text
stringlengths
3
16.2k
T L
Tags
You can share this post!
Previous article
Samidoh ang’aa Murang’a akitishia kuzima nyota ya...
Next article
UDAKU: Jua Cali adai Tanzania haina pesa mastaa wakifurika...
T L
You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MUNGUTI MASKWOTA wapatao 10,000 wamewasilisha upya kesi katika Mahakama ya Upeo wakiomba ibatilishe uamuzi kwamba wafukuzwe kutoka kwa shamba la ukubwa wa ekari 25,000 wanalong’ang’ania umiliki wake na familia ya mwanasiasa marehemu Mark Too. Maskwota hao wanaodai mababu zao ndio waliotimuliwa kutoka kwa shamba hilo enzi za ukoloni, wanasema walipewa shamba hilo rasmi na aliyekuwa Rais hayati Daniel arap Moi, kisha Kamishna wa Ardhi M Okundu akaratibisha uamuzi huo mwaka 2007. Katika ombi lililowasilishwa na wakili William Arusei chini ya sheria za dharura, kikundi cha maskwota hao–Sirikiwa Squatters Group–kimeomba mahakama ibatilishe uamuzi huo kwa vile ilitegemea ushahidi ambao haukuwa umewasilishwa katika kesi waliyoshtaki katika Mahakama ya kuamua kesi za mashamba (ELC), Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu. Pia wameeleza bayana Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu, majaji Mohammed Ibrahim, Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Isaack Lenaola, na William Ouko walitegemea ushahidi wa Afisa wa Ugavi wa Mashamba R J Simiyu kutoa uamuzi wang’atuke shambani. Maskwota hao wamesema ushahidi wa Bw Simiyu uliowasilishwa mbele majaji hao saba kwa njia ya afidaviti ni mpya na kamwe “haukuwasilishwa mbele ya Jaji Antony Ombwayo aliposikiliza na kuamua kesi hiyo 2017.” Pia wanasema ushahidi huo haukuwasilishwa Mahakama ya Rufaa iliyosikiliza rufaa iliyowasilishwa na kampuni ya Fanikiwa, familia ya marehemu Mark Too, kampuni ya Lonrho Agribusiness (EA) Ltd, na Bw David K Korir. Hivyo basi, maskwota hao wanaeleza mahakama hii ya upeo kwamba ni kinyume cha sheria kutegemea ushahidi mpya kutoa uamuzi wa kesi hii iliyo na umuhimu mkubwa kwa umma. “Uamuzi huu wa Mahakama ya Juu wa Desemba 15, 2023, hauna mashiko kisheria na kamwe hauna nguvu kisheria kuwatimua maskwota hawa kutoka kwa shamba lao,” asema Bw Arusei. Pia maskwota hawa wanadai kwamba badala ya Mahakama ya Juu kujadili masuala ya kikatiba jinsi ilivyo jukumu lake, majaji hao walianza kufafanua na kutafsiri ushahidi wa watu binafsi na kuelezea maana ya ‘skwota’. Mahakama hii imeombwa ikague upya uamuzi iliyotoa kwa vile ilidanganywa na walalamishi na pia kutendewa ujanja. Akinukuu maamuzi ya majaji wastahiki kama vile Lord Dening, Bw Arusei amesema, mahakama ikigundua ilipotoshwa au kudanganywa na upande mmoja, iko na mamlaka na uwezo wa kufutilia mbali uamuzi iliyotoa na kuandika mwingine. Maskwota hao wanaomba Mahakama ya Juu iwarudishe shambani kama ilivyokuwa imeamuliwa na Jaji Ombwayo na Mahakama ya Rufaa. Vile vile mahakama hiyo imekosolewa kwa kumshambulia hayati Moi katika uamuzi huo pasi kutoa agizo wasimamizi wa mali yake wafike mbele yao kutoa mwanga kuhusu suala la umiliki wa shamba hili lililorudishwa kwa serikali na kampuni iliyokuwa inakuza miti inayotumika katika viwanda vya ngozi. Naibu msajili wa Mahakama ya Juu Nelly Kariuki aliwaamuru maskwota hao wawakabidhi nakala za kesi hii yao mpya wahusika wote kabla ya Januari 31, 2024, kesi itakapotajwa tena kwa maagizo zaidi. Jaji aliyesikiliza kesi hii mpya hakuiratibisha kuwa ya dharura ila aliamuru pande zote ziwasilishe ushahidi katika muda wa siku 14 kuanzia Desemba 21, 2023. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA RICHARD MAOSI WAMILIKI wa nyumba za wapangaji mtaani Kayole wameamua kulala mchana na kukaa macho usiku ili kupambana na wahalifu ambao wametawala ploti zao. Aidha wapangaji wanapoendelea kufurahia sikukuu wakiwa mashambani, wezi kwa upande mwingine wanavunja nyumba na kuiba bidhaa kutoka ploti moja hadi nyingine. Mbali na Kayole, maeneo mengine ambapo wizi umeripotiwa ni Kangemi, Korogocho, Githurai, Umoja, Kariobangi, Starehe, Syokimau, na Buruburu. Wanavunja nyumba na kuiba vyombo, fanicha, mitungi ya gesi ya kupikia, televisheni, na redio, huku hatimaye bidhaa hizo zikiuzwa kwa bei ya kutupa mtaani. Bw Gilbert Ambani ambaye ni mlinzi katika mojawapo ya ploti eneo la Syokimau, anasema wezi wengi huko katika msimu huu wa shamrashamra wanalenga vyuma chakavu kwa sababu huwapatia hela za haraka. “Baadhi ya wezi wanabomoa lango kuu na kuchukua vyuma huku wengine wakivunja mifereji,” Bw Ambani akaambia Taifa Leo. Naye Amon Andika ambaye ni landilodi mtaani Kayole, alisema kwamba imemlazimu kufanya kazi ya ziada ya kulinda nyumba za wapangaji wake ambao wengi walienda mashambani almaarufu ‘ushago’. Anasema mwaka 2023 ameamua kufanya kazi ya usoja kama wengi wanavyoiita, baada ya kubaini kuwa baadhi walinzi wake wa awali walikuwa wakishirikiana na wezi kutekeleza wizi. Bw Andika ameingia gharama ya kuwekeza upya kwenye mradi wa maji baada ya wezi kuvunja mfereji wake usiku wa Desemba 24, 2023, na kutoweka na paipu ya thamani ya Sh70,000. Anasema kwa sababu ya hali ngumu ya kiuchumi, hana uwezo wa kuajiri soja wa usiku. Ndiposa imemlazimu kuhatarisha maisha yake kwa kulinda mali mpaka ifikapo Mwaka Mpya 2024. Anasema ni desturi yake kila mwaka wapangaji wanapokuwa wameelekea ‘ushago’ kufurahia sikukuu, yeye anadumisha usalama. Mnamo Desemba 27, 2023, washukiwa 34 wa wizi walikamatwa katika eneobunge la Starehe katika operesheni iliyoongozwa na chifu na maafisa wa polisi. Hali ni kinyume na baina ya mwaka wa 2020 na 2021 ambapo wakazi wengi wa jiji waliamua kutosafiri kwa sababu ya mlipuko wa janga la Covid-19. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA KIONGOZI wa Narc-Kenya Martha Karua amesema kuwa muungano wa Azimio La Umoja-One Kenya ulitoka mikono mitupu katika mazungumzo kati yake na mrengo wa Kenya Kwanza (KKA). Kwenye mahojiano na runinga ya Citizen mnamo Alhamisi usiku, Bi Karua alidai wanachama wa Azimio katika Kamati ya Kitaifa ya Mazungumzo (Nadco) walisaidia KKA kuendeleza ajenda zao. “Kwa mtazamo wangu, mazungumzo hayo hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu hakuna muafaka uliofikiwa kuhusu ajenda zetu tatu kuu ambazo ni gharama ya maisha, haki katika uchaguzi, na heshima kwa demokrasia ya vyama vingi,” akasema Bi Karua. Akaongeza: “Muafaka ulipatikana kuhusu ajenda za Kenya Kwanza kama vile kuundwa kwa afisi ya kiongozi rasmi wa upinzani, na kuhalalishwa kwa afisi ya Mkuu wa Mawaziri, ambazo tayari Ruto alikwisha kuwasilisha bungeni.” Kiongozi huyo wa Narc Kenya alieleza kuwa vikao vya kamati ya Nadco vilivyodumu kwa miezi minane vilikuwa ni vya kuwapotezea Wakenya hela na muda kwa sababu serikali haikuongozwa na nia njema iliposhiriki mazungumzo na upinzani. “Mazungumzo hayo yalilenga kutuchezea shere na kutuliza maandamano. Matokeo ya mazungumzo yetu na utawala wa KKA hayakuzaa matunda yoyote kwa sababu Wakenya bado wanaumizwa na kupanda kwa gharama ya maisha. Kwa mtazamo wangu, ripoti ya Nadco haina maana yoyote kwa Wakenya kwa sababu haishughulikii madhila yao,” Bi Karua, ambaye alikuwa ni mgombea mwenza wa Raila Odinga katika uchaguzi wa urais wa Agosti 9, 2022, akaongeza. Alielekeza lawama kwa utawala wa Kenya Kwanza kwa kile alichodai ni kufeli kufikiwa kwa malengo ya mazungumzo yake na upinzani. “Licha ya sisi kama upinzani na wananchi kuendelea kuushinikiza utawala huu upunguze gharama ya maisha, walipuuza na badala yake kuendelea kuongeza bei ya bidhaa za kimsingi na kuanzisha aina nyingine za ushuru,” akasema. Ili mazungumzo yoyote yafaulu, kulingana na Bi Karua, chama au mrengo ulioko mamlakani ni sharti kuonyesha nia njema kwa sababu wao ndio wanasukumwa kutimiza matakwa ya wananchi. Kiongozi huyo wa Narc-Kenya aliutaja utawala wa sasa kama ambao hauheshimu sheria na maamuzi ya mahakama. “Utawala huu unaendesha majukumu ya serikali kwa namna ambayo haijeshimu sheria na kudharau maoni ya wananchi ulivyofanya wakati wa ukusanyaji maoni ya umma kuhusu Sheria ya Fedha,” akasema. “Unapodharua Katiba na watu ambao walikupa mamlaka na matakwa ya wengi, unageuka serikali mbaya,” akaeleza alipoulizwa sababu yake ya kuirejelea serikali hivyo. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA FARHIYA HUSSEIN MWAKA 2023, unyama uliokuwa ukifanywa ndani ya wa Shakahola katika Kaunti ya Kilifi, ulifichuliwa ambapo zaidi ya watu 400 walipoteza maisha yao kwa itikadi kali za kidini. Mhubiri Paul Mackenzie ambaye alitajwa kuwa kiongozi wa wafuasi wake, anachunguzwa kwa madai ya kuwapotosha katika mafundisho ya kidini ambapo waumini walichanganyikiwa, wakiwemo watoto, wakaanza kufunga au kususia chakula hadi wakaanza kudhoofika na hatimaye kuanza kuaga dunia mmoja baada ya mwingine. Habari hizo zilipofahamika, idadi hii ya watu waliopoteza maisha ilikuwa nyingi sana, jambo liloshangazaa ulimwengu mzima. Walionusurika waliozungumza na Taifa Leo alisema waliokufa waliambiwa wafunge hadi kufa ili wakutane na ‘Yesu’. Miezi tisa baadaye, miili zaidi ya 400 inaendelea kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha muda katika Kaunti ya Kilifi, ukumbusho wa kusikitisha kuashiria msimamo wao mkali wa kidini waliofuatilia. Watu hawa, ambao walitajwa na jamaa zao kuwa watu wachangamfu na maisha hapo awali walionekana kuishi maisha ya kudhoofisha na ya hali ya kusikitisha, maisha yao yalikatishwa na imani zile walizofuatilia kwa kina. Msitu huo ambao hapo awali ulikuwa sehemu nzuri ya mandhari ya kiasili, sasa umekuwa shahidi kwa ukatili uliofanywa huko ndani. Shakahola, kijiji katika Kaunti ya Kilifi, kilikuwa kimegubikwa na ukimya wa kutisha kwa miezi kadhaa. Makazi hayo ambayo wanakijiji walitaja zamani yalikuwa ya uchangamfu na yenye shughuli nyingi, sasa yalionekana yametawaliwa na ukimya mkuu. Katika msitu huo wa Shakahola, nyumba zilikuwa za udongo huku zikiezekwa kwa mapaa ya makuti. Njia zilizokuwa na watu wengi sasa zilikuwa kimya kwa kutisha, kana kwamba wanakijiji walikuwa wametoweka wakiacha nyuma vitu vya kibinafsi kama vile Biblia, ushahidi kuwa waliondoka ghafla. Sahani zilizotelekezwa zilizofunikwa ziliashiria ‘mlo wa mwisho’ wa wafuasi wa Kanisa la Good News International la Mchungaji Paul Mackenzie, ambalo inadaiwa lilichochea wao kuchukua mkondo hatari wa kufunga hadi kufa. Katika mazingira haya ya kutatanisha, ambapo ibada inayodhaniwa ilikuwa imezama katika unabii wa apocalyptic, cha kusikitisha ni kwamba baadhi yao hawakunusurika katika safari ya kuenda katika Hospitali Kuu ya Malindi. Wahanga walizikwa bila mpangilio makaburi yao yakiashiria kuzikwa kwao kwa haraka. Miezi kadhaa baadaye, miili yao ilifukuliwa. Watu hawa walionekana kutengwa na kusukumwa kwenye ukingo wa jamii, sauti zao zikiwa zimenyamazishwa na nguvu za itikadi kali. Maisha yao yalipochukuliwa kwa uchungu, heshima waliyostahili katika umauti wa iliondolewa pia. Ni wale tu walioaga dunia wangejua ikiwa kweli walikutana na Mungu wao. Miili yao ilizikwa kwa haraka msituni Shakahola, jambo lililodhihirishwa na jinsi makaburi hayo yalivyofukuliwa ambapo kwa kila mojawapo, miili zaidi ya mmoja ilipatikana ndani. Waumini hao hawakuzikwa na sanduku kama ilivyo kwa Wakristo bali walifunikwa na blanketi na nguzo nyinginezo. Miezi tisa baadaye, chumba cha kuhifadhia maiti cha muda bado kimesalia katika hopsitali ya Malindi, ukumbusho wa mkasa uliotokea mwaka 2023. Waathiriwa wamesalia katika hali ya kutatanisha, utambulisho wao bado haujathibitishwa, hadithi zao kubaini kiini cha kilichotokea ndani ya msitu wa Shakahola bado haijabainika. Hata katika kifo, ibada iliwanyima utambulisho wao, na kuacha miili hiyo ‘haijulikani’ kutokana na ukosefu wa nyaraka zozote. Ukweli uligundulika ni kwamba baadhi ya wanachama hao walitoka kaunti za mbali katika mikoa mingine nchini, jambo la kutatanisha katika kutambua na kudai miili hiyo. Mwezi Mei, serikali ilianzisha mpango wa DNA kulenga familia zinazoshuku kuwa jamaa zao waliopotea au walioaga wanaweza kuhusishwa na msitu wa Kilifi’ Shakahola. Takriban miezi saba imepita tangu kuzinduliwa kwake, lakini familia zinalalmikia kungoja matokeo ya DNA kwa hamu. Miongoni mwa walioathiriwa ni Bw Rodgers Mwibo, ambaye anatafuta mama yake, dada yake, na mpwa wake amabye alisema ni wafuasi waaminifu wa mhubiri Paul Mackenzie kutoka Kanisa la Good News International, waliohamia kwenye msitu huo mwaka mmoja uliopita. Akielezea masikitiko yake, Bw Mwibo alieleza kuwa kufuatia tangazo la serikali, alitoa sampuli zake za DNA kaunti za Nairobi na Malindi. “Badala ya kupata faraja, huku kusubiri kwa muda mrefu kunazidisha kiwewe changu. Kila nikiona picha ya mama yangu, natamani sana uwepo wake, hata kama ni kumuaga tu,” alilalamika Bw Mwibo huku akihoji ufanisi wa taratibu za DNA za serikali. Kulingana na Bw Mwibo, uhakikisho ulitolewa kwamba matokeo yatatolewa mara moja baada ya ukusanyaji wa DNA. Hata hivyo, kile kilichoahidiwa kuwa kipindi kifupi kimeongezeka hadi mwaka mmoja, na kumuacha yeye na wengine katika hali ya huzuni ya kihisia moyo. “Ni katika nchi gani miili hubaki kuhifadhiwa kwenye friji huku familia zikistahimili uchungu huu?” aliuliza Bw Mwibo. Jamaa mwingine, Bi Mary Mwikali anabainisha kuwa hatajua iwapo dadake na mpwa wake ni miongoni mwa waliofukuliwa kutoka msitu wa Shakahola au la. Kusubiri kwa hamu kunaendelea, na kuwaacha wakihangaika na sintofahamu ikiwa wapendwa wao bado wako hai au ni miongoni mwa watu 400 na zaidi wakiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Malindi. Afisa wa Masuala ya Dharura katika Shirika la Haki Africa, Bw Mathias Shipeta, alisema wasiwasi wake ni kwamba serikali imechukua muda mrefu unaohitajika ili kulinganisha na kulinganua DNA. “Inachukua muda gani hadi ulinganishaji wa DNA ukamilike? Familia zinamaliza mwaka bila kujua jamaa zao waliko. Haijafahamika wazi kama wameaga dunia au wapo hai. Ili kulifunga suala hili, ulinganishaji wa DNA lazima ukamilike na kukamilika kwa wakati kabla ya mwisho wa mwaka,” Bw Shipeta alisisitiza. Mwezi Julai, sampuli 266 zilikusanywa kwa madhumuni ya utambulisho wa vinasaba DNA. Uchunguzi wa DNA ni ulinganifu wa kisayansi wa maelezo ya kinasaba ya watu wasiojulikana au waliokufa na yale ya watu waliotambuliwa (waliokufa au walio hai). Mchakato huo ni muhimu kwa sababu za kisheria na za kibinadamu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MASHABIKI wa klabu ya Arsenal mjini Murang’a sasa wameonywa na wenzao wa Manchester United na Chelsea wajiandae kumpokea ndovu wao akianguka pasipo hiari kutoka juu ya mti kumaanisha kushuka katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL). “Huku kulimwa ambako mmeanza kulimwa ni mwanzo tu wa namna ambavyo mambo yatakuwa magumu kwenu katika mzunguko wa pili,” akafoka Bw David Njuguna ambaye ni mshirikishi wa the Red Devils mjini humo. Cheo chake hakitambuliki rasmi na klabu ya Manchester United. Bw Njuguna alisema kwamba Arsenal kuwa juu ya jedwali hata kwa mwanya wa pointi 10 sio tishio kwa kuwa katika mkondo wa lala salama, wao huwa butu, wasio na maono na mwelekeo na lazima wajihujumu wao wenyewe kama ilivyokuwa msimu jana. Katika mechi ya usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, Arsenal walirambishwa magoli 2-0 na West Ham. “Hata hamna heshima na wawekezajj na mnatuchomea beti. Kwa kuwa sikuamini kabisa mngeshinda hicho kipute, nilikuwa nimebashiri timu zote mbili angalau zingejipa goli. Sasa ona hamkufunga hata la kukataliwa,” akafoka Stacy Keach, mfuasi wa Chelsea. Janga hilo kwa wanabunduki Arsenal limewaacha