi wa viongozi hao. “Tulikuwa na msafara siku ile kwa sababu tulikuwa tunakwenda kwa mkurugenzi kudai viapo vya mawakala wetu hivyo mtu wa kwanza alisababisha kifo cha huyu mwanafunzi ni msimamizi wa uchaguzi. “Risasi iliyopigwa ikamwua yule mwanafunzi Mambosasa (Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa) anasema ni moja halafu wamekamata askari sita, sasa askari wote hao walipiga risasi moja na aliyeamuru risasi zipigwe juu ni nani? “Risasi zile zililenga viongozi wa chadema ndio maana waliopatwa ni walinzi wao. Watu wanne wote waliopigwa risasi ukiachana na huyo mwanafunzi wako hospitali wamepigwa sehemu za nyonga na miguu,”alisema Kigaila. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema chama hicho kinatoa pole kwa familia ya marehemu na kwamba tayari Mbunge wa Kibamba, John Mnyika na Meya wa Ubungo wametangulia nyumbani kwa ndugu wa mwanafunzi huyo eneo la Kibamba. “Kwa sasa kina Mnyika wametangulia nyumbani kwa ndugu ambao walikuwa wakimlea marehemu baada ya hapo tutawaeleza ushiriki wetu kwenye msiba huu mzito. “Jeshi la polisi lichukue hatua waache visingizio, tumechoka na mauaji haya…tumechoka viongozi wetu kuwindwa kama digidigi ,”alisema Mrema. Alieleza kushangazwa kwa hatua ya Kamanda Mambosasa kumtafuta Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe wakati hajajificha na kwamba hajapewa wito wowote wa kwenda kuripoti polisi. “Wanazo taratibu za kumwita mtu polisi, wanafahamu nyumbani kwake, ofisini kwake makao makuu ya chama au ofisi za Bunge,”alisema. HABARI HII IMEANDALIWA NA UPENDO MOSHA (KILIMANJARO), Asha Bani, Nora Damian, Elizabeth Hombo na Tunu Nassor (DAR)
1kitaifa
Inatarajiwa kuwa fedha hizo za kigeni zitokanazo na kahawa, ni kutoka Dola za Marekani milioni 230 kwa sasa na kufikia Dola milioni 325 kwa mwaka 2020.Taarifa ya Bodi ya Kahawa (TCB) mjini Moshi juzi imeeleza kuwa uzalishaji kwa sasa umeongezeka kutoka tani 55,000 mwaka 1983/84 hadi kufikia zaidi ya tani 75,000 za Kahawa.Aidha, taarifa hiyo imefafanua kuwa zaidi ya kaya 400,000 zinajihusisha na kilimo cha mibuni aina ya Robusta na Arabika nchini.Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wakulima hao huchangia asilimia 90 ya uzalishaji wote huku asilimia 10 ya kahawa ikitokana na wakulima wanaomiliki mashamba makubwa (Estate).TCB imesisitiza kuwa hivi sasa kilimo cha mibuni nchini hutoa ajira kwa Watanzania milioni 2.4, ambapo kahawa aina ya robusta huchangia asilimia 40 ya uzalishaji wa kahawa hapa huku arabika ikichangia asilimia 60 Taarifa hiyo imeeleza kuwa zaidi ya hekta 265, 000 nchini ndizo zinazotumika kwa kilimo cha zao hilo katika maeneo mbalimbali ya nchi.Aidha, imeelezwa kuwa kilimo cha mibuni kinakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo za kukidhi mahitaji makubwa ya miche.Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na TCB kuongeza upatikanaji wa miche ya uhakika ya aina bora ya mibuni ya arabika na robusta, ambapo mkazo unapaswa ulenge kuzalisha miche milioni 75, ili kupanda eneo la hekta 56,000 ndani ya miaka mitano ijayo.
0uchumi
Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Muro, kikosi kitakachoondoka sio 21 na sasa hata wale waliopangwa kuachwa yaani Antony Mateo, Geofrey Mwashiuya na Benedikti Tinoco watakwenda na kufanya idadi ya wachezaji jumla kufikia 24.Awali, walitangaza kuondoka juzi kwa ndege ya Shirika la Ndege ya Afrika Kusini lakini ilishindikana baada ya shirika hilo kushindwa kuwapatia ndege ya kuunganisha mapema mjini Johannesburg kwenda Curepipe na hivyo wakaamua kukodi ndege ambayo itawasubiri baada ya mechi kesho na kuwarudisha.“Safari imeiva, jumla ya wachezaji 24 wataondoka kuelekea Mauritius wakiongozana na viongozi saba wa benchi la ufundi, kikosi kimekamilika tunaomba mashabiki waiombee timu ifanye vizuri,” alisema Muro.Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Jumamosi kuanzia Saa 9:30 alasiri kwa saa za Mauritius Uwanja wa Curepipe kabla ya timu hizo kurudiana wiki mbili baadaye Dar es Salaam. Kikosi hicho jana kilifanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini.Lengo la kwanza lililowekwa na timu hiyo ni kufika katika hatua ya makundi. Kocha wa Yanga Pluijm alisema kikosi kimejipanga na kiko tayari kwa mapambano.Alisema mbinu atakazotumia hazina tofauti na zile ambazo amekuwa akitumia kwenye Ligi Kuu Tanzania bara.Mkuu wa Msafara wa Yanga katika safari hiyo ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Ayoub Nyenzi wakati upande wa viongozi wa timu hiyo wanaokwenda ni Kaimu Katibu Mkuu, Baraka Deusdedit na Muro.Kikosi kitakachoondoka leo ni Makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Deo Munishi ‘Dida’ na Benedicto Tinocco.Washambuliaji ni; Malimi Busungu, Paul Nonga, Amissi Tambwe (Burundi) na Donald Ngoma (Zimbabwe).Mabeki; Juma Abdul, Mbuyu Twite (DRC), Oscar Joshua, Mwinyi Mngwali, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Vincent Bossou (Togo) na Pato Ngonyani huku Viungo ni; Said Juma ‘Makapu’, Salum Telela, Thabani Kamusoko (Zimbabwe), Haruna Niyonzima (Rwanda), Simon Msuva, Issoufou Boubacar (Niger), Godfrey Mwashiuya na Deus Kaseke.Kikosi hicho kitakaporejea kitakwenda moja kwa moja kuweka kambi Pemba kujiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya watani wao Simba utakaochezwa Februari 20, mwaka huu.
2michezo
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa, wilaya na viongozi wengine kuhakikisha wanasimamia uanzishwaji wa Kamati za Ulinzi wa Wanawake na Watoto katika ngazi za mikoa, halmashauri, kata na vijiji. Alisema maelekezo hayo yapo katika mwongozo wa uratibu wa Mpango wa Taifa wa Kutotokemeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.Waziri Mkuu Majaliwa vile vile aliwaagiza wakurugenzi wa halmashauri nchini kuanzisha programu za kijamii za kutokomeza ukatili wa kijinsia katika halmashauri husika zitakazozingatia hali halisi na kuzitengea bajeti kama ilivyoelekezwa kwenye mpango huo wa kitaifa .Alisema serikali imefanya mambo mengi katika kutukomeza ukatili huo, lakini pia inatumia gharama nyingi katika kushughulikia waathirika wa ukatili wa kijinsia ambapo fedha hizo zingeweza kutumika katika kutoa huduma nyingine katika jamii.“Kimsingi, Serikali ya Awamu ya Tano haiwezi kuvumilia vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kuwa vinaathiri maendeleo yetu na kusababuisha uvunjivu wa amani,” alisema. Alisema serikali tayari imeanzisha madawati 415 kwa ajili ya kuhudumia waathirika wa ukatili, lakini akalitaka Jeshi la Polisi nchini kuongeza huduma hiyo kwa kushughulikia ukatili wa kijinsia dhidi ya watu wenye ulemavu.Waziri Mkuu akizungumzia vitendo vya ukatili wa kijinsia unatumika mitandano, alizitaka kampuni za simu kudhibiti na kuwachukulia hatua kali wote wanaotumia mitandano kudhalilisha na kutukana wengine. Pia aliitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusimamia kikamilifu wale wote wanaojidanganya kwamba kuna mitandao haionekani na kuhakikisha wanaendesha vitendo vya udhalilishaji wakamatwe na kushughulikiwa. Pia alizitaka taasisi kama Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kuendelea kuwachukulia hatua wale wote ambao wanatumia mitandao kwa nia ya kudhalilisha watu wengine.
1kitaifa
NEW YORK, MAREKANI MKE wa rapa Kanye West, Kim Kardashian, inadaiwa anasumbuliwa na ugonjwa wa meno, hivyo anashindwa kutafuna vitu vigumu. Mrembo huyo aligundua hilo juzi jijini New York, na kujikuta akishindwa kula chakula kutokana na maumivu makali kwenye meno. Kupitia akaunti yake ya Instagram, mrembo huyo aliweka wazi kupatwa na tatizo hilo, lakini iliweza kuwasiliana na daktari wake kwa ajili ya matibabu. “Nilipatwa na maumivu ya ghafla nikawa nashindwa kutafuna kitu chochote chenye ugumu, lakini niliwasiliana na daktari wangu kisha nikafanyiwa matibabu, kwa sasa naendelea vizuri na chakula kinaliwa kama kawaida,” aliandika Kim Kardashian.
4burudani
Wakati mabingwa watetezi wa Ligi kuuya soka Tanzania bara Simba wakishusha kipigo cha goli 3 kwa bila dhidi ya Mtibwa wakiwa ugenini watani zao Yanga wameshindwa kutamba nyumbani. Katika mchezo uliopigwa uwanja wa uhuru Yanga ambayo maskani yake ni Jangwani jiji Dar es Salaam imeshindwa kutamba na kujikuta ikiambukia droo ya goli 1 kwa 1 dhidi ya Mbeya City. Mbeya City walianza kuongoza katika mchezo huo baada ya beki wa Yanga Lamine kujifunga goli dakika ya 42 ya mcgezo huo ulioanza saa 1 jioni katika uwanja wa uhuru. 'Bao la kujitundika', Lamine Moro alipowazawadia Mbeya City. 60' | Yanga SC 0-1 Mbeya City. LIVE #AzamSports2 #LigiKuuTanzaniaBara #VodacomPremierLeague #VPLUpdates #VPL #YangaSC #MbeyaCity #YangaMbeya @yangasc @baraka_mpenja @officialmbeyacityfc @antonionugaz A post shared by Azam Sports (@azamsports2) on Feb 11, 2020 at 9:16am PST Hata hivyo kipenzi cha wanajangwani Bernard Marrison alifanikiwa kuisawazishia Yanga kwa bao la kichwa Dakika ya 72 ya mchezo huo ambao ulijawa na shamrashamra kwakuwa Yanga ilikuwa inaadhimisha miaka 85 tangu kuanzishwa kwake. Bao la Wananchi, Bernard Morrison alipoisawazishia Yanga kwa assist ya Juma Abdul tena. FT: Yanga SC 1-1 Mbeya City. #AzamSports2 #LigiKuuTanzaniaBara #VodacomPremierLeague #VPLUpdates #VPL #YangaSC #MbeyaCity #YangaMbeya @yangasc @baraka_mpenja @officialmbeyacityfc @antonionugaz A post shared by Azam Sports (@azamsports2) on Feb 11, 2020 at 10:18am PST Yanga ilitawala mchezo huo kwa asilimia 66 na ilipiga mashuti ya kulenga goli matano kwa sifuri huku ikipata kona 9 kwa moja. Aidha katika maandalizi ya mchezo huo Yanga ilijinasibu kuwa ingeifunga timu hiyo ambayo haijawa na msimu mzuri kwa mwaka huu lakini imekuwa tofauti wameishia kulingana nguvu.
2michezo
JESHI la Polisi Tanzania, Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), limewasilisha mifumo miwili ya teknolojia katika mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na limesema lipo tayari kuipeleka katika nchi zote za jumuiya hiyo zisizo na teknolojia hiyo. Mifumo hiyo iliyobuniwa na wataalamu wa Tehama wa jeshi hilo nchini, ni wa Usimamizi wa Makosa ya Usalama Barabarani na kupata Taarifa ya Upotevu ya Polisi kwa njia ya mtandao bila kulazimika kwenda kituo cha Polisi. Jeshi hilo, Kitengo cha Tehama, Makao Makuu, limeifikisha mifumo hiyo katika mkutano huo unaoendelea jijini Dar es Salaam, unaowahusu mawaziri wa sekta ya Tehama, Habari, Mawasiliano, Uchukuzi (Usafirishaji) na Hali ya Hewa kutoa elimu na kueleza utayari wao kuzisaidia nchi nyingine za SADC. Akizungumza na gazeti hili juzi katika eneo la mkutano huo; Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) walikoweka Banda lao la Jeshi la Polisi, Msimamizi wa Kitengo cha Tehama, makao makuu ya Polisi, Dar es Salaam, Gabriel Mukungu, alisema jeshi hilo lipo tayari kuifikisha mifumo hiyo katika nchi za jumuiya hiyo. “Tuko hapa kuoneshauwezo wa kiteknolojia wa Jeshi la Polisi. Mifumo hii miwili tuliyoileta hapa imebuniwa na vijana wa jeshi wenyewe, hatujanunua kutoka nje. Hatua hii imesaidia pia kupunguza gharama kwa Jeshi la Polisi na kwa wananchi,” alisema Mukungu. Akifafanua kuhusu mifu- mo hiyo, akianza na Mfumo wa Usimamizi wa Makosa ya Usalama Barabarani, Mukungu alisema miaka ya zamani wakosaji wa sheria za usalama barabarani wali- andikiwa faini kwa karatasi (vitabu vya notification) vilivyokuwa vinatengenezwa kwa gharama na kulazimika kusafirishwa mikoa yote kwa magari. Alisema baada ya kuanza kwa mfumo huo Aprili 2017 katika Mkoa wa Pwani na Julai kusambazwa nchi nzima, mabilioni ya Serikali yaliokuwa yakipokea sasa hakuna tena wizi huo kwa kuwa fedha zinapelekwa moja kwa moja serikalini na adhabu imeainisha kosa la dereva na mwenye gari tofuati na awali. “Sasa hivi mtu akikosa, ana nafasi ya kulipa faini ya kosa lake katika kipindi cha siku saba na kwa wanaokiuka utaratibu huo wanageuka kuwa wadaiwa sugu na hukamatwa kwa kamera maalum zinazowekwa barabarani na kuwabana kulipa faini hizo mara mbili ya faini ya awali (penalty),” alisema Mukungu. Kuhusu Taarifa ya Upotevu ya Polisi (Police Loss Report), Mukungu alisema umeanza Julai Mosi mwaka huu na unafanya kazi nchi nzima. Alisema mtu aliyepoteza kitu anaingia moja kwa moja kwenye mtandao wa intaneti kwa tovuti ya https://lormis.tpf. go.tz kusajili taarifa zake za upotevu. “Masharti hapa ni lazima mtu awe na kitambulisho cha taifa. Tumefanya hivi ili kuhimiza kila mwananchi apate kitambulisho hiki kuonesha umuhimu wake. Kwa hiyo kama umepo- telewa na nyaraka kama vyeti, laini ya simu na kadi za benki, hana ulazima wa kwenda Kituo cha Polisi, anaweza kuipata ‘loss re- port’ mtandaoni,” alisema. Akieleza zaidi, Mukungu alisema gharama ya kuipata ni Sh 500 kiasi ambacho watu wengi wanaweza kukipata kwa njia ya simu ya mkononi. Hata hivyo, alisema mtu hatopata taarifa ya upotevu kwa vitu kama kadi ya gari, gari lenyewe na vyombo vya moto, hati za nyumba, mashamba, kampuni, silaha, kifo na mtu kupotea kwa kuepuka hatari ya mwizi wa vitu husika, hawajaziweka mtandaoni kuepuka matumizi mabaya na watu kujihalalishia vitu hivyo. “Kwa aina hii ya upotevu, mtu atalazimika kwenda kituo cha polisi”. Alisema hivi sasa wanaunganisha mifumo hiyo na kampuni za simu ili kurahisisha taarifa kuwafikia kampuni hizo mara moja kama zinavyowafikia Polisi.
1kitaifa
Na Malima Lubasha-Musoma MAHAKAMA Kuu Kanda ya Musoma, imewahukumu kunyongwa hadi kufa watu watatu kwa kosa la kumuua Tabu Makanya (58) kwa kumchinja na kutenganisha kichwa na kiwiliwili. Waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa ni Musiba Maregeba, Abeid Casimil na Ndaro Sumuni wote wakazi Kijiji cha Kwibara Kata ya Mugango Wilaya ya Musoma vijijini mkoani Mara, huku Wandwi Mugulu diwani wa Kata ya Mugango, akiachiwa huru. Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Girson Mdeme wa hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa Jamuhuri.  Jaji Mdeme, alisema ametoa adhabu hiyo ya kunyongwa hadi kufa kwa washtakiwa baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi saba pamoja na vielelezo vilivyotolewa mahakamani na upande wa mashtaka.  Awali washtakiwa hao walihukumiwa kunyongwa hadi kufa na Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza katika kesi namba 189/2013 ambayo hukumu yake ilitolewa Julai 14,2015. Jaji Mdeme alisema, wakati washtakiwa wakisubiri kunyongwa baada ya hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, walikata rufaa ambayo ilisikilizwa na na Mahakama Kuu Kanda ya Musoma  Agosti 16. Washtakiwa hao walikuwa wakituhumiwa kumuua Tabu Makanya (58) mkazi wa Kijiji cha Kwibara Kata Mugango, ambapo Februali 21 mwaka 2013 majira ya saa 5.00 usiku walivamia nyumba ya mwanamke huyo kwa kubomoa mlango kwa jiwe kubwa marufu fatuma. Ilidaiwa wakiwa na mapanga na tochi, baada ya kuingia ndani walitoa onyo kwa watoto wa Tabu na kuwata kukaa kimya bila kupiga kelele. Baada ya kuwatisha watoto, walimvamia mwanamke huyo kisha kumchinja na kutenganisha kichwa na kiwiliwili na kukiweka ndani ya mfuko wa sandarusi na kuondoka nacho.  Ilidaiwa wakati watuhumiwa hao wakiwa katika harakati za kutoka eneo la tukio, wananchi walifanikiwa kumkamata mtuhuniwa mmoja akiwa na kichwa hicho. Kuhusu diwani aliyekuwa amejumuishwa kwenye kesi hiyo, inadaiwa alikamata baada ya uchunguzi wa awali kuonesha kwamba yeye ndiye aliwatuma watu hao kumtafutia kichwa cha binadamu kwa makubaliano ya kuwapatia fedha.  Ilidaiwa kuwa, diwani huyo alitaka kichwa hicho ili kukitumia kishirikina kwenye masuala ya uvuvi wa samaki lakini baada ya jalada lake kupelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali, aliondolewa kwenye kesi hiyo.
1kitaifa
NA MWAMVITA MTANDA-KIGALI KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amefichua kuwa alifanya jitihada za kumshawishi aliyekuwa mshambuliaji wa timu hiyo, Emmanuel Okwi ili asalie Msimbazi, lakini nyota huyo wa kimataifa wa Uganda aligoma katakata. Okwi mwenye umri wa miaka 27, ameachana na Simba, baada ya mkataba wake kumalizika msimu msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku kukiwa na taarifa kuwa anakaribia kujiunga na Fujairah FC inayoshiriki Ligi Kuu ya Falme za Kiarabu (UAE). Mshambuliaji huyo, amekuwa na mchango mkubwa katika kikosi cha Simba, tangu alipojiunga nayo mwaka 2009, akitokea klabu ya SC Villa ya nyumbani kwako Uganda. Akiichezea Simba, Okwi amefanikiwa kutwaa mataji matatu ya Ligi Kuu Tanzania Bara huku pia akiiwezesha timu hiyo kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika katika mashindano yaliyopita. Katika fainali za mataifa ya Afrika(Afcon)zilizomalizika hivi karibuni na Algeria kutwaa ubingwa, Okwi aliisaidia Uganda kutinga hatua ya 16 bora, huku akifunga mabao mawili. Akizungumza na MTANZANIA kwa njia ya mtandao, Aussems alisema mshambuliaji huyo ambaye msimu uliopita wa Ligi Kuu alifunga mabao 14, ameacha pengo katika kikosi chake. “Nilizungumza na Okwi akiwa Misri na timu yake ya Taifa iliyokuwa inashiriki michuano ya mataifa ya Afrika(Afcon), nilimwambia bao nataka kufanya naye kazi. “Aliniambia anataka kubadilisha mazingira kwani amekaa sana Tanzania na ametumikia timu kubwa za Simba na Yanga hivyo anataka kumaliza muda wake wa soka nchi zingine,”alisema Mbelgiji huyo na kuongeza. “Pia niliongea na mabosi wa Simba wamuongeze dau maana nilifikiri labda tatizo lilikuwa fedha lakini bado hakuwa tayari.” Wakati huo huo, Aussem alizungumzia fununu za mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco, Simon Msuva kuwa yu mbioni kujiunga na Simba kwa kusema hakuwahi kuuomba uongozi wake umsajili, lakini akakiri ni mchezaji mzuri na anatamani kufanya naye kazi. “Namfahamu Msuva, ni mchezaji mzuri na ningependa kufanya naye kazi Simba,”alisema Aussems. Katika hatua nyingine, Klabu ya Simba imetangaza ratiba ya michezo minne ya kirafiki ya kikosi chake ambacho kwa sasa kimepiga nchini Afrika Kusini, kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa Afrika. Ratiba hiyo inaonyesha Julai 23, kikosi hicho kitashuka dimbani kujipima na Orbret TVET, Julai 24 itapepetana na Platinum Stars, Julai 27 kitavaana na Township Rollers na kukamilisha kwa mchezo dhidi ya miamba ya Afrika Kusini, timu ya Orlando Pires kwa kumenyana nayo Julai 30.
2michezo
WASHINGTON, MAREKANI  WAGOMBEA urais wa chama cha Democrat nchini Marekani wamemlaumu Rais Donald Trump baada ya kutokea visa viwili vya mashambulizi ya bunduki vilivyosababisha vifo vya watu 29 Texas na Ohio. Wagombea hao wanasema matamshi ya Trump ya kibaguzi dhidi ya walio wachache nchini humo yanachochea mgawanyiko na machafuko. Katika mikutano ya umma na hata kwenye televisheni wagombea kadhaa wamezungumzia haja ya kuwepo kwa sheria kali za udhibiti wa bunduki.  Pamoja na hayo wanasiasa hao wameelekeza kiasi kikubwa cha lawama zao kwa Trump wakisema mashambulizi hayo ya Dayton na El Paso yana uhusiano na matamshi yake ambayo amekuwa akiyatoa kwa miezi sasa dhidi ya wahamiaji na watu watu wasio wazungu. Seneta Bernie Sanders amesema “Namwambia Rais Trump, tafadhali achana na matamshi ya kibaguzi dhidi ya wahamiaji, wachana na chuki inayoshuhudia nchi hii ikitumbukia katika machafuko tunayoyaona.” Rais Trump mwenyewe amelaani mashambulizi yote mawili.  “Ninachotaka kusema ni kwamba hizi ni sehemu mbili nzuri na tunawapenda watu wake. Chuki haina nafasi katika nchi yetu na tutalishughulikia suala hilo,” alisema Trump. Alipoulizwa kuhusiana na hatua atakazochukua baada ya tukio hilo la mauaji, Trump alisema; “Tumefanya mengi zaidi kuliko tawala zilizopita na jambo hilo halizungumziwi sana, lakini tumefanya mengi kusema kweli. Lakini labda mengi zaidi yanastahili kufanyika.” Watu 20 waliuwawa katika duka la jumla la Walmat mjini El Paso huko Texas na polisi wanasema kisa hicho kitachukuliwa kama ugaidi wa ndani ya nchi wakati ambapo wanachunguza madai ya shambulizi lililotokana na chuki.  Mshukiwa wa tukio hilo, Connor Betts e huenda akahukumiwa kifo iwapo atapatikana na hatia.  Polisi pia inasema haijui bunduki hiyo iliponunuliwa ingawa inasema pia kuwa sheria za Texas zinakubali kubeba bunduki kubwa katika sehemu ya umma. Wakati hayo yakijiri wanafunzi waliokuwa darasa moja na Connor Betts huko Ohio wanasema kuna wakati alifukuzwa shule baada ya kuandika orodha ya watu anaotaka kuwauwa na orodha nyingine ya wasichana anaonuia kuwabaka.
3kimataifa
Na NORA DAMIAN, MWANAFUNZI Cynthia Mchechu, ambaye ameshika nafasi ya pili kitaifa kwenye matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika Novemba mwaka jana, amesema Rais Mstaafu wa Marekani, Barack Obama, amechangia mafanikio yake. Cynthia aliyekuwa akisoma Shule ya Sekondari ya Wasichana ya St. Francis Mbeya, alisema ndoto yake ya baadaye ni kuja kuwa mwanasheria. “Wakati Rais Obama anaapishwa mwaka 2009 (yeye alikuwa darasa la nne) nilifuatilia historia yake nikajikuta nimevutiwa nayo na kuamua kuongeza juhudi katika masomo.  “Kumwamini Mungu pia ni siri kubwa ya mafanikio yangu, uhusiano mzuri kati ya wazazi na walimu wangu na kusoma kwa bidii,” alisema. Akielezea ratiba yake ya kila siku mwanafunzi huyo alisema huamka saa 12:00 asubuhi kisha hufanya usafi wa mwili na wa shule. Ikifika saa 12:45 huenda kunywa chai hadi saa 1:15 wanapokwenda mstarini. Alisema kuanzia saa 1:30 huingia darasani hadi saa 10:20 jioni ambapo hutoka na kwenda kuoga kisha kwenda kupata chakula kuanzia saa 11:30 hadi saa 12:15 jioni ambapo huingia tena darasani kwa ajili ya kusali rozali. Alisema husali rozali hadi saa 1:00 usiku kisha kuingia kujisomea hadi saa 5:30 usiku na kwenda kulala. “Kidato cha kwanza hadi cha pili walikuwa wanalala saa 3:30 usiku lakini kidato cha tatu na cha nne tukawa tunalala sasa 4, lakini baadaye sisi wa kidato cha nne tulibadilishiwa ratiba tukawa tunalala saa 5:30 usiku,” alisema. ATAMANI KUWA MWANASHERIA Mwanafunzi huyo alisema matarajio yake ni kuja kuwa mwanasheria kwa sababu anapenda kutetea watu na anapenda kuona haki ikitendeka kila mahali. “Kuna gazeti lilimuandika Rais Obama kuwa ni mwanasheria, baada ya kulisoma ndoto yangu ikaanzia hapo…na nitaendelea kusoma kwa bidii nataka nije kusoma Chuo Kikuu cha Havard Marekani…nataka niwe mwanasheria tena jaji na ikiwezekana zaidi niwe jaji mkuu,” alisema. Aliwashauri wanafunzi kuwa na imani katika kile wanachokifanya na kuzingatia muda na kwenda mbele zaidi ya yale wanayofundishwa na walimu wao. Alisema pia anajivunia wakati alipokuwa kiongozi shuleni kwani aliweza kujifunza mambo mengi. “Nilikuwa dada mkuu msaidizi, kuna mambo mengi mazuri na ya kujifunza unakuwa mtu wa kati ya mwalimu na mwanafunzi kwahiyo unapata uchungu na utamu wa pande zote, kwakweli nilijifunza mambo mengi sana,” alisema. Mwanafunzi huyo alisema anapenda sana kusoma vitabu, kuandika mashairi na kusafiri. WAZAZI Cynthia ni mtoto wa pili kuzaliwa kati ya watoto wanne na msichana pekee katika familia ya Nehemia Mchechu na Mercy Mchechu. Mama mzazi wa Cynthia, Mercy alisema alikuwa akitegemea matokeo ya mwanawe kuwa mazuri kutokana historia yake katika madarasa ya nyuma. “Kwa kweli ni jambo la kumshukuru Mungu na ni ndoto ya kila mzazi kuona mwanawe anafanya vizuri katika mitihani. Cynthia alikuwa akipenda sana mambo ya shule na amekuwa akisoma zaidi ya vitu ambavyo hupewa darasani. “Tuliposikia habari hizi kwamba ameongoza kitaifa tumefurahi sana tunaendelea kumwombea kwa sababu safari yake bado inaendelea,” alisema Mchechu.
