text
stringlengths
1
24.2k
label
int64
0
5
['Arsenal wapo tayari kumuuza mshambuliaji wao raia wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, lakini si kwa Manchester United ama Liverpool. (90min.com)', 'Mshambuliaji wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, ameiomba klabu yake ya Crystal Palace imruhusu ahamie Arsenal. Palace inamthaminisha streka huyo streka huyo kuwa na thamani ya pauni milioni 80. (Mirror)', 'Manchester United wanamini kuwa wataweza kukamilisha usajili wa kuwanasa Sean Longstaff, 21, kutoka Newcastle na Bruno Fernandes, 24, kutoka Sporting Lisbon ya Ureno. (Evening Standard)', 'Real Madrid watalazimika kulipa kitita cha pauni milioni 150 ili kumsajili kiungo Mfaransa Paul Pogba 26, kutoka Manchester United. (Mirror)', 'Gareth Bale yawezekana akasilia na Real Madrid baada ya klabu hiyo kushindwa kumpata mnunuzi anayemtaka winga huyo mwenye miaka 29. (Mirror)', 'Chelsea wanampango wa kumtangaza Frank Lampard kuwa kocha wao mpya kabla ya wachezaji kurudi mpaumzikoni wiki ijayo kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao. plan to announce Derby. (Sun)', 'Liverpool wamefikia makubaliano na Sporting ada ya usajili ipatayo pauni milioni 7 ili kumnunua mshambuliaji kinda Rafael Camacho, 19. (Evening Standard)', "Kumefanyika mkutano baina ya viongozi wakuu wa Atletico na Real Madrid juu ya usajili wa usajili wa mshambuliaji Antoine Griezmann, 28, kuelekea dimba la Bernabeu. (L'Equipe - in French)", 'Streka wa Colombia Radamel Falcao, 33, anataka kujiunga na timu inayomilikiwa na David Beckham nchini Marekani Miami pale mkataba wake watakapofiki tamati na klabu ya Monaco. (Sun)', 'Aston Villa wapo tayari kutuma maombi ya kutaka kumsajili beki wa Southampton Matt Targett. (Express and Star)', 'Kocha wa West Brom Slaven Bilic anamtaka mchezaji mwenzake wa zamani klabuni hapo Julian Dicks kujiunga naye kama sehemu ya benchi la ufundi.. (Express and Star)', 'Manchester United inafikiria kumnunua beki wa Ufaransa na Barcelona Samuel Umtiti, 25. (Mundo Deportivo - in Spanish)', 'Mshambuliaji wa Manchester City na Ujerumani Leroy Sane, 23, anasalia kuwa mchezaji anayelengwa sana na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich msimu huu licha ya mpango huo kusita hapo awali. (Sky Sports)', 'Mkufunzi wa klabu ya Sporting Marcel Keizer anaamini kwamba nafasi ya kumzuia kiungo wa kati wa Portugal Bruno Fernandez katika klabu hiyo ni ndogo, huku Manchester United ikiwa miongoni mwa klabu ambazo zimevutiwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 (Record, via Manchester Evening News)', 'Babake mshambuliaji wa Juventus Moise Kean, 19, ametangaza kwamba raia huyo wa Italia anataka kuhamia Inter Milan. (Mirror)', 'Atletico Madrid inafikiria kumsajili mchezaji wa Real Madrid na Colombian James Rodriguez, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 akiwa hahitajiki tena Real . (Cadena SER, via AS)', 'Naibu mkufunzi wa Chelsea Gianfranco Zola ataondoka Chelsea wikendi hii wakati ambapo kandarasi yake itakuwa inakamilika baada ya kukataa ofa ya kuwa balozi wa klabu hiyo. (Guardian)']
2
NA FESTO POLEA, BAGAMOYO BAADA ya kuhudhuria matamasha mbalimbali na kuona faida yake, mwanamuziki wa muziki wa taarabu, Isha Mashauzi, amesema kuna haja ya wadau wa taarabu kuandaa tamasha la muziki huo ili kuutangaza kimataifa. “Matamasha ni muhimu, kuna mambo mengi tunajifunza na pia hatuwezi kualikwa waimbaji wote wa taarabu katika matamasha hayo, lakini kama kukiwa na tamasha la taarabu kubwa kama yalivyo matamasha mengine makubwa yanayofanyika nchini itasaidia kututangaza wasanii wake na muziki wetu wa taarabu kimataifa kupitia wasanii tutakaowaalika katika tamasha hilo,” alieleza Isha. Isha usiku wa kuamkia jana alitumbuiza katika tamasha la Karibu Music Festival, lililofanyika katika uwanja wa Mwanakarenge, uliopo Bagamoyo, mkoani Pwani. Tamasha hilo lilihitimishwa na mkali wa muziki na bongo fleva kutoka kundi la Wanaume Halisi, Juma Nature, kwa shoo kali akiwa na wasanii wa kundi hilo, akiwemo aliyejiengua katika kundi hilo, Rich One. Ingawa mvua ilikuwa changamoto kubwa, lakini tamasha hilo lilihitimishwa vema huku wadau mbalimbali wa muziki wakipongeza waandaaji kwa kujipanga vema, huku wakiwataka waongeze juhudi zaidi na kuleta wasanii wenye majina makubwa kutoka nje na ndani ya nchi ili washiriki katika tamasha hilo.
4
Taarifa hizo za ukuaji wa Pato la Taifa, zilitolewa jana Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Morrice Oyuke wakati akizungumza na waandishi wa habari.Hata hivyo Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Uchumi Dk Stephen Kirama alisema yako malalamiko kuwa uchumi unakua lakini haumnufaishi mtu mmoja mmoja.“Ni jambo ambalo pia linaweza kuangaliwa na kutiliwa mkazo, kuna umuhimu wa kusimamia sera kukuza uchumi kupitia sekta nyingine pia,” alisema Dk Kirama.Taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu iliyotolewa jana, ilionesha katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka huu, uzalishaji umeme na usambazaji maji umekua kwa kasi ya asilimia 12.6 ikilinganishwa na asilimia 6.2 katika kipindi kama hicho kwa mwaka jana.Shughuli za uchukuzi na mawasiliano zilifikia kasi ya asilimia 16.5. Sekta nyingine na asilimia za ukuaji katika mabano ni uchumi na kilimo (1.6), uvuvi (2.5), uchimbaji madini, mawe na kokoto (8.7) na uzalishaji wa bidhaa viwandani (8.5).
0
TATIZO la utapiamlo linatajwa kuendelea kuathiri kasi ya kupunguza umaskini nchini. Kauli hiyo ilitolewa katika hotuba ya Mkuu wa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, Deogratias Ndejembi iliyowasilishwa kwa niaba yake na Katibu Tarafa ya Kongwa, Denis Semindu kwenye kikao kazi cha maandalizi ya awali ya mipango na Bajeti ya Afua za lishe 2020/2021.Semindu alisema, lishe duni si tu huathiri tu maendeleo ya mtoto katika ukuaji, bali humuathiri kimwili, kiakili tangu kipindi cha ujauzito na kuathiri mchango wake wa maendeleo kipindi chote cha uhai wake.Kwa mujibu wa Ripoti ya Utafiti wa Taifa wa Hali ya Lishe 2018/2019 kwa watoto chini ya miaka mitano, Dodoma ina asilimia 37.2 ya utapiamlo. Pia kwa takwimu za afya wilayani Kongwa asilimia 24 ya watoto waliohudhuria kliniki kuanzia Januari hadi Desemba 2018 wameonekana wana uzito pungufu na watoto 235 wana utapiamlo.Naye Mtaalamu wa Masuala ya Lishe, Eloy Sigalla akitoa mada alisema lishe yenye kuzingatia makundi yote ya chakula ina umuhimu mkubwa sana katika siku 1000 za makuzi ya ubongo kwa mtoto yaani siku 270 za mimba, siku 365 mwaka wa kwanza 365 za mwaka wa pili.Sigalla aliainisha baadhi ya sababu za utapiamlo kuwa ni pamoja na ulaji duni, ukosefu wa chakula, ukosefu wa huduma za afya, mila na desturi ambapo kuna baadhi ya makabila hukataza wajawazito ulaji wa baadhi ya vyakula kwa hofu ya mtoto kuzaliwa wanene na mgawanyo duni wa vyakula na sababu zao zingine za kimila.Ofisa Lishe wilayani Kongwa, Maria Haule akitoa taarifa fupi ya utekelezaji wa shughuli za lishe alisema pamoja na changamoto za upungufu wa wataalamu wa hali ya lishe, changamoto kubwa katika utekelezaji wa shughuli za lishe ni upatikanaji wa fedha hii inaleta ugumu kufikia malengo yaliwekwa na kamati hiyo katika kupambana na utapiamlo.
1
AVELINE KITOMARY -DAR ES SALAAM MWANDISHI  wa habari wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, ambayo inachapisha magazeti ya MTANZANIA, Rai, Bingwa, Dimba na The African, Eliya Mbonea, amefariki dunia jana wakati akiendelea kutibiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam. Tangu Oktoba mwaka jana, Mbonea alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) kwa nyakati tofauti tofauti. Akizungumza na MTANZANIA jana, Msemaji wa familia, Wilfred Hume alisema Mbonea alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kuishiwa damu. “Wakati huo alianza kuumwa nimonia akapatiwa matibabu katika Hospitali ya KCMC akapona ila baadae akaumwa tena homa ya manjano akafanyiwa operasheni, baada ya hapo miguu ikaanza kuvimba. “Tukamrudisha tena KCMC wakaja kugundua kuwa alikuwa na uvimbe tumboni, wakamtibu huo uvimbe ikawa hautoki na damu ikawa inamuishia, wakasema tumpeleke Muhimbili,” alisema Hume. Alisema kuwa Mbonea alivyofika hospitali ya Muhimbili alitibiwa kwa wiki tatu hadi umauti ulipomkuta jana. “Bado hatujajua atasafirishwa lini kwa sababu kikao hakijakaa ila atazikwa Arusha,” alibainisha Hume. Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha, Claude Gwandu alisema kifo cha Mbonea kimeacha pengo kubwa katika tasnia ya habari. “Mbonea pia alikuwa Katibu Mkuu wa APC kuanzia 2010 hadi 2013 na tumekuwa tukishirikiana naye hadi umauti ulipomkuta. Kwetu sisi tumepoteza mtu muhimu sana,” alisema Gwandu. Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) lilitoa salamu za pole kwa uongozi wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited kwa msiba wa Mbonea. “TEF imeshtushwa na kusikitishwa na taarifa za kifo hicho na hakika kinaacha pengo kubwa siyo tu ndani ya Kampuni ya New Habari (2006) Limited bali kwa tasnia nzima ya habari,” ilieleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu wa TEF, Neville Meena. WASIFU WA MBONEA Eliya Mbonea alizaliwa Februari 14, 1975  Shinyanga Vijijini, Mkoa wa Shinyanga. Kuanzia mwaka 1984 hadi 1990 alipata elimu ya msingi Shule ya Msingi Korogwe iliyoko wilayani Kahama mkoani humo. Kuanzia 1991 hadi 1994 alipata elimu ya kidato cha nne Shule ya Sekondari Kahama iliyoko mkoani Shinyanga. Agosti, 2002 alihitimu taaluma ya habari ngazi ya cheti katika Chuo cha Tanzania Institute of Media Education (TIME) na kisha kuendelea na chuo hicho mwaka 2002 hadi 2003 alipohitimu masomo katika ngazi ya cheti cha uandishi wa habari. Mwaka 2007 hadi 2009 alipata mafunzo ya uandishi wa habari katika ngazi ya diploma chuoni hapo. Kuanzia Januari 2004 hadi 2006 Mbonea alifanya kazi na magazeti ya Majira na Business Times ambayo yanachapishwa na Kampuni ya Business Times Limited (BTL). Agosti 3, 2006 alijiunga na Kampuni ya New Habari (2006) Ltd akiandikia gazeti la Rai. Aidha, Agosti 3, 2010 hadi Mei 31, mwaka jana alikuwa mwakilishi wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd Kanda ya Kaskazini inayojumuhisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
1
NA SHARIFA MMASI CHIPUKIZI kwenye muziki wa Bongo Fleva, Ramadhan Jafar ‘Ronki’, yupo mbioni kutoka na wimbo wake wa kwanza wa kimapenzi alioupa jina ‘Mapenzi Siri’. “Nimeingia kwenye familia ya muziki wa bongo fleva nikiwa nafahamu ushindani wa hali ya juu uliopo kwenye muziki wa sasa, lakini kipaji changu ndicho kinachonipa jeuri ya kuja kufanya vizuri siku zijazo,’’ alisema chipukizi huyo. “Tayari nimeachia wimbo wa kwanza tangu nijikite kwenye muziki na ninamshukuru Mungu unaendelea kufanya vema,” alisema Ronki.
4
WASHINGTON, MAREKANI RAIS Donald Trump wa Marekani anapanga kulitangaza Udugu wa Kiislamu kuwa la kigaidi, hatua ambayo inaweza kulisababishia kundi hilo kongwe zaidi la Kiislamu nchini Misri kuwekewa vikwazo. Msemaji wa Ikulu ya White House mjini hapa, Sarah Sanders, ametoa taarifa kwa njia ya barua pepe, akieleza Trump ameijadili hatua hiyo na washauri wake wa kiusalama pamoja na viongozi wa kikanda wenye mtazamo sawa na wake kuhusu kundi hilo. Ripoti ya gazeti la New York Times la hapa, ambayo imethibitishwa na ofisa mwandamizi wa Serikali ya Marekani, imesema Rais Abdel Fattah al-Sisi wa Misri alimuomba Trump kuchukua hatua hiyo wakati alipofanya ziara nchini hapa Aprili 9 mwaka huu. Licha ya wasiwasi ulioelezwa na wabunge wa vyama vyote nchini Marekani kuhusu rekodi mbaya ya haki za binadamu ya Rais al-Sisi, Trump alimsifu kiongozi huyo, akimwita ‘rais bora kabisa’.
3
NEW YORK, MAREKANI MAREKANI imekua nchi ya kwanza duniani kurekodi zaidi ya vifo 2000 vya virusi vya corona kwa siku moja. Takwimu kutoka Chuo Kikuu Johns Hopkins zinaonyesha kuwa watu 2,108 wamekufa katika kipindi cha saa 24, huku kukiwa sasa na zaidi ya watu nusu milioni walioambukia virusi hivyo nchini humo. Marekani hivi karibuni inaweza kuipita Italia kwa idadi zaidi ya vifo vinavyotokana na virusi hivyo kote duniani. Lakini Mtaalamu wa Ikulu ya White House kuhusu Covid-19 anasema mlipuko unaanza kuwa wa kiwango cha chini kote nchini Marekani. Dokta Deborah Birx, anasema kuwa kuna ishara nzuri za kupungua kwa mlipuko, lakini akaonya kuwa: “Licha ya kwamba matokeo yanaweza kutia moyo, hatujafikia kilele cha maambukizi.” Rais Donald Trump pia amesema anatarajia Marekani kushuhudia kiwango cha chini cha vifo kuliko makadirio ya awali ya vifo 100,000 , akiongeza kuwa :  ” Tunaona ishara za wazi kwamba mikakati yetu mizuri inanusuru maisha ya watu wasiohesabika “. Rais Donald Trump pia amesema kuwa anatarajia Marekani kushuhudia kiwango cha chini cha vifo kuliko makadirio ya awali ya vifo 100,000. Marekani sasa ina takribani vifo 18,693 na idadi ya visa vilivyothibitishwa ni 500,399, kwa mujibu wa Chuo Kikuu cha Johns Hopkins, ambacho ndicho kinachofuatilia takwimu za ugonjwa huo kote duniani. Takriban nusu ya vifo hivyo vilirekodiwa katika eneo la New York. Italia imeripoti vifo 18,849 huku vifo zaidi ya 102,000 vikiripotiwa kote duniani kutokana na virusi vya corona. Watafiti walikua wamekadiria idadi ya vifo nchini Marekani ingefikia kilele chake Ijumaa na hatimae kuanza kushuka, vilishuka hadi kufikia vifo vipatavyo 970 kwa siku ilipofika Mei Mosi-siku ambayo utawala wa Trump ulikua umeitaja kama siku ya kuanza shughuli zake za kiuchumi. “Ninataka shughuli za uchumi zifunguliwe mapema iwezekanavyo ,” Trump alisema katika hotuba yake ya siku ya Ijumaa Kuu aliyoitoa Ikulu.  “Ninaweza kusema bila shaka ni uamuzi mkubwa ambao nimewahi kuufanya” Hatahivyo, hakuna hatua ambayo itachukuliwa hadi serikali itakapofahamu kuwa “nchi itakua katika hali nzuri ya afya “, alisema.  “Hatutaki kurudi nyuma na kuanza tena kupambana na virusi .” JINSI CORONA ILIVYOBADILI MAISHA NEWYORK Virusi vya corona vimebadili kila kitu kuhusu maisha jijini New York, na sasa imegeuka kuwa uwanja wa vifo. Wakazi wa New York wamekua wakishitushwa na magari ya Ambulance yanayopita mara kwa mara, malori yanayobeba miili ya watu na idadi kubwa ya vifo. Wakazi wa New York wameshitushwa na kushuhudia: magari ya kubebea wagonjwa karibu wakati wote yakiwasha vimulimuli katika mitaa iliyokimbiwa na watu. Mara kadhaa wamekuwa wakishuhudia miili iliyowekwa kwenye mabegi ya plasitiki inayowekwa kwenye malori ya friji nje ya hospitali na sasa makaburi mapya yanachimbwa katika kisiwa Hart kwa ajili ya uwezekano wa kufanya mazishi ya pamoja. Makaburi yaliyoko mbali , yanayoweza kufikiwa kwa njia ya maboti, ni sehemu inayofahamika kihistoria kama eneo la huzuni kwasababu ni mahala pa makaburi ya jumla yasiyojengwa na mawe kutokana na kwamba ni eneo inapozikwa miili isiyo na wenyewe. Hifadhi ya maiti ya jiji la New York ilikuwa na uwezo wa kupokea miili mingi kabla dharura ya mazishi ya wahanga wa mlipuko wa Covid-19. Lakini sasa lazima wazikwe haraka ili kuepusha maambukizi. Wakurugenzi wa mazishi wanaongea wazi jinsi ongozeko la vifo vinavyotisha na kufadhaisha.  Hata kabla ya rekodi ya wiki hii ya idadi ya vifo, baadhi ya familia zililazimika kusubiri kwa wiki moja au zaidi kuizika au kuiteketeza miili ya wapendwa wao. MATUMAINI MLIPUKO KUANZA KUPUNGUA HIVI KARIBUNI  Dk. Anthony Fauci, Mkuu wa magonjwa ya maambukizi nchini Marekani, alisema kuwa nchi hiyo itaanza  kushuhudia kupungua kwa visa na vifo.  Lakini akaongeza kuwa ni muhimu juhudi za kupunguza maambukizi kama kuepuka watu kukaribiana zikaendelezwa. Ubashiri mpya wa Taasisi ya hesabu na tathmini katika Chuo kikuuu cha Washington unatabiri kuwa kutakua na vifo 60,000 ifikapo Agosti 4 kama sheria zilizowekwa zitaendelea kuwepo.  Mwezi uliopita, Dk Fauci alikadiria kuwa kutakua na vifo walau 100,000. Ijumaa , Gavana wa New York, Andrew Cuomo alisema kuwa data za hivi karibuni zinaonyesha kuwa jimbo limefanikiwa “kupunguza usaambaaji wa virusi “, lakini pia akaonya kuwa ni mapema mno kwa watu kuanza kupuuza hatua ya watu kutokaribiana .  “Ingawa ni jambo linalosumbua, hata kama ni vigumu, lazima tuizoee.” Katika hotuba yake Ijumaa Rais Trump alisema pia kuwa aliona picha za ndege zisizokua na rubani za masanduku mengi ya maiti yakiwa yamekwama kwenye makaburi ya jumla katika kisiwa cha New York cha Hart.  Maofisa huko wanasema kisiwa, ambacho kimekuwa kikitumiwa kuzika maiti za watu wasiokua na ndugu kwa miaka zaidi ya 150, sasa wanazika miili mara tano zaidi ya kiwango cha kawaida.
3
ARODIA PETER DODOMA Na PATRICIA KIMELEMETA-DAR NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema Serikali imeanza uchunguzi wa tukio la kutowekwa kwa kada wa Chadema, Yona Nyagali (Mdude Nyagali). Vilevile ameelekeza polisi kumtafuta Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema)  alisaidie jeshi hilo kuhusiana na tukio hilo. Masauni alisema hayo bungeni jana wakati akitoa taarifa za awali baada ya Msigwa kutoa hoja ya dharura kwa mujibu wa Kifungu cha 47 cha Kanuni za Bunge. Msigwa aliomba kutoa hoja ya dharura bungeni jana kwa kuliomba Bunge kusimamisha shughuli zake na kujadili kile alichokiita kukithiri kwa vitendo vya mauaji, utekaji na kupotea kwa watu huku Serikali ikiwa haitoi majibu. “Hivi karibuni katika nchi yetu kumekuwa na matukio ya mauaji, utekaji na watu kupotea, ninapozungumza leo (jana) juzi kuna kijana mmoja anaitwa Mdude Nyagali kule Mbozi ametekwa akiwa nyumbani kwake mbele ya  macho ya watu. “Alipojaribu kupiga kelele wale watu walionyesha silaha wakamkamata wakamuweka kwenye buti ya gari na kuondoka naye. “Tumekwenda kwenye vituo vya polisi wamesema siyo wao lakini wamekataa kufungua jalada. “Mheshimiwa mwenyekiti haya matukio ambayo ukiangalia huku nyuma watu wengi ambao tuliwajadili hata kwenye hotuba ya Mambo ya Ndani tulitaka serikali iji-commit yamekuwa yakiendelea… “ Sasa trend hii imekuwa ikiendelea na wajibu wa polisi na serikali ni kulinda raia na mali zao, ningeomba mheshimiwa mwenyekiti suala hili tulichukue kwa uzito wake kwa sababu watu wanapotea na serikali haitoi majibu, ningeomba kutoa hoja ili jambo hili liweze kujadiliwa,” alisema Msigwa. Kutokana na hoja ya Msigwa, Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge alitoa mwongozo wake akisema: “Suala lolote linalohusu uhai wa binadamu na wa Mtanzania ni suala zito sana, hata hivyo haimaanishi kwamba mtu anapotowekwa… hata mimi nina taarifa jimboni kwangu kuna kijana aliondoka nyumbani kwake tangu juzi hajaonekana hadi leo (jana), sasa haiwezekani mtu ameamua kwenda kwa shughuli zake halafu hakurejea, tuwe tuna…  “Lakini katika hili ambalo umesema (Msigwa) na wananchi wameona na jitihada zikafanyika lakini bado maelezo yake hayajanyooka vizuri. “Haitakuwa vizuri sisi wabunge kuanzisha mjadala ambao maudhui yake hatuyafahamu sana, .. ni vema serikali ikatoa maelezo, kama wanaweza sasa hivi au waji-comit baadaye watoe maelezo Watanzania wajue kuhusiana na hali hiyo. Baada ya maelezo hayo ya Chenge, Mnadhimu wa Shughuli za Serikali bungeni ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Jenista Mhagama aliomba mwenyekiti kuruhusu Serikali kutoa taarifa ya awali. “Ninaomba uridhie angalau kwa hatua ya awali wakati mwingine yanapotokea matukio kama hayo na serikali ikakaa kimya sidhani kama tunajitendea haki sisi serikali na wananchi kwa ujumla. “Hivyo kwa hatua hii ya mwanzo uturuhusu mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi aweze kusema kitu kama anacho cha kusema kwa hatua ya awali,” alisema. Akitoa taarifa ya serikali, Masauni alisema taarifa iliyotolewa na Msigwa bungeni haina usahihi kwa sababu  jeshi la polisi tayari limeshafungua jalada na kuanza kuchunguza suala hilo. “ Lakini kutokana na hoja hii mahsusi ambayo Mheshimiwa Msigwa ameizungumza, kwanza nataka nimsahihishe, si vizuri kumuita mbunge mwenzio ni muongo. “Lakini nimsahihishe na usahihi wa taarifa ambazo amezungumza amesema kwamba huyo mtu ametekwa na vile vile polisi wamekataa kufungua jalada kitu ambacho si sahihi. “Usahihi wa taarifa ni kama ifuatavyo:  “Ni kweli mtu huyu hakuonekana, hivyo ukisema ametekwa maana yake wewe unajua, sasa kwa sababu Mheshimiwa Msigwa amelithibitishia bunge kwamba mtu ametekwa bila shaka yeye ana taarifa, kwa hiyo nilielekeze Jeshi la Polisi wamtafute Mheshimiwa Msigwa aisaidie polisi”.  Masauni alisema mpaka sasa Jeshi la Polisi limeshafungua jalada na serikali inalichukulia kwa uzito suala hilo na  tayari imeshaanza uchunguzi. “Mpaka   hivi sasa tunavyozungumza jeshi la polisi limeshafungua jalada, si kweli kama Mheshimiwa Msigwa alivyosema na uchunguzi umeshaanza na kuonyesha serikali  imelichukulia suala hili uzito na  tumeongeza nguvu kutoka makao makuu kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa jambo hili. “Kama ambavyo tunachukua uzito kwa matukio yoyote ya uhalifu yanayotokea nchini  tutaendela kulichukulia kwa uzito kama serikali na pale ambako tutabaini kwamba tukio hili limetokea kwa njia ya uhalifu basi hatua zitachukuliwa,” alisema. Masauni pia ametaka wananchi kuacha vyombo vya dola kufanya kazi yake na kuwaonya ambao wamekuwa wakitumia mitandao vibaya kwa kuichafua serikali huku akisisitiza watu hao watachukuliwa hatua. Wakati huohuo, Chadema kimedai kusikitishwa na polisi kushindwa kuzungumzia suala hilo tangu kupotea kwa mwanachama wao mwishoni mwa wiki iliyopita. Akizungumza na waandishi wa habari   Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje, John Mrema, alisema Mdude alichukuliwa na watu wasiojulikana Mei 4, ofisini kwake Mkoani Songwe, wakati akiwa anaendelea na majukumu yake. Alisema  baada ya kutokea   tukio hilo, viongozi wa chama hicho Mkoa wa Songwe walikwenda kituo cha polisi kutoa taarifa lakini mpaka sasa hakuna taarifa zozote zilizotolewa. Alisema tukio hilo siyo la kwanza kutokea chini kwa sababu  kumekua na matukio mbalimbali ya kupotea  wananchi wakiwamo wanachama wao, lakini majibu yanayotolewa na polisi hayaridhishi, jambo ambalo limesababisha kujitokeza shaka. Alisema kutokana na hali hiyo, chama hicho kitafanya kikao maalumu  baada ya viongozi wao kumaliza ziara za mikoani na kutoa tamko la pamoja na hatua zitakazochukuliwa. “Kwa sasa viongozi wapo mikoani kwenye shughuli mbalimbali za chama, wakimaliza, watarudi na kuitisha kikao ambacho kitatoa uamuzi kuhusiana tukio hilo pamoja na matukio mengine ya kupotea kwa wananchi yanayojitokeza nchini,hali ambayo inahatarisha amani,”alisema Mrema.
1
BAKARI KIMWANGA NA RAMADHAN HASSAN-DODOMA BAADA ya kukaa gerezani kwa takribani miaka 13 wakitumikia kifungo cha maisha, mwanamuziki Nguza Viking, maarufu kama Babu Seya na mtoto wake, Johnson Nguza (Papi Kocha), hatimaye wameachiwa huru, baada ya Rais Dk. John Magufuli kutoa msamaha. Saa sita baadaye baada ya Rais Magufuli kutangaza msamaha huo, Gereza la Ukonga, Dar es Salaam liliwaachia huru Babu Seya na mwanawe. Babu Seya na mwanawe, Papii walitoka ndani ya gereza hilo saa 12:08 jioni, huku wakiwa wamebeba magitaa mgongoni. Wakiwa wameambatana na maofisa wa Jeshi hilo wenye silaha, Babu Seya, ambaye alivalia shati la rangi ya pinki na Papii yeye la drafti lenye rangi ya zambarau na bluu, baada ya kutoka walikutana na umati mkubwa, wakiwamo ndugu zao na wanamuziki King Kiki, Bushoke na wengine waliokuwa wakiwasubiri nje ya gereza. MTANZANIA Jumapili, ambalo lilifika gerezani hapo, lilishuhudia watu wanaokadiriwa kufikia 100 ambao walifunga sehemu ya barabara ya kuingilia katika geti la Magereza, huku wakiimba Nguza, Nguza, hali iliyowapa furaha Babu Seya na mwanawe. Tofauti na matarajio ya wengi, baada ya kutoka, Babu Seya na Papii hawakuzungumza chochote, zaidi waliingia katika gari dogo la rangi ya fedha aina ya Caldina namba T 670 CAW  na kisha kuelekea katika Kanisa la Life Christ Ministry, lililopo Seregerea Mwisho, ambako mtoto wake aliyeachiwa huru mwaka 2010, Nguza Mbangu, ni Mchungaji wake. Walipofika kanisani hapo waliingia ndani wakapiga picha na kisha wakaondoka, huku Nguza akiomba waachwe wakapumzike na kuahidi kuzungumza leo. Msamaha huo ambao Rais Magufuli aliutoa jana wakati akihutubia umma katika maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru yaliyofanyika mjini Dodoma, unaowagusa wafungwa 8,157, miongoni mwao wakiwa Babu Seya na mwanaye, umeacha bumbuwazi, mshangao na kicheko. Babu Seya na Papi, ambao Rais Magufuli aliwaingiza kwenye kundi la wafungwa 1,828 waliotakiwa kuachiwa huru jana hiyo hiyo, walikuwa wakitumikia adhabu hiyo tangu Juni 5, 2004, baada ya kutiwa hatiani na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa makosa ya kuwabaka na kuwanajisi watoto wa kike 10  wenye umri chini ya miaka 10. Gazeti hili la Mtanzania ndilo lililokuwa la kwanza kuripoti taarifa za kukamatwa kwa Babu Seya na wanawe watatu, akiwamo Nguza Mbangu na Francis ‘Chichi’, baada ya kufikishwa katika Kituo cha Polisi cha Urafiki, Dar es Salaam. Baada ya kukata rufaa mbili na kuambulia patupu chini ya wakili wao, Mabere Nyaucho Marando,  ile ya mwaka 2010 ambayo marejeo yake yalisikilizwa na kutolewa hukumu mwaka huo huo, Mahakama iliridhia hukumu ya kifungo cha maisha kwa Babu Seya na Papii Kocha, huku ikiwaachia huru watoto wake, Mbangu na Francis Nguza. Msamaha wao umekuja wakati tayari wamekata rufaa Mahakama ya Haki za Binadamu Afrika (AfCPHR), yenye makazi yake jijini Arusha, ambayo tayari ilikwishakutana mara tatu na kubaini kuwa, hukumu ya Babu Seya na Papii ilikuwa na kasoro. Mwanzoni mwa mwaka huu, mtoto wa Babu Seya, Mbangu, alikaririwa na gazeti moja akisema turufu ya mwisho ya hukumu ya baba na kaka yake ni mwaka huu, wakati AfCPHR itakapokuwa inatoa uamuzi wake. Jana wakati Rais Magufuli alipotangaza kuwaachia huru Babu Seya na mwanaye, si tu Uwanja wa Jamhuri uliolipuka kwa shangwe na pengine kuwaacha baadhi katika hali ya mshangao, bali hata katika maeneo mbalimbali. Msamaha huo pia umekumbusha barua ya wazi iliyowahi kuandikwa na Babu Seya mwanzoni mwa mwaka huu akiilenga kwa Rais Magufuli. Barua yenyewe ilisomeka hivi: “Nawaomba muambieni Rais Magufuli juhudi zake nazisikia, Mungu azidi kumpa  maarifa zaidi azidi kuliongoza jahazi la Watanzania. Rais huyu nimependa hekima zake, nami namfananisha na mwandishi wa makala za kitabu cha Methali na Muhubiri Nabii Suleimani, mwambieni Rais nimeiweka akiba yangu ya tumaini la mwisho kwake, kwani Mungu ndiye Mfalme wa kwanza anayeweza kumaliza msiba wangu huu wa kuishi kwenye kuta za magereza. Ni yeye John Joseph anayeweza kunitenganisha mimi na maisha ya gereza, sipendi ndoto yangu ya kuja kufia gerezani, naichukia kama tawala za Herode pale Galilaya, naumwa na huku hakuna makaburi mazuri ya kuzika wafu wetu. Mwambieni anisaidie, japo nije nifie mikononi mwa mama yangu tu aliyeteseka ‘leba’ kwa kumwaga damu zake nyingi wakati akinizaa, kama ikishindikana sio mbaya. ‘You can see my dead body through my window coffin’, mtaweza kushuhudia maiti yangu yenye pamba masikioni na puani ikiwa ndani ya jeneza langu kupitia upenyo wa dirisha la jeneza hilo, nimekinai na huku nimejifunza mengi. Siku nitakapotoka ndiyo siku nitakapolivaa joho la uchungaji na kupita mitaani nikilihubiri neno la Mungu mpaka jasho langu ligeuke damu, natumaini katika mkono wa Bwana, natumaini katika mkono wa John Joseph haleluya! Tunaonana madhabahuni thank you! Kila la heri Banza Stone RIP, kaka Ndanda Kosovo RIP, Amina Ngaluma (Japanese) RIP, Kakaangu Amigolasi RIP, kaka MCD RIP na wanamuziki wote mlioniacha nikiendelea kuishi kwenye kuta za gereza, Kiss you, bye!” Kabla ya waraka huo kwa Rais Magufuli, Babu Seya na mwanawe, Juni 2014 walimwomba Rais wa wakati huo, Jakaya Kikwete awasamehe. Walitoa ombi hilo kupitia wimbo wakati wakitumbuiza katika maadhimisho yaliyofanyika katika Chuo cha Magereza Ukonga. Papii huku akionyesha mikono kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu kububujikwa na machozi aliimba; “Kosa gani tusilosamehewa, vifungo miaka 30 jela havifundishi. “Waziri Chikawe (Waziri wa Mambo ya Ndani wa wakati huo) tunaomba umfikishie Rais Jakaya Kikwete ombi letu, mwambie atusamehe, hata Yesu alimkana Yesu mara tatu lakini alimsamehe, kwanini sisi?” KAULI YA RAIS MAGUFULI Akihutubia jana mjini hapa katika kilele cha miaka 56 ya Uhuru, Rais Dk. Magufuli, alisema ameamua kutekeleza kwa vitendo Ibara ya 45 ya Katiba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huku akinukuu ibara hiyo alisema; “Bila kuathiri masharti mengine katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais anaweza kutenda lolote kati ya mambo yafuatayo: “A. Kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama kwa kosa lolote na anaweza kutoa msamaha huo ama kwa masharti au bila sharti lolote kwa mujibu wa sheria. “B. Ibara hiyo pia inasema, Rais anaweza kumuachia kabisa mtu yeyote aliyehukumiwa au kuadhibiwa kwa kote lolote ili mtu huyo asitimize adhabu hiyo wakati wa muda maalumu na C, kulingalinisha adhabu ili adhabu tahfif, waswahili wanajua tafsiri yake vizuri, kina Kikwete (Rais mstaafu wa Awamu ya Nne), sisi wa Bara hapa ni kazi ngumu,” alisema Rais Magufuli. Alisema Tanzania ina wafungwa 39,000 hadi kufikia juzi ambapo kati yao, 37,000 ni wanaume na 2,000 ni wanawake. Alisema waliohukumiwa kunyongwa ni 522, ambapo kati yao, 503 ni wanaume na 19 ni wanawake. “Waliohukumiwa kifungo cha maisha ni 666, ambapo kati yao wanaume ni 655 na 11 ni wanawake. Kwa mujibu wa ibara hii ya 45 na hasa kwa kuzingatia kuwa sisi ni binadamu. “Nimeamua kuwasamehe wafungwa 8,157 ambapo wafungwa 1,828 watatoka leo (jana) na 6,329 wamepunguziwa muda wa kukaa gerezani na watatoka kwa mujibu wa vifungo vyao. Lakini pia kwa mujibu wa ibara hiyo hiyo ya 45, wapo waliohukumiwa kunyongwa, wapo wenye umri zaidi ya miaka 85. Pia wapo wafungwa ambao waliotubu kweli dhambi zao. “Ndugu zangu baada ya kukaa na kufikiria na kwa sababu sisi wanadamu kila siku huwa tunaomba kusamehewa. Nimeguswa ndugu zangu Watanzania na hasa ukiangalia hawa waliofikisha mpaka miaka 85 ni wazee na hii nimepata taarifa ya magerezani,” alisema. Rais Magufuli pia alisema ameamua kuwasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa na kuwataka wahusika wafanye mchakato wa kuwatoa jana au leo. “Yupo mzee mmoja anaitwa Mganga Matonya ana miaka 85 na amekaa gerezani miaka 37 na mahabusu miaka 7, ukimjulisha hii utaona amekaa gerezani miaka 44. Ninaomba orodha hii nitamkabidhi Waziri Mkuu awashughulikie,” alisema. IBARA ILIYOTUMIKA KUMSAMEHE BABU SEYA NA MWANAWE Rais Magufuli pia alitumia ibara hiyo hiyo ya 45 kutoa msamaha kwa familia ya Babu Seya. “Kwa mujibu wa ibada hii ya 45, pia ninatoa msamaha wa kuachiwa huru familia ya Nguza Viking, jina lingine anaitwa Babu Seya na mwanawe ndugu Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ nao waachiwe huru,” alisema. Rais Magufuli alionya na kusema kuwa msamaha huo hautawahusu wale waliofanya vitendo vya mauaji ya watu wenye ualbino pamoja na ujambazi. MREMA KUMTEMBELEA BABU SEYA Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Augustino Mrema, mbali na kumpongeza Rais Magufuli kwa kufanya uamuzi aliouita kuwa ni wa kihistoria, alisema atakwenda kumtembelea Babu Seya nyumbani kwake. Mrema, ambaye alizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, mbali na kusema Babu Seya ni kama ndugu yake kutokana na kuishi pamoja katika eneo la Sinza, alisisitiza juu ya nguvu ya kusamehe. “Wengine wamekwishaanza kusema Rais Magufuli amevunja sheria, huu ni unafiki, wasome Katiba inampa Rais Mamlaka ya kubadili kifungo cha kunyongwa kuwa cha maisha, Babu Seya hata kama alifanya kosa amekwishajutia, tujifunze kusamehe tusiishi kwa chuki na visasi,” alisema Mrema. Katika hilo, Mrema alisema Rais Magufuli ameonyesha ubinadamu na anaamini kutokana na hulka yake ya udadisi amethubutu kuingia magereza na kuona shida nyingi, ikiwamo msongamano wa wafungwa. Alisema wao kama Bodi ya Parole, moja kati ya mambo ambayo waliamua kushughulikia ipasavyo ni suala la msongamano wa wafungwa, lakini kwa bahati mbaya walikwamishwa. “Mimi nilijaribu hilo, tulikwenda Gereza la Isanga, Dodoma tuligundua kuna wafungwa 80 ambao walishindwa kulipa faini wakafungwa, nikamtafuta Mchungaji Getrude Rwakatare akakubali kutoa milioni 12  tukahesabu wakapatikana 43 wa kuwalipia tukaenda nao mahakamani, mahakama ikakubali, lakini baadaye wakakataliwa eti nikaambiwa hawawezi kujutia makosa, labda hiyo faini ilipwe na ndugu zake, nikajiuliza hao ndugu zake ni akina nani?” alisema Mrema na kusisitiza kuwa, kule gerezani kuna mawazo potofu. Mrema alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa kuliona hilo, na kutumia Katiba na kufanya maamuzi pasipo kuogopa lawama. Alipoulizwa anazungumziaje endapo Rais Magufuli akitumia mamlaka hayohayo kuwaachia huru masheikh wa Uamsho waliopo gerezani wanaotuhumiwa kwa ugaidi, Mrema alisema kwa kuwa suala hilo ni tatizo kubwa la kidunia, anaamini Rais Magufuli hawezi kukubali mtu awekwe ndani bila sababu za msingi na kushauri atumie vyombo vyake kuchunguza jambo hilo. Awali akizungumza katika uwanja wa Jamhuri mkoani hapa, mara baada ya Rais Dk. Magufuli kutangaza kuipa msamaha familia ya Babu Seya, Mkurugenzi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka, alisema alilia mara baada ya Rais Magufuli kutamka msahama dhidi ya Babu Seya na mwanawe. “Nimelia, nimetoa machozi ya furaha, Rais amefanya jambo jema sana, kila mmoja alikuwa akimwombea Babu Seya ili aweze kutoka, hakika ameifanya nchi yetu iheshimike sana nje ya nchi,” alisema. Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Molel (CCM), alisema Serikali ilikuwa ikitumia fedha nyingi kwa ajili ya kulisha wafungwa, hivyo kitendo cha Rais Dk. Magufuli kutoa msamaha ni kizuri. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alimpongeza Rais Dk. Magufuli kwa kutoa msamaha kwa wafungwa, huku akimtaka kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania. “Ni vizuri, ni vizuri sana, amefanya jambo zuri, hakika huu ni uungwana, ila bado tuna changamoto nyingi katika miaka yetu hii 56, kwani takwimu zinaonesha asilimia 33 ya watoto wana utapiamlo,” alisema. WIZARA YAFAFANUA MSAMAHA WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi ilitoa taarifa na kufafanua msamaha ambao Rais Magufuli aliutangaza kwa wafungwa 8,157. Taarifa  iliyotolewa jana kwa vyombo vya Habari na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali mstaafu Projest Rwegasira, ilieleza kuwa, kati ya hao 6,329 watabaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya kupewa msamaha huo. Akifafanua zaidi, alisema Ibara ya 45(1) (d) ya Katiba ndiyo inampa mamlaka Rais kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa ajili ya kosa lolote au kufuta adhabu yote. Katika taarifa hiyo, Rwegasira alisema kuwa, wafungwa wengine waliosamehewa ni wale wenye magonjwa kama Ukimwi, Kifua Kikuu (TB) na saratani, ambao wako kwenye hatua za mwisho ambao walipaswa kuthibitishwa na jopo la waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya. Alisema wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini (70) au zaidi.  Umri huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya. Alisema msamaha huo pia unawahusu wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani, pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya. “Wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili. Ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga chini ya uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya,” alisema Meja Jenerali mstaafu Rwegasira. Meja Jenerali mstaafu Rwegasira alisema msamaha wa Rais hautawahusu wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa au kwa makosa ya kujaribu kuua. Wengine ni wale waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani. Aliwataja wengine kuwa ni waliohukumiwa kifungo cha maisha gerezani, wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kujihusisha na usafirishaji na matumizi ya madawa ya kulevya kama vile cocaine, heroin, bangi n.k. Alisema pia hauwahusu wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kujihusisha na uombaji na upokeaji au utoaji rushwa, wanaotumikia kifungo kwa makosa ya unyang’anyi na unyang’anyi wa kutumia silaha au kujaribu kutenda makosa hayo. Alisema wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya kupatikana na silaha, risasi au milipuko isivyo halali na wale wa kifungo kwa makosa ya shambulio la aibu, kunajisi, kubaka na kulawiti, ukatili kwa watoto au kujaribu kutenda makosa hayo pia haitawahusu. Alisema msahama huo pia hauwahusu waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa kosa la kuwapa mimba wanafunzi wa Shule za Msingi na Shule za Sekondari na ambao walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa miaka kumi na nane (18) na kuendelea. Aliwataja wengine ambao hawaguswi na msahama huo kuwa ni wanaotumikia kifungo kwa makosa ya wizi wa magari na pikipiki, uharibifu wa miundombinu au kujaribu kutenda makosa hayo. Wengine ni wale wanaotumikia kifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole na Sheria ya Huduma kwa Jamii na waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yao na kuhujumu uchumi. Alisema msamaha huo pia hautawahusu wafungwa waliowahi kupunguziwa kifungo na msamaha wa Rais na bado wangali wanaendelea kutumikia sehemu ya kifungo kilichobaki. Wafungwa wengine ambao hawataguswa ni wale waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kuzuia watoto kupata masomo, hatia na kuhukumiwa kwa kosa la utekaji wa watoto, kupoka na kufanya biashara ya binadamu. Alisema wasioguswa pia ni wale waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kukutwa na viungo vya binadamu, vifungo kwa makosa ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za Serikali na ujangili. Aliwataja wengine kuwa ni wanaotumikia vifungo kwa makosa ya wizi/ubadhirifu wa fedha za Serikali, wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya ulinzi halali, walioingia gerezani baada ya Oktoba 30, 2017 na waliowahi kufungwa gerezani. Naye Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Bahame Tom Nyanduga, alimpongeza Rais Dk. Magufuli kwa kuwafutia adhabu ya kifo watu 61 waliokuwa magereza mbalimbali nchini, wakisubiri utekelezaji wake. Nyanduga alisema uamuzi huo unaendana na Azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Na. 62/149 la Desemba 18, 2007 linalozitaka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kufuta au kusimamisha utekelezaji wa adhabu ya kifo na kuweka adhabu mbadala.