katika nafasi ya pili kwenye jedwali wakiwa na pointi 40 huku Liverpool ikibakia kidedea kwa pointi 42. Hii ina maana kwamba Man City ambayo iko na pointi 37 kwa sasa lakini ikiwa imecheza mechi 18 Arsenal ikiwa imecheza mara 19 itaifurusha kutoka nafasi hiyo ya pili iwapo itachapa Sheffield United hapo Jumamosi kwa ubora wa magoli. “Kuna uwezekano mkubwa kwamba Arsenal itaingia mwaka Mpya ikiwa nambari tano nyuma ya Liverpool, Man City, Aston Villa na Tottenham na kabla ya tufike mechi ya 27, hata West Ham, Man United… watakuwa mbele ya Arsenal,” akasema Junita Kasyoki ambaye anashabikia Man United. Ni usiku ambao wafuasi wa Arsenal hawakujibu mipigo, waliondoka polepole na kimyakimya kutoka kwa mkahawa wa Green Park ambapo wengi walikuwa wakifuatilia mtanange huo ulioanza saa tano na robo usiku. “Lakini hata hivyo kushindwa kwetu kulisaidia West Ham kuruka Man United katika jedwali. Tungeshinda mchuano huo Man U wangebakia nafasi ya sita lakini kung’atwa kwetu kulisaidia Mashetani Wekundu kuteremka hadi nafasi ya saba,” akajituliza Bw Simon Ngonjo. Kwa sasa, maombi ya Arsenal ni kuzuke mikosi ya kushindwa kwa timu zote zilizo katika kumi bora katika mechi ya 20 lakini wao washinde ndipo warejee juu ya jedwali na presha ya kutwaa ligi ipungue. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MWANAMUME mmoja wa umri wa miaka 33 aliuawa usiku wa kuamkia Desemba 29, 2023, kwa kupigwa na majirani wa wakwe zake baada ya kile kinadaiwa alijaribu kutekeleza mauaji katika boma hilo alimokuwa amelala na bibi yake. David Kimani alikuwa amesafiri kutoka kijiji cha Kiunyu kilichoko eneobunge la Gatanga kwa msingi kwamba alikuwa na nia ya kumuona mkewe waliyetengana, binti yake wa umri wa miaka sita na pia mama mkwe. Mwanamume huyo alikuwa ametengana na Bi Esther Nyawira, 28, kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu na katika shamrashamra za msimu huu wa sherehe, akafika kwa boma la wakwe Desemba 28, 2023, katika kijiji cha Mung’etho kilichoko eneobunge la Maragua, akisema alienda kuwajulia hali. Lakini hata baada ya giza kuingia, hakuonyesha nia ya kuondoka arejee kwao na ndipo akakubaliwa alale kwa nyumba ya mama mkwe akiwa na bibi huyo wake. Mwendo wa saa sita usiku, Kimani anasemwa kwamba aliamka na akatwaa kisu na akaanza kumshambulia bibi yake aliyekuwa amelala huku kwa sauti akiapa kumuua na kisha aue mama mkwe na pia mtoto. Kwa mujibu wa Kaimu Naibu Kamishna wa Murang’a Kusini Bw Joshua Okello, mwanamume huyo baada ya kujaribu mara kadha warejeane na bibi yake pasipo mafanikio, akaamua kufika katika boma hilo akijipamba kama malaika wa mauti. Aliongeza kwamba mshukiwa alimdunga mwanamke huyo visu vitano “mara moja umbavuni upande wa kulia na mara nne kwa mkono wa kulia, majeraha yote yakiwa matano”. Bw Okello aliongeza kwamba sauti za juu za mwanamume huyo zilimwamusha mama mkwe na alipiga nduru ambayo iliwavutia majirani waliofurika katika boma hilo huku mvamizi baada ya kuingiwa na taharuki akitimua mbio hadi nje ya nyumba na akaingia katika kichaka. “Huku mwaathiriwa akikimbizwa hadi hospitali ya Murang’a kutibiwa, majirani nao walizindua msako ulioishia kumnasa Bw Kimani akiwa amejikunyata ndani ya kichaka hicho na wakamuua kwa kumpiga kwa vifaa butu,” akasema Bw Okello. Afisa huyo aliongeza kwamba ndani ya mkoba ambao marehemu alikuwa nao kulikuwa na sumu ya kuua wadudu kwa mimea na pia waraka wa mauti unaoaminika ulikuwa umeandikwa na mwanamume huyo. “Alikuwa amefichua katika waraka huo kwamba alinuia kuua mama mkwe, bibi yake na mtoto wake wa kike aliyekuwa akiishi kwa wakwe hao na kisha yeye mwenyewe ajitoe uhai,” akasema. Mwanamume huyo alikuwa aidha ameteta kwamba mama mkwe ndiye alikuwa kizingiti cha ndoa yake kupata uthabiti na kwa kuwa hakuwa na nia ya kumpenda mwingine, akaafikia uamuzi wa kuwaua watatu hao na kisha naye ajitume kuzimu akome mahangaiko ya mapenzi. Bw Okello alisema kwamba “huu ni mkasa ambao ungeepukika iwapo mwanamume huyo ambaye alikuwa mfanyabiashara Jijini Nairobi angepata ushauri nasaha ili kuwajibika changamoto zake za kimapenzi ndani ya mashauriano”. Alisema kwamba “ndipo ifike kiwango hicho cha kupanga mauaji ni kumaanisha alikuwa akisaka mbinu ya kusuluhisha changamoto hiyo lakini akaamua kufuata ushawishi wa pepo mbaya kujipa afueni”. Huku akiwakemea waliomuua mwanamume huyo na kuahidi uchunguzi wa kunasa washukiwa, Bw Okello alisema “hata jamii inafaa kuwa macho kuwatambua wanaoonekana kusombwa na mawazo na usaidizi wa ushauri usakwe kabla ya vishawishi vya janga kuzuka”. Bw Okello alionya watu wa kijiji hicho cha Mung’etho kwamba “kwa sasa mnaweza kuwa mnasherehekea mkisema eti ni umati wa raia uliotekeleza mauaji hayo lakini wakati kutajitokeza shahidi aseme alikuona wewe ukishiriki mauaji hayo ndipo utajua ni watu binafsi wala si kundi ambalo huvunja sheria”. “Mchango wa raia katika kuimarisha usalama ni kupitia kutupasha habari kuhusu washukiwa na visa na wakimnasa mshukiwa, kazi yao inafaa tu kutuita tumtie mbaroni au wamwasilishe katika kituo cha polisi kilicho karibu,” akasema Bw Okello. Mwili wa marehemu ulipelekwa hadi mochari ya Murang’a. [email protected] You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MUSTAKABALI wa Kanisa Katoliki uko kwenye njia panda barani Afrika, kufuatia agizo la Papa Francis kwa mapadre katika kanisa hilo kubariki wapenzi wa jinsia moja. Ingawa lengo kuu la agizo hilo linaonekana kama njia ya kuwavutia washiriki zaidi na kutowabagua watu hao, wachambuzi na wasomi wa masuala ya dini wanasema huenda agizo hilo lilitolewa bila Papa kupewa ushauri wa kina na uongozi wa kanisa hilo. Kanisa Katoliki lina mamilioni ya washiriki hapa Kenya na barani Afrika kwa jumla. Kulingana na takwimu kutoka kwa serikali, kanisa hilo ndilo linaloongoza kwa kuwa na washiriki wengi nchini, huku likifuatwa na makanisa ya Kiprotestanti. Tangu Papa Francis alipotoa agizo hilo, viongozi tofauti wa kanisa wameeleza na kutoa hisia tofauti,  baadhi wakijitokeza wazi kulipinga. Baadhi ya viongozi wakuu ambao wamejitokeza kulipinga ni kiongozi wa kanisa hilo nchini, Askofu Philip Anyolo, ambaye pia ndiye Askofu Mkuu katika Dayosisi ya Nairobi. Kulingana na askofu huyo, agizo hilo linakinzana vikali na tamaduni za Kiafrika, hivyo hawataliruhusu. “Kiafrika, ndoa za jinsia moja hazikubaliki hata kidogo. Ndoa hizo pia zinaenda kinyume na mafunzo ya Biblia,” akasema Askofu Anyolo. Maaskofu wengine ambao wamejitokeza wazi kupinga agizo hilo ni Cornelius Odiwa wa Homa Bay na mwenzake wa dayosisi ya Eldoret, Askofu Dominic Kimengich. Askofu Odiwa alisema watafuata msimamo wa Askofu Anyolo, kwani ndiye kiongozi wa kanisa hilo nchini. Pia, alisema ndoa hizo hazikubaliki kabisa Kiafrika. Kando na viongozi wa Kanisa Katoliki, watu kutoka dini nyingine pia wameunga mkono pingamizi hizo. Baadhi yao ni Bw Samuel Kamitha, ambaye ni mwanahistoria na msomi wa masuala ya dini. Bw Kamitha pia ni mmoja wa waandalizi wakuu wa maombi maalum ambayo hufanyika Desemba 27 kila mwaka karibu na Mlima Kenya. Mnamo Jumatano, wakati wa maombi hayo, Bw Kamitha alisema hawatakubali hata kidogo tamaduni za kigeni kutumika kuharibu desturi asilia za Kiafrika. “Tunasimama kidete kupinga uhalalishaji wa ndoa za jinsia moja nchini. Hilo ni jambo linalokinzana kabisa na tamaduni zetu,” akasema. Maombi hayo yalihudhuriwa na Wakristo, Waislamu, watu wanaofuata dini za kitamaduni kati ya madhehebu mengine. Kutokana na hisia hizo, wasomi wa masuala ya dini wanasema kuwa mwelekeo huo mpya unafaa kuufungua macho uongozi wa Kanisa Katoliki kuhusu mustakabali wake barani Afrika. “Kikawaida, maagizo yote kutoka Vatican (makao makuu ya Kanisa Katoliki) huwa hayapingwi hata kidogo. Ni vigumu kusikia usemi au agizo la Papa likikosolewa au kupingwa. Hata hivyo, viongozi kadhaa wanapojitokeza wazi kupinga agizo lake, basi hiyo ni ishara wazi kuwa kuna tatizo kubwa ambalo lazima litatuliwe,” asema Dkt Rita Khamisi, ambaye ni msomi wa historia ya dini. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Fans Follow Us Subscriber © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU JUMLA ya watu 4,139 walifariki kutokana na ajali za barabarani mwaka 2023, imesema Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani (NTSA). Mnamo Jumapili, Desemba 24, 2023, mamlaka hiyo ilisema kuwa idadi hiyo ilipungua kiasi ikilinganishwa na mwaka 2022, kwani ni watu 4,517 waliofariki kutokana na ajali. Kwenye takwimu ilizotoa kuhusu hali ya usalama barabarani mwaka 2023, mamlaka hiyo ilisema kuwa kijumla, watu 21,684 walihusika kwenye ajali. Watu 10,201 walipata majeraha mabaya huku 7,344 wakipata majeraha madogo madogo. Idadi hiyo ni ongezeko kubwa ikilinganishwa na mwaka 2022, kwani watu 8,495 ndio walipata majeraha mabaya, huku watu 6, 841 wakipata majeraha madogo madogo. Kulingana na takwimu hizo, idadi kubwa ya watu waliofariki ni watembeaji wa miguu, wakifuatwa na wahudumu wa bodaboda. Jumla ya watembeaji wa miguu 1,506 walifariki mwaka 2023, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo ni watembeaji miguu 1,620 waliofariki. Wahudumu 1,096 wa bodaboda walifariki mwaka 2023, idadi hiyo ikiwa chache ikilinganishwa na mwaka 2022, ambapo ni wahudumu 1,209 waliofariki. Abiria 709 walifariki katika muda huo, idadi hiyo ikipungua kutoka mwaka uliopita, kwani ni abiria 800 waliofariki. Madereva wapatao 369 ndio waliofariki, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo jumla ya madereva 408 walifariki. Waendeshaji baiskeli 85 walifariki mwaka 2023, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo ni waendeshaji baiskeli 58 waliofariki. Mamlaka hiyo imetangaza kuzindua mpango kabambe wa kupunguza idadi ya ajali hasa msimu huu wa sikukuu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU JUMLA ya watu 4,139 walifariki kutokana na ajali za barabarani mwaka 2023, imesema Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani (NTSA). Mnamo Jumapili, Desemba 24, 2023, mamlaka hiyo ilisema kuwa idadi hiyo ilipungua kiasi ikilinganishwa na mwaka 2022, kwani ni watu 4,517 waliofariki kutokana na ajali. Kwenye takwimu ilizotoa kuhusu hali ya usalama barabarani mwaka 2023, mamlaka hiyo ilisema kuwa kijumla, watu 21,684 walihusika kwenye ajali. Watu 10,201 walipata majeraha mabaya huku 7,344 wakipata majeraha madogo madogo. Idadi hiyo ni ongezeko kubwa ikilinganishwa na mwaka 2022, kwani watu 8,495 ndio walipata majeraha mabaya, huku watu 6, 841 wakipata majeraha madogo madogo. Kulingana na takwimu hizo, idadi kubwa ya watu waliofariki ni watembeaji wa miguu, wakifuatwa na wahudumu wa bodaboda. Jumla ya watembeaji wa miguu 1,506 walifariki mwaka 2023, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo ni watembeaji miguu 1,620 waliofariki. Wahudumu 1,096 wa bodaboda walifariki mwaka 2023, idadi hiyo ikiwa chache ikilinganishwa na mwaka 2022, ambapo ni wahudumu 1,209 waliofariki. Abiria 709 walifariki katika muda huo, idadi hiyo ikipungua kutoka mwaka uliopita, kwani ni abiria 800 waliofariki. Madereva wapatao 369 ndio waliofariki, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo jumla ya madereva 408 walifariki. Waendeshaji baiskeli 85 walifariki mwaka 2023, ikilinganishwa na mwaka uliopita, ambapo ni waendeshaji baiskeli 58 waliofariki. Mamlaka hiyo imetangaza kuzindua mpango kabambe wa kupunguza idadi ya ajali hasa msimu huu wa sikukuu. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MWANAJESHI alitiwa mbaroni Jumamosi akiwa na mpenzi wake wa kike kwa madai ya kumwibia mkazi wa Kirinyaga bastola yake ikiwa na risasi 14. Maafisa takriban 20 wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) walijitahidi kadri ya uwezo wao kumtia mbaroni afisa huyo ambaye majukumu yake ni ya kulinda mipaka ya nchi dhidi ya uvamizi wa wahalifu na magaidi wa kigeni. “Mimi nilikuwa nikiendesha gari langu nikielekea kwetu Murang’a kwa sikukuu ya Krismasi lakini kufika Chai, viungani mwa Juja, nilishuhudia maafisa hao karibu 20 wakijitahidi kumkamata mwanajeshi mmoja. Ni kama walichukua tahadhari kuu wakifahamu kwamba ni mtu mwenye weledi mkubwa wa kutumia silaha,” akasema Bi Charity Wambui. Baadaye, makao makuu ya DCI  yalitoa taarifa rasmi kusema kwamba maafisa hao walikuwa na habari za ujasusi kwamba mwanajeshi huyo kwa jina Sajenti William Kabuu Wageni, 54, alikuwa mshukiwa wa ujambazi. “Maafisa wetu kutoka vitengo mbalimbali walimfumania akiwa na mpenzi wake, Bi Salome Kimani, pamoja na kijana Benson Wanjau Wakiai,25, wakawakamata na kisha wakawasafirisha hadi katika kituo cha polisi cha Wang’uru ambapo malalamishi dhidi yao yalikuwa yameandikishwa,” taarifa hiyo ikasema. Walisemekana kwamba waliiba bunduki aina ya CZ ikiwa na risasi 14 mnamo Novemba 25, 2023, lakini baada ya uchunguzi, ikapatikana kwa afisa huyo wa KDF ikiwa na risasi nane, kumaanisha tayari sita zilikuwa zimetumika kwa njia ambayo itabainika katika mahojiano na washukiwa. Kwa sasa, mwanajeshi huyo pamoja na washirika wake wawili watakaa ndani hadi Desemba 27, 2023, ambapo harakati za mahakama zitarejea kutoka likizo ya Krismasi na Boxing Dei. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MWANGI MUIRURI MWANAJESHI alitiwa mbaroni Jumamosi akiwa na mpenzi wake wa kike kwa madai ya kumwibia mkazi wa Kirinyaga bastola yake ikiwa na risasi 14. Maafisa takriban 20 wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) walijitahidi kadri ya uwezo wao kumtia mbaroni afisa huyo ambaye majukumu yake ni ya kulinda mipaka ya nchi dhidi ya uvamizi wa wahalifu na magaidi wa kigeni. “Mimi nilikuwa nikiendesha gari langu nikielekea kwetu Murang’a kwa sikukuu ya Krismasi lakini kufika Chai, viungani mwa Juja, nilishuhudia maafisa hao karibu 20 wakijitahidi kumkamata mwanajeshi mmoja. Ni kama walichukua tahadhari kuu wakifahamu kwamba ni mtu mwenye weledi mkubwa wa kutumia silaha,” akasema Bi Charity Wambui. Baadaye, makao makuu ya DCI  yalitoa taarifa rasmi kusema kwamba maafisa hao walikuwa na habari za ujasusi kwamba mwanajeshi huyo kwa jina Sajenti William Kabuu Wageni, 54, alikuwa mshukiwa wa ujambazi. “Maafisa wetu kutoka vitengo mbalimbali walimfumania akiwa na mpenzi wake, Bi Salome Kimani, pamoja na kijana Benson Wanjau Wakiai,25, wakawakamata na kisha wakawasafirisha hadi katika kituo cha polisi cha Wang’uru ambapo malalamishi dhidi yao yalikuwa yameandikishwa,” taarifa hiyo ikasema. Walisemekana kwamba waliiba bunduki aina ya CZ ikiwa na risasi 14 mnamo Novemba 25, 2023, lakini baada ya uchunguzi, ikapatikana kwa afisa huyo wa KDF ikiwa na risasi nane, kumaanisha tayari sita zilikuwa zimetumika kwa njia ambayo itabainika katika mahojiano na washukiwa. Kwa sasa, mwanajeshi huyo pamoja na washirika wake wawili watakaa ndani hadi Desemba 27, 2023, ambapo harakati za mahakama zitarejea kutoka likizo ya Krismasi na Boxing Dei. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MBUNGE Mwakilishi wa Nairobi Esther Passaris amewataka wazazi kuwapa watoto wao mafunzo kuhusu masuala ya ngono katika msimu huu wa sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya. Kupitia video aliyopakia kwenye ukurasa wake rasmi wa X, zamani Twitter Jumamosi, Desemba 23,2023, Bi Passaris anasema mafunzo kama hayo yatawazuia watoto wa kike kupata uja uzito na hata magonjwa ya zinaa. “Ni muhimu kwako ewe mzazi kumpa mtoto wako elimu ya ngono wakati huu wa msimu wa sherehe kwani ni muhimu na itawakinga dhidi ya mimba za mapema na maradhi ya zinaa,” “Enyi akina mama, msione haya kuzungumza masuala ya ngono na mabinti zenu, msisema elimu ya ngono inakwenda kinyume na mila na tamaduni za Kiafrika,” Bi Passari akaeleza. Mbunge huyo, anayehudumu muhula wa pili, alieleza kusikitishwa kwake na data zinazoonyesha wasichana 300,000 wenye umri wa chini ya miaka 15 walipata uja uzito 2020 wakati wa janga la Covid-19 kwa sababu walisalia nyumbani kwa muda mrefu. Serikali, kupitia Wizara ya Elimu, iliamuru kufungwa kwa shule zote kwa miezi tisa ili kuzuia kuenea kwa virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa huo. Wakati wa likizo ya mwaka huu wa 2023, shule zimefungwa kwa muda wa miezi miwili, kuanzia Novemba 8, 2023 hadi Januari 8, 2024.