1kitaifa
LAS VEGAS, Marekani MKALI JAY Z amefichua kwamba, hafikirii kuachana na muziki kwa kuwa bado hajafikia malengo aliyojiwekea kabla ya kukaa pembeni. Staa huyo anayetamba na albamu yake ya 4:4:4 ambayo inafanya vizuri sokoni kwa sasa, alidai kuwa mbali na mafanikio, muziki uko kwenye damu yake, hivyo huenda ikamchukua muda kuachana nao. “Nataka kuendelea kufanya vizuri kadiri nitakavyoweza. Nina mipango mingi, zaidi ni kufurahia kazi nzuri na si kupata fedha,” alisema rapa huyo. Itakumbukwa kuwa kutoka kwa albamu yake hiyo kuliambatana na kuibuka upya kwa bifu lake na swahiba wake wa zamani, Kanye West. Lakini pia, ni baada ya albamu hiyo ndipo Jay Z mwenyewe alipofichua kuwa aliwahi kumsaliti mkewe, Beyonce.
4burudani
Shirika la Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF) limeandaa kongamano la kitaifa kujadili masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa shirika hilo Koshuma Mtengeti amesema, lengo la kongamano hilo ni kutafuta namna ya kutokomeza ukatili kwenye jamii.Kongamano hilo litakalofunguliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa litafanyika Machi 21-22, katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) litahudhuriwa na wajumbe 600.Kati ya mada zitakazojadiliwa ni pamoja na ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, ukatili wa kimtandao, hali ya ukatili kwenye familia na mashuleni, rushwa ya ngono vyuoni na nyinginezo.“Nchi yetu ina sera nzuri zinazopinga ukatili wa aina zote lakini matukio ya ukatili yanaendelea, hivyo mijadala kama hii itasaidia sana kuendelea kuongeza uelewa wa masuala haya, na kuhimiza vitendo hivi kuendelea kuripotiwa, “amesema Mtengeti.Utafiti wa kidemografia wa afya 2015/16 unaonyesha kuwa 40% ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15-49 nchini wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kimwili tangu wakiwa na umri wa miaka 15.
1kitaifa
Msanii wa Bongo fleva Diamond Platinumz ameamua kufanyia kufuru msanii wake aliyemsajili hivi karibuni ‘Zuchu’. Zuchu ambaye ni mtoto wa msanii Hadija Koppa alisajiliwa na lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) Aprili 8. Tangu kusajiliwa mwamadada huyo katika lebo hiyo kubwa ya muziki nchini Nyota wa Bongo Fleva Diamondi amekuwa akimposti katika ukurasa wake wa Instagram mfululizo. Pengine ni mkakati wa Diamond kumpromoti msanii wake huyo mpya ambaye tayari ameachia nyimbo kadhaa ndani ya muda mfupi miongoni mwa nyimbo hizo ni ‘Wana’. Tangu Aprili 7, 2020 Diamond ashamposti Zuchu takribani mara 50, ikiwa ni wastani wa posti 5 kwa siku tofauti na kawaida yake. Welcome to @wcb_wasafi Family @officialzuchu …. Subscribe, ADD and Follow Zuchu on Her Official Social Media pages so that you can be the first one to get her First Release…. YOUTUBE: ZUCHU TWITTER: OfficialZuchu FACEBOOK: OfficialZuchu TIKTOK: OfficialZuchu SNAPCHAT: OfficialZuchu TRILLER: OfficialZuchu #WCB4Life @wcb_wasafi @boomplaymusic_tz A post shared by SIMBA..!🦁 (@diamondplatnumz) on Apr 8, 2020 at 11:36am PDT imagine jus Within 7 Days of her introduction to the Music industry…… @officialzuchu is Now Living to the Max with #PepsiMaxTz ….This Proves the Power of Women in the World🌍 Yani Ndani ya Siku 7 Tu!….Hakika Wanawake Wakiwezeshwa wanaweza…. Jamani Hii PEPSI MAX nyie Wenzangu Mshaionja??? Hebu Fanya Kuifata kwa Mangi Hapo Dukani Half utajua ni namna gani hawa PEPSI Wana balaa Zito!!👌🏼#PepsiBabaLao #PepsiMaxTz @pepsi_tz #IAmZuchu A post shared by SIMBA..!🦁 (@diamondplatnumz) on Apr 16, 2020 at 2:22am PDT Jeje, wewe Unaishije Mpaka Max? ISHI MPAKA MAX na PEPSI MAX…. @pepsi_tz #IshiMpakaMax #LiveToTheMax A post shared by SIMBA..!🦁 (@diamondplatnumz) on Apr 17, 2020 at 9:36am PDT
4burudani
MKUU wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti ameagiza kukamatwa mara moja kwa mawakala wawili wa kampuni binafsi  wanaopita vijijini wilayani Karagwe na Kyerwa kwa tuhuma za kuwapotosha na kuwalaghai wakulima wa kahawa wasikubaliane na mfumo wa serikali.RC Gaguti alitoa maelekezo hayo katika mkutano wa viongozi wa vyama vya msingi, watendaji wa kata na viongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoani KDCU Limited, wilayani Karagwe mara baada ya kukagua viwanda vitatu vya kukoboa kahawa vya Karim Amri, ASU Company Limited na KDCU Limited.“Nimeona nije kujionea msimu unaendeleaje na kama kuna changamoto yoyote tuitatue kwa pamoja na si kusubiri…... pia nina taarifa kuwa kuna mawakala wawili wa Kampuni binafsi wamekuwa wakipita vijijini kupotosha wakulima wasifuate mfumo wa Serikali ili baadae waje wanunue kahawa yao kwa bei ndogo tu namuagiza Kamanda Polisi Mkoa….wawakala hao wakamatwe mara moja.” aliagiza Mkuu wa Mkoa.Alisema kuwa maelekezo ya Serikali yapo wazi kuwa kama kuna mfanyabiashara yeyote anataka kununua kahawa, awasiliane na ofisi yake lakini awe na bei inayomnufaisha mkulima huku akidai kuwa mpaka sasa hakuna mfanyabishara aliyekidhi vigezo vya kununua zao hilo.Hadi sasa vyama vikuu vya ushirika mkoani Kagera; KCU 1990 LTD na KDCU LTD vimekusanya jumla ya kilogramu milioni 8.5 sawa na asilimia 20% ya malengo ndani ya msimu huu wa 2019/20.Taarifa zinabainisha zaidi kuwa Shilingi bilioni 6.2 zimelipwa kwa wakulima.
1kitaifa
Na AGATHA CHARLES – Dar es Salaam MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete, amesema hatamani kuwa rais bali anataka siku moja awe Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kauli hiyo aliitoa Dar es Salaam jana alipohojiwa katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Televisheni ya Clouds. Jibu hilo la Ridhiwani lilitokana na swali aliloulizwa na watangazaji wa kipindi hicho kama ana ndoto za kuwa rais wa nchi. “Sijawahi kutamani kuwa rais ila muda ukifika natamani kuwa Katibu Mkuu wa CCM,” alisema. Ridhiwani alisema mafaniko yake hadi hapo alipofikia ni kutokana na mchango wa baba yake ambaye ni Rais mstaafu Jakaya Kikwete. “Malezi yangu, kuzaliwa na kiongozi kumenisaidia kufika hapa, nisingezaliwa huko labda ningekuwa mtu tofauti na nilivyo, mzee wangu ana mchango mkubwa hata jimboni, ananipa changamoto, ananielekeza, ana nafasi ya kunishauri,” alisema. Pia alisema katika kutekeleza sera ya Tanzania ya viwanda, tayari Mkoa wa Pwani una viwanda 164 vikiwamo vinavyojengwa na vilivyokamilika, huku 84 vikiwa ni vikubwa. Alisema uwekezaji wa viwanda hivyo umegawanyika katika sehemu mbili, chini ya Sh bilioni tano na ule ulio juu zaidi. “Sehemu kubwa ni viwanda vya kuchakata malighafi, kuna vya matunda, marumaru, nondo, korosho, mabati, saruji na malighafi ya nyumba na vinavyofanya kazi nikivitaja ni zaidi ya 40,” alisema. Ridhiwani alisema jimbo lake na mkoa wote wa Pwani, unafanya jitihada kuhakikisha bidhaa zilizokuwa zikipatikana China ziweze kupatikana Chalinze ili kuepuka gharama za usafirishaji. Alisema uwekezaji wa kiwanda cha Twyford Tanzania Ceramics kilichotembelewa wiki hii na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, uligharimu Dola za Marekani milioni 158. Ridhiwani alisema kiwanda hicho kinachotarajia kukamilika katika kipindi cha Julai hadi Agosti, kitakuwa na uwezo wa kutoa kontena 28 hadi 30 kwa siku. Alisema kupitia kiwanda hicho, wananchi watapata faida kwa kufanya biashara na kuongezeka kwa ajira. “Kitakuwa na ajira zaidi ya 2,000 zilizo rasmi, huku zisizo rasmi zikiwa ni zaidi ya 4,000. Hata hivyo, bado nasisitiza ajira izingatie wazawa kwa sababu wananchi tayari wanalalamikia upendeleo katika kupeana ajira, walioajiriwa pale wengi si wakazi wa Chalinze, hata Waziri Mwijage nilimwambia,” alisema. Pamoja na jitihada hizo, alisema utekelezaji wa sera ya Tanzania ya viwanda unaweza ukakwamishwa kutokana na uwezo wa kutafsiri neno na nia nzuri ya Rais Dk. John Magufuli. “Rais hawezi kujenga viwanda peke yake, wasaidizi tutoe tafsiri sahihi ya nia yake nzuri, tutekeleze. Sitokubali kumdhalilisha rais, akisimama mwaka 2020 akiulizwa kuwa viwanda viko wapi aseme viko Pwani, atoe mfano Chalinze,” alisema.
1kitaifa
MANILA, PHILIPPINES RAIS wa Philippine, Rodrigo Duterte, ametishia kuwarusha viongozi mafisadi kutoka katika ndege angani, akisema ameshawahi kufanya hivyo kitambo. Duterte aliyasema hayo Jumanne wiki hii wakati akiwahutubia waathirika wa kimbunga katikati ya Philippines. “Kama wewe ni fisadi, nitakubeba kwa kutumia helikopta hadi Manila na kukurusha nje,” alisema Duterte, ambaye ameanzisha vita dhidi ya ufisadi na mihadarati. Alitishia kutoa adhabu hiyo kwa yeyote atakayeiba fedha za msaada alizoahidi kuzitoa. “Nimefanya hivi kitambo, kwanini nisiweze kufanya tena?” alisema huku akishangiliwa na watu hao. Haya ni madai mapya ya rais huyo ambaye amekiri kutekeleza mauaji ya kiholela. Hata hivyo, msemaji wake amepinga madai hayo. Mapema mwezi huu, msemaji mwingine, Martin Andanar, alisema kauli za mwajiri wake zipokewe kwa makini, lakini zisipewe uzito baada ya kusema kuwa aliwaua watu watatu alipokuwa Meya wa Davao nchini humo. Wakati kauli hiyo mpya akiitoa Jumanne wiki hii, jana Rais Duterte alionekana kujiweka kando na kauli zake za awali. “Helikopta, nimtupe mtu? Na iwapo ni kweli, sitakiri,” alisema wakati wa mahojiano na shirika la habari la ABS-CBN. Rais huyo ana historia ya kuyakana maneno yake. Watu 6,000 wanasemekana kuuawa na polisi, wanamgambo na wauaji wa kukodi nchini hapa tangu Duterte azindue vita dhidi ya mihadarati baada ya kuchaguliwa kuwa rais Mei, mwaka huu. Wanasiasa wa upinzani na makundi ya haki za binadamu wamekuwa wakitaka aondolewe madarakani, lakini amebakia maarufu miongoni mwa wapigakura wanaotaka aisafishe nchi hiyo.
3kimataifa
MASHIRIKISHO ya sanaa nchini yanatarajia kutoa tuzo ya heshima kwa viongozi mbalimbali akiwemo hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kutokana na mchango wake mkubwa katika tasnia hiyo.Pia yamepanga kumpa tuzo Rais John Magufuli na Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Shein kutokana na michango yao ya kufuata nyayo za Mwalimu Nyerere katika uongozi wao.Tuzo hizo zinatarajiwa kukabidhiwa keshokutwa katika tamasha lililoandaliwa na mashirikisho hayo manne ya sanaa za maonesho, ufundi, muziki na filamu. Katika tamasha hilo, litakaloanza kwa kongamano la wasanii, Rais Magufuli atafungua pamoja na kukutana na wasanii.Hayo yalisemwa jana nyumbani kwa Mwalimu Nyerere, Mikocheni Dar es Salaam baada ya viongozi wa shirikisho hizo kwenda kushukuru familia ya Mwalimu kutokana na mchango aliouonesha wakati wa uhai wake.Akizungumza jana, Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifamba alisema lengo la tamasha hilo lililoandaliwa na wasanii ni kutambua mchango wa mwalimu lakini pia kutangaza aliyoyafanya ili wale walio na umri wa miaka 20 kwa sasa ambao hawakumfahamu wamfahamu.“Hatutaki historia ife, wapo wasiomjua mwalimu na ni wale ambao wenye miaka 20 kwa sasa, hivyo tutatumia sikuhiyo kumzunguzia mwalimu kama kiongozi mashuhuri kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla,” alisema Mwakifamba.Alisema katika tamasha hilo litaambatana na shughuli mbalimbali zikiwemo burudani, mashairi, nyimbo na hata video ili kizazi cha sasa kiendelee kumtambua mwalimu kwa kazi mbalimbali alizofanya.Akiwapokea wasanii nyumbani kwa Mwalimu Mikocheni, mtoto wa Mwalimu, Makongoro Nyerere alitumia muda mwingi kueleza ratiba ya mwalimu wakati wa uhai wake kuanzia asubuhi hadi jioni na kuwashukuru kwa kukumbuka mchango uliotolewa na Mwalimu.Alisema Mwalimu Nyerere pamoja na waasisi wenzake waliwatumia wasanii katika harakati mbalimbali, na kuwapongeza kwa kutambua suala hilo. Makongoro aliyekuwa akiwafurahisha wasanii kwa muda mrefu kutokana na maelezo yake, alisema kwa sasa amerudi CCM na ni mjumbe wa Halmashauri Kuu.
2michezo
UKITAZAMA kwa jicho la tatu, mwenendo wa mbio za marathon za kuwania ubingwa kwenye Ligi Kuu ya England (EPL) kati ya Manchester City na Liverpool, ilikuwa patashika ya nguo kuchanika, kwani City ilifanikiwa kubeba ubingwa huo kwa tofauti ya pointi moja dhidi ya mpinzani wake Liverpool.Mfano huo unaweza kuuleta Tanzania na ‘ku-paste’ kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL), kwani vigogo wa ligi hiyo, Simba na Yanga walikuwa wanafukuzana kama farasi jangwani kuwania taji hilo.Mpaka ligi inakaribia ukingoni bado kulikuwa na kitendawili juu ya nani ataibuka bingwa kutokana na hesabu zilivyokuwa zikiibeba Simba, lakini uhalisia wa soka ulikuwa umeegemea upande wa Yanga.MABINGWA SIMBA Lakini mwisho wa siku mashabiki wa soka waliishuhudia Simba ikifanikiwa kutetea taji hilo kwa shida na kulinyakua kwa mara ya pili mfululizo baada ya kufikisha pointi 91, ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote huku ikiwa na michezo miwili mkononi. Hiyo ni baada ya kumuacha mpinzani wake Yanga ambaye ana hazina ya pointi 86, ambaye wakati huo alikuwa amebakiwa na mchezo mmoja tu kabla ya kuhitimisha ligi hiyo iliyofikia kileleni Mei 28.Simba tunaweza kusema kilichombeba ni kuwa na viporo vingi, ambavyo pia alijitahidi kuvila vizuri kwa kuondoka na pointi tatu kila alipocheza ukiondoa sare chache na kufungwa mara chache tofauti na Yanga.Pamoja na Simba kufanikiwa kutetea taji lake, lakini vita kubwa ilikuwa kwa timu za kushuka daraja, ambazo zilipambana kufa au kupona huku zingine kama Kagera Sugar ikicheza play-off. Mwandishi wa gazeti hili anachambua mwenendo mzima wa ligi hiyo na ushindano ulivyokuwa hadi Simba kufanikiwa kutwaa taji hilo kwa mara ya pili mfululizo.AZAM ILIPEWA NAFASIKabla ya ligi hiyo kuanza timu zilizokuwa zinapewa nafasi kubwa ya kuweza kuleta ushindani mkubwa mbele ya Simba kulingana na maandalizi iliyoyafanya ni Azam pekee. Kila mmoja anafahamu fika Azam ilikuwa miongoni mwa timu zilizowekeza vya kutosha kwa kufanya usajili mzuri wa wachezaji ambao ulitegemewa kuleta ushindani mkubwa mbele ya Simba iliyojizatiti vya kutosha chini ya bilionea Mohamed Dewji ‘Mo’. Licha ya Yanga kubebwa na jina lake kulingana na historia yake ya kutwaa taji hilo mara nyingi kuliko timu yoyote kwenye ligi hiyo, lakini hakuna aliyekuwa akitarajia kuona Yanga ikileta ushindani kutokana na timu hiyo kutokuwa na mfadhili wala fedha za usajili.UPINZANI WA YANGALicha ya mabingwa hao wa kihistoria kupitia kwenye kipindi kigumu ikiwemo kukosa viongozi na kushindwa kulipa stahiki za wachezaji kwa wakati, lakini walifanikiwa kuleta upinzani dhidi ya Simba na kuongoza ligi hiyo kwa muda mrefu zaidi kuliko timu nyingine 19 zilizoshiriki ligi hiyo.Ni wazi shukurani kubwa zinapaswa kupelekwa kwa benchi la ufundi linaloongozwa na Kocha Mkuu wa kikosi hicho, Mwinyi Zahera aliyesimama bila kujali kipindi hicho cha mpito na kuwajenga kisaikolojia kuweza kupambana bila kuchoka na kufanikiwa kuleta ushindani kwa Simba, ambao walikuwa wamefanya maandalizi makubwa kwa kupanga bajeti kubwa na kusajili wachezaji wa maana.Haikuwa rahisi kuona wachezaji wa timu kama Yanga wakidai mishahara ya mpaka miezi mitatu, lakini walionesha kucheza kwa moyo na kujitolea. Hata walipofikia kukata tamaa kabisa bado Zahera alionekana kuyeyusha huzuni na kuibua furaha katikati ya mioyo yao.Mwisho ikaonekana inawezekana, Yanga ikawa tishio bila ‘meno’ na ukisogea vibaya unapigwa nyingi. Yanga haikuwa na wachezaji wengi wa hadhi yao, lakini kwa pamoja ilionesha wao ni nani na muhimu kwao ilikuwa mabao, mengine yanafuata. Kimasihara ikauweka ubingwa wa Simba rehani na kubadili mawazo ya wengi kuwa mwisho wa msimu watarajie lolote, tofauti na ilivyotarajiwa, kwamba Simba itatetea ubingwa kirahisi baada ya Azam nayo kuyumba ilipofika katikati baada ya kucheza muda mrefu bila ya kupoteza mchezo.Muvi imeisha na Yanga imemaliza kwenye nafasi ya pili ikiacha historia kwa ilichokifanya kwa Simba waliokuwa wanapewa nafasi kubwa ya kufanikiwa kutetea ubingwa huo, kutokana na usajili wa wachezaji walioufanya na kuweka bajeti ya maana iliyokuwa inasababisha wachezaji wa kikosi hicho kucheza kwa kujiamini muda wote uwanjani. Simba walipewa kila kitu.Mshahara kwa wakati, ‘bonus’ za kutosha na waliishi katika mazingira ya juu ya kama timu kweli inayohitaji kufanya mapinduzi Afrika lakini spidi ya Yanga ilibaki kidogo iyeyushe matumaini yao ya ubingwa na kushika chati za juu kwenye msimamo. Ilifika wakati ilikuwa inaonekana ngumu kwao kuikimbiza Yanga, huku wakiwa na mtihani wa michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika.Wapinzani wao Yanga walijikuta wakitawala usukani wa ligi hiyo hadi wanafikia utofauti wa pointi 21. Hakika Yanga inastahili pongezi kwa ushindani walioonesha licha ya kuonekana ni timu dhaifu mbele ya Simba msimu huu.AZAM HAIKUWA MBALIUkiachilia mbali Simba, Azam ni timu ya pili iliyokuwa inapewa nafasi ya kuleta ushindani kutokana na usajili walioufanya kujiandaa katika ligi hiyo. Lakini walijikuta kikosi hicho kilishindwa kufikia malengo ya timu na kujikuta wakipoteza michezo kadhaa na kulazimisha sare zilizosababisha kukata tamaa ya ubingwa na kupelekea uongozi wa timu hiyo kuvunja benchi la ufundi lililokuwa likiongozwa na Mholanzi Hans Van Der Pluijm na kikosi hicho kukabidhiwa kwa makocha wa mpito, Abdul Mingange na msaidizi wake Iddi Cheche.Pamoja na mabadiliko hayo, walishindwa kuleta ushindani na kujikuta wakizorota kwenye zoezi la kutwaa ubingwa huo na kuishia kupigania nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo ili kulinda heshima yao ambapo wamekalia nafasi ya tatu. Tumezoea kuona Mtibwa Sugar ni miongoni mwa timu zinazofanya vyema ukiachilia Yanga, Simba na Azam ambapo nayo inafuatia lakini wameshindwa kuonesha umwamba wao na kujikuta wakipoteza michezo mingi tofauti na hadhi yao.KMC ni timu ngeni kwenye ligi hiyo lakini imeleta ushindani mkubwa hadi imefanikiwa kushika nafasi ya nne na kujitoa kwenye hadhi ya ‘underdog’ na kuzizidi timu nyingine tano zilizopanda pamoja msimu huu. Timu hiyo sasa itashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho la Afrika baada ya Tanzania kupewa nafasi nne, mbili Ligi ya Mabingwa wa Afrika na idadi kama hiyo, Kombe la Shirikisho.Biashara United na JKT Tanzania zilipanda pamoja na KMC mwishoni mwa msimu uliopita, lakini zenyewe zilikuwa zinapambana na hali yao kwa muda mrefu zikigombea kutoshuka daraja. Wengine waliopanda ligi hiyo na KMC ni Coastal Union na Alliance ambao michezo yao ya mwisho ndio iliyozihakikishia timu hizo kutoshuka daraja na sasa wana uhakika wa kuendelea kuwepo katika ligi hiyo msimu ujao.Ya mwisho iliyopanda sambamba na KMC au Kino Boys ni African Lyon ambayo yenyewe ilikuwa ya kwanza kabisa kushuka daraja na sasa inajiandaa na michezo ya Ligi Daraja la Kwanza na maisha yao mengine mapya waliyoyaacha kwa takriban miezi nane tu iliyopita na sasa wanarejea tena huko walikotoka.
2michezo
KINSHASA, DRC Shirika la afya la kimataifa WHO, limetangaza kuwa hatari ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola kuzidi kusambaa na kiwango chake kiko juu zaidi miongoni mwa wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. WHO limeeleza kuwa vyanzo vya maambuziko ya ugonjwa wa Ebola vimeongezeka na sasa njia za usafiri na shughuli za umma ni hatari kwa wananchi kuambukizana huku tathimini ya kusambaa kimataifa imebaki hatari ndogo. Taarifa ya WHO imesema kuwa kitaifa na majimboni nchini humo hatari ya kuambukizana iko juu na kushauri majimbo jirani na mataifa kuimarisha tahadhari dhidi ya maradhi hayo. Aidha WHO wamesisitiza kuendelea kushirikiana na mataifa jirani na washirika kuhakikisha mamlaka za afya zinachukua tahadhari na zinakuwa tayari kuchukua hatua.Jumanne iliyopita Naibu mkurugenzi wa WHO Peter Salama alionya taifa jirani la Uganda kuchukua tahadhari kufuatia tishio la maambukizi mpakani jirani na ziwa Albert.Kwa mujibu wa takwimu wa shirika la WHO mlipuko wa Ebola umesababisha vifo vya watu 101 tangu ulipolipuka mnamo mwezi Agosti mwaka huu. Huu unakuwa mlipuko wa mara ya kumi kutokea nchini DRC tangu mwaka 1976, ambapo hali ya hatari iko juu sana katika jimbo la kaskazini mashariki ambako kunavikundi kadha avinavyomiliki silaha jirani na mpaka wa Uganda Rwanda na Sudani kusini.