1
LIVERPOOL, ENGLAND BAADA ya Manchester City kupokea kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Everton katika michuano ya Kombe la Capital One hatua ya nusu fainali, kocha Manuel Pellegrini, amemtupia lawama mwamuzi wa mchezo huo, Bobby Madley. Mchezo huo ambao ulipigwa kwenye Uwanja wa Goodison Park, ambayo ni nusu fainali ya kwanza, Pellegrini amedai kwamba Everton walibebwa kwa kiasi kikubwa. Pellegrini amesema mwamuzi wa kati, Bobby Madley na wasaidizi wake walishindwa kuumiliki mchezo huo hasa katika bao la kwanza ambalo lilifungwa na Romelu Lukaku. “Nimechukizwa sana na matokeo hayo, kwa kuwa hauwezi kuwa na furaha wakati umepoteza mchezo lakini ninaamini hatukustahili kupoteza mchezo huo kwa kuwa bao lao la kwanza lilikuwa wazi ni lakuotea. “Lukaku alikuwa mbele kabisa bila beki yeyote, lakini ninashangaa kuona waamuzi wakiwa kimya wakati ilikuwa wazi kwamba Lukaku ameotea, kila mtu aliliona hilo. “Hata hivyo, tulistahili kupata penalti baada ya Jesus Navas kuchezewa vibaya katika eneo la hatari, lakini kikubwa ni kujipanga na mchezo ujao tukiwa nyumbani ili kuhakikisha tunasonga mbele,” alisema Pellegrini.
2
Na Kulwa Mzee-Dar es Salaam MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imeyatupa maombi ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ya kutaka asikamatwe na kuwekwa kizuizini, hadi maombi yake yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi. Wakili Jenerali Ulimwengu ameungana na Wakili Peter Kibatala kumwakilisha Mbowe mahakamani. Maombi ya Mbowe yalitupwa jana na jopo la majaji watatu, Jaji Sakieti Kihiyo, Jaji Lugano Mwandambo na Jaji Pellagia Khaday baada ya kukubaliana na pingamizi la awali lililowasilishwa na Jamhuri. Akisoma uamuzi huo, Jaji Mwandambo alisema maombi yaliwasilishwa kimakosa chini ya kifungu namba 2(3) cha Sheria ya Jala (Sheria ya Usimamiaji Haki na Matumizi ya Sheria). “Kifungu cha sheria kilichotumika si sahihi kwa sababu sheria hiyo hutumika pale ambapo sheria zetu ziko kimya, waleta maombi watafute vifungu sahihi vya kuwasilisha maombi mahakamani,”alisema. Alisema sababu hiyo moja ni ya msingi hivyo mahakama inayatupa maombi na kesi ya kikatiba itasikilizwa Machi 8 mwaka huu. Katika maombi hayo yaliyotupwa Mbowe aliomba mahakama itoe amri asikamatwe wala kuwekwa kizuizini mpaka maombi yake ya zuio yatakaposikilizwa na kutolewa uamuzi. Hata hivyo Wakili Ulimwengu alidai watasoma sheria za Uingereza kuangalia vifungu ambavyo vitasaidia kuyarudisha maombi hayo mahakamani. “Tutatumia siku ya leo na kesho….kesho tutawasilisha maombi haya mahakamani,” alidai. Kabla ya maombi hayo kuanza kusikilizwa Wakili wa Serikali Mkuu, Gabriel Malata aliwasilisha pingamizi, akiomba mahakama iyatupilie mbali kwa sababu  yako nje ya muda, hayana msingi na kifungu cha sheria kilichotumika si sahihi. Wakili huyo, alidai mahakama hiyo ni ya madai, hivyo haina mamlaka ya kusikiliza masuala ya jinai. Alidai suala la Mbowe kukamatwa na Polisi ni la kijinai na Polisi wamefanya kazi yao kwa mujibu wa sheria hivyo maombi hayo hayakupaswa kupelekwa katika mahakama hiyo badala yake walitakiwa kuyapeleka kwenye mahakama husika. Katika kesi ya kikatiba namba 1ya 2017, mdai ni Mbowe na wadaiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Ofisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.  Katika kesi hiyo ya katiba, Mbowe anaomba Mahakama Kuu itamke   kuwa Mkuu wa Mkoa hana mamlaka ya kudhalilisha na kukamata. Mbowe pia anaomba mahakama itengue vifungu vya 5 &7 vya Sheria ya Tawala za Mitaa kwa kuwa ni batili na vinakiuka haki ya katiba.
1
['Bruno Fernandes, 25, ameambia Sporting Lisbon anataka kujiunga na Man United na mazungumzo zaidi yamepangwa wiki hii baada ya kugonga mwamba kuhusu thamani ya mchezaji huyo wa Portugal. (Sky Sports)', 'Beki wa Paris St-Germain na Ufaransa Layvin Kurzawa, 27, atajiunga na Arsenal kwa uhamisho wa bila malipo wakati kandarasi yake itakapokamilika mwezi Juni na amekubali mkataba wa miaka mitano na The Gunners.. (France Football - in French)', 'Arsenal itajaribu kumsaini beki wa Bayern Munich na Ujerumani Jerome Boateng, 31, kwa mkopo mwezi Januari kabla ya kuwasilisha ombi la £50m ili kumnunua beki wa kati wa Ufaransa na klabu ya RB Leipzig Dayot Upamecano, 21, mwisho wa msimu. (Star)', 'Inter Milan inataka kumsajili kiungo wa kati wa Tottenham na Denmark Christian Eriksen, 27, kwa wakati mzuri ili aweze kushiriki katika mechi ya ligi ya Serie A dhidi ya klabu ya Cagliari mnamo tarehe 26 mwezi Januari. (Mail)', 'Afisa mkuu wa klabu ya Inter Beppe Marotta anasema kwamba klabu hiyo ina hamu ya kumsaini winga wa Chelsea Victor Moses, 29, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo katika klabu ya Fenerbahce, pamoja na mshambuliaji wa klabu hiyo Olivier Giroud, 33, mbali na Eriksen. (Sky Sports)', 'Antonio Conte amemshutumu Jose Mourinho kwa kubadilisha maneno yake baada ya mkufunzi huyo wa Spurs kumkosoa mwenzake wa Inter kwa kuzungumzia kuhusu mchezaji wake Eriksen. (Mirror)', 'Inter Milan pia ina hamu ya kumsaini kiungo wa kati wa Croatia Luca Modric , 34, kutoka Real Madrid(Sport - in Spanish)', "Atletico Madrid imeipatia Paris St-Germain Yuro milioni 10 (£8.5m) ili kumnunua mshambuliaji wa Uruguay Edinson Cavani, 32. (L'Equipe - in French)", 'Tottenham huenda ikamnunua mshambuliaji wa Leicester na Algeria Islam Slimani, 31, ambaye kwa sasa anacheza Monaco kwa mkopo. (Telegraph)', 'Leicester na Aston Villa zinamlenga mshambuliaji wa Ufaransa Serhou Guirassy, 23, kutoka klabu ya Ligue 1 Amiens mwezi Januari. (Mail)', 'Maombi ya Manchester City na Barcelona ya kutaka kumsajili beki wa kati wa Inter Milan Alessandro Bastoni, 20, yamekataliwa. (La Gazetta dello Sport - in Italian)', 'Liverpool inafikiria kumsajili kinda wa Portugal na klabu ya Nice mwenye umri wa miaka 17 Pedro Brazao. (RMC Sport, via Mail)', "Klabu ya Lyon ina hamu ya kumsajili beki wa Athletico Bruno Guimaraes, 22, ambaye pia ameripotiwa kunyatiwa na Arsenal. (L'Equipe - in French)", "Real Madrid itatangaza usajili wa dau la 30m euro (£25.6m) la mchezaji wa Flamengo's Reinier Jesus siku ya Jumatatu wakati ambapo kiungo huyo wa kati wa Brazil amefikisha miaka 18. (AS)"]
2
['Mkufunzi wa Man United Ole Gunnar Solskjaer anahofia kwamba hatma ya kazi yake itakuwa haijulikani iwapo timu yake itashindwa kwa mabao mengi ugenini Liverpool.(Mail)', 'Baadhi ya wachezaji wamepoteza matumaini na raia huyo wa Norway anaamini baadhi yao wamekataa kumsikiliza. (Sun)', 'Solskjaer anahitaji kitita cha £300m kutumia katika dirisha lijalo la uhamisho na kumnunua mshambuliaji kama vile mshambuliaji wa Tottenhama na England Harry Kane,26, kulingana na winga wa zamani Lee Sharpe. (Talksport)', 'Kane anafaa kuondoka Tottenham na badala yake kuhamia Manchester City, kulingana na beki wa zamani wa England Glen Johnson. (Betdaq, via Independent)', 'Liverpool huenda ikapokea kitita cha £4.5m kati ya kile cha £84m wanazodaiwa na Barcelona baada ya kumnunua kiungo Philippe Coutinho, 27, ambaye alihamia Nou Camp mwaka 2018. (Mirror)', 'Everton inafikiria kumnunua mchezaji anayelengwa na Manchester United Moussa Dembele katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari. Mshambuliaji huyo wa Ufaransa , mwenye umri wa miaka 23 anaweza kugharimu £40m kutoka Lyon. (Star)', 'Chelsea na mshambuliaji wa Marekani Christian Pulisic, 21, amekiri kukasirishwa kwake kwa kukosa muda wa kucheza zaidi tangu uhamisho wake wa £58m kutoka Borussia Dortmund. (Guardian)', 'Mshambulaji wa Arsenal Gabriel Martinelli, 18, anakabiliwa na chaguo katika hatma yake ya kimataifa kwa kuwa anahitajika na Itali pamoja na Brazil. Alizaliwa nchini Brazil lakini lakini babake ni raia wa Itali hivyobasi anaweza kuwakilisha timu zote mbili.. (Mirror)', 'Mshambuliaji wa Venezuela Salomon Rondon, 30, amekiri kwamba angependelea kuandikisha mkataba wa kudumu na klabu ya Newcastle lakini akasema kwamba hakupatiwa fursa kubadili uhamisho wake wa mkopo wa msimu uliopita kuwa kandarasi ya kudumu na hivyobasi akaelekea katika klabu ya China ya Dalian Yifang. (Newcastle Chronicle)', 'Mkufunzi Roy Hodgson anasema kwamba klabu ya Crystal Palace italazimika kumsaini mshambuliaji mpya mwezi januari iwapo wanataka kumaliza katika orodha ya timu sita za kwanza katika jedwali na pia analenga kuwasajili mabeki wawili wapya wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa. (Standard)']
2
MADRID, HISPANIA MSHAMBULIAJI wa timu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Wales, Gareth Bale, jana alitajwa kuwa katika kinyang’anyiro cha tuzo ya Ballon d’Or ya mchezaji bora wa mwaka 2016. Tuzo hiyo inayotolewa kila mwaka, pia ilimtaja mshambuliaji mwingine wa Madrid, Cristiano Ronaldo, kuwania mwaka huu pamoja na  mshambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero, Borussia Dortmund,  Pierre-Emerick Aubameyang na kipa wa Juventus, Gianluigi Buffon. Kwa mujibu wa jarida la France Football  linaloandaa tuzo hiyo, limewataja jumla ya wachezaji 30 katika kinyang’anyiro hicho na kutarajia kuwapunguza wachezaji watano kila baada ya saa mbili kuanzia jana. Tuzo hiyo imekuwa ikitolewa na jarida hilo kila mwaka tangu mwaka 1956, lakini kwa miaka sita ya hivi karibuni ilikuwa ikitambulika kama Fifa Ballon d’Or kutokana na ushirikiano uliokuwapo na Bodi ya Shirikisho la Soka la Kimataifa. Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi, alishinda tuzo hiyo mwaka uliopita na kuweka rekodi ya kushinda mara tano. Mara ya mwisho mchezaji aliyeshinda zaidi ya Messi au Ronaldo ilikuwa mwaka 2007 wakati aliyekuwa mchezaji wa AC Milian, Ricardo dos Santos ‘Kaka’ kushinda tuzo hiyo. Wachezaji watano wa Ligi Kuu England waliowahi kutajwa katika tuzo hiyo ni  mchezaji wa  Manchester City, Yaya Toure, Aguero na Kevin de Bruyne na Arsenal, Alexis Sanchez na Chelsea,  Eden Hazard. Wakati wachezaji wa Manchester United ni Paul Pogba na Zlatan Ibrahimovic ambao wamejumuishwa kabla ya kujiunga na timu hiyo.
2
Na  PENDO FUNDISHA-MBEYA JESHI la polisi mkoani Mbeya limewafukuza kazi  polisi wawili  kwa   kukiuka maadili ya kazi baada ya kuwafanyia vitendo vibaya wanafunzi wa kike wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Isuto  iliyopo Mbeya vijijini. Askari hao ni PC Petro Mgana mwenye namba H 4925 wa kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Mbeya (FFU) na PC Lukas Ng’weina wa Wilaya ya Polisi Mbalizi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea November 15 usiku,   katika Shule ya Sekondari ya Isuto iliyopo Kijiji na Kata ya Isuto Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Polisi   Mbalizi. Alisema inadaiwa   askari hao kwa pamoja wakiwa kwenye ulinzi wa mitihani ya taifa ya kidato cha nne ya mwaka huu,  waliwatoa kwenye hosteli wanafunzi wa kike kwa kile walichodai kuwa walikuwa wanapiga kelele. “Baada ya kuwatoa wanafunzi hao nje, waliwapeleka eneo la foleni na kuwapa adhabu zikiwamo kupiga push up, kuruka kichura, kushika masikio na kuwachapa viboko,”alisema. Alisema  adhabu hizo ziliwasababishia maumivu makali na baadhi yao kuondoka shuleni kurudi  nyumbani kwao. “Baada ya vitendo hivyo, jeshi la polisi limewachukulia hatua za  nidhamu askari hao kwa kuwafukuza kazi kuanzia tarehe 08.11.2016 na baadaye watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika,”alisema. Hata hivyo, habari zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kwamba  Magana  amelitumikia jeshi hilo kwa miezi minne tu tangu afuzu mafunzo yake katika Chuo Cha polisi Moshi (CCP) huku Lukas akiwa amekwisha kuilitumikia kwa miaka miwili.
1
MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amewataka wazazi na walezi wilayani Karatu kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule hata kama hawana sare za shule.Aidha ameagiza uongozi wa serikali ya kijiji cha Lositete kuchukuliwa maelezo na polisi kuhusu sababu za kutochangia maendeleo ya elimu, badala yake wanaingiza siasa na kusababisha saruji kuganda.Gambo ametoa agizo hilo leo katika kijiji cha Lositete, kata ya Mbulumbulu wilayani Karatu alipokwenda kukagua hali halisi ya madarasa pamoja na idadi ya wanafunzi walioanza masomo ya kidato cha kwanza.Ameagiza hivyo kutokana na taarifa ya Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Upper Kitete, Josephat Mau iliyodai kuwa wanafunzi tisa kati ya 171 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza shuleni hapo wameripoti shule.Mwalimu Mau amesema wanafunzi hao 162 hawajaripoti shuleni hapo kutokana na kukosekana na sare za shule huku walioripoti wakiwa ni tisa kwa sababu ya wazazi au walezi wao kutouza maharage kwani hakuna soko.Baada ya mwalimu huyo kutoa taarifa hiyo, Gambo aliagiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza kuripoti shuleni na nguo za nyumbani hata kama hawana sare ili waendelee na masomo wakati wazazi wao wakisubiri kuwanunnulia mahitaji ya shule."Rais ameagiza elimu bure hivyo wazazi au walezi watoeni watoto wenu majumbani ili waende shule bila ya kuwa na sare za shule huku mkiendelea kutafuta sare lakini pia nasisitiza nyie wananchi acheni kuingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo, "amesema.Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Lositete na Upper Kitete, Gambo aliagiza mwenyekiti wa kijiji cha Upper Kitete, William Safari pamoja kuhakikisha wanasoma mapato na matumizi ya kijiji ambayo wananchi wanadai hawajasomewa tangu mwaka 2017 hadi mwaka jana.Awali, baadhi ya wananchi walidai kuwa wameshindwa kujenga madarasa pamoja na maabara kwa sababu walichanga fedha ambazo inadaiwa zililiwa na aliyekuwa mkuu wa shule hiyo, Andrew Sulle.Anadaiwa kuchukua Sh milioni nane.Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo amesema wananchi zaidi wa vijiji vya Lositete na Upper Kitete wanapenda kuingiza masuala ya siasa katika maendeleo.Amesema amejitahidi kutatua changamoto zao ikiwamo kuhakikisha mwalimu huyo anachukuliwa hatua za kinidhamu na ameshahukumiwa kifungo.Amesema wanafunzi 5,313 walifanya mtihani wa darasa la saba mwaka jana huku wanafunzi 4,000 sawa na asilimia 75.3 walifaulu.Wanafunzi 3,446 wamepangwa kwenye shule za kata zilizokuwa na madarasa 83 na wanafunzi 539 walikosa nafasi.Alisisitiza kuwa wanafunzi hao 539 waliokosa nafasi hivi sasa wameshaanza masomo katika shule mbalimbali za wilaya hiyo kutokana na kubainika kuwapo shule ambazo wanafunzi hawakupangwa.Alisema wanaandika barua kwa wadau na kuhamasisha wanananchi kujenga madarasa pamoja na kukarabati viti na meza ili wanafunzi waweze kusoma.
1
Kibaha JESHI la Polisi mkoani Pwani linamshikilia mkazi wa mtaa wa Vitendo katika kata ya Misugusugu wilayani Kibaha, Pwanim, Robison Ernest (33) kwa tuhuma za kumwua kwa kumnyonga mtoto wake wa Modesta Robison miezi sita akidai kuwa si mwanae.Inadaiwa kuwa Ernest ambaye ni fundi ujenzi alifanya kitendo hicho cha kinyama wakati mama wa mtoto huyo akiwa sokoni kwa ajili ya kununua mahitaji ya nyumbani.Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amesema kuwa baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho, aliuficha mwili chini ya uvungu wa kitanda kisha huku baba huyo akihamia chumba kingine.Akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha leo Jumanne (Aprili 2, 2019), Kamanda Nyigesa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Aprili Mosi, mwaka huu majira ya saa 4:30 asubuhi kwenye mtaa huo.
1
Na RENATHA KIPAKA-BUKOBA MKUU wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu, ameyataka mashirika mbalimbali pamoja na wananchi kujitolea katika zoezi la kuchangia damu kwa hiyari. Alitoa kauli hiyo juzi wakati akipokea vinywaji kutoka katika tasisi za kifedha za CRDB, NMB pamoja na kiwanda cha kahawa Tanica ambapo alisema  kuchangia damu kuna faida kubwa sana  ikiwemo kufahamu hali ya afya pamoja na kujua kundi la damu ulilonalo. “Niwatake wananchi wote pamoja na mashirika kushiriki katika kampeni hii kwa hiyari ili kila mtu ahusike katika kuhakikisha hosipitali zetu zina akiba ya kutosha ya damu,” alisema Kijuu. Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Kagera, John Mwombeki, alisema malengo ya kuwepo kampeni hiyo ni maandalizi ya kuwa na damu ya kutosha katika kipindi hiki cha sikukuu kwani kipindi hicho kuna  wahitaji wengi wa damu hivyo maandalizi ya kutosha yanahitajika. “Damu inayohitajika ni uniti 900, hivyo kila wilaya inatakiwa kukusanya uniti 100 na kwa timu ya mkoa nayo inatakiwa kuwa na uniti 100 ambayo itasaidia kupunguza uhitaji wa damu,” alisema Mwombeki. Mwombeki alisema damu imekuwa ikipatikana shuleni na katika majeshi sasa mwanafunzi wapo likizo na majeshi pia wapo likizo, hivyo itakuwa vigumu kuwasaidia wahitaji usipofanyika utaratibu mapema na kuwaomba wananchi mmoja mmoja kujitokeza ili kuchangia damu kwa hiyari. “Kama tunavyojua wahitaji wakuu wa damu ni akina mama wanaofanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua, watoto wenye umri chini ya miaka mitano pamoja na wahanga wa ajali za pikipiki na magari, hivyo damu ni muhimu sana,” alisema Mwombeki
5
BAADA ya mshiriki kutoka Uganda, Kakunda kujiondoa katika shindano la Maisha Plus East Afrika 2016, mshiriki mpya kutoka Uganda, Ronald Mutebi, ameripoti katika kijiji hicho huku akidai kwamba ana aleji ya ugali. Kuongezeka kwa mshiriki huyo ambaye alishinda katika usaili wa Uganda lakini alichelewa kupata taarifa ya kufika kijijini, kumeongeza idadi ya washiriki kutoka Uganda kufikia watatu  baada ya mmoja wao kuyaaga mashindano hayo. Washiriki wengine wanabaki kuwa kama walivyokuwa ambapo Kenya (4), Uganda (3), Burundi (4), Rwanda (4), isipokuwa Tanzania kupungukiwa na mshiriki mmoja kutoka Zanzibar aliyejitoa kutokana na tatizo la ugonjwa, hivyo kubaki washiriki 15.
4
  Na JANETH MUSHI -ARUSHA MAWAKILI wanaomtetea Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) katika kesi ya kuhamasisha watu kukusanyika na kufanya maandamano kinyume cha sheria, wameomba shauri hilo kuhamishiwa Mahakama Kuu mbele ya jopo la majaji watatu kutokana na kuwapo kwa masuala ya kikatiba kwenye hati ya mashtaka. Lema anashikiliwa katika mahabusu ya Gereza Kuu la Kisongo kwa zaidi ya miezi miwili, baada ya kukosa dhamana ya kesi mbili (namba 440 na 441) za uchochezi dhidi ya Rais Dk. John Magufuli. Alikamatwa Novemba 2, mwaka jana. Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Benard Nganga, kesi hiyo namba 352 ya mwaka jana, ilitarajiwa kuanza kusikilizwa jana kwa shahidi wa kwanza, Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha (RCO), George Katabazi kutoa ushahidi wake ambao ulikwama, baada ya wakili wa utetezi kudai kuwa na hoja za kisheria. Katika kesi hiyo ambayo Lema anadaiwa kuhamasisha maandamano ya Ukuta yaliyopangwa kufanyika Septemba mosi, mwaka jana, upande wa Lema unawakilishwa na mawakili John Mallya na Sheck Mfinanga, huku Jamhuri ikiwakilishwa na Wakili Alice Mtenga. Wakili Mallya, alidai kuwa masuala ya kikatiba ambayo yamehusishwa kwenye hati ya mashtaka katika mahakama hiyo ya chini mashahidi wa upande wa jamhuri hawataweza kujibu pale watakapokuwa wanahojiwa na mawakili wa utetezi.
1
Aveline Kitomary, Dar es Salaam Mmoja wa pacha waliotenganishwa nchini Saudi Arabia na kurejea nchini Agosti 30, mwaka huu, Anisia Bernard, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 3. Daktari aliyekuwa akiwahudumia watoto hao, Dk. Petronila Ngiloi amesema chanzo cha pacha huyo kupoteza maisha ni baada ya kutapika kwa muda mrefu na matatizo kwenye utumbo hali iliyosababisha kupoteza maji mengi na kushindwa kula chakula. “Tangu walivyotoka safarini mmoja alionekana hakuwa na hali nzuri na tulivyotoka uwanja wa ndege tulikwenda moja kwa moja hospitali kumfanyia uchunguzi baada ya kuanza kutapika na kupandisha homa, hali hiyo iliyosababisha ashindwe hata kula lakini tukiwa kwenye ndege alikuwa anatapika. “Hata hivyo vipimo ulioonesha kulikuwa na hitilafu kwenye utumbo ulikuwa umejikunja tulimfanyia upasuaji lakini hali iliendelea kuwa mbaya na baadaye kupoteza maisha akiwa ICU,” amesema Dk. Ngiloi. Pacha hao Anisia na Melnes, walizaliwa January 29, mwaka jana wakiwa wameungana huko Misenyi mkoani Kagera na kupelekwa nchini Saudi Arabia kwa ajili ya kutenganishwa kazi iliyofanikiwa na kurudishwa nchini Agosti 31, mwaka huu.
1
TUHUMA nne zimemtia hatiani Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita (pichani), ambapo yeye amesema ‘Maji yamenifi - ka shingoni’.Tuhuma hizo ni zilizotajwa kwenye ripoti, iliyowasilishwa jana na kusomwa na Mkurugenzi wa Jiji, Sipora Liana, inayotaka kumng’oa madarakani meya huyo. Mwita ni Diwani wa Kata ya Vijibweni wilaya ya Kigamboni kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ripoti hiyo imemtia hatiani kutokana na kukabiliwa na tuhuma nne, ambazo ni kutotumia Sh bilioni 5.8 za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA).Fedha hizo ni asilimia 51 ya hisa zilizotolewa na Kampuni ya Simon Group, kama sehemu ya ununuzi wa asilimia 51 ya hisa za UDA. Tuhuma nyingine ni kutumia vibaya gari ya ofisi, ambalo alipata nalo ajali, kushindwa kuongoza kikao cha Baraza la Madiwani na kusababisha Meya wa Ubungo, Boniface Jacob kugombana na Meya wa Temeke, Abdallah Chaurembo na kudaiwa kuwapendelea baadhi ya mameya kuingia kwenye kamati za fedha.Akisoma ripoti hiyo, Liana alisema kamati imemkuta na hatia meya huyo wa Dar es Salaam, kwa makosa yote anayotuhumiwa nayo. Mkutano huo maalumu, uliokuwa na ajenda ya kupokea Taarifa ya Timu Iliyochunguza Tuhuma dhidi Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita, iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salama Paul Makonda, ulifanyika katika Ukumbi wa Karimjee jana.Kikao hicho kiliketi na kupiga kura ya kutokuwa na imani na Meya huyo, kwa mtindo wa kusimama. Kikao hicho kikiongozwa na Naibu Meya, Abdallah Mtinika na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Liana. Meya huyo alipinga mchakato mzima wa kura, ulivyoendeshwa wa kutokuwa na imani naye.Mwita alisema “Kiukweli sasa maji kwangu yapo shingoni, mbele sioni wala nyuma sioni, ila naamini Mwenyezi Mungu atasimama.”Aliongeza kuwa: “Umeya wangu sasa unapimwa, ikiwa imebaki miezi mitatu kabla hatujavunja Baraza la Madiwani. Hivi karibuni nimeanza kupata wakati mgumu kwenye kiti change. Naomba viongozi wa dini waniombee.”Gari layeyuka, amuangukia Rais Magufuli Katika hali asiyoitarajia, Meya huyo wa Jiji la Dar es Salama alipigwa na butwaa baada ya kufika eneo la maegesho, lakini hakulikuta gari aina ya Prado, alilokuwa akilitumia katika shughuli zake za kila siku, ambalo alipewa kutokana na nafasi hiyo.“Nashangaa nimenyang’ nywa gari na bendera imeshushwa. Nawaambia mimi bado ni meya. Namuomba Rais Dk John Magufuli aingilie kati suala hili, kwa sababu wakati naingia madarakani ilikuwa hivi hivi.“Sio gari tu, hata ofisi imefungwa. Sielewi kinachoendelea dhidi ya wadhifa wangu. Nasisitiza mimi bado meya wa jiji hili, kwa mujibu wa Kanuni Ibara ya 82 (2) meya ataondolewa kwa kura mbili ya tatu (theluthi mbili) “alisema Mwita Alisema mahudhurio yalikuwa watu 16, ambapo kati yao 13 ndio walipiga kura za kutokuwa na imani naye.Wawili walipinga suala hilo na mmoja hakupiga kura, hivyo akidi hiyo haikutimia kumuondoa. “Sisi kama Watanzania tumeapa kulinda Katiba yetu, kanuni na miongozo. Tusitie aibu. Mimi ni mmoja tu, sing’ang’anii kuwa meya ila taratibu zifuatwe. Sitaacha kupigania haki yangu. Namuomba Rais Magufuli aingilie hili. Namuomba sana Rais,”alisisitiza Mwita.Makonde yazuka Diwani wa Kata ya Tabata, Patrick Assenga alimtwanga makonde Naibu Meya, Abdallah Mtinika baada ya kusoma matokeo ya Azimio la wajumbe waliopiga kura ya kutokuwa na imani na Mwita. Mtinika aliyekuwa akiongoza kikao hicho, alisema idadi ya waliopiga kura, kwa kusimama kwenye viti vyao ni 16.Assenga alimtwanga makonde hayo ya nguvu Naibu Meya, kwa kile madai ya kuchukizwa na matokeo aliyotangaza ya kutokuwa na imani na Mwita. Makonde hayo yalifanya askari kutumia nguvu na kumkwida mzobe mzobe Assenga mpaka kwenye gari defender ya Polisi, ambapo walimpeleka Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Dar es Salaam. Hali ilikuwa hivi kabla ya Naibu Meya kusoma matokeo.Alianza kwa kusema “Naomba nisome uamuzi wa mwanasheria wetu wa jiji la Dar es Salaam, kuhusu uamuzi wa kutokuwa na imani ya meya.“Kura zilizopigwa ni 16 na mjumbe mmoja ameomba udhuru na wawili hawakupiga kura, uamuzi wenu umepitishwa, baada ya hapo nafunga kikao”.Hata hivyo, Mtinika hakusema kama Mwita ameondolewa katika nafasi, badala yake alisema ni uamuzi wa wajumbe 16 ambao ni wa CCM. Baada ya kutoa uamuzi huo, wajumbe wa Chadema walionekana wakishangilia na kusema: “Hoja yenu imeshindwa, kwisha habari yenu.” Waliendelea kushangilia na kudai kuwa Mwita bado ni meya wa jiji hilo.Hata hivyo, vurugu zilitamalaki katika ukumbi huo, kwa Assenga kuchukuliwa na Polisi. Vurugu ukumbini Awali, kabla ya kupiga kura kuanza, kuliibuka vurugu katika Ukumbi wa Karimjee. Msingi wa vurugu hizo ni baada ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob kudai kuwa kuna saini feki ya jina la mjumbe, Kassim Mshamu kwenye kikao hicho. Alishika kitabu cha mahudhurio na kunyoosha juu, huku akisema kuna saini feki.“Usinisumbue, usiniguse, acha kunisukuma” Jacob alimwambia askari aliyemfuata kutaka kumshika, wakati akipaza sauti kuwaeleza wajumbe kuhusu saini hiyo feki. Wakati Jacob akipaza sauti, ukumbi ulikuwa unazizima kwa kelele na kutoelewana, huku wajumbe wa Chadema wakionekana kupandwa na hasira.Kesi yake Kisutu Wakati yanatokea hayo ukumbini, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeshindwa kutoa uamuzi wa maombi yaliyowasilishwa na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita aliyeomba mahakama hiyo itoe amri ya kusitisha mchakato wa kung’olewa kwenye nafasi hiyo hadi maombi ya msingi yatakaposikilizwa. Wakati askari wakiimarisha ulinzi mahakamani hapo jana, Hakimu Mkazi Mkuu, Janeth Mtega aliahirisha shauri hilo hadi leo saa 5:00 asubuhi kwa sababu hajamaliza kuandika uamuzi huo.Shauri hilo lilipoitwa upande wa wajibu maombi, waliwakilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wa serikali, likiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Tango huku upande wa mleta maombi, ukiwakilishwa na Wakili Hekima Mwasipo na wenzake wawili.Mwita amewasilisha maombi hayo dhidi ya Mkuu wa Mkoa huo, Paul Makonda, Halmashauri ya Jiji hilo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Wakili Mwasipo aliwasilisha maombi hayo chini ya hati ya dharura na yanalenga kuwazuia Mkuu wa Mkoa na Halmashauri hiyo, kujihusisha katika mchakato wa kumng’oa kwenye nafasi ya Umeya wa jiji hilo.