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MBUNGE Mwakilishi wa Nairobi Esther Passaris amewataka wazazi kuwapa watoto wao mafunzo kuhusu masuala ya ngono katika msimu huu wa sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya. Kupitia video aliyopakia kwenye ukurasa wake rasmi wa X, zamani Twitter Jumamosi, Desemba 23,2023, Bi Passaris anasema mafunzo kama hayo yatawazuia watoto wa kike kupata uja uzito na hata magonjwa ya zinaa. “Ni muhimu kwako ewe mzazi kumpa mtoto wako elimu ya ngono wakati huu wa msimu wa sherehe kwani ni muhimu na itawakinga dhidi ya mimba za mapema na maradhi ya zinaa,” “Enyi akina mama, msione haya kuzungumza masuala ya ngono na mabinti zenu, msisema elimu ya ngono inakwenda kinyume na mila na tamaduni za Kiafrika,” Bi Passari akaeleza. Mbunge huyo, anayehudumu muhula wa pili, alieleza kusikitishwa kwake na data zinazoonyesha wasichana 300,000 wenye umri wa chini ya miaka 15 walipata uja uzito 2020 wakati wa janga la Covid-19 kwa sababu walisalia nyumbani kwa muda mrefu. Serikali, kupitia Wizara ya Elimu, iliamuru kufungwa kwa shule zote kwa miezi tisa ili kuzuia kuenea kwa virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa huo. Wakati wa likizo ya mwaka huu wa 2023, shule zimefungwa kwa muda wa miezi miwili, kuanzia Novemba 8, 2023 hadi Januari 8, 2024.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MKENYA Monica Bene Mutumi ni miongoni mwa wanaharakati wa haki za kibinadamu waliotuzwa na shirika moja la kupigania haki, umoja na amani Afrika kwa kutumia sanaa kutetea haki za wanyonge katika jamii. Bi Mutumi, ambaye ni mshairi, alitawazwa mshindi katika kitengo cha Msanii Mwanaharakati wa Mwaka wa 2023 katika tuzo za Africa Rising Activism Awards zinazodhaminiwa na shirika la Africa Rising Movement. “Kupitia ushairi, msanii huyo, maarufu kama Bene3, huburudisha na kufunza jamii kuhusu masuala kama ukatili wa polisi, dhuluma za kijinsia, siasa na afya ya akili katika mtaa wa mabanda ya Mukuru, Nairobi,” mshirikishi wa shirika hilo, Hardi Yakubu, alisema wakati wa kutangazwa kwa washindi katika vitengo vitatu vya tuzo hiyo. Makao Shirika la Africa Rising lenye makao yake nchini Gambia, lilianzishwa 2017 na kuendeleza juhudi za kutetea umoja, haki, amani na heshima ya Waafrika kupitia uanaharakati. Kundi la wasanii vijana la Wahenga Youth Group, kutoka mtaa wa Kayole, Nairobi, lilitwaa nafasi ya pili katika kategoria ya tuzo ya Movement of the Year (Vuguvugu Bora la Mwaka). Hii ni kutokana na weledi wao katika kutumia sanaa ya uigizaji kama njia mojawapo kukabiliana na visa vya uvunjaji wa haki katika jamii. “Mwaka huu washindi katika kila kitengo watapokea dola 1, 000 za Amerika (Sh152, 000) ilhali nambari mbili na tatu watapokezwa dola 500 (Sh76, 000) na dola 300 (Sh45, 600), mtawalia,” Bw Yakubu akasema. Hii ni kando na taji, nafasi ya kushiriki mipango ya Africa Rising na vitabu vya kumbukumbu. Wengine waliotuzwa ni Joseph Tsongo kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC) aliyeibuka wa kwanza katika kitengo cha Mwanaharakati wa Mwaka na kundi la Centre Badilika kutoka nchi hiyo hiyo, lililoibuka nambari ya kwanza katika kitengo cha Vuguvugu la Mwaka.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA CHARLES WASONGA MKENYA Monica Bene Mutumi ni miongoni mwa wanaharakati wa haki za kibinadamu waliotuzwa na shirika moja la kupigania haki, umoja na amani Afrika kwa kutumia sanaa kutetea haki za wanyonge katika jamii. Bi Mutumi, ambaye ni mshairi, alitawazwa mshindi katika kitengo cha Msanii Mwanaharakati wa Mwaka wa 2023 katika tuzo za Africa Rising Activism Awards zinazodhaminiwa na shirika la Africa Rising Movement. “Kupitia ushairi, msanii huyo, maarufu kama Bene3, huburudisha na kufunza jamii kuhusu masuala kama ukatili wa polisi, dhuluma za kijinsia, siasa na afya ya akili katika mtaa wa mabanda ya Mukuru, Nairobi,” mshirikishi wa shirika hilo, Hardi Yakubu, alisema wakati wa kutangazwa kwa washindi katika vitengo vitatu vya tuzo hiyo. Makao Shirika la Africa Rising lenye makao yake nchini Gambia, lilianzishwa 2017 na kuendeleza juhudi za kutetea umoja, haki, amani na heshima ya Waafrika kupitia uanaharakati. Kundi la wasanii vijana la Wahenga Youth Group, kutoka mtaa wa Kayole, Nairobi, lilitwaa nafasi ya pili katika kategoria ya tuzo ya Movement of the Year (Vuguvugu Bora la Mwaka). Hii ni kutokana na weledi wao katika kutumia sanaa ya uigizaji kama njia mojawapo kukabiliana na visa vya uvunjaji wa haki katika jamii. “Mwaka huu washindi katika kila kitengo watapokea dola 1, 000 za Amerika (Sh152, 000) ilhali nambari mbili na tatu watapokezwa dola 500 (Sh76, 000) na dola 300 (Sh45, 600), mtawalia,” Bw Yakubu akasema. Hii ni kando na taji, nafasi ya kushiriki mipango ya Africa Rising na vitabu vya kumbukumbu. Wengine waliotuzwa ni Joseph Tsongo kutoka Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC) aliyeibuka wa kwanza katika kitengo cha Mwanaharakati wa Mwaka na kundi la Centre Badilika kutoka nchi hiyo hiyo, lililoibuka nambari ya kwanza katika kitengo cha Vuguvugu la Mwaka.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA ERIC MATARA MADUKA makubwa Nakuru yamefurika huku wakazi katika eneo hilo waking’ang’ana kununua bidhaa za kutumia siku ya Krismasi. Baadhi ya maeneo ya kuegesha magari pia yalikuwa yamejaa. Uchunguzi uliofanywa na Taifa Leo Dijitali ulibaini kuwa bei za bidhaa katika maduka mengi zimepunguzwa ili kuvutia wateja wengi zaidi. Maduka makubwa kama vile Naivas, Woolmart, Cleanshelf na Gilanis sasa yanatoa ofa za chini ili kuvutia wateja. Baadhi ya bidhaa ambazo kwa sasa zinauzwa bei ya chini ni mafuta ya kupikia, sukari, unga wa ugali, unga wa ngano, maziwa miongoni mwa zingine zinazotafutwa sana-msimu huu wa sikukuu. Kwa mfano, katika duka kuu la Naivas, pakiti ya mililita 500 ya maziwa ya Brookside ambayo imekuwa ikiuzwa Sh 61 sasa inauzwa Sh 55. Unga wa ugali kilo mbili Naivas inauzwa kati ya Sh135 na Sh180 kulingana na chapa. Ofa hizo zinalenga kuwapunguzia mzigo wananchi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA ERIC MATARA MADUKA makubwa Nakuru yamefurika huku wakazi katika eneo hilo waking’ang’ana kununua bidhaa za kutumia siku ya Krismasi. Baadhi ya maeneo ya kuegesha magari pia yalikuwa yamejaa. Uchunguzi uliofanywa na Taifa Leo Dijitali ulibaini kuwa bei za bidhaa katika maduka mengi zimepunguzwa ili kuvutia wateja wengi zaidi. Maduka makubwa kama vile Naivas, Woolmart, Cleanshelf na Gilanis sasa yanatoa ofa za chini ili kuvutia wateja. Baadhi ya bidhaa ambazo kwa sasa zinauzwa bei ya chini ni mafuta ya kupikia, sukari, unga wa ugali, unga wa ngano, maziwa miongoni mwa zingine zinazotafutwa sana-msimu huu wa sikukuu. Kwa mfano, katika duka kuu la Naivas, pakiti ya mililita 500 ya maziwa ya Brookside ambayo imekuwa ikiuzwa Sh 61 sasa inauzwa Sh 55. Unga wa ugali kilo mbili Naivas inauzwa kati ya Sh135 na Sh180 kulingana na chapa. Ofa hizo zinalenga kuwapunguzia mzigo wananchi. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MWANAMUME nchini Amerika ameachiliwa gerezani baada ya kufungwa miaka 48, alipopatikana bila hatia kutokana na mashtaka ya mauaji. Mwanamume huyo, aliyetambuliwa kama Glynn Simmons, 71, aliachiliwa baada ya viongozi wa mashtaka kukubali kwamba ushahidi uliotolewa dhidi yake haukuthibitisha kwamba alishiriki kwenye mauaji hayo. Mfungwa huyo alikuwa akizuiliwa katika jimbo la Oklahoma. “Baada ya uchunguzi wa kina, mahakama hii imebaini kwamba ushahidi uliowasilishwa dhidi ya mshtakiwa haukumhusisha kwa vyovyote vile na mauaji aliyokabiliwa nayo,” akasema Jaji Amy Palumbo. Simmons alihudumu gerezani kwa jumla ya miaka 48, mwezi mmoja na siku 18, hilo likimfanya mahabusu aliyezuiliwa kwa muda mrefu zaidi nchini Amerika. Simmons alitaja hatua hiyo kuwa afueni kubwa katika maisha yake, huku akisisitiza kwamba hakuhusika kwa vyovyote vile na mauaji hayo. Simmons alifungwa gerezani mnamo 1975. Amekuwa akisisitiza kuwa hakuwepo katika jimbo la Loiusiana, anakodaiwa kutekeleza mauaji hayo.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU MWANAMUME nchini Amerika ameachiliwa gerezani baada ya kufungwa miaka 48, alipopatikana bila hatia kutokana na mashtaka ya mauaji. Mwanamume huyo, aliyetambuliwa kama Glynn Simmons, 71, aliachiliwa baada ya viongozi wa mashtaka kukubali kwamba ushahidi uliotolewa dhidi yake haukuthibitisha kwamba alishiriki kwenye mauaji hayo. Mfungwa huyo alikuwa akizuiliwa katika jimbo la Oklahoma. “Baada ya uchunguzi wa kina, mahakama hii imebaini kwamba ushahidi uliowasilishwa dhidi ya mshtakiwa haukumhusisha kwa vyovyote vile na mauaji aliyokabiliwa nayo,” akasema Jaji Amy Palumbo. Simmons alihudumu gerezani kwa jumla ya miaka 48, mwezi mmoja na siku 18, hilo likimfanya mahabusu aliyezuiliwa kwa muda mrefu zaidi nchini Amerika. Simmons alitaja hatua hiyo kuwa afueni kubwa katika maisha yake, huku akisisitiza kwamba hakuhusika kwa vyovyote vile na mauaji hayo. Simmons alifungwa gerezani mnamo 1975. Amekuwa akisisitiza kuwa hakuwepo katika jimbo la Loiusiana, anakodaiwa kutekeleza mauaji hayo.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU SERIKALI imetangaza hatua mpya ya kuongeza ada zaidi zinazotolewa kwa raia kupitia mtandao wa e-Citizen. Hatua hiyo mpya ilitangazwa na Waziri wa Fedha, Profesa Njuguna Ndung’u, kwenye tangazo lililowekwa katika Gazeti Rasmi la Serikali mnamo Desemba 14, 2023. Baadhi ya huduma zitakazoathiriwa na nyongeza hiyo ni kutuma pesa kwa nja ya simu za mkononi, malipo kwa njia ya kadi za kielektronini kati ya nyingine. Kulingana na tangazo hilo, Mkenya atatozwa ada ya Sh5 kwa huduma zote zitakazimgharimu chini ya Sh199. Wale watakaolipia huduma za kati ya Sh200 na Sh299 watatozwa ada ya Sh10. Malipo ya kati ya Sh300 na Sh499 yatatozwa ada ya Sh15. Kwa huduma za mtandao wa e-Citizen zilizo kati ya Sh500 na Sh669, Wakenya watatozwa ada ya Sh20. Malipo ya huduma za kati ya Sh700 na Sh999 yatamgharimu Mkenya ada ya Sh25. Malipo yoyote yaliyo zaidi ya Sh1,000 yatamgharimu Mkenya ada ya Sh50. Huduma zozote zitakazolipiwa kupitia dola za Amerika zitatozwa ada ya dola moja. “Ada hizo zitaanza kutozwa mara moja,” akasema Waziri Ndung’u. Aidha, Waziri alishauri Wakenya kwenda katika tovuti www.eCitizen.go.ke kutazama mabadiliko hayo kwa kina. Baadhi ya Wakenya wameeleza kughadhabishwa sana na hatua ya serikali kuongeza ada hizo, hasa wakati huu wakati hali ya uchumi nchini ni ngumu.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA WANDERI KAMAU SERIKALI imetangaza hatua mpya ya kuongeza ada zaidi zinazotolewa kwa raia kupitia mtandao wa e-Citizen. Hatua hiyo mpya ilitangazwa na Waziri wa Fedha, Profesa Njuguna Ndung’u, kwenye tangazo lililowekwa katika Gazeti Rasmi la Serikali mnamo Desemba 14, 2023. Baadhi ya huduma zitakazoathiriwa na nyongeza hiyo ni kutuma pesa kwa nja ya simu za mkononi, malipo kwa njia ya kadi za kielektronini kati ya nyingine. Kulingana na tangazo hilo, Mkenya atatozwa ada ya Sh5 kwa huduma zote zitakazimgharimu chini ya Sh199. Wale watakaolipia huduma za kati ya Sh200 na Sh299 watatozwa ada ya Sh10. Malipo ya kati ya Sh300 na Sh499 yatatozwa ada ya Sh15. Kwa huduma za mtandao wa e-Citizen zilizo kati ya Sh500 na Sh669, Wakenya watatozwa ada ya Sh20. Malipo ya huduma za kati ya Sh700 na Sh999 yatamgharimu Mkenya ada ya Sh25. Malipo yoyote yaliyo zaidi ya Sh1,000 yatamgharimu Mkenya ada ya Sh50. Huduma zozote zitakazolipiwa kupitia dola za Amerika zitatozwa ada ya dola moja. “Ada hizo zitaanza kutozwa mara moja,” akasema Waziri Ndung’u. Aidha, Waziri alishauri Wakenya kwenda katika tovuti www.eCitizen.go.ke kutazama mabadiliko hayo kwa kina. Baadhi ya Wakenya wameeleza kughadhabishwa sana na hatua ya serikali kuongeza ada hizo, hasa wakati huu wakati hali ya uchumi nchini ni ngumu.   You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA LABAAN SHABAAN WAZIRI wa Barabara na Uchukuzi Kipchumba Murkomen amewarai Wakenya kuripoti visa vya utepetevu miongoni mwa madereva na wahudumu wa uchukuzi ili kuzuia visa vya ajali msimu huu wa Krismasi 2023 na Mwaka Mpya. Angalau watu 4, 000 hufa kila mwaka kwa ajali za barabara na matukio yaliongezeka kwa asilimia 5 mwaka wa 2022. Haya ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama Barabarani (NTSA). Tangu msimu wa shamrashamra za Krismasi kuanza, kumeshuhudia visa vya ajali mfululizo, vingi vikihusisha usafiri wa umma. Bw Murkomen amesema iwapo watumiaji wa barabara watawajibika, ajali zitadhibitiwa. “Makini na uwajibikaji unahitajika miongoni mwa watumiaji wa barabara ikiwa tunalenga kuangazia changamoto za barabarani,” alisema waziri Murkomen katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa X akirai Wakenya kuripoti visa vya utepetevu barabarani ili hatua mwafaka zichukuliwe. Waziri alikuwa anarejelea video iliyoonyesha basi la abiria lililokuwa limejaa kupindukia wengine wakining’inia huku likiendeshwa kwa kasi mnamo Desemba 22, 2023. Video hiyo inaendelea kusambaa mitandaoni. “Mtumiaji wa barabara aliyejali usalama alinasa tukio la matatu kuendeshwa vibaya na kujazwa pomoni. Nilielekeza NTSA kuwakamata wahudumu na kuwachukulia hatua ifaayo. Sasa ninaweza kuthibitisha kuwa dereva na kondakta wake wametiwa nguvuni na wako katika kituo cha polisi cha Capitol Hill,” Bw Murkomen alisema akishukuru wananchi kwa kuwajibika. Kwa mujibu wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), watu 16 wamefariki kupitia ajali ndani ya majuma mawili yaliyopita.       You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA LABAAN SHABAAN WAZIRI wa Barabara na Uchukuzi Kipchumba Murkomen amewarai Wakenya kuripoti visa vya utepetevu miongoni mwa madereva na wahudumu wa uchukuzi ili kuzuia visa vya ajali msimu huu wa Krismasi 2023 na Mwaka Mpya. Angalau watu 4, 000 hufa kila mwaka kwa ajali za barabara na matukio yaliongezeka kwa asilimia 5 mwaka wa 2022. Haya ni kwa mujibu wa Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama Barabarani (NTSA). Tangu msimu wa shamrashamra za Krismasi kuanza, kumeshuhudia visa vya ajali mfululizo, vingi vikihusisha usafiri wa umma. Bw Murkomen amesema iwapo watumiaji wa barabara watawajibika, ajali zitadhibitiwa. “Makini na uwajibikaji unahitajika miongoni mwa watumiaji wa barabara ikiwa tunalenga kuangazia changamoto za barabarani,” alisema waziri Murkomen katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa X akirai Wakenya kuripoti visa vya utepetevu barabarani ili hatua mwafaka zichukuliwe. Waziri alikuwa anarejelea video iliyoonyesha basi la abiria lililokuwa limejaa kupindukia wengine wakining’inia huku likiendeshwa kwa kasi mnamo Desemba 22, 2023. Video hiyo inaendelea kusambaa mitandaoni. “Mtumiaji wa barabara aliyejali usalama alinasa tukio la matatu kuendeshwa vibaya na kujazwa pomoni. Nilielekeza NTSA kuwakamata wahudumu na kuwachukulia hatua ifaayo. Sasa ninaweza kuthibitisha kuwa dereva na kondakta wake wametiwa nguvuni na wako katika kituo cha polisi cha Capitol Hill,” Bw Murkomen alisema akishukuru wananchi kwa kuwajibika. Kwa mujibu wa Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), watu 16 wamefariki kupitia ajali ndani ya majuma mawili yaliyopita.       