3kimataifa
WATU wawili wanaodaiwa kuwa majambazi wamefariki dunia kwa kupigwa risasi na wenzao, baada ya kutaka kuwatoroka askari wakati wa operesheni ya kuwasaka majambazi mkoani Shinyanga.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Saimon Haule alithibitisha hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari. Alieleza kuwa mauaji hayo yalitokea juzi saa 3:00 usiku katika vichaka vya Mtaa wa Buhangija Kata ya Ibinzamata Manispaa ya Shinyanga. Kamanda aliwataja waliouawa ni Geoffrey Ntabazi (29) na Ramadhani Masoud (33), ambao walikuwa wahusika kwenye matukio ya unyang'anyi na uvunjaji ya Januari 28 na 30, mwaka huu.Kamanda Haule alisema watu hao wanaodaiwa kuwa ni majambazi, walikufa kwa kupigwa risasi na majambazi wenzao, baada ya kutaka kuwatoroka wakati wa operesheni ya kuwasaka majambazi waliotajwa na marehemu hao kuhusika kwenye matukio ya unyang'anyi na uvunjaji.Alisema majambazi hao walitaja silaha ambayo huitumia pamoja na wenzao, waliokuwa wamejificha kwenye vichaka eneo la Buhangija. Baada ya kufika hapo, ghafla majambazi hao waliokuwa wamejificha, walianza kuwashambulia askari na kumpata jambazi mmoja na mwingine aliyekuwa ameongozana na askari.
1kitaifa
Na MWANDIHI WETU, DAR ES SALAAM WAKAZI wa Kata za Kivule na Msongola wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam waliovunjiwa nyumba zao wamemwomba Rais Dk. John Magufuli kuwatembelea kwenye makazi yao ili wamweleze unyama waliofanyiwa na kikundi kinachojiita Umoja wa Kikristo Tanzania (UVIKIUTA). Wakazi hao zaidi ya 2000 ni miongoni mwa wamiliki wa nyumba 500 zinazodaiwa kuvunjwa kimakosa kwa amri ya Baraza la Ardhi la Wilaya ya Temeke. Wakizungumza na MTANZANIA mwishoni mwa wiki, baadhi ya wakazi hao walisema mtu pekee ambaye wanaona anaweza kuwasaidia ni Rais Dk. Magufuli kwani wanao uhakika kwamba waliowafanyia unyama huo wana mkono wa mtu mzito aliyeko serikalini. “Kama rais wetu (Dk John Magufuli ) anatusikia tunamwomba aje hapa katika ziara zake za kushtukiza ili tumweleze ukweli wa jambo hili, kuna wateule wake wachache wameamua kututesa na kutufanyia hila, hawa wana mkono wao humu. Hii si mara ya kwanza, kila wakijisikia wanakuja kutubomolea nyumba bila haki yoyote” alisema mmoja wa wananchi hao Aneth Athuman. Naye Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema) aliiomba Serikali kukifanyia uchunguzi kikundi cha Uvikiuta kwani huenda kimetumika kubeba ajenda za watu wengine. Mwita ambaye alikwenda kutoa misaada ya kibinadamu kwa wananchi waliobomolewa nyumba zao alisema kuna baadhi ya wateule wa rais wapo nyuma ya kikundi hicho ambacho kimejificha kwenye mgongo wa dini kuhodhi eneo kubwa la ardhi kinyume cha taratibu. “Ukitaka kujua kwamba huu unyama una mkono wa baadhi ya wateule wa Rais, angalia namna viongozi hao walivyokaa kimya hadi sasa bila kuchukua hatua, leo hii hatumwoni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akija hapa kusikiliza kero za wananchi kama alivyofanya maeneo mengine. “Kama RC Makonda alifanya ziara maeneo mbalimbali ya Dar es salaam na baadhi ya mikutano yake ikaripotiwa ‘live’ na vyombo vya habari kwa nini asije hapa akawasikiliza wananchi ambao wamebomolewa nyumba zao bila hatia, kama hakuna ajenda ndani yake ni nini?,” alihoji Waitara. Wiki iliyopita Polisi wilayani Temeke kwa kushirikiana na dalali wa mahakama walibomoa nyumba 500 za wakazi wa Kivule na Msongola kwa madai kuwa Uvikiuta wameshinda kesi ya ardhi namba 73 ya mwaka 2014 ambapo iliamriwa nyumba hizo zibomolewe. Hata hivyo wananchi wanadai kuwa hati iliyotolewa na mahakama hiyo inahusu nyumba tano tu na si vinginevyo. Washtakiwa katika kesi hiyo walitajwa kuwa ni Elia Mharage, Astria Charles, Daud Zebedayo na Chacha Marwa.
1kitaifa
MADRID, HISPANIA KOCHA wa klabu ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid, Zinedine Zidane, ameweka wazi kuwa nyota wake, Cristiano Ronaldo na nahodha Sergio Ramos, wamemaliza tofauti zao. Uongozi wa klabu hiyo uliwakutanisha wachezaji hao juzi, kabla ya kuelekea katika mchezo wao dhidi ya Atletico Madrid kwenye Ligi Kuu nchini Hispania. Sababu za wawili hao kuwa kwenye mgogoro ni baada ya Real Madrid kukubali kichapo cha mabao 3-1 dhidi ya Tottenham kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Novemba 1, kwenye Uwanja wa Wembley, hivyo Ronaldo akatupia lawama kwa uongozi wa klabu hiyo kwa kudai kwamba, walifanya makosa makubwa kuwauza wachezaji wao, James Rodriguez na Alvaro Morata. Kauli hiyo ya Ronaldo ilionekana kumchukiza sana Ramos na ndipo nahodha huyo alisema kuwa, Ronaldo ni mchezaji mbinafsi sana na hakupaswa kuongea kauli kama hiyo na alitakiwa kushirikiana na wenzake ili kuisaidia timu. Hata hivyo, baada ya mgogoro huo kuwa mkubwa, Ronaldo aliweka wazi kuwa, hana mpango tena wa kuendelea kuwa na timu hiyo mara baada ya kumaliza mkataba wake. “Ni wazi kwamba Sergio Ramos ni miongoni mwa wachezaji wenye akili sana ndani na nje ya uwanja, anaweza kumwambia kitu mchezaji yeyote hata kama ni Cristiano Ronaldo, isitoshe wachezaji hao wamekuwa pamoja kwa muda mrefu na wamezoeana. “Mchezaji huyo alistahili kumwambia hivyo Ronaldo kutokana na kauli yake, lakini ukweli ni kwamba kila kitu kipo sawa kwa sasa, uongozi wa klabu uliamua kukaa pamoja na wachezaji hao kwa ajili ya kumaliza tofauti zao na kila kitu kinakwenda sawa sasa. “Kwa pamoja naweza kusema nina wachezaji wawili kwenye kikosi ambao wanatengeneza historia ndani ya timu hii, wamekubali kumaliza tofauti zao ili kuweza kuipigania timu yao katika michezo inayofuata,” alisema Zidane. Wababe hao wa soka barani Ulaya, msimu huu wanaonekana kuwa wameuanza vibaya kutokana na kiwango chao na ushindi wanaoupata, huku baadhi ya mshabiki wakidai kuwa, mshambuliaji wao huyo ambaye ana tuzo nne za Ballon d’Or, amekuwa kwenye kiwango cha chini.
2michezo
WAZAZI wa wanafunzi wanaosoma Shule ya Sekondari ya Dodoma kwa kushirikiana na Bodi ya shule wamekubaliana kuchangishana Sh milioni 264.3 kujenga uzio kuzunguka shule.Uamuzi huo wa kujenga uzio, ulifikiwa katika kikao hicho, baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tamisemi, Selemani Jafo kuagiza bodi hiyo wakati wa mahafali ya kidato cha nje mwaka jana kujenga ukuta kuzunguka shule.Akizungumza na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Sekondari ya Dodoma, Philbert Bagenda alisema, serikali imetoa agizo la elimu bure na kuwataka walimu au bodi kutochangisha wazazi katika michango, lakini haijazuia kuchangia elimu kwa hiari. “Serikali imekataza kutoza michango, lakini bado haijazuia wazazi au wadau wa elimu wenye nia njema kuchangia elimu kwa hiari yao kwa manufaa ya jamii kwa ujumla,” alisema.Mwenyekiti huo alisema pamoja na serikali kutoa Sh bilioni 1.44 kukarabati majengo ya shule na mabweni ya wananfunzi, inakabiliwa na tatizo la uzio, jambo ambalo linasababisha wanafunzi kukosa utulivu wawapo shuleni hapo. Alisema pamoja na kupata kiasi hicho kwa ajili ya ukarabati ya shule hiyo na ujenzi mabweni, shule ni kongwe lakini haina uzio miaka mingi.Bagenda alisema walianza kuweka mipango kwa kutafuta na kuweka mipaka ya shule kwa usahihi, kufuatilia michoro ya uzio na kutafuta thamani halisi ya ujenzi wa uzio na hayo yote yalifuata utaratibu kupitia Halmashauri ya Jiji. “Mipango hiyo imekamilika na kupata kibali cha kuanza ujenzi na wataalamu wa Jiji ndiyo waliotupatia thamani halisi ya Sh milioni 264.3 hadi ujenzi wa uzio unakamilika,” alisema.Bagenda alisema kutokana na kumaliza taratibu hizo, bodi iliona ni jambo jema kuwashirikisha wadau wa maendeleo ya elimu kabla ya yote ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wazazi ili kuchanga kwa hiari bila kushurutishwa. Mzazi Nasoni Manyere alisema licha ya serikali kukataza michango, si jambo baya wazazi kukubaliana kufanya shughuli za kimaendeleo.
1kitaifa
Simba na Singano wamekuwa kwenye mgogoro kwa takriban wiki ya pili sasa, ambapo mchezaji huyo anadai kutaka kuondoka kwa vile amemaliza mkataba wake wa miaka miwili huku uongozi wa klabu yake ukisema bado mchezaji wake halali kwani alisaini mkataba wa miaka mitatu unaotarajiwa kumalizika mwakani.Taarifa ya TFF kwa vyombo vya habari jana ilisema imepokea kwa masikitiko taarifa za mgogoro wa kimkataba kati ya Singano na Simba.“TFF imeagiza mwakilishi wa klabu ya Simba pamoja na mchezaji wa Simba wafike ofisi za TFF siku ya Jumanne tarehe 09/06/2015 kwa mazungumzo,” ilisomeka taarifa hiyo.Aidha taarifa hiyo ilisema kila upande unatakiwa kufika na vielelezo vyake.“Katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye mazungumzo, TFF inaziasa pande zote mbili zijiepushe na kutoa matamko yanayoweza kuchochea hali ya kutoelewana na kuamsha hisia mbaya katika familia ya mpira wa Miguu Tanzania,” ilisomeka taraifa hiyo.Mwanzoni mwa wiki hii Simba ilitishia kumshitaki mchezaji huyo, kwa madai ameidhalilisha klabu kwa kitendo chake cha kudai hajasaini mkataba wa miaka mitatu na kumtaka apeleke mkataba wake wa miaka miwili anaodai alisaini.Katika moja ya malalamiko yake, Singano ambaye anahusishwa na kutaka kujiunga na Azam anasema uwepo wake Simba haujamnufaisha kwani licha ya kufanya vizuri lakini hana pakuishi mpaka sasa.
2michezo
TIMU ya Taifa ya Tanzania Bara U20 imefuzu nusu fainali ya mashindano ya CECAFA yanayochezwa nchini Uganda baada ya kuwafunga wenyeji Uganda, Hippos, kwa mabao 4-2 katika mchezo uwa robo fainali kwenye Uwanja wa Pece, Gulu. Tanzania Bara U20 inayonolewa na kocha Zuberi Katwila ilianza kuzifumania nyavu za wapinzani wao dakika ya 25 bao likifungwa na Andrew Simchimba likadumu hadi mapumziko. Dakika ya 46 Uganda walisawazisha bao lililofungwa na Abdul Kayondo na dakika ya 60, Andrew Simchimba aliifungia bao la pili Tanzania Bara, lakini Uganda walifanikiwa kusawazisha dakika ya 60. Baada ya mabao kuwa 2-2 kila timu ilijitahidi kumsoma mpinzani wake na kujaribu kutumia makosa yake, lakini Tanzania Bara kupitia kwa Kelvin John ilifanikiwa kuzifumania nyavu za Uganda katika dakika ya 88 na 90 na kuzima ndoto za ufalme wa Uganda kwa timu za Tanzania. Tanzania Bara ambayo ilitinga robo fainali baada ya kumaliza ikiwa na pointi saba kinara wa Kundi B baada ya kushinda michezo miwili na kutoka sare mchezo mmoja, sasa itacheza nusu fainali ya mashindano hayo.Katika mchezo mwingine wawakilishi wa Zanzibar, walifungwa na Eritrea kwa mabao 5-0, na Kenya ikamfunga Burundi kwa mabao 2-1.
2michezo
NEW YORK, MAREKANI  STAA wa muziki wa pop, Justin Bieber, amewashtua mashabiki wake baada ya kuomba pambano la ngumi dhidi ya staa wa filamu, Tom Cruise. Wawili hao wamekuwa wakijifunza ngumi mchanganyiko maarufu kwa jina la UFC, hivyo Bieber anaamini yupo tayari kwa ajili ya kushuka ulingoni ili kushindana na mpinzani wake huyo. Bieber amekuwa rafiki wa karibu na bingwa wa ngumi duniani Floyd Mayweather, hata katika mazoezi yake, Mayweather amekuwa akimfundisha baadhi ya mbinu za kupambana na mpinzani wake. “Nipo tayari kwa ajili ya kupambana na Tom Cruise. Tom kama hautokuwa tayari kukubali pambano hilo basi utakuwa unaniogopa, lakini nipo tayari kupambana na mtu yeyote atakaye kuwa tayari,” aliandika Bieber kwenye Instagram. Bieber ana umri wa miaka 25, wakati huo mpinzani wake Tom ana umri wa miaka 56, lakini anaamini anaweza kumgalagaza.
2michezo
['Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa, watoto wanne kati ya watano wenye umri wa miaka 11-17 duniani hawafanyi mazoezi ya viungo ya kutosha.', 'Shirika la afya duniani (WHO) limesema kuwa afya za watoto zinaharibiwa kutokana na ukosefu wa mazoezi hivyo kuathiri ukuaji wa ubongo na shughuli zao za ujuzi kupungua uwezo.', 'Utafiti huo umesema kwamba chanzo ni kutokufanya mazoezi, inashauriwa kuwa ni vyema mtoto kufanya mazoezi walau kwa saa moja kwa siku.', 'Tatizo hili limekuwa kubwa duniani kote katika mataifa maskini na tajiri.', 'Watoto wa kiume wanaoneka kujishughulisha zaidi katika kufanya mazoezi kuliko watoto wa kike katika nchi 4 kati ya 146 zilizofanyiwa utafiti.', 'Mazoezi gani wanapaswa kuyafanya?', 'Mazoezi yoyote yanayofanya mapigo ya moyo yaende kwa haraka na mapafu kupumua kwa nguvu, kama vile;', '-Kukimbia', '-Kuendesha baiskeli', '-Kuogelea', '-Kucheza mpira ', '-Kuruka kwa mguu mmoja', '-Kuruka Kamba', '-Sarakasi', 'Daktari kutoka shirika la afya dunia, Dkt Fiona Bull amesema kuwa hadhani kwamba ni lengo kubwa sana la kujiwekea lakini ni vyema kuzingatia afya.', "''Ni vizuri kujijengea afya nzuri na maendeleo ya mwili.''", 'Tofauti kati ya mazoezi ya wastani na yale ya kutumia nguvu ni kwamba mazoezi ya wastani unakuwa unaweza kuzungumza lakini ya mazoezi ya nguvu hayakuruhusu kuzungumza, kwa sababu unakuwa hauna pumzi ya kutosha.', 'Kwanini ni muhimu kujali?', 'Sababu kubwa ni afya ya sasa hivi na ya baadae. ', 'Kwa muda huu mfupi, kuwa mchamgamfu kunamaanisha:', '-Moyo na mapafu yanakuwa na afya', '-Mifupa na misuli imara', '-Afya ya akili ya mwili inakuwa nzuri', '-Uzito mdogo', "''Vijana wachangamfu wana uwezekano wa kuwa watu wazima wachangamfu,'' Anaeleza Daktari kutoka shirika la afya duniani.", 'Na vilevile muda unavyozidi kwenda basi unapunguza hatari ya kupata magonjwa kama mshtuko wa moyo, kiharusi, na aina ya pili ya ugonjwa wa kisukari.', 'Ukosefu wa mazoezi unamuweka mtu mmoja kati ya watu wazima wanne hatarini.', 'Lakini uchunguzi unasema kuwa kuna ushahidi wa kutosha unaoonesha kujishughulisha ni kitu kizuri kwa ukuaji wa ubongo.', "''Wanakuwa na uwezo wa kutambua, kujifunza kwa urahisi, na tabia nzuri ya kujichanganya na wengi.'' Amesema Dkt Guthold.", 'Je kwa kawaida watoto ni wavivu tu?', 'Je, utafiti huu unatuambia nini kuhusu misingi ya watoto?', "Dkt Bull amesema kuwa ''Watoto sio wavivu''", "''Hii inatueleza kuhusu kitu kikubwa zaidi lakini sio kuhusu watoto peke yake. "]
2michezo
Serikali imeokoa zaidi ya Bilioni 1/-  kupitia upandikizaji wa vifaa vya kusaidia kusikia watoto tangu ianze kuendesha zoezi hilo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.Katika taarifa yake na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumapili, Mkuu wa Idara ya magonjwa ya pua, koo na masikio na mdomo, Hospitali hiyo, Edwin Liyombo amesema kua uwezo wa upasuaji wa upandikizaji vifaa vya kusaidia kusikia umeongezeka kwa wataalamu wazalendo wandaniDk Liyombo amesema kuwa mpaka sasa serikali imetumia kiasi cha Sh. 777 milioni kwa watoto 21 kwa gharama ya Sh37 milioni kwa mtoto mmoja. Imeelezwa kuewa endapo wangepelekwa nje ya nchi kutibiwa ingegharimu Sh 2.1 bilioni ambayo ni sawa na Sh 100 milioni kwa kila mtoto.Aidha Dk Liyombo ameogeza kuWa Tanzania inakua nchi ya kwanza kwa nchi za Afrika mashariki kufanya upasuaji huo kwa hospitali za umma.
1kitaifa
Agizo hilo lilitolewa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga alipofungua mkutano wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (ALAT), uliofanyika mjini hapa.Ngaga alisema viongozi wa Halmashauri, wasipokuwa wabunifu katika kuongeza mapato, hawatakwenda mbele na kuhudumia jamii, ikiwemo ujenzi wa miundombinu, kama vile barabara na miradi ya kilimo.“Tukijiongezea wigo wa mapato katika maeneo tunayowaongoza wananchi wetu, tutaweza kusonga mbele, ni vyema tuzingatie hilo”, alisema Ngaga.Alisema Halmashauri ikitegemea chanzo kimoja cha mapato kufikia malengo iliyojiwekea, itakuwa ni vigumu na kusababisha kushindwa kutoa huduma husika kwa wananchi.Pamoja na mambo mengine, Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza uboreshaji wa kiwango cha elimu katika shule za msingi na sekondari mkoani humo ili kuufanya mkoa huo, ufikie malengo mazuri ya ufaulu, ambayo imejiwekea katika sekta hiyo.
0uchumi
NA ZAINAB IDDY UONGOZI wa Simba umetangaza kamati maalumu ambayo imepewa jukumu la kutafuta mwekezaji atakayenunua asilimia 50 ya hisa ili kukamilisha azma ya klabu hiyo kujiendesha kisasa. Hatua hiyo inatokana na klabu hiyo kubadili mfumo wake wa uendeshaji kutoka ule wa wanachama uliodumu kwa miaka mingi hadi kuwa wa hisa. Kamati hiyo inaundwa na watu watano ambao ni Wakili Damas Ndumbaro, Mbunge wa Ilala, Musa Hassani ‘Zungu’. Pia yumo Abdallah Lazak Badru, Yusuph Majib na  Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji  Thomas Mihayo. Mfanyabiashara maarufu na mwanachama wa klabu hiyo, Mohamed Dewji, anapewa nafasi kubwa ya kupewa fursa hiyo, baada ya kuweka wazi kuwa yuko tayari kununua hisa zenye thamani ya Sh bilioni 20. Wanachama wengi wa Simba wanamuunga mkono bilionea huyo kukabidhiwa timu yao kutokana na mchango wake uliowezesha kusajiliwa kwa  wachezaji kadhaa wapya wenye ubora msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara, akiwemo aliyekuwa kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima. Akizungumza wakati akitangaza kamati hiyo Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Simba, Dk. Arnold Kashembe, alisema kamati hiyo itafanya kazi yake katika kipindi cha siku 45 kabla ya kuwasilisha jina la mshindi katika kamati ya utendaji. “Tumeunda kamati hiyo ambayo itakuwa huru kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria za nchi na baada ya kuona wote hao ni wazuri katika masuala ya kisheria pamoja na kifedha kwa maana ya uuzaji na ununuzi wa hisa. “Kamati hiyo inatarajia kukutana kwa mara ya kwanza kati ya Jumatano na Alhamis, baada ya hapo wataweka mikakati yao juu ya vipi wataanza majukumu yao ya kumpata mwekezaji mkubwa, lengo likiwa ni kuifanya timu yetu iendeshwe kisasa zaidi,” alisema. “Baada ya kamati hiyo kumpata mwekezaji kwa asilimia 50, itapeleka jina lake kwenye kamati ya utendaji kabla ya kuitishwa mkutano wa wanachama ambao ndio utakaoidhinisha iwapo kama apewe hisa hizo au la. “Kama wanachama watapitisha jina la mwekezaji huyo aliyepatikana, hapo ndipo mfumo rasmi wa uendeshaji wa klabu utakapoanza, kati ya asilimia 50 zitakazobaki zitatolewa asilimia 10 na kupewa wanachama wote hai, huku zile asilimia 40 zitauzwa kwa wanachama kulingana na uwezo wa mhusika, lakini yule mwekezaji mkubwa kwenye hisa hataruhusiwa kuja kuchukua katika zile 40% za wanachama,” alisema Kashembe.
2michezo
HATIMA ya watumishi waliogundulika kuwa na vyeti feki itajulikana Aprili mwaka huu, iwapo watalipwa au laa. Hayo yamebainika baada ya kikao cha pamoja baina ya Serikali na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) kilichofanyika wiki iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari Dare es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TUCTA, Dk. Yahya Msigwa, alisema katika kikao hicho walielezwa kwamba suala hilo linashughulikiwa na mamlaka mbalimbali na majibu yatajulikana kabla ya Machi au Aprili mwaka huu. “Walisema walilofanya (wenye vyeti feki) ni kosa la jinai na la nidhamu, ni sawa lakini bado tunaendelea kuipigia magoti serikali, tunaomba ufanyike ………………………………….
1kitaifa
Kiungo wa zamani wa Yanga Salvatory Edward ameingilia kati suala la kipa timu yake hiyo ya zamani Claus Kindoki.Kindoki aliyeletwa Yanga na kocha wa timu hiyo Mwinyi Zahera amekuwa akishutumiwa na mashabiki wa timu hiyo kutokana na kiwango kibovu anachoonyesha tangu alipojiunga na timu hiyo akitoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC).Kipa huyo alisajiliwa kama chaguo la kwanza baada ya klabu hiyo kuachana na Youthe Rostand ambae aliachwa kwa kwa kuwa aliruhusu mabao mengi ya kizembe.Kindoki amejikuta akifungwa mabao rahisi kwenye ligi na mechi za kirafiki na hadi sasa ameruhusu mabao 10.Hata hivyo Salvatory Edward aliyewahi kutamba na Yanga na Taifa Stars katikati ya miaka ya 1990 mpaka katikati ya miaka ya 2000, ameibuka na kuisihi klabu yake hiyo kuwa nyuma ya kipa huyo kwani tayari wameshamsajili.“Kindoki sio kipa mbaya ingawa sio wa kiwango cha kuitwa wa kulipwa; lakini tayari Yanga imeshamsajili , hivyo wanachotakiwa ni kumuunga mkono tu kwa sasa, kumlaumu watamuondolea kabisa hali ya kujiamini na wao sasa hivi wamebakiwa na makipa wawili tu, kwani Beno Kokalonya wanasema amegoma.“Binafsi sipendi na lawama wanazompa hata kama ni kipa wa kawaida lakini ndio tayari wako nae, wanapaswa kumuunga mkono tu na sio vinginevyo,”alisema Edward aliyetamba kwa jina la Dokta wakati akimudu vyema nafasi ya kiungo.
2michezo
NA GLORY MLAY  BAADA ya kutamba na wimbo wa ‘Baba Swalehe’ mkali wa Bongo Fleva, Nickson Simon ‘Nikki wa Pili’, anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa ‘Sweet Mangi’.   Katika wimbo huo aliomshirikisha Chidy Benzi, anayepatiwa matibabu baada ya kutumia dawa za kulevya, Nikki kutoka kundi la Weusi amezungumzia kabila la Wachaga kwamba ni wazuri na wanajua kupenda. “Wengi wanasema wasichana wa Kichaga hawajui kupenda wanawaza fedha, lakini ukisikiliza wimbo wangu utajua namna wanavyopenda kuliko wanavyofikiriwa na wengi,” alisema Nikki.  
4burudani
WATU watatu wamekufa na wawili wamejeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, baada ya kufukiwa na kifusi kwenye machimbo ya moramu.Machimbo hayo yanayotumika kwa ajili ya shughuli za ujenzi, yapo eneo la Moivaro katika Kata ya Moshono jijini hapa.Tukio hilo limetokea umbali wa kilometa nane kutoka katikati ya Jiji la Arusha, baada ya mabonge makubwa ya moramu kuporomoka, wakati watu hao wakiwa kwenye shughuli ya uchimbaji.Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana alisema tukio hilo ni la Aprili 23, mwaka huu saa 2:00 asubuhi.Kamanda Shana alisema tangu kutokea ajali hiyo vikosi vya uokoaji kutoka mamlaka za ulinzi na usalama, vilikusanyika eneo la tukio na kuendelea kufukua udongo, kuwatafuta watu waliofukiwa. “Lakini pia vifaa mbalimbali vya uokoaji viliwasili mara moja ili kufanikisha ufukuaji kifusi linaenda kwa haraka na vizuri,” alisema Kamanda Shana.Alisema watu watatu waliofariki, walikuwa wamefunikwa na ngema iliyobomoka kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo na wawili walijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini. Alishukuru Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ), mgambo, viongozi mbali mbali na jeshi lake kwa kufanya kazi hiyo kuwa rahisi. Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Gabriel Daqarro alisema hiyo ni mara ya pili kwa machimbo hayo kuporomoka na kusababisha maafa.Kwamba mwaka 2013 hali kama hiyo ilijitokeza na kuua watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa. “Lakini katika tukio hili watu watatu waliofariki baada ya kufukiwa na gema lililobomoka kutokana na mvua zilizonyesha usiku wa jana na wawili walijeruhiwa na gema tu na tumewakimbiza hospitalini,” alisema. Shuhuda wa ajali hiyo, Ruben Jacob ambaye ni mchimbaji wa moramu Moivaro, alisema aliona gari linapakia moramu chini ya machimbo hayo, ila ghafla alisikia kishindo kikubwa cha kuanguka kwa gema na kufunika watu.“Viongozi mbali mbali walipofika niliona miili mitatu imetolewa chini ya kifusi na watu wawili walikimbizwa hospitalini kwa matibabu,” alisema Jacob. Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Calist Lazaro alisema taarifa ya kufukiwa kwa watu hao, aliipata asubuhi na alijaribu kusambaza taarifa kwa viongozi wenzake, ambao walitoa mashine za kuchimba kifusi ili kuokoa watu hao. “Wizara ya Madini kama imetoa leseni ya uchimbaji sisi jiji tutachukua ushuru, ila sina hakika sababu machimbo haya yalifungiwa, lakini nitafuatilia baada ya shughuli hizi kuisha,” alisema.