1
WATU wawili wamefariki dunia papo hapo baada ya magari mawili waliyokuwa wakisafi ria kugongana uso kwa uso na kisha kuwaka moto na kuteketea kabisa.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Willbroad Mutafungwa alithibitisha jana ajali hiyo ilitokea eneo la Makunganya katika Manispaa ya Morogoro kwenye Barabara Kuu ya Morogoro – Dodoma. Kamanda Mutafungwa alisema ajali hiyo ilitokea saa 11 alfajiri ikihusisha gari lenye namba za usajili T.661 DKS aina ya Leyland Ashok ambalo ni la kuchimba visima lililokuwa likitokea Morogoro kwenda Dodoma lililogongana na lori aina ya MAN lenye namba za usajili JA. 4417/ T.0806 likitokea Dodoma.Alisema lori Man lilibeba mkaa na kuwaka moto na kutekeza magari yote na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi wengine wawili waliopelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kutibiwa. Alisema Polisi walifika eneo la ajali na juhudi za kuzima moto huo zilichukuliwa ingawa magari hayo yaliteketea lakini waliyaondoa barabarani baada ya kuziba njia na kuwezesha magari mengine kupita.Alisema baada ya kuudhibiti moto huo na kuchunguza ndani ya magari hayo, walikuta watu wawili wameshafariki dunia ambao aliwataja kuwa ni Mzambile Sadoki (27) ambaye ni dereva wa gari aina ya Man, raia na mkazi wa wa Burundi aliyekuwa akitokea nchini humo kwenda jijini Dar es Salaam. Mwingine ni dereva wa Leyland Ashok, Chekeli Redy (45) mkazi wa Morogoro aliyekuwa akitokea Dodoma. Aliwataja majeruhi kuwa ni Mateso Hassan (32) mkazi wa Morogoro aliyekuwa kwenye gari kutoka Burundi, Madua Zuberi (25) mkazi wa Burundi aliyekuwa kwenye gari la kwenda Dodoma. Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, uchunguzi wa Polisi unafanyika ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.
1
Na Mwandishi wetu -Dodoma WANAWAKE wenye fistula nchini wametakiwa kuacha kujifungia ndani na badala yake waenda kupata matibabu katika hospitali zilizoainishwa na Serikali. Hayo yamesemwa jana Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya siku ya fistula duniani inayoadhimishwa Mei 23. Alisema takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) za mwaka 2018 zinaonyesha wanawake millioni mbili  wanaoishi na fistula duniani kote. Inakadiriwa wagonjwa wapya kati ya 50,000 na 100,000 hupatikana kila mwaka, wakati juhudi za kutibu fistula ulimwenguni kote huishia kutibu wagonjwa 20,000 tu.  Kwa upande wa Tanzania, Ummy alisema inakadiriwa wanawake 2,500 wanapata fistula kila mwaka, huku idadi ya wanaopatiwa matibabu ikiwa ni  1,000. “Katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2015 hadi Disemba, 2019 wanawake zaidi ya 5,500 wametibiwa Fistula. Mafanikio haya yanatokana na kampeni iliyoendeshwa kwa ushirikiano baina ya Serikali na wadau ambayo imeweka mabalozi wa fistula zaidi ya 3,000 nchi nzima wanaosaidia kuratibu rufaa na usafiri kwa wagonjwa kwenda hospitali zinazotoa huduma ya fistula,”alisema Ummy. Ummy aliwataka akinamama wajawazito kuhudhuria kliniki mara tu anapojihisi mjamzito ili kuweza kuchunguza afya yake pamoja na mtoto. “Mama mjamzito endapo atawahi kliniki mapema kwa ajili ya uchunguzi wa maendeleo ya afya yake na mtoto na kuhakikisha anajifungulia katika kituo cha kutolea huduma za afya atapunguza uwezekano wa kupata tatizo la fistula.  “Nitumie fursa hii kuendelea kuhimiza akina mama wajawazito kuwahi kliniki mapema, kukamilisha mahudhurio yote manne na kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Afya,”alisema i Ummy.
5
MWANDISHI WETU NA MTANDAO KATIKA ulimwengu wa sayansi na teknolojia, kila siku kunaibuka mahitaji na ulazima wa uundwaji na uvumbuzi wa vitu mbalimbali vyenye teknolojia ya hali ya juu. Lakini pia wakati teknolojia mpya zikizidi kubuniwa, uvumbuzi duniani na matumizi ya teknolojia zilizopo unabadilisha utendakazi wa kampuni nyingi na jinsi wanadamu wanavyotangamana. Maendeleo katika uwezo wa kompyuta kufanya kazi za wanadamu, uchanganuzi wa data kubwa na upanuzi wa mtandao wa intaneti ni miongoni mwa mambo yanayochochea mapinduzi hayo. Kwa msaada wa mtandao, zifuatazo ni orodha ya teknolojia kuu zinazoweza kubadili maisha mwaka huu wa 2019. 1.Matumizi ya mashine kufanya kazi za binadamu Teknolojia ya roboti inatarajiwa mwaka huu kuwa na sifa kamili za mwanadamu kama kuzungumza, kusoma, kuona, kufikiria na kutambua vitu au watu wanaotembea. Kwa kutumia teknolojia ya hesabu ya mashine (algorithms) inayowiana na mahali, zitaweza kufanya kazi ambayo inachosha au hatari kwa binadamu, kwa kasi zaidi na kwa umakini zaidi. Teknolojia hii inatarajiwa kuvuruga kila sekta ya uchumi, huku kampuni nyingi zikiipendelea kwa uwezo wake wa kupunguza gharama na kuongeza ubora. Mifumo inayohusisha video za 3D, sauti, uwezo wa kushika, kuonyesha maeneo na hata uwezo wa kunusia itabadilisha utendaji wa mitambo kwa uwezo wake wa kutambua mazingira kwa mbashara. 2. Teknolojia ya Blockchain Thamani ya sarafu ya dijitali ya Bitcoin imewasisimua wengi kutokana na kutumia kwake teknolojia ya Blockchain. Hii ni teknolojia salama ya kurekodi na kuthibitisha ununuzi na uuzaji pamoja na uhifadhi wa data muhimu. Ina uwezo wa kuzima matukio mengi ya kihalifu kama vile wizi wa fedha kidijitali katika benki, wizi wa data, wizi wa kura na kutathimini utendaji wa wafanyakazi huku historia ya watumiaji  wote wa data ikionekana na kila mtumiaji. Tayari kampuni nyingi duniani zinatumia teknolojia hii, lakini mwaka huu wadau wa teknolojia wanatarajia Blockchain kuanza kutumika kikamilifu hata na serikali na mashirika. 3. Magari ya kielektroniki Kuna uwezekano mkubwa mno kuwa kufikia mwishoni mwa 2019, kila kampuni ya kuunda au kuuza magari itakuwa na magari ya kielektroniki kwenye maegesho yake ya mauzo. Tayari kampuni ya Amerika ya Tesla inauza magari haya ambayo badala ya kutumia dizeli au petroli, yanatumia betri moja hutiwa kwa umeme wakati nguvu zake zimeisha. Hii inawiana na ajenda ya kimataifa ya kutumia nishati safi na kukoma kutumia nishati inayotoa moshi. Magari machache ya kielektroniki tayari yameingia Afrika Mashariki hususani Kenya lakini yanatarajia kuongezeka idadi yake mwaka huu. Pia teknolojia ya magari yanayojiendesha yenyewe bila dereva mwanadamu yanatarajiwa kutua Afrika Mshariki mwaka huu. 4. Malipo ya kidijitali Tayari tumeshuhudia malipo mengi yakifanywa kupitia Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money, lakini huduma muhimu kama usafiri na ununuzi wa bidhaa umebakia kufanywa kwa kutumia sarafu na noti. Huduma ya kulipia ugeshaji wa magari katika Kaunti ya Nairobi ya eJijiPay nchini Kenya na ile ya kutuma na kupokea hela kutoka benki tofauti ya Kenswitch zimeongoza katika malipo ya kidijitali. Hata hivyo, baadhi ya kampuni nchini Uswisi zimewaweka wafanyakazi wake kidude mkononi ambacho kinatumika kulipia kila huduma na bidhaa. Kampuni ya Google ina huduma kwa wateja inayoitwa Google Pay huku Apple Inc ikiwa na Apple Pay. Huduma hizi zinatarajiwa kuvumisha malipo ya kidijitali kupitia kwa simu. Hivyo, Afrika Mashariki mwaka huu itashuhudia mapinduzi zaidi ya malipo ya kidijitali kutokana na fedha taslimu kuwa sumaku ya kuvuta wezi. 5. Uchapishaji wa 3D Kwa Afrika Mashariki, teknolojia hii tayari ni maarufu katika mtaa wa Westlands, Nairobi lakini haijaenea sana kwingineko kwa kuwa Wakenya na raia wengi wa Afrika Mashariki bado hawajatambua uwezo wake. Ni uvumbuzi unaokuwezesha kutengeneza vifaa vingi vya miundo aina tofauti kama vyombo vya jikoni, samani ya plastiki na vioo. Lakini katika mataifa yaliyoendelea, teknolojia hii hutumika kujenga nyumba, kutengeneza viungo vya mwili katika matibabu huku pia ikiwa na uwezo wa kupika vyakula kama pizza. Mtumiaji hutakiwa kuchora muundo wa chombo anachotaka kutengeneza kwa kutumia kompyuta kwanza. Kisha mashine ya uundaji hujazwa na viambato vya kutengeneza chombo hicho kama plastiki iliyosagwa kuwa uji kisha kubonyeza kitufe cha ‘Chapisha’. Ikiwa teknolojia hii inatumika mijini, utaanza kuona uagizaji wa bidhaa nyingi kutoka mataifa ya nje ukipungua. 6. Uzinduzi wa mtandao wa 5G Kizazi cha tano cha teknolojia isiyotumia waya inatazamiwa kutawala matumizi ya simu kote duniani. Hii ndiyo teknolojia itakayochukua nafasi ya Wi-Fi, kwani itapunguza muda wa kutuma na kupokea data kwa intaneti kutoka milisekunde 30 hadi milisekunde moja. Hii itaongezea uzito wa muunganisho baina ya mashine mbili kwenye mtandao. Tofauti na Wi-Fi ambapo data inaweza kuzuia na kutekwa, 5G data itakuwa salama huku mtandao binafsi wa 5G ukiwezesha upakiaji na upakuaji wa data kubwa. Kasi ya intaneti itakuwa juu zaidi na kutazama video ndefu au kuipakia kwa YouTube kutakuwa haraka zaidi, ukitumia kompyuta, tableti au simu. Hivi karibuni kongamano la kimataifa kuhusu teknolojia lililofanyika jijini Las Vegas, Marekani wiki liyopita, kampuni mbalimbali zilionyesha namna intaneti hiyo ambayo itakuwa na kasi ajabu itainua ufanisi wa wa mitandao. Ikianza kazi, intaneti ya 5G itawezesha watumizi wa mitandao kufanya mambo mbalimbali kwa kasi, takriban mara 10 zaidi ya ile ya 4G. baadhi ya huduma ambazo zitanufaika na intaneti hiyo ni kama kuingia katika tovuti, kuchota’ nyimbo ama filamu ama kutazama filamu moja kwa moja mitandaoni. Teknolojia hiyo inatarajiwa kuanza kufanya kazi Marekani kuanzia 2020, japo baadhi ya kampuni zimeeleza kuwa zinalenga kuanza kuitumia mwaka huu. Kampuni ya Verizon ilisema kuwa intaneti hiyo ya 5G itasaidia hata katika sekta ya afya na madaktari wa upasuaji kurahisisha kazi ili kufikia habari muhimu za mazoezi hayo kwa haraka.
3
Aidha, Senegal ilibanwa na kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Uzbekistan mjini Casablanca huku Moussa Konate akifunga bao la kusawazisha kwa Simba hao wa Teranga.Mjini Turin, Morocco ikiwa kwenye kiwango chake iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Serbia. Hakim Ziyech alifunga bao la kuongoza kwa mkwaju wa penalti kabla ya mapumziko.Penalti hiyo ilitolewa na mwamuzi baada ya Nikola Maksimovic kumuangusha Nordin Amrabat, lakini Wamorocco walisawazisha bao hilo dakika nane baadaye kupitia kwa Dusan Tadic baada ya kuua mtego wa kuotea wa Serbia.Kikosi hicho cha Herve Renard hakijaruhusu nyavu zake kutikiswa wakati wote wa michuano ya kufuzu kombe la dunia. Aidha dakika ya 40 walipata bao lingine la pili likifungwa na Khalid Boutaib kwa kichwa akiunganisha mpira wa krosi wa Ziyech.Morocco itaanza kampeni za kuwania kombe la dunia dhidi ya Iran Juni 15 kabla ya kukutana na mabingwa wa Ulaya Ureno mjini Moscow siku tano baadaye.Watamaliza raundi ya kwanza kwa kumenyana na Hispania mjini Kaliningrad Juni 25. Katika mechi nyingine, Tunisia dhidi ya Iran ilionekana kama ingemalizika kwa suluhu, lakini katika dakika ya 71 Milad Mohammadi alijifunga akiwa kwenye harakati za kuokoa mpira wa Wahbi Khazri, hivyo kuipa Tunusia ushindi.Ushindi huo wa bao 1-0 ni kama umeongeza morali kwa Tunisia ambao itacheza na England, Ubelgiji na Panama kwenye kombe la dunia.Mjini Casablanca, Uzbekistan inayoshika nafasi ya 72 kwenye viwango vya ubora wa Fifa, ilipata bao la kuongoza dakika ya 20 ya mchezo wake dhidi ya Senegal kupitia kwa Otabek Shukurov aliyefunga kwa mkwaju wa penalti. Simba hao wa Teranga walisawazisha bao hilo kupitia kwa Konate.Senegal inatarajiwa kucheza mechi nyingine dhidi ya Bosnia-Herzegovina mjini Le Havre kesho katika mfululizo wa mechi za kujipima nguvu.Mjini Zurich, Uswisi mabao mawili ya Cristiano Ronaldo yalizima ndoto za nyota wa Liverpool, Mohamed Salah kuipa ushindi Misri dhidi ya Ureno katika mechi nyingine ya kirafiki. Ikiwa mbele kwa bao 1-0 kwa muda wote wa mchezo, Misri ilijikuta ikitoka uwanjani vichwa chini baada ya mabao ya dakika za majeruhi aliyofunga Ronaldo kwa timu yake ya Ureno na kuipa ushindi wa 2-1.Nyota huyo wa Real Madrid alicheza akiwa mwenye presha kwa muda wote wa mchezo huo huku Salah akionekana kuwa nyota wa Misri na ilionekana dhahiri anawaadhiri mabingwa hao wa Ulaya.Lakini katika muda wa majeruhi, Ronaldo alibadili matokeo kwa kufunga mabao mawili ya haraka haraka na kuibuka na ushindi, hivyo kujiweka vizuri katika maandalizi ya kombe la dunia Urusi.Matokeo kama hayo ya kushangaza yalitokea Paris Ufaransa pale wenyeji walipokuwa mbele kwa 2-0 lakini mpaka mwisho wakachapwa mabao matatu na Colombia.Ikicheza muda mrefu ikiwa nyuma kwa mabao 2-0 Colombia ilipambana na kuibuka na ushindi huo huku bao la tatu likiwekwa kimiani na Juan Quintero kwa mkwaju wa penalti yenye utata.Kiungo huyo alifunga bao hilo zikiwa zimesalia dakika tano kabla mechi kumalizika kwenye uwanja wa Stade de France kufuatia mabao ya Luis Muriel na Radamel Falcao, baada ya wenyeji kuwa mbele kwa mabao ya Olivier Giroud na Thomas Lemar.Ufaransa ilianza mechi hiyo ikimuweka benchi Paul Pogba na kuwaanzisha Lemar, Kylian Mbappe, Antoine Griezmann na Giroud na mshambuliaji huyo wa Chelsea aliifungia nchi yake bao la 30 baada ya makosa yaliyofanywa na David Ospina.Matokeo hayo yanaifanya Ufaransa kujipanga upya keshokutwa itakapowakabili wenyeji wa kombe la dunia, Urusi, katika mechi nyingine ya kimataifa ya kirafiki.Nayo Uholanzi imelala kwa bao 1-0 dhidi ya England katika mechi nyingine ya kirafiki kuelekea michuano hiyo ya kombe la dunia iliyochezwa mjini Amsterdam.Bao hilo lilifungwa na Lingard katika dakika ya 59 na kuiongezea England morali ya kombe la dunia.Ushindi huo ni baada ya kutoka suluhu mfululizo katika mechi dhidi ya Brazil na Ujerumani Novemba mwaka jana, kikosi cha Gareth Southgate juzi kiling’ara licha ya kutokuwepo kwa mshambuliaji wake nyota Harry Kane kutokana na kuwa majeruhi.Katika mechi nyingine, Ever Banega na Manuel Lanzini walidhihirisha kukosekana kwa Lionel Messi siyo sababu ya Argentina kukosa ushindi baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Italia.Messi, ambaye anasumbuliwa na misuli, hakuwepo kwenye kikosi cha Argentina kilichocheza mechi hiyo kwenye uwanja wa Etihad.Kipa wa Italia Gianluigi Buffon, ambaye ameghairi uamuzi wake wa kustaafu soka ya kimataifa baada ya Azzurri kushindwa kufuzu kombe la dunia, juzi alicheza mechi yake ya 176.Kikosi cha Italia kinatarajia kusawazisha makosa yake katika mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya England keshokutwa huku Argentina ikitarajiwa kuikabili Hispania katika mechi nyingine ya maandalizi ya kombe la dunia.Aidha katika mechi nyingine zilizochezwa juzi, Ujerumani ilitoka sare ya bao 1-1 na Hispania, Scotland ilifungwa bao 1-0 na Costa Rica, Uturuki ilitoka sare ya bao 1-1 na Jamhuri ya Ireland, na Norway ilishinda mabao 4-1 dhidi ya Australia.
2
 AVELINE KITOMARY Na BRIGHITER MASAKI -DAR ES SALAAM  MGONJWA mmoja wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (Covid-19) nchini amepona, huku mwingine akithibitika kuwa na virusi hivyo.  Kutokana na taarifa iliyotolewa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, hadi sasa watu waliothibitika kuwa na virusi hivyo nchini ni 20 huku wawili wakiwa wamepona na mmoja kufariki dunia.  Wakati hali ikiwa hivyo nchini, hadi jana waliofariki dunia kwa virusi hivyo duniani ni zaidi ya 42,000 huku 178,000 wakiwa wamepona na 860,000 wamethibitika kuwa na virusi hivyo.  Taarifa kwa umma iliyotolewa na Waziri Ummy jana, ilisema mmoja kati ya wagonjwa waliokuwa katika kituo cha matibabu cha Temeke, Dar es Salaam juzi amethibitika kupona.  “Ameruhusiwa kurudi nyumbani na hivyo kufanya jumla ya watu waliopona kuwa wawili,” alisema Ummy.  Machi 26, Ummy alitangaza kupona kwa mgonjwa wa kwanza, Isabela Mwampamba (46).  Machi 16, Ummy alimtangaza Isabela kuwa mgonjwa wa kwanza wa corona ambaye aliwasili nchini akitokea Ubelgiji.  Baada ya Isabela kugundulika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo, aliwekwa karantini na Serikali iliendelea kuwafuatilia watu wake wote wa karibu ili kubaini hali zao.  MGONJWA MPYA  Jana kwenye taarifa yake, Ummy alitangaza kubainika kwa mgonjwa mpya ambaye ni mwanamke mwenye umri wa miaka 42, raia wa Marekani.  “Wizara inathibitisha kuwepo kwa kesi mpya ya maambukizi ya virusi vya corona (Covid-19) nchini iliyopatikana jijini Dar es Salaam, mgonjwa huyo amekuwa karibu na mtu aliyesafiri nje ya nchi na kuthibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya Covid-19 aliporejea nchini.  “Hivyo hadi sasa jumla ya kesi za maambukizi ya virusi vya corona (Covid-19) zilizothibitishwa hapa nchini ni 20.  “Aidha ninatoa taarifa kuwa Machi 31 mwaka huu mmoja wa wagonjwa waliokuwa katika kiituo cha matibabu cha Temeke amethibitika kupona maambukizi aliyokuwa nayo na amerudishwa nyumbani,” alieleza Ummy.  MAKONDA NA KODI  Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewataka wamiliki wa nyumba za kupanga, maofisi, vibanda na hoteli kwenye mkoa wake kuwapunguzia wapangaji wao kodi kwa asilimia 50 katika miezi mitatu kutokana na hali ya uchumi wakati huu wa janga la corona.  “Nimeongea na wenye nyumba na kuwataka wapunguze kodi kwa asilimia 50 ili kusaidia kufanya biashara na kuangalia hali ya uchumi ilivyo kwa sasa, kama mnavyofahamu corona imeathiri hali ya kifedha.  “Tuwasaidie wenzetu waweze kupata fedha ya kununua chakula na kuweka ndani chakula kwa kuwapunguzia majukumu kama kodi za nyumba, fremu na hoteli,” alisema Makonda.  Pia alitangaza kuwa madereva wa bodaboda na bajaji wataruhusiwa kuingia katikati ya jiji ili kusaidia kubeba abiria ambao wanamudu usafiri huo ili kusaidia wanaokwama kutokana na agizo la daladala kutosimamisha abiria.  “Mnaruhusiwa kuingia mjini kwa kufuata sheria na taratibu za kutoingia kwenye barabara ya mwendo kasi na mnatakiwa kuvaa elementi unapokuwa kwenye chombo chako, zoezi hili litaendelea hadi corona itakapoisha.  “Tunachotakiwa kufanya hivi sasa ni kusaidia wafanyakazi kuwahi kazini na kufanya shughuli kwa wakati ili tuweze kuepukana na hali ngumu ya maisha,” alisema Makonda.  Vilevile aliwataka wazazi kutulia nyumbani kama hawana safari za lazima ili kuepusha kusababisha maambukizi ya corona kuleta nyumbani na kuathiri familia.  Pia Makonda ameitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu (Latra), kuhakikisha ifikapo leo saa 6:00 mchana wawe wameshabadilisha ruti za magari kuwa fupi.  “Magari kuwa na ruti ndefu ndio sababu mojawapo ya abiria wa vituo vya katikati kukosa usafiri, unakuta abiria wamepanda kutoka Mbagala hadi Ubungo abiria wengine wanakosa pa kukaa.  “Naomba Latra wakae na wamiliki wa magari na wakubaliane kubadilisha ruti ziwe fupi fupi kama Buruguni hadi Ubungo, hadi kesho (leo) saa 6 wasipobadilisha ruti saa saba mchana nitatangaza na kubadilisha ruti mimi mwenyewe,” alisema Makonda.   ELIMU YA CORONA  Katika hatua nyingine, Taasisi isiyo ya kiserikali ya Walter Nnko Foundation (WNF) imejitolea kupita mitaani na kugawa vifaa na kutoa elimu kuhusu corona.  Akizungumza na MTANZANIA jana Dar es Salaam, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Dk. Walter Nnko, alisema ameamua kujitolea kuwasaidia wananchi ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupambana na Covid-19.  “Nilishaanza kutoa elimu katika Jiji la Dar es Salaam, naangalia hasa maeneo ya sokoni na stendi ambako watu wanaendelea na shughuli zao, na mwitikio wa watu kufuatilia elimu hii ni mkubwa.  “Matarajio yetu ni kuona kila mmoja ajue madhara ya ugonjwa huu na jinsi gani ya kujikinga ili taifa letu lisiingie kwenye janga la kuwa na wagonjwa wengi,” alibainisha Nnko.  Alishauri taasisi mbalimbali binafsi na za umma kutoa elimu ya kutosha kwa jamii kuhusu Covid-19. 
5
Hayo yalisemwa na Mwakilishi wa jimbo la Micheweni, Subeit Khamis Faki (CUF) wakati akichangia muswada wa maendeleo ya Karafuu uliowasilishwa na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Ahmed Nassor Mazrui.Faki alisema kitendo cha Serikali cha ujasiri kupandisha bei juu ya Karafuu kwa wakulima kwa kiasi kikubwa kimeongeza ari kwa wakulima kuongeza uzalishaji wa Karafuu na kuliingizia taifa fedha.“Tunaipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuongeza bei nzuri ya Karafuu kwa wakulima ambayo imeongeza ari na kupunguza magendo ya karafuu kwa wakulima,”alisema Faki.Kwa mfano alisema magendo ya karafuu zilizokuwa zikisafirishwa hadi Kenya zilifanya nchi hiyo kutambuliwa na kupewa zawadi ya kuzalisha Karafuu bora.“Kenya ilipata zawadi kwa kuzalisha karafuu bora yenye hadhi ya juu kutokana na magendo ya wakulima waliokuwa wakisafirisha karafuu kutoka Pemba kwenda Mombasa nchini Kenya,”alisema.Kauli hiyo iliungwa mkono na Mwakilishi wa viti maalumu, Panya Abdalla Ali (CCM) aliyewataka wakulima wa karafuu Pemba kukomesha moja kwa moja magendo ya karafuu ambayo yalikuwa yakilitia hasara kubwa taifa.“Tunampongeza kwa dhati rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein mara alipoingia madarakani alipandisha bei ya karafuu na kufikia Sh 14,000 kwa kilo moja,” alisema.Mwakilishi wa jimbo la Mtambwe, Salim Abdalla Hamadi(CUF) aliitaka Serikali kuondoa sheria kali zinazowabana wakulima na kuwanyima uhuru ikiwemo kusafirisha karafuu sehemu moja kwenda nyingine lazima upate kibali kutoka kwa sheha.Kwa mfano, Hamadi alisema sheria inayowataka wananchi kupata kibali kutoka kwa sheha wakati wanaposafirisha karafuu kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwamba sheria hizo zimepitwa na wakati.“Sheria kama hizi zimepitwa na wakati kwa sababu zinawabana wananchi na wakulima wetu uhuru katika kazi zao hizo...leo unamtaka mkulima lazima apate kibali wakati anaposafirisha zao hilo kwenda sehemu nyingine ni kumnyima uhuru na kuweka vikwazo ambavyo vimepitwa na wakati,” alisema.Aidha Mwakilishi Hamad ambaye jimbo lake linaongoza kwa uzalishaji wa karafuu nyingi ameitaka Serikali kudhibiti tatizo la 'uchakachuaji’ wa karafuu.“Naiomba Serikali ipambane na tatizo la uchakachuaji wa karafuu ambapo wakulima wasiokuwa waaminifu wanachanganya karafuu na makonyo pamoja na majani yaliyosagwa,” alisema.Muswada wa maendeleo ya karafuu lengo lake kuwasaidia wakulima kuanzisha mfuko wa karafuu pamoja na kudhibiti magendo ya karafuu.
0
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
0
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii waliokuwa wakitembelea miradi ya vikundi vilivyonufaika na fedha zinazotolewa na serikali kwa ajili ya kuinua vijana.Miradi iliyokaguliwa juzi ni ya vikundi vitatu katika wilaya ya Temeke ambao wamekopeshwa fedha na Mfuko wa Vijana wa Wizara kupitia vyama vya kuweka na kukopa vya vijana katika wilaya.Vikundi hivyo ni Waungwana Family kinaendesha mradi wa saluni na muziki wa kizazi kipya, African Legends kinachoundwa na vijana wahitimu wa vyuo kikuu wanaendesha mgahawa wa chakula na ofisi ya ICT na Sokoine Youth Development, wanaojishughulisha na kilimo eneo la Somanga, Kigamboni.Nkamia alisema changamoto ya mfuko wa vijana, unaosimamiwa na wizara ni vijana kutokuwa na uelewa wa kuandika andiko mradi kwa mujibu wa mwongozo wa serikali hivyo kukosa fursa hiyo.“Tulipobaini changamoto hii tuliona lazima tutoe mafunzo kwa vikundi vya vijana ili wauelewe mfuko na namna ya kukopa, mambo mengi yanayoletwa hayaandikwi kwa kuzingatia mwongozo wa Serikali,” alisema.Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, Said Mtanda aliutaka uongozi wa Manispaa ya Temeke kutoa ripoti na kuweka orodha ya vikundi vyote vilivyokopeshwa fedha kuanzia mwaka 2000 hadi 20014.Fedha hizo ni za Mfuko wa Vijana, fedha asilimia 10 ya mapato ya manispaa (kwa vijana na wanawake) na zile zinazotolewa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa vikundi vya wanawake.“Tunataka tuone vikundi vyote vya wanawake na vijana vilivyokopeshwa na mifuko hiyo mitatu, tunataka kujua ni kiasi gani mmewapa na hali ya marejesho. Tunataka hilo ili tusije tukauziwa mbuzi kwenye gunia,” alisema.Agizo la Mtanda lilitokana na taarifa iliyosomwa na Ofisa Maendeleo wa Temeke, John Mbwana kwa kuelezea jinsi Sh milioni 17 zilizotolewa na Wizara ya Habari kupitia Mfumo wa Vijana zilivyokopeshwa kwenye vikundi vitatu vya vijana.Awali, Mbunge Maua Daftari alitaka maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Photidas Kagambo ni kiasi gani kimekuwa kikitengwa kila mwaka na manispaa hiyo katika kutekeleza agizo la serikali la kila halmashauri nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wanawake na vijana.Aidha, kamati imeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa kilimo unaofanywa na kundi la Sokoine Youth Development wanaomiliki hekari 43 na kutaka wizara kuangalia uwezekano kwa kuwaongezea mkopo waweze kutatua shughuli zao na kuwa na vifaa vya kisasa vya kilimo.
0
WATOTO wawili wa familia moja wamekutwa wameuawa kwa kukatwa shingo zao na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia juzi, baada ya kutoweka nyumbani kwao.Tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Mashule kata Kyamulaile Halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, ambapo watoto hao walikuwa wakiishi na baba yao, Resipikius John ambaye aliwaogesha pale walipotaka kwenda kutembea.Baba mzazi huyo aliwataja watoto hao kuwa ni Auson Resipikius (7) anayesoma darasa la kwanza, na Alistidia Resipikius (5) anayesoma darasa la awali shule ya msingi Mashule.Alisema kuwa watoto hao waliondoka Oktoba 21, siku ya Jumapili jioni nyumbani na kwenda kutembea na yeye ndiye aliwaandaa na baadaye walirudi nyumbani tena wakabadilisha nguo na kutoweka moja kwa moja.Alisema kuwa alipoona muda unakwenda alimuuliza mke wake, Judith Charles mama wa watoto hao, ambaye alishatengana naye lakini alisema kuwa hawajaonekana kwake, ndipo walitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji na kuanza kuwatafuta usiku kucha bila mafanikio yoyote.“Tuliendelea na kuwatafuta na viongozi wa serikali ya kijiji siku iliyofuata ndipo tukawakuta wamechinjwa na kutelekezwa vichakani, jambo ambalo hatukulitegemea kabisa na hatujui nani anahusika na kifo cha watoto wangu,” alisema Resipikius.Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Deodatus Kinawilo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo alithibitisha vifo vya watoto hao na kuagiza jeshi la polisi na vyombo vinavyohusika kuanza uchunguzi haraka kuhakikisha wanachunguza kijiji kizima.Alisema kuwa uchunguzi ukikamilika watakaobainika wakamatwe haraka kwani tukio la kuuawa watoto wawili wasio kuwa na hatia ni la kinyama na halikubaliki.“Ebu tujiulize huu ni unyama wa aina gani jamani mtoto wa mtu unamchinja kama mnyama, ninachoweza kusema jeshi la polisi vuruga kijiji chote nadhani nikisema kuvuruga naeleweka,” alisema Kinawilo akibubujikwa na machozi mbele ya wananchi wa kijiji hicho.Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Izack Msangi alisema kuwa jumla ya watu 9 wamekamatwa kuhusiana na vifo vya kuchinjwa watoto hao na miili yao imezikwa kijijini hapo, na uchungizi wa polisi ukiwa unaendelea.Alisema kuwa watu waliokamatwa ni wale watu mbalimbali ambao wanahojiwa ili kubaini ukweli wa tukio hilo. “Hawa watu hatuwezi kuwataja majina kwa sababu bado uchunguzi unaendelea, tutahakikisha watu wanajihusisha na vitendo hivyo wanakamatwa, jeshi la polisi haliwezi kunyamaza kuona ndoto za watoto zinateketezwa,” alisema Msangi.Hata hivyo, mwananchi mmoja ambaye hakutaja jina lake alisema kuwa mauaji hayo huenda yanahusishwa na imani za kishirikina huku akikiri kuwa hivi karibuni katika kata jirani ya Rubale kuna mtoto ambaye amechinjwa na kutelekezwa kichakani na alikuwa na miaka 9.Mkoa wa Kagera umekuwa ukikumbwa na masuala mbalimbali ya ukatili ambapo miezi michache iliyopita viliibuka vitendo vya kuwachinja waendesha pikipiki hata hivyo haijulikani vitendo hivyo viliishia wapi.Aidha, miaka miwili iliyopita vilijitokeza vitendo vya kuwakata watu koromeo na watuhumiwa walikamatwa na kuhukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani ambapo jumla ya watuhumiwa watatu walikiri kukata koromeo mwananchi pamoja na pia kuchoma makanisa.
1
Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira imelieleza Bunge kuwa, bara la Afrika linachangia uzalishaji gesi joto kiasi kisichozidi asilimia tatu.Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mussa Sima amesema Tanzania huzalisha tani 0.09 za hewa ya ukaa kwa mwaka."Hivyo Tanzania inachangia kiasi kidogo sana katika tatizo la uzalishaji wa gesijoto ambazo ndio chanzo cha mabadiliko ya tabianchi" amesema Sima wakati anajibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Gimbi Masaba.Mbunge huyo alitaka kufahamu kauli ya Serikali kwa wamiliki wa viwanda wanaokiuka sheria ya mazingira  ili kukabili tishio la mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na uchafuzi wa mazingira hasa viwandani.Sima  amewaeleza wabunge kuwa, tatizo  la mabadiliko ya tabianchi kwa kiasi kikubwa linasababishwa na uzalishaji wa gesi joto unaotokana na matumizi ya nishati kwa 47%, uzalishaji viwandani 30% na usafirishaji kwa asilimia 11 unaosababishwa na shughuli za maendeleo katika nchi zilizoendelea kiviwanda hasa ulaya, Marekani, Asia na Australia."Haa hivyo, pamoja na kuchangia kidogo kiasi hicho, Tanzania imeendelea kuathirika kutokana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi kama vile kupungua kwa barafu ya mlima Kilimanjaro, kuongezeka kwa usawa wa bahari, ukame, mafuriko ya mara kwa mara na mlipuko wa magonjwa"amesema Sima.Amesema, tatizo kubwa linatokana na uchafuzi mazingira unaofanywa na baadhi ya viwanda kutirirsha majitaka yenye sumu na kemikali  zinazoathiri viumbe hai na mazingira kwa ujumla.
1
RAMADHAN HASSAN-DODOMA WANAWAKE waliotelekezwa na waliotelekezewa watoto, wametakiwa kufika katika Ofisi za Ustawi wa Jamii kwenye halmashauri zao ili hatua stahiki zichukuliwe kwa maslahi ya watoto na wao. Hayo yalielezwa jana bungeni na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Faida Mohammed Bakari (CCM). Katika swali lake, Faida alitaka kujua tamko na hatua za Serikali kwa kina baba wanaotelekeza watoto wao. “Wanawake wengi walioachika na wajane, watoto wao hutelekezwa na kukosa matumizi toka kwa baba zao na kusababisha watoto kukosa huduma muhimu na wazazi hao wa kike kuteseka na watoto,”aliuliza  Faida. Akijibu, Dk Ndugulile alisema huduma za matunzo, malezi na ulinzi kwa watoto zinatolewa kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Na. 21 ya Mwaka 2009 kifungu cha 7 – 9, ambavyo vinatoa majukumu kwa wazazi na walezi wote kuhakikisha wanawalea na kuwatunza watoto wao. Alisema kifungu cha 14 cha sheria hiyo, kinatoa adhabu kwa mzazi/ mlezi atakayekiuka kifungu hicho, atatozwa faini isiyozidi Sh milioni 5 au kifungo kisichozidi miezi sita, au vyote viwili, faini na kifungo. Alisema kwa kipindi cha 2018/19 mashauri 11,897 yaliyohusu matunzo kwa watoto na wanawake yalishughulikiwa katika ngazi za Serikali za Mitaa. “Idadi hii ni ongezeko la asilimia 148 ukilinganisha na idadi ya mashauri 11,815 yaliyopokelewa katika kipindi cha 2017/2018,” alisema. Alisema ongezeko hilo ni ishara ya kuongezeka kwa hamasa kwa wakinamama wanaotelekezwa kuchukua hatua kwa kufika Ofisi za Ustawi wa Jamii kwa ajili ya utatuzi wa malalamiko yao. “Niwaombe Ustawi wa Jamii katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha wanaendelea kusimamia utekelezaji wa sheria hii na kanuni zake ipasavyo,”alisema. Zebaki ni hatari Katika hatua nyingine, Serikali imesema kuna madhara ya kiafya na kimazingira katika matumizi ya kemikali ya zebaki kutokana na shughuli za uchenjuaji wa dhahabu. Hayo yalielezwa jana bungeni na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kaliua,Magdalena Sakaya(CUF). Katika swali lake Mbunge huyo alitaka kujua kauli ya Serikali inasemaje juu ya kuendelea kutumika kwa madini haya hapa nchini. “Tafiti zilizofanywa ndani na nje ya nchi zimethibitisha kuwepo kwa madhara ya kiafya, kimazingira, ardhini katika matumizi ya madini ya zebaki kuchenjua dhahabu,”alisema Magdalena. Akijibu swali hilo, Nyongo alisema Serikali kupitia Wizara ya Madini imechukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na madhara hayo kwa kutoa elimu kwa wachimbaji wadogo wanaotumia zebaki katika shughuli za uchenjuaji wa madini ya dhahabu. Alisema Wizara ya Madini imejenga vituo vya mfano katika maeneo ya Katente wilayani Bukombe, Lwamugasa wilayani Geita na Itumbi wilayani Chunya ambavyo vitatumika kufundisha teknolojia mbadala za uchenjuaji wa madini ya dhahabu zisizotumia kemikali ya zebaki na njia bora za utunzaji wa mazingira kwa wachimbaji eadogo.