You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII RAIS William Ruto amesema nafasi aliyopata ya kuliongoza taifa hili ni sehemu ya utabiri wa wazee wa jamii ya Wakalenjin kuhusu ufanisi wa kundi la rika lake la Kaplelach, “atakapotwaa uongozi wa taifa hili”. Akiongea Ijumaa nyumbani kwake katika eneo la Sugoi, Turbo, Kaunti ya Uasin Gishu, Dkt Ruto alieleza kuwa sasa ni wajibu wake kuiwezesha nchi hii kupata ufanisi au iangamie. “Mimi ni mmoja wa wanachama wa rika la Kaplelach na ni fahari yangu kujitambulisha nao na kuchangia kutimia kwa utabiri wa wazee kwamba mmoja wetu ama atastawisha Kenya au ataiporomosha,” Dkt Ruto akaambia umati mkubwa wa watu waliokongamana nyumbani kwake eneobunge la Turbo. Alisema hayo alipoandaa dhifa ya Krismasi kwa wakazi wa Uasin Gishu nyumbani kwake Sugoi. Dkt Ruto alitumia fursa hiyo kumshambulia mtangulizi wake Uhuru Kenyatta akisema rais huyo mstaafu alimrithisha hazina ya serikali isiyo na pesa zozote, akiilinganisha na ghala ambalo limetorokwa hata na panya. Alisema kwa muda wa miezi 15 ambayo ameshikilia wadhifa huo, amefaulu kurejesha imani ya wawekezaji, hali ambayo imefufua uchumi na kuboresha maisha ya wananchi. “Mnajua yale ambayo reggae na watu wa BBI walifanya kwa uchumi wetu. Nilipoingia afisini hakukuwa na chochote kwenye ghala, hata panya walikuwa wamelitoroka. Tangu wakati huo nimefaulu kushawishi washirika wetu wa kimaendeleo na tumefufua uchumi licha ya kukosolewa na wapinzani wetu,” akasema Dkt Ruto. Mpango wa mageuzi ya katiba kupitia mchakato wa maridhiano (BBI) uliungwa mkono na Bw Kenyatta na kiongozi wa Azimio Raila Odinga. Mahakama iliupiga breki. Hatua hiyo ilimfaidi pakubwa Dkt Ruto aliyetumia uamuzi huo kujipigia kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2022. Rais Ruto aliwaambia wakazi wa Uasin Gishu kuwa yu katika tapo la viongozi ambao nia yao kuu ni kustawisha taifa hili.Rais ambaye alikuwa ameandamana na Mkewe Rachel, alisambaza zawadi mbalimbali kwa wakazi hao. Miongoni mwa zawadi hizo ilikujwa; unga wa mahindi, unga wa ngano, mchele, sukari, mafuta ya kupikia miongoni mwa bidha nyinginezo. Bidhaa hizo zilikuwa ni zawadi ya Krismasi kwa wakazi hao. Dkt Ruto aidha, alitumia nafasi hiyo kukariri kujitolea kwa serikali yake kupunguza gharama ya matibabu kupitia Sheria za kufanikisha Mpango wa Afya kwa Wote (UHC). “Chini ya sheria hii wale raia wasio na ajira ambao wamekuwa wakilipa ada ya Sh500 kwa mwezi kama mchango wa Bima ya Kitaifa ya Afya (NHIF) sasa watalipa Sh300 pekee na kutibiwa maradhi yote yakiwemo kansa,” Rais akaeleza. Dkt Ruto alisema ni makosa kwa watu fulani kuwenda Kortini kusitisha miradi inayolenga kuimarisha maisha ya Wakenya kama vile mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu. “Chini ya mpango wa ujenzi wa nyumba, nyumba 200,000 zitajengwa kila mwaka. Kufikia sasa zaidi ya watu 12,000 wameajiriwa katika maeneo 31 kunakojengwa nyumba hizo,” akasema Rais Ruto. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA BARNABAS BII RAIS William Ruto amesema nafasi aliyopata ya kuliongoza taifa hili ni sehemu ya utabiri wa wazee wa jamii ya Wakalenjin kuhusu ufanisi wa kundi la rika lake la Kaplelach, “atakapotwaa uongozi wa taifa hili”. Akiongea Ijumaa nyumbani kwake katika eneo la Sugoi, Turbo, Kaunti ya Uasin Gishu, Dkt Ruto alieleza kuwa sasa ni wajibu wake kuiwezesha nchi hii kupata ufanisi au iangamie. “Mimi ni mmoja wa wanachama wa rika la Kaplelach na ni fahari yangu kujitambulisha nao na kuchangia kutimia kwa utabiri wa wazee kwamba mmoja wetu ama atastawisha Kenya au ataiporomosha,” Dkt Ruto akaambia umati mkubwa wa watu waliokongamana nyumbani kwake eneobunge la Turbo. Alisema hayo alipoandaa dhifa ya Krismasi kwa wakazi wa Uasin Gishu nyumbani kwake Sugoi. Dkt Ruto alitumia fursa hiyo kumshambulia mtangulizi wake Uhuru Kenyatta akisema rais huyo mstaafu alimrithisha hazina ya serikali isiyo na pesa zozote, akiilinganisha na ghala ambalo limetorokwa hata na panya. Alisema kwa muda wa miezi 15 ambayo ameshikilia wadhifa huo, amefaulu kurejesha imani ya wawekezaji, hali ambayo imefufua uchumi na kuboresha maisha ya wananchi. “Mnajua yale ambayo reggae na watu wa BBI walifanya kwa uchumi wetu. Nilipoingia afisini hakukuwa na chochote kwenye ghala, hata panya walikuwa wamelitoroka. Tangu wakati huo nimefaulu kushawishi washirika wetu wa kimaendeleo na tumefufua uchumi licha ya kukosolewa na wapinzani wetu,” akasema Dkt Ruto. Mpango wa mageuzi ya katiba kupitia mchakato wa maridhiano (BBI) uliungwa mkono na Bw Kenyatta na kiongozi wa Azimio Raila Odinga. Mahakama iliupiga breki. Hatua hiyo ilimfaidi pakubwa Dkt Ruto aliyetumia uamuzi huo kujipigia kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa 2022. Rais Ruto aliwaambia wakazi wa Uasin Gishu kuwa yu katika tapo la viongozi ambao nia yao kuu ni kustawisha taifa hili.Rais ambaye alikuwa ameandamana na Mkewe Rachel, alisambaza zawadi mbalimbali kwa wakazi hao. Miongoni mwa zawadi hizo ilikujwa; unga wa mahindi, unga wa ngano, mchele, sukari, mafuta ya kupikia miongoni mwa bidha nyinginezo. Bidhaa hizo zilikuwa ni zawadi ya Krismasi kwa wakazi hao. Dkt Ruto aidha, alitumia nafasi hiyo kukariri kujitolea kwa serikali yake kupunguza gharama ya matibabu kupitia Sheria za kufanikisha Mpango wa Afya kwa Wote (UHC). “Chini ya sheria hii wale raia wasio na ajira ambao wamekuwa wakilipa ada ya Sh500 kwa mwezi kama mchango wa Bima ya Kitaifa ya Afya (NHIF) sasa watalipa Sh300 pekee na kutibiwa maradhi yote yakiwemo kansa,” Rais akaeleza. Dkt Ruto alisema ni makosa kwa watu fulani kuwenda Kortini kusitisha miradi inayolenga kuimarisha maisha ya Wakenya kama vile mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu. “Chini ya mpango wa ujenzi wa nyumba, nyumba 200,000 zitajengwa kila mwaka. Kufikia sasa zaidi ya watu 12,000 wameajiriwa katika maeneo 31 kunakojengwa nyumba hizo,” akasema Rais Ruto. You can share this post! Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
NA MHARIRI
BAADHI ya shule nchini zimejitokeza na kupinga matokeo ya Mtihani ya Darasa la Nane (KCPE) yaliyotangazwa Jumatano na Waziri... NA MHARIRI
SERIKALI za kaunti zitalazimika kutafuta mbinu za usimamizi wa fedha iwapo magavana wanataka kujitolea kutimiza ahadi zao kwa... NA MHARIRI
KILA Juni 14, ulimwengu huadhimisha Siku ya watu kuchangia damu duniani. Mwaka huu, kaulimbiu ilikuwa “Utoaji damu ni suala... NA MHARIRI
UCHAGUZI mkuu wa Agosti 9 ulikuwa wa kipekee kwa jinsi ulivyokuwa na ushindani mkali kuliko mwingineo wowote ambao umewahi... NA MHARIRI
MNAMO Ijumaa Rais William Ruto alipozuru eneo la Magharibi mwa Kenya, alisisitiza ahadi yake ya kuhakikisha kuwa viwanda vya... NA MHARIRI
TANGAZO la Benki Kuu ya Kenya (CBK) kwamba wateja wataanza kutozwa ada ya kutoa pesa kutoka kwa benki hadi simu zao linajiri... NA MHARIRI
RIPOTI ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali inayoonyesha kuwa mabunge ya kaunti yanapitisha bajeti kiholela bila kuhusisha... NA MHARIRI
MKOPO wa Hustler Fund ulioanza kutolewa kwa wananchi wenye uwezo mdogo kimapato mnamo Jumatano huenda usiwafaidi raia jinsi... NA MHARIRI
UZINDUZI wa Hazina ya Hustler jana Jumatano sasa unawapa matumaini mamia ya mama mboga, wanabodaboda na wafanyibiashara ndogo... NA MHARIRI
HATUA ya serikali kuondoa marufuku dhidi ya mahindi ya GMO imezua mjadala mkali nchini.