1kitaifa
Na ZAINAB IDDY-DAR ES SALAAM TIMU ya taifa ya vijana walio chini ya miaka 17, Serengeti Boys, leo inarusha karata yake muhimu dhidi ya Niger katika mchezo wa Kombe la Afrika kwa vijana nchini Gabon. Mchezo huo utafanyika katika Uwanja wa Port Gentil mjini Port Gentil, ambapo kikosi hicho kikiwa kimevuna poibnti nne katika michezo yake miwili ya awali, ikianza kupata suluhu dhidi ya Mali Mei 15, mwaka huu kabla ya kuifunga Angola mabao 2-1. Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Bakari Shime amesema kuwa mchezo huo ni muhimu kupata matokeo ili kujiweka katika nafasi ya kucheza hatua inayofuata. “Tumejiandaa vema kuwania nafasi ya angalau kuingia nusu fainali,” alisema Shime. Naye Nahodha wa timu hiyo, Dickson Job aliwatoa shaka Watanzania akisema vijana wote wako vema kwa ajili ya mchezo huo kwani mpira wa miguu kwao ni ajira kwa manufaa ya yao binafsi, familia na taifa ambalo limewatua Gabon kutafuta Kombe la Mataifa ya Afrika. Serengeti Boys inahitaji sare ya aina yoyote ili iweze kuvuka huku Niger ambayo ina pointi moja ikiburuza mkia katika Kundi B.
2michezo
Katika mechi hiyo Simba ililazimika kusawazisha dakika 10 kabla ya kumalizika mchezo kupitia kwa Brian Majwega baada ya Mwadui kuongoza kwa karibu muda wote wa mchezo kwa bao lililofungwa na Nizar Khalfan.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya mtandao jana, Kerr alisema anajua mashabiki wa timu hiyo wanatamani kushinda hivyo wanajipanga kupata ushindi katika mechi zijazo.“Najua Simba wanahitaji ushindi, lakini matokeo ya sare ni moja ya matokeo kwenye mchezo, wachezaji wangu jana (juzi) walicheza kwa jitihada wawezavyo lakini mchezo wa soka ndivyo ulivyo,” alisema.Alisema anaendelea kurekebisha makosa yaliyojitokeza katika mechi zilizopita ili Januari Mosi wapate ushindi kwenye uwanja wa Ngwanda Sijaona dhidi ya Ndanda ya Mtwara. Baada ya mechi hiyo Simba itacheza na Mtibwa Sugar Januari 16 baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar.Simba ina pointi 24 ikiwa nyuma ya Yanga kwa pointi tisa, Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 33 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 32 na Mtibwa Sugar ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi 27.
2michezo
Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema haki ya uhuru wa kujieleza na kukusanyika iko shakani, kutokana na kuwapo kwa udhaifu katika sheria mbalimbali. Hapa nchini uhuru wa kujieleza unalindwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 18 na mikataba ya kimataifa na kikanda ambayo taifa limeridhia. Akizungumza jana wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kulinda Uhuru wa Kujieleza na Kukusanyika, Mkurugenzi wa Utetezi na Maboresho wa LHRC, Ana Henga, alisema uhuru wa kujieleza ni muhimu kwani unaweza kulitoa taifa kutoka hapa lilipo na kuliwezesha kusonga mbele. Kampeni hiyo imeandaliwa na kituo hicho kupitia mradi wa uhakiki kwa kushirikiana na wadau washirika ambao ni Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Baraza la Habari (MCT), Policy Forum, Twaweza, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WiLDAF) na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. “Watu wengi wanaogopa kujieleza, vyombo vya habari vinafungiwa kwa ujumla hali si nzuri, uhuru wa kujieleza na kukusanyika uko katika hatihati. “Baada ya Serikali kukataza mikutano ya kisiasa mpaka mwaka 2020 utaratibu wa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kabla ya kukusanyika umegeuzwa na kuwa si taarifa tena bali ni kuomba idhini au kibali jambo ambalo linapingana na katiba ya nchi,” alisema Henga. Alisema wameamua kuendesha kampeni hiyo baada ya kubaini changamoto kadhaa zinazofifisha uhuru wa kukusanyika nchini ambazo ni uzuiaji holela wa mikusanyiko. Nyingine ni mkanganyiko wa sheria, matumizi holela ya nguvu katika kutawanya mikusanyiko, kukosekana kwa utaratibu maalumu katika matumizi ya maeneo ya wazi na kukataliwa kukusanyika. Naye Mwakilishi kutoka MCT, Paul Malimbo, alizitaja sheria kinzani kuwa ni Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015, Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ya mwaka 2016 na Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ya mwaka 2015 na kupendekeza zifanyiwe marekebisho kuendana na Katiba na mikataba ya kimataifa na kikanda ambayo taifa limeridhia. Kwa mujibu wa Malimbo, sheria ya takwimu inazuia mjadala juu ya usahihi wa takwimu, inazuia watu na taasisi kuchapisha taarifa zao wenyewe na kuyumbisha uhuru wa kujieleza kwa kuwaisha watu adhabu ya kifungo na kulipa faini. Naye Mwenyekiti wa TEF, Theophil Makunga, alisema uhuru wa kujieleza na kukusanyika ni muhimu hasa kwa waandishi wa habari kwani huwarahishia kupata habari. “Tunashiriki kwenye kampeni hii ili kuwafanya watu wajieleze tupate habari na kuandika, vyombo vya habari tunatakiwa tupate habari kwa serikali na watu wote sasa wasipozungumza tutakosa cha kuandika na matokeo yake tutashindwa kufanya kazi. “Mfumo wa vyama vingi tumeukubali wenyewe kama jamii hivyo, haiwezekani baada ya miaka 25 tafiti zionyeshe serikali inabinya upinzani, si sifa nzuri kwa nchi ni lazima tuuruhusu uzungumze,” alisema Makunga. Kampeni hiyo iliyobeba kaulimbiu ya ‘Bila uhuru wa kujieleza na kukusanyika hatuwezi kuendelea’ni ya nchi nzima na inatarajiwa kuhitimishwa Novemba mwaka huu.
1kitaifa
 MWANDISHI WETU WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amepokea hundi ya Sh bilioni 1.1 kutoka Kampuni ya Uchimbaji Madini Geita (GGML) ili kukabiliana na mapambano dhidi ya maambukizi ya corona. Akipokea hundi hiyo, Ummy alitoa wito kwa viwanda vya ndani kuchangamkia fursa za uzalishaji wa vifaa tiba na kinga dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 kutokana na fedha zinazochangwa na kampuni mbalimbali nchini.  Ummy alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akipokea hundi hiyo kutoka GGML ambayo mbali na kutoa fedha hizo pia imeandaa mikakati kadhaa kudhibiti corona nchini. Alisema Serikali inaendelea kuthamini msaada mkubwa unaotolewa na wadau hao katika kuonyesha jitihada za kuwalinda watumishi wa afya walio mstari wa mbele kudhibiti maambukizi. “Niwaombe wadau wanaotoa misaada kutoka nje ya nchi kuzingatia mwongozo wa upokeaji wa dawa na vifaa tiba kwa kuhakiki ubora. Tutaendelea kuelekeza TMDA, kuhakikisha wanaongeza umakini uhakiki na usalama, kumekuwa na wimbi la uingizaji wa vifaa tiba, lazima kuhakikisha ni salama na vina vigezo vinavyohitajika. “Pia natoa wito kwa viwanda vya ndani kwamba tunahitaji sana barakoa, PPE, sanitizer, hela hii ielekezwe kununua vifaa vinavyozalishwa ndani ya nchi, mfano barakoa za ndani ya nchi, kuna kiwanda Pugu, uwezo bado mdogo,” alisema Ummy. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi hundi hiyo, Makamu Rais, Maendeleo Endelevu GGML, Simon Shayo alisema kampuni yao pia imezindua mikakati kadhaa ya kupambana na janga hili ambalo lilibisha hodi hapa nchini Machi 16, mwaka huu na kuathiri zaidi ya watu 400 hadi kufikia sasa. Alisema mikakati hiyo inalenga kushirikiana na Serikali pamoja na wataalamu wa afya kuelimisha jamii kuhusu virusi vya corona ikiwa ni pamoja na kugawa vifaa kwa jamii inayozunguka mgodi na wafanyakazi wa GGML kujikinga dhidi ya ugonjwa huo. “Kwanza tumekabidhi hundi hii ya Sh bilioni 1.1, ni sehemu ya Sh bilioni 1.6 fedha ambazo GGML imetoa katika kutekeleza mikakati mbalimbali ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona nchini. “Fedha hizi Sh bilioni 1.1 zitaelekezwa kwenye ngazi ya kitaifa kupitia mfuko maalumu wa mapambano dhidi ya Covid–19 ambao unasimamiwa na ofisi ya Waziri Mkuu. “Hata hivyo, fedha nyingine kiasi cha Sh milioni 500 zinatumika kwa ajili ya kusaidia juhudi zinazofanywa katika ngazi ya mkoa na jamii, zitakazojumuisha ununuzi wa vifaa-tiba muhimu na vitendea kazi kama vile vifaa vya kujikinga, barakoa, mashine za kusaidia upumuaji,” alisema Shayo. Pia alisema GGML ilikabidhi matanki 10 yenye ujazo wa lita 1,000 kila moja yaliyowekwa kwenye sehemu za wazi za mji wa Geita ili kuwawezesha wananchi kunawa mikono.  “GGML pia imetoa kimiminika cha klorini ambacho kinatumika kutakasa mikono badala ya sabuni. “Mradi huo pia unawezeshwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Mjini Geita (Geuwasa) ambayo itatoa maji kila mara ili kuhakikisha kuwa huduma hiyo inapatikana kwa umma wakati wote.  “Matanki hayo ambayo ni sehemu ya usambazaji wa msaada huo yamewekwa katika maeneo yafuatayo: Kituo cha mabasi (2), Kituo cha Mwatulole (1), Kituo cha Shilabela (1), Kituo cha Nyankumbuko (1), Soko la Nyankumbuko (1), Hospitali ya Geita (1), Soko la Dhahabu (2) na kituo cha Moyo Watoto Yatima cha Huruma (1),” alisema Shayo. Aidha, aliongeza kuwa katika kujenga uelewa kuhusu janga hili kwa jamii zinazozunguka mgodi, GGML imekuwa ikigawa vipeperushi vyenye taarifa za virusi vya corona ndani na nje ya mgodi.
5afya
KIBALI cha kukariri kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, kimeleta kizaazaa na kusababisha wanafunzi 11 wa kidato cha nne kutolewa chumba cha mitihani na kuingizwa katika karandinga na kupelekwa kituo cha polisi.Tukio hilo lilitokea Ijumaa saa 2.15 asubuhi katika shule hiyo ambayo wanafunzi walichukuliwa kupelekwa kituoni, na saa 5 asubuhi walitolewa kupelekwa kwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa (RCO) na waliachiliwa saa 2 usiku walipoitwa wazazi wao na kuambiwa hatima yao wataipata kupitia shuleni.Mkurugenzi Mwendeshaji wa shule hiyo, Richard Magessa alithibitisha kizaazaa hicho na kudai kilichofanyika kwa wanafunzi wao kilikuwa sio sahihi kwani hao ni halali na taarifa zao zipo ofisini na wana sifa za kufanya mitihani. Aliwataja wanafunzi walizuiliwa kufanya mitihani kuwa ni Simon Kaugila, Said Mabuyu, Jasmin Ally, John Benjamin, Abdulmaliki Said, Ramadhani Majuto, Yona Yuda, Regina Kasanga, Said Nuru, Juma Hassan na Ramadhani Nasibu.Alibainisha kuwa vibali hivyo hutolewa na Kitengo cha Elimu Mkoa na Usajili kwa kawaida unaanza Januari kila mwaka na baada ya kusajili Baraza la Mitihani la Taifa hufika mikoani kwa ajili ya kupata taarifa za watoto.Mkurugenzi huyo alisema Necta walifika Aprili katika Ofisi ya Elimu Mkoa na walikabidhiwa nyaraka mbalimbali zinazowahusu watoto na kama kuna makosa huwa wanatakiwa kuorodheshewa taarifa kama sio sahihi.Alisema changamoto hizo ni namba halisi za matokeo kidato cha pili, orodha ya masomo yanayotakiwa kufanya kwa kila mtahiniwa na vibali vya kukariri kwa watahiniwa waliokariri kidato cha tatu, lakini wanafunzi hao waliondolewa pasipo na maelekezo yoyote.Kwa upande wao, wazazi na wananchi waliokuwepo katika maeneo hayo, walidai wamesikitishwa kwa Ofisa Elimu Sekondari Manispaa ya Tabora, Chatta Luleka, kuchukua maamuzi hayo ya kufika shuleni hapo akiongozana na gari la polisi na kuwatoa wanafunzi kwenye chumba cha mtihani na kuwalazimisha kuingia kwenye gari hilo.Walidai ofisa huyo alitakiwa kutoa maelekezo mapema ili uongozi wa shule waufanyie kazi na sio kukurupuka kuwatoa wanafunzi kwenye vyumba vya madarasa kama watuhumiwa, hivyo kuwatia wasiwasi.Wazazi hao ambao hawakutaka kutaja majina yao kwenye vyombo vya habari, walidai wamedhalilishwa watoto wao kwa sababu shule hiyo kwa sasa inafanya vizuri na walipata tuzo na kikombe cha ushindi na walimu watatu walipewa pongezi katika mwaka 2015, 2016 hadi 2017.
1kitaifa
EVANS MAGEGE N LEONARD MANG’OHA-DAR ES SALAAM KANISA Katoliki nchini limewaelekeza waumini wake kufunga, kufanya hija, mikesha na maombi maalumu kwa lengo la kuombea mvua. Pamoja na hilo, kanisa hilo limewaelekeza viongozi wake kuadhimisha misa kwa lengo hilo hilo. Maelekezo hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa kanisa hilo (TEC), Askofu Tarcsius Ngalalekumtwa, kupitia barua yenye kumbukumbu namba ya TEC/PR/ 1/2017 iliyoandikwa Januari 13, mwaka huu kwenda kwa maaskofu wote wa kanisa hilo. “Ni kipindi cha mvua za kilimo katika maeneo yetu mengi lakini hali ya hewa siyo ile tuliyoizoea. Mvua hazifiki kuruhusu shughuli zetu za kilimo kuendelea na baadhi ya maeneo tayari yana uhaba mkubwa wa chakula. “Ninaomba kasi ya sala iwepo pote nchini. Mungu aliyewatunza wana wa Israeli walipokuwa safarini kuelekea nchi ya ahadi kwa kipindi cha miaka 40, atuangalie kwa wema, huruma na upole. Tuombe baraka juu ya kazi zetu za kilimo, tukayapate mazao ya nchi tuweze kumtumikia Mungu kwa mioyo yenye utulivu na shukrani,” inasomeka barua hiyo. Katika barua hiyo yenye kichwa cha habari ‘Ukame nchini’ ambayo pia ina saini ya Askofu Ngalalekumtwa inawaelekeza viongozi wake kuadhimisha misa za kuomba mvua, kuwepo kwa hija, mfungo, mikesha na maombi maalum kwa lengo hilo huku ikisisitiza kuwa; aombaye hupewa. Katika hatua nyingine baadhi ya waumini wa Kanisa Katoliki kupitia Jumuiya zao jana asubuhi walieleza kujulishwa juu ya jambo hilo. Mmoja wa waumini aliyezungumza na gazeti hili alisema wamejulishwa kufanya ibada za kuombea mvua lakini pia nchi na viongozi wake. Gazeti hili lilimtafuta Askofu Ngalalekumtwa kwa njia ya simu ili kuthibitisha kama tamko hilo ameliandika yeye ambapo alisema: “Mimi nimewaandikia maaskofu basi ndio kazi yangu”. Askofu Ngalalekumtwa ambaye yupo mkoani Iringa alipoulizwa kama kuna msukumo wowote wa kuandika barua hiyo kwa sasa alijibu kwa kumhoji mwandishi wa habari hizi akisema: “Ulichokisoma ni kweli au si kweli? Kuna mvua au hakuna?” Wakati Kanisa Katoliki likija na uamuzi huo, Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini (TMA), imesema maeneo mengi yamepata mvua za vuli chini ya wastani na kwa kuchelewa hivyo kuathiri mfumo wa kawaida wa mvua hasa katika maeneo ambayo yamekuwa yakipata mvua mara mbili kwa mwaka. Kutokana na hilo, Mtaalamu wa kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, amewataka wakulima kuacha kulima mahindi na badala yake wajielekeze kwenye mazao yanayostahimili ukame. Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, Meneja Ofisi Kuu ya Utabiri, Samwel Mbuya, alisema kuchelewa kwa mvua hizo ambazo zilitarajiwa kuanza kati ya Septemba na Oktoba mwaka jana katika baadhi ya mikoa nchini, zilisababisha mikoa hiyo kukabiliwa na vipindi virefu vya kiangazi tofauti na ilivyozoeleka. Aliitaja baadhi ya mikoa iliyokumbwa na ukosefu mkubwa wa mvua uliokwamisha kufanyika kwa shughuli za kilimo ni pamoja na Dar es Salaam, Morogoro na mikoa yote ya Kanda ya Ziwa. Alisema pia mvua zilizokuwa zikitarajiwa katika baadhi ya maeneo ambayo hupata mvua za vuli kuanzia Novemba zimenyesha kwa kiwango cha chini na kwa kuchelewa. “Lakini kuanzia Januari hii na Februari tunatarajia mvua za msimu zitaanza hasa katika maeneo ambayo hupata mvua mara moja kwa mwaka lakini zitakuwa za wastani, ambapo kwa mikoa ya Dodoma na Singida kutakuwa na mvua za chini ya wastani hali inayotegemewa pia katika mikoa ya Ruvuma na Mtwara,” alisema Mbuya. Mbuya alisema maeneo mengi ambayo muda wa mvua za vuli umepita wasitegemee kupata mvua za uhakika na kuwataka wananchi kuendelea kufuatilia taarifa na maangalizo yanayotolewa na TMA ili kufahamu hali ya mwelekeo wa mvua katika siku zijazo. Aliitaja baadhi ya mikoa inayotarajiwa kupata mvua hizo zinazotarajiwa kunyesha kati ya mwezi huu na ujao kuwa ni pamoja na Tabora, Kigoma, Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa. Katika taarifa aliyoitoa kwa gazeti hili ilionyesha kuwa mvua za kati ya Oktoba na Desemba mwaka jana zilinyesha chini ya wastani katika maeneo mengi ya Nyanda za Juu Kaskazini Mashariki ikijumuisha mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara. “Mvua za chini ya wastani zimenyesha pia katika maeneo ya ukanda wa Pwani ya Kaskazini mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, visiwa vya Pemba na Unguja,” ilieleza taarifa hiyo. Alipotafutwa Mtaalamu wa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Lilian Mpinga, kuelezea hali hiyo ya mvua na mwelekeo wake katika masuala ya kilimo, aliwataka wananchi kujielekeza kulima mazao yanayostahimili ukame. “Mazao yanayopaswa kulimwa ni yale yanayostahimili ukame ambayo ni mihogo, viazi vitamu, uwele, mbaazi lakini mazao kama mahindi hayafai kulimwa wakati huu kutokana na kuhitaji kiasi kikubwa cha mvua,” alisema Mpinga. Awali, Meneja huyo wa TMA akizungumzia hali ya upepo uliokuwa ukivuma baharini kiasi cha kusababisha ajali ya jahazi lililokuwa likitoka Tanga kuelekea Pemba na kukatisha maisha ya zaidi ya watu 12 mwanzoni mwa wiki hii, alisema kwa sasa hali imerejea kawaida. “Ni kweli kulikuwa na upepo mkali uliosababisha kuwapo kwa mawimbi makubwa na baada ya kuona hali hiyo tulitoa angalizo siku mbili kabla ya siku ya tukio lile ambapo kulikuwa na viashiria vilivyoonyesha kuwapo upepo mkali kati ya Januari 10 na 12. “Lakini hali imerejea kawaida kama kutakuwa na mabadiliko na kukawa na kuimarika kwa mfumo wa upepo ambao mwanzo ulionekana kuimarika na upepo kuvuma kutoka Kaskazini mwa Bahari ya Hindi tutatoa taarifa,” alisema.