5
MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa  Rais (Muungano na Mazingira ) January Makamba, amesisitiza kuwa  zuio la mifuko ya plastiki litakuwa la  sheria na hivyo hakutakuwa na msalie mtume. Hayo aliyasema   Dar es Salaam jana katika mahojiano na redio moja. Alisema hatua ya kupiga  marufuku  mifuko hiyo lengo  lake ni  kulinda afya za wananchi na mazingira. “Madhara yanayotokana na  matumizi ya mifuko hiyo ni makubwa   na hivyo siyo rahisi  kwa mtu kuona katika hali ya kawaida. “Wizara itahakikisaha hatua hiyo inafanikiwa bila vikwazo na   wananchi wataendelea kuelimishwa. “Katika kukabiliana na zuio hili  changamoto ni nyingi ikiwamo kutokuwa na ufahamu mpana wa wananchi juu ya athari zake, lakini tumejipanga kuhakikisha linafanikiwa na hatua muhimu zaidi ni kutoa elimu kwa wananchi. “Katazo la kitu kama hiki halikosi vikwazo, kelele na hata vitisho kutoka kwa watumiaji na wazalishaji, hivyo tumejipanga kukabiliana na yote hayo,” alisema Makamba. Alisema elimu ya kutosha itatolewa kuhusu madhara ya mifuko ya plastiki na njia mbadala zitaanza kutumika wakati wa kipindi cha zuio. “Tumejipanga kiasi cha kutosha juu ya namna ya kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza na jambo muhimu  ni ushirikiano kwa kuwa mazingira ni suala muhimu kwa kizazi cha leo na kesho;  hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuyalinda,” alisema Makamba. Baraza laTaifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wiki iliyopita lilieleza kuwa litatekeleza kwa ukamilifu agizo la serikali kwa kutumia sheria. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dk. Samuel Gwamaka,   Sheria ya Mazingira na Kanuni zake vinazuia utengenezaji na matumizi ya kitu chochote kinachoharibu mazingira, ikiwa ni pamoja na mifuko ya plastiki. “Marufuku hii ina maana kubwa sana katika ustawi wa mazingira ya nchi yetu. Usimamizi wa marufuku hii utaanzia ngazi ya mtaa hadi taifa maana katika ngazi zote hizi tuna ofisi za mazingira. “Tutatumia sheria kwa nguvu zetu zote, bila ubaguzi.  Tutatumia sheria bila kujali nafasi ya mtu katika jamii, cheo, rangi au mahali anakotoka,” alisema. Marufuku ya matumizi ya plastiki ilitangazwa bungeni na  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kikao cha Bajeti  kinachoendelea   Dodoma na mwisho wa matumizi wa mifuko hiyo ni Juni 1, mwaka huu.
1
Na Mwandishi wetu, Mbeya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara ambao hawajakadiriwa Kodi ya mapato kwa kipindi kinachoishia Marchi 31, mwaka huu kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kukadiriwa na kulipa Kodi zao kabla ya Juni 30,2020. Hayo yamezungumzwa leo jijini Mbeya na Kaimu Meneja wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Stephen Kauzeni ambaye amewahimiza hayo wakati wa kampeni ya uhamasishaji wa ulipaji kodi inayoendelea mkoani humo. Aidha amewakumbusha wafanyabiashara wote ambao mwaka wao wa mahesabu unaishia Desemba 31,2019  kuwasilisha ritani zao TRA kabla ya mwisho wa mwezi huu. Amesema kwa upande wa wafanyabiashara wanaolipa kwa awamu lakini bado hawajakadiriwa kodi zao ni vyema wakafika TRA ili wakadiriwe na walipe mapema kabla ya tarehe ya mwisho ili kuepuka adhabu na riba. “Tunawatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao ya biashara ili kuwakumbusha na  kuwahimiza wale ambao bado hawajafanyiwa makadirio, wakakadiriwe na wawahi kulipa kodi zao kwa wakati bila bughudha kuliko kusubiri siku ya mwisho kabisa”, amesema. Kauzeni ameongeza kuwa, kutokana na janga la ugonjwa wa korona, TRA isingependa kuona msongamano wa watu katika ofisi zake na kwamba imewalazimu maofisa wake kuwafuata walipakodi  kwenye maeneo ya biashara zao ili kuwapa elimu ya kodi na kuwasisitiza wakailipe kwa. “Ni wajibu wa mlipakodi kulipa kodi zake kwa wakati lakini pia TRA ina wajibu wa kutoa elimu pamoja na  kumkumbusha mlipakodi kulipa kodi na ndiyo maana tumewafuata huku madukani kwao kuwapatia elimu na kuwahimiza kulipa kodi kwa wakati,’’ amesema Kauzeni. Amesema kwa wafanyabiashara ambao mwaka wao wa hesabu unaishia Desemba 31, 2019 wanatakiwa kuhakikisha wanawasilisha ritani zao kabla au Juni 30, 2020 ili ritani zao ziweze kuhakikiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati kwa mujibu wa sheria za kodi zinavyoelekeza.  “Niwasihi walipakodi wafuate sheria ya Usimamizi wa kodi na kuwasilisha ritani zao ziweze kufanyiwa kazi mapema”, amesisitiza Kauzeni. Kauzeni amesema kampeni hii ya uhamasishaji ulipaji kodi kabla ya Juni 30, 2020 inalenga kuwakumbusha walipakodi kulipa kodi zao kwa wakati pamoja na kuongeza hamasa ya ulipaji kodi kwa hiyari miongoni mwa wafanyabiashara na watoa huduma zinazolipiwa kodi kama vile mawakili, wahasibu na fani zingine zilizosajliwa. Amesema kampeni hii ya utoaji elimu na uhamasishaji ulipaji kodi kwa wakati na hiyari inaendelea katika mkoa wa Mbeya na wilaya zake.
0
WANANCHI 875 wamepatiwa huduma ya macho bure baada ya kubainika idadi kubwa ya watoto wenye umri wa kuanzia miaka mitatu hadi minane na kuanzia miaka 45 na kuendelea Babati mkoani Manyara ndio wanasumbuliwa na magonjwa ya macho kwa kiasi kikubwa.Hayo yalibainika jana wilayani Babati baada ya watoto na wazee wengi kujitokeza kupata matibabu ya macho bure na Lion’s Club ya Arusha katika kituo cha afya cha Magugu.Huduma hizo zilikuwa zikitolewa kwa siku mbili kwa ufadhili wa msikiti wa dhehebu la Kalasinga katika sherehe za maadhimisho ya miaka 550 tangu kuanzishwa na Guru Nanak.Akizungumza wakati wa majumuisho, Katibu wa klabu hiyo, Chief Maswanya alisema wametoa huduma za matibabu ya macho kwa wananchi Babati na kuwapa dawa, miwani na kuwafanyia upasuaji waliokutwa na matatizo.“Idadi kubwa ya watu wamejitokeza kupata huduma hii ya macho, wengi wao waliokutwa na matatizo ya macho ni watoto wa miaka miaka mitatu hadi minane na wazee miaka 45. Kupitia takwimu za waliohudhuria tumeona kuna watu wengi wenye matatizo ya macho na hawana elimu kujikinga na ugonjwa,” alisema.Alieleza watu waliofanyiwa vipimo kwa siku mbili ni 875, kati ya hao 714 walipatiwa dawa, 632 miwani na 102 walikutwa na mtoto wa jicho na kufanyiwa upasuaji, huku wanne wakipewa rufaa hospitali ya rufaa ya KCMC.Alisema, watu wengine sita waliandikiwa barua kwenda kufanyiwa uchunguzi katika hospitali ya Mtakatifu Elizabeth iliyopo jijini Arusha.
1
Na RAMADHAN HASSAN-DODOMA SERIKALI inatafakari namna ya kusaidia sekta ya uwindaji isiathirike zaidi katika kipindi hiki cha sakata la ugonjwa wa corona. Hayo yalielezwa jana, jijini hapa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantino Kanyasu, alipokutana na wawakilishi wenye vitalu vya utalii nchini. Kanyasu alikiri kuwa biashara hiyo imekuwa ngumu zaidi katika kipindi hiki hivyo kwa namna yoyote hali haiwezi kutengemaa kwa wakati mfupi na kuwapa faida wenye vitalu. Alisema tishio la corona limekuwa na madhara katika sekta ya utalii ambapo Serikali inapaswa kutupia jicho kwa wazawa waliowekeza mitaji yao kwenye vitalu. Hata hivyo alisema ombi la kuwaondolewa kodi za vitalu linaweza kuwa gumu kutokana na kuwa lipo kisheria, lakini kwa upande wa tozo ambazo zipo chini ya Waziri wa Maliasili, jambo hilo ni muhimu kuwasaidia. “Mimi mwenyewe hivi karibuni nilitembelea baadhi ya hoteli ambazo zinaweza kulaza hadi watu 100, lakini nilikuta wapo watano hadi sita kwa baadhi maeneo kwa hiyo wanachokisema wako sahihi,” alisema Kanyasu. Mwenyekiti wa Chama cha Wawindaji Nchini (TAHOA), Michel Mantheakis alisema hali ilikuwa mbaya kwa zaidi ya miaka 10 iliyopita lakini kwa sasa imekuwa mbaya zaidi kutokana na corona. Michel alisema wageni wengi wameamua kuahirisha safari zao na baadhi wametoa taarifa kuwa watakuja mwakani huku wengine wakidai kurudishiwa fedha walizokuwa wametanguliza kwa madai watajipanga upya hali ikitulia jambo alilosema ni hatari kwa sekta ya utalii. Mwenyekiti huyo alisema kiwango cha fedha kinachopotea katika sekta hiyo ni kikubwa kwani Tanzania ingeingiza dolla 200,000 hadi 300,000 kwa kuwinda asilimia mbili tu ya wanyama wenye sifa za kuwindwa. Makamu Mwenyekiti wa Tahoa, Hilali Diffi alisema wanapitia katika kipindi kigumu kwa sasa lakini wanaamin Serikali ikiwasikiliza watavuka salama. Diffi alisema moja ya mapendekezo yao kwa Serikali ni kuongezewa muda wa siku 60 katika vitalu ambavyo walitakiwa kuvirudisha machi 30 badala yake wapewe muda wa hadi Mei 30 kabla ya kuvirudisha au kuhuisha.
1
 NA TUNU NASSOR -DAR ES SALAAM CHAMA cha ACT-Wazalendo kinatarajia kufanya Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia jijini Arusha, Machi 25, Mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Katibu wa Uenezi na Mawasiliano kwa Umma, Ado Shaibu, alisema katika mkutano huo kutafanyika mjadala wa kitaifa kutafakari miaka 50 ya Azimio la Arusha, mafanikio na mapungufu yake. “Mjadala huo utakuwa ni jukwaa la kutafakari misingi na nafasi ya Azimio la Arusha katika Tanzania ya leo, hivyo wananchi wote wanakaribishwa kuhudhuria,” alisema Shaibu. Alisema chama hicho kimealika vyama na kufanya mazungumzo na Chama cha Labour cha Uingereza, Economic Freedom Fighter (EFF) cha Afrika Kusini, Die Linke cha Ujerumani na Syriza cha Ugiriki. “Mkutano huo utajadili pia nafasi ya siasa za kijamaa na za mlengo wa kushoto barani Afrika na duniani katika zama za kukua kwa kasi kwa siasa za mlengo wa kulia,” alisema Shaibu. Katika hatua nyingine, Chama hicho kimemkumbusha Rais John Magufuli kutoingilia utawala wa sheria. “Katika kilele cha siku ya sheria duniani, Rais alisema watakaofanya makosa wafungwe siku hiyo hiyo, jambo linalokwenda kinyume na utawala wa sheria kwa mujibu wa Ibara ya 13.6,” alisema Shaibu.
1
Kwa mujibu wa taarifa ya TPDC kwa umma, kuingia kwenye mchakato wa zabuni ya nne ya vitalu vya utafiti uliozinduliwa Oktoba 25 mwaka huu, kila kampuni inayoomba itapaswa kulipa dola za Kimarekani 50,000 (Sh milioni 81.5 za Kitanzania) ambazo hazitarudishwa.Zabuni za safari hii zinahusisha vitalu saba vilivyoko bahari kuu na kitalu cha Kaskazini mwa Ziwa Tanganyika na kwamba waombaji wanapaswa kuwasilisha maombi kati ya sasa na Mei 15 mwaka kesho.Vitalu vya bahari kuu vipo katika kina cha maji kati ya mita 2000 na 3000 wakati kitalu cha Ziwa Tanganyika kinafikia kina cha mita 1,500.Aidha, kwa mwombaji wa vitalu vya baharini atalazimika pia kununua kifurushi cha lazima cha zabuni za vitalu vya bahari kuu kinachogharimu Dola 750,000 (Sh bilioni 1.2) kwa kila kifurushi, wakati kwa waombaji wa kitalu cha kaskazini ya Ziwa Tanganyika watalazimika kununua kifurushi cha dola 350,000 (Sh milioni 570).Makampuni yatakayobahatika kuingia katika mchakato na kupata vitalu, yatalazimika kuwa na mtaji wa dola za Kimarekani bilioni 2.4 (Sh trilioni 4 za Kitanzania) kwa ajili ya gharama za awali za shughuli za utafutaji mafuta na gesi asilia.“Makadirio haya hayahusishi gharama za kuweka miundombinu ya kuwezesha uzalishaji, usafishaji, uchakataji, uuzaji na gharama zinginezo. Gharama za uendelezaji kuweka miundombinu hadi kufikisha gesi kwa mtumiaji huweza kufikia hadi Dola za Marekani bilioni 15 (Sh trilioni 24.45),” inasema sehemu ya taarifa hiyo.Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya TPDC, gharama ya tathimini za kijiofizikia na kijiolojia ni dola milioni 10 (Sh bilioni 16), ukusanyaji wa takwimu za 2D na 3D 5 (dola milioni 25, sawa na Sh bilioni 40).Gharama za tathmini zote za kimazingira zinaonesha kufikia dola milioni 12 (Sh bilioni 19.5) na uchimbaji wa visima vitatu vya awali vya utafiti ni dola milioni 510 (Sh bilioni 831), kila kimoja kikigharimu dola 170,000 (Sh bilioni 277).Aidha, gharama nyingine kuelekea upatikanaji wa mafuta na gesi asilia ni dola milioni 900 (Sh trilioni 1.46) kwa ajili ya visima sita vya tathmini, huku visima vingine kumi vya uendelezaji vikigharimu dola bilioni 1 (Sh trilioni 1.63).Pamoja ya ukubwa wa gharama hizo, taarifa hiyo imeeleza licha ya zabuni kuwa wazi kwa makampuni ya ndani na ya nje ya nchi, utaratibu umewekwa ili kutoa upendeleo kwa makampuni ya ndani yaliyosajiliwa kwa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kumilikiwa na wazawa kwa asilimia zisizopungua 50 ikiwa yatatimiza vigezo vilivyowekwa.
0
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha ya awamu ya tatu yenye jumla ya wanafunzi wa mwaka kwanza 4,785 waliopata mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 14.3 bilioni. Kutokana na orodha hiyo sasa imefanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 162.86 hadi sasa kufikia 46,838.Orodha ya kwanza ilitolewa Oktoba 17 mwaka huu na ilikuwa na wanafunzi wa mwaka wa kwanza 30,675 waliopata mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 113.5. Orodha ya pili ilitolewa Oktoba 26 mwaka huu ikiwa na wanafunzi wa mwaka wa kwanza 11,378 waliopangiwa mikopo yenye thamani ya Sh bilioni 35.06. Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdulrazaq Badru imeeleza kuwa wanafunzi waliopata mikopo katika awamu ya tatu wanaweza kupata taarifa zao kupitia akaunti walizotumia kuomba mkopo maarufu kama SIPA(Student’s Individual Permanent Account). Pamoja na SIPA, Badru alisema majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo katika awamu hii ya pili yanapatikana katika mtandao wa HESLB wa uombaji mkopo (https://olas.heslb.go.tz) na tovuti ya Bodi (www.heslb. go.tz).“Awamu hii ya tatu inajumuisha wanafunzi wahitaji ambao wamekamilisha taratibu za udahili pamoja na kukamilisha marekebisho ya maombi yao yaliyokuwa na dosari ... tutaendelea kufanyia kazi maombi yanayorekebishwa na wale wenye sifa watapangiwa,”alisema.Kuhusu taratibu za malipo kwa wanafunzi, Badru alisema fedha za wanafunzi waliopata mikopo zimeshapelekwa vyuoni na vyuo vimeleekezwa kuhakikisha fedha zinawafikia wanafunzi walengwa mara wanapofika na kukamilisha taratibu za usajili. “Serikali imeshatupatia Sh bilioni 125 ambazo tulikuwa tunazihitaji kwa ajili ya malipo ya robo ya kwanza ya Oktoba hadi Desemba mwaka huu, sisi tumeshatuma vyuoni na maofisa wetu wameanza kwenda vyuoni ili kukutana na wanafunzi na kutatua changamoto iwapo zitajitokeza,”alisema. Badru alisema katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga Sh bilioni 450 kwa ajili ya jumla ya wanafunzi 128,285.Kati yao, wanafunzi 83,285 ni wenye mikopo wanaoendelea na masomo ya mwaka wa pili, tatu na kuendelea.
1
NCHI ZA za Tanzania na Uganda zimekubaliana kuuziana sukari pale nchi moja inapokuwa na ziada huku nyingine ina uhaba wa zao hilo, lakini baada ya wataalamu wa pande zote mbili kukutana na kujiridhisha kuwepo kwa ziada.Kujiridhisha huko ni pamoja na kuhakikisha wanaangalia uzalishaji na matumizi ya nchi husika kwa bidhaa hiyo ambayo mara nyingi imekuwa na changamoto kutokana na ukweli kuwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) hazijitoshelezi katika uzalishaji wa bidhaa hizo.Utata huo ulikuja baada ya sukari tani 600 kutoka Uganda kuzuiliwa kuingia Tanzania kutokana na kutofuatwa kwa taratibu.Akizungumza na gazeti hili, Ofisa Biashara wa wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Elia Chilangazi aliyeshiriki katika mazungumzo ya kuondoa utata wa kuuziana bidhaa hiyo kati ya Tanzania na Uganda jijini Kampala hivi karibu, amesema suala la bidhaa ya sukari ndani ya EAC ni nyeti, hivyo hawaruhusu kuuziana kutokana na kuwepo viwanda vidogo na kuchangia ajira katika nyanja mbalimbali ikiwemo wakulima wa miwa.Anabainisha kuwa ikitoa uhaba wa sukari wenye mamlaka ya kuagiza nje ya Tanzania ni Wizara ya Kilimo kupitia bodi ya sukari kwa kutoa vibali maalumu huku takwimu zikionesha Uganda uzalishaji wao bado chini kiasi ambacho nao wanaagiza nje.“Hivyo katika majadiliano haya, ni lazima kujiridhisha kama kuna ziada hususan katika kipindi cha Machi mpaka Juni ambapo kunakuwa na mvua hivyo miwa kukosa sukari na viwanda kufanya matengenezo nchini,” amesema.Alisema katika kipindi hicho lazima wataalamu wa nchi husika kujadiliana kama nchi mojawapo ina sukari ya ziada na kujiridhisha inatoka nchi husika kwa kuunda timu ya wataalamu wa nchi hizo mbili kuangalia mifumo ya kuagiza ili kuepuka kufanyiwa ujanja wa kuagiziwa sukari nje ya EAC na kuuza nchi nyingine.Alibainisha kuwa ikiwa itatokea kuridhika na kufikia muafaka wa nchi moja kuuziwa sukari katika jumuiya hiyo hakuna kutozwa kodi kwa kuzingatia vigezo stahili kwa lengo la kulinda viwanda ndani ya Jumuiya.“Kawaida katika jumuiya hatufanyi biashara, kwani tunazalisha sukari lakini haitutoshi hivyo siku nchi moja ikiwa na sukari ya kutosha kwa matumzi ya nchi hiyo pamoja na ziada, baada ya matumizi unaweza kuuzia nchi nyingine kwa kufuata utaratibu,” alisisitiza.Alisema katika majadiliano hayo ambayo hakukuwa na wataalamu wa wizara ya kilimo na bodi ya sukari, walikubaliana kuendelea na majadiliano mengine katika vikao vya wataalamu wa nchi hizo.Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania, Miraji Kipande alibainisha kuwa bado kuna upungufu katika uzalishaji wa sukari nchini ambapo sukari ya viwandani haizalishi kabisa nchini hivyo kuingiza zote kutoka nje ya nchi.Amesema, lakini kwa mwaka huu wanatarajia kuzalisha kwa wastani wa tani 355,641 za sukari ya mezani huku kukiwa na upungufu wa sukari hiyo kwa takribani tani 159,359.Kipande amesema katika kuhakikisha wanaziba pengo la upungufu huo, wanaendelea kutekeleza mpango wa miaka mitano, ikiwa ni pamoja na hivi karibuni kufunguliwa kwa kiwanda cha sukari cha Bakhresa na Mkulazi huku viwanda vingine vikiwa katika hatua mbalimbali.“Pia bodi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwenye mpango wetu wa miaka mitano ni ujenzi wa viwanda vipya na upanuzi wa mashamba ya miwa ikienda sambamba na kuwaalika wawekezaji zaidi huku wakihakikisha wanalinda soko la sukari nchini,“ amesema.Aliunga mkono maamuzi ya serikali katika kikao cha pamoja cha Uganda na Tanzania kwa kueleza kuwa walishafanya majadiliano ya ndani ya wadau wa sukari kabla ya maofisa na wataalamu kwenda Uganda.Katika mkutano huo, ilidaiwa kuwa kuwa Tanzania inatoza asilimia 25 ya ushuru wa forodha kwa bidhaa za Uganda kama sukari, pipi na nyinginezo. Bidhaa hizo hupitishwa bila kodi chini ya protokali ya soko la pamoja.Ripoti maalumu ya mkutano huo iliyotolewa nchini Uganda inaeleza kuwa ulihudhuriwa na makatibu wakuu kutoka nchi hizo mbili ya Jumuiya ya EAC na kubainisha kuwa, Uganda inazalisha ziada ya tani 40,000 za sukari kwa mwaka.“Mkutano huu wamekubaliana nchi hizo mbili kukiwa na uhaba wa sukari, Tanzania itapatiwa kipaumbele kuingiza sukari kutoka Uganda, ikiwa kuna shaka yoyote kuhusu uzalishaji wa sukari hizo, ni vema kufanyika uhakiki,“ ilisema ripoti ya mkutano huo.Katika Mkutano wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Dk John Magufuli wa Tanzania hivi karibuni, walijadiliana kuhusu watanzania kuingiza sukari kutoka nchi hiyo.Magufuli alibainisha kuwa Uganda imekuwa ikiingiza sukari kutoka nchi nyingine na kuuza nchini Tanzania, jambo ambalo ni kwenda kinyume na Protokali ya Soko la Pamoja ya jumuiya ya EAC.Mei mwaka huu, Tanzania ilizuia takribani tani 600 za sukari zilizokuwa zikiingizwa kutoka Uganda kutoka kiwanda cha Kakira Sugar Works.Mwenyekiti wa Chama cha wenye viwanda Uganda, Jim Mwine Kabeho, alieleza kuwa ni ngumu kulifikia soko la Tanzania kwa sababu baadhi ya maofisa wagumu katika kuruhusu biashara hiyo.Katibu Mkuu wa wizara ya viwanda Uganda, Balozi Julius Onen, alisema nchi hiyo inataka kuwepo na mifumo inayoruhusu nchi wanachama kuwa za kwanza inapotokea upungufu.
1
  HAVANA, CUBA VIONGOZI kadhaa wa Afrika na Amerika ya Kusini jana walihudhuria ibada ya mazishi na mkutano mkubwa wa hadhara kumkumbuka aliyekuwa Kiongozi wa Cuba, Fidel Castro, aliyefariki dunia Ijumaa iliyopita akiwa na umri wa miaka 90. Hata hivyo, Rais wa Marekani, Barack Obama na viongozi kadhaa wa Ulaya hawakuhudhuria ibada hiyo. Marekani ilikuwa haijatangaza atakayeongoza ujumbe wake, huku Canada ambayo Waziri Mkuu wake Justin Trudeau alishutumiwa kwa kumtaja Castro kama kiongozi wa kipekee, ikiwakilishwa na Gavana David Johnston. Kansela wa zamani wa Ujerumani, Gerhard Schroeder alimwakilisha Kansela Angela Merkel katika ibada hiyo. Waziri Mkuu wa Ugiriki, Alexis Tsipras ni kiongozi pekee wa Ulaya aliyethibitisha kuhudhuria. Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, Teodoro Obiang Nguema wa Guinea ya Ikweta, Jacob Zuma wa Afrika Kusini na Uhuru Kenyatta wa Kenya walihudhuria ibada hiyo. Aidha viongozi wa nchi za Amerika ya Kusini wakiwamo Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro na Evo Morales wa Bolivia walihudhuria ibada hiyo. Kwa wengi katika nchi za Amerika ya Kusini na Afrika, Castro ni ishara ya shujaa aliyepinga ubeberu, kwa kumng’oa madarakani kiongozi dikteta aliyekuwa anaungwa mkono na Marekani, Fulgencio Batista. Hata hivyo, wengine wanamshutumu kuwa dikteta ambaye sera zake za ujamaa ziliuharibu uchumi wa Cuba. Korea Kaskazini iliyosema kuwa imempoteza mshirika wake mkubwa dhidi ya Marekani, imetangaza siku tatu za maombolezo.
3
Uhusiano kati ya msanii Diamond Platnamz na Tanasha Donna ilisambaratika ghafla bila kutarajiwa, hii ni baada ya Tanasha mwenyewe kujitokeza wazi na kueleza kuwa uhusiano wao ulikuwa imara na kuwa hakuna lolote ambalo lingeweza kuusaambaratisha. Mwezi mmoja baadaye, wawili hao walipeana visigo na visigino. Huku wengi wakisalia na uvumu tu kuhusu kilichowakosanisha wawili hao, Diamond sasa amejitokeza wazi kutegua kitendawili. Akihojiwa katika Wasafi fm Jumatatu, Aprili 27, Mondi alieleza kuwa alikuwa na mpango wa kumfungisha pingu za maisha Donna kabla mambo yote kuenda mrama na kila mmoja kuenda zake. #GoodMorning "Misukumo ya kusaidia watu , imetokana na malezi niliyolelewa, maisha niliyotokea na historia yangu ya nyuma. Nikikumbuka shida nilizopitia , napata Moyo wa kusaidia Wengine " – @diamondplatnumz . . Endelea kusikiliza 88.9 @wasafifm MUDA HUU mpaka saa 2:30 asubuhi na Kutazama @wasafitv, pia unaweza kufuatilia matangazo haya moja kwa moja kupitia Channel yetu ya YouTube #WasafiMedia #GoodMorning na @zembwela @rwenyagira salmadacotha @charles_william2 #HabariZaAsubuhi A post shared by DIAMOND PLATNUMZ 🦁 (@diamondplatnumzfamily) on Apr 26, 2020 at 10:23pm PDT Kulingana na msanii huyo, walitofautiana kuhusu baadhi ya masuala muhimu na ndiyo ikabidi watengane. ‘’ Siwezi kusema kiundani maana hata Tanasha hajajitokeza wazi kwa umma kueleza kuhusu chanzo cha kutegana kwetu. Kilichofanyika kilituzidi na ndiyo maana tukaamua kujipa nafasi. Hatukuachana maana nilikuwa na mpenzi wa kando. Nilikuwa mtiifu kabisa nilipokuwa katika uhusiano na Tanasha na nilikuwa tayari kumuoa. Ni ile tu hatukukubaliana kuhusu masuala mengine muhumi kama vile familia na maisha ya baadaye. Tulikuwa tukihitaji vitu tofauti na hakuna aliyekuwa tayari kulegeza msimamo. Tuliachana na Mungu akipenda tunaweza kurudiana,’’ Alisema Mondi. By @diamondplatnumz Nisikile Live kupitia GOOD MORNING ya 88.9 @wasafifm Muda Huu… waweza sikiliza na kutazama pia kupitia Channel yao ya youtube WASAFI MEDIA A post shared by DIAMOND PLATNUMZ 🦁 (@diamondplatnumzfamily) on Apr 26, 2020 at 10:19pm PDT Baba huyo wa wanne alikiri kuwa alikuwa na nia kubwa ya kumuoa Tanasha. ”Ukweli nilitaka kumuoa Tanasha 100% lakini hatukuwa katika ukurasa mmoja kwa baadhi ya vitu,’’ aliongezea. Tofauti na jinsi wengi walivyotarajia kuwa msanii huyu tayari amekwachua kipenzi mwengine baada ya kutengana na Donna, alikiri kuwa  hayuko katika uhusiano wowote wa kimapenzi. Mondi alieleza kuwa anaipa kazi kipaumbele  nakuamua kupigisha breki kidogo masuala ya mahusiano.
4
Na Bethsheba Wambura,Dar es Salaam IKIWA imepita miezi sita tangu mwanamuziki, Ambwene Yessayah (AY) na Remy wafunge ndoa usiku wa kuamkia Jumatatu Agost 13,2018 leo wamebarikiwa kupata mtoto wa kiume waliyempa jina la Aviel lenye maana kwamba ‘God is my father’,. Akitumia ukurasa wake wa Instagram kuweka wazi kuhusu ujio wa mtoto huyo AY ameandika kwamba mkewe amejifungua katika hospitali ya Medical City Healthcare Dallas- Texas huko Marekani. “Mungu ni mwema na namshukuru sana kwa kutubariki mimi na mke wangu mrembo Remy, tumempata mtoto wa kiume na tumempa jina la Aviel lenye maana ya ‘God is my father’, ameandika AY. AY na Remy ambae ni raia wa Rwanda walifunga ndoa Februari 24,mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo kulihudhuriwa na mastaa kibao.
4
NA CHRISTOPHER MSEKEN MICHORO ya mwilini inayofahamika kama ‘Tattoo’ imekuwa ikitumiwa na watu mbalimbali katika kuhifadhi kumbukumbu ya vitu ambavyo mchorwaji anakuwa amavidhamiria kuviweka kwenye mwili wake. Tattoo inaweza kuchorwa kama urembo, kumbukumbu  au alama ya kitu fulani ambacho kinakuwa na umuhimu kwa mtu aliyechora ndiyo maana tunaona wapendanao wengi wakichorana michoro hiyo kama alama ya inayoonyesha upendo wao. Bongo pia tumeendelea kushuhudia mastaa mbalimbali wakionyeshana ubabe wa kupendeza kwa kuchora tattoo zenye maana tofauti huku kapo kadhaa za mastaa nazo zikichorana michoro hiyo iliyoanza kuchworwa kitamaduni nchini Japani mnano karne ya 18. Juma3tata leo tunakuletea orodha ya mastaa wa Bongo ambao walipagawa na mapenzi kiasi cha kuchora tattoo za wapenzi wao na baadaye kuzifuta baada ya kapo zao kuvunjika. Amber Lulu & Young Dee Julai 20 mwaka huu, ilifahamika kuwa Amber Lulu ameifuta tattoo yenye jina la Young Dee katika mkono wake na kubadilisha mchoro. Wawili hao wote wawili wamewahi kukanusha kuwa wapenzi japo kuwa Young Dee amewahi kunukuliwa akisema yeye na Amber Lulu waliwaahi kudondoka kitandani. Shilole & Nuh Mziwanda Shilole hivi sasa ameposwa na jamaa anayeitwa Asharafu Uchebe na ndoa yao inatarajia kutikisa nchi ifikapo Desemba 20 mwaka huu, siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mrembo huyo. Lakini Shilole enzi za ujana wake kwenye tasnia ya mapenzi aliwahi kuwa na uhusiano na msanii, Nuh Mziwanda, penzi lao lilikuwa maarufu mno kutokana na matukio waliyokuwa wanayafanya pamoja. Desemba 30 mwaka 2015 ilifahamika kuwa Shilole aliifuta tattoo yenye jina la Nuh Mziwanda aliyoichora katikati ya maziwa yake, aliibadili na ikawa kama ua fulani hivi nzuri nzuri. Hali kadharika Februari 7 mwaka 2016, Nuh naye aliifuta tattoo ya Shilole iliyokuwa kwenye mkono wa kushoto ikisomeka Shishi Baby, alifanya hivyo baada ya penzi lao kuvunjika. Nawal Huyu ni mzazi mweza wa Nuh Mziwanda. Wawili hawa walifunga ndoa kamili ya Kiislamu, Novemba 10 mwaka jana na kufanikiwa kupata  mtoto mmoja anayeitwa Anyagile. Mwaka huu ndoa hiyo ilivunjika baada ya Nuh kurudi kwenye dini yake ya Kikristo ambapo enzi wapo pamoja, Nawal alijichora Tattoo yenye jina la Nuh Mziwanda ambayo hivi sasa ameibadilisha na imekuwa kama mchoro wa ua. Fahamu Kuwa hao ndiyo mastaa ambao walifuta Tattoo za wapenzi wao baada ya kapo zao kuvunjika lakini pia nikujuze kuwa msanii Harmonize naye aliwahi kufuta tattoo yenye sura ya bosi wake (Diamond Platnumz,) kisha kuichora tena nyingine nzuri kwenye mkono ikiwa chini ya tattoo nyingine yenye sura ya mama yake mzazi, hiyo ilikuwa mwaka jana mwezi Agosti. Kwa maoni, ushauri na pongezi zako tuma meseji kwenye namba 0756 074 048.
4
RAIS wa Tanzania Dk John Magufuli ameruhusu makontena yenye makinikia yaliyokamatwa bandarini Dar es Salaam yauzwe.Ameagiza yakabidhiwe kampuni ya Twiga Minerals Corporation, atafutwe mteja yauzwe ili Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick wanufaike.Ametoa ruhusa hiyo leo Ikulu, Dar es Salaam baada ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Barrick kusaini mikataba tisa ya makubaliano yakiwa ni matunda ya mazungumzo yaliyoanza mwaka 2017.Kwenye tukio hilo lililohudhuriwa pia na viongozi wakuu wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais amesema, kusainiwa kwa mkataba kati ya Tanzania na kampuni ya Barrick ni ushindi mkubwa na anamshukuru Mungu kwa hilo.“Na hicho ndicho tulichokuwa tunakitaka, kwa hiyo makubaliano haya yamemaliza tag of war kati ya pande zote mbili. Na kuanzishwa kwa kampuni hii ya Twiga sasa nataka kuwahakikishia katika pande zote mbili mnaoendesha kampuni yale makontena ambayo yako bandarini ambayo tuliyashika sasa mkatafute wabia vizuri muuze kwa faida ya kampuni ya Twiga”amesema Rais Magufuli.Rais amesema kusainiwa huko ni mwanzo wa ukurasa mpya msafi sana na maisha mapya na amezitaka pande mbili zinazomiliki kampuni ya Twiga zisimamie utekelezaji wa makubaliano hayo.Ameihakikishia kampuni ya Barrick na wawekezaji wengine duniani kuwa kuwa Tanzania ni eneo bora zaidi kwa uwekezaji hasa ikizingatiwa kuwa ni nchi tajiri.“Na ndugu zetu Barrick I can guarantee you now the game is over (nawahakikishia tatizo limekwisha), chapeni kazi, kafanyeni kazi kwa sababu ninyi Barrick mna expertise (utaalamu), mna capital (mtaji), sisi we have the raw materials (tuna malighafi). Dhahabu iliwekwa Tanzania, haikuwekwa kwingine, aliyeiweka Tanzania ana makusudi nayo”amesema Rais Magufuli.
0
WAZIRI wa Nchi, Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika anaondoka nchini leo kwenda Japan kuhudhuria sherehe za kuapishwa na kutambulishwa kwenye Jumuiya ya Kimataifa, Mfalme Naruhito wa Japan.Kwa kujibu wa taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkuchuka na ujumbe wake wanamwakilisha Rais John Magufuli katika sherehe hizo zitakazofanyika Oktoba 22 mjini Tokyo na watarejea nchini Oktoba 24,mwaka huu. Safari hiyo imekuja kufuatia mwaliko rasmi uliotolewa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwa Rais Magufuli.Kwa mujibu wa katiba na sheria za Kifalme za Japan, Mfalme Naruhito amerithi kiti cha Baba yake, Mfalme Akihito ambaye alitangaza kujiuzulu rasmi nafasi yake Aprili 30, mwaka huu, kutokana na umri wake kuwa mkubwa sanjari pia na kusumbuliwa na matatizo ya kiafya. Mfalme Naruhito alichukua madaraka hayo Mei Mosi mwaka huu.
1
KULWA MZEE -DAR ES SALAAM VIGOGO sita wa Kampuni ya Viettel Tanzania akiwemo Mkurugenzi wa Halotel, Son Nguyen (46), wanaokabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh bilioni 78, wanaendelea kusota rumande wakisubiri majibu kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini. Washtakiwa hao ambao kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Machi 27 mwaka huu, jana walisomewa kesi yao kwa njia ya Mahakama Mtandao ambapo upande wa Jamhuri ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kwamba upelelezi haujakamilika. Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alidai upelelezi haujakamilika na akaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Wakili wa utetezi, Benedict Ishabakaki akijibu alidai waliandika barua kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kumaliza kesi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) hivyo wanaendelea na mazungumzo na ofisi ya DPP. Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja hizo, alisema mazungumzo yakikamilika kabla ya tarehe ya kutajwa tena Julai 22 mwaka huu washtakiwa wataletwa kwa hati ya wito. Awali ilidaiwa kuwa washtakiwa hao  Aprili 21 mwaka huu waliandika barua kwa DPP kukiri makosa. Barua hiyo inadaiwa ilipokewa, majadiliano yalianza na yalikamilika kwa kiasi kikubwa, kinachosubiriwa ni hati ya kuipa mamlaka Mahakama ya Kisutu kuendelea na shauri hilo kutoka kwa DPP. Mbali na Nguyen washtakiwa wengine ni Nguyen Minh (40)  na Vu Tiep wote ni Mameneja wa Halotel, Ha Than (39) ambaye ni Mtaalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) Halotel, Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni hiyo, Nguyen Cong na Kampuni ya Viattel. Awali waliposomewa mashtaka Machi 27 mwaka huu mbele  ya Hakimu Simba, washtakiwa hao walidaiwa  kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, waliongoza genge la uhalifu ili kujipatia faida. Inadaiwa kati ya Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020  maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi, kwa pamoja walitumia masafa ya redio bila kupata kibali kutoka TCRA. Pia inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu maeneo hayo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Vietnam kwa pamoja walitengeneza mfumo ambao ulitumia huduma za mawasiliano zinazojulikana kama Virtual Private Network (VPN) kinyume na taratibu. Katika shtaka la nne, inadaiwa washtakiwa hao walikwepa kulipa kodi kwa TCRA kwa kutumia mitambo ya mawasiliano yaliyounganishwa Viettel Tanzania na Vietnam  kinyume na sheria. Inadaiwa Juni 8, 2017 na Machi 26, 2020 maeneo hayo kwa kutumia masafa ya redio bila kupata kibali cha TCRA walisababishia mamlaka hiyo hasara ya Sh bilioni 75. Pia wanadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu kwa kutumia mitambo ya VPN waliisababishia TCRA hasara ya Sh bilioni 3.03. Katika shtaka la saba, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 3.03 wakati wakijua fedha hizo ni zao la makosa ya kuongoza genge la uhalifu. Kampuni ya Viettel Tanzania inadaiwa kati ya Julai 7, 2016 na Machi 26, mwaka huu ilitakatisha Sh bilioni 3.03 na shtaka la tisa na 10, washtakiwa wote wanadaiwa kutakatisha Sh bilioni 75 wakati wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu.