Suala la GMO limetekwa nyara na... NA MHARIRI
KWA wiki chache sasa, kumekuwa na wasiwasi katika baadhi ya sehemu za nchi kuhusu homa ambayo inaonekana kuenea kwa... NA MHARIRI
RIPOTI kwamba wabunge, kupitia Tume ya Huduma ya Bunge (PSC), wanataka kushinikiza Tume ya Mishahara na Marupurupu (SRC)... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na BENSON MATHEKA
NAIBU wa Rais William Ruto atatumia muungano ‘ulioundwa’ mwaka 2021 na kiongozi wa Amani National Congress (ANC)... Na WANDERI KAMAU
Naibu Rais William Ruto na waandani wake wameapa kufanya kila wawezalo kulemaza juhudi za Kiongozi wa ODM, Raila Odinga... Na CHARLES WASONGA
WABUNGE wandani wa Naibu Rais William Ruto jana walifaulu kuzuia kupitishwa kwa Mswada tata wa marekebisho ya Sheria... BRIAN OCHARO na VALENTINE OBARA
UBABE wa kisiasa kati ya Kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, na Naibu Rais William Ruto katika Kaunti ya... Na CHARLES WASONGA
HATUA ya Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga kushikilia kuwa wawaniaji wanaounga azma zao za... Na WANDERI KAMAU
SUALA lililozua gumzo wiki hii ni majibizano yaliyozuka kati ya mrengo wa Naibu Rais William Ruto na mwanasiasa Maina... Na JUSTUS WANGA
GAVANA wa Meru Kiraitu Murungi amekiri kwamba umaarufu wa Naibu Rais William Ruto umekita mizizi zaidi katika eneo la... Na CECIL ODONGO
INASIKITISHA kuwa Naibu Rais Dkt William Ruto na Seneta wa Baringo Gideon Moi sasa wanalitumia suala la msitu wa Mau kwa... Na WYCLIFFE NYABERI
NAIBU Rais Dkt William Ruto amemshambulia Rais Uhuru Kenyatta huku akisema ataondoka mamlakani bila kulipa deni la... Na CHARLES WASONGA
NAIBU Rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga wanaonekana kuendeleza mbinu za kampeni za kulambana visigino... Na IAN BYRON
HATUA ya Gavana Okoth Obado kujihusisha na siasa za chama cha United Democratic Alliance (UDA) cha Naibu Rais, Dkt William... BENSON MATHEKA NA CHARLES WASONGA
?WASHIRIKA wa Naibu Rais William Ruto wamegeuka kupe kwa ‘ kufyoza mamilioni ya fedha anazoyapa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na MASHIRIKA
LONDON, Uingereza
WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson, jana alitangaza masharti makali kudhibiti maambukizi ya... Na ELIZABETH MERAB
WANASAYANSI wanachunguza kuhusu mchipuko wa virusi vipya vya corona aina ya Delta, katika nchi za Amerika, Uingereza,... Na MAUREEN ONGALA
MASAIBU ambayo wagonjwa wa Covid-19 hupitia katika kaunti za Pwani, yameanikwa wazi baada ya kifo cha afisa mkuu wa... SIAGO CECE na ANTHONY KITIMO
UFISADI miongoni mwa baadhi ya maafisa wa serikali katika mpaka wa Kenya na Tanzania, umezidi kuwaweka... Na WAANDISHI WETU
WINGU la maangamizi limetanda kote nchini huku aina mpya ya corona maarufu kama 'Delta' ikiua watu kwa... Na WINNIE ONYANDO
HUENDA visa vya wasafiri kulazimishwa kupima upya corona mpakani mwa Kenya na Tanzania vikakoma baada ya serikali hizo... NA WANGU KANURI
AGIZO la serikali la kudhibiti mkurupuko wa ugonjwa wa corona mwaka jana limewashurutisha Wakenya wengi kufanyia kazi... Na Titus Ominde
VIONGOZI wa kidini Kaskazini mwa Rift Valley (North Rift) wameshutumu wanasiasa kwa kupepeta usambazaji wa virusi vya... Na WANTO WARUI
Huku wanafunzi wa kidato cha kwanza wakiripoti katika shule zao mpya za sekondari hii leo, kuna uwezekano wa maambukizi... Na CHARLES WASONGA
NAKUBALIANA na kauli ya maafisa wa afya katika kaunti ya Nairobi kwamba wanasiasa ndio wanachochea ongezeko la visa... Na SAMMY WAWERU
DICKSON Muceri amekuwa mkazi wa Nairobi kwa muda wa miaka kadhaa ila sasa kitovu hicho cha jiji kuu la nchi hakikaliki... Na MARY WANGARI
WANASAYANSI wamethibitisha kuwa kuchelewesha upokeaji dozi ya pili ya chanjo ya Covid-19 kwa kiasi cha miezi 10 baada ya... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na KINYUA BIN KINGORI
WAKATI huu viongozi wa kisiasa wameanza mapema kampeni zao kwa kuzuru maeneo mbalimbali nchini, ili kushawishi... Na WANDERI KAMAU
KULINGANA na Ripoti ya Jaji Mstaafu Akilano Akiwumi (1997) kuhusu chimbuko la ghasia za kikabila nchini, wanasiasa ndio... Na WANTO WARUI
KWA mara nyingine tena tuzo inayoenziwa sana kote ulimwenguni imerudi katika eneo letu la Afrika Mashariki mara hii... Na DOUGLAS MUTUA
MWAFRIKA akiwajibishwa na Mzungu hupiga kamsa na kudai anaonewa, ati msingi wa maonevu ni ubaguzi wa rangi... Na WANDERI KAMAU
MOJA ya changamoto kuu zinazokikumba kizazi cha sasa nchini ni ukosefu wa ufahamu wa lugha zao asili.
Ingawa lugha... Na KINYUA BIN KINGORI
JUHUDI za kuhakikisha taifa limefanikiwa kupiga vita ufisadi lazima ziendeshwe kuambatana na Katiba, bila njama... Na WANDERI KAMAU
UFICHUZI wa sakata ambapo watu maarufu duniani wamekuwa wakificha mabilioni ya fedha katika akaunti za siri ng’ambo... Na FAUSTINE NGILA
NINA imani kuwa iwapo kufikia sasa hujawahi kuelewa teknolojia ya blokcheni, leo utaelewa kwa kuwa jana uliathirika... Na CHARLES WASONGA
NI jambo la kusikitisha kuwa ni wakati kama huu ambapo uchaguzi mkuu unakaribia ndipo wanasiasa wametambua umuhimu wa... Na MARY WANGARI
IDADI ya watu wanaoandaa hafla za uchangishaji pesa za kugharamia matibabu imeongezeka pakubwa katika siku za hivi... Na CECIL ODONGO
CHAMA cha Kanu bado kina safari ndefu kurejelea umaarufu wake wa enzi za utawala wa chama kimoja na miaka ya 90 hata... Na CHARLES WASONGA
UTEUZI wa waliokuwa maafisa wanne wa ngazi za juu katika Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kushikilia nyadhifa... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Naomi Wamboi, 21, ndiye anatupambia yeye ni mwanamitindo aliyewahi kushinda tuzo za Miss Nakuru. Akipata muda anapenda kusafiri na... Winnie Miriam Nechesa 21, ni mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu Cha Maasai Mara kaunti ya Narok.Anapenda kuchora, na kujumuika na... Lilian Njeri mwenye umri wa miaka 21 ndiye anatupambia jarida letu leo.Yeye ni mwanamitindo na mkaazi wa Narok.Uraibu wake ni kusafiri na... Mary Njeri mwenye umri wa miaka 21 ni mkaazi wa mtaa wa Langalanga kaunti ya Nakuru.Yeye ni mwanafasheni wa mapambo na vipodozi.Uraibu wake... Marylene Watiri mwenye umri wa miaka 22 ni mtaalam wa Beauty Therapy jijini Nairobi, aidha yeye ni mwanamitindo na mlimbwende.Uraibu wake... Zaweria Njoki mwenye umri wa miaka 21 ni Video Vixen kutoka kaunti ya Nakuru.Uraibu wake ni kuandika makala ya kitaaluma na kujumuika na...
Malkia wetu leo ni  Babra Ingasiani mwenye umri wa miaka 21, yeye ni mzaliwa wa kaunti ya Kakamega.Uraibu wake ni kusakata densi ya... Pauline Kimani mwenye umri wa miaka 23 ndiye anatupambia jarida letu leo.Yeye ni mkaazi wa eneo la Lanet na mfanyikazi mjini Nakuru.Uraibu...
Sayfer Godez ni mkaazi wa Nakuru .Anapenda kushiriki kwenye majukwaa ya mapambo na urembo.Uraibu wake ni kusafiri na kujumuika na... Sylvia Wangeci 23 ni mzaliwa wa Molo, na mwanafunzi katika Chuo Kikuu Cha MKU tawi la Nakuru.Uraibu wake ni kusafiri na... Mical Abulatsia Imbukwa, 28, ni mwanahabari katika shirika moja jijini Nairobi. Uraibu wake ni kutazama filamu za Afro sinema na kujumuika... Faith Karungari mwenye umri wa miaka 22 ni mwanafasheni na mwanamitindo maarufu kutoka Nakuru.Uraibu wake ni kuogelea na kusikiliza muziki... Be our fan Follow us Join us Subscribe our newsletter to stay updated © Copryright 2023 Taifa Leo. All Rights Reserved
Na RICHARD MUNGUTI
MAHAKAMA ya Juu jana ilianza kusikiza rufaa ya mpango wa kubadilisha katiba (BBI) huku Mwanasheria Mkuu Bw Paul... Na BENSON MATHEKA
RAIS Uhuru Kenyatta jana Jumapili alisema kuwa ndoto yake ya kubadilisha katiba ya Kenya iliyopitishwa 2010 kupitia... Na CHARLES WASONGA
KWA mara nyingine Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza kuwa mageuzi ya katiba yaliyopendekezwa katika Mswada wa Mpango wa... Na JOSEPH WANGUI
Mwanasheria Mkuu, Paul Kihara Kariuki hatimaye amewasilisha rasmi rufaa katika Mahakama ya Juu kupinga uamuzi wa... Na Gitonga Marete
KIONGOZI wa chama cha Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi amesisitiza kuwa Bunge linapaswa kurejelea Mpango... Na Leonard Onyango