1kitaifa
ENDAPO ningembiwa kitu gani nikibadilishe kwenye tasnia ya muziki nchini basi ningebadilisha upepo wa Bongo Fleva uende sawa na muziki wa Dansi, muziki mama uliozaa aina zote za miziki unazozisikililiza. Miaka ya 80 wakati haijulikana kama kuna muziki utazaliwa unaoitwa Bongo Fleva, muziki wa Dansi ulikamata sehemu kubwa ya jamii, vijana wa zamani mpaka wazee wa wakati huo waliuhusudu muziki huu. Hakukuwa na lugha chafu zinazoweza kuvuruga maadili ya jamii yetu, hakukua na video zinazoonyesha sehemu kubwa ya miili ya wanawake ikiwa wazi ndiyo maana jumbe zilizosokotwa kwenye nyimbo zile zilifika mubashara kwa watu wote. Sasa leo hii Bongo Fleva imetawala, muziki wa Dansi umeminywa na vyombo vya habari vimeutenga muziki huu, nauliza hivi ikitokea Dansi ikafa kabisa mamilioni ya mashabiki wake mtawapeleka wapi? Ni kweli Dansi ya zamani na ya sasa imekuwa tofauti, wanamuziki wa zamani waliimba kulingana na mazingira ya wakati ule hata hawa wanamuziki wa sasa wanapiga muziki kulingana na mazingira ya sasa lakini hawapati nafasi ya kusikika sababu Bongo Fleva imepewa kipaombele. Nafurahi kuona Sikinde Ngoma ya Ukae wanajaribu kukimbizana na wakati. Akina Mjusi Shemboza wanakung’uta gitaa kwa uhodari ili kukishawishi kizazi hiki cha dotcom kielewe muziki ni nini. Maisha ya msanii wa Bongo Fleva na mwanamuziki wa Dansi yana utofauti mkubwa. Bongo Feva imewekwa kibiashara hivyo ni lazima vijana hawa watengeneze fedha ila upande wa muziki wa Dansi ni tofauti. Dansi ni muziki wenye mashabiki wengi ila tatizo bado wadau hawajauweka katika levo za kibiashara ndiyo maana wanamuziki wake hawanufaiki kama wale wana Bongo Fleva. Hivi sasa wasanii wa Bongo Fleva wanauza kazi zao kimtandao na kupata diliza matangazo kwenye kampuni mbalimbali lakini wanamuziki wa Dansi hutegemea maonyesho pekee. Kuna ulazima madereva wanao iendesha Bongo Fleva wakaushika pia usukani wa muziki wa Dansi ili mambo yawe sawa kwa wanamuziki wote
4burudani
HISTORIA ya aina yake imeandikwa katika sherehe za miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miaka 57 ya Jamhuri, zilizofanyika kwa mara ya kwanza katika Kanda ya Ziwa, na mkoani Mwanza.Kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jana, uwanja huo na maeneo ya jirani vikiwamo Viwanja vya Furahisha, kuliandikwa historia kutokana na kufana kwa sherehe hizo, zilizohanikizwa na burudani mbalimbali za kwaya, muziki wa kizazi kipya, wa jadi (Sungusungu), gwaride, halaiki na maonesho ya ndege vita.Historia hiyo inatokana na ukweli kwamba katika sherehe za jana, mambo ya msingi ya kitaifa yalipewa kipaumbele cha pekee na Rais John Magufuli na viongozi wengine wa kitaifa.Mbali ya Rais Magufuli, sherehe hizo zilihudhuriwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hasssan, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, maspika Job Ndugai (Bunge la Tanzania), Zubeir Ali Maulid (Baraza la Wawakilishi Zanzibar).Pia walikuwapo majaji wakuu, Profesa Hamis Juma (Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) na Othman Makungu (Zanzibar) pamoja na marais wastaafu Benjamin Mkapa na Ali Hassan Mwinyi, mawaziri wakuu wastaafu Mizengo Pinda, John Malecela, Edward Lowassa na Frederick Sumaye.Lakini pia walikuwapo viongozi wa vyama vya upinzani akiwamo Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuhudhuria sherehe za kitaifa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani 2015.Mbowe alifuatana na viongozi wake mbalimbali wakiwamo wabunge John Mnyika (Kibamba), John Heche (Tarime Vijijini), Godbless Lema (Arusha Mjini) na aliyekuwa Mbunge wa Ilemela, Ezekiel Wenje na aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu. Viongozi wengine wa upinzani walikuwa ni John Cheyo (UDP), Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), John Shibuda (ADA-TADEA), Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima (AFFP), Said Soud Said na Hamad Rashid Mohammed (ADC).Mambo yaliyofanya sherehe hizo kuwa za kihistoria ni pamoja na uamuzi wa Rais Magufuli, kuwasamehe wafungwa 5,533, idadi ambayo ni kubwa na haijawahi kutokea katika historia ya nchi hii.Wafungwa hao waliosamehewa ni wale walioko magerezani kwa kufungwa kuanzia siku moja hadi mwaka mmoja, waliofungwa miaka mingi kuanzia miaka mitano hadi 30 waliobakiza mwaka mmoja kumaliza vifungo vyao. Rais Magufuli alisema ametoa msamaha huo kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 45(1)(a-b) na Sheria ya Magereza Kifungu cha 49 Sura ya 58.Uamuzi huo wa kihistoria wa Rais kusamehe idadi kubwa ya wafungwa, pia unatokana ziara yake ya hivi karibuni kwenye Gereza Kuu la Butimba mkoani Mwanza ambako alishuhudia msongamano mkubwa wa wafungwa na mahabusu, lakini pia hali hiyo iko katika magereza yote nchini. Alisema kwa mujibu wa takwimu alizo nazo, kuna jumla ya wafungwa 17,547 na mahabusu 18,256 nchini, hivyo kufanya jumla yao wote kuwa 35,803.“Pia Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) na Waziri wa Katiba na Sheria wamefanya kazi kubwa na kuwasamehe mahabusu 345 na waliokuwa wanakabiliwa kesi mbalimbali na 256 wa kesi za uhujumu uchumi, kwa hiyo watu 601 wameachiwa huru,” alieleza Rais Magufuli.Aliwataka wanufaika wa msamaha huo, kujutia makosa yao na wasirudie makosa au kusiwepo na mtu mwingine yeyote, kufanya makosa akidhani atapa msamaha.Idadi ya waliosamehewa kila mkoa Aliitaja mikoa na idadi ya wafungwa na mahabusu waliosamehewa kwenye mabano kuwa ni Kagera (713), Dodoma (385), Morogoro (365), Mara (260), Mbeya (259), Kigoma (252), Tanga (245), Geita (230), Rukwa (214), Arusha (208) na Manyara 207.Mikoa mingine ni Tabora (207), Mwanza (190), Ruvuma (181), Singida (139), Simiyu (136), Lindi (299), Pwani (128), Iringa (110), Songwe (96), Katavi (74), Shinyanga (74) na Njombe 70.Alisema wanufaika wa msamaha huo, wataanza kutoka magerezani leo. Rais alimkabidhi Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike orodha ya wafungwa wote watakaonufaika na msamaha huo.Alimkabidhi orodha hiyo papo hapo mbele ya umati. Viongozi watoa kauli Jambo jingine la kihistoria kwenye sherehe hizo jana ni uamuzi wa Rais Magufuli kuwapa nafasi ya kuzungumza viongozi mbalimbali, wakiwamo wastaafu na viongozi wastaafu.Sherehe za Uhuru zilizoeleka kuwa ni za gwaride tu na shughuli nyingine chache bila ya kuwapo kwa hotuba, lakini katika miaka ya karibu, kiongozi wa nchi amekuwa akitumia kutoa hotuba, lakini jana akaenda mbali zaidi na kuwapa nafasi wastaafu, wapinzani na viongozi wengine kusalimia wananchi. Miongoni mwa walioongumza ni marais wastaafu Mkapa na Mwinyi, lakini pia Rais wa Zanzibar, Dk Shein, mawaziri wakuu wastaafu Pinda, Lowassa, Malecela na Sumaye, pamoja na viongozi kadhaa wa upinzani.Viongozi hao kwa sehemu kubwa walisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja, mshikamano na kufanya kazi ili taifa liondokane na utegemezi.“Mimi nawahimiza Watanzania wote tuendelee kudumisha umoja, amani na tufanye kazi kwa bidii,” alisema Mkapa aliyewasalimu wananchi kwa salamu yake iliyokuwa maarufu wakati wa utawala wake, akisema “Mambo.”Kwa upande wake, Mzee Mwinyi aliyekuwa maarufu kwa jina la “Ruksa” wakati wa utawala wake kati ya mwaka 1985 hadi 1995, alianza kwa kuonesha umahiri wake katika lugha ya Kiswahili, akionesha utofauti wa matumizi ya maneno ya “Nawapongezeni na “Nawapongeza.”Lakini ujumbe wake, ulikuwa ni kukubali kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Rais Magufuli, akimpongeza. Aliwataka Watanzania kumwombea dua Rais ili jicho la wabaya lisimdhuru, lakini pia alisisitiza umuhimu wa kuendelea kutunza amani, umoja na usalama wa nchi.Naye Lowassa ambaye mwaka 2015 alipambana na Dk Magufuli kuwania urais akiwa na Chadema kabla ya kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivi karibuni, aliwataka Watanzania wamuunge mkono Rais Magufuli kwani mtindo wake wa uongozi, utaletea taifa maendeleo makubwa katika kipindi chake cha miaka 10.Sumaye ambaye kama Lowassa alikimbilia Chadema mwaka 2015, kabla ya kujitoa wiki iliyopita, akidai kufanyiwa ‘figisu’ katika kuwania Uenyekiti wa Kanda ya Pwani na ule wa Taifa wa Chadema, alisema kama taifa bado kuna kazi kubwa ya kufanya ya kupata uhuru wa kiuchumi ili kuondokana na utegemezi.Cheyo wa UDP na Profesa Lipumba wote walipongeza kazi kubwa, inayofanywa na Rais Magufuli, na kuwataka kuendelea kuwaunga mkono. Hamad Rashid ambaye ni Waziri wa Afya katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, alizungumzia suala la kulinda amani na Muungano wa pande mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia viongozi hao wa vyama vya upinzani, wakiongozwa na Mbowe, walitaka sherehe hizo zisaidie kuwepo na maridhiano ya kisiasa na utengamano wa kisiasa na kuimarisha demokrasia.“Miaka 58 ya Uhuru ni uthibitisho kwamba kuna haja ya kuwepo kwa maridhiano, mshikamano na upendo kati yetu, siku ya leo ifungue milango ya kupendana, maridhiano yatakayotusaidia katika kujenga taifa letu,” alisema Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro.Mbowe alisema Rais Magufuli ana nafasi ya pekee ya kujenga maridhiano na utengamano nchini.Sherehe Kanda ya ZiwaKatika kuvunja mazoea, serikali iliamua sherehe hizo kufanyika Kanda ya Ziwa katika Mkoa wa Mwanza. Hiyo ni historia kubwa iliyobebwa na sherehe za miaka 58 ya Uhuru, kwani mara nyingi sherehe hizo hufanyika Dar es Salaam na Dodoma. Rais Magufuli aliwasifu wananchi wa Kanda ya Ziwa, kwa kujitokeza kwa wingi ndani na nje ya Uwanja wa CCM Kirumba katika sherehe hizo. Alisema haijapata kutokea.“Ikumbukwe kuwa hatukufanya sherehe hizi kwa miaka miwili, mwaka 2015 na mwaka 2018 na badala yake fedha zake zilifanya kazi za maendeleo,” alisema Rais Magufuli.“Hivyo hivyo ndio sababu tukaamua tufanye sherehe hizi mkoani Mwanza tofauti na ilivyozoeleka, hii ni kwa sababu ya kubadili mazoea.”Alisema sherehe hizo huambatana na fursa mbalimbali, kuchochea maendeleo ya mkoa huo. Jambo jingine la kihistoria lililopamba sherehe hizo jana ni kundi la wananchi wa kabila la Wasukuma 1,200 walioingia uwanjani, wakiwa wamevalia mavazi ya asili.Wasukuma hao ni walinzi wa jadi maarufu Sungusungu. Wakiwa uwanjani hapo walicheza na kuimba na kuzunguka uwanja, hali iliyonogesha zaidi sherehe hizo.Watanzania wapongezwaKatika hatua nyingine, Rais Magufuli amewapongeza Watanzania kwa maendeleo waliyoyapata katika miaka 58. Alisema mafanikio hayo ni matokeo ya kazi nzuri, inayofanywa na Watanzania wenyewe. Katika hilo, aliwataka Watanzania wote kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili matunda ya kuwa huru kisiasa, yatoe mbegu bora ya kuwa huru kiuchumi.Aliyataja baadhi ya mambo makubwa ya kimaendeleo, yaliyofanyika katika kipindi cha miaka 58 ya Uhuru ni ujenzi wa kilometa 12, 679.55 za barabara za lami kutoka kilometa 360 za lami wakati nchi inapata Uhuru, kilometa zingine zaidi ya 2,400 zinajengwa na zingine 7,087 zipo katika hatua mbalimbali za kuanza kujengwa.Kuhusu sekta ya afya, alisema vituo vya kutolea huduma ya afya, alisema vimeongezeka kutoka 1,095 wakati tunapata Uhuru hadi kufikia 7,293 kwa sasa, lakini pia wataalam katika sekta mbalimbali nao wameongezeka.Nafasi ya Tanzania kimataifa Kwa mujibu wa Rais Magufuli, katika kusherehekea miaka 58 ya uhuru, Tanzania inajivunia kwa mchango ilioutoa kimataifa ikiwemo ukombozi wa Bara la Afrika, kutafuta amani na kujenga mtangamano, kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Pia alisema katika miaka 58 ya Uhuru, Tanzania imekuwa na mahusiano mazuri na mataifa mbalimbali duniani.
1kitaifa
Na NORA DAMIAN – DAR ES SALAAM WAKATI mchakato wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwapata wagombea watakaopeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba ukitarajiwa kuanza kesho, joto linaonekana kuanza kupanda. Katika uchaguzi wa mwaka huu, mchuano mkali unatarajiwa kuwa ndani ya chama haswa kwenye nafasi ya Urais wa Zanzibar, ubunge, uwakilishi na udiwani. Ratiba iliyotangazwa juzi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, imegeuzwa kuwa ajenda katika mitandao ya kijamii huku wengi wakihoji iwapo wataibuka wanachama watakaotaka kupambana na Rais Dk. John Magufuli ambaye anatarajiwa kuomba tena ridhaa ya chama chake kuwania ngwe ya pili. Hata hivyo hali hiyo haitarajiwi sana kwasababu CCM ina utaratibu wa kumpitisha rais anayemaliza muhula wake wa kwanza kugombea tena miaka mitano bila kupingwa. Kwa upande wa Zanzibar kumekuwa na mjadala nani atapewa kijiti cha kumrithi Rais wa sasa, Dk. Ali Mohamed Shein, anayemaliza kipindi chake cha pili hasa baada ya kuwapo wanasiasa mbalimbali wanaotajwa kutaka kuwania nafasi hiyo. Katika dakika za lala salama wanaotajwa kugombea wamekuwa wakipigana vikumbo huku baadhi yao wakitumia upepo wa shughuli mbalimbali kujinadi kiaina na wengine wakionekana kufanya harakati za kimya kimya ili kujitengenezea mtaji wa kura katika vikao vya ndani ya chama. Kiongozi mmoja mwandamizi wa CCM aliliambia MTANZANIA Jumapili kuwa, “huku Bara hakuna shida kazi imeshaisha, gumzo liko Zanzibar subirini.” Rekodi zinaonyesha mbali ya Dk. Shein marais wengine waliowahi kuiongoza Zanzibar ni Sheikh Abeid Amani Karume (1964-1972),  Sheikh Mwinyi Aboud Jumbe (1972-1984), Ali Hassani Mwinyi (1984-1985), Idris Abdul Wakili (1985-1990), Salmin Amour (1990-2000) na Amani Abeid Karume (2000-2010). Rais wa kwanza wa Zanzibar, Abeid Amani Karume,  alipata wadhifa huo baada ya kutokea mapinduzi yaliyosababisha kupinduliwa kwa Sultani wa mwisho wa Sultan Jamshid bin Abdullah Januari 1964. Miezi mitatu baadaye, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilianzishwa na Karume akawa makamu wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huku Mwalimu Julius Nyerere akiwa Rais. Jina la Karume lilirejea tena baada ya Amani Abeid (mtoto wa Karume) kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na kuingia madarakani Novemba 2000 hadi Novemba 2010. WANAOTAJWA ZANZIBAR Miongoni mwa wanaotajwa kuwania urais Zanzibar ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, Balozi Ali Karume, Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni na Waziri wa Viwanda upande wa Zanzibar, Balozi Amina Ali ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 alijitokeza kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea urais wa Jumuhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika orodha hiyo yumo pia aliyekuwa Waziri wa Fedha wa Zanzibar, Dk. Khalid Salum Mohamed, ambaye aliondolewa kwenye wadhifa huo Machi 3 mwaka huu baada ya kile kilichoelezwa kukaidi agizo la chama chake la kutoanza kampeni kabla ya wakati. Mbali na hao, pia wanatajwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Abood, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Issa Haji Ussi Gavu na Makamu wa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan. Hata hivyo Agosti 26, mwaka huu, Samia alisema hana nia ya kuwania urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020. urais Zanzibar. UBUNGE, UDIWANI UWAKILISHI Kulingana na ratiba iliyotolewa juzi wanaotaka kugombea ubunge, uwakilishi, udiwani na viti maalumu watachukua na kurejesha fomu Julai 14 hadi 17 mwaka huu. Wanachofanya makada wengi hivi sasa hasa wale wanaotajwa kutaka kugombea nafasi hizo ni kutafuta ushawishi au ‘kiki’ ya kuwafanya waonekane ili kujitengenezea mtaji wakati wa vikao vya ndani na nje ya CCM.  Wengine wamekuwa wakiitumia kwa kasi mitandao ya kijamii kujipambanua kwa kueleza yale waliyotekeleza wakati wakiomba kura mwaka 2015. Wamo pia baadhi ya wabunge wa kuteuliwa na wale wa Viti Maalumu ambao pia ni mawaziri wameonyesha dalili ya kutaka kugombea majimbo mbalimbali. Mapema wiki hii wakati akihitimisha hotuba ya Makadirio ya Mapato ya Matumizi ya Serikali kwa mwaka 2020/21, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa alisema; “Watanzania msisahau kumpatia rais wetu wabunge na madiwani wanaomudu maadili na mwendo wa Hapa Kazi Tu…na kama itawapendeza wananchi wenzangu wa Buhingwe na chama chetu (CCM) basi iwe pamoja na mimi mtumishi wenu. Jimbo la Buhingwe kwa sasa linaongozwa na Albert Obama. Katika kile kinachoonekana ni kumjibu Dk Mpango,  Obama, wakati akichangia bajeti hiyo alisema wananchi wa Buhingwe wanajua alipowatoa na atakapowapeleka na ana imani atapitishwa tena na CCM kugombea jimbo hilo. “Ukija kwenye orodha ya majina yangu bungeni utaambiwa Obama anaitwa nani, utaambiwa ni mashine ya jimbo, mashine ya kusaga na kukoboa, jina la nne utakaloambiwa kwangu ni simba wa yuda la mwisho ni katapila. “Naomba hayo majina yawe katika ‘hansard’ ya Bunge, Buhingwe wanajua tulikotoka, tuliko na tunakoelekea. Niseme 2020 Magufuli hapa, Obama hapa,” alisema Obama. Wachambuzi wa kisiasa wanasema uamuzi wa baadhi ya wabunge wa kuteuliwa na wale wa viti maalumu kuamua kuingia ‘mzima mzima’ katika kinyang’anyiro hicho unachochewa pia na rekodi zao za kiutendaji. RATIBA ILIVYO Kwa mujibu wa Polepole, kwa upande wa Tanzania Bara tukio la kwanza litakuwa ni uchukuaji fomu kwa nafasi ya kiti cha urais, litakaloanza Juni 15 hadi 30 mwaka huu. Alisema tukio la pili ambalo litakwenda sambamba na muda huo wa siku 15 ni utafutaji wa wadhamini mikoani. Alisema tukio la tatu litakuwa ni vikao vya uchujaji, ambapo Julai 6 hadi 7 mwaka huu, kitaketi kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kitakachoanzisha mchakato wa uchujaji, kisha Julai 8 mwaka huu kitaketi kikao cha Kamati ya Usalama na Madili ya Taifa chama hicho. “Julai 9 mwaka huu, kitaketi Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, ambacho kitatoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM juu ya majina ya wanachama wasiozidi watano, wanaoomba kugombea nafasi hiyo ya urais,”alisema Polepole. Vilevile Polepole alisema Julai 10 mwaka huu, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kitapendekeza kwa Mkutano Mkuu wa CCM, majina yasiyozidi matatu ya wanachama wa chama hicho, wanaoomba kugombea urais. Katibu huyo wa itikadi na uenezi wa CCM, alisema Julai 11 hadi 12 mwaka huu, Mkutano Mkuu wa CCM Taifa utachagua jina moja la mgombea wa urais wa Tanzania. ZANZIBAR Kwa upande wa Zanzibar, Polepole alisema Juni 15 hadi 30 mwaka huu itakuwa ni tukio la uchukuaji fomu na kurejesha. “Juni 15 hadi 30 mwaka huu, kutafuta wadhamini mikoani, baada ya hapo vitafuata vikao vya uchujaji, Julai 1 hadi 2 mwaka huu, itaketi Sekretarieti ya Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar, Julai 3 kitaketi kikao cha Kamati ya Usalama na Maadili Zanzibar,”alisema Polepole. Polepole alisema Kikao cha Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya CCM kitakuwa Julai 4 mwaka huu kwa ajili ya kutoa mapendekezo juu ya wanachama waliojitokeza kuomba kugombea urais wa Zanzibar. “Kikao hicho kitafuatiwa na Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa kitakachoketi Julai 9 kwa ajili ya kupendekeza majina matatu ya wanachama wanaoomba kugombea kiti hicho. Kisha, Julai 10 mwaka huu, Halmshauri Kuu ya Taifa ya CCM kitachagua jina moja la mgombea. Aidha alisema Julai 11 hadi 12, Mkutano Mkuu wa CCM taifa utaketi kwa ajili ya kuthibitisha jina la mwanachama atakayesimama katika uchaguzi wa
1kitaifa
 Na ASHA BANI – Dar es Salaam WACHIMBAJI, wauzaji na wasafirishaji wadogo wa madini, wamemwomba Rais Dk. John Magufuli kuondoa zuio la kusafirisha mchanga wenye madini alilolitoa wiki iliyopita, baada ya kutembelea Bandari ya Dar es Salaam. Pia wachimbaji hao wamesikitishwa na hatua ya watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, kumpotosha Rais kuwa makontena yaliyozuiwa bandarini yana mchanga wa dhahabu, badala ya mchanga wenye madini mengine, ikiwa ni pamoja na shaba, chuma, salfa, mercury na nickel. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kiongozi wa wachimbaji wa madini ya nickel kutoka Dodoma, Thobias Rweyemamu, alisema tangu Machi 2, mwaka huu walizuiwa kusafirisha mchanga na mawe jambo ambalo limewasababishia hasara kubwa. Alisema hata shughuli za uzalishaji katika maeneo ya machimbo zimesimama na kusababisha hasara ya Sh milioni 4 kila siku. “Tunapata hasara kubwa tangu Machi 2, tunapoteza Sh milioni 4 kila siku, wachimbaji waliokuwa wanaendelea na shughuli zao wamesimama, hali imekuwa ngumu, tutashindwa kuendesha maisha, familia zetu zinatutegemea na kundi kubwa la vijana migodini… hali hii ikiendelea tutawafanyaje?” alihoji Rweyemamu. Alisema hadi sasa wachimbaji wadogo zaidi ya 110 wamezuiliwa, huku mchanga wenye nickel zaidi ya makontena 60 na copper makontena saba yakiwa na mchanganyiko wa madini yamezuiliwa. Rweyemamu alisema kutokana na hali hiyo, bado wanaingia hasara ya kulipia ushuru wa Dola za Marekani 20 kila siku ambazo ni  sawa na Dola 12,000 kwa mwezi jambo linalowatia gharama kubwa. Alisema wamekuwa wakifanya biashara hiyo kwa miaka mingi, baada ya kupata vibali halali kutoka Wizara ya Nishati na Madini na wapo kihalali si kama ilivyoelezwa. Mchimbaji mwingine, Paul Kaliyemba, alisema Rais Magufuli alipotoa agizo hilo, hawakupaswa kuchanganywa na maelezo ya wataalamu wa wizara. Kaliyemba alisema wanafanya biashara hiyo kihalali, hata wizara inatambua kwa sababu leseni zilitolewa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) na  walifanya ukaguzi na kujiridhisha. Alisema kutokana na hali hiyo, wamemwandikia barua Rais Magufuli kupitia Wizara ya Nishati na Waziri Mkuu kupitia upya uamuzi wao na wachimbaji wadogo waruhusiwe kuendelea na biashara yao. Kuibuka kwa wachimbaji hao, kumetokana na Rais Magufuli kupiga marufuku usafirishaji wa mchanga wenye madini ya dhahabu kwenda nje ya nchi. Kutokana na agizo hilo, Rais Magufuli aliagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kuzuia makontena 262 yenye mchanga unaodaiwa kuwa na madini usisafirishwe kwenda nje ya nchi. Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Deusdedit Kakoko, alisema baada ya Rais kushuhudia makontena hayo, Alhamisi iliyopita walianzisha operesheni maalumu na kubaini makontena 262 yaliyokuwa na mchanga wa dhahabu tayari kwa kusafirishwa nje. Alisema makontena hayo ni mali ya mgodi wa Buzwagi, unaomilikiwa na Kampuni ya Acacia yaliyokuwa yamehifadhiwa bandari kavu ya Mofed iliyopo Kurasini, Temeke. Hata hivyo, Meneja Uhusiano wa Acacia, Asa Mwaipopo, alisema makontena hayo ni ya mchanga wa madini ya shaba na yalifikishwa bandarini kabla ya zuio la Rais Magufuli. 
1kitaifa
ABDUCADO EMMANUEL NA MITANDAO DIMBA la White Hart Lane linatarajia kuwaka moto kesho saa 9.00 alasiri kwa mchezo wa watani wa jadi wa jiji la London ‘London Derby’, wakati wenyeji Tottenham Hotspur watakapoikaribisha Chelsea katika Ligi Kuu England. Kuelekea mchezo huo, Kocha wa Tottenham, Mauricio Pochettino, ameanza kuuona mgumu kufuatia timu yake kutopata muda mwingi wa kujiandaa ukilinganisha na Chelsea. “Tunakabiliana na timu ngumu, katika hali hii Chelsea ambayo inazo siku tatu zaidi za kujiandaa kuliko sisi ambao tunayo moja. Hii inawapa faida wapinzani wetu. Tunatakiwa kukubali kanuni za mchezo, lakini tunahitaji kusema nini ni kweli kuhusu sisi,” alisema Pochettino. Hiyo inatokana na timu zote hizo kucheza katikati ya wiki hii, Spurs ikicheza juzi dhidi ya Qarabag na kuifunga bao 1-0 kwenye Kombe la Ligi ya Europa na Chelsea ikakipiga na Maccabi Tel Aviv Jumanne iliyopita na kuichapa mabao 4-0 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya. Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho, yeye kwa upande wake ameendelea kupatwa na kicheko kufuatia mwenendo mzuri wa timu yake hivi sasa. “Ni jambo la muhimu na tunafurahia kushinda mechi zetu mbili zilizopita (Norwich City na Maccabi Tel Aviv). Naamini itatuongezea hali ya kujiamini. Ni jambo la muhimu kwa sababu tulicheza mechi nyingi bila ushindi mfululizo. Kufanya hivyo ni jambo zuri.” Hata hivyo, Chelsea inaweza kuwa kwenye wakati mgumu dhidi ya Spurs kutokana na rekodi bora waliyonayo kwa sasa wakiwa hawajapoteza mechi yoyote ya ligi, toka walipofungwa na Manchester United katika mchezo wa ufunguzi (1-0). Vile vile Spurs imeimarika hivi sasa baada ya straika wake tegemeo, Harry Kane, kuanza kuonyesha makeke yake ya msimu uliopita kufuatia kuanza vibaya msimu huu mpaka sasa amefunga mabao tisa ndani ya mechi sita zilizopita. Kane, 22, ana rekodi nzuri dhidi ya Chelsea ikiwa ni baada ya kufunga mabao mawili wakati Spurs ikiwalaza matajiri hao mabao 5-3 msimu uliopita kwenye siku ya Mwaka Mpya. Kwa upande mwingine, Chelsea imeanza msimu huu vibaya baada ya kufungwa michezo saba kati ya 13 waliyocheza mpaka sasa, matokeo ambayo yamemweka kwenye presha kubwa Mourinho ya kutimuliwa ndani ya kikosi hicho. Msimu uliopita kwenye mechi zao mbili baina yao zilitengeneza jumla ya mabao 11, hiyo inaonyesha kuwa safu ya ulinzi ilikuwa katika wakati mgumu sana na kutokana na vipaji vya washambuliaji wa pande zote mbili, mabao yanatabiriwa kufungwa leo. Winga wa Chelsea, Eden Hazard, amefunga mabao kwenye mechi tatu za mwisho dhidi ya Spurs, huku Kane naye akifunga mawili katika mchezo wa mwisho waliokutana. Uwepo wa wakali Kane, Christian Eriksen, Mousa Dembele na Mkorea Son Heung-min kwenye eneo la ushambuliaji la Spurs, unatarajia kuwaweka kwenye wakati mgumu mabeki wa Chelsea hasa rekodi yao ikionyesha kuwa wameruhusu mabao 23 ndani ya mechi 13 za ligi msimu huu. TAARIFA ZA KLABU Spurs itamkosa kiungo wake Dele Alli, ambaye atakuwa akitumikia adhabu ya kukosa mchezo mmoja baada ya kukusanya kadi tano za njano huku pia ikitarajia kuwakosa Erik Lamela, Nabil Bentaleb, Nacer Chadli na Alex Pritchard walio majeruhi. Chelsea itamkosa nahodha wake, John Terry, aliyeumia kwenye mchezo uliopita dhidi Maccabi Tel Aviv ya Israel. REKODI ZAO Chelsea imefungwa mechi tano na kushinda mmoja kwenye michezo saba iliyopita ya ligi waliyocheza ugenini, pia imeshinda mmoja tu kati ya tisa iliyopita katika Uwanja wa White Hart Lane. Mshambuliaji wa Spurs, Kane, amefunga mabao saba katika mechi nne zilizopita za ligi, pia imepiga mashuti mengi yaliyolenga lango msimu huu kuliko timu nyingine yoyote ya ligi hiyo. Spurs imepoteza mechi mbili tu kati ya 20 zilizopita walizocheza kwenye uwanja wa nyumbani. Huku Chelsea ikifunga mabao matatu tu katika mechi zake nne zilizopita za ligi. Kiungo wa Chelsea, Cesc Fabregas, ametengeneza mabao 11 dhidi ya Spurs, matano zaidi ya timu nyingine yoyote kwenye ligi hiyo. Mechi nyingine kali kesho, Liverpool iliyokuwa kwenye makali tokea ianze kunolewa na Mjerumani, Jurgen Klopp, itawaalika Swansea ndani ya Uwanja wa Anfield huku Arsenal ikisafiri kuwafuata Norwich, zote zikichezwa saa 1.15 usiku.   LEICESTER V MAN UNITED Wakati shughuli hiyo ikiwa pevu kesho, leo saa 2.00 usiku kutakuwa na mtanange mwingine mkali kwa vinara wa ligi, Leicester City kuwakaribisha Manchester United walio nafasi ya pili kwenye Uwanja wa King Power. Kocha wa Leicester City, Muitaliano Claudio Ranieri, atakuwa akiangalia tena namna wachezaji wake watakavyopambana na vigogo hao, akichagizwa na kasi nzuri ya nyota wake, Jamie Vardy na Riyad Mahrez. Vardy ambaye ni mshambuliaji anaamini ya kuwa leo atavunja rekodi ya nyota wa zamani wa Man United, Ruud van Nistelrooy, kwa kufunga bao la 11 mfululizo baada ya kuifikia rekodi ya Mholanzi huyo ya kufunga mabao 10. Akiwa na mabao 13 mpaka sasa kileleni kwenye ufungaji bora ndani ya mechi 13, Mwingereza huyo amekuwa na msimu mzuri sana akiisaidia Leicester kuongoza ligi kwa pointi 28 huku United wakiwa nazo 27. MAN CITY V SOUTHAMPTON Shughuli nyingine pevu itakuwa kwenye Uwanja wa Etihad kwa Manchester City kuwakaribisha Southampton, zote zikitoka kupoteza mechi zao zilizopita, Saints ikifungwa na Stoke City bao 1-0 huku Man City ikipigwa na Liverpool mabao 4-1.   Saints chini ya kocha Ronald Koeman, ina rekodi nzuri msimu huu, ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja ugenini ikishinda miwili na sare nne, ikiwemo ule walioichapa Sunderland kwenye mchezo wake wa mwisho wa ugenini.   City yenyewe ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi 26 sawa na Arsenal, imeshinda mchezo mmoja kati ya minne iliyopita ya ligi, pia imepoteza mechi iliyopita ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kufungwa na Juventus bao 1-0 jijini Turin, Italia.   Msimu uliopita, Saints ilifungwa na City mabao 3-0 nyumbani, lakini vijana wa Manuel Pellegrini wakapoteza mchezo Etihad kwa kupigwa na Southampton 2-0.   Nyota wa Saints, Jay Rodriguez, ataukosa mchezo huo baada ya kufanyiwa upasuaji wa mguu wake mwanzoni mwa wiki hii, itamkosa pia staa wake, Graziano Pelle, anayetumikia adhabu, huku Fraser Forster na Florin Gardos nao wakiendelea kukosekana.   City itamkosa kipa wake tegemeo Joe Hart, nahodha Vincent Kompany, walio majeruhi huku mabeki Pablo Zabaleta na Eliaquim Mangala wakiwa kwenye hati hati ya kucheza, lakini itawapokea kiungo wake nyota David Silva na mshambuliaji Wilfried Bony, watakaorejea dimbani.  