0
JanethMushi, Longido Shirika la Kijamii la Tembo Trust, limetoa elimu kwa wanafunzi wa kike wa Shule ya Msingi Orbomba ya namna ya kuripoti matukio ya ukatili yanayowakabili katika jamii zao na kuwataka wanafunzi hao kuwa mabalozi wazuri katika kupinga vita dhidi ya ndoa za utotoni na ukeketaji. Akizungumza juzi katika mafunzo hayo mwezeshaji wa elimu kutoka shirika hilo, Mery Tembo, alisema kwa sasa katika jamii nyingi hususani za kifugaji wamekuwa wakiwakeketa watoto katika umri mdogo hali inayochangia ukatili kwa mtoto wa kike. Amesema mbali na ukeketaji kumekuwa na tabia ya kuozesha watoto wa kike wakiwa katika umri mdogo hali inayochangia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, hivyo kuwataka wanafunzi hao kuripoti matukio ya ukatili wa kijinsia wanaofanyiwa ili sheria ichukue mkondo wake na kudhibiti vitendo hivyo. Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika hilo Paulina Sumayani, alisema hadi sasa wamefanikiwa kuwaokoa wasichana 14 waliokuwa wafanyiwe ukeketaji na kuwasaidia kupata haki zao za msingi ikiwamo elimu. Naye mwakilishi wa wanafunzi kutoka katika shule hiyo, Prisila Lazaro, amewaomba wadau wa maendeleo kushirikiana na serikali kutoa elimu kwa jamii hasa juu ya athari za ukeketaji kwa watoto wa kike ili jamii iachane na mila na desturi potofu. “Tunaomba wadau waendelee kushirikiana naserikali kutoa elimu kwa wazazi na jamii nzima, kuna wakati hatuna amani ya kurejea majumbani shule zinapofungwa, kutokana na baadhi ya wazazi hasa akina baba kulazimisha watoto wa kike waolewe, wasirudi shule,” amesema.
5
Na KYALAA SEHEYE INAKUWAJE Pale ambapo unakuwa na hamu ya kutoka kimapenzi na mtu maarufu harafu hupati nafasi hiyo kufuatia staa unayemtamani yupo kwenye penzi zito na mtu mwingine? Bila shaka picha zake zinaweza kuwa tulizo lako tosha. Ukubwa wa majina ya mastaa unaongeza idadi ya mashabiki wanaotamani kutoka nao kimapenzi ila hawapati fursa hiyo kwa sababu tu ya umbali na ugumu wa kukutana na mastaa hao. Mara nyingi wasanii wakike hupiga picha za utupu na kusisambaza kwenye mitandao ya kijamii kwa lengo la kusaka kiki na kukata kiu ya mashabiki wa kiume wenye mawazo ya kuja kutoka nao kimapenzi. Ni nadra mtu maarufu wa kiume kupiga picha zinazoonyesha sehemu kubwa ya mwili wake kwa lengo la kuwaridhisha watoto wa kike ambao wamekuwa wakimsumbua kwa kumtaka kimapenzi. Wiki hii Chombezo Tata limekutana na staa wa filamu za kibongo Daudi Michael ‘Duma’ ambaye wiki jana kwenye mitandao ya kijamii zilisambaa picha zinazoonyesha sehemu kubwa ya mwili wake. Picha hizo zimepokelewa kwa mitazamo tofauti na mashabiki ambao walianza kumuona toka akiwa kwenye tamthilia ya Siri ya Mtungi na ile ya Nira aliiyofanya nchini Kenya hali kadharika katika filamu kama Mchongo Siyo, Mfadhili Wangu  na Chutama. AZITOLEA UFAFANUZI Baada ya Chombezo Tata kumuweka kikaangoni, Duma anasema yeye ni mwanamitindo ambaye ameshafanya matangazo kadhaa na kampuni mbalimbali na zile picha zilizovuja mtandao zilikuwa ni kwa ajili ya moja ya kazi zake. Na jambo la kushangaza zaidi picha hizo ziliwafurahisha wanawake wengi waliokuwa wanamsumbua kwa kumtaka kimapenzi, wengi wao walimpigia simu na kumpongeza kwa kuwa ziliwavutia. “Najua watu wameni tafsiri vibaya ila nashukuru baada ya picha zile kusambaa, simu za wanawake waliokuwa wananitongoza zimepungua, kwani wametumia picha zangu kwa kujiliwaza na kumaliza matamanio yao hivyo sitegemei tena kusumbuliwa kama zamani,” anasema Duma. LENGO LAKE HASA Duma anasema hii ni dunia ya utandawazi, watu maarufu wanapendwa kimapenzi na watu wengi hivyo njia rahisi ya kukata kiu ya maelfu ya mashabiki warembo/watanashati ni kuwapa fursa ya kuwa picha hizo za utupu. “Nchi nyingi zilizoendelea mastaa wanafanya hivi, ili kulinda afya zao na kuepusha skendo za kutoka na wanawake au wanamume wengi, hii ni njia rahisi ya kumsaidia yule mwanamke ambaye hawezi kunifikia, nimeonekana mtu wa ajabu ila nalinda afya na jina langu,” anasema Duma. MPENZI NA FAMILIA YAKE JE? Mkali huyu anasema kwa sasa yupo singo japo kuwa ni baba wa watoto wawili ila upande wa familia yake jambo hilo walilipokea vibaya lakini aliwaelewesha wakaelewa. “Hakuna ndugu anayependa ndugu yake aharibikiwe au afe kwa maradhi kwa hiyo mimi nina sababu za msingi za kufanya hivyo ndiyo maana familia yangu ikanielewa pia,” anasema. AJIBU VIJEMBE VYA MASHABIKI Duma anasema amepokea maoni mbalimbali ya mashabiki ila kwa wale waliomuelewa vibaya na kumtukana wanapaswa kufahamu kuwa yeye anajitambua na endapo asingefanya hivyo na kushiriki ngono na wanawake wengi pia wangemtukana. “Najua watu wamelipokea tofauti jambo hili ila ningekuwa na mademu wengi pia ingekuwa ni tatizo na pia siwezi kufanya jambo likampendeza kila mtu aliyeelewa ameelewa na atakayechukia basi acha achukie,” anasema. KAZI KAMA KAWA Anasema yeye ni msanii wa kwanza wa filamu anaye washirikisha mashabiki kazi zake kabla hazijatoka na kuvutia kampuni mbalimbali kutangaza kwenye filamu zake anazoziweka katika chaneli yake ya Youtube.
4
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM KIJANA Baraka Elias (35), mwenye urefu wa futi 7.4 ambaye ameshindwa kufanyiwa matibabu ya kubadilishwa nyonga katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI), amevunja ukimya na kueleza changamoto zilizosababisha ashindwe kupatiwa matibabu kutokana na urefu wake usiokuwa wa kawaida. Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwa wazazi wake Mtaa wa Bwela, Pugu Majohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam jana, Elias alisema madaktari wameshindwa kumtibu kwa sababu mashine za MOI hazilingani na urefu wake. Alisema anatarajia kupewa rufaa ili akatibiwe nje ya nchi. “Madaktari wamenieleza bado wanafanya mazungumzo na wenzao wanaoshirikiana nao kutoka nje ya nchi ili wajue ni nchi gani itakuwa tayari kunichukua kufanikisha matibabu yangu. “Sielewi matibabu yatagharimu kiasi gani cha fedha, nitatumia muda gani na vifaa gani hadi kukamilika,” alisema. Elias alisema alifikishwa katika taasisi hiyo, Aprili mwaka huu baada ya kupewa rufaa kutoka Hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma. Akizungumzia chanzo cha tatizo lake, Elias alisema alipata hitilafu ya nyonga baada ya kuanguka kwenye ngazi za nyumbani kwake mkoani Ruvuma na tangu wakati huo hakuweza kuendelea kufanya shughuli zake za kiuchumi. Alisema baada ya muda kidogo alipelekwa Hospitali ya Peramiho ambako alifanyiwa kipimo cha X-ray na kuonekana nyonga yake ilikuwa imevunjika.   ALIVYOPOKEA RIPOTI YA MOI Elias ambaye muda wote anaonekana kuwa mchangamfu, alisema taarifa aliyopatiwa na madaktari wa MOI kwamba anapaswa kupewa rufaa kwenda kutibiwa nje ya nchi aliipokea kwa mtazamo chanya. “Niliona ni hali ya kawaida kwa sababu kupewa rufaa ni mfumo wa kawaida wa kimatibabu, madaktari wana utendaji wao… wanapoona wameshindwa wanakupeleka kwingine ambako unaweza kupata msaada zaidi na ndiyo maana nilitolewa Peramiho kuja MOI.   HAWEZI KUPANDA DALADALA Alisema kwa sasa hawezi kupanda daladala kutokana na urefu wake kwani kukaa kwenye kiti huwa ni changamoto kubwa kwake kwa sababu siti zake zimetengenezwa kwa kujibana. “Zamani nilipokuwa mzima nilikuwa napanda daladala, nilikuwa napata shida kukaa, jinsi zilivyotengenezwa hazina nafasi ya kutosha tofauti na gari za wenzetu (wazungu) zimetengenezwa kwa kuachanishwa nafasi mtu yeyote anaweza kukaa bila usumbufu,” alisema.   UREFU KWENYE DNA Elias alisema wazazi wake wamemweleza kuwa urefu alionao ni wa kurithi kutoka kwenye kizazi chao, kwani hata mababu zake wapo ambao walikuwa warefu. “Wazee hao wanatoka katika pande zote mbili, yaani kwa baba na kwa mama, sijui watu wananichukuliaje jinsi nilivyo, binafsi najiona kawaida na wengine kwa sababu hata hapa nyumbani hakuna aliye mrefu zaidi yangu,” alisema.   CHANGAMOTO Alisema changamoto kubwa anayokabiliana nayo hivi sasa ni usafiri wa kumtoa nyumbani hadi Muhimbili kupata matibabu. “Huwa tunalazimika ama kukodi gari kutoka nyumbani hadi hospitalini au tunaazima la mtu tunaweka mafuta,” alisema.   KUPANDA NDEGE Elias alisema iwapo rufaa itapatikana hahofii kama atashindwa kuingia ndani ya ndege kwa safari ya matibabu nje ya nchi. “Kama nilivyoeleza awali, wazungu huwa wanafikiri mbali, wanafanya vitu vikubwa. Huko kwenye nchi zao wapo warefu zaidi yangu na wanapanda ndege kama watu wengine. “Hata gari zao wanazotengeneza siku hizi ni za tofauti, hivi karibuni tu Japan ilitoa hizi gari ndogo ambazo zina uwezo wa kusogeza kiti nyuma na ukakaa vizuri, najua nitaweza kuingia ndani ya ndege,” alisema.   AOMBA MSAADA Elias alisema ingawa kanisa analoabudu linashirikiana naye bega kwa bega, msaada mkubwa kwake umebaki kwa familia yake. Kutokana na hali hiyo, anaomba msaada kutoka kwa mtu, mashirika au taasisi yoyote itakayoguswa na mkasa wake. “Siwezi kufanya kazi, kila siku nahitaji fedha za matumizi, nahitaji msaada, naamini wapo watakaoguswa, nipo tayari kwa msaada wowote kwa sababu nina changamoto nyingi, naumwa sijui lini nitapata matibabu, nategemea majibu ya madaktari,” alisema. Soma historia yake kesho
1
WANAHARAKATI ngazi ya jamii kutoka Kituo cha Taarifa na Maarifa Kipunguni, Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam, wamezindua kampeni ya kupinga rushwa ya ngono na ukeketaji kwa mwaka 2018. Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo ambayo imefadhiliwa na Shirika la Women Fund Tanzania (WFT), Mwenyekiti wa Mtaa wa Amani, Dani Maragashimba, aliwataka wananchi katika mtaa wake kuhakikisha kila mmoja anasimama katika nafasi yake kukomesha vitendo vya ukeketaji na rushwa ya ngono. Mbali na kutoa wito huo, alisema atasimama kidete pamoja na wanaharakati hao katika kupinga vitendo hivyo vya ukatili na ili kumfanya mtoto wa kike kupata furaha sawa na anayoipata mtoto wa kiume ikiwa ni pamoja na kupata elimu. “Lengo ni hadi kufikia Desemba mwaka 2018, tusisikie kunaripotiwa vitendo vyovyote vya rushwa za ngono maofisini na mitaani ikiwa ni pamoja na ukeketaji watoto wa kike na udhalilishaji wa kijinsia,” alisema Maragashimba. Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo hicho, Seleman Bishagazi, alisema wameamua kuanzisha harakati hizo mapema kutokana na kwamba shughuli za ukeketaji hufanyika katika miaka inayogawanyika kwa mbili. Alisema wanaamini kama wazazi na watoto watakuwa na uelewa wakutosha kuhusu madhara ya vitendo vya ukatili wa kingono na ukeketaji, itasaidia kujua namna ya kukabiliana navyo pale vinapotokea kwenye jamii. “Tunaamini mzazi akijua maana na madhara ya rushwa ya ngono, itakuwa rahisi kumwelimisha mwanawe na lengo letu ni kuona watoto wajue madhara ya jambo hili wakiwa wangali wadogo kwani hata wakienda shuleni, vyuoni na maofisini watakuwa wanajua namna ya kukabiliana na vitendo hivyo. “Suala la ukeketaji sisi kama wanaharakati ngazi ya jamii tumekuwa tukifanya jitihada kubwa kupambana na suala hili hasa ukilinganisha kila mwaka unaogawanyika kwa mbili ndio watoto huwa wanakeketwa. “Kesi ambazo tumekuwa tukikimbizana nazo kwa kuwakamata wazazi na mangariba wanaokeketa na kuwapeleka polisi mwisho wa siku zimekuwa zikiishia hewani kwa sababu zimekuwa zikikosa ushahidi kwani ni vigumu mtoto kwenda kuwatolea ushahidi familia yake,” alisema Bishagazi.
1
KIONGOZI wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amesema kuwa matamshi ya Rais wa Marekani Donald Trump aliyemtaja kuwa ‘’na matatizo ya kiakili’ yamemwongezea motisha zaidi ya kuendelea kutengeneza makombora ya taifa lake. Katika taarifa  binafsi isiyo ya kawaida, Kim amesema Rais Trump ‘atalipia kauli’ zake alizotoa wakati akihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambapo alionya ataiangamiza Korea Kaskazini pale Marekani itakapolazimika kujilinda. Trump naye alijibu akisema kuwa ‘mwenda wazimu’ hajawahi kufanyiwa atakachofanyiwa akijaribu. Mataifa hayo mawili wamejibizana kwa kurushiana maneno makali katika siku za hivi karibuni. Rais Kim alimaliza taarifa yake kwa kusema atamnyamazisha kiongozi huyo ”aliye na akili pungufu’ kwa vita. China ilijibu vita hivyo vya maneno ikionya kuwa hali ni mbaya. ”Pande zote zinapaswa kujikaza badala ya kuchokozana” , alisema msemaji wa Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Lu Kang. Urusi pia ilitoa wito wa kuvumiliana  na kusema vita maneno ya kitoto baina ya viongozi hao wawili ni kama wanafunzi wa chekechechea. Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Dmitry Peskov alisema kuwa Moscow ina wasiwasi kuhusu kiwango cha wasiwasi kinachozidi kuongezeka. Korea Kaskazini imekuwa ikifanyia majaribio makombora yake katika kiwango kisicho cha kawaida na kufanya jaribio lake la sita la kinyuklia licha ya vikwazo na shutuma za kimataifa.
3
.Chris Brown ameweka wazi sura ya mtoto wake wa kiume na Mwanamitindo Ammika Harris aliepewa jina la Aeko Catori Brown.Chris Brown ametumia kurasa zake za mitandao ya kijamii leo kwa kuposti picha mbalimbali za mtoto wake Aeko’ ni mtoto wa pili kwa Chris Brown akifatana na binti yake Royalty Brown mwenye umri wa miaka mitano
4
WAZIRI wa Michezo wa Kenya, Amina Mohamed ana uhakika jiji la Nairobi litakuwa tayari kwa ajili ya kuandaa mashindano yajayo ya Riadha ya Dunia kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 20 kwenye Uwanja wa Kasarani.Pia imeelezwa kuwa Naiobi imekwenda mbele zaidi kwani imeomba kuandaa mashidano makubwa zaidi ya Riadha ya Dunia ya mwaka 2025. Wakati mashindano hayo makubwa kabisa ya riadha yakifanyika kwa kupokezana miongoni mwa mabara, asili, Afrika itarejea kuanzaa mashindano ya mwaka 2025 huku Nigeria ikiwa nayo pia imeonesha nia ya kutaka kuomba uenyeji wa mashindano hayo, ambayo mwaka huu yalifanyika Doha, Qatar. Hadi sasa haijajulikana jiji gani la Afrika lina nia ya kuandaa mashindano hayo.Ikiongoza kwa mafanikio huko nyuma baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya Riadha ya Dunia chini ya umri wa miaka 18 Kasarani mwala 2017, Nairobi ilipata kirahisi uenyeji wa kuandaa mashindano ya Dunia ya mwakani kwa chini ya miaka 20, yatahayofanyika kuanzia Julai 7 hadi 12.Lakini maandalizi ya taratibu limekuwa tatizo kwa Kenya, kama vile kuahirisha uwekaji sakafu kwenye uwanja wa mazoezi katika Chuo Kikuu cha Kenyatta (mbako wanariadha watakuwa wakikaa), na mwendo wa kusuasua kwa mambo mengine kunatishia nafasi ya Kenya kupata fursa ya kuandaa mashindano mengine makubwa.Hata hivyo, kujiamini kwa Amina juzi kunaondoa wasiwasi wowote, ambapo aliwaambia waandishi wa habari baada ya kutolewa tuzo za wanariadha bora wa Dunia hapa kuwa, mambo yako vizuri na Nairobi iko tayari kwa ajii ya mashindano hayo.Akiongozana na Katibu Mkuu Kirimi Kaberia, Rais wa Riadha Kenya, Jack Tuwei na wajumbe wa kamati ya Maandalizi ya Nairobi 2020, ikiongozwa na Mtendaji Mkuu, Myke Rabar, Amina alisema mambo yanaenda vizuri na kila kitu kitamalizika kwa wakati.Karibu kiasi Sh bilioni 1.4 zimetengwa kwa ajili ya mashindano hayo mwakani. Kwa hatua nzuri, Amina na Kaberia waliungana na Rais Riadha wa Dunia (zamani IAAF), Sebastian Coe kuzindua tovuti mpya ya mashindano hayo: www. worldathleticsu20. com/ nairobi2020.“Mipango yetu sasa ni kuomba kuandaa mashindano ya Dunia ya Riadha ya mwaka 2025 na tumeshapeleka barua katika Shirikisho la Riadha la Dunia na tunatarajia kupata jibu zuri. “Kenya sio tu iko tayari kuandaa riadha, lakini pia shehere kubwa”.
1
NA THERESIA GASPER, DAR ES SALAAM MWIGIZAJI wa filamu za Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’, amesema yeye kama kioo cha jamii hana budi kutumia muda wake kuelimisha wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao. Akizungumza na MTANZANIA jana, Dude alisema amekuwa akiwahamasisha wanafunzi, kupitia zawadi kama madaftari, vitabu, viatu hata sare za shule. “Kama unavyojua mtoto unapompatia zawadi na kumuahidi mambo mazuri, lazima atajitahidi, nitaendelea kutembelea shule mbalimbali kuhamasisha masomo,” alisema Dude. Dude alisema ana imani malengo aliyoweka yatawasaidia wanafunzi wengi ambao wamekuwa wagumu kupenda masomo.
4
TIMU ya Taifa ya Soka ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kushuka dimbani leo ugenini kuikabili Sudan katika mchezo wa kufuzu fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (Chan 2020).Mchezo huo utachezwa ugenini kuanzia saa 1:00 usiku, huku Stars ikiwa imetoka kupoteza mchezo wa kwanza bao 1-0 uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Ni mchezo muhimu kwa Taifa Stars kuhakikisha inapata matokeo ya ushindi kuanzia mabao 2-0 na kuendelea ili kupata nafasi ya kufuzu kwa mara ya kwanza baada ya miaka 10 Tanzania ilipofuzu kwa mara ya kwanza mashindano hayo yalipofanyikia Ivort Coast.Timu hizo zina historia mara ya kwanza katika michuano kama hiyo ya kufuzu zilikutana Dar es Salaam na Stars kushinda 3-1 kisha ziliporudiana Stars ikashinda tena 2-1 ugenini. Lolote linawezekana kama tu Stars itakuwa imejipanga vizuri dhidi ya mpinzani wake huyo. Beki wa Stars, Erasto Nyoni alisema maandalizi yako vizuri na anaamini watapata matokeo mazuri.“Sisi tuko salama hakuna mtu mwenye majeruhi na tumejiandaa vizuri, kikubwa ni Watanzania kutuombea heri tupate matokeo mazuri,”alisema.Stars kabla ya kuvaana na Sudan ilicheza mchezo mmoja wa kirafiki dhidi ya Rwanda ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo huo ambapo licha ya kutoka suluhu Kaimu Kocha Mkuu Ettiene Ndayiragije aliwatumia wachezaji wengi wa ndani kuwapa mazoezi.Katika michezo iliyopita safu ya ushambuliaji ilionekana kuwa butu kwa kutengeneza nafasi nyingi na kushindwa kufunga, lakini ameongezwa mshambuliaji mpya Ditram Nchimbi hivyo, huenda mambo yakawa mazuri. Sudan imekuwa ikicheza mchezo wa kujilinda na mashambulizi ya kushtukiza na ilifanya hivyo katika mchezo wa kwanza labda watacheza kwa kufunguka zaidi leo. Timu hizi zimekutana baada ya Stars awali kuwatoa Kenya.
1
NEW YORK, MAREKANI MCHEKESHAJI maarufu nchini Marekani, Kevin Hart, ameomba tena radhi kwa kauli yake ya kuwazungumzia vibaya watu wanaoshiriki tendo la jinsi moja. Msanii huyo ambaye aliteuliwa kuwa mshereheshaji kwenye tuzo za Oscar ambazo zinatarajiwa kufanyika Februari 25 mwaka huu, lakini kutokana na kauli za kuwazungumzia mashoga akaondolewa nafasi hiyo. “Nitaendelea kuyasema haya kwa ajili ya kuacha kila kitu kikienda sawa sawa, nataka kuweka wazi kuwa, sina tatizo na watu wanaoshiriki matendo ya jinsia moja, nataka kila mmoja ajisikie huru na furaha. “Nadhani maneno yangu hayakuwa na maana mbaya, lakini nilieleweka vibaya na ndio maana natumia muda mwingi kuweka sawa kwa kuomba radhi kwa kila mmoja ambaye aliguswa na maneno hayo,” alisema Kevin Hart.
3
SEKTA ya Afya inatarajiwa kuwa na mabadiliko makubwa ya kiteknolojia nchini na katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kutoa huduma kwa njia ya teknolojia ya habari na mawasiliano (Tehama) huku ikiikinga jamii na maradhi mbalimbali.Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari Kambi alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia kongamano na maonesho ya awamu ya saba ya afya, sayansi na biashara katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashakiri (EAC).Kongamano hilo ambalo ni la saba linaloandaliwa na Kamisheni ya Afya na Utafiti ya Afrika Mashariki linajumuisha nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, likitarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza nchini kuanzia Machi 27 hadi 29, mwaka huu na kufunguliwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.Akizungumzia hilo, Profesa Kambi alisema teknolojia kwa ajili ya kubadili mifumo ya afya ili kutimiza Malengo Endelevu ya Maendeleo ya Umoja Mataifa. “Tanzania imepokea jukumu la kuandaa kongamano hilo ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili, ikijikita kuonesha maisha ya kesho ya afya kujikita zaidi katika Tehama,” alisema Profesa Kambi.
1
BENKI ya NBC imesema itaendelea kushirikiana kikamilifu na Serikali ya Awamu ya Tano katika azma ya kukuza uchumi wa wananchi na maendeleo kwa ujumla.Akizungumza wakati wa kongamano la wadau juu ya upatikaji wa fedha na usimamizi wa hatari zinazoweza kujitokeza katika miamala ya kifedha lililoandaliwa kwa wadau jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Idara ya Hazina na Masoko wa NBC, Peter Nalitolela alisema NBC imejizatiti kuhakikisha nchi inafaidika na kiasi cha pesa inachotumia katika miradi mikubwa ya maendeleo inayofanyika.Kongamano hilo lililohudhuriwa na wadau kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Shirika la Umeme (Tanesco), Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) na Wizara ya Fedha na Mipango.Alisema lengo lake kuu ni kuangalia vyanzo mbalimbali vya fedha vinavyopatikana katika miradi mbalimbali mikubwa inayofanywa na serikali pamoja na kuangalia usimamizi wa hatari katika miamala ya kifedha inayoweza kutokea katika miradi hiyo.“Kama mjuavyo miradi mbalimbali mikubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kama vile mradi wa Reli ya Kisasa (SGR), mradi wa umeme wa Mto Rufiji wa Stiegler’s Gorge, ujenzi wa barabara na madaraja.“Baadhi ya miradi hufanywa kwa mikopo kutoka pande tofauti, hivyo tulitaka kuonesha uwezo wetu kama NBC katika kusaidia upatikanaji wa fedha na pia linapokuja suala la uzimamizi wa hatari za kifedha katika miamala hiyo.“Kilicho kikubwa ni kwa NBC kuangalia uwezo wetu kwa njia tofauti tofauti ikiwemo katika kukopesha, lakini pia kuona serikali haipati hasara kutokana na masuala ya riba, fedha za kigeni na kushuka kwa thamani ya shilingi.“Hivyo NBC tumejiandaa kushirikiana na serikali kikamilifu katika kutimiza azma yake, kwa uwezo wetu tunaweza kushirikiana zaidi na zaidi,” aliongeza Nalitolela.Pamoja na hayo Mkurugenzi huyo alisema kama inavyofahamika kuwa NBC inamilikiwa kwa pamoja na Serikali ya Tanzania, Benki ya Absa ya Afrika Kusini na Benki ya Dunia, hiyo huiweka NBC katika nafasi nzuri ya kusaidia juhudi za serikali.Katika kongamano hilo pia NBC Ilileta wataalam kutoka benki mama ya Absa ili kuweza kuonesha uzoefu wao walioupata kupitia miamala waliyofanya na serikali za nchi mbalimbali barani Afrika.
0
Na Mwandishi Wetu -DAR ES SALAAM RAIS Dk. John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Ichiro Aisawa Ikulu, Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo, waziri huyo wa Japan alimpongeza Rais Magufuli kwa uongozi mzuri, kupambana na rushwa na msukumo mkubwa anaoutoa katika maendeleo, juhudi ambazo zinasaidia kuimarisha uchumi na kuboresha huduma za kijamii. Waziri Ichiro alitembelea baadhi ya miradi inayojengwa hapa nchini na kampuni za Japan ukiwamo mradi wa ujenzi wa barabara za juu (Flyover) wa Tazara na mradi wa kuzalishaji umeme kwa gesi wa Kinyerezi II na alimuhakikishia Rais Magufuli kuwa kampuni hizo zitafanya kazi nzuri na zitakamilisha kazi kama ilivyopangwa. Alisema baada ya kuona changamoto ya foleni katika Jiji la Dar es Salaam, amebaini kuwa nchi yake bado inahitaji kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha miundombinu ya jiji hilo na aliahidi kufikisha ujumbe huo kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe. Kwa upande wake, Rais Magufuli alimshukuru Waziri Ichiro kwa kuja nchini na amemuhakikishia kuwa Tanzania inatambua mchango mkubwa ambao Japan inautoa katika maendeleo. “Naomba unifikishie ujumbe kwa Waziri Mkuu Shinzo Abe kuwa Tanzania inamshukuru kwa ushirikiano huu mkubwa, tunamkaribisha sana Tanzania na kwa kuwa Serikali yetu imehamia Dodoma, tutafurahi sana kama Japan itaweka alama ya urafiki wetu kwa kutujengea barabara za Dodoma mjini, iwe ni flyover au kilometa 20 za barabara, sawa tu,” alisema Rais Magufuli.
1
      NAPLES, ITALIA BAADA ya klabu ya Napoli kushinda mabao 3-2 dhidi ya AC Milan, kocha wa timu hiyo, Carlo Ancelotti, amefunguka na kusema kuifunga klabu hiyo kumemfanya akumbuke mbali sana Katika mchezo huo Napoli ilianza kwa kuwa nyuma kwa mabao 2-0 hadi dakika ya 49 kipindi cha pili yakiwekwa wavuni na Davide Calabria na Giacomo Bonaventura, lakini Napoli waliweza kusawazisha kupitia kwa nyota wake, Piotr Zielinski, aliyefunga mabao mawili na lingine likifungwa na Dries Mertens. Ushindi huo umemfanya Ancelotti ambaye alikuwa kocha wa timu hiyo tangu 2001 hadi 2009, kuwa na hisia kali na kukumbuka wakati anaifundisha. “Ni ushindi umbao umenifanya niikumbuke AC Milan wakati ninaifundisha, niliikumbuka klabu hiyo pamoja na wachezaji wake kama vile Gattuso ambaye kwa sasa ni kocha wao. “Bado AC Milan ni timu bora nchini Italia, lakini katika mchezo huo hawakuwa tishio sana japokuwa waliweza kupata mabao mawili ambayo yalikuwa yanafanana,” alisema Ancelotti. Kocha huyo alisaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo tangu Mei 23 mwaka huu kuchukua nafasi ya Maurizio Sarri. Mchezo wake wa kwanza kwenye ligi aliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Lazio, Agosti 19.
2
SAO PAULO, BRAZIL BAADA ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu nchini England, Chelsea, kufikia makubaliano na klabu ya Atletico Madrid ya nchini Hispania juu ya kuwauzia mchezaji wao wa zamani, Diego Costa, mchezaji huyo amefunguka na kusema hana tatizo na kocha wake, Antonio Conte. Kocha huyo baada ya kuchukua ubingwa wa ligi msimu uliopita na wachezaji wakiwa kwenye mapumziko nchini kwao, alimtumia ujumbe wa maandishi mchezaji huyo ambaye alikuwa anaongoza kwa mabao ndani ya Chelsea na kumwambia kwamba hayupo kwenye mipango yake katika msimu wa 2017/18. Kutokana na hali hiyo, Costa hakuweza kurudi kikosini japokuwa kuna wakati uongozi ulikuwa unamhitaji, ila aliweka wazi kuwa hana mpango wa kurudi na mikakati yake ni kuhakikisha anajiunga na klabu yake ya zamani na Atletico Madrid. Costa alijiunga na Chelsea mwaka 2014 akitokea Atletico Madrid kwa uhamisho wa pauni milioni 32, lakini kwa sasa anarudi Atletico Madrid baada ya kukubaliana kwa kitita cha pauni milioni 60. Tayari mchezaji huyo amewasili nchini Hispania kwa ajili ya kumalizana na Atletico ndani ya saa 48 kuanzia sasa baada ya kukamilisha vipimo vyake. “Ninaamini kila kitu kipo sawa ndani ya klabu ya Chelsea, sina tatizo na mchezaji yeyote ndani ya klabu hiyo wala kocha Antonio Conte ambaye alinitumia ujumbe wa kwamba hanitaki kwenye kikosi chake. “Hata kama kuna mtu ambaye nilikwaruzana naye, lakini nadhani kila kitu kilikuwa sawa baada ya muda, hivyo ninaondoka kwa amani bila tatizo na mtu yeyote,” alisema Costa. Costa mwenye umri wa miaka 28, anatarajia kumalizana na Atletico Madrid mapema wiki ijayo, lakini hataweza kucheza hadi Januari kutokana na klabu hiyo kufungiwa kusajili wachezaji kwa mwaka mmoja ambapo adhabu yake itamalizika Januari mwakani. Mshambuliaji huyo ataendelea kuchukua kiasi cha pauni 150,000 kwa wiki, ambazo ni zaidi ya milioni 452, kiasi ambacho kinalingana na kile alichokuwa anachukua katika klabu ya Chelsea msimu uliopita. Akiwa katika klabu ya Chelsea, alifanikiwa kupachika jumla ya mabao 59 kwa michezo 120 aliyocheza na kutwaa taji la Ligi Kuu England mara mbili na Kombe la Ligi mara moja.
2
POLISI jijini Mwanza imemkamata askari magereza Kibemba Warioba (27) mwenye namba za usajili B.9205 WDR, akiwa na simu tano za aina tofauti na mitandao tofauti akijihusisha na makosa ya kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi saa nne na nusu asubuhi, ambapo polisi wa mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi la Mkoa wa Kagera walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa anafanya kazi wilayani Biharamulo mkoani Kagera na tayari amesimamishwa kazi kwa hatua zaidi za kisheria.Kamanda Muliro alisema polisi walimbaini mtuhumiwa huyo akitumia njia ya mitandao hiyo ya simu ambapo alianzisha Saccos ‘Bandia,’ iliyojulikana kwa jina la Info Tell CCM, akilenga kuwatapeli wanachama wa CCM na wengine katika mikoa ya Mara na Kagera.Alitoa onyo kwa wananchi wenye tabia ya kufanya vitendo hivyo vya uhalifu waache mara moja kwa kuwa ni kinyume cha sheria.Katika hatua nyingine, jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watano kwa tuhuma za makosa ya unyang’anyi yaliyotokea Aprili 16, mwaka huu, majira ya saa saba na robo usiku.Alisema watuhumiwa hao kwa kutumia silaha (mapanga) wilayani Ukerewe katika eneo la Kisiwa cha Ghana na walipora injini Out boat HP 99, No X06-2369 yenye thamani ya Sh milioni 2.2, kokoro moja la dagaa aina ya Japan yenye thamani ya Sh milioni 2.15, tangi moja la mafuta lenye thamani ya Sh 400,000, fuel line moja ya Sh 80,000 na simu moja aina ya Tecno.Alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya jitihada za askari wa cyber crime na intelejensia kwa kushirikiana na wananchi kufanya ufuatiliaji na kufanikiwa kuwakamata.Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Rerdinand Tungaraza, Andrew Masumbuko, Sabato Msita, Laurent Julius na Sherida Paulo wote wakiwa ni wakazi wa Ukerewe.Katika tukio lingine, Kamanda Muliro alisema jeshi la polisi linawashikilia watuhumiwa wengine wawili ambao ni wavuvi kwa tuhuma za kufanya mauaji ya kinyama ambapo Mei 18, mwaka huu, majira ya saa tano usiku katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe waliwakamata na kuwafunga kamba wavuvi wawili na kuwatumbukiza majini( ziwani) kwa lengo la kuwapotezea maisha.Aliwataja waliokamatwa katika tukio hilo kuwa ni Joseph Charles (35) maarufu mashine na Juma Lisinge (39) maarufu Masonga wote wakiwa ni wakazi wa wilayani Ukerewe.Aidha, katika tukio jingine Kamanda Muliro alisema polisi imewakamata watuhumiwa watatu katika manispaa ya Ilemela kwa kosa la kukutwa na dawa ya kulevya aina ya mirungi yenye uzito wa kilogramu 58.1 yaliyokuwa yamefungwa kwenye gazeti na kuzungushiwa majani mabichi ya mgomba, ikiwa ni mbinu nyingine mpya inayotumiwa na wahalifu wanaojihusisha na dawa za kulevya ili kukwepa kutiwa nguvuni.Alisema tukio hilo lilitokea Mei 20, mwaka huu majira saa 11 alfajiri Nyamanoro C katika Kata ya Nyamanoro, ambapo aliwataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Masawe Moshi (23), Maginga Zacharia (24) na Amen Amaniel(27) wote wakiwa ni wakazi wa Nyamanoro C.Aidha, kamanda huyo alisema jeshi hilo pia limekamata na kuwashikilia watuhumiwa 14 kwenye misako iliyofanyika kuanzia Mei 14-18, mwaka huu, katikati ya jiji la Mwanza ambapo walikamatwa kwa makosa ya uvunjaji, unyang’anyi na kukutwa na TV flat screen 6, kompyuta mpakato saba, simu 14 aina mbalimbali, redio (sabufa) mbili, king’amuzi kimoja cha StarTime, rimoti moja na chaja nne za kompyuta mpakato(laptop) vyote hivyo wakiwa wamevipata kwa njia ya uhalifu.
1
WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema kuanzia sasa umeme vijijini utaunganishwa kwa Sh 27,000 bila kujali kama unasambazwa na Shirika la UmemeTanzania (Tanesco) au ni wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini (REA).Aidha amesema uamuzi wa kuigawa Tanesco hauna faida yoyote zaidi ya kuiweka nchi katika hatari. Aliyasema hayo wakati wa kujibu hoja zilizoibuliwa na wabunge waliochangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2019/2020 ambayo ilipitishwa juzi usiku.Kuhusu hoja ya gharama za kuunganisha umeme, Dk Kalemani alisema kuanzia mwezi huu, serikali imetoa waraka wa kutaka gharama za kuunganisha umeme kuwa Sh 27,000 kwa umeme unaopelekwa na REA, Tanesco au taasisi iliyopewa kazi na serikali. “Kuanzia Mei 1, mwaka huu, waraka umetolewa kuwa gharama za kuunganisha umeme maeneo yote vijijini iwe unapelekwa na REA, unapelekwa na Tanesco au yeyote aliyepewa kazi na serikali ni shilingi 27,000 tu.Hivyo niwatake Mameneja wa Tanesco wa Kanda, mikoa, wilaya kuhakikisha wanalisimamia hilo.” Dk Kalemani aliongeza: “ Kumekuwa na tabia ya halmashauri kulalamika kutofikishwa umeme kwenye taasisi za umma wakati hawajalipia, hivyo niwaagize Tanesco na wakandarasi kupeleka umeme kwenye taasisi za umma bila kujali umbali endapo tu malipo yamefanyika.”Akizungumzia hoja ya Tanesco kugawanywa, Waziri Kalemani alisema badala ya wabunge kujadili wazo la kuigawa Tanesco ni vyema wakafikiria namna bora ya kuliimarisha shirika hilo ili liweze kuwahudumia wananchi kwa tija. Alisema pia kuwa endapo itaamuliwa kuwa kazi ya kutoa huduma ya umeme ipewe kampuni binafsi kuna hatari ya kampuni hiyo kuamua kuzima umeme nchi nzima jambo ambalo litakuwa ni hatari kwa nchi. “Umeme ni usalama, umeme ni uchumi, kabla ya kuligawa shirika hili lazima tuwe makini.Tukisema uzalishaji ufanywe na mtu binafsi na amiliki mitambo ina maana anaweza kuamua kuzima umeme nchi nzima na matokeo yake nchi inaweza kuingia gizani. “Katika kusambaza umeme tukiamua kulipa shirika binafsi kupeleka umeme hadi vijijini, watapenda kupata faida kubwa na uwezo wa watanzania ni mdogo watashindwa kumudu.Hivyo tufikirie namna bora ya kuimarisha shirika badala ya kuligawa vipande vipande.” Alisema Tanesco ilikuwa ikijiendesha kwa hasara kutokana na kuingia mikataba na kuwa na mitambo ya kukodi ya kutumia mafuta mazito ambayo ilikuwa ikiliumiza shirika hilo kutokana na gharama za uendeshaji kufikia hadi Sh bilioni 635 kwa kituo kimoja. “Kuna vituo vya kuzalisha umeme vilivyokuwa vikitumia mafuta jambo ambalo lilikuwa likiongeza mzigo kwa Tanesco.Mfano Kituo cha Ludewa kilikuwa kinatumia mafuta ya shilingi bilioni 703, lakini makusanyo yanayotokana na uuzaji wa umeme yalikuwa ni shilingi bilioni 331, hii ilikuwa ni hasara,” alisema. Alisema ili kuondokana na hilo serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha maeneo yote yanaunganishwa na Gridi ya Taifa ili kuondokana na uzalishaji wa umeme wa mafuta jambo ambalo litaipunguzia serikali mzigo.
1
Wafanyabiashara mbali mbali nchini wametakiwa kuacha kuweka fedha majumbani badala yake waweke fedha hizo katika kadi za kibenki ili kuwa na usalama wa fedha zao. Meneja Mauzo wa Kampuni ya Data Vision, Maclen Gmwaijonga, amesema kuweka fedha katika kadi ni njia bora zaidi na salama kuliko kuweka fedha ndani. “Kumekuwa na wizi mkubwa wa fedha na hii yote inatokana na usalama wa uwekaji wa fedha,” alisema Gmwaijonga. Alisema tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo mwaka 1998 mpaka sasa zaidi ya benki 35 na taasisi za kifedha zimejiunga na Data Vision kibishara kwa zaidi ya miaka 10 sasa. Alisema licha Tanzania kukua kiteknolojia bado ipo chini katika kwa matumizi ya kadi za kibenki katika suala zima la ufanyaji wa biashara hii inatokana na kukosa kwa uelewa wa huduma hizo, hivyo eimu zaidi inahitajika.        
1
Aveline Kitomary, Dar es salaam Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu leo amethibitisha kifo cha kwanza cha mgonjwa wa virusi vya corona ambaye ni mwanamume aliyekuwa akitibiwa katika kituo cha matitabu ya wagonjwa wa corona kilichopo nje ya hospitali ya Mloganzila. Waziri Ummy amesema mgonjwa aliyepoteza maisha ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 49 aliyekuwa akipatiwa matibabu katika kituo hicho. “Nasikitika kutangaza kifo cha kwanza cha mgonjwa wa Covid -19 hapa nchini kilichotokea alfajiri ya leo tarehe Machi 31, wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika kituo cha Mloganzila Dar es salaam. “Marehemu ni Mtanzania mwenye umri wa miaka 49 ambaye pia alikuwa akisumbuliwa na maradhi mengine, tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na tunatoa pole kwa ndugu hasa wa marehemu,” amesema Waziri Ummy. Hadi sasa jumla ya wagonjwa waliopata maambukizi ya Covid-19 nchini ni 19, aliyepona ni mmoja na aliyefariki dunia ni mmoja.
1
KIUNGO wa Simba, Gerson Fraga, amethibitisha kuwa yeye ni Mbrazil halisi, baada ya jana kuweka nyavuni mabao yote mawili katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi Coastal Union uliochezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa ushindi wa bao 2-0.Katika mchezo huo uliochezwa muda mchache baada ya mvua kunyesha Fraga alifunga bao la kwanza dakika ya saba, kwa mpira wa kichwa akiwa ndani ya eneo la goli akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na kiungo, Clatous Chama ambaye jana alikuwa mwiba kwa wapinzani wao.Fraga tena aliwainua mashabiki wa Simba dakika ya 78, baada ya kufunga bao la pili kwa mpira uliotemwa na kipa wa Coastal Union, Soud Dondola, shuti lililopigwa na kiungo Hassan Dilunga aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ibrahim Ajib.Ufundi na utulivu kwa wachezaji ulikosekana katika mchezo huo, baada ya uwanja kuwa na maji maji, na kufanya timu zote mbili kucheza mipira ya juu hasa katika kipindi cha kwanza.Kwa matokeo hayo Simba inaendelea kuongoza ligi ikiwa na pointi 47, katika michezo 18 kwa pointi 11 zaidi ya Azam FC wanaofuatia katika nafasi ya pili wakiwa na pointi 36 katika mechi 17 na Coastal Union inashika nafasi ya tano ikiwa na pointi 30, baada ya kucheza michezo 18.Mechi nyingine za ligi kuu leo, JKT Tanzania na Polisi Tanzania ilisitishwa dakika ya 53 kufuatia Uwanja wa Uhuru kujaa maji na mpaka mchezo unaahirishwa walikuwa hawajafungana na mchezo kati ya Tanzania Prisons na KMC haukufanyika kabisa sababu ya mvua kubwa.Kagera Sugar iliifunga Singida United kwa 3-0 katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba mabao yoye yakifungwa na Kelvin Sabato na katika Uwanja wa Majaliwa Namungo FC iliibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Mbao FC, mabao mawili yakifungwa na Reliants Lusajo na Hashim Manyanya na Ndanda ikicheza nyumbani kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona iliifunga Alliance FC kwa bao 1-0 lililofungwa na Vitalis Mayanga, Biashara United iliifunga Mwadui FC kwa mabao 2-1 yakifungwa na Mpapi Nasibu na Ramadhan Chombo ‘Redondo’ lile la Mbao lilifungwa na Mussa Chamgenga na Ruvu Shooting ikaichapa Lipuli FC 3-1 na mabao yake yakifungwa na Graham Naftari, Rajab Zahir na Sadat Mohamed huku bao la Lipuli likifungwa na Daruweshi Saliboko.
2
WAKATI binti wa miaka 17 aliyekuwa akifanya kazi za ndani jijini Dar es Salaam akieleza ukatili aliokuwa akifanyiwa na bosi wake, ikiwemo kuwekewa mwiko sehemu za siri hali inayosababisha asione siku zake (hedhi) kwa mwaka mmoja sasa, taasisi mbalimbali zimeelezwa kushangazwa na ukatili wa aina hiyo na kutaka hatua kali zichukuliwe.Mkuu wa Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Vumilia Nyamoga alilaani ukatili huo uliofanywa na mwajiri wa mtoto huyo, Happines Mathew ambaye ni muuguzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na kutaka vyombo vya dola kuchukua hatua katika suala hilo.DC Nyamoga alisema Happiness na mumewe, Dk Tito Lunobo, ni wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na wanawajibika katika suala hilo la ukatili dhidi ya binti huyo. “Ninalaani ukatili wa kijinsia uliofanywa kwa binti huyo ambaye nimemuona kwa macho yangu, ni tukio la kusikitisha sana lazima tulisemee hili tusikae kimya.Unyama aliofanyiwa huyu binti unashangaza na hauingii akilini kama unaweza kufanywa na watumishi wa afya, unawezaje kumwadhibu mtoto wa mwenzio kwa kumuingiza mwiko kama fundisho la kumuonesha uchungu wa kuzaa kwa kosa la kumdondosha mtoto?” Alihoji Nyamoga.“Navitaka vyombo vya dola vichukue hatua kali kwa wote pamoja na watendaji wote ambao kwa njia moja au nyingine wamekuwa wakipotosha ukweli kwa kumkandamiza binti ambaye alipata mateso kwa muda wa miaka mitatu mfululizo.” Pia mkuu huyo wa wilaya alisema Ofisi ya Ustawi wa Jamii na Polisi (Chamwino na Temeke) wanapaswa kufuatilia na kuangalia upya jalada la kesi ya binti huyo, ilikuwaje lilifungwa na mambo yakaishia nyumbani wakati binti huyo amefanyiwa ukatili ambao ni jinai. Alisema ofisi yake itahakikisha inasimamia haki ya binti huyo ilipokwama na kuhakikisha kuwa binti huyo anafanyiwa vipimo na kupata tiba sahihi.DC Nyamoga alisema anamshukuru hata msamaria mwema aliyetoa habari za kikao cha ukoo kutoa fidia ya Sh milioni 1.3 na huo ni ushahidi kuwa kuna uovu ulikuwa unafichwa.Kauli ya HappinessAkizungumza kwa njia ya simu, Happiness alisema suala liko Polisi, hivyo hawezi kusema kitu na kama kuna jambo lolote waulizwe Polisi.Diwani azungumzaDiwani wa Kata ya Manchali, Mary Mazengo alisema alikwenda kumuona binti huyo na alichokiona ni ukatili ambao unaumiza moyo. “Binti ana majeraha ya kupigwa na mwiko kichwani, nimehesabu ana majeraha 19 na sehemu zake za siri zimeharibika vibaya,” alisema Mazengo na kuongeza kuwa pia binti huyo ana makovu ya kuchomwa na pasi mgongoni, macho na midomo yake, na matatizo ya kiafya.Alisema mara ya kwanza binti huyo alipelekwa hospitali na mama wa mtuhumiwa, lakini kinachoonekana madaktari wa Dar es Salaam na Dodoma wana mawasiliano na huyo binti alipimwa kutokana na maelekezo. Alisema wanataka kutafuta utaratibu ili binti atibiwe na madaktari watakaowachagua wao (halmashauri) na si madaktari wanaopata maelekezo ya familia kwani huyo binti hatapata matibabu kikamilifu.Binti mwenyewe anasemaje?Akisimulia mkasa huo, binti huyo alisema sasa analazimika kuvaa kofia muda wote ili kuficha makovu ya kichwani yaliyotokana kupigwa na mwiko kila mara.Katika mazungumzo hayo, binti huyu alidai pia macho yake yamekuwa mekundu kwa kile alichodai kusuguliwa macho mara kwa mara na mwajiri wake. Anasema kwa sasa ana uoni hafifu. Alisema alimaliza darasa la saba katika Shule ya Msingi Manchali mwaka 2016, hakufaulu ndipo alipochukuliwa na ndugu yake, mtoto wa mama yake mkubwa, Happiness Mathew au Happiness Job ambaye ni Muuguzi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili akafanye kazi za ndani. Alisema katika maisha yake alikuwa akikutana na vipigo vya mara kwa mara kwani mwajiri wake huyo hata akimkuta mtoto analia alikuwa anamwangushia kipigo.Alisema kuna siku mtoto alikuwa akicheza na akaanguka, dada huyo aliporudi akamsema hamuangalii mtoto kwa vile hajui uchungu wa kuzaa na atamfanyia kitu ili asikie uchungu kama huo. Ndipo alipompiga na kuchukua mwiko ambao aliuingiza sehemu za siri na tangu wakati huo ni zaidi ya mwaka sasa hajapata siku zake (hedhi) na amekuwa akipata maumivu anapoenda haja ndogo. Binti huyo anasema pia aliwahi kupewa adhabu ya kulala wima mpaka asubuhi. “Siku hiyo alikasirika akasema utalala ukiwa umesimama, muda wa kulala ulipofika akaniingiza chumbani kwake, akaniambia adhabu yako utasimama hadi asubuhi, basi yeye akalala kitandani mimi kwa hofu nikabaki nimesimama mpaka asubuhi,” alidai.Binti huyo alisema alikuwa akilipwa Sh 50,000 mshahara wa mwezi na fedha hizo alikuwa akitumiwa mama yake mzazi moja kwa moja. Akimbilia polisi “Kuna siku nikajiuliza nitateseka mpaka lini, pale nyumbani aliletwa mfanyakazi mwingine wa ndani, tukapanga tutoroke, lakini nikaamua kwenda hadi Kituo cha Polisi Chang’ombe nikatoa maelezo yangu na mhusika alikamatwa,” alisema. Alisema baada ya mwajiri wake kukamatwa aliwekwa rumande na yeye kutoa maelezo yake na kisha alikwenda kukaa nyumbani kwa mjumbe wa mtaa.Wakata tamaaAlisema isingekuwa rahisi kwao kuendelea na kesi jijini Dar es Salaam kwani hawakuwa na sehemu hata ya kulala. “Tuliamua kesi iishe tu hatuna mtu wa kutusaidia, isitoshe hatukuwa hata na pa kukaa kufuatilia kesi hiyo mpaka iishe, mama aliamua tu turudi nyumbani,” alisema. Alisema waliporudi Dodoma, ujumbe ulifika nyumbani kwao kuja kuomba msamaha. “Mama yake na Happiness alitumwa ili aje kumuombea mtoto wake msamaha ili mambo hayo yaishe na siku ya Jumanne iliyopita nilipelekwa hospitali kwa ajili ya kufanyiwa X-ray,” alisema.Hata hivyo, haelewi majibu ya vipimo hivyo kwani aliyempeleka alisema hakuonekana na tatizo wakati yeye anaumwa.Maumivu yapo wapi?Anasema hajatibiwa macho kwani hospitali waliyokwenda hakuna daktari wa macho na macho yamekuwa yakimsumbua na hata midomo yake imekuwa imevimba muda wote. Pia alisema amekuwa akipata maumivu ya kichwa kutokana na ukweli kuwa kuna wakati alikuwa akipigizwa ukutani mara kwa mara na maumivu ya shingo kutokana kukabwa mara kwa mara. Alisema anachohitaji sasa ni kusaidiwa ili apate matibabu kwani amekuwa na maumivu makali ya mwili na hajui atapata hedhi lini na hajui kilichovurugwa mwilini mwake hadi anakosa hedhi.“Sijui ule mwiko alioniingiza umeleta madhara gani katika mwili wangu naona nisaidiwe ili nifanyiwe vipimo,” alisema. Alisema alivunja ungo mwaka 2014 na alikuwa akipata hedhi kawaida, lakini baada ya kuingiziwa mwiko haoni kabisa hedhi.Mama mzazi asimuliaMama mzazi wa binti huyo, Rehema Richard alisema mwaka 2017, Happiness alikwenda kumuomba mtoto wake akamsaidie kazi za ndani na aliahidi atakaa naye vizuri. “Kumbe mtoto alikuwa akiteseka na alikuwa hataki nijue mtoto alikuwa akiteseka kwa kiwango hiki,” alisema na kuongeza alijua hayo alipoitwa katika shauri jijini Dar es Salaam.“Nilienda nikakuta mtoto kapigwa hata sura yake imebadilika, nikasema sina la kusema nipeni mwanangu nirudi naye nyumbani,” alieleza mama huyo. Alisema ingawa mama wa Happiness alimchukua binti huyo na kumpeleka hospitali, alipewa tu vidonge vya maumivu, “huyu anahitaji vipimo ili matatizo yake ya mwili yajulikane na yatibiwe.”Milioni 1.3/- kama fidiaMama wa binti huyu alisema baada ya kurudi na bintiye, kuliitishwa kikao cha ukoo iliamriwa suala hilo limalizwe kimila na familia ya Happiness iliagizwa kulipa fidia na yeye mwenyewe kukubali kutoa Sh milioni 1.3 kama fidia.“Januari 22, walitukabidhi hela hizo, nimeziweka tu,” alisema mama mzazi wa binti huyo. Nakala ya barua ya makabidhiano hayo ambayo gazeti hili inalo inaonesha fedha hizo zililipwa Januari 22, mwaka huu. Naye mama yake Happiness, Evelina Mchiwa ambaye pia ni mkazi wa Kijiji cha Manchali, alisema baada ya kupewa taarifa kuhusu kukamatwa kwa mwanawe alifika Dar es Salaam, na kumkuta akishikiliwa katika Kituo cha Polisi Chang’ombe. “Wakaandika jalada niliona suala hili tukalijadili nyumbani japo polisi walikuwa wakitaka suala hilo liende mahakamani,” alisema.Kwa upande wake kuhusu suala hilo la kuendesha kesi katika mahakama za Dar es Salaam, mama wa binti aliyefanyiwa ukatili alisema hakuwa na uwezo wa kuendesha shauri hilo akiwa Dar es Salaam, hakuwa na ndugu wala uwezo ndio maana aliamua kurudi nyumbani. Suala la binti huyo kufanyiwa ukatili liliibuliwa na msamaria mmoja ambaye alipiga simu kwa Ofisa Maendeleo wa Wilaya ya Chamwino, Sophia Swai aliyesema kwamba kuna binti ameletwa kutoka Dar es Salaam anaumwa baada ya kufanyiwa ukatili.Ilijulikana vipi?Sophia alisema kutokana na hamasa kwa wananchi kutoa taarifa juu ya matukio ya ukatili, suala hilo lilibuliwa na msamaria aliyempigia simu juu ya kuwapo kwa binti mwenye afya mbaya aliyefanyiwa ukatili jijini Dar es Salaam na kuamua kufuatilia tukio hilo kubaini ukweli wake. Swai alisema baada ya kupata taarifa hizo alikwenda kuonana na Mkuu wa Kituo cha Polisi Chamwino ambaye alifanya mawasiliano na OCD wa Chang’ombe, ambako ilibainika kuwa faili hilo limefungwa, jambo ambalo lilizua maswali kutokana na hali ya binti kuwa mbaya.Kamanda Temeke azungumzaAkizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Awadhi Haji alisema kadhia hiyo ya ukatili ipo katika Dawati la Jinsia na wanasubiri hati ya matibabu (PF3) ili kuifikisha mahakamani na haki itendeke.Alisema binti huyo ambaye anaonekana ana undugu na mtuhumiwa, alifika polisi Januari 4, mwaka huu kulalamikia ukatili anaofanyiwa. Kamanda Haji alisema baada ya kumsikiliza mlalamikaji, Polisi walishughulikia malalamiko hayo kwa kufanya upelelezi pamoja na kumkamata mtuhumiwa Happiness Job kwa mahojiano. Alisema baada ya kukamilika kwa upelelezi, shauri hilo halijaenda mahakamani kwa kuwa mlalamikaji ambaye ndiye shahidi wa kwanza katika shauri hilo, hajarejesha PF 3 kama inavyotakiwa.“Shauri hilo ni kama linakosa ushirikiano, mlalamikaji hajarejesha PF 3 ili twende mahakamani. Nimemwagiza Mkuu wa Upelelezi kuhakikisha kwamba wanalipeleka shauri hili mahakamani kwani suala kama hili halimalizwi kienyeji, kuna ukatili mkubwa hapa,” alisema Kamanda Haji. Kwa mujibu wake, katika mahojiano wakati wa upelelezi, familia hizo zilionekana kutaka suala hilo liishie kienyeji, wao wanataka mlalamikaji huyo kupata haki zake pamoja na waajiri wanaofanyia ukatili wafanyakazi wao kutambua serikali ina mkono mrefu katika kulinda wananchi wake. Alisema jamii inapaswa kukemea vitendo vya kikatili na kuviripoti mara moja Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe.
1
    Na MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM MMOJA wa wazazi ambao watoto wao wamefariki katika ajali ya gari iliyosababisha vifo vya wanafunzi 33 wa Shule ya Msingi Lucky Vincent, alikuwa miongoni mwa mashuhuda wa ajali hiyo pasipo kujua kama mtoto wake, Justine Alex, alikuwamo katika msafara wa gari hilo. Mzazi huyo, aliyetambulika kwa jina la Lemburis Saruni, inadaiwa kuwa  alishuhudia ajali hiyo akiwa kwenye gari la  nyuma, huku lile lililobeba wanafunzi  hao likiwa mbele. Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, ndugu wa karibu na Lemburis ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema baada ya kuona gari hilo limeanguka kwenye korongo alilazimika kushuka ili kwenda kuangalia bila kujua kama mtoto wake ni miongoni mwa waathirika wa ajali. “Hiyo ajali imeua ndugu zangu, akiwamo mtoto wa baba yangu mdogo, na yeye leo alikuwa anakwenda Ngorongoro, alifuatana na hilo basi la wanafunzi bila kujua na  kaliona likidondoka, akashuka akalifuata akakuta mwanawe ndio yupo ananing'inia mlangoni,” alisema ndugu huyo. Alisema baada ya kumuona akiwa katika hali hiyo, alilazimika kumwondoa na kumuweka pembeni, lakini kwa bahati mbaya alikufa akiwa amemshika mkononi. Alisema Justine alikuwa mtoto pekee wa Lemburis. Alisema mama wa Justine alifariki dunia mwaka juzi. Gazeti hili lilijaribu kumtafuta mzazi huyo kwa njia ya simu ya kiganjani ili aweze kuelezea tukio hilo, lakini hakupatikana hewani. Mbali na mtoto huyo, mtoa taarifa alibainisha kuwa ajali hiyo huenda ikawa imesababisha vifo vya ndugu zao wengine watano ambao walikuwapo katika msafara huo, ambao ni wanafunzi na walimu.
1
Na FESTO POLEA-DAR ES SALAAM ‘WANAKUJAAA hao!’ Msemo huu si mgeni masikioni mwa wafuatiliaji wa tamthilia za kikorea, kifilipino, kizungu, kichina na filamu mbalimbali ambazo zimewekwa vionjo vya lugha ya kiswahili. Maneno hayo hutumiwa zaidi na Ahmada Abdulrahman maarufu Dj Mark, G Mashine, Jogoo kutoka lebo ya Acheche Production. Licha ya biashara hiyo kupingwa na Serikali kwa kukiuka sheria za hakimiliki na kulalamikiwa kukiuka maadili ya Watanzania, lakini ni kimbilio kubwa la vijana katika kujipatia ajira zisizo rasmi. Miaka ya 80, Kapten Lufufu Mkandala (marehemu) ndiye aliyeingiza mfumo huo nchini baada ya kupata mafunzo nchi za Vietnum. Kazi hiyo iliwavutia wengi kwani miaka ya 90 vijana wengi akiwemo Dj Mark ambaye katika makala haya anaeleza mengi, naye alikuwa mmojawapo kama anavyoeleza katika mahojiano haya. MTANZANIA: Uliingiaje katika kazi hii? Dj Mark: Nilikuwa nikimfuatilia sana mzee Lufufu, nilipofikisha miaka 18 nikiwa naishi Tandika nilitamani sana kufanya kazi aliyokuwa akiifanya mzee Lufufu ya kuweka maneno katika filamu mbalimbali za nje. Hivyo mama yangu alivyoanza kuugua wakamuhamishia Zanzibar na baba yangu alihamia Arusha kwa shughuli zake, mimi nikabaki na kaka ambaye hata hivyo hakukuwa na uangalizi mzuri, nikaamua kuacha shule nikiwa kidato cha pili, nilipomweleza baba kwamba sitaki tena shule aliniuliza ninachotaka, nikamwambia nataka kazi anayofanya mzee Lufufu. MTANZANIA: Vipi baba yako alikuelewa? Dj Mark: Alielewa baada ya kumueleza mahitaji yangu, alirudi Dar es salaam akauza kiwanja chake Sh 400,000, akanunua TV ambayo nayo ilikuwa ikiuzwa Sh 400,000, aliongeza fedha nyingine Sh 180,000 akanunua deki akanikabidhi, aliniambia kwamba hayo ndiyo maisha yako uliyoyataka. Hapo nikashukuru ingawa maneno yale yaliniingia akilini nikaamua kwenda kuanza maisha Arusha, huko nikafungua kibanda cha kuonyesha filamu za nje huku nikijitahidi kufikiria mzee Lufufu jinsi anavyoingiza sauti katika filamu, bila ya kujua alivyokuwa akifanya, nikawa kila ikifika saa 12 jioni naweka CD ya filamu za kizungu kisha nakaa pembeni na TV nawasimulia kinachojiri katika filamu hiyo, wakapenda watu wengi zaidi wakawa wanakuja katika banda langu, lakini baadaye kuna mzee alikubali kazi yangu aliamua kunipa redio yake ya kizamani iliyokuwa na spika mbili, nikawa naongea kwenye mic sauti inasikika kwenye spika za redio. Kipindi hicho nilikuwa eneo la mgodi lakini baada ya kutokea ugomvi mkubwa kwa wachimba mgodi, wafanyabiashara wote tukafukuzwa huko, nikaamua kurudi Ungalimited nikafungua mabanda matatu ya kuonyesha video na duka moja la kawaida. MTANZANIA: Ulifanikiwaje kuingiza sauti moja kwa moja katika filamu. Dj Mark: Baadaye ulikuja utaalamu wa kurekodi kwa deki la mikanda VHS kwa VHS, nikaanza kurekodi kwa kutumia deki mbili, lakini sikuwa na soko la kuuzia filamu hizo, hivyo nikaja Dar ambapo niliona kazi za mtu mwingine anayefanya kazi kama yangu anaitwa Juma Kan filamu zake zilikuwa na picha ya Kava. Katika tafuta tafuta ya mteja, nikapelekwa kwa mhindi anaitwa Ajey akaniambia yeye anafanya kazi kama yangu lakini anatafsiri za kihindi ila aliniambia kwamba soko la filamu za kizungu lilishikwa na mzee Lufufu, nikajua nimekosa kazi lakini baadhi ya watu walimshauri mhindi huyo akachukua na kazi zangu kwa kuwa Lufufu alikuwa peke yake anaishi Bukoba na umri ulikuwa umekwenda na hakuweza kutoa filamu nyingi zaidi. MTANZANIA: Malipo yako ya mara ya kwanza yalikuwaje baada ya kupata soko? Dj Mark: Mwaka huo ulikuwa 2007, yule mhindi alianza kunilipa Sh 6500 kwa mkanda mmoja lakini baada ya muda mfupi wa kufanya kazi na yule mhindi nikaona anazidi kuvunja na kutanua duka lake, kumbe alikuwa anaingiza fedha nyingi sana kutokana na kazi yangu, nikakataa kuendelea na malipo yele akaniongezea ikawa Sh 8500, baadaye ikawa Sh 15,000 kwa mkanda mmoja. Nikawa kwa siku najitahidi naingiza maneno ya Kiswahili mikanda minne ili nipate fedha nyingi. Mwaka 2009, Steps wanaofanya kazi na Bongo Movie waliniita walitaka niingize sauti kwa kufuata sauti za wahusika kulingana na jinsia zao, tukashindwana lakini wakakubali niendelee na aina yangu ya kuingiza sauti kwa filamu zao walizonipa wakawa wananilipa kwa mkanda mmoja Sh 50,000 lakini baada ya miezi takribani sita, yule mhindi  wa awali alikamatwa na polisi hivyo Steps wakasitisha kuendelea na kazi hiyo. MTANZANIA: Baada ya kukamatwa huyo mnunuaji wa kazi zako, maisha yaliendeleaje? Dj Mark: Baada ya hali hiyo, ilinibidi niingie mwenyewe sokoni kwa kutumia namba za simu katika kila mkanda  nilioutoa, niliweka namba nikawa nawapelekea watu mtaani hadi nikazoeleka. Na sasa nafanyia kazi zangu Kariakoo kwa kuwa kodi ni kubwa hadi milioni moja inafika, hivyo tumeamua watu watatu tunaofanya kazi za aina moja tumechangishana tumekodisha lakini kila mtu anafanya shughuli yake. Tunajua kazi hii si rasmi kwetu lakini imesaidia ajira watu wengi kama mimi nina miaka 20, kuna ugumu mkubwa wa kupata hakimiliki za watu tunaotumia kazi zao mfano inawezekanaje kupata hakimiliki za kutumia kazi za Rambo, naanzia wapi kuzipata na gharama yake kama ataniambia milioni 100 nitawezaje kujilipa wakati katika CD moja napata faida 300. MTANZANIA: Sasa una ujumbe gani kwa Serikali kuhusu kazi yenu? Dj Mark: Mimi naiomba Serikali ijenge mazingira mazuri kwa kazi zote za sanaa ikiwemo yetu, watusaidie hakuna asiyetaka kulipa kodi lakini tutengenezewe mazingira mazuri, mfano mdogo waende kwenye vituo vyote vya daladala ama masoko nchini lazima kazi zetu zipo au waende Kariakoo kwenye maduka ya CD kuanzia asubuhi hadi jioni waangalie wanaonunua CD zile kwa ajili ya wao nao kwenda kuziuza wataona watu wa kila aina wazee, vijana na wanawake, hii inaonyesha ni kazi inayotoa ajira, inatakiwa iwekewe mazingira mazuri si kutukataza kuifanya. MTANZANIA:  Hivi mna chama cha kuwasaidia kufikisha malalamiko yenu kwa Serikali? Dj Mark: Chama kipo lakini tumejiunga na watu wa library ila huwa tunakutana kama kuna jambo kubwa la kugusa masilahi yetu linatokea ndipo tunakutana tunazungumza tofauti na hapo kila mtu anajijua mwenyewe. MTANZANIA: Mwaka 2016 mmeliteka sana soko la Bongo Movie kwanini? Dj Mark: Bongo Movie hawajajitambua hadi leo wanatafuta mchawi wakati wachawi ni wao wenyewe, wanatakiwa kumwangalia mlaji wao ni nani? Anapenda nini? Je, malalamiko yake yanafanyiwa kazi? Wao hawayafanyi kazi hayo ndiyo maana wanafeli. Sisi si washindani wa Bongo Movie kwa maana CD zetu ni chafu katika sauti, tunakata tunaweka sauti nyingi za Kiswahili wakati mwingine tunakosea kutafsiri lakini cha ajabu wananchi wanazipenda zaidi zetu kuliko filamu za Bongo Movie, lazima hapo kuna tatizo. Na tatizo kubwa ni kwamba wananchi wamewachoka waigizaji wale wale, mfano Ray Kigosi, JB na wengine uigizaji wao ni ule ule hadi leo na bado wanaendelea kutoa filamu zile zile zenye sehemu mbili hadi tatu na bei ni zaidi ya 3000, halafu kama wanaigiza kuhusu polisi kuanzia mavazi ni uongo hayana uhalisia wa nguo za polisi wa Tanzania, kituo cha polisi hatujawahi kuonyeshwa kituo cha polisi cha kweli wala gari la polisi la kweli, location zao hadi uigizaji wa ovyo unategemea watu waendelee kununua kazi mbovu. MTANZANIA: Nini wafanye Bongo Movie ili warudi katika ushawishi wao? Dj Mark: Wawekeze tu, tena haihitaji akili nyingi waige kwa Diamond, video yake ya dakika mbili na sekunde kadhaa ya ‘My Namber One’ ametumia zaidi ya milioni 50 kwa sasa ni msanii wa kimataifa, anapata shoo nyingi za fedha nyingi zaidi ya uwekezaji wake, inakuwaje Bongo movie wanawekeza milioni 10 kwa filamu za zaidi ya dakika 90 wahusika kibao, location za kuungaunga, hiyo filamu kweli ama utani ndiyo maana nasema hawajielewi. Wazungumze vizuri na Serikali kupitia waziri mwenye dhamana ya sanaa awasaidie wapate vifaa kama magari ya polisi, sare na vitu vingine ili waendane na uhalisia maana sanaa kwa sasa imekuwa kubwa mno hakuna wa kumdanganya, kila mtu anataka kitu bora lakini jingine wawekeze waache utani katika kazi.
4
Mchezaji huyo alitarajia kurejea jana nchini kwa ajili ya safari ya Ubelgiji kwenda kuanza maisha mapya katika soka la Ulaya.Samatta tayari amekwishasaini mkataba wa awali na Genk wa miaka minne na sasa anakwenda kukamilisha taratibu zilizobaki.Samatta na Genk wanataka kukimbizana na muda ili kuwahi kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la usajili.Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo alisema kuwa hatimaye Katumbi ameridhia Samatta aende klabu anayoipenda ili kuendeleza soka lake.Katumbi alikuwa anataka Samatta aende Nantes ya Ufaransa, ili kucheza soka huko, lakini mchezaji huyo hakupenda kwenda huko na alikuwa tayari kubaki Congo kumalizia mkataba wake unaomalizika Aprili.
2
Upendo Mosha- Same MAMA mzazi wa Mtanzania Rashid Mberesero, aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela nchini Kenya, baada ya kukutwa na hatia ya kufanya shambulio la kigaidi eneo la Garissa  na  kusababisha vifo vya wanafunzi 148, amevunja ukimya. Mberesero ambaye alihukumiwa kifungo cha maisha huku wenzake Hassan Edin na Mohamned Ali Abikar kila mmoja akihukumiwa miaka 41 gerezani, walipatikana na hatia ya kupanga shambulio hilo chini ya ushirikiano wa kundi la Al-Shabaab. Akizungumza na MTANZANIA, Fatma Ally ambaye ni mama mzazi wa Mberesero, alisema kutokana na hukumu iliyotolewa anamwachia Mungu. Hata hivyo, aliomba msaada wa mashirika mbalimbali na taasisi zinazojihusisha na masuala ya kisheria kumsaidia mwanawe kupunguziwa adhabu. “Tangu hukumu ya mwanangu kutolewa, hali yangu ya kiafya si nzuri, zaidi sana namwachia Mungu maana yeye ndiye hakimu wa kweli, lakini pia naomba kama kuna uwezekano wa kujitokeza taasisi au watu wanaojua masuala ya sheria, wamsaidie walau apunguziwe adhabu,” alisema. Aidha alisema tangu kesi hiyo ianze kusikilizwa kwa kipindi cha miaka minne, hakubahatika hata mara moja kuhudhuria mahakamani kutokana na hali ngumu ya maisha inayomkabili jambo ambalo lilimfanya kutojua kitu kinachoendelea. “Tangu kesi hii ianze ni miaka minne sasa na sijwahi kufika mahakamani kusikiliza, hata siku ya hukumu sikuweza kwenda kwa sababu sina uwezo wa kupata nauli ya kutoka huku kijijini hadi huko Kenya,” alisema. Mberesero aligundulika eneo la tukio akiwa si mwanafunzi wala mfanyakazi wa chuo hicho. Kulingana taarifa zilizoripotiwa, Mberesero aliyesoma Shule ya Bihawana mjini Dodoma, alidaiwa kutoroka shule baada ya kukatazwa kuvaa kofia. Kulingana na mwalimu mkuu wa shule hiyo wakati huo, Mberesero alijiunga mwaka 2015 baada ya kutoka Shule ya Bahi Kagwe. Cha kushangaza ni kwamba licha ya kutoweka shule, hakuna aliyefuatilia alikokwenda. Kwa takriban miezi minne wazazi wa kijana huyo walidhani mtoto wao yupo shule suala ambalo halikuwa la kweli. Hata hivyo, wazazi walishangaa kugundua mtoto wao alikuwa miongoni mwa waliopanga na kutekeleza shambulio la Garissa. Kwa takriban miezi minne, wazazi wa kijana huyo walidhani kwamba mtoto wao yupo shule suala ambalo halikuwa la kweli.
1
NEW YORK, MAREKANI BINGWA namba moja wa zamani wa mchezo wa tenisi duniani kwa upande wa wanawake, Venus Williams, ametupwa nje kwenye michuano ya wazi ya US dhidi ya mpinzani wake, Sloane Stephens. Venus alipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri kwenye michuano hiyo baada ya mdogo wake, Serena Williams, kushindwa kushiriki kutokana na mambo ya uzazi, hivyo waliamini Venus angeweza kuiwakilisha vizuri familia hiyo. Katika mchezo huo wa juzi, Venus alijikuta akichezea kichapo cha seti 6-1, 0-6 na 7-5, kwenye mchezo huo wa nusu fainali, wakati huo mpinzani wa Venus, Sloane akitokea majeruhi na kuweza kushinda mchezo huo. Sloane anashika nafasi ya 83 kwa ubora duniani upande wa wanawake, huku Venus akishika nafasi ya tisa, lakini alishindwa kuonesha uwezo wake huku wadau wa mchezo huo wakidai umri wa Venus unaanza kumtupa mkono akiwa na miaka 37 sasa, wakati huo Sloane akiwa na miaka 24. Sloane anatarajia kucheza fainali dhidi ya Mmarekani mwenzake, Madison Keys, mwenye umri wa miaka 22 akiwa anashika nafasi ya 16 kwa ubora duniani upande wa wanawake, fainali hiyo itapigwa kesho. Fainali hiyo itakuwa ya kwanza kwa nyota wawili wa nchini Marekani kukutana huku mara ya mwisho ikiwa mwaka 2002 ambapo ndugu kutoka familia moja, Serena Williams na dada yake Venus walipokutana, lakini Venus aliipoteza fainali hiyo. Safari hii kwenye michezo ya nusu fainali walikutana mastaa wote wanne kutoka nchini Marekani na ndio maana fainali wanakutana mabingwa kutoka nchi hiyo. Sloane amedai kukutana fainali na nyota mwenzake kutoka nchini Marekani ina maana kubwa sana kwa Taifa hilo katika upande wa tenisi. “Tuliweza kuingia wachezaji wanne hatua ya nusu fainali wote tukitokea hapa nchini Marekani, hii inamaanisha kwamba Marekani kwa sasa katika tenisi tunafanya vizuri. “Kwa upande wangu ninajivunia kuwa katika nafasi hii, lengo langu kubwa ni kutwaa ubingwa, haikuwa kazi rahisi kuweza kushinda mbele ya bingwa namba moja wa zamani Venus, lakini ninashukuru nimeweza kushinda mbele ya mbabe huyo. “Hakuna maneno mazuri ambayo ninaweza kuyasema yakaelezea hisia zangu jinsi zilivyo baada ya kufika fainali, ila nawashukuru mashabiki kwa sapoti yao,” alisema Sloane. Venus mara ya mwisho kufika fainali katika michuano hiyo ilikuwa mwaka 2002, hivyo hadi sasa ni miaka 15 hajafanikiwa kufika fainali. “Kila wakati nimekuwa nikipambana kuhakikisha ninatwaa taji, lakini hali imekuwa tofauti kutokana na ushindani ninaokutana nao, lakini ndivyo tenisi ilivyo,” alisema Venus.