2michezo
  Na Eliya Mboneya, Arusha Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu(AfCHPR), imesema Mahakama za ndani Tanzania katika kesi ya kubaka na kulawiti iliyokuwa inamkabili mwanamuziki Nguza Viking (Babu Seya) na mwanawe Johnson Nguza (Papii Kocha) zilitenda haki kwa kiwango kikubwa na kwa upande mwingine zilikiukwa. Aidha, kutokana na kukiukwa kwa baadhi ya haki zao hizo, mahakama hiyo imewaruhusu kuwasilisha hoja na kuainisha ni namna wanaweza kuomba fidia kulingana na haki zao ziliokiukwa ndani ya siku 30 huku upande wa Jamhuri ukitakiwa kujibu hoja hizo ndani ya siku 30. Akitoa hukumu hiyo katika mahakama hiyo leo Ijumaa Machi 23, Kiongozi wa majaji nane waliokuwa wakisilikiza shauri hilo, Gerald Niyungeko mbele ya Rais wa Mahakama hiyo, Jaji Sylvain Ore, amesema baadhi ya haki zilizotendwa ni pamoja na kuwaachia watuhumiwa watatu kwenye kesi hiyo pamoja na kubakiza mashitaka manne kati ya 21 yaliyokuwa yakiwakabili. “Haki zao hazikukiukwa kulingana na uamuzi uliotolewa na mahakama za ndani za Tanzania kwa kuwaachia washtakiwa wengine na kupunguza mashtaka 21 hadi manne, lakini kwa upande mwingine zilikiukwa, kwa mfano wakiwa Mahakama ya Halimu Mkazi Kisuti walikaaa mahabusu kwa siku nne bila kufahamishwa makosa yao lakini pia hawakuwa na wakili wa kuwatetea. “Aidha, waleta maombi pia waliomba kupimwa mkojo na damu ili kuthibitishwa kama waliwaingilia wale watoto ambao upande wa jamhuri ulidai waliambukizwa magonjwa ya zinaa lakini walikataliwa. “Kwa upande mwingine, Nguza aliomba kupimwa kama ana uwezo wa kufanya tendo la ndoa au lakini pia alikataliwa,” amesema Jaji Niyungeko. Hata hivyo, kuhusu kupinga kifungo cha maisha, Jaji Niyungeko amesema mahakama haikujielekeza katika shauri hilo kwa sababu waleta maombi wako huru kwa msamaha wa rais hivyo haikuona sababu ya kushughulikia hilo kwani wako nje kwa mujibu wa sheria. Babu Seya na Papii Kocha waliachiwa kwa msamaha wa rais Desemba 9, mwaka jana kutokana na kifungo cha maisha jela walichohukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Juni mwaka 2004 baada ya kumkuta na hatia ya kunajisi na kulawiti watoto 10 ambapo walikata rufaa Mahakama za juu na kugonga mwamba na hivyo kulazimika kukimbilia AfCHPR wakidai haki zao zilivunjwa.
1kitaifa
KLABU ya Yanga imewatuliza mashabiki wake kufuatia kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikisema kazi haijaisha wanajipanga upya kwa ajili ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho Afrika. Yanga imetolewa na Zesco United ya Zambia kwa jumla ya mabao 3-2, wakitoka sare nyumbani ya bao 1-1 na kufungwa ugenini mabao 2-1 na hivyo kuangukia Kombe la Shirikisho. Akizungumzia mipango yao jana, Ofisa Habari wa Yanga Hassan Bumbuli (pichani) aliwaomba mashabiki kusahau yaliyopita na kuungana kuiunga mkono timu kuelekea katika michezo ijayo. “Tumepokea matokeo kwasababu ni sehemu ya mchezo, bado tuna kazi kubwa naamini umoja wetu upo, tuendelee kuisapoti timu kwa hali yoyote kwa kuangalia na michuano iliyoko mbele yetu,”alisema. Kikosi hicho tayari kimewasili Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Polisi Tanzania utakaochezwa kesho.Bumbuli alisema hawatakuwa na muda wa kumpumzika timu itafanya maandalizi ya mchezo huo na mwingine dhidi ya Coastal Union ili kupata matokeo mazuri.Yanga ilianza vibaya ligi msimu huu baada ya kupoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Ruvu Shooting kwa bao 1-0 huku ikielezwa sababu huenda wana kikosi kipya kisichokuwa na muunganiko mzuri.
2michezo
KOCHA wa AFC Leopards Casa Mbungo ameondoka klabuni hapo baada ya kusitisha mkataba wake. Kocha huyo mnyarwanda jana alikwenda mazoezini na kuwaaga wachezaji na wafanyakazi wenzake.“Nitawakumbuka, nitaikumbuka Kenya. Tafadhali endeleeni kufanya kazi kwa bidii, hamuwezi kujua kitakachokuja mbele,” Mbungo aliwaambia wachezaji wake.Mbungo ameondoka kwenye klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Kenya kutokana na kukumbwa na ukata. Amelazimika kusitisha mkataba wake baada ya kutolipwa mshahara wake kwa miezi mitano na huku akidaiwa kudai malimbikizo ya mshahara wake zaidi ya sh milioni mbili za Kenya.Ametoa siku 15 kwa klabu hiyo kumlipa fedha zake vinginevyo atawashitaki kwa Shirikisho la soka la kimataifa, Fifa. AFC Leopards kwa siku za karibuni imekumbwa na ukata na haijalipa wafanyakazi wake tangu SportPesa ilipositisha mkataba nao tangu Agosti mwaka huu.“Inasikitisha safari hii kuisha hivi, tumejifunza mengi kutoka kwako, yatabaki kwenye fikra zetu, Mungu akuvariki kocha Andre Casa Mbungo,” alisema nahodha wa timu hiyo Robinson Kamura.Kocha msaidizi Anthony Kimani anatarajiwa kuiongoza Leopards katika mechi ya mwishoni mwa wiki dhidi ya Zoo Kericho mjini Kakamega
2michezo
Mwenyekiti wa Shiwata, Cassim Taalib alisema jana kuwa kikao cha Kamati Utendaji ya Mtandao huo kilichoketi juzi kilifikia uamuzi huo baada ya kufuatilia kwa karibu mafanikio ya Samatta akiwa na timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na klabu yake ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kufanya vizuri katika mashindano ya Afrika hadi kuchaguliwa kuwa mchezaji bora.Alisema Shiwata inatoa kiwanja hicho kama zawadi kwa mchezaji huyo kutokana na uwezo wake wa kulitangaza taifa katika medani ya kimataifa katika mchezo wa soka ambako wengine watafuata nyayo zake.Taalib alisema taratibu za makabidhiano zinafanywa kwa mawasiliano na baba yake mzazi, Ali Samatta na atakabidhiwa eneo hilo mara baada ya kurudi kutoka Ubelgiji ambako anaenda kusaini mkataba na timu ya KRC Genk ya Ligi Kuu ya Ubelgiji.Shiwata yenye wanachama zaidi ya 8,000 inamiliki ekari 300 za kujenga makazi, kumbi za starehe, viwanja vya michezo na nyumba za kuishi katika kijiji cha Mwanzega wilayani Mkuranga na ekari 500 eneo la Ngarambe kwa ajili ya kilimo.
2michezo
Mkurugenzi mtendaji wa klabu ya Atletical Madrid bwana Gil Marin amethibitisha kuwa Mshambuliaji wa klabu hio raia wa Ufaransa Antoine Griezmann atajiunga na Barcelona msimu huu. Griezmann alisemakuwa mwishoni mwa msimu wa mwaka 2018/19 ataondoka Wanda Metropolitano baada ya kuitumikia klabu hio kwa miaka mitano (5). Ikumbukwe nyota huyo Alikuwa akiwindwa na Barcelona tokea msimu uliopita kabla ya kutangaza kubakia Atretical Madrid kupitia makala iliyoitwa “The Decision” Iliyorushwa kabla ya kombe la dunia. Bwana Marin ameongeza kuwa “Kuna wachezaji wanohisi kuwa wao Ni wakubwa zaidi ya kikosi , Tunahitaji kuunda kundi la wanaume” amesema hayo alipokuwa akihojiwa na kituo Cha redio Cha (Estadio). Ikumbukwe Griezmann amefunga Mabao 133 katika michezo 256 aliyoitumikia Atletical Madrid Anatajwa kuwa na thamani ya €200 million lakini inakadiliwa huenda thamani yake ikashuka kufikia €120 Million kufikia July 1.
2michezo
MKUU wa Wilaya ya Chemba, Saimon Odunga amesema kesho watazindua utaratibu wa ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali baada ya kupitisha vigezo ambavyo wanaona wanaweza kupata wajasiriamali.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Odunga alisema sifa ambazo zimewekwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuwa ngumu kupata mjasiriamali, ambaye anastahili kupewa kitambulisho. “Leo (jana) tumekutana na kuangalia utekelezaji wa ugawaji wa vitambulisho kwa kutumia sifa za TRA, tumeona hazina uhalisia na hatutaweza kumpata mjasiriamali hata mmoja wa kupata kitambulisho, hivyo tunaweka vya kwetu.“Tumeona wajasiriamali wa maduka na migahawa na biashara zinazofanana na hizo, tuwaondoe katika orodha ya watu watakaonufaika na tuwalenge hasa wale wanaopanga biashara barabarani,” alisema Odunga. Wakati wakuu wa wilaya wakikabidhiwa vitambulisho na Mkuu wa mkoa, Dk Binilith Mahenge, Meneja wa TRA Mkoa wa Dodoma, Kabula Mweneri alisema wajasiriamali wanaostahili kupata vitambulisho hivyo ni wale wenye mapato ghafi yasiyozidi Sh milioni nne kwa mwaka.Pia asiwe amewahi kupata Kitambulisho cha Mlipa Kodi (TIN) ya biashara na kutakiwa kujaza fomu maalumu. Odunga alisema baada ya kupitia vigezo vyao, ambavyo ambavyo ni kwa yule anayepanga bidhaa zake chini, watawatumia watendaji wa mitaa kuwabaini wafanyabaishara wa aina yiyo. “Hata wangesema anayepata faida, pia tusingeweza si mama ntilie au machinga, hivyo sheria ya kuwa na mapato ghafi milioni nne imekuwa ngumu, hivyo sisi tumepanga kuwapa wale wanaopanga biadhaa zao chini.Alisema ili utaratibu huo ufanikiwe, leo wanaendesha semina kwa watendaji wa mitaa na vijiji, ili kuwapa mafunzo ya vigezo hivyo ili kesho wazindue rasimu ugawaji wa vitambulisho. Hivi karibuni, Rais John Magufuli alizindua vitambulisho vya wajasiriamali na kuwakabidhi wakuu wa mikoa kwa ajili ya kwenda kuvigawa kwa wajasiriamali wadogo. Mkoa wa Dodoma ulipokea 25,000 na viligawiwa kwa uwiano wa idadi ya watu ambapo Halmashauri ya Jiji imepatiwa vitambulisho 5,000, Chamwino 4,000, Kongwa 3,750, Mpwapwa 3,500 na Bahi vitambulisho 2,750. Pia Halmashauri ya Chemba walipatiwa vitambulisho 2,750, Kondoa Mji 2,500 na Halmashauri ya Kondoa Vijijini ilipata mgawo wa vitambulisho 750.
1kitaifa
Na BADI MCHOMOLO UKIWA unakumbwa na msongo wa mawazo mara kwa mara unaweza kufanya mambo ambayo utakuja kuyajutia katika maisha yao kama utashindwa kuwa makini na kufanya maamuzi sahihi juu ya mawazo ambayo yanakusumbua. Wadau wengi wa muziki duniani waliguswa na kifo cha staa wa muziki wa Pop nchini Marekani, Michael Jackson, ambacho kilitokea Juni 25, 2009. Wapo ambao walipoteza fahamu baada ya kupata taarifa ya kifo cha msanii huyo. Msanii huyo aliacha watoto watatu ambao ni Michael Joseph Jackson Jr mwenye umri wa miaka 20, Paris Jackson mwenye umri wa miaka 18 na Prince Michael Jackson II mwenye miaka 15. Kila mmoja kati ya wote hao waliguswa sana na kifo hicho cha baba yao, lakini ilikuwa tofauti kwa Paris ambaye alionekana kama anataka kuchanganyikiwa. Kipindi Jackson anapoteza maisha Paris alikuwa na umri wa miaka 11, alikimbizwa hospitalini baada ya kupata taarifa ya kifo hicho cha baba yake, lakini baada ya muda alirudi katika hali ya kawaida, ila kila mara alikuwa anaonekana akiwa na mawazo, hivyo alikuwa anasimamiwa na wataalamu wa kuondoa mawazo ili aweze kuwa sawa. Tangu hapo alianza kufikiria kuvuta Sigara huku akiwa na lengo la kutaka kupunguza mawazo ya baba yake na kuna wakati alikuwa anafikiria kunywa pombe ili alewe sana na apate usingizi akiwa na lengo la kupoteza ndoto za mara kwa mara juu ya baba yake. Alishindwa kunywa pombe kwa kipindi hicho, lakini aliweza kuvuta sigara kwa kujificha sana, uvutaji wa kujificha mara kwa mara ulimfanya aizoee sigara, lakini baada ya kufikisha miaka 17 alianza kuonekana wazi kuwa anavuta sigara. Majimbo mbalimbali nchini Marekani yamekuwa yakipiga marufuku uvutaji wa sigara kwa vijana wenye umri chini ya miaka 18, hata hapa Tanzania, lakini kwa Paris akiwa na miaka hiyo 17 alikuwa anavuta mitaani na kukumbana na misukosuko ya kila mara na polisi. Alikuwa na furaha sana baada ya Aprili mwaka jana kutimiza miaka 18, hivyo aliamua hatoweza kujificha tena katika uvutaji wa sigara, ni wazi alikuwa anavuta kila kona jambo lililomfanya kuathirika na uvutaji wa sigara. Familia yake ilijaribu kukaa naye pamoja na kumshauri kuachana na uvutaji wa sigara lakini aliwajibu kuwa anatamani kuachana na uvutaji lakini anashindwa kabisa na alianza kuvuta kutokana na kutaka kupunguza mawazo ya baba yake, lakini kwa sasa anashindwa kuacha. “Mawazo yanaweza kukuweka katika mazingira magumu ndani ya maisha yako, wakati nina umri wa kuanzia miaka 11 nilikuwa katika wakati mgumu baada ya kumpoteza baba yangu kipenzi, nilifikiria kufanya mambo mengi ambayo ni mabaya katika maisha yangu kama vile kunywa pombe, kuvuta sigara na mambo mengine. “Lakini kikubwa ambacho nilikifikiria na nikakifanya ni kuvuta sigara, jambo ambalo lilikuwa baya zaidi kwa kuwa nilikuwa na umri mdogo, hivyo limeniharibu na hadi sasa najaribu kutaka kuacha lakini ninashindwa. “Nikikaa muda mrefu bila kuvuta sigara najisikia vibaya, lakini ninaamini kama ningeweza kuzuia hisia zangu katika kipindi cha kifo cha baba yangu basi nisingekuwa kwenye hali nilionayo kwa sasa na sipendi kuwaona vijana wadogo wakifikiria kuvuta sigara,” alisema Paris. Uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya, mbali na Paris kujitaja kuwa anashindwa kuachana na uvutaji wapo wengi ambao wameathirika na uvutaji wa sigara na wanashindwa kuacha, hilo ni tatizo.
4burudani
MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo ifi kapo Juni 30, mwaka huu, wawe wamekamilisha ununuzi wa mashine za kielektroniki za kukusanyia mapato.Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), Dk Mahenge alisema halmashauri zote saba zinatakiwa kukamilisha ununuaji wa mashine za kukusanyia mapato (POS) na akazipongeza ambazo tayari zimekamilisha ununuzi huo.Amemuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Muduka Kessy kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha halmashauri za Kondoa Mjini, Vijijini, Chemba, Bahi, Jiji, Kongwa, Chamwino na Mpwapwa zinakamilisha ununuzi wa mashine hizo.Dk Mahenge ameipongeza Halmashauri ya Kondoa Vijijini ambayo imenunua mashine 59 na hivyo hakuna kituo cha kukusanya mapato ambacho hakina mashine hiyo.Ameipongeza pia halmashauri ya Kondoa Mjini kwa kuweka lengo la kununua mashine 56 na kuvuka lengo kwa kuongeza mashine tatu zaidi kwa ajili ya kukusanya mapato.Akaziomba zote zilizobaki kuhakikisha kwamba zinakamilisha ununuzi huo, ambapo takwimu zinaonesha kwamba Halmashauri ya Kongwa haijakamilisha mashine 77, kati ya 150 zinazotakiwa, hivyo inatakiwa kutumia fedha za ndani au kukopa ili kupata mashine hizo.Pia takwimu zinaonesha kwamba, Halmashauri ya Chemba bado mashine 65, kati ya mahitaji ya mashine 130, hivyo mikakati madhubuti inahitajika ili kununua mashine zilizobaki.Halmashauri ya Bahi bado mashine 20, kati ya 80 zinazotakiwa kuwapo katika maeneo mbalimbali ya kukusanya mapato katika wilaya hiyo na kuachana na mtindo wa kutumia risiti.Pia aliitaka, Halmashauri ya Chamwino ambayo bado mashine 50, kati ya 120 zinazotakiwa kuwapo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, kuhakikisha nayo inakamilisha.“Halmashauri ya Mpwapwa imenunua mashine 110 kati ya mashine 113 na hivyo bado mashine tatu, hivyo inatakiwa kukamilisha idadi ya mahitaji yake kupitia mkakati wa kukamilisha katika robo ya nne ya mwaka (Aprili-Juni),” alisema.Akisoma takwimu katika halmashauri ya Jiji, mkurugenzi wake, Godwin Kunambi alisema ina mashine 339 za kukusanyia mapato ambazo ni zaidi ya malengo ya mashine 336.Alisema mashine zilizoongezeka zimewekwa katika maeneo yaliyobuniwa ya makusanyo ya mapato na mkakati ni kupeleka katika shule ili kuhakikisha kila mapato yanayoingia yanaingizwa kwenye mashine hizo.Alizitaka halmashauri nyingine zilizobaki kuhakikisha zinakamilisha ifikapo Juni 30, mwaka huu, ambao ni mwisho kutokuwa na mashine hiyo, ili kuondoa mwanya wa kupotea mapato ya mkoa.Mkuu wa Mkoa, Dk Mahenge aliwataka viongozi wa halmashauri hasa wakurugenzi kuhakikisha wanatekeleza maazimio yanayofikiwa katika vikao, kwani tayari jambo la kila halmashauri kuwa na mashine hizo lilijadiliwa na kuwekewa maazimio katika vikao vilivyotangulia.
0uchumi
MWAMVITA MTANDA-DAR ES SALAAM BAADA ya Simba kupata ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambao umewapa nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Patrick Aussems, amesema atapambana kuhakikisha kikosi chake kinachukua ubingwa wa Afrika. Simba ilitinga hatua hiyo baada kupata ushindi katika mchezo huo uliochezwa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ushindi huo uliifanya Simba kufikisha pointi tisa na kumaliza kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi hilo nyuma ya Al alhly ya Misri iliyomaliza na pointi 10, JS Soaura iliyomaliza nafasi ya tatu ikiwa na pointi nane, wakati AS Vita ikimaliza mkiani na pointi zake saba. Akizungumza na MTANZANIA jana, Aussems alisema mipango yake kwa sasa ni kuhakikisha wanafanikiwa kuchukua ubingwa wa michuano hiyo. Alisema awali walikuwa na malengo ya kufikia hatua ya makundi ya michuano hiyo, lakini baada ya kufanikiwa alipata morali iliyopelekea asonge mbele zaidi. “Nitapambana kwa hali na mali kuhakikisha kuwa Simba inafanikiwa kuchukua ubingwa, hakuna sababu  ya kuhofia timu yoyote ambayo tutakutana nayo, nina imani timu yangu inaweza na ndio maana mpaka hapa tumefanikiwa kwa kiasi kubwa sana,” alisema Aussems.  “Nataka Simba iweke historia mwaka huu ipate ubingwa wa Afrika na pia ishinde tena michuano ya Ligi Kuu, hata kama nitaondoka basi nitakuwa nimeacha historia nzuri,” alisema Aussems.  Aussems alimmwagia sifa kiungo wake, Haruna Niyonzima, kwa kiwango alichokionesha katika mchezo huo.
2michezo
LONDON, ENGLAND MSHAMBULIAJI wa klabu ya Arsenal, Danny Welbeck, atakuwa nje ya uwanja kwa miezi mitatu hadi mitano kutokana na kusumbuliwa na goti. Mchezaji huyo wa timu ya Taifa ya England pia ataikosa michuano ya Euro ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi majira ya joto nchini Ufaransa na atashindwa kuungana na klabu yake katika maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu ambapo Arsenal inatarajia kwenda Marekani. Welbeck alipata maumivu ya goti katika mchezo wa mwishoni mwa wiki iliyopita wakati klabu yake ikipambana na Manchester City alipogongana na Bacary Sagna, mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 2-2. Hata hivyo, kocha wa England, Roy Hodgson, amesema kwamba kumkosa mchezaji huyo katika kikosi chake kutakuwa na pengo kubwa. “Welbeck ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa katika safu ya ushambuliaji, kumkosa kwake ni tatizo kwetu katika michuano ya Euro, lakini bado tuna kikosi kipana ambacho kitaweza kupambana na kufanya vizuri,” alisema Hodgson.
2michezo
Lulu Ringo, Dar es Salaam Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga, Mwinyi Zahera amesema msimu huu wa 2018/2019 ukimalizika ataachana na timu hiyo kutokana na washabiki, wanachama wa klabu hiyo kushindwa kujitolea kuisaidia timu yao. Zahera ameiambia Mtanzania Digital kwamba anashangaa kuona Yanga ikijiita timu ya wananchi na yenye matajiri wengi lakini inashindwa kujisaidia yenyewe. “Mimi nasema hivi ukijisaidia na Mungu anakusaidia, sasa mimi Kocha Zahera nimeamua Ligi hii ikimalizika naweza kuondoka Yanga sababu nimefanya mambo mengi sana kuisaidia timu lakini naona wanayanga wenyewe hawapendi kujisaidia. “Kama nawaambia washabiki na wanachama tuijenge timu yetu sisi wenyewe na hakuna chochote kinachofanyika sitaweza kuendelea hivi,” amesema Zahera. Mwanzoni mwa Februari mwaka huu Kocha Zahera alianzisha kampeni ya kuchangia klabu ya Yanga ambapo amesema pesa itakayopatika itatumika kununua wachezaji na kujenga uwanja wa mazoezi kwa msimu ujao. Mratibu wa klabu ya Yanga, Hafidh Salehe Jana Februari 21, alitanga zaidi ya shilingi milioni 21 ndizo zilizopatika tangu kampeni hiyo kuanzishwa, kiasi kilichoonekana kutomridhisha Kocha Zahera kutokana na mipango mikubwa aliyo nayo baada ya msimu huu kuisha. Zahera amesema anashangaa kuona wanachama na washabiki wa Yanga kuchangia kiasi hicho kwa takribani wiki nne toka kampeni hiyo ilipoanza. “Hao matajiri wengi walioko Yanga kama kila wiki wanachangia Yanga pamoja na wanachama, mashabiki tunauwezo wa kupata fedha nyingi na mwezi wa tano tukanunua wachezaji wazuri na tukajenga uwanja wa mazoezi,” amesema Zahera. “Kinachonishangaza zaidi mashabiki na wanachama wao wanalalamika tu timu inapofungwa, sasa nawaomba wajipange ni jinsi gani watayaepuka maumivu kila mara timu ikicheza wapende kujisaidia wenyewe. “Basi nadhani Mungu hawezi kunilaumu kwa maamuzi ntakayochukua kwa kuamua kuachana na timu ya Yanga maana itakua vigumu sana kuendelea kujitolea wakati watu wao wenyewe hawapendi kujitolea,” amesema Kocha Zahera.
2michezo
MANCHESTER, ENGLAND NAHODHA wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney, amedai kwamba wachezaji wanapaswa kulaumiwa na sio kocha wao, Van Gaal. Mshambuliaji huyo amesisitiza kwamba, wachezaji hawachezi kulingana na majukumu yao hivyo lawama anatupiwa kocha badala yao ambao wanatakiwa kuonesha uwezo wao kwa lengo la kuitetea klabu. Mwishoni mwa wiki iliyopita timu hiyo ilishuka dimbani katika mchezo wa Kombe la FA na kufanikiwa kushinda mabao 3-1 dhidi ya wapinzani wao Derby County. Kutokana na ushindi huo, Rooney anaamini kuwa wachezaji wanatakiwa kuwajibika kama timu ina shida au kufungwa na sio kocha wa kutupiwa lawama. “Sio vizuri lawama kutupiwa kocha pale timu inapopoteza mchezo wake, sisi wachezaji tunakuwa uwanjani hivyo tunatakiwa kuonesha majukumu yetu ili kuweza kuibeba timu. “Najua kila mchezaji anaingia uwanjani kwa ajili ya kutafuta ushindi, lakini kama hachezi kufuatana na majukumu yake basi timu haiwezi kushinda kisha kosa linakuja kuwa la kocha badala ya wachezaji,” alisema Rooney. Hata hivyo, kocha wa klabu hiyo, Van Gaal, anaamini kuwa watafanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo ya Kombe la FA msimu huu.
2michezo
ALIYEKUWA mpenzi wa rapa Tyga, Kylie Jenner, amefurahia akaunti yake ya Twitter kufungiwa ambayo inadaiwa kuwa na mkanda wake wa ngono na aliyekuwa mpenzi wake huyo. Mrembo huyo alifanikiwa kufikisha marafiki zaidi ya milioni 16, lakini mara baada ya kuachana na Tyga mwezi uliopita ikadaiwa kwamba kuna mkanda wa ngono umetupiwa kwenye akaunti hiyo waliocheza yeye na aliyekuwa mpenzi wake huyo. Kupitia akaunti yake ya Instagram, mrembo huyo aliandika kwamba kwa sasa hana wasi wasi kuenea kwa mkanda wake huo. “Kwa sasa mkanda wangu wa ngono ambao nilicheza na Tyga hauwezi kuonekana kwa kuwa akaunti yangu ya Twitter imefungiwa, hivyo hakuna anayeweza kuona chochote,” aliandika Kylie. Mrembo huyo kwa sasa anatoka na msanii wa hip hop nchini Mrekani anayejulikana kwa jina la PartyNextDoor.
4burudani
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA MWANASIASA Mkongwe nchini na Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, John Shibuda amewataka waliopokea fedha za mgao wa Escrow kuzirejesha. Vilevile alimwomba Rais Dk.John  Magufuli awasamehe. Shibuda ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Maswa Magharibi na  kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Chama cha Ada Tadea, alisema dini zote zinasema asamehewe yule ambaye anatubu na kukubali. Alisema   anaona  Ngeleja anatakiwa asamehewe kwa vile  amefanya kitendo cha kishujaa, kukiri  na kuamua kuzirejesha fedha hizo Shibuda ametoa kauli hiyo siku chache baada ya Mbunge wa   Sengerema, William Ngeleja (CCM) kurejesha Sh milioni 40.4 alizopewa na mfanyabiashara, James Rugemalira. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Shibuda alisema kitendo kilifanywa na Ngeleja ni cha kishujaa na anapaswa kusamehewa kwa kuwa ametambua kosa lake mbele ya umma. ‘’Kwa kitendo chake Ngeleja kutubu, tukubali tusiwe na inda na choyo ila wale wengine nao wakubali kuzirejesha fedha na Mheshimiwa Rais awasamehe kama dini zetu zinavyosema, mtu akitubu asamehewe,’’alisema. Wakati huohuo,  Shibuda amewashambulia wapinzani kwa akidai   wanatakiwa kuwa  na ajenda mpya kwa vile  zilizopo, Rais wa sasa Dk. John Magufuli amekwisha kuzitatua kwa kiwango kikubwa. Alisema Serikali ya awamu ya tano imo katika dunia ya mabadiliko ya mila, jadi na utamaduni na kokomesha uzembe. Alisema ajenda ya vyama vya upinzani kama rushwa, ufisadi  imenyauka na kuvitaka kutafuta sehemu ya kutokea. “Vyama vya upinzani kwa sasa ajenda yao ni nini? Ni zile zile za wakati ule Mwalimu   Nyerere aliporuhusu vyama vingi. “Wanasayansi walianza na dawa ya Panadol  lakini leo kuna dawa zaidi ya tatu basi na wapinzani wawe na vikosi kazi vya kubuni tiba mbadala ya kutengua utumishi uliotukuka wa Rais Magufuli,’’ alisema. Shibuda alisema serikali ya awamu ya tano inafanya vizuri huku akidai Taifa limepata Rais mwenye utumishi wachangamfu na kugusa hisia za jamii.
1kitaifa
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Dismas Ten amerusha kijembe kwa watani wao jadi Simba kufuatia usajili wa beki Kennedy Wilson Juma kutoka Singida United. Jana kupitia akaunti yao rasmi, klabu ya Simba ilitangaza umsajili beki huyo ambaye ana sifa ya matumizi makubwa ya nguvu awapo uwanjani kutokana na ukubwa wa umbo lake. “Ingizo jipya kwenye kikosi cha Mabingwa, beki wa kati Kennedy Wilson Juma amesaini mkataba wa miaka miwili. Uwepo wa Kennedy kwenye kikosi kwa kushirikiana na mabeki wengine tulionao ni hakika safu yetu ya ulinzi itakuwa imara zaidi,” taarifa kutoka Simba imeeleza. Kutokana na taarifa hiyo, Dismas Ten hakuwa nyuma kurusha kijembe kama ilivyojadi ya utani wao pindi moja ya timu zinapofanya usajili au tukio lolote lazima upande mwingine uponde.     Jamani fanyeni mumpe hati yule Mnyaturu.. Msije shangaa mnaletewa Sholo Mwamba hapo 😂😂😂😂😂 . . Kutoka kugombania wachezaji na TP Mazembe,Al ahly ,As Vita mpaka Singida United?😂😂😂 Toeni hati jamani..!😂😂😂 . Tunapitia comment Kisha tuta Press Play A post shared by Dismas Ten Sylvester (@dismasten) on Jun 18, 2019 at 4:29am PDT “Jamani fanyeni mumpe hati yule Mnyaturu.. Msije shangaa mnaletewa Sholo Mwamba hapo. Kutoka kugombania wachezaji na TP Mazembe,Al ahly ,As Vita mpaka Singida United? Toeni hati jamani! Tunapitia comment Kisha tuta Press Play,” Ten ameandika Kennedy amesaini mkataba wa miaka miwili na ataitumikia Simba mpaka mwaka 2021.     Ingizo jipya kwenye kikosi cha Mabingwa, beki wa kati Kennedy Wilson Juma amesaini mkataba wa miaka miwili. Uwepo wa Kennedy kwenye kikosi kwa kushirikiana na mabeki wengine tulionao ni hakika safu yetu ya ulinzi itakuwa imara zaidi. #NguvuMoja A post shared by Simba Sports Club (@simbasctanzania) on Jun 18, 2019 at 3:00am PDT
2michezo
WAKATI kocha wa Yanga SC, Charles Mkwasa, akiendelea kutupa vijembe vya kuwafunga wapinzani wao Simba SC kwenye mchezo wao wa mwishoni mwa wiki hii, kikosi hicho leo kimetamba kuendeleza makali yake dhidi ya Biashara United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.Yanga wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na hasira ya kuendeleza dozi ya kichapo lengo likiwa ni kuongeza idadi ya pointi kutoka 21 na kufikisha 24 na kuishusha Kagera Sugar.Yanga wanaoshika nafasi ya tano wanaingia kwenye mchezo huo wa 11 wakiwa na ari ya ushindi baada ya kuifunga Tanzania Prisons kwa bao 1-0 na kuvunja rekodi iliyowekwa na timu hiyo kushindwa kupoteza mchezo toka walipoanza msimu, wanakutana na Biashara ambayo ina morali ya kuibuka na ushindi kwenye michezo miwili iliyopita licha ya kushika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi 15.Mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu kwani toka Biashara imepanda ligi hiyo msimu uliopita ni miongoni mwa timu inayoleta ushindani mkali kila inapokutana na Yanga. Aidha rekodi zinaonesha kwa msimu uliopita timu hizo zilipokutana kwenye michezo ya ligi hiyo Yanga ilishinda mara moja kwa mabao 2-1 Uwanja wa Taifa na mchezo wa mzunguko wa pili Biashara ilishinda kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Karume Mara .Kocha Mkwasa alisema ushindi walioupata kwenye mchezo wa juzi umewapa nguvu na huo ni mwanzo wa kuvuna matokeo mapya kuchagiza mbio zao za ubingwa.
2michezo
MKUU wa Jeshi la Polis Nchini (IGP), Simon Sirro amewang’oa rasmi wakuu wa Polisi wa mikoa watatu (RPC), walioachishwa kushika nyadhifa zao na Waziri wa Mambo ya Ndani na Nchi, Kangi Lugola.Hivi karibuni Lugola alitangaza kuwa wakuu hao wa Polisi, wanatakiwa kuachia wadhifa wao kutokana na sababu tatu kuu, ambazo alisema kuwa walishindwa kutokomeza rushwa na kuwalinda wauzaji wa dawa za kulevya na biashara ya magendo. Waliotakiwa kuachia wadhifa wao ni aliyekuwa RPC wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, Salum Hamdun, RPC wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Emmanuel Lakula na Mkuu wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhan Nganzi.Kwenye uamuzi wake huo wa kuwaachisha wadhifa huo, Lugola aliingia kiundani kwa kusema kuwa kati ya hao, makamanda wawili wametenguliwa kutokana na kukaidi maagizo aliyoyatoa ya kufyeka vichaka vya rushwa katika mikoa yao, huku mmoja anajihusisha na kuwalinda wauzaji wa dawa za kulevya na kusindikiza wafanyabiashara wa magendo. Agizo hilo la Lugola lilionekana kusababisha taharuki hasa ya kisheria, ambapo alikosolewa na wadau mbalimbali wa sheria kuwa hana mamlaka ya kuwatoa kwenye madaraka askari hao.Taharuki iliongezeka zaidi, baada ya askari hao kuonekana wakiendelea na majukumu yao kwa takribani wiki moja tangu waziri huyo alipotaka waachie nyadhifa zao hizo. Wakili Jebra Kambole alizungumza na gazeti hili, ambapo alibainisha kuwa Sheria ya Jeshi la Polisi Sura Namba 322 kama alivyorejewa Mwaka 2002, ndiyo inatoa mamlaka ya Waziri na Mkuu wa Jeshi la Polisi, ambapo Kifungu cha 7(1) cha sheria hiyo kinampa waziri uwezo wa kumpa IGP maelekezo na miongozo mbalimbali. Alisema Kifungu cha 7(2) Cha sheria hiyo, kinampa mamlaka IGP uwezo wa kupanga vikosi vyake na kiwemo kuwapandisha na kuwashusha vyeo.Japo sheria pia inampa uwezo waziri kutoa maelekezo kwa IGP juu ya utendaji kazi huo na kifungu hicho cha sheria kimetumia neno “May” na kwa mujibu wa Sheria ya Tafsiri Tanzania Kifungu cha 53 Sura Namba 1 ya Sheria za Tanzania Kama ilivyorejewa 2002, May lina maana sio sharti la lazima.Alisema waziri hana mamlaka ya kuwaondoa kwenye nafasi zao, bali kumpa maelekezo mwenye mamlaka afanye hivyo, ambaye ni IGP ambaye naye sio lazima atende, kama alivyoambiwa anatumia akili yake na mamlaka yake kuamua hafanyi kama kasuku. Lakini, jana IGP Sirro aliamua kuwango’a rasmi RPC hao wote watatu na kusema kuwa kwa sasa wamerejeshwa makao makuu ya Polisi, kupisha uchunguzi dhidi yao. Uamuzi huo wa IGP Sirro, umemaliza taharuki hiyo, kwa kuwa kwa sasa wanakuwa nje ya wadhifa wao, kama alivyoagiza Waziri Lugola.
1kitaifa
Na UPENDO MOSHA, MOSHI BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, limepitisha sheria mbili za kudhibiti utumiaji wa mifuko ya plastiki pamoja na kudhibiti ufungaji wa mazao kwa mtindo wa lumbesa. Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika jana mjini Moshi wakati wa mjadala wa kupitisha sheria hizo, Meya wa Manispaa hiyo, Raymondy Mboya, alisema sheria  ya kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ina lengo la kulinda mazingira na afya za Wananchi, wakati sheria ya lumbesa inalenga kuwasaidia wakulima kiuchumi. “Halmashauri yetu tumepiga hatua kubwa  kwa kupitisha sheria hii ya kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ina lengo kubwa la kutunza mazingira na afya za wananchi wetu pamoja na sheria ya ufungaji wa mazao kwa mtindo wa lumbesa. “Sheria hii ya Lumbesa itawasaidia wakulima kuuza mazao yao vizuri na kupata faida, tofauti na ilivyo sasa ambapo wafanyabiashara wamekuwa wakiwanyonya wakulima kwa njia hiyo. “Hiyo Sheria ya Lumbesa imepitishwa bila kipingamizi na wajumbe wote wa baraza, wakati sheria ya matumizi ya mifuko ya plasiti imepitishwa kwa kupigiwa kura na madiwani 28 wakiwamo 16 walioikubali na 10 walioikataa. “Matumizi ya mifuko ya plasitii ni hatari kwa afya za wananchi kwani kwa mujibu wa taarifa za wataalamu wa afya, mifuko hiyo imekuwa ikisababisha magonjwa mbalimbali ikiwamo kansa na ugumba. “Kwa hiyo, huu ni wakati wa wananchi kujiandaa kuachana na matumizi ya mifuko hiyo kwa sababu sasa sheria ya kuizuia imepitishwa,” alisema Mboya. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo, Michael Mwandezi, alisema sheria hizo zitaanza kutumika baada ya mamlaka husika kuzisaini.
1kitaifa
NA MOHAMED KASSARA-DAR ES SALAAM MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili Simba, Zakaria Hanspope, amesema kwa sasa hayupo tayari kukaimu nafasi ya raisi wa klabu hiyo, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi. Aveva na Makamu wake Kaburu, Juni 28, mwaka huu walipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka matano ikiwamo kutakatisha fedha, huku wakiwekwa ndani hadi Julai 13, mwaka huu kutokana na makosa hayo kutokuwa na dhamana. Kutokana na tuhuma hizo kuwabili viongozi wa juu wa klabu hiyo waliokuwa wakisimamia shughuli mbalimbali za klabu, baadhi ya mashabiki wametaka jina la  Hanspope kukaimu moja ya nafasi hizo kutokana na kukaa muda mrefu  kwa mujibu wa  Katiba ya Simba. Hanspope ameibuka na kutoa kauli hiyo saa chache baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya Simba kukutana kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimbali, ikiwemo uendeshaji wa klabu hasa katika kipindi hiki wanachokabiliwa na maandalizi ya msimu ujao. Inaelezwa kuwa idadi kubwa ya mashabiki wanaunga mkono kati ya Hanspope au msaidizi katika Kamati ya Usajili, Kassim Dewji, mmoja kuchukua mikoba ya kuiongoza klabu hiyo hadi pale mambo yatakapokaa vizuri. Akizungumza na MTANZANIA jana, Hanspope aliwataka wanachama wa klabu hiyo kutafuta mtu mwingine sahihi atakayeweza kuingoza Simba kwa kipindi hiki ambacho viongozi wao wamepatwa na matatizo. “Siko tayari kukaimu moja ya nafasi za juu za kuiongoza Simba kutokana na kukabiliwa na shughuli nyingi binafsi ambazo zinanifanya kusafiri mara kwa mara, hivyo muda mwingi sitakuwa karibu na timu. “Wanachama wanatakiwa kuchagua mtu sahihi ambaye ataiongoza Simba kwenye kipindi hiki kigumu cha mpito, hasa ukizingatia sasa hivi tupo katika mchakato wa kujenga kikosi imara kwa ajili ya msimu ujao pamoja na michuano ya kimataifa,” alisema Hanspope.
2michezo
MOSCOW, URUSI UFARANSA wamefanikiwa kuingia hatua ya fainali kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi, baada ya juzi kushinda bao 1-0 dhidi ya Ubelgiji. Ushindani ulikuwa wa hali ya juu katika mchezo huo kutokana na ubora wa kila timu, lakini Ufaransa imeweza kuwazidi wapinzani kutokana na vitu vifuatavyo. Mlinda mlango Hadi kufikia mchezo wa juzi, Ufaransa imeruhusu jumla ya mabao manne tangu kuanza kwa michuano hiyo huku wakiwa wamecheza jumla ya michezo sita. Walikuwa na mlinda mlango ambaye alikuwa kwenye kiwango cha hali ya juu, Hugo Lloris, anayekipiga katika klabu ya Tottenham. Safu ya ulinzi Tangu kuanza kwa michuano hiyo, Ufaransa haijapoteza hata mchezo mmoja kati ya sita waliocheza, walitoka suluhu dhidi ya Denmark katika hatua ya makundi, lakini michezo mingine yote mitano waliibuka na ushindi. Ubora wa safu ya ulinzi ulikuwa unaundwa na beki wa kati, Samuel Umtiti (Barcelona), Raphael Varane (Real Madrid), Benjamin Pavard (Stuttgart), Lucas Hernandez (Atletico Madrid) na wengine. Hao waliweza kumuweka sehemu salama mlinda mlango wao, Lloris, ili asiwe kwenye wakati mgumu. Viungo Wachezaji ambao walikuwa wanaunda safu ya kiungo walikuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha washambuliaji wake wanalishambulia lango la wapinzani. Katika safu hiyo kulikuwa na N’Golo Kante (Chelsea), Blaise Matuidi (Juventus), Paul Pogba (Man United) na Corentin Tolisso (Bayern Munich). Wachezaji hao walikuwa kwenye kiwango bora kuhakikisha wanaleta mawasiliano kati ya safu ya ulinzi na ushambuliaji. Kila mchezaji alionekana kuvaa jezi kwa ajili ya kulipigania taifa hilo na kutaka kuandika historia mpya baada ya mwaka 1998 kufanya hivyo. Pogba alikuwa anahakikisha anapiga mipira mirefu ili kuwafikia washambuliaji, kazi hiyo ilikuwa inafanywa na mchezaji mwingine Kante. Washambuliaji Uwepo wa Kylian Mbappe mwenye umri wa miaka 19, akitokea klabu ya PSG, Antoine Griezmann wa Atletico Madrid, kulileta changamoto kubwa kwa safu ya ulinzi ya wapinzani wao katika kila mchezo. Wachezaji hao hadi sasa kila mmoja ana jumla ya mabao matatu. Mbappe alionekana kuwa tishio tangu kwenye mchezo dhidi ya Argentina katika hatua ya 16 bora ambapo Ufaransa ilishinda mabao 4-3, huku mchezaji huyo akifunga mabao mawili na kutoa pasi ya mwisho. Kwa hali ya kawaida Ufaransa imeonekana kuwa na kikosi chenye wachezaji wengi vijana wakiwa na kasi kubwa na hadi sasa wamefunga jumla ya mabao 10. Hata hivyo, kocha wa timu hiyo, Didier Deschamps, amekuwa na lengo la kutaka kuandika historia mpya katika timu hiyo kuwa wa kwanza kutwaa taji hilo mara mbili akiwa mchezaji na kocha. Alikuwa nahodha mwaka 1998 wakati timu hiyo inatwaa ubingwa kwenye ardhi ya nyumbani na sasa ana ndoto ya kufanya hivyo akiwa kocha. Timu inayokutana na Ufaransa katika fainali Jumapili lazima iwe makini katika kuwazuia wapinzani wao katika safu ya ushambuliaji na viungo.
2michezo
TRIPOLI, LIBYA MAELFU ya wananchi nchini Libya wamefanya maandamano katika mji mkuu wa nchi hiyo wa Tripoli wakiwa wamevalia vizibao vya njano kama wanavyofanya washiriki wa maandamano ya vizibao vya njano kupinga siasa za kiuchumi za serikali ya Ufaransa, ambapo nao wamelaani mienendo hasi ya Serikali ya Rais Emmanuel Macron dhidi ya nchi yao. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari nchini humo, washiriki wa maandamano hayo wamelaani vikali operesheni za Jenerali Khalifa Haftar, kiongozi wa kundi linalojiita ‘Jeshi la Kitaifa la Libya’ pamoja na uungaji mkono wa kijeshi wa Ufaransa dhidi ya nchi yao.  “Sisi wazawa wa Tripoli kama walivyo wakazi wa miji mingine ya Libya, tumekuja hapa kuonyesha upinzani wetu kwa utawala wa mtutu wa bunduki wa Haftar na mashambulizi yake,” amesema mmoja wa waandamanaji. Siku chache zilizopita, Shirika la Habari la Al Jazeera liliripoti kwamba, meli ndogo ya kivita mali ya Ufaransa ilituma silaha na zana za kijeshi kwa wapiganaji wa Jenerali Khalifa Haftar nchini Libya. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, boti ndogo za mwendo kasi zilitumika kupakua shehena ya silaha kutoka kwenye meli hiyo ya kivita ya Ufaransa.  Aidha wiki iliyopita, Waziri wa Ulinzi wa Tunisia, Abdelkrim Zbidi alinukuliwa akisema kuwa maofisa wa usalama wa nchi hiyo waliwatia mbaroni watu 13 wakiwa na pasi za kusafiria za Ufaransa kwenye kivuko cha Ra’s Ajdir katika mpaka wa Libya.  Wiki iliyopita, Serikali ya Maridhiano ya Kitaifa nchini Libya ilitangaza kukata ushirikiano wake wa kiusalama na serikali ya Ufaransa kutokana na hatua ya nchi hiyo kuliunga mkono kundi la wapiganaji wa Jenerali Khalifa Haftar.  Wapiganaji wa kundi hilo walianzisha mashambulizi makali Aprili 4 mwaka huu, dhidi ya mji wa Tripoli sambamba na kushambulia makao makuu ya Serikali ya Maridhiano ya Kitaifa mjini humo. Hujuma hizo hadi sasa zimepelekea karibu watu 270 kuuawa na wengine 1300 kujeruhiwa, sambamba na watu 35,000 kuwa wakimbizi.
3kimataifa
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kinatarajia kuanza kutoa Mitihani ya Kimataifa ya Ujuzi wa lugha ya Kiswahili (MKUKi) kuanzia mapema mwakani.Hayo yalibainishwa jana jijini hapa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo, alipokuwa akizungumzia mpango huo ambao pia umelenga kukuza na kuinua lugha ya Kiswahili. Alisema hatua hiyo ni jitihada za kuikuza na kuieneza lugha ya Kiswahili ulimwenguni kwa kuwa ni miongoni mwa lugha 10 zenye wazungumzaji wengi duniani.“Mtakumbuka kwamba Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alishafanya jitihada kubwa kuiendeleza na kuieneza Lugha ya Kiswahili, pamoja na kusimamia ubora wake ndani na nje ya nchi. Pia, marais waliofuata katika awamu zote za uongozi wa nchi yetu walitilia mkazo suala hili,” alisema.Alisema mitihani itafanyika mara sita kwa mwaka ikiendana na kipindi cha masomo ya Kiswahili kwa kila ngazi na itafanyika kwa njia za kielektroniki katika vyuo na vituo mbalimbali vya Kiswahili duniani, ambavyo tayari yamekwishafikiwa makubaliano maalumu kuhusu mitihani hiyo.“Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinakuwa ni chuo kikuu cha kwanza duniani kutunga mitihani hii, kusimamia utahini na usahihishaji na kisha kutoa cheti cha kimataifa kinachoonesha kiwango cha ujuzi wa mtahiniwa,”alisema.Alisema UDSM ina uzoefu wa kutosha na umahiri katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili na vyuo vikuu vingi hapa duniani vimekuwa vikipata uzoefu huo kutoka kwenye chuo hicho. Alisema tayari kuna makubaliano baina ya walimu wa Kiswahili wa UDSM na walimu wanaofundisha Kiswahili katika vyuo vya nje, kuhusiana na mitihani hiyo itakayoanza mwakani.“Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimejiandaa kuhakikisha kuwa mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano iko madhubuti kuwezesha mitihani hiyo kufanyika kwa ufanisi na kwa viwango vya kimataifa, kwa sababu kuna wahitaji ambao watafanyia mitihani hii wakiwa katika nchi zao, si lazima wasafiri na kuja kufanyia mitihani yao Tanzania,” alisema.Alisema walengwa wa mitihani hiyo ni wote wanaojifunza Kiswahili kama lugha ya pili au lugha ngeni katika ngazi mbalimbali, wakilenga kujipima usanifu katika kusoma, kuandika, kuongea na kusikiliza.Naye Profesa Aidin Mutembi kutoka Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema hatua hiyo itatoa fursa kwa watu mbalimbali wakiwemo wanadiplomasia, wafanyabiashara na wana taaluma tofauti wanaotaka kufanya kazi nchini kwenye nchi zinazozungumza lugha ya Kiswahili kufanya mtihani huo na kutambuliwa kimataifa.
1kitaifa
NAIROBI, KENYA STAA wa muziki nchini Kenya, David Mathenge (Nameless), amesema ubora wa nyimbo zake unasababisha apendwe na idadi kubwa ya wasichana warembo waliopo nchini humo bila kujali kwamba ni mume wa mtu. Alisema ingawa asilimia 80 ya nyimbo zake ‘Juju’, ‘Deadly’ na ‘Butterfly’ hulenga wasichana, waishie kuzipenda nyimbo hizo na si zaidi ya hapo kwa kuwa anaiheshimu na kuijali ndoa yake. “Sina uhakika kama wanapenda kazi zangu tu, kwa kuwa kuna wengine wanaonekana kuwa na maelezo mengi nje ya muziki wangu, lakini wanatakiwa kutambua kwamba nipo kwenye ndoa na nina familia yangu,” alifafanua Nameless. Msanii huyo amefunga ndoa na msanii wa muziki nchini humo, Wahu na wana takribani miaka 10 ya ndoa yao.