2
AMINA OMARI Na OSCAR ASSENGA-TANGA RAIS Dk. John Magufuli, amesema kwamba serikali ina kila sababu ya kuendelea uhusiano mzuri kati yao na madhehabu ya dini nchini kwa sababu kazi wanayoifanya haina mbadala wake kwenye jamii. Hayo yalisema jana katika hotuba yake ilisomwa na niaba yake na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Ummy Mwalimu  ambapo alimwakilisha katika  Jubilee ya miaka 25 uaskofu wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Tanga, Anthony Banzi. Jubilee hiyo ilikwenda sambamba na ibada iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali Askofu Mstaafu Kadinali Policapy Pengo pamoja na viongozi mbalimbali wakimiwa wa serikali na kisiasa. Alisema kwamba wanaimani kwa pamoja wanaweza kujenga na kuimarisha kuendelea amani na umoja uliopo hapa nchini wakishirikiana kwa pamoja kuongeza kasi ya watawezesha Watanzania kupata maendeleo. “Baba Askofu sisi kama serikali tutatimiza wajibu wetu kutengeneza mazingira mazuri kwa madhehebu ya dini kutekeleza wajibu wake kwani uhuru wa kuabudu uliopo nchini unaheshimiwa na kutekelezwa kwa vitendo,” alisema Rais Magufuli katika hotuba yake hiyo Waziri Ummy alisema kwamba licha ya utofauti za dini, kabila rangi au vyama Rais Dk. Magufuli,  anasema tofauti hizo hatuna budi kuishi nazo na wasiziache zikawa nyufa za uhasama ambao sio zitaligawa taifa bali linaweza kulimonyony’oa hata kanisa. “Wana Tanga wanayo matumaini makubwa kwa sababu wanathamini na kutambua manufaa makubwa yanayofanya kwenye harakati za kujilete maendeleo kutokana na kazi kubwa mnayoifanya kuwapa maendeleo,” alisema Awali akitoa salamu za kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Balozi wa Papa hapa nchini, Kadinali Kindondi alisema kuwa mchango waAskofu Banzi ni mkubw kwa kanisa na uhudumu wake wa kazi za kanisa umekuwa ni kichocheo cha maendeleo .
1
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema atapita kila vituo vya polisi nchini kukagua bodaboda, bajaji au baiskeli ili kubaini zimefi kishwa katika vituo hivyo kwa makosa gani.Lugola alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalumu, Fatuma Tawfiq (CCM) aliyetaka kujua serikali ina mkakati gani wa kudhibiti ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha waathirika bila kulipwa bima.Lugola alisema polisi wanatakiwa kuwasaidia waathirika wa ajali kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo michoro ya ajali za watu ili walioathirika na ajali walipwe na bima za magari yaliyosababisha ajali hizo.Alisema polisi ambao wanakamata bodaboda hata kwa makosa madogo na kuziweka vituoni wanakiuka maagizo ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ibara namba 4 ambayo inataka vijana hao wajiajiri ili kupambana na umaskini.Alisema hategemei kuona bodaboda zinakamatwa kwa kutokuwa na kofia ngumu, kupakia mishikaki au haina kioo cha pembeni au makosa mengine madogo, ambayo wanatakiwa kupewa muda wa kulipa faini na kuendelea na kazi.Alisema atatembelea vituoni na anategemea bodaboda atakazozikuta ni zile zenye makosa manne ya kuhusika katika uhalifu, haina mwenyewe, imesababisha ajali au kuibiwa mahali na si vinginevyo.Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalumu, Hawa Mwaifunga (Chadema) aliyetaka kujua serikali imejipanga vipi kukabiliana na ajali za barabarani ambazo zimekuwa tishio kwa maisha ya Watanzania, Naibu Wziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yususu Msauni alisema, kutokana na athari kubwa za ajali barabarani kwa taifa, serikali ina mkakati wa madhubuti wa kupambana na tatizo hilo.Alisema mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza wigo wa elimu ya usalama barabarani kwa watumiaji wa vyombo vya moto kwa njia ya redio, runinga, machapisho na vipeperushi.Aidha, mikakati mingine ni kuboresha mifumo ya utendaji katika maeneo ya ukaguzi wa mabasi na malori, mfumo wa ufuatiliaji wa magari barabarani na mfumo wa utoaji nukta katika leseni za madereva utakaodhibiti tabia za madereva wazembe.
1
PARIS, Ufaransa POLISI jijini Paris nchini Ufaransa, wamesema mke wa  msanii wa hip hop, Kanye West, Kim Kardashian, ameporwa vito vya thamani ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 10 na watu waliokuwa na silaha akiwa amepumzika katika makazi yake jijini hapo. Mwanadada huyo aliibiwa vito hivyo baada ya kuvamiwa sehemu alipokuwa amepumzika, watekaji walimfunga kamba kisha wakamfungia bafuni na baada ya kumwibia, walitoweka eneo la tukio. Msemaji wa mwanamama huyo, alisema Kim alikuwa katika Jiji hilo kwa ajili ya kuhudhuria maonyesho ya wiki ya Fashion yaliyokuwa yakifanyika jijini humo. “Hakuumia sehemu yoyote, alishtuka tu baada ya uvamizi huo na kuibiwa vito vyenye thamani hiyo, lakini yupo vizuri na anaendelea vyema,” alieleza msemaji wake. Polisi walieleza kwamba watekaji hao watano waliiba boksi lenye vito vya thamani ya euro milioni 6 sawa na dola milioni 6.7 na pete yenye thamani ya euro milioni 4. Wakati tukio hilo likitokea, mume wa mwanadada huyo, Kanye West, alikuwa jukwaani kwenye tamasha la muziki na sanaa lililokuwa likifanyika jijini New York, Marekani ambapo alilazimika kukatisha shoo yake huku akiwaomba radhi mashabiki wake kutokana na hilo. “Samahani nimepatwa na taarifa za tatizo kwa familia yangu, hivyo nasimamisha shoo,” Kim aliwaeleza mashabiki wake. Kim alishawahi kukutana na matukio ya kuvamiwa ambapo mwaka 2014, aliwahi kuvamiwa lakini pia hivi karibuni aliwahi kuvamiwa na shabiki wake na kutukanwa alipokuwa akiingia katika moja ya mgahawa nchini Marekani.
4
London, England LICHA ya kucheza dakika 66 pekee katika mchezo wa usiku wa kuamkia jana dhidi ya Leicester City, mwanasoka wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta, amefanikiwa kuwateka mashabiki wa Aston Villa. Katika mchezo huo wa marudiano ya nusu fainali ya Kombe la Ligi, Samatta alikuwa sehemu ya kikosi chake kwanza, huku Villa wakishinda mabao 2-1 kupitia kwa Matt Targett na Mahmoud Hassan ‘Trezeguet’. Samatta alikaribia kuzitikisa nyavu za Leicester wakati Villa wakiwa wanaongoza bao 1-0 lakini alishindwa kuunganisha mpira wa krosi uliopigwa na Jack Grealish. Nyota huyo aliyetua Villa akitokea Genk alikaribia tena kuwatungua Leicester katika dakika ya 26 lakini alishakuwa kwenye eneo la kuotea wakati anapokea pasi ya Frederic Guilbert. Akimzungumzia Samatta aliyeitwa benchi katika dakika ya 66 na nafasi yake kuchukuliwa na Keinan Davis, mmoja kati ya mashabiki wa Villa, Ash, alitumia ukurasa wake wa Twitter kuandika: “Nimeona kitu kwa Samatta, ni mzuri. Alitakiwa kuondoka na bao lakini apewe wiki chache na hakika tutaona mabao yake.” Shabiki mwingine, Alex Franklin, aliandika: “Ni mwanzo mzuri kwa Samatta. Nimekoshwa na hilo. Hakuna kinachoweza kunipa hofu kwa alichokionesha.” Dale Wootton ni shabiki wa Villa pia, naye aliandika: “Nilichokiona kwa Samatta kinaniambia atafunga mabao mengi.” Jumamosi ya mwishoni mwa wiki hii, Samatta atacheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu ya England akiwa na Villa, endapo kocha wake, Dean Smith, atampa nafasi dhidi ya Bournemouth.
2
Mwandishi Wetu,Dar es Salaam ZAIDI ya wafanyabiashara 2000 katika mkoa wa kodi wa Ilala wamepatiwa elimu ya kodi inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini.Mamlaka hiyo imekuwa na ikifanya kampeni ya elimu ya kodi mara kwa mara kwa kuwafata wafanyabiashara kwenye biashara zao (mlango kwa mlango). Akizungumzai zoezi hilo Afisa Msimamizi wa Kodi wa mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Zakeo Kowelo alisema kuwa katika siku sita za zoezi hilo, jumla ya wafanyabiashara 2,165 wamepatiwa elimu mbalimbali ya kodi. Alisema maeneo ambayo wamewafikia wafanyabiashara na kuwapatia elimu ni Tabata, Relini, Bima, Liwiti, Barakuda, Kimanga, Segerea, Kinyerezi, Kisiwani na Bonyokwa Mkoa wa Kodi wa Ilala. Alisema zoezi limeenda vizuri na kwamba wafanyabiashara wametoa ushirikiano wa kutosha kwa kutoa taarifa muhimu na kuonyesha nyaraka ambazo zilihitajika jambo ambalo limewawezesha kuwapa ushauri na elimu inayostahili. “Kwa hili tunawashukuru sana kwani tumeweza kuwaelimisha kama tulivyopanga”, alisema KoweloAlisema zoezi lilihusisha kupita duka kwa duka na kuangalia taarifa za wafanyabiashara za kodi ambapo baada ya kuangalia taarifa walifanya majadiliano na kumshauri mfanyabiashara jinsi ya kutunza kumbukumbu. Aliongeza kuwa kwa wale ambao hawajasajili biashara zao wameelekezwa taratibu za kusajili ili watambulike kuwa walipakodi na kwamba pamoja na kusajili biashara pia wafanyabiashara wameshauriwa jinsi ya kujisajili na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale wanaostahili kutumia mashine za kodi za kielektroniki wamepewa utaratibu wa kupata na kuzitumia mashine hizo. “TRA ni sehemu ya biashara za wananchi hivyo lengo letu ni kuwaelimisha wananchi ili wafanye biashara kwa usalama zaidi na kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi sahihi na kwa wakati’, alisema Kowelo. Naye Stewart Kimbaga mfanyabiashara wa duka la urembo maeneo ya Bonyokwa alisema kuwa kampeni hiyo ya elimu ya kodi ni nzuri na kwamba itasaidia kutokana na kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawana uelewa wa jinsi ya kufanya biashara ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kulipa kodi. Alisema hiyo ni fursa muhimu na kwamba ukaguzi peke yake hautoshi bali unatakiwa uambatane na elimu ili kuwaongezea wananchi uelewa na kujenga uhusiano mzuri baina ya TRA na walipakodi. Zoezi la kutembelea walipakodi katika maeneo yao ya biashara ni mkakati ambao TRA inautekeleza ili kuwaelimisha walipakodi, kuwapa ushauri wa kitaalamu kuhusu taratibu za kulipa kodi, kusajili biashara ambazo hazijasajiliwa, kuwakumbusha kulipa kodi, kutatua changamoto zinazo wakabili na kupata maoni yao kuhusu huduma inayotolewa na TRA kwa ajili ya kuboresha utendaji wake.
0
Akizungumza baada ya mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Nsimbe alisema hana wasiwasi na Yanga kwani wachezaji wa Yanga anawafahamu.“Udhaifu wa wachezaji wa Kitanzania naufahamu hivyo sipati shida namna ya kuifunga Yanga kwani nia yetu ni kutwaa ubingwa,” alisema Nsimbe ambaye amewahi kuifundisha Azam FC.Tusker FC yenye makao yake katika mtaa wa Ruaraka jijini Nairobi inaundwa na wachezaji wenye miili iliyojengeka na warefu Tusker FC inayodhaminiwa na SportPesa imeshinda taji ya Ligi Kuu Kenya mara 11 katika mwaka 1972, 1977, 1978, 1994, 1996, 1999, 2000, 2007, 2011, 2012 na 2016.Baada ya mchezo kati ya Yanga na Tusker FC utafuatiwa na mchezo wa Singida United na AFC Leopards Simba inatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza Jumanne dhidi ya Nakuru All Stars ya Kenya na Gor Mahia ikichuana na Jang’ombe Boys ya Zanzibar.Bingwa ataondoka na zawadi ya sh milioni 66 zinazotolewa na Kampuni ya SportsPesa inayoendesha bahati nasibu nchini Kenya na hapa na inaidhamini Everton katika Ligi Kuu England ambayo itacheza na bingwa wa SportPesa Juni 13.
2
Stars itakabiliana na Algeria ukiwa ni mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018, zilizopangwa kufanyika Urusi.Akizungumza na gazeti hili Cannavaro alisema huo ni mchezo mgumu ambao ili kukabiliana na timu hiyo ni lazima waanze maandalizi mapema ikiwezekana wapate hata siku 10 za kuweka kambi nje ya nchi.“Algeria ni timu bora Afrika ndiyo sababu nasema mchezo huo utakuwa mgumu, itapendeza kama tutapata kambi hata ya siku 10 nje ya nchi ambayo naamini itatuongezea ari ya kuwakabili na kupata ushindi angalau wa mabao 2-0, ili waweze kujiweka katika mazingira mazuri ya kusonga mbele,”alisema Canavaro.Nahodha huyo alisema endapo watapata ushindi wa mabao mawili itakuwa rahisi kwao kusonga mbele kwa sababu timu yao ina uwezo mkubwa wa kuzuia pindi watakapokwenda kucheza ugenini kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika Algeria.Alisema anazijua vyema timu za Waarabu watakuja nchini kutafuta angalau sare ili katika mchezo wa marudiano waweze kumaliza kazi.Stars inayofundishwa na kocha Charles Mkwasa imepangiwa kucheza na Algeria baada ya kuitoa Malawi kwa jumla ya mabao 2-1, mechi ya kwanza iliyochezwa Dar es Salaam ilishinda 2-0 na katika mchezo wa marudiano uliofanyika Malawi ilifungwa bao 1-0.
2
SIMBA imeweka wazi kuwa itahakikisha inavuna pointi zote sita kwa kushinda michezo yake miwili ijayo ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya timu za Kanda ya Ziwa, Kagera Sugar na Biashara United.Simba ambayo inaongoza ligi ikiwa na pointi sita baada ya kushinda mechi zake mbili, Septemba 28 katika Uwanja wa Kaitaba, Kagera itavaana na Kagera Sugar iliyonafasi ya pili nayo ikiwa na pointi sita, kisha kucheza katika Uwanja wa Karume Mara dhidi ya Biashara United iliyonafasi ya pili kutoka mkiani mwa msimamo wa ligi. Simba ina kumbukumbu mbaya ya kufungwa mabao 2-1 mara ya mwisho walipocheza na Kagera katika Uwanja wa Kaitaba, Aprili 20, mwaka huu, lakini kwa Biashara wana kumbukumbu ya kupata ushindi wa mabao 2-0 walipokutana Aprili 27 katika Uwanja wa Karume, Mara.
2
BARCELONA, HISPANIA RAIS wa zamani wa klabu ya Barcelona Joan Laporta, ameikosoa bodi ya klabu hiyo kwa kushindwa kukitunza kipaji cha mshambuliaji Lionel Messi uwanjani. Laporta aliwahi kuwa rais wa klabu hiyo mwaka 2003 na kufanikiwa  kusimamia mafanikio ya klabu hiyo kabla ya kumaliza muda wake miaka saba iliyopita. Mgogoro wa  katikati ya msimu wa  2014/15 katika klabu hiyo usababisha kuitishwa kwa uchaguzi ambapo Laporta alisimama kugombea lakini alishindwa kutamba mbele ya Josep Maria Bartomeu. Akiwa katika mahojiano na redio moja maarufu jijini Catalunya, Laporta alisema kwamba hafurahishwi kabisa na namna ambavyo Bartomeu anavyoendesha klabu hiyo. Laporta alisisitiza kwamba Bartomeu alitakiwa kujua namna ya kuishi katika kipaji cha Messi. “Klabu hadi sasa haijafahamu namna ya kuishi na kipaji cha Messi, ni mchezaji bora wa kihistoria pia mchezaji bora duniani. “Bartomeu amefeli kutimiza moja ya ahadi yake wakati akisaini dili la udhamini mpya na Qatar Airways” alisema Laporta. Laporta aliendelea kumtupia lawama mpinzani wake huyo kwa kudai kwamba ni mwongo. “Alitudanganya kwenye kampeni kwamba angeweza kupokea dili zenye thamani ya euro milioni 60, lakini hadi sasa hakuna kitu kama hicho,” alihoji Laporta.
2
Na WAANDISHI WETU-DAR ES SALAAM SERIKALI, vyama vya siasa na wadau mbalimbali, wametoa matamko kuhusu Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana. Akizungumzia siku hiyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema Serikali inatambua ukatili dhidi ya wanawake bado ni tatizo ambalo linaathiri ushiriki wao katika shughuli za uchumi na jamii. Alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeandaa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. “Serikali inatambua ukatili dhidi ya wanawake bado ni tatizo kubwa ambalo linaathiri ushiriki wao katika shughuli za uchumi na jamii. “Katika kukabiliana na tatizo hilo, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeandaa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (2017/18 – 2021/22) ambao ulizinduliwa Desemba 13, mwaka jana,” alisema. Alisema kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu, ‘Tanzania ya Viwanda; Wanawake ni Msingi wa Mabadiliko ya Uchumi’, imetolewa kutokana na kaulimbiu ya kipaumbele ya Umoja wa Mataifa mwaka huu katika mkutano wa 61 wa Hali ya Wanawake Duniani (CSW). “Kaulimbiu hii ya “Tanzania ya Viwanda: Wanawake ni Msingi wa Mabadiliko ya Uchumi” inalenga kuhamasisha jamii, asasi za raia, sekta binafsi, taasisi za Serikali, vyama vya siasa, wabia wa maendeleo, mtu mmoja mmoja na wadau wengine nchini kuongeza wigo wa fursa za uchumi kwa wanawake kuwawezesha kushiriki na kunufaika na hatua za maendeleo,” alisema. SAMIA Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, amelaani na kukemea vitendo vya ukeketaji wa wanawake na ubakaji vinavyoendelea katika jamii. Aliwataka wananchi kote nchini kushirikiana kukabiliana na vitendo hivyo. Alitoa wito kwa wananchi na wadau wote bila kujadili dini, kabila wala rangi kupambana ipasavyo na vitendo hivyo ambavyo vinarudisha nyuma jitihada za kumkwamua mwanamke katika uchumi. Kuhusu maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Samia alisema jukumu kubwa la Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha wanawake wanaboreshewa ipasavyo mazingira ya kufanyia kazi, hasa shughuli za ujasiriamali waweze kufikia malengo waliyojiwekea. “Inapofika katika shida zetu wanawake ni lazima tuwe kitu kimoja na sauti moja katika kulinda na kutetea haki zetu bila kujali itikadi za siasa,” alisema. CHADEMA Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa wito kuwahamasisha na kuwataka wanawake wote duniani kutambua nguvu waliyonayo na umuhimu wao kama chachu ya mabadiliko ya siasa, uchumi na jamii. “Tunatambua nguvu ya wanawake katika harakati za mabadiliko. Tunatoa wito kwa jamii nzima kuendelea kuwahamasisha wanawake na wasichana wa Tanzania tupambane pamoja kuleta mabadiliko,” alisema Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliao wa chama hicho, Tumaini Makene.    Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, alisema endapo wanawake wataelimishwa, watakuwa ni chachu ya kupunguza matumizi ya dawa za kulevya. Alisema katika maadhimisho hayo wametembelea hospitali ya Wilaya ya Ubungo ya Palestina iliyopo Sinza, Kituo cha Afya  Kimara na Mbezi ambako waligawa zawadi kwa wanawake waliokuwa wamelazwa. “Tumegawa kanga, sabuni za unga na vipande, maji, soda na pampas, lengo likiwa ni kuwasaidia wanawake ambao ndio chachu ya maendeleo katika jamii kwa ujumla,” alisema Jacob. Alisema kwa vile Manispaa ya Ubungo ina maeneo mengi, wamejipanga kuhakikisha inajengwa hospitali kubwa itakayokuwa ya wilaya na itakuwa na uwezo wa kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi. ACT-WAZALENDO   Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema akiwa amelelewa na mwanamke mwenye ulemavu na mpiganaji wa kweli wa haki za wananchi walio pembezoni, hana budi kutoa heshima zaidi ya kuongoza chama chenye misingi thabiti ya kumkomboa mwanamke. “Kwa wanawake, ninyi ndio mhimili wa taifa hili, wazalishaji wakuu na walezi wa taifa letu. Kuirejesha nchi kwenye misingi ni wajibu wa kutambua nafasi yenu stahili katika jamii. “Nikiwa nimelelewa na mwanamke mwenye ulemavu na mpiganaji wa kweli wa haki za wananchi walio pembezoni, sina namna kutoa heshima yangu zaidi ya kuongoza chama chenye misingi thabiti ya kumkomboa mwanamke. “Msitarajie watu wengine kuwapigania, mnapaswa kuchukua hatua kupitia jukwaa la ACT-Wazalendo,” alisema Zitto. TAMWA Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Edda Sanga, alisema azma ya Serikali kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati wa viwanda itafikiwa endapo haki ya elimu kwa mtoto wa kike itapewa kipaumbele na kuhakikisha sera na sheria kandamizi zinarekebishwa. “Tunaamini kuwa azma ya nchi ya kuipeleka Tanzania katika uchumi wa kati na viwanda  itafikiwa endapo haki ya elimu kwa mtoto wa kike itapewa kipaumbele na kuhakikisha sera na sheria kandamizi kwa wanawake na watoto wa kike zitarekebishwa na kuwezesha ushirikishwaji wa wanawake katika ngazi mbalimbali za uongozi na uamuzi,” alisema Sanga. DC TEMEKE Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, aliwataka wanaume wanaonyanyaswa na kupigwa na wake zao kujitokeza hadharani kuwashtaki katika madawati ya jinsia. “Wapo baadhi ya wanaume nao wananyanyaswa na wake zao… nawaomba msione aibu jitokezeni nanyi mshtaki katika dawati la jinsia,” alisema Lyaniva. Lyaniva alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
1
WIKI hii, Julai 1, Benki ya Dunia iliingiza Tanzania katika kundi la nchi zenye kipato cha kati. Hizi ni habari njema hata pamoja na kwamba wapo wanaoona kuna mapungufu fulani fulani katika utendaji. Hatua ya kutoka katika umaskini na kupanda kwenda katika hatua nyingine ya juu huusisha suala zima la uchumi au maendeleo ya kiuchumi. Lakini pamoja na hayo maendeleo ya kiuchumi huguswa na vitu au mambo mengi mfano kutenda haki, amani, usalama, utulivu nakadhalika. Mtu yeyote anapokuwa katika mazingira yenye kutenda haki, amani, utulivu humwezesha kufanya kazi kwa bidii na hatimaye kuwa mzalendo kwa nchi yake ikiwa ni pamoja na kulipa kodi. Sasa mazingira yanapokuwa tofauti na hayo, ndiyo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya nchi . Kwa sababu hiyo sisi tunaweza kusema tumekuwa mabalozi wazuri wa kusisitiza suala la haki kila wakati, kwa sababu tumekuwa tukiamini haki ni msingi wa mambo yote mazuri. Na ndio maana tumekuwa tukikosa na wakati mwingine kukumbusha kutenda haki hasa katika vyombo vile vya kimaamuzi na kiutendaji. Tumekuwa tukisisitiza kwamba vyombo hivyo vinapaswa kutambua wajibu wao kuwa ni kutafuta namna ya kutatua matatizo na si kuyaongeza. Yapo baadhi ya matukio si yote ambayo yamefanywa na vyombo hivyo na hivyo kutoa taswira ya kukomoa au kuumiza baadhi ya watu kwa makusudi. Tumekuwa tukisisitiza  hayo kutokana na kuwapo kwa ripoti ambazo zinaonyesha kuwa barani Afrika kwa muda mrefu sasa watu wameumizwa na vitendo vya kudhulumiwa haki zao msingi. Kwa mujibu wa ripoti hizo hata kutopea katika umaskini wa kimawazo, na hivyo wengi kuhadaika na kauli za wanasiasa, viongozi na watu wenye nafasi katika jamii, msingi wake ni dhuluma ya haki zao za msingi.  Kwa misingi kama hiyo sisi kama  chombo cha habari  tunao wajibu wa kukumbusha kwamba vyombo hivyo kila inachofanya kabla ya kutoa uamuzi wowote basi vitambue vinao wajibu wa kuchunguza, kusikiliza, kubadilisha na kuboresha. Zipo nyakati tumeshuhudia vyombo hivi vikichukua uamuzi wa ghafla hata katika masuala nyeti sana katika mifumo ya sheria, utumishi nk.  Vyombo hivi vinapaswa kutambua kwamba chochote kitakachofanyika bila kufuata misingi hiyo tuliyoitaja hapo juu kitakwenda kuathiri mustakabali mwema wa Taifa letu. Wakati fulani aliyepata kuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedikto wa XVI, alitoa changamoto kubwa kwa watawala wa dunia.  Kwa maneno yake mwenyewe alisema; “jamii yenye haki hujengwa na wanajamii wenye haki”.  Maana yake tukitaka kujenga jamii yenye haki hatuna budi sisi wenyewe kuwa wenye haki. Kiongozi huyo alikwenda mbali na kusema; wao kama kanisa hawana mbinu za kiufundi wala nafasi ya kuingilia mambo ya siasa moja kwa moja lakini alibainisha wazi utume ambao alisema kama kanisa haliwezi kuuacha hata kidogo ni ule wa kuutangaza ukweli. Ukweli si jambo ambalo linapaswa kubebwa na taasisi zetu za kidini tu bali hata katika serikali zetu na taasisi zake, mahakama zetu, vyombo vya ulinzi na uslama kama Jeshi la Polisi,  Bunge nk. Kuna msemo mmoja kwamba; ukweli ndio utakaowaweka watu wote huru: iwe katika siasa au katika nyanja yoyote ya kijamii.  Kwa sababu hiyo tunaamini ujenzi wa jamii yenye misingi ya haki ni wajibu wetu sote lakini serikali, mahakama na Bunge linawajibika kujenga dhamira hiyo.  Mahakama itambue kama ni taasisi ya kupigania haki, serikali ni wakala wa haki vivyo hivyo hata Bunge.  viongozi  wakiwamo wale wa kisiasa, na wananchi watambue kuwa wao ni wawajibikaji katika shughuli za kijamii na iwapo wote hawa watauzingatia ukweli ndani ya dhamiri zao zilizojengwa juu ya ukweli na ukweli tupu, basi jamii ina uhakika wa kujenga haki na amani na matokeo ya hayo ni kupaa kimaendeleo.
0
Na SAMWEL MWANGA WAKULIMA wa  pamba   mkoani Simiyu wameitaka serikali kuivunja Bodi ya Pamba Tanzania (TCB) kwa kuwa imekuwa na kiburi. Wamedai bodi hiyo inataka kuua biashara ya bei ya zao hilo huku wakulima wakinyanyasika. Vilvile  wamewataka viongozi   serikalini wanaoikumbatia bodi hiyo kuacha mara moja kwa kuwa  imekuwa hata ikishindwa kutekeleza maagizo mbalimbali  yanayofikiwa na mkutano mkuu wa wadau wa zao hilo ikiwamo   kuwapo   mashamba ya kuzalisha mbegu za   pamba. Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Bariadi, walisema   wanashangazwa na kitendo cha bodi hiyo kugeuka kuwa  ndiyo msimamizi mkuu wa upangaji wa bei ya pamba   kwa mkulima wa pamba badala ya kusaidia kilimo hicho kikue. Walisema    umefika wakati kwa bodi hiyo kuvunjwa kwa sababu imeshindwa kuendeleza zao hilo na kila kukicha mkulima wa   pamba amekuwa akinyanyasika huku watumishi wa bodi hiyo wakiendelea kuneemeka kupitia jasho la wakulima. “Mimi nataka serikali kupitia  Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi avunje bodi hii kwa sababu kazi yake ni kupanga bei ya pamba badala ya kuwasaidia wakulima kuendeleza kilimo hicho “Hata bei wanayopanga ni ya kumnyanyasa mkulima huku wao wakiendelea kunufaika kwa kutumia jasho letu sisi wakulima,” alisema Khija Malimi. Madirisha Saguda alisema watu milioni 16   wanategemea kilimo hicho na wamekuwa wakilia kila siku kupata soko zuri la zao hilo lakini bodi hiyo imekuwa haina faida kwao. Alisema  hivyo ivunjwe na kusisitiza kuwa  ndiyo mchawi mkubwa wa zao hilo hivyo haina umuhimu ivunjwe tu. “Wakulima tupatao milioni 16   nchini tunaolima zao hili la pamba kila mwaka tumekuwa tukililia tupate bei nzuri ya pamba kutokana na gharama kuwa kubwa za uzalishaji. “Lakini kinachotokea ni hawa bodi ya pamba wanakuja na kutupangia bei  kwa maslahi yao na kwa uhalisia mchawi wa   pamba ni bodi yetu hii ya pamba, naona haina umuhimu ni vizuri ikavunjwa,”alisema Saguda. Naye Mayunga Kisena alisema bodi hiyo imekuwa ni kikwazo cha kuendeleza zao hilo kwa vile  imekuwa ikimkandamiza mkulima  na wafanyabiashara wadogo  wa zao hilo huku w wafanyabiashara wakubwa wakikumbatiwa kwa manufaa yao binafsi. Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga,   alisema  bodi hiyo imekuwa ikifanya kazi kwa ujanjaujanja. Alisema bodi hiyo inashindwa hata kusimamia maagizo yaliyopitishwa kwenye mkutano wa mwaka jana wa wadau wa zao hilo ya kutaka   ianzishe mashamba ya kuzalisha mbegu ya zao hilo,   badala yake inatumia mashamba ya wananchi.
1
Aidha, wasanii wengi wa muziki wamekacha semina hiyo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) iliyokuwa na lengo la kutoa elimu ya matumizi mazuri ya huduma za mawasiliano ikiwa ni pamoja na simu na mitandao ya kijamii.Akitoa mada ya ukuaji wa sekta ya mawasiliano, Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy alisema huduma za mawasiliano zikitumika vizuri zinaweza kumsaidia msanii wa muziki kufanyakazi zake kwa ufanisi.Alisema ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano ambao umekuwa na fursa nyingi unakabiliwa na changamoto ambazo zimekuwa zikiathiri uchumi wa nchi na wananchi wakiwemo wasanii wa muziki.“Makusudi ya mawasiliano kwa msanii yanaweza kumsaidia kufanyakazi kwa ufanisi lakini sasa wasanii wanatumia kuwindana. Hivyo wasanii kutumia mitandao ya jamii kuweka vitu vya maana badala ya kuweka picha za “kantangaze”, “alisema.Alisema wasanii wa muziki kama ilivyo jamii nyingine ni waathirika wa matumizi mabaya ya huduma za mawasiliano kama mitandao ya kijamii.Hata hivyo katika semina hiyo ambayo ilitakiwa kuhudhuriwa na wasanii wamuziki wapatao 70, lakini mpaka semina inaanza walikuwa wasanii wapatao 15 waliofika ikiwa ni saa mbili kupita muda uliopangwa kuanza.Naye Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dk Ally Simba alisema mamlaka yake imeandaa semina hiyo kwa kujua kuwa wasanii ni watumiaji wa huduma nyingi za mawasiliano.“Wasanii ni watu muhimu katika jamii yetu na wana kitu cha ziada kwani wanashiriki katika kutoa elimu kupitia kazi zao,” alisema.Alisema wasanii wa muziki wana mchango katika kuletea taifa sifa kwa kuiwakilisha nchi na kushinda tuzo mbalimbali shughuli wanazofanya kwa kutumia mawasiliano, ikiwamo mitandao ya kijamii, internet , simu na huduma za utangazaji kama radio na tv ambazo husimamiwa na TCRA.
2
WANAJESHI kadhaa wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi Tanzania (JWTZ) wameondoka kwenda Sudan kulinda amani kwa kipindi cha mwaka mmoja.Wanajeshi hao kwa mara ya kwanza kwa kipindi cha miaka 12 ya ushiriki wa Tanzania kwenye ulinzi wa amani Sudan, wamesafirishwa kwa kutumia ndege ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) aina ya Boeing 787- 8 Dreamliner. Akizungumza na waandishi wa habari jana Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa JWTZ, Meja Jenerali Alfred Kapinga alisema kusafirisha wanajeshi hao kwa kutumia ndege ya ATCL ni uzalendo wa hali ya juu kwa nchi.Alisema; ” leo tunawaaga wanajeshi wetu wanaokwenda kulinda amani Sudan, wanajeshi hawa wana mafunzo na weledi wa hali ya juu katika ulinzi wa amani, kwanza wana nidhamu na uelewa wa kazi lakini kikubwa zaidi na cha kujivunia wanakwenda kwa kutumia usafiri wetu wenyewe wa ndege. “Awali tulikuwa tunatumia usafiri wa mashirika mengine ya ndege ambayo yalikuwa yakiwapeleka wanajeshi wetu nchi mbalimbali kulinda amani, lakini leo kwa mara ya kwanza tangu tumeanza kwenda kulinda amani Sudan, tumetumia ndege yetu ya nyumbani, hii ni hatua nzuri sana.”Alisema, pamoja na kuwasafirisha kwa mashirika ya ndege ye nje ya nchi lakini pia walikuwa wakitumia ndege za kijeshi lakini kwa ubora wa ndege za ATCL za hivi sasa, wanajeshi hao watasafirishwa kwa ndege hiyo ya ATCL kwenda na kurudi. Pia Meja Jenerali Kapinga alibainisha kuwa kwa kuwasafirisha wanajeshi kwa ndege za hapa nchini kunawaongezea ari ya uzalendo na uhakika wa usalama wao kutokana na imani yao kuwa wanasafirishwa kwa kutumia chombo cha nyumbani hadi kwenye eneo lao la kazi.Aliongeza kuwa wanajeshi wa Tanzania wamekuwa wakifanya kazi ya ulinzi wa amani kwa nguvu zao zote na kwa kuzingatia miiko inayotakiwa na ndio maana Umoja wa Mataifa (UN) umekuwa ukiitumia nchi ya Tanzania kwenye shughuli nyingi za ulinzi wa amani. Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi alishukuru JWTZ kwa uamuzi wake wa kuishauri UN kutumia ndege ya ATCL kwa ajili ya kusafirisha wanajeshi.Alisema,”pongezi zetu nyingi kwa Mkuu wa Majeshi na jeshi zima kwa kuamua kuwasafirisha wanajeshi wetu kwa kutumia ndege yetu, hakika ni hatua kubwa ya mafanikio.” Mmoja kati ya wanajeshi wanaokwenda kulinda amani Sudan, Wilfrida Sabath alisema kuwa wamejipanga kwenda kulinda amani na kurejea nyumbani salama huku akipeleka pongezi kwa Rais John Magufuli kwa kununua ndege hiyo iliyowawezesha kusafiria kwenda Sudan.
1
ANJOUAN, COMORO WAKAZI wa kisiwa cha Anjouan nchini Comoro wamesema kumekuwa na milio ya risasi katika mitaa ya mji mkuu wa nchi hiyo, Mutsamudu, baada ya vikosi vya ulinzi kuvunja vizuizi vya barabarani, serikali inavyosema viliwekwa na upinzani. Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchi hiyo Mohamed Daoudou amewalaumu waandamanaji kwa kutumia silaha za moto na kupinga madai kuwa askari wake walifyatua risasi. Amesema Gavana wa Anjouan Abdou Salami Abdou, ambaye anatokea upinzani ndiye aliyepanga na kusababisha machafuko hayo. Kumekuwa na maandamano na wandamanaji wengi kukamatwa katika kisiwa hicho chenye mkusanyiko wa visiwa vingi katika Bahari ya Hindi tangu Julai mwaka huu. Machafuko hayo yanatokana ushindi wa Rais Azali Assoumani katika kura ya maoni yenye utata iliyomaliza utamaduni wa kuongoza kwa mzunguko katika nchi hiyo yenye visiwa vikubwa vitatu. Ushindi huo unamaanisha kwamba Rais Azali ataendelea kubakia madarakani.
3
Na Kulwa Mzee -Dar es Salaam MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeutaka upande wa Jamhuri kukamilisha haraka upelelezi katika kesi ya  kughushi, kutakatisha fedha na  kujipatia Dola za Marekani 540,390 kwa udanganyifu inayomkabili mfanyabiashara Ndama Shabani Hussein, maarufu kama Pedeshee Ndama Mtoto wa Ng’ombe (44). Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Victoria Nongwa, alisema hayo jana baada ya Wakili wa Serikali, Leonard Challo kudai mahakamani wakati kesi ilikuwa inatajwa, kuwa upelelezi haujakamilika. Mwita aliomba kesi hiyo iahirishwe hadi tarehe nyingine kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika. Hakimu Nongwa, aliiahirisha kesi hiyo hadi Januari 24, mwaka huu na kuamuru upande wa mashtaka kuhakikisha upelelezi unakamilika haraka. Awali ilidaiwa Februari 20, 2014 Dar es Salaam kuwa mshtakiwa alighushi kibali cha kusafirisha madini na sampuli za madini kwa kusudi la kuonesha kuwa Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment iliruhusiwa kusafirisha maboksi manne ya dhahabu kilogramu 207 yenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000 kwenda Australia kwa Kampuni ya Trade TJL DTYL Limited wakati akijua si kweli. Mshtakiwa huyo, anadaiwa kuwa Machi 6, 2014, Dar es Salaam, alighushi kwa kutengeneza hati ya kibali (Certificate of Clearance) ya Umoja wa Mataifa ofisi ya Dar es Salaam akijaribu kuonesha kilo 207 za dhahabu kutoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zinatarajiwa kusafirishwa na Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment kwenda Australia kwa Kampuni ya Trade TJL DTYL Limited, zimesafirishwa bila jinai yoyote wakati akijua si kweli. Inadaiwa Februari 20, 2014 mshtakiwa huyo anadaiwa kughushi fomu ya forodha yenye namba za usajili R.28092 akionesha Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment imelipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) dola za Marekani 331,200 kama kodi ya uingizaji wa bidhaa ambazo zina uzito wa  kilogramu 207 za dhahabu zenye thamani ya Dola za Marekani 8,280,000 kutoka Kongo kitu ambacho si kweli. Iliendelea kudaiwa kuwa Februari 20, 2014, mshtakiwa huyo alighushi nyaraka ya bima kutoka Phoenix of Tanzania Assurance  Company Ltd akionesha Kampuni ya Muru Platnum Tanzania Investment Company Limited imeyawekea bima maboksi manne yaliyokuwa na dhahabu hizo zenye uzito wa kilogramu 207 wakati akijua ni uongo. Kati ya Februari 26 na Machi 3, 2014 jijini Dar es Salaam kwa njia ya udanganyifu anadaiwa alijipatia kutoka kwa kampuni ya nchini Australia ya Trade TJL DTYL Limited dola za Marekani 540,390 baada ya kudanganya atawapa na kusafirisha dhahabu hizo zenye uzito wa kilogramu 207 na thamani ya dola 8,280,000 wakati akijua kuwa ni uongo.
1
UELEWA mdogo katika masuala ya kodi umetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa wafanyabiashara wengi kuona ulipaji kodi ni mzigo.Akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na Benki ya NBC kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mjini Arusha, Ofisa Elimu Mkuu wa TRA, Rose Mahendeka alisema wafanyabiashara na wananchi wanapaswa kufahamu kuwa kodi ndio chanzo kikuu cha mapato ya serikali.“Ni vema jamii ifahamu kuwa bila kodi huduma za kijamii haziwezi kupatikana, malipo ya mishahara, huduma za hospitali, barabara na madaraja, zinachangiwa kwa kiasi kikubwa na kodi kutoka kwa wananchi wake”, alisema.Pamoja na hayo ofisa elimu huyo alisema licha ya serikali kutumia misaada na mikopo kwa shughuli za kimaende- leo, lakini ingependa kutumia kodi kuondoka na mzigo wa riba zinazotokana na mikopo na pia kuepuka kuomba na kutegemea misaada.“Ni vyema wananchi wakaelewa kuwa suala la kulipa kodi sio la hiari, kodi ni tozo la lazima, kila mwananchi anapaswa kuichangia Serikali kwa kipato alichonacho”, alisema.Awali akizungumza katika semina hiyo, Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Elvis Ndunguru alisema lengo la semina hiyo ni kujaribu kuondoa tofauti iliyopo kati ya wafanyabiashara na mamlaka hiyo ambayo sehemu kubwa inachangiwa na uelewa mdogo kwa baadhi ya wafanyabiashara.“Ni matumaini yetu kuwa semina hii itasaidia kuwafanya wafanyabiashara na TRA kuwa marafiki na pia kusaidia wafanyabiashara kufahamu haki zao na aina mbalimbali za kodi kutakakopelekea ulipaji wa kodi kwa hiari kwa maendeleo ya nchi yetu”, alisema Bwana Ndunguru.Aliongeza kuwa wao ni wakala wanakusanya maduhuli ya serikali hivyo akasema wafanyabiashara na wananchi wanaweza kwenda katika benki hiyo kulipa maduhukli na kodi mbalimbali za serikali.Mmoja wa wafanyabiashara waliohudhuria semina hiyo, Rowland Phares alisema changamoto kubwa waipatayo ni uelewa mdogo juu ya taratibu, sheria na kanuni za TRA.Alishauri TRA kwa kushirikiana na wadau wake kama vile NBC kuandaa semina hizo mara kwa mara bila kuchoka kwa wanyabiashara wadogo wa kati na wakubwa waelewe
0
HALMASHAURI ya Wilaya ya Bahi inatekeleza mradi wa maji wenye thamani ya Sh milioni 637.9 ambao umeondoa kero ya mjini hapo na sasa utasambaza maji katika kijiji cha Mkakatika ili kuwapa huduma wananchi lilipojengwa tangi hilo.Akisoma taarifa za mradi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge aliyekuwa katika ziara ya kukagua miradi wilayani humo, Kaimu Ofisa wa Maji Wilaya ya Bahi, Juma Hafidh alisema mradi huo utakamilika Agosti 28, mwaka huu.Alisema mradi huo unajengwa na Kampuni ya Nipo Africa Engineering Ltd, baada ya kusambaza maji katika mji wa Bahi awamu ya pili unaolenga kusambaza maji katika kijiji cha Mkakatika ili kuwapa huduma wananchi mahali lilipo tangi hilo la maji.“Mradi huo unatekelezwa kupitia Programu ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RWSSP) katika Awamu ya Pili ya Proragamu ya Maendeleo ya Maji (WSDP II) na lengo ni kusogeza huduma ya maji karibu na wananchi na kutumia muda mfupi kupata huduma hiyo,” alisema.Alisema chanzo cha mradi huo ni kisima kirefu chenye urefu wa mita 120 kilichochimbwa mwaka 1985 na mwaka 2014 kilisafishwa na kupimwa wingi wa maji na ubora na kubainika kitakuwa na uwezo wa kuzalisha lita 11,200 kwa saa.“Pamoja na kujenga njia kuu ya bomba, kujenga njia ya kusambaza maji, kujenga tangi, kufunga pampu na kujenga lambo kwa ajili ya kunyweshea mifugo, pia unajenga vituo 11 vya kuchota maji wananchi wa kijiji hicho,” alisema.Alisema katika kutekeleza mradi huo, kwa sasa umefikia asilimia 55, huku mkandarasi akiwa amelipwa Sh milioni 128.9 ambazo ni sawa na asilimia 20.2 ya fedha za mradi na anadai Sh milioni 508.9 sawa na asilimia 79.8 ya fedha zote za mradi huo.Akizungumza mkandarasi wa Kampuni ya Nipo, Adisan Haule alisema, ataendelea na kujenga vituo vya kutolea maji na hadi jana alikamilisha saba kati ya 11, huku akishughulikia suala la kupeleka cheti kwa ajili ya kuomba alipwe malipo ya kazi aliyofanya.Akizungumza baada ya kusikiliza ripoti hiyo, Dk Mahenge alisema mkandarasi anatakiwa kuendelea na kazi ili kumalizia mradi huo pamoja na kwamba hajalipwa fedha zake na mara atakapopeleka wizarani cheti atalipwa fedha zake.Akizungumzia mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda alisema Kampuni ya Nipo ni wadau wa siku nyingi wa wilaya hiyo, hivyo ana imani kwamba atakamilisha mradi huo wakati suala la kulipwa fedha zake likishughulikiwa.
1
Mbunge wa Starehe nchini Kenya, Charles Njagua maarufu Jaguar yupo nchini Tanzania kuanzia jana Ijumaa Julai 18, 2019. Huku akieleza kuwa atakuwa Tanznaia hadi Jumapili Julai 21, 2019, Jaguar amesema hana tatizo na Watanzania. Juni 25, 2019 mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki kupitia mitandao ya kijamii video yake ilisambaa akieleza kuwafukuza wafanyabiashara wa kigeni wakiwemo Watanzania ndani ya masaa 24 kurudi kwao la sivyo watawapiga na kuwarudisha nchini mwao. Serikali ya Kenya ililaani kauli yake hiyo na kusema si msimamo wa nchi hiyo, pia alikamatwa na kusota rumande kwa siku nne katika kituo cha Polisi Kileleshwa baada ya mahakama kusema kuna haja ya kulinda uchunguzi unaoendeshwa kuhusu matamshi ya uchochezi anayodaiwa kuyatoa. Hata hivyo aliachiwa kwa dhamana. …Good morning from Dar es Salaam. A post shared by Hon. Jaguar (@jaguarkenya) on Jul 17, 2019 at 9:16pm PDT Akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) jana Julai 18, 2019, Jaguar amesema amekuja Tanzania kwa kuwa hana tatizo na Watanzania na kauli aliyoitoa hakuwa amewalenga wao, bali wanaofanya biashara kinyume na taratibu za Kenya. “Nimekuja kutembea Tanzania naipenda Tanzania na kama unavyojua ile kauli ambayo watu walishindwa kuielewa, nilikuwa namaanisha wanaofanya kazi kinyume na taratibu,” amesisitiza. ….. A post shared by Hon. Jaguar (@jaguarkenya) on Jul 17, 2019 at 1:54am PDT Alipoulizwa kuhusu kuomba msamaha kwa kauli hiyo, amesema hana cha kusema na hajakosea, akisisitiza kuwa aliwalenga wanaofanya biashara kinyume na taratibu. Alipoulizwa kilichomleta Tanzania, amesema familia yake ipo Tanzania amekuja kuiona. “Pia nina marafiki kama Joseph Haule (Profesa J- mbunge wa Mikumi) pamoja na Joseph Mbilinyi (Sugu-mbunge wa Mbeya Mjini). Hawa nitapata nafasi ya kukutana nao,” amesisitiza.
4
Mwandishi Wetu -Singida BENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 katika wilaya kadhaa nchini. Misaada iliyotolewa na benki hiyo inayoongoza kwa kutengeneza faida kati ya benki zote zinazofanya biashara humu nchini ndani ya miezi mitano mwaka huu, inahusisha vifaa vya ujenzi, madawati na vifaa vingine vinavyowezesha ukamilishaji wa miradi ya afya,elimu na usalama wa raia. Benki  ya NMB imeshatoa  msaada wa  vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa mikoa ya Kanda ya Kati. Akifafanua kuhusu misaada hiyo wakati akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani ingida, Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Nsolo Mlozi, alibainisha kuwa misaada hiyo ya zaidi ya Sh milioni 200 iliyotolewa imelenga sekta ya elimu, afya  na majanga kwa mikoa mitatu ya  Kanda ya kati. Akikabidhi msaada wa madawati na vitanda kwa baadhi ya shule za Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, MkoaniSingida, katika shule ya Sekondari ya New Kiomboi, Mlozi alisema fedha hizo zilizotolewa na NMB zimetumika kununua madawati, viti vya shule za sekondari,vitanda na vifaa tiba kwenye sekta ya afya. Aidha, alisema lengo la misaada hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuwahudumia wananchi kwenye sekta mbalimbali. Pia alisema misaada hiyo imekabidhiwa kwa baadhi ya shule, zahanati, hospitali katika mikoa ya Singida, Dodoma na Manyara. Pia NMB walikabidhi madawati 250 na vitanda 80 vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 29.5 kwa baadhi ya shule za Wilaya ya Iramba mkoani humo. Katika hatua nyingine, Benki hiyo imevipatia kituo cha Polisi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro pamoja na shule ya msingi Msowelo mabati 160 yenye thamani ya Sh5 milioni kwa ajili ya kuezekea maboma. NMB iliamua kutoa msaada huo ikiwa ni mpango wa kuzipunguza baadhi ya changamoto kwa taasisi za serikali hapa nchini, Meneja wa NMB kanda ya mashariki, Baraka Ladislaus, alisema na kubainisha kuwa msaada huo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo kurudisha sehemu ya faida kwa jamii ili kusaidia kuinua miradi ya maendeleo. Baraka alisema kuwa kati ya mabati hayo, kituo cha polisi wilaya kimepa tamabati 80 huku shule ya msingi Msowelo nayo ikipata mabati 80.
0
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema), amesafirishwa kuelekea Dodoma chini ya ulinzi wa polisi tayari kwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge. Kubenea amesafirishwa kwa ndege leo Jumatano Septemba 20, saa moja asubuhi baada ya polisi kujiridhisha kuwa afya yake si njema usafiri kwa barabara. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa ameiambia Mtanzania Digital kuwa Mbunge huyo alikuwa na hati ya kukamatwa kutoka Jeshi la Polisi mkoani Dodoma, iliyokuwa inamtaka afikishwe huko jana. “Kutokana na afya yake jana tulishindwa kumsafirisha kwa gari ikabidi tufanye taratibu za usafiri wa ndege leo, nafikiri tayari atakuwa ameshasafiri maana ilipangwa aondoke saa moja asubuhi,” amesema Kamanda Mambosasa. Mbunge huyo anahojiwa na kamati hiyo kutokana na agizo la Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyezitaka kamati hiyo na ile ya Ulinzi na Usalama kumhoji mbunge huyo kwa kauli yake aliyoitoa katika Kanisa la Ufufuo na Uzima wiki iliyopita kuwa Spika ni mwongo kwani ametaja idadi chache ya risasi alizoshambuliwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, aliyeko nchini Kenya kwa matibabu.
1
Huduma hiyo ilizinduliwa Dar es Salaam mwanzoni mwa mwaka jana na baadaye ilisambazwa kwenye mikoa ya Arusha, Tanga, Dodoma na Morogoro na hivyo kuufanya mtandao wa 4G kuwa mpana na wa kasi nchini Teknolojia ya 4G LTE ina kasi ya nguvu takribani mara tano ikilinganishwa na teknolojia ya 3G inayotumiwa na watoaji wengine wa huduma hiyo kwenye soko la Tanzania.Mtandao wa 4GLTE una kasi kubwa kwenye kusambaza na kupakua vitu mbalimbali kutoka kwenye intaneti pamoja na kupiga miito ya simu ya skype.Hali kadhalika inawezesha wateja kwa kiwango kikubwa kuwa na uzoefu wa kutiririsha video au kufanya mikutano na inaweza kuhimili kutumika kwenye kupata video, mikutano, mwonekano wa hali ya juu, blogu za video, michezo mbalimbali na kupakua video kwenye mitandao ya kijamii.Ofisa Biashara Mkuu wa Tigo, Shavkat Berdiev alisema katika taarifa kwa vyombo vya habari kuwa mipango ya kupanua teknolojia ya 4G hadi kwenye maeneo yote nchini, inafanyika ikiwa ni mkakati wa kampuni hiyo wa kuwapatia wateja wake huduma ya hali ya juu duniani ili kuwawezesha kuendesha maisha ya kidigitali.Tangu mwaka jana, Tigo ilishawekeza Dola za Marekani milioni 120 kwa mwaka kwenye upanuzi wa mtandao wake pamoja na kuboresha maeneo ya mitandao ya 4G na 3G na Mkongo wa Mawasiliano.Hali kadhalika kuongeza idadi ya kufikiwa kwa huduma kwa wateja nchi nzima. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) takribani asilimia 67 ya idadi ya watu wazima wanamiliki simu za mkononi, huku idadi ya watumiaji wa intaneti hadi mwaka 2014 ilikuwa imeongezeka kufikia watu milioni 9.3.
0
* Mashabiki kushuhudia mbinu, ufundi na falsafa  * Sera mpya za kuzibadili timu kuchagiza mchezo huo NA SAMUEL SAMUEL, DAR ES SALAAM LICHA ya kutokuwa na maendeleo makubwa ya kisoka barani Afrika, soka bado umekuwa mchezo pendwa zaidi Tanzania na kugeuka kama alama ya umoja, mshikamano na chachu ya maendeleo kijamii. Ndani ya jamii hii umeibuka upinzani mkali, ulioibua dhana ya upinzani wa jadi katika soka. Unapolizungumzia pambano la soka kati ya Simba na Yanga, unazungumzia pambano la watani wa jadi la tatu kwa umaarufu barani Afrika, baada ya lile la Al Ahly na Zamaleki pale Misri na Kaizer Chiefs dhidi ya Orlando Pirates kule Afrika Kusini, kwenye mji maarufu wa Soweto (Soweto Derby). Homa ya watani wa jadi, yaani Simba na Yanga inaongezeka kila uchao kuelekea Oktoba Mosi, siku mtanange huo utakapopingwa kwenye Uwanja wa Taifa, hii ni kutokana na ubora wa vikosi vyote. Mara ya mwisho timu hizo zilikutana Februari 20, 2016 msimu uliopita na mabingwa watetezi, Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, mabao yaliyofungwa na Donald Ngoma dakika ya 36 kipindi cha kwanza na Amisi Tambwe dakika ya 77 kipindi cha pili. Ukitazama uimara kimbinu na kiufundi kwa timu zote msimu uliopita kabla ya pambano lao la Februari 20, utaona Yanga walikuwa juu na Simba haikuwa vema kutoa ushindani na ndicho kilichosababisha kupoteza mechi zote mbili walizokutana. Yanga Oktoba Mosi wanakutana na Simba mpya, ambayo ipo vizuri kimbinu na kiufundi kutokana na marekebisho makubwa waliyoyafanya kwenye kikosi chao msimu huu. Simba wamebadili benchi lao la ufundi kwa kumleta Joseph Omog, ambaye analijua vema soka la Tanzania akiwa na rekodi ya kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu msimu wa 2013/14 akiwa na Azam FC. Hivyo si mgeni sana katika joto la watani wa jadi, anajua raha na karaha za mmoja wao kupoteza pambano hilo. Uwepo wa Mayanja kama kocha msaidizi Simba, ambaye alikuwa kwenye benchi la ufundi msimu uliopita kama Kocha Mkuu, Simba ikilambwa 2-0, utasaidia kuwa mshauri mzuri kimbinu, kiufundi na falsafa sahihi kulipiza kisasi kwa mabingwa hao watetezi. Muunganiko kimbinu na kiufundi kwa Simba na Yanga, katika mchezo huo utaona kabisa wapenzi wa soka msimu huu wanakwenda kushuhudia mechi nzuri na yenye upinzani halisi pande zote. Ukiangalia usajili wa Simba, Laudit Mavugo kutoka Burundi, mwenye uwezo mkubwa wa kucheka na nyavu ni msumari wa moto kwa walinzi wa Yanga. Blagnon toka Ivory Coast, ana fiziki ya kutosha na mzuri kucheza kama mshambuliaji namba mbili kificho, anazidi kutoa taswira ya umakini wa Simba katika usajili wa mwaka huu. Yanga wanasifika sana kwa uimara wao wa mashambulizi ya pembeni, yanayoanzia kwa walinzi wa pembeni au mawinga wao, hususan Simon Msuva kulia na Deus Kaseke kushoto. Msuva na Kaseke watarajie upinzani mkali kwa wekundu hao wa Msimbazi, ambao msimu huu wameongeza idadi ya viungo  wenye uwezo mzuri kukaba na kupunguza eneo la kati na pembeni kimbinu kwa kuziba sehemu zilizo wazi ‘open spaces’ ambazo huwafanya viungo wa pembeni wa Yanga au mabeki wao kupanda kwa kasi. Shiza Kichuya na Mzamiru Yassin wanaiweza vyema kazi hiyo, hivyo walinzi wa Yanga wawe makini sana na Kichuya aliyetokea Mtibwa Sugar. Kichuya ni kiungo makini katika ukabaji, kuchezesha wenzake lakini hatari zaidi kucheza kama kiungo mshambuliaji kificho, tayari ana goli zake mbili za maana. Simba msimu uliopita ilikuwa inakosa wachezaji wazuri katika benchi la ufundi wenye uwezo wa kuingia ndani, ama kuendeleza kasi ya mchezo au kubadilisha mfumo wa uchezaji kimbinu kama timu imebanwa, lakini msimu huu Simba ipo vizuri na kuonekana tishio. Kichuya, Mzamiru, Mnyate, Mavugo, Janvier Bokungu ni wachezaji wapya wanaokutana na wakali wengine, kwa uchache ni Said Ndemla, Mwinyi Kazimoto, Ibrahim Ajib na nahodha Jonas Mkude. Si kwamba ubora wa Simba wamejihakikishia ushindi kwa mabingwa hao watetezi. Yanga wenyewe katika mechi zake nne mpaka sasa imetuma salamu za tahadhari kwa wekundu hao, wana rekodi nzuri ya kutoruhusu goli lolote kugusa nyavu zake, hii ina maana wakali hao wa Jangwani wana safu nzuri ya ulinzi, tofauti na Simba walioruhusu nyavu zao kutikisika mara tatu licha kushinda. Uimara wa Vicent Bossou na ingizo jipya Andrew Vicent ‘Dante’ katika safu ya ulinzi ni karata ya turufu kimbinu kwa Yanga mbele ya washambuliaji wasumbufu wa Simba SC. Walinzi hao wa kati ni kombinesheni namba mbili mbele ya pacha kongwe ya ulinzi chini ya Nadir Haroub na Kelvin Yondani, hapa ndio utaona ni jinsi gani joto la watani hawa toka 1935 na 1936 linavyofukuta. Licha ya ubora wa viungo wa Simba SC msimu huu, itawahitaji kuvuta kweli soksi zao mbele ya Deusi Kaseke, Thaban Kamusoko, Said Makapu, Haruna Niyonzima, Mahadhi Juma, Yusufu Mhilu, Pato Ngonyani na Mbuyu Twite, msitu wa viungo wazuri na wenye kasi ya ajabu. Simba wakiwaangalia Amisi Tambwe na Ngoma ni lazima nyuzi joto za mchezo huo kwa upande wao zipande, wakikumbuka alichowafanyia msimu uliopita. Mchezo huu kifalsafa unachagizwa na ujio wa sera mpya za kuzibadili timu hizo katika mfumo wa uendeshaji. Tayari bilionea Mohamed Dewji amekwisha kuchukua dhamana ya kuwalipa mishahara wachezaji wa Simba kwa miezi sita, ikiwa ni sehemu ya kusakafia wazo lake la kuzitaka hisa za asilimia 51 za timu hiyo. Ni dhahiri atawajenga vema wachezaji wa timu kisaikolojia kwa posho na ahadi nono kuelekea mchezo huo. Manji, ambaye anakitaka kikosi cha Yanga kwa miaka 10 kwa asilimia 75, naye sidhani kama atakuwa nyuma kuisadia timu kisaikolojia kushinda mchezo huo ili thamani ya soko lake kibiashara iongezeke. Ni mpambano mzuri endapo waamuzi watafuata sheria 17 za soka kwa usawa bila upendeleo, pia wachezaji wa timu zote kuzingatia nidhamu ya mchezo huo pendwa zaidi.
2
RAMADHAN HASSAN -DODOMA MFUMUKO wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020, umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Hayo yalielezwa jana jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu na Sensa ya Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ruth Minja alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari. Alisema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umebaki kuwa asilimia 3.2 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Minja alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa za vyakula na bidhaa kwa mwaka ulioishia Juni 2020 umebaki kuwa sawa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Mei 2020. Alisema kuwa sawa kwa mfumuko huo kumechangiwa na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Juni 2020 zikilinganishwa na bei za Juni 2019. Minja alisema baadhi ya bei za vyakula zilizopungua ni pamoja na unga wa mahindi kwa asilimia 1.6, matunda asilimia 2.1, viazi mviringo asilimia 5.0 na mihogo asilimia 13.3. Alisema baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizoongezeka bei ni pamoja na mavazi kwa asilimia 2.7, gesi ya kupikia asilimia 7.8, mkaa kwa asilimia 11.2, samani asilimia 2.7 na vitabu vya shule asilimia 1.5. Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi ulioishia Juni mwaka 2020 umepungua hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 4.4 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Alisema kwa upande wa Afrika Mashariki, nchini Kenya mumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umepungua hadi kufikia asilimia asilimia 4.59 kutoka asilimia 5.33 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020. Kwa upande wa Uganda, alisema mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni 2020 umeongezeka hadi asilimia 4.1 kutoka asilimia 2.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei 2020.
0
TAH ARUKI imewakumba watu wa kada mbalimbali, wakiwamo wasomi, wazazi na walimu nchini kutokana na taarifa ya kufutwa kwa Mtihani wa Kumaliza El imu ya Msingi (P SLE) kat ika halmashauri moja na shule nane nchini, huku wakipendekeza hatua kali, ikiwamo adhabu ya kufungwa maisha jela kwa walimu waliohusika.Tayari Mkoa wa Dodoma umewavua madaraka waratibu elimu ngazi ya kata watano na walimu wakuu watano, na kuwasimamisha kazi walimu wanne waliokuwa wasimamizi wa mitihani katika Shule ya Msingi Kondoa Integrity. Aidha, imefahamika kuwa baadhi ya walimu katika shule za Dar es Salaam waliohusika katika udanganyifu na uvujishaji wa mtihani huo wamekamatwa na Polisi na wanasota rumande.Maoni hayo yamekuja siku moja baada ya B araza la Mitihani la Tanzania (NE CTA) kutangaza kufuta matokeo ya Mtihani wa Kumaliza E limu ya Msingi (PS L E ) kwa shule zote za msingi za H almashauri ya Chemba mkoani Dodoma na zingine nane kutokana na kubainika uvujishaji na wizi wa mtihani.S hule nyingine zilizoingia katika kashfa hiyo ni H azina, New H azina za Kinondoni, Aniny Nndumi na Fountain of Joy za Ubungo jijini Dar es S alaam, Alliance, New Alliance na Kisiwani za Mwanza na Kondoa Integrity ya Dodoma. Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde aliwaambia waandishi wa habari juzi Dar es Salaam kuwa mitihani hiyo itarudiwa wiki ijayo O ktoba 8 na 9, mwaka huu kwa shule hizo zilizofutiwa matokeo.Shule, wazazi wapata mshtukoMmoja wa maofisa wa Shule ya Aniny Nndumi ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini, alieleza kupatwa na mshtuko mkubwa baada ya kuona wametangazwa kwenye vyombo vya habari, kwani walishahojiwa na kueleza kuwa hawakuhusika. O fisa huyo alisema shuleni hapo jana kuwa baada ya tuhuma hizo kutokea, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Justus Mapesa yuko katika mahabusu ya Keko iliyopo Dar es Salaam, tangu S eptemba 14, mwaka huu. Alieleza kuwa Mapesa alitokea katika Shule ya Alliance iliyopo jijini Mwanza mwaka mmoja uliopita ambayo nayo imefutiwa mtihani huo.Aliongeza kuwa Septemba 20, baadhi ya wafanyakazi wa shule hiyo na wapishi waliokuwepo siku ya mtihani, walihojiwa pamoja na wanafunzi waliofanya mtihani huo. Alisema baada ya mwalimu mkuu huyo kutokuonekana, wazazi walianza kuhoji, na uongozi wa shule ulitoa taarifa kwao O ktoba mosi mwaka huu, kuwa mwalimu Mapesa na Kennedy Malago hawapo shuleni hapo kwa sasa. Pia baada ya taarifa hiyo kutolewa na vyombo vya habari, jana uongozi wa shule ulitoa taarifa kwa wazazi kuhusu changamoto iliyojitokeza na kuwaomba radhi wazazi hao.Uongozi watuliza wazaziTaarifa hiyo kwa wazazi ilisema, “Uongozi wa Shule ya Aniny Nndumi unapenda kuomba radhi kwa tukio lililotokea ambalo wengi tumelipata kupitia vyombo vya habari. Tunaomba radhi kwa usumbufu na sintofahamu mliyoipata kutokana na kadhia hii. Akizungumzia mtihani huo wa marudio, alisema muda wa watoto kujiandaa ni mfupi, kwani walipaswa kuandaliwa kwa mtihani baada ya kumaliza shule. Uongozi wa Shule ya H azina iliyopo Magomeni jiini Dar es S alaam haukutoa ushirikiano kwa wanahabari walipofuatwa shuleni hapo jana.Katika Shule ya Fountain of Joy iliyopo Mbezi, Mwalimu Mkuu Msaidizi Charles Thomas alisema Mkurugenzi wa shule hiyo, Joyce William na Mkuu wa Shule, Mwita Dunstan hawakuwepo.Wasomi waipongeza serikaliKutokana na uamuzi huu wa Necta, wasomi wakiwamo wa Chuo Kikuu cha Dar es S alaam (UDSM), wamepongeza serikali kwa hatua waliyoichukua, huku wakipendekeza adhabu kali zaidi.Profesa kutoka Shule Kuu ya E limu chuoni hapo, H erme Mosha alisema suala la udanganyifu lazima liendane na adhabu kali ili kukataza tabia hiyo mbaya. Alisema kwa hatua hiyo watu ambao sio waaminifu hawatarudia tabia hiyo mbaya. Profesa Mwajabu Possi kutoka Idara ya Saikolojia na Mitaala Shule Kuu ya E limu, alisema hiyo si mara ya kwanza kwa shule kufutiwa mitihani, hivyo mpaka ifikie hatua hiyo lazima wahusika wameona kuna hali isiyo ya kuridhisha na lazima watu wawajibishwe.Profesa Possi alisema japo wanaopata shida ni watoto, lakini isiwe ikawa kuna watoto ambao walijua kilichokuwa kikiendelea kuwa wamepata mtihani huo wa udanganyifu. “ Tabia hiyo kwa watoto wanaojua inaanza kidogo kidogo mwisho inakuwa katika maisha yao yote. H ivyo adhabu itolewe ili iwe fundisho na wale waliobainika kufanya hivyo sheria ichukue mkondo wake,” alisema Profesa Possi.Profesa wa Sayansi ya S iasa na Utawala wa UDSM, Dk B enson B ana alisema watu wote wakiwemo viongozi wa maeneo husika wanaotuhumiwa na udanganyifu huo, wanapaswa kujiondoa kabla hatua zaidi hazijachukuliwa.Walimu wafungwe jela maishaB aadhi ya viongozi kutoka taasisi mbalimbali zinazojihusisha na elimu kikiwemo Chama cha Wamiliki wa S hule B inafsi Tanzania (TAMO NG S CO ), walisema hatua kali zinapaswa kuchukuliwa dhidi ya wahusika wa kashfa hiyo.Katibu Mkuu wa Tamongsco, Axwesso Mao alisema kimsingi suala hilo halipaswi kufumbiwa macho kwa kuwa matokeo yake ni kuzalisha Taifa la watu mbumbumbu, ambao mwisho wake ni hasara kwa maendeleo ya nchi. “ L engo la mtihani wowote ni kupima uwezo wa mwanafunzi kwa kipindi chote alichokaa darasani, unafanya wizi na kumpa mwanafunzi nyenzo ya kuvuka kikwazo hicho, inaleta maana gani ya kukaa naye darasani kipindi chote alichokuwapo hapo shuleni? S erikali inapaswa kuwapa adhabu kali wahusika,” alisema Mao.Alisema pamoja na hilo, serikali pia inapaswa kufanya uchunguzi wa kina kwa wahusika na watu wengine kwani inachoonekana kuna mtandao umehusika, na ili kudhibiti lisijirudie, ni vyema tukio hilo likafuatiliwa kwa karibu. Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Shirikisho la Watoaji wa E limu Wasiotegemea Serikali Afrika kusini mwa Jangwa la S ahara (CIE PS S A), B enjamini Mkonya alisema mbali na kufutiwa matokeo, wanafunzi waliohusika katika udanganyifu huo, shule na walimu wao wanapaswa kuchukuliwa hatua zingine kali ili iwe fundisho kwa wengine.Alisema kwa kuwa wanafunzi waliopewa mitihani hiyo ni watu wanaojielewa, wanapaswa kupewa adhabu hiyo kwa kushindwa kutoa taarifa zozote ambazo zingeweza kudhibiti wizi huo kwa mamlaka husika na kwamba kinachoonekana hata wao walipenda wizi huo.Shule zakaliwa kooniMwalimu wa Shule ya Joyland International School (JIS ) ambaye hakutaka kutajwa jina lake, alisema yawezekana shule hizo zimefanya hayo ili kutaka kuonekana kuwa ni shule bora zaidi kwa ajili ya kupata wanafunzi wengi.Naye Mwalimu Mkuu wa S hule ya Msingi Maruango, Mercy Kitomari alisema kwa sasa ufaulu umegawanywa katika sehemu tatu; Utepe wa Kijani ambao ni ufaulu wa juu na shule nyingi zinazofikia hapo ni za binafsi, Utepe wa Njano ambao ni ufaulu wa wastani na Utepe Mwekundu ambao ni zile shule zinazofanya vibaya.“ Mara nyingi shule zinapoingia katika Utepe Mwekundu mfululizo lazima wizara ije na maofisa elimu wanakuja kuangalia tatizo ni nini... hivyo unakuta wengi wanatumia mbinu mbadala na wengine ndio kujiingiza katika vitendo vya udanganyifu na wizi wa mitihani,” alisema Kitomari. Alitoa mwito kwa walimu wote nchini kubuni mbinu za kuwafundisha wanafunzi na kuelewa vyema kuanzia ngazi za chini, na kuwajengea kujiamini ili wafanye mitihani yao wenyewe badala ya kutegemea kufanya udanganyifu.Pia aliiomba serikali kuongeza maslahi ya walimu na kuwapa motisha ili kuipenda na kuifurahia kazi yao na kuifanya kwa bidii kwa kuwajengea uwezo wanafunzi ili wanapofanya mitihani ya Taifa wafaulu kwa kiwango cha juu badala ya kutegemea kuanya udanganyifu. Mzazi Julius John alisema siyo shule zote zilizofutiwa matokeo wanafunzi wake hawana uwezo, ila ni baadhi ya walimu na wamiliki kutafuta sifa ambazo zimewaponza na kuwaumiza watoto waliofutiwa matokeo.Mkazi wa Ubungo, Nyakasa Mboni alisema hatua hiyo ya kufutiwa matokeo ni hasara kubwa kwa wazazi na watoto wenyewe, kwa kuwa tayari zipo familia ziliaanza maandalizi kwa masomo ya mbele kwa watoto wao. Mwalimu wa Shule ya Msingi Kimara, Janeth O keso alisema hatua ya kufuta matokeo ni adhabu kwa watoto na hata kwa wazazi, lakini haina budi hatua kuchukuliwa ili kuepusha kuendelea kuwepo kwa udanganyifu.Alisema licha ya wazazi kupata hasara kwa kuwasomesha watoto kwa miaka saba halafu kupata taarifa kama hizo, lakini ili kujenga Taifa madhubuti lenye elimu na ujuzi stahiki, ni lazima hatua kuchukuliwa ili kudhibiti matukio ya aina hiyo.Dodoma yawavua vyeoMkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk B inilith Mahenge amewataka wazazi na walezi wa wanafunzi wanaopaswa kurudia mitihani wao wa darasa la saba, kuhakikisha watoto wao hawapotezi fursa ya kufanya mitihani hiyo.Aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa hatua ya serikali ya kutoa fursa nyingine kwa wanafunzi kurudia mtihani ni jambo la huruma na kuwa si vyema fursa hiyo ikapotea kwa mwanafunzi kutofanya mtihani huo.“ B inafsi, kwa niaba ya mkoa napenda kubainisha masikitiko kwa tukio hii na vitendo vyote vilivyo nyuma yake. Athari za tukio hili ni kubwa kuanzia kwa watoto wenyewe, familia na pia limetia doa juhudi za mkoa kuinua kiwango cha elimu na ufaulu,” alisema Dk Mahenge na kuongeza: “ Pia limesababisha serikali hasara kubwa kwa kuingia gharama za kurudia mtihani kwa maana na muda na nguvu kazi. Niipongeze serikali kwa huruma iliyotoa ya kufuta matokeo, lakini pia kuwaruhusu watoto kurudia mtihani.”Alisema ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata fursa hiyo, watatumia serikali za wilaya na vijiji katika wilaya zote mbili ili kuwatangazie wazazi ili wahakikishe wanafunzi wanakwenda kufanya mtihani wa marudio. Kuhusu adhabu, alisema mkoa umewavua madaraka waratibu elimu ngazi ya kata watano na walimu wakuu watano waliobainika waziwazi katika hatua za awali za uchunguzi kujihusisha na jama za udanganyifu.Alisema pia walimu wanne waliokuwa wasimamizi wa mtihani katika shule binafsi ya Kondoa Integrity wilayani Kondoa wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi. Pia alisema wameshirikiana na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika kutengua uteuzi wa uongozi wa Idara ya E limu ngazi ya wilaya iliyohusika katika kufanya udanganyifu, ambapo O fisa E limu, O fisa Taaluma wa Wilaya ya Chemba na O fisa E limu Msingi Wilaya ya Kondoa DC, teuzi zao zimetenguliwa.Naye Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Saimon O dunga alisema kwa sasa uchunguzi wa kina unaendelea kwa vyombo vya dola ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ili wahusika wafikishwe mahakamani. Serikali kubeba gharama Aidha, Necta imesema hakuna mtoto au mzazi atakayeechangishwa fedha kwa ajili ya marudio ya mtihani wa Kumaliza E limu ya Msingi (PS L E ) 2018 baada ya shule zao kufutiwa matokeo. Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, O fisa H abari na Mawasiliano wa Necta, John Nchimbi alisema wazazi na walezi wanachopaswa kufanya ni kuwaandaa watoto wao kwa ajili ya mtihani huo wa marudio utakaofanyika wiki ijayo O ktoba 8 na 9, mwaka huu.“ Ninachojua mitihani hugharamiwa na serikali, hivyo hakuna mtoto au mzazi atakaechangishwa fedha kwa ajili ya mitihani hiyo ya marudio,” alisema Nchimbi na kuongeza kuwa anaamini wanafunzi wote wamefundishwa na kujifunza vyema kwa kipindi chote walichokaa shuleni, hivyo wana uwezo wa kufanya mitihani hiyo bila usaidizi.“ L engo la kurudia mitihani siyo kumkomoa mwanafunzi, bali ni kuhakikisha tunaendelea kusimamia viwango bora na wanafunzi wanatumia ujuzi na maarifa waliyopata wakiwa shuleni,” alisema. Aliwataka walimu na wamiliki wa shule kuridhika na uwezo wa wanafunzi wao kwa kuwa vitendo vya udanganyifu na wizi wa mitihani vinatia doa shule husika. Polisi yachunguza, yahoji Akizungumzia kuhusu kushikiliwa kwa baadhi ya watuhumiwa, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Muliro Jumanne alisema kwa sasa wanaendelea na uchunguzi wa suala hilo, hivyo wanaweza kuwashikilia watuhumiwa, kuwahoji na kuwaachia kwa dhamana.
1