4burudani
MAREGESI PAUL Na RAMADHAN HASSAN -DODOMA MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), amesema wananchi wamewageuza wabunge wa Tanzania na kuwa kama mashine za kutolea fedha (ATM) na Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS). Kutokana na hali hiyo, amesema kuna haja Serikali kuboresha mafao yao ili yaendane na majukumu wanayokabiliana nayo. Waitara aliyasema hayo jana mjini hapa wakati wa semina ya wabunge walioko katika mabunge ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA). “Mshahara wa mbunge kila mwezi unakatwa shilingi milioni 1.2, lakini baada ya kumaliza miaka mitano ya ubunge, mafao yake yanakatwa tena. “Hivi huo utaratibu mliutoa wapi wakati haupo nchi yoyote duniani? Sisi wabunge tumegeuzwa kama ATM au saccos kwa sababu tutatoa pesa kila mahali. “Kule Kenya ofisi ya mbunge ni kama taasisi kwa sababu ina mbunge na ina mtafiti anayemsaidia mbunge kila anapotaka kufanya mambo yake. "Hata kukiwa na harambee, mbunge unaitwa na kutakiwa uchangie fedha nyingi, sasa utachanga kwa fedha zipi wakati mnatulipa kidogo, yaani huu ni mzigo kwetu wabunge. “Kwa hiyo, tuongezeeni mafao kwa sababu tunalipwa kidogo sana ikilinganishwa na nchi zingine,”alisema Waitara. Kwa upande wake, Mbunge wa Songwe, Philipo Mulugo (CCM), pamoja na kulalamikia mafao madogo, alitaka kujua takwimu halisi za malipo wanayolipwa wabunge wa Kenya na nchi zingine ili wayalinganishe na wanayolipwa wabunge wa Tanzania. Naye Mbunge wa Viti Maalum, Shally Raymond (CCM), alisema kuna haja kwa wabunge hao kuboreshewa mafao yao ili waweze kufanya kazi kwa mafanikio zaidi. Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), pamoja na kulalamikia mafao, alilalamikia utaratibu wa vyama vya siasa kukutanisha wabunge wao ili wakubaliane kupitisha mambo yenye masilahi ya chama badala ya kuangalia utaifa. Wakati hao wakisema hayo, Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM), alitaka wabunge wawekewe bima ya afya ya maisha kama sheria inavyotaka. “Kwanza kabisa nimeshangaa kusikia makao makuu ya CPA Barani Afrika yapo Tanzania na pia ofisi yao iko hapa bungeni. “Kuhusu hilo suala la bima ya afya ya maisha ya wabunge, nashangaa kwanini Serikali haitaki kuliruhusu kwa wabunge kwani hata Tume ya Utumishi ya Bunge, imekuwa ikisisitiza juu ya jambo hilo. “Yaani Tume ya Utumishi imelifuatilia kwa muda mrefu, lakini Serikali haitaki kukubali, jambo ambalo hakitendi haki kwa sababu baadhi ya wabunge wameshafariki na wengine wamepata ulemavu,” alisema Lugola. Hata hivyo, wakati akijibu hoja hizo, Katibu wa Spika wa Bunge, Said Yakub, alisema chanzo cha wabunge kugeuzwa ATM ni wao wenyewe kwa sababu ndivyo walivyowazoesha wapiga kura wao.
1kitaifa
BAADHI ya wachambuzi na makocha wa soka nchini wametaja timu tano zinazoweza kufika mbali kwenye fainali za Mataifa ya Afrika zinazoendelea nchini Misri, huku wenyeji wakipewa asilimia 100.Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wachambuzi hao Ally Mayai, Dominick Salamba na Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ kila mmoja ameitaja Misri kuwa inaweza kufika mbali zaidi na hata kuchukua Kombe la Afrika. Kwa upande wa Mayai alisema sababu ya kuwapa nafasi wenyeji ni kutokana na historia iliyopita, ikionesha kuwa Misri iliwahi kuandaa michuano hiyo mara nne na mara tatu kombe likabakia kwao.Pia, alizitaja timu nyingine zenye nafasi kuwa ni Cameroon kwa kuwa wameanza vizuri na huenda wakataka kupambana ili kutetea taji walilolitwaa Gabon, huku akisema Algeria ina kikosi bora chenye uwezo, Ghana wana wachezaji wenye uzoefu na Morocco kwa sababu ina kocha aliyewahi kutwaa mataji mara tatu. “Kila timu ina ubora wake na yeyote anaweza kufanya makubwa kutokana na uzoefu wa wachezaji wao kwenye mashindano hayo,” alisema.Kocha wa zamani wa Simba, Mwadui na Dodoma FC, Julio alisema bado pana ugumu kwa sababu ndio kwanza mapema ila anaziona Misri, Algeria na Senegal katika jicho la mbali.Alisema timu nyingi ni bora na nyingine hubadilika kutoka mechi moja kwenda nyingine hivyo, ni kazi kutabiri mapema. Mchambuzi Salamba alisema michuano hiyo inaonekana migumu kutokana na mbinu za kiufundi kutofautiana ila anaipa nafasi Senegal kutokana na kuwepo kwa muunganiko bora wa kikosi chao.Pia, Nigeria kutokana na uwezo wa kumiliki mpira ingawa katika kasi ya kushambulia kwao sio kubwa, Cameroon kuwa wana vijana wenye kasi, Misri ikibebwa na uzoefu na ni wenyeji lakini pia, Algeria kutokana na kucheza mpira wa nguvu na wenye kasi. Nigeria juzi ndio ilikuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya kucheza hatuia ya 16 bora kabla ya wenyeji Misri hawajaifuata baadae.
2michezo
Kikwete alitoa agizo hilo katika hafla ya kumuaga iliyoandaliwa na wasanii kutokana na mchango wake mkubwa katika tasnia ya sanaa.Katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam, Kikwete alisema kuwa Cosota inatakiwa kuhakikisha inadhibiti wizi wa kazi za wasanii nchini kutokana na watu wengi kunufaika na kazi hizo huku wasanii wakiambulia malipo kidogo ambayo hayaendani na kazi wanazofanya.Alisema katika kutekeleza mpango wa awali wa kupambana na wizi wa kazi za wasanii serikali imejipanga kutekeleza utaratibu wa wasambazaji wote wa kazi za wasanii kubandika stika ya usalama kwenye kila nakala ya kazi itakayosambazwa ili kuhakikisha kazi za wasanii haziibwi.Alisema katika utaratibu huo kila msambazaji ataingia mkataba na msanii kusambaza idadi fulani ya nakala na kupewa stika ambazo zitabandikwa katika kila nakala ili kudhibiti wizi na hatimaye wasanii kunufaika na kazi zao tofauti na ilivyo sasa ambapo anaenufaika ni msambazaji.“Nimeshazungumza na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kuhakikisha kwamba kazi zote za wasanii zinawekwa stika ili kuondoa usumbufu kwa wasanii kutonufaika na kazi zao ambazo wanatumia muda wao mwingi katika kuzitengeneza,” alisema Kikwete.Akizungumzia malipo ya wasanii katika miito ya simu, Rais Kikwete alisema kua tayari umeshaandaliwa utaratibu mzuri ambao utamwezesha msanii kulipwa kiasi cha fedha kulingana na nyimbo zake ambazo zinatumika katika kampuni za simu kama milio.Akitoa ushahidi wa kuanza kunufaika na mpango huo wa malipo, msanii wa Bongo Fleva Nikki wa Pili alisema kuwa awali kampuni ya Tigo ilikuwa ikimlipa shilingi laki moja kama ada ya nyimbo zake kutumika katika miito ya simu ambapo sasa kila mwezi kampuni hiyo inamlipa shilingi milioni mbili.Hafla hiyo ya kumuaga Rais pia ilihudhuriwa na wageni mbalimbali akiwemo Waziri wa Ujenzi ambae pia ni mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM, John Magufuli, Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye na Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
2michezo
Kulwa Mzee, Dar es Salaam Msanii wa Filamu nchini, Wema Sepetu aliyekuwa mahabusu katika Gereza la Segerea ameachiwa kwa onyo na dhamana yake inaendelea. Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Juni 24, saa nne asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde. Akitoa uamuzi wa aidha Wema afutiwe dhamana au la, Hakimu Kasonde amesema kazingatia kiapo kilichowasilishwa na Wakili Albert Msando na maelekezo ya mshtakiwa lakini mahakama inaona ni kweli alivunja masharti ya dhamana. Amesema sababu kubwa ni kuumwa ghafla ambapo alitakiwa siku ile ile angefika mahakamani kutoa taarifa si kuamua kuondoka. “Mahakama inakuonya, uhakikishe pale ambapo haupo mahakamani, Mahakama ijulishwe kupitia mdhamini wako na si vinginevyo,” amesema Hakimu Kasonde. Hakimu Kasonde amesema kosa hilo likijirudia Mahakama haitasita kumfutia dhamana. Wema alienda gerezani Juni 17 mwaka huu, ambapo anakabiliwa na mashtaka ya kusambaza video ya ngono katika mitandao ya kijamii kupitia simu yake ya kiganjani. Juni 11 mwaka huu  Mahakama ilitoa hati ya kumkamata Wema kwa kosa la kuruka dhamana.
1kitaifa
 WASHINGTON, MAREKANI  RAIS wa Marekani, Donald Trump amesema ni ‘’ ni heshima ‘’Marekani ina idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya corona duniani.  ‘’Ninalitazama suala hili kama heshima fulani, kama jambo zuri kwasababu inamaanisha kuwa vipimo vyetu viko vizuri,’’ alieleza akiwa Ikulu ya Marekani.  Marekani ina watu milioni 1.5 walioathiriwa na virusi vya corona na karibu vifo 92,000, kwa mujibu wa takwimu zinazokusanywa na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins.  Nchi inayoshika nafasi ya pili, ni Urusi ikiwa na maambukizi ya watu 300,000.  Jumatatu Rais ,Trump alikuwa akizungumza mkutano wake wa kwanza wa baraza la mawaziri tangu kuanza mlipuko wa virusi nchini humo.  Aliwaambia waandishi wa habari, ‘’Unajua unaposema tunaongoza kuwa na watu wengi walioambukizwa, ni kwa sababu tuna vipimo vingi kuliko mtu mwingine yeyote.  ‘Virusi vya corona vimefichua uongozi wa Trump kuwa haujui unachofanya’  Trump anakunywa ‘dawa ya corona’ isiyothibitishwa  ‘’Sijali. Ninachotaka nikupata chanjo tu inayofanya kazi”  ‘’Hivyo tuna watu wengi walioambukizwa,’’ aliendelea, ‘’Sitazami kama jambo baya, ninalitizama kwa heshima fulani, kama jambo jema kwa sababu ina maanisha kuwa tuna vipimo vizuri.’’  Aliongeza: ‘’Hivyo ninaliona kama nembo ya heshima. Kweli ni heshima.  ‘’Ni heshima kwa vipimo na kazi ambayo wataalamu wameifanya.’’  Kwa mujibu wa kituo cha kupambana na kudhibiti magonjwa , Marekani imepima watu milioni 12.6 mpaka siku ya Jumanne.  Rais Trump, alikuwa akijibu swali kuhusu kama alikuwa akifikiria kuweka marufuku ya kusafiri kwenda Amerika ya Kusini hasa Brazil. Nchi hiyo ni ya tatu kwa kuwa na idadi kubwa ya waathirika.  Kamati ya uongozi ya kitaifa ya Chama cha Democratic, imekosoa kauli ya Rais Trump, ikisema kwenye ukurasa wake wa Twitter kuwa na waathirika wa Covid-19 milioni 1.5 nchini Marekani kunaonesha ‘’kushindwa kabisa kwa uongozi’’.  Wakati Marekani, ikiwa imefanya vipimo zaidi kuliko nchi nyingine yoyote, si ya kwanza duniani kwa ulinganifu wa idadi ya watu na vifo nchini humo kwa mujibu wa takwimu za chapisho la kisayansi la Our World in Data la Chuo Kikuu cha Oxford.  Katika chati, Marekani ya 16 kwa vipimo kwa watu 1,000 ikiwa mbele ya Korea Kusini, lakini nyuma ya Iceland, New Zealand, Urusi na Canada.  Katika kipindi cha juma lililopita, Marekani imekuwa ikifanya vipimo kwa watu 300,000 na 400,000 kwa siku, kwa mujibu wa mradi uitwao Covid Tracking, zikiwa ni jitihada za watu waliojitolea.  Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Global Health, Ashish Jha wiki iliyopita aliuambia mkutano wa Congress kuwa: ‘’Marekani inahitaji vipimo zaidi ya 900,000 kila siku. Kwa sasa tuna theluthi tu ya vipimo.’’  Marekani pia imeripoti vifo vingi vinavyotokana na virusi vya corona kuliko nchi nyingine yoyote, ingawa kwa ulinganifu wa idadi ya watu na vifo Marekani ni ya sita nyuma ya Ubelgiji, Uingereza na Ufaransa kwa mujibu wa takwimu za Chuo cha Johns Hopkins 
3kimataifa
LONDON, ENGLAND UONGOZI wa timu ya Tottenham umethibitisha utaikosa huduma ya mlinda mlango wake Hugo Lloris hadi 2020 baada ya kupata tatizo la kugeuka kiwiko kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Brighton mwishoni mwa wiki iliopita. Katika mchezo huo, Tottenham ambao walikuwa ugenini walikubali kichapo cha mabao 3-0, lakini mlinda mlango huyo hakuweza kuumaliza mchezo huo kutokana na kuumia na kisha kutolewa nje. Kupitia website ya Tottenham, uongozi wa timu hiyo umedai mchezaji huyo amepata tatizo ambalo litaweza kumuweka nje ya uwanja kwa kipindi kirefu. “Hugo Lloris ataendelea kufanyiwa uchunguzi zaidi kutokana na tatizo alilolipata la kugeuka kiwiko kwenye mchezo wetu dhidi ya Brighton mwishoni mwa wiki iliopita. “Kutokana na uchunguzi wa awali mchezaji huyo anaweza hasifanyiwe upasuaji wowote kutokana na hali hiyo, lakini nahodha huyo hawezi kurudi kufanya mazoezi na timu hiyo kabla ya kumalizika kwa mwaka 2019. “Mchezaji huyo atakuwa nje huku akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari kwa kipindi chote hadi pale atakapokuwa fiti kurudi viwanjani,” waliandika Tottenham. Tottenham kwa sasa wanashika nafasi ya tisa kwenye msimamo wa Ligi wakiwa na pointi 11 baada ya kucheza michezo nane. Hata hivyo, kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps, amedai kumkosa mlinda mlango huyo ambaye alibeba taji la Kombe la Dunia mwaka jana nchini Urusi ni pigo kubwa kwake hasa kwenye michezo ya kuwania kufuzu Euro 2020 dhidi ya Iceland na Uturuki, lakini ni nafasi kwa makipa wengine kuonesha uwezo wao. “Hatokuwepo kwenye kikosi chetu, hivyo tutakuwa kwenye wakati mgumu wa kufuzu, yeye ni mchezaji muhimu sana kwetu, lakini ninaamini wachezaji waliopo wanaweza kuziba nafasi hiyo,” alisema kocha huyo.
2michezo
Na NORA DAMIAN-DAR ES SALAAM SERIKALI inapoteza dola za Marekani milioni 100 kila mwaka kutokana na kuagiza dawa kutoka nje ya nchi. Viwanda vya dawa vilivyopo nchini ni 13 tu ambapo uwezo wake wa kuzalisha ni asilimia 20 ya dawa zote zinazohitajika nchini. Hayo yalisemwa juzi na Mfamasia wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Siana Mapunjo, wakati wa mkutano wa wadau wa mradi wa kiwanda cha dawa za binadamu cha Zinga ambacho kinatarajiwa kujengwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Mapunjo alikuwa akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. “Hii ni fursa kwa Kiwanda cha Zinga kusaidia nchi kupata dawa muhimu kwa wakati na kuokoa fedha za kigeni, kuongeza ajira na kuiwezesha Tanzania ya Viwanda kufikiwa,” alisema Mapunjo. Alisema gharama hizo zinaongezeka kila mwaka na inakadiriwa ifikapo mwaka 2021 zitafikia Dola za Marekani milioni 350 kwa mwaka. Awali Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Dk. Mary Mayige, alisema ujenzi huo utagharimu zaidi ya Sh bilioni 70 na wanatarajia kutumia teknolojia za kisasa kutoka Ujerumani. "Dawa zitakazotengenezwa zitakuwa na kiwango cha juu cha ubora kuweza kushindanishwa na dawa zinazotoka kwenye soko la kimataifa," alisema Dk. Mayige. Alisema kiwanda hicho kitatengeneza dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi (ARVs), antibiotiki, malaria, kisukari, presha, magonjwa ya kuambukiza na zile za magonjwa yasiyoambukiza. Alisema uzalishaji wa dawa za binadamu nchini bado ni mdogo na upatikanaji wa dawa zinazozalishwa na viwanda vya ndani umeshuka kiwango ikilinganishwa na miaka ya nyuma.
1kitaifa
Na MAREGESI PAUL – DODOMA BOMOABOMOA inayoendelea nchini kwa wananchi waliojenga katika maeneo ya Shirika la Reli Tanzania (TRC), imewakera baadhi ya wabunge. Wabunge hao walionyesha hali hiyo bungeni jana wakati walipokuwa wakichangia Muswada wa Sheria ya Reli ya Mwaka 2017, uliowasilishwa bungeni na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa. Katika mchango wake, Mbunge wa Kaliua, Magdallena Sakaya (CUF), alionyesha kutoridhishwa na bomoabomoa hiyo kwa kuwa baadhi ya wanaovunjiwa majengo, walianza kuyamiliki miaka mingi iliyopita. Kwa upande wake, Mbunge wa Moshi Mjini, Jafary Michael (Chadema), pamoja na kulalamikia bomoabomoa hiyo, alitaka viongozi waliosababisha wananchi wakajenga katika maeneo ya reli, kuchukuliwa hatua. “Hii bomoabomoa inaumiza wananchi na kwa kuwa inaonekana baadhi ya waliojenga katika maeneo hayo walikuwa na vibali vya Serikali, basi waliotoa vibali hivyo wachukuliwe hatua kwani wamesababisha wananchi wapate hasara bila sababu,” alisema Michael. Mbunge wa Tabora Mjini, Emmanuel Mwakasaka (CCM), alisema kuna haja kwa Serikali kuangalia namna ya kuwafidia waliovunjiwa nyumba zao kwa kuwa baadhi waliuziwa viwanja na Serikali. Mbunge wa Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM), alilalamikia bomoabomoa hiyo na kusema mkoani Tabora kaya zaidi ya 500 zitavunjiwa nyumba, akiwamo kikongwe mwenye miaka zaidi ya 70 ambaye alianza kumiliki eneo lake miaka mingi iliyopita. Mbunge wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema), alisema nyumba zaidi ya 3,244 zitabomolewa na kwamba kuna haja watakaobomolewa, kulipwa fidia ili wakajenge makazi mapya. Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Lupembe (CCM), alitaka Serikali iimarishe ulinzi wa reli ili kudhibiti majangiri wanaong’oa mataluma kwa lengo la kupora mali za abiria.
1kitaifa
Na RAMADHAN LIBENANGA-MOROGORO WAFUGAJI wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro, wamesema wamekuwa wakitumia fedha nyingi kununua mihtasari ya vikao vya vijiji ili kuzionyesha mamlaka mbalimbali jinsi walivyoruhusiwa kumiliki ardhi waliyonayo. Hayo yalielezwa jana na mchungaji Joseph Sepuke, alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kibaoni wilayani Mvomero. “Wamasai wanapata mihtasari ya kijiji kwa gharama kubwa na viongozi hawa hawa wa vijiji ndio wanaowauzia hii mihtasari ili waweze kumilikishwa maeneo. “Kwa hiyo, tunaomba gharama za mihtasari hiyo zipunguzwe ili tuweze kuzipata kwa urahisi zaidi,” alisema Sepuke. Awali, akizungumza katika mkutano huo, mjumbe wa Serikali ya Kijiji cha Kibaoni, Fabian Beatus, alisema kijiji chao kimegundua kuna baadhi ya wananchi walioghushi mihtasari ya vijiji na kufanikiwa kupata ardhi. “Kuna watu wameghushi mihtasari kwa sababu sharti kuu linalomwezesha mwananchi kumiliki ardhi ni kuwa na muhtasari unaoonyesha vikao halali vya kijiji vilikaa kumjadilli na kuridhia kumpa eneo,” alisema. Akizungumza katika mkutano huo, mfugaji mwingine wa jamii ya kimasai, Songambili Mfaume, aliwatupia lawama baadhi ya viongozi wa kijiji hicho kwa kusema wamekuwa wakimfuata awape milioni mbili ili wampe muhtasari aweze kumilikishwa eneo lake. Hata hivyo, tuhuma hizo zilikanushwa na Kaimu Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Stephano Udoba ambaye alisema wamekuwa wakifuata taratibu wakati wa kuwamilikisha wananchi ardhi. Akizungumza katika mkutano huo ulioandaliwa na Mradi wa Kuendeleza Kilimo katika Safu za Milima ya Uluguru (UMADEP) unaotekelezwa chini ya usimamizi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Ofisa Miradi wa UMADEP, Pesa Kusaga, alisema SUA inashirikiana na Serikali kuhakikisha migogoro ya ardhi inamalizika mkoani Morogoro.
1kitaifa
Na Said Ameir, MAELEZO KUWAPATIA wananchi dawa zenye viwango bora, salama na ufanisi ni moja kati ya malengo makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kuimarisha afya za watu. Pamoja na lengo hilo, utekelezaji wake mbali ya kukabiliwa na chagamoto za kibajeti, changamoto nyingine kubwa ni upungufu wa wataalamu wa ukaguzi na kudhibiti ubora na usalama wa dawa. Kwa mujibu wa takwimu za miaka ya hivi karibuni, soko la dawa katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki linategemea bidhaa hiyo kutoka nje kwa kati ya asilimia 70 na 75 hivyo uzalishaji wa ndani ni kati ya asilimia 30 na 25. Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Ulisubisya Mpoki anasema Tanzania huagiza nje ya nchi asilimia 80 ya mahitaji yake ya dawa. Nchi nyingine zinazoagiza dawa nje ya nchi ni Rwanda asilimia 90, Uganda asilimia 90, Burundi asilimia 100, Zanzibar asilimia 100 na Sudan Kusini asilimia 100. Katika nchi wanachama wa Jumuiya hii, ni Kenya pekee ambayo imepiga hatua katika utengenezaji dawa ambapo takwimu zinaonesha kuwa inatengeneza karibu asilimia 25 ya mahitaji ya soko la nchi wanachama. Mbali ya Jumuiya kuwa na mpango maalumu wa muda mrefu kuwezesha nchi wanachama kutengeneza zaidi dawa kuliko kutegemea watengenezaji wa nchi za nje, lakini pia imeweka mkazo katika kuwapatia uwezo na ujuzi  wa udhibiti na ukaguzi wa viwango vya ubora na usalama wa dawa wataalamu wa nchi wanachama. Mkakati wa Jumuiya katika kujenga uwezo wa wataalamu wa nchi wanachama umejikita katika kuhakikisha dawa zinazotengenezwa katika nchi wanachama na zile zinazoingizwa toka nchi za nje zinakidhi viwango vya ubora unaotakiwa. Nchi hizo zimekubaliana kuwianisha viwango vya dawa ili dawa zinazotengenezwa na kuingizwa katika Jumuiya ziwe na viwango vinavyofanana ubora, usalama na ufanisi. Hivi karibuni, Jumuiya hiyo kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Shule ya Famasi ya Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi za Afya Muhimbili (MUHAS) waliendesha mafunzo maalumu kwa wataalamu wa udhibiti na ukaguzi wa dawa kutoka nchi wanachama. Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Kituo Mahsusi cha Kanda cha Ukaguzi na Udhibiti wa Dawa kwa Afrika Mashariki, kilichopo Chuo Kikuu cha Tiba na Sayansi ya Afya, Muhimbili yaliendeshwa kwa pamoja na wataalamu wa TFDA, MUHAS, Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) na mtaalamu mbobefu kutoka Bodi ya Dawa ya Uholanzi. Kituo hicho kilianzishwa mwaka 2014 na kuanza shughuli zake mwaka 2015 na kinaendeshwa kwa pamoja kati Jumuiya ya Afrika Mashariki, TFDA na Shule ya Phamasi ya Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili. Mafunzo hayo ni ya pili tangu kuanzishwa kwa kituo hicho ambapo mafunzo ya kwanza yalifanyika mara tu kilipoanza kufanya kazi mwaka 2015. Ni vyema kubainisha kuwa katika programu ya uwianishaji wa dawa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, TFDA ndio taasisi kiongozi ya uratibu na usajili dawa. Hii inadhihirisha uwezo mkubwa wa kitaalamu na kitaasisi ilionao TFDA katika masuala hayo katika nchi wanachama wa jumuiya. Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo anaeleza kuwa moja ya majukumu ya mamlaka za udhibiti wa dawa katika nchi wanachama ni kufanya tathmini ya dawa kabla hazijaingia katika soko kuhakikisha kuwa zinakidhi viwango vya ubora, usalama na ufanisi vilivyokubalika kisheria. “Mafunzo haya ni sehemu ya uwezeshaji wa utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka za Udhibiti na Usimamizi wa Dawa katika nchi zetu, pia ni sehemu ya mpango wa uwianishaji  wa dawa wa jumuiya ili kujenga uwezo kwenye ngazi ya nchi za ukanda huu  kwa kufanya tathmini ya maombi ya usajili wa bidhaa za dawa,” anafafanua Sillo. Akizungumzia tathmini ya mafunzo hayo, Mratibu wa Mafunzo Mhadhiri Mwandamizi na Meneja wa Maabara ya Utafiti na Maendeleo, Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili, Profesa Eliangiringa Kaale anasema yana umuhimu mkubwa katika kulinda afya ya wananchi wa Jumuia ya Afrika Mashariki. Kama takwimu za uingizaji dawa katika nchi wanachama zinavyoonesha, ni vyema kueleza kuwa kiwango hicho kikubwa cha dawa kinachoagizwa kutoka nje kinalazimu nchi wanachama kushirikiana kwa karibu kwa sheria, kanuni na viwango vinavyofanana ili ukanda wote uwe salama katika suala la dawa. Kama inavyoeleweka biashara ya dawa na vifaa tiba ni moja kati ya biashara inayonyemelewa na kushamiri kwa udanganyifu, hivyo ushirikiano wa karibu ni kitu muhimu katika udhibiti. Ukaguzi wa mipakani na ukaguzi wa mara kwa mara kwenye soko ndio utakaowalinda wananchi. Zaidi, uwezo mkubwa wa kitaalamu, rasilimali na kimiundombinu ndio silaha madhubuti kukabiliana na udanganyifu huo ambao Jumiya imekuwa ikichukua hatua kuimarisha uwezo wa wananchama wake wa usimamizi, ukaguzi na kudhibiti.